®HADITHI PICHA® Mussabhai & YuYuShortstory 👙👙👙 DADA VUA👙👙👙 PICHA NO:_16 LIKE PAGE UWE WA KWANZA KUIPATA HII KILA SIKU. https://www.facebook.com/YuYuTzHotStory HAYA HAYAAA ZILE SIDIRIA AMBAZO KWA SASA NDO HABARI YA MUJINI TUNAZO KAZI KWENU MASTISA DUU UKIVAA MUGONGO WAZI KWA AJILI YA MTOKO NDO ZENYEWE HAZINA MIKANDA NZURI KWA MABIBI HARUSI PIA UKINUNUA LEO UTAUZIWA KWA BEI YA OFA 30000 WAHII KABLA OFA HAIJAISHA TUPO DAR MIKOANI TUNATUMA ILA BAADHI YA MIKOA TUNA MAWAKALA mawasiliano 0711462866 0711462866 WhatsApp TUNAUZA JUMLA PIA Bonyeza link hapo chini kuangalia jinsi ya kuzivaa 👇👇👇👇 https://youtu.be/oWwe9rFZaxo ..........ilipoishia Wakati baba na mama walikuwa wakiagana kwa kupeana mautamu vitu urojo urojo.Huku sule huku sule mambo yalikuwa magumu balaa.Lakini alipomuona Shangazi yake na helena alishtuka sana kwani alitokea ghafla tuu.Hali hiyo ilimpa mashaka sana Sule.Wakati anaduwaa alishangaa kuona shangazi anawazuia wale wanyama ambao ni kina Helena.Shangazi aliongea kwa sauti ya kutisha"Tabia yako ndio imekusababisha uko hukuuuu!!! na ulivyo na tamaa ulitaka kuzini na dada zako mbwa wewe...... SHUKA NAYO LAKINI NAOMBA TUU USIACHE KULIKE. Shangazi aliwakamata kina Helena kwa kitambaa cheupe na kuwazuia wasimdhuru Kijana sule.Sule hakuamini kama mpaka dakika hiyo yuko mzima kwani alishaamini ndio mwisho wake.Shangazi hakutaka kumficha alimpasulia sule japo sule hakuelewa moja kwa moja ni dada zake kivipi maana ni kitambo sana walifariki na hakuwaza kuhusu ushirikina.Basi Shangazi Alimtazama Sule huku ameikunja sura yaani alikaa kikazi zaidi si unajua mambo ya kichawi tena.Shangazi aliongea "Vijana wa siku hizi mnapenda kuvamia vamia wanawake ungezini na dada zako. na hizo tamaa za kijinga,Na ulikuwa na nafasi nzuri sana kwani nyota yako ni ya bahati lakini hizo tamaa zimekuponza". Sule alimsikiliza Bi kidako lakini hakumuelewa kwani hajui chochote alibaki kumshangaa tuu. Wakati huo dereva alifika mpaka hotel moja inaitwa MOMELA HOTEL maana aliambiwa apitie njia hiyo atakutana na sule njiani,Alizidi kuingia ndani zaidi yaani porini lakini hakuona mtu.Kwa kuwa ilikuwa ni usiku aliogopa kuendelea mbele kwani ni porini na alikuwa mwenyewe tuu.Alifika mahali akasimama na kupark gari pembeni" Sasa huyu mtu yuko wapi??"Alijiuliza bila kupata majibu kisha akaegesha gari yake kando ya barabara na kumngoja.Yaani dereva alibakiza mita chache sana kufika eneo ambalo Sule,Shangazi na kina Helena walikuwepo.Wakati huo Mama wa Sule alipomaliza kumfurahisha mzee wake aliomba ruhusa kwa mumewe atoke kidogo kwani mama anamdai hivyo kamwita akachukue pesa yake.Mumewe kwa kuwa tayari alishapata haki yake hakuwa na hofu hata kidogo.Alimruhusu bila shaka"Nenda lakini usikawie maana usiku saiz"Mama alienda parking na kuchukua gari safi na kutoka.Mama aliondoka na kuelekea Mount meru hotel.Alipofika alimchukulia mwanae chumba kizuri sana na ilikuwa ni chumba namba 15. Wakati huo yule dereva aliyetumwa kumfuata Sule alikata tamaa kwani aliona kama anasubiri hewa tuu yaani hakuna mtu.Aliwasha gari yake kisha akaenda mbele kidogo ili apate sehemu ya kugeuzia gari.Sasa wakati anatafuta sehemu ya kugeuzia,Mwanga wa taa za gari ulikutana na macho ya wale wanyama ambao ni kina Helena,Dereva presha,Woga vilianza kumuingia kwani yeye si mzoefu wa porini.Aliigeuza gari kwa spidi ya haraka,Alirudi mpaka momela hoteli Alisimama na kumpigia simu mama yake Sule"Haloo mama,Yaani mama hii ni adhabu mama yangu huwezi amini nimekutana na masimba huku.Kiukweli mama mi siwezi narudi tuu Sule mwenyewe simuoni mie"........Mama alimjibu"Hapana usifanye hivyo nakuomba sana usiache kuja na Sule nakuahidi nitakulipa mara mbili ya tulivyokubaliana".Dereva mwenyewe mchaga sasa ukimtajia mambo ya hela anachanganyikiwa kabisa,Alikubali lakini hakurudi tena kule alibaki pale pale hotelini. Huku kwa Sule Bi kidako aliamua kumsamehe lakini alimpa onyo"Kuwa makini na zipu lako la sivyo utajua mi ni nani?Na ukiondoka hapa uelekee nyumbani"Sule alivyosikia vile hakutaka kuchelewa hadi begi aliliacha.Alitoka spidi ya hatari,Bi kidako alicheeeka kwa dharau kisha akawarudisha kina Helena katika hali yao ya kawaida.Wakati Bi kidako anajiandaa kurudi na shangazi zake nyumbani simu yake iliita,Aliichomoa pale kwenye kile kimfuko cha kuvaa shingoni,Aliangalia namba iliyopiga alifurahi na kumwambia"Kazi imekwenda vizur sana mwanangu sasa mwambie huyo kijana aliyemfuata amngoja kwa barabarani anapitia barabara kubwa ya Usa"........"Sawa mama yangu nashukuru sana na lile swala letu hakikisha kesho linakaa sawa".........Bi kidako alijibu kwa dharau"Mwanangu hivi huniamini mie sasa akipanda tuu ndege utasikia habari yake muda mfupi tuu"........Mama wa sule alifurahi sana kisha akauliza tena,"Vipi hali ya hao kina Lucy??"......"Kina Lucy wako vizur ila tuu mwanao huyu Sule alitaka kuvuruga mambo kwani alitaka kuzini na nduguze bila kujua na ingekuwa ni hatari sana kwa upande wenu,Ila nashukuru nilifanikiwa kuzuia hali hiyo".Mama yake Sule alifurahi sana. Baada ya mazungumzo Mama yake Sule alimpigia dereva na kumwambia awe makini Sule asipitilize maana anapita pale muda si mrefu"Wewe Dereva kuwa makini asikupite amevaa kaushi nyeupe na suruali ya blue".....Sawa mama niko makini kuliko unavyofikiria,Ebu ngoja!!!!! subiri!!!!"........Wakati wanaongea na simu kwa mbali aliona mtu anakimbia kwa kasi sana.Kwa kuwa dereva aliipaki gari ikiwa imeelekea huko alipoambiwa sule yupo,Basi aliwasha taa ili ajue kama ni sule ndiye anayekuja.Ni kweli alikuwa ni sule na alikuwa akikimbia sana,Sule alipoona anapigwa na mwanga wa gari alisimama kwanza kwani alishajua kuwa Bi kidako ni mchawi hivyo kila kinachomtokea alijua ni uchawi.Sule alijishauri"Niende au nisiende!!?"Mara dereva yule alimpigia honi"Piiiipiiii!!!",Kisha akashuka na kumuita"Suuule!!!".Ukweli ni kwamba sule aliingiwa na woga alisimama kwa muda mrefu sana pale. Dereva kwa kuwa alishajua huyu ni Sule alimfuata aliamua kumfuata.Wakati huo Bi kidako alikuwa anarejea kwenye nyumba yake akiwa na kina Lucy,Wakiwa wanatembea Lucy aliona begi la Sule"Heee!! Shangazi nini kimetokea mbona begi la sule liko hapa na linaonekana limetupwa!!?"......Kina helena wakibadilika huwa hawajui kilichoendelea hivyo hawajui nini kimeendelea baada ya kugezwa wanyama labda shangazi yao awasimulie,Shangazi alijibu"Achaneni na huyu kichaa"Lucy alibeba begi hilo kaenda nalo mpaka ndani.Kwa kuwa Lucy na Helena wanalala chumba kimoja basi walianza kupekua begi lile kwa pamoja na kukuta mapicha mengi Sule akiwa katika majumba ya kifahari na warembo.Walikuta business card yenye anwani na namba za simu zenye jina SULEIMANI.Helena alichukua ile business card na kwenda kuichukua simu ya shangazi yao ili wajaribu kupiga ile namba.......Nini kitaendelea,Usikose kigongo cha kesho maana story yetu yote imebebwa na episod ya 17. HAKIKISHA UNALIKE PAGE MWANAWANE. PATA SIMULIZI 4 TOFAUTI KWA SIKU UWAPO KATIKA GROUP LA KIJANJA KULE WHATSAPP.STORY ZOTE NI HOT NA UNAZIPATA MAPEMA YAANI ZIKIWA ZAMOTO KABISA KAZI KWAKO,JIUNGE NA WENZAKO KWA TSH 3000/-TUU ZA KITZ Kwa wewe unayehitaji kuungwa group nicheki kupitia 0678641147 au 0688911112 whatsapp ni kuhusu simulizi tuu mambo mengine nicheki fb inbobo KAMA HUJALIKE PAGE FANYA IVO SASA ILI UWEZE KUPATA VITU MUBASHARA. #MussaBhai & #YuYuTz_ ®Newvission_2017

at 11:00 PM

Bagikan ke

0 comments:

Copyright © Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top