Home → simulizi
→ STORI YA MAPENZI; MALKIA WA JELA
SEHEMU YA PILI
..................................
"Mimi ni mkeo hata ingekuwa usiku wa manane wewe niamshe uniage nijue kabisa kweli unakurupuka tu asubuh unaondoka hata ujumbe basi ungeandika nao umeshindwa
"Baby nimekuelewa nisamehe basi nitafanyia kazi
BENSON anajarbu kumbembeleza kwa kusogea na kupeleka mikono yake taratibu na kumshka LINDA kiunoni kwa nyuma na kumbusu shingoni
"Baby sikujua Kama nitakuudh kuondoka bila ya kukuambia nisamehe nakuahd hata nikiwa naenda choon lazima nikuage
"Hahahah anaangua kicheko
"Unafrah nini sasa ?
"Ushaanza matan yako chooni ukienda Mimi hata usiniage
"Utajua nimeenda wapi Kama nisipofanya hvo
"Sitak " wanacheka wote wawili
Baada ya muda LINDA aliandaa chai na kuweza kukaa katika meza ya chakula na kunywa
Wiki moja baadae BENSON akiwa seburen peke yake mkewe akiwa ameondoka ameenda nyumban kwao Mara moja kusalimia BENSON aliamua kuitumia nafas ile kumpigia simu kimada wake na kuongea naye kabla ya LINDA kurud nyumban
"Halloo! Baby ! Alipokea simu kimada huku akitoa saut lain na nyororo
"Hallo ! Baby nambie
"Safi nimekumith ile mbaya BEN wangu
"Hunishind Mimi
"Unanitania.... kweli Baby ?
"Ndiyo kwanini nikuongopee nimeimis Sana ile mechi ya siku ile ulinifanya nione sinto maliza mchezo niliona uwanja mkubwa
"Hahahaahah Ikasikika saut ya kicheko
"Nilihisi kufa kufa
"Amna bhana usingekufa woga wako tu kufa huwez kufa ila cha moto lazima ungekipata
"Aa sikufich mke wangu anasubir we mtoto kibokoooo lini tena ligi yetu ya ugenini ?
Muda wako Uwanja wako sikuzuii kuja kufanya mazoez afu mechi kwa mkeo
"Hahahahah BENSON akaangua kicheko
"Baby hata ukitaka sahv tutafanya hata kwa kutumia "whatsapp" voice note
"Hahahah ndo maana nakupendaga Bab..................Kabla hajamalizia kuongea LINDA alifungua mlango BENSON alistuka na kuikata simu LINDA alibakia kasimama pale mlangon huku akimtazama Mumewe na kuanza kudondokwa na machozi Mkoba aliokuwa ameubeba aliuachia na kuuangusha chin
"BABY umewah nilijua utachelewa " Huku akionekana kuwa na wasiwasi Alinyanyuka na kutaka kumsogelea alipokuwa
"BENSON naomba usinisogelee "akamzuia kwa ishara ya mkono
"Mbona sielew Nyumban wazima mbona hukuondoka hivo afu umewah kurud kuna tatzo kwani
"Malaya mkubwa wewe Endelea kuongea na simu uliyekuwa unaongea naye nimesikia kila kitu
"Nan ? Mimi nilikuwa naongea na DAVID ananieleza habar za NITTY
"Mwanaume huna shukran BEN ni mangapi nimekufanyia kumbe ndo unavyo niongelea kwa hao Malaya zako
"LINDA mke wangu kwanini tugombane nilikuwa naongea na DAVID jarbu kunielewa Nakupenda hakuna mwingine zaid yako
"Mwongo mkubwa kwanini nilipoingia hukuendelea kuongea ukakata simu
"Tulikuwa tumeshamaliza maongez
"Ahsante kwa kunidanganya " Kumbe LINDA alikuja na DAVID ,DAVID alikuwa kwa nje akiwasikiliza akaona bora aingie alipoingia BEN aliishiwa nguvu na kuinamisha uso chin huku akijarbu kumtizama mkewe kwa kuibia ibia
"Endelea kuniongopea siumezoea haya ulokuwa unaongea nae huyu hapa Endelea BEN... LINDA kwa hasira alimfuata BEN na kuanza kumpiga mingumi huku akilia kwa uchungu DAVID alimshika LINDA na kuomba wasigombane
Alipowaamua aliamua kuwaacha kwa muda watulie kwanza baada ya robo saa kupita DAVID akamgeukia BEN na kutaka aseme alikuwa anaongea na nan
"DAVID sema ukweli "
"Mimi nilikuwa naongea na Dada yangu alinipigia kunijulia hali
"Unamwon a alivyo mwongo Dada yako gani umwambie maneno Yale BEN niambie "kwa jazba huku akijarbu kutaka kunyanyuka alipokaa
"Aaa shemej punguza jazba Mimi nipo hapa kila kitu kitaisha BEN Una uhakka
"Ndiyo Kwanini nimwongopee amesikia vibaya tu
"Shemej huenda ikawa ni kweli jaribu kusahau hili
"DAVID unapendelea au kwa kuwa BEN ni mwanaume mwenzio Ahsantee
LINDA Alinyanyuka na kuondoka kuelekea chumban
"Kaka bora hata ulivyokuepo sijui ingekuaje Leo
"BEN punguza hata Kama Una kimada nje hapa ni nyumban kwako paheshimu ukitaka kuongea nae Hakikisha mkeo kaenda mbali
"Saw a kaka
"Mi nilipita kukusalimia nilikutana na mkeo kwenye folen nikaon a bora Nam nipite kukuona kwahyo Mimi nafikir nimeshakuon a naondoka jarbu kumpoza mkeo
"Haina shida
BEN alimtoa DAVID mpka nje na kuweza kuagana kisha akarud na kuingia chumban alimkuta mkewe amejilaza kitandani kifudifudi amelalia mto huku akiwa Analia"LINDA mke wangu kwanini unapenda kujiumiza kwa vitu ambavyo siyo kwanini Mimi na wewe tugombane kwa vitu vidogo "Aliongea BEN
LINDA alijigeuza na kunyanyuka pale kitandan akaanza kuzunguka mule chumban huku na kule
"Unajua sikuekewi sasa unapozunguka hivi unamaanisha nini ? Alirudia tena kumwuuliza baada ya kuona hajibiw
"BEN lazima utaona ni jambo la kawaida kwasababu lipo kwangu ila ipo siku BEN unajua Mimi na wewe tumetokea wapi siyo kwamba hujui unajisahau Sana BEN "Aliongea LINDA huku akionekana kuwa na hasira Sana
BEN anaamua kumsogelea na kujishusha akaamua kupiga magoti kumbembeleza "Sawa naamua kukubali kosa nisamehe Mke wangu kipenzi nakupenda najua unajua siwez kukusaliti "
"BEN acha kuniigizia Mkeo "Aliongea LINDA
"Mke wangu nakuahd Kama nitakukosea basi amua lolote lile uwezalo
"Unanifanyia kusud kwakuwa unajua nakupenda
"Najua hilo Mke wangu ndo maana nimeamua kukupigia magoti kuomba msamaha
"Sawa umeshajua Mimi ni mdhaifu kwako kila ukikosea unakimbilia kuomba msamaha kwakuwa unajua siwez kukataa sawa utumie udhaifu wangu "Aliongea LINDA kwa uchungu huku machozi yakimtiririka
Baada ya siku kadhaa kupita LINDA akiwa seburen anaonekana kuna kitu anakitafuta pale seburen baada ya kutafuta kwa muda na kuonekana kukikosa aliamua kuchukua simu yake na kumpigia Mume wake hili aweze kuuliza
Katika maeneo ya Gesti BEN alikuwa ameingia Bafuni kuoga na kitandan amemwacha Kimada wake TABU ,Simu ilikuwa ikiita TABU alinyanyuka kitandan na kwenda kwenye dressing kuichukua na kuangalia ni nan anaye piga alipoona ni Mke wa BEN aliirudsha LINDA alipoona simu haipokelew akaamua kupiga tena TABU alipokuwa anataka kurud kitandan akaona simu tena kwa mara nyingine inaita alimua kuipokea "Nikusaidie nini mbona hamtulii majumban kwenu Asubuh yote hii unampigia simu kakwambia harud nyumban au unatafuta matatzo (Alipokea TABU kwa kusema maneno hayo
"We nan unapokea simu ya Mme wangu !!!? Aliuza LINDA
"Mke mwenzio
"Tafadhar usinitanie najua mume Wangu yupo kazin kama wewe ni mfanyakaz mwenzie naomba niongee nae Mara moja
"Dada sikujui hunijui Ila mume Kama hakuwah kukwambia shukuru nimekwambia na hapa niko nae Gesti
"Eti nini !
"Ndo ivo tunakula raha tu Kama kakwambia yupo kazn kaz Gan za saa kum na mbili
LINDA alikata simu na kwenda kukaa kwenye kochi huku akitokwa na machozi
TABU alipokuwa anairudsha simu BEN nae akawa anatoka Bafuni
"Vipi ulikuwa unaongea na nani ? Aliuliza BEN
"Mkeo
"Kwenye simu yangu ??!
"Ndiyo kwani kuna ubaya
"Umemwambia nini "BEN akionekana kupanik
"Nimemweleza ukwel kwann tuendelee kujificha
"TABU huu siyo wakat wa utani naomba usinitafutie tabu Kama jina lako
"Mmh! Sasa nikutanie nalipwa au nimemwambia yupo na mke mwenzie Gesti au nimekosea
BEN alimvamia TABU na kuanza kumpiga vibao
"BEN unanipiga Mimi kwaajil ya huyo mke wako Kama hukunipenda kwanini ulinambia tukutane
BEN alivaa nguo zake haraka haraka huku akiwa amejawa na hasira "Ole wako kitokee kitu chochote kile TABU nitakuonesha "Aliongea BEN kwa hasira huku akiondoka
"Mtu mzima hatishiw nyau kwenda kulee hapa utakuja tu mkeo mkeo ungempenda ungeendekeza umalaya
LINDA aliamua kuondoka na kwenda nyumban kwao
_______________
STORI YA MAPENZI; MALKIA WA JELA SEHEMU YA PILI .................................. "Mimi ni mkeo hata ingekuwa usiku wa manane wewe niamshe uniage nijue kabisa kweli unakurupuka tu asubuh unaondoka hata ujumbe basi ungeandika nao umeshindwa "Baby nimekuelewa nisamehe basi nitafanyia kazi BENSON anajarbu kumbembeleza kwa kusogea na kupeleka mikono yake taratibu na kumshka LINDA kiunoni kwa nyuma na kumbusu shingoni "Baby sikujua Kama nitakuudh kuondoka bila ya kukuambia nisamehe nakuahd hata nikiwa naenda choon lazima nikuage "Hahahah anaangua kicheko "Unafrah nini sasa ? "Ushaanza matan yako chooni ukienda Mimi hata usiniage "Utajua nimeenda wapi Kama nisipofanya hvo "Sitak " wanacheka wote wawili Baada ya muda LINDA aliandaa chai na kuweza kukaa katika meza ya chakula na kunywa Wiki moja baadae BENSON akiwa seburen peke yake mkewe akiwa ameondoka ameenda nyumban kwao Mara moja kusalimia BENSON aliamua kuitumia nafas ile kumpigia simu kimada wake na kuongea naye kabla ya LINDA kurud nyumban "Halloo! Baby ! Alipokea simu kimada huku akitoa saut lain na nyororo "Hallo ! Baby nambie "Safi nimekumith ile mbaya BEN wangu "Hunishind Mimi "Unanitania.... kweli Baby ? "Ndiyo kwanini nikuongopee nimeimis Sana ile mechi ya siku ile ulinifanya nione sinto maliza mchezo niliona uwanja mkubwa "Hahahaahah Ikasikika saut ya kicheko "Nilihisi kufa kufa "Amna bhana usingekufa woga wako tu kufa huwez kufa ila cha moto lazima ungekipata "Aa sikufich mke wangu anasubir we mtoto kibokoooo lini tena ligi yetu ya ugenini ? Muda wako Uwanja wako sikuzuii kuja kufanya mazoez afu mechi kwa mkeo "Hahahahah BENSON akaangua kicheko "Baby hata ukitaka sahv tutafanya hata kwa kutumia "whatsapp" voice note "Hahahah ndo maana nakupendaga Bab..................Kabla hajamalizia kuongea LINDA alifungua mlango BENSON alistuka na kuikata simu LINDA alibakia kasimama pale mlangon huku akimtazama Mumewe na kuanza kudondokwa na machozi Mkoba aliokuwa ameubeba aliuachia na kuuangusha chin "BABY umewah nilijua utachelewa " Huku akionekana kuwa na wasiwasi Alinyanyuka na kutaka kumsogelea alipokuwa "BENSON naomba usinisogelee "akamzuia kwa ishara ya mkono "Mbona sielew Nyumban wazima mbona hukuondoka hivo afu umewah kurud kuna tatzo kwani "Malaya mkubwa wewe Endelea kuongea na simu uliyekuwa unaongea naye nimesikia kila kitu "Nan ? Mimi nilikuwa naongea na DAVID ananieleza habar za NITTY "Mwanaume huna shukran BEN ni mangapi nimekufanyia kumbe ndo unavyo niongelea kwa hao Malaya zako "LINDA mke wangu kwanini tugombane nilikuwa naongea na DAVID jarbu kunielewa Nakupenda hakuna mwingine zaid yako "Mwongo mkubwa kwanini nilipoingia hukuendelea kuongea ukakata simu "Tulikuwa tumeshamaliza maongez "Ahsante kwa kunidanganya " Kumbe LINDA alikuja na DAVID ,DAVID alikuwa kwa nje akiwasikiliza akaona bora aingie alipoingia BEN aliishiwa nguvu na kuinamisha uso chin huku akijarbu kumtizama mkewe kwa kuibia ibia "Endelea kuniongopea siumezoea haya ulokuwa unaongea nae huyu hapa Endelea BEN... LINDA kwa hasira alimfuata BEN na kuanza kumpiga mingumi huku akilia kwa uchungu DAVID alimshika LINDA na kuomba wasigombane Alipowaamua aliamua kuwaacha kwa muda watulie kwanza baada ya robo saa kupita DAVID akamgeukia BEN na kutaka aseme alikuwa anaongea na nan "DAVID sema ukweli " "Mimi nilikuwa naongea na Dada yangu alinipigia kunijulia hali "Unamwon a alivyo mwongo Dada yako gani umwambie maneno Yale BEN niambie "kwa jazba huku akijarbu kutaka kunyanyuka alipokaa "Aaa shemej punguza jazba Mimi nipo hapa kila kitu kitaisha BEN Una uhakka "Ndiyo Kwanini nimwongopee amesikia vibaya tu "Shemej huenda ikawa ni kweli jaribu kusahau hili "DAVID unapendelea au kwa kuwa BEN ni mwanaume mwenzio Ahsantee LINDA Alinyanyuka na kuondoka kuelekea chumban "Kaka bora hata ulivyokuepo sijui ingekuaje Leo "BEN punguza hata Kama Una kimada nje hapa ni nyumban kwako paheshimu ukitaka kuongea nae Hakikisha mkeo kaenda mbali "Saw a kaka "Mi nilipita kukusalimia nilikutana na mkeo kwenye folen nikaon a bora Nam nipite kukuona kwahyo Mimi nafikir nimeshakuon a naondoka jarbu kumpoza mkeo "Haina shida BEN alimtoa DAVID mpka nje na kuweza kuagana kisha akarud na kuingia chumban alimkuta mkewe amejilaza kitandani kifudifudi amelalia mto huku akiwa Analia"LINDA mke wangu kwanini unapenda kujiumiza kwa vitu ambavyo siyo kwanini Mimi na wewe tugombane kwa vitu vidogo "Aliongea BEN LINDA alijigeuza na kunyanyuka pale kitandan akaanza kuzunguka mule chumban huku na kule "Unajua sikuekewi sasa unapozunguka hivi unamaanisha nini ? Alirudia tena kumwuuliza baada ya kuona hajibiw "BEN lazima utaona ni jambo la kawaida kwasababu lipo kwangu ila ipo siku BEN unajua Mimi na wewe tumetokea wapi siyo kwamba hujui unajisahau Sana BEN "Aliongea LINDA huku akionekana kuwa na hasira Sana BEN anaamua kumsogelea na kujishusha akaamua kupiga magoti kumbembeleza "Sawa naamua kukubali kosa nisamehe Mke wangu kipenzi nakupenda najua unajua siwez kukusaliti " "BEN acha kuniigizia Mkeo "Aliongea LINDA "Mke wangu nakuahd Kama nitakukosea basi amua lolote lile uwezalo "Unanifanyia kusud kwakuwa unajua nakupenda "Najua hilo Mke wangu ndo maana nimeamua kukupigia magoti kuomba msamaha "Sawa umeshajua Mimi ni mdhaifu kwako kila ukikosea unakimbilia kuomba msamaha kwakuwa unajua siwez kukataa sawa utumie udhaifu wangu "Aliongea LINDA kwa uchungu huku machozi yakimtiririka Baada ya siku kadhaa kupita LINDA akiwa seburen anaonekana kuna kitu anakitafuta pale seburen baada ya kutafuta kwa muda na kuonekana kukikosa aliamua kuchukua simu yake na kumpigia Mume wake hili aweze kuuliza Katika maeneo ya Gesti BEN alikuwa ameingia Bafuni kuoga na kitandan amemwacha Kimada wake TABU ,Simu ilikuwa ikiita TABU alinyanyuka kitandan na kwenda kwenye dressing kuichukua na kuangalia ni nan anaye piga alipoona ni Mke wa BEN aliirudsha LINDA alipoona simu haipokelew akaamua kupiga tena TABU alipokuwa anataka kurud kitandan akaona simu tena kwa mara nyingine inaita alimua kuipokea "Nikusaidie nini mbona hamtulii majumban kwenu Asubuh yote hii unampigia simu kakwambia harud nyumban au unatafuta matatzo (Alipokea TABU kwa kusema maneno hayo "We nan unapokea simu ya Mme wangu !!!? Aliuza LINDA "Mke mwenzio "Tafadhar usinitanie najua mume Wangu yupo kazin kama wewe ni mfanyakaz mwenzie naomba niongee nae Mara moja "Dada sikujui hunijui Ila mume Kama hakuwah kukwambia shukuru nimekwambia na hapa niko nae Gesti "Eti nini ! "Ndo ivo tunakula raha tu Kama kakwambia yupo kazn kaz Gan za saa kum na mbili LINDA alikata simu na kwenda kukaa kwenye kochi huku akitokwa na machozi TABU alipokuwa anairudsha simu BEN nae akawa anatoka Bafuni "Vipi ulikuwa unaongea na nani ? Aliuliza BEN "Mkeo "Kwenye simu yangu ??! "Ndiyo kwani kuna ubaya "Umemwambia nini "BEN akionekana kupanik "Nimemweleza ukwel kwann tuendelee kujificha "TABU huu siyo wakat wa utani naomba usinitafutie tabu Kama jina lako "Mmh! Sasa nikutanie nalipwa au nimemwambia yupo na mke mwenzie Gesti au nimekosea BEN alimvamia TABU na kuanza kumpiga vibao "BEN unanipiga Mimi kwaajil ya huyo mke wako Kama hukunipenda kwanini ulinambia tukutane BEN alivaa nguo zake haraka haraka huku akiwa amejawa na hasira "Ole wako kitokee kitu chochote kile TABU nitakuonesha "Aliongea BEN kwa hasira huku akiondoka "Mtu mzima hatishiw nyau kwenda kulee hapa utakuja tu mkeo mkeo ungempenda ungeendekeza umalaya LINDA aliamua kuondoka na kwenda nyumban kwao _______________
Artikel Terkait
CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA KWANZA (01) Ilikuwa alfajiri moja nyepesi, katika jiji la dar-es-salaam, katika mtaa mmoja tulivu sana mbezi beach, dio kwanza nikama pilika zilikuwa zinaanza, yalionekana magari machache ya kifahari, yakikatiza kwenye viji barabara vya mtaa, na kupoteea barabara kuu, watu wakikwep foleni kwa kuwai makazini na mashuleni, au sehemu mbali mbali za kijamii, mapema namna hii, huku watu wachache walio tembea kwa miguu wakionekana wakitembea haraka kuelekea barabarani, Ndani jumba moja la kifahari lililo zungukwa na uzio(fensi) wa ukuta mkubwa, ilisikika sauti ya msichana mmoja, mrembo mwenye asili ya Kihindi akiongea na mama yake, ilionekana alikuwa anataka kutoka. "mama mi naondoka naenda shule, maana kuna mitihani muhimu nawahi ingekuwa bila ya hiyo mitihani nisingeenda" alisikika binti mwenye sauti kinanda, akimwambia mama yake, ambae pia, ni mwenye asili ya Kihindi,japo alionekana ni mama wa makamo, lakini akika alifanana na binti yake., maana unge weza kuona uzuri wa mama huyu, japo tayari alisha kuwa mkubwa, "basi haya, chukua gari hiyo nyeusi, uwahi mwanangu" alisema mama huyu huku anawonyeshawanae funguo ya hili gari alilo mtajia, "hapana mamy, ntaomba lifti huko huko, leo sijisikii kuendesha" alijibu binti mrembo, huku akichukuwa begi lake juu ya meza na kuanza kuondoka, akiufwata mlango mkubwa wa kutokea nje. "haya basi baadaye mwanangu, jitazame huko uendako" aliongea mama huku anamsindikiza kwa macho binti yake, ambae toka akiwa mdogo amekuwa nae makini sana, ungesema amezaliwa peke yake, "ok mumy" alijibu binti chotara, huku anainua mkono wake na kuchezesha vidole, akimaanisha ana mpungia mkono mama yake, kisha akatoweka. Naam huyu ni binti mrembo NIRAM, ni binti wakihindi, mwenye sura nzuri ya kuvutia, macho ya duara, pua iliyochongoka vizuri, mwenye midomo mipana ambayo kila anapo tabasamu, basi uacha vijishimo mashavuni mwake, alikuwa na urefu wa futi tano, na pointi kadhaa, kifua cha wastani na tumbo dogo, kiuno chake kilibeba makalio ma nene kihasi na pia, vi hips vya kumwagika vilivyojazia na kuchomoza pembeni, vilizidi kumpendezesha, asa anapokuwa katika mwendo, kiufupi mdau wa story hii, ilikuwa si rahisi upishane nae, ushindwe kumgeukia, iliuone uumbaji. Huyu anaitwa Niram Popat, baba yake ni mfanya biashara mkubwa, na kwa sasa yupo nchini Uingereza, kwa shughuli zake za kibiashara, binti huyu akualiwa peke yake, Niram alikuwa na kaka yake, ambae kwa sasa yupo chuo kikuu cha Indira Gandhi nchini india akijichukulia masters yake, kifupi katika familia yao wamezaliwa wawili tu! yani yeye na kaka yake, Niram alipendwa kuliko kawaida. Hiyo ndo historia fupi ya niram, ebu tuendelee na kisa hiki cha Chaguo langu, Niram alitembea taratibu akiongozana na watu waliokuwa wanaelekea huko kwenye kituo cha dala dala, dakika chache baadae, Niram alifika kituoni, nakuwakuta watu wengi wakisubiri usafiri,binti huyu, alijitenga pembeni kabisa na abiria wengine, usafiri ilionyesha ulikuwa wa shida sana siku hiyo, maana magari yalifika pale yakiwa yamesha jaa, hivyo waliofanikiwa kupanda, walijibana kama nyanya kwenye matenga, Niram alijikuta ana kumbuka gari ambalo amelikataa nyumbani,”haaa, kwanini niliamua hivi?” alijilahumu binti huyu mzuri, ambae asilimia tisini ya wanaume waliokuwepo pale, walikuwa wanamkodolea macho, wakisanifu uumbaji, Lakini wakati anawaza hayo,mara ghafla ilisimama range nyeusi, mbele yake na paka shushwa vioo, ilionekana sura moja matata sana, ya mwanaume mtanashati, hakika alifaa kuitwa handsome wa Kiafrika "hellow" yule kijana ndani yagari alimsabahi Niram, nae akajibu kwa kichwa, yule jamaa akatabasamu kidogo, "naweza kukupa lifti? Aliuliza kijana yule. na Niram akuwa mbishi, aliitikia kwa kichwa kama kawaida yake, hapo ukafunguliwa mlango Niram akaingia. na kufunga mlango, sasa akawa ametulia kwenyeseat yake, huku macho mbele, akitegemea kuona gari linaondoka, na maswali yanaanza, lakini zika pita dakika kadhaa na gari halikuondoka. Muda wote haku endesha gari, alikuwa ameduwaa, kumshangaa msichana alie ingia garini mwake. Alizidi kushangaa "sorry kaka mimi nashuka vituo vinne mbele ndipo ilipo shule yetu"aliongea niram. Maskini kijana yule aligutuka, akababaika huku anaondoa gari, "oooh! aaagh sawa unasoma shule ipi dada?" aliongea huku gari ikienda taratibu "shadhiliya slamic internation school" alijibu Niram, "ooh ile shule ya kiislam "aliuliza kijana. "yap! nasoma kidato cha tano pale" alijibu niram "ok mi mwenyewe nasoma pale st joseph international school kidato cha sita "alisema kijana "aah kumbe" alisema Niram kwa uchangamfu kidogo, akiona kuwa yupo na mwanafunzi mwenzie, "ndiyo ninaitwa Vincent, sijui naweza kulijuwa juna lako kama hutojali?" aliuliza Vincent huku anatabasamu, kidogo wengee lilianza kumtoka, "mimi naitwa Niram..” alisema Niram lakini kama alistuka kidogo, “ooh! kaka nishushe unapitiliza" aliongea niram kwa mshtuko "ooh sorry, kwa kweli" alijibu Vincent,huku ana peleka mguu wake wkulia katikati na kukanyaga bleack, akippunguza mwendo na kuweka gari pembeni ya barabara, kisha akasimama, Niram alishuka, na akashukuru Vincent kwa kupitia kwenye dirisha la upande aliokaa, na kuondoka zake. Vicent alibaki kaduwaa, maana alishangazwa na uzuri wa aina yake, kwa yule msichana. "daah nimesahau kuomba namba" alijilahumu Vicent, lakini hakuwa na lakufanya, akawasha gari akasepaaa. Anaitwa Vicent Ngosha, ni mtoto wa mzee Emanueli Ngosha mfanya biashara mkubwa nchini Tanzania na nje ya nchi.Vincent alikuwa ni mvulana wa kisukuma, mama yake ni muhaya, Vicent ni mtoto pekee kwenye familia yao, ni familia yenye uwezo mkubwa, baba yake alikuwa mkoani kibiashara, hivyo alibaki pale nyumbani na mama yake, pamoja na house girl, Vicent alifika shuleni akiwa na mawazo lukuki, “ok! mdau huu nimwanzo wa mkasa huu wakusisimua, ...... CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA PILI (02) ILIPOISHIA SEHEMU YA KWANZA : Anaitwa Vicent Ngosha, ni mtoto wa mzee Emanueli Ngosha mfanya biashara mkubwa nchini Tanzania na nje ya nchi.Vincent alikuwa ni mvulana wa kisukuma, mama yake ni muhaya, Vicent ni mtoto pekee kwenye familia yao, ni familia yenye uwezo mkubwa, baba yake alikuwa mkoani kibiashara, hivyo alibaki pale nyumbani na mama yake, pamoja na house girl, Vicent alifika shuleni akiwa na mawazo lukuki. ENDELEA......... Vincent alifika shule akiwa na mawazo kibao. Aliwaza kwamba alikutana na jini au mtu wa kawaida, hakika alikuwa hayupo sawa alishachanganywa na mtoto wa Kihindi, akujua afanye nini ili aweze kuwa karibu na binti yule, akika Vicent likuwa katika wakati mgumu, alijikuta anatembea bila kujielewaakinyoosha moja kwamoja mpaka darasani, “dah! nime kuwa mjinga sana, ninge omba namba, mbona demu alikuwa poa kabisa” alijilahimu Vicent, akiwa amekaa kwenye kiti chake, na kuegemea meza, kama vile anataka kulala, "hey! niggar vipi mbona umezubaa mwanangu?, yani tumekutafuta pande zote, mpaka kule bustanini, kumbe umekuja kujichimbia class, tena hata assemble ukuja" Vicent aligutushwa kidogo na kuinua kichwa kumtazama alie msemesha, japo sauti alisha itambua, kuwa alikuwa Richard, ni rafiki kipenzi wa vicent, nikama Vicent aliganda kidogo, akimtaza Richard, ambae alishangazwa na rafiki yake,Richard akageuka nakumtazama kijana mwingine alie kuwepo pembeni yake, "vipi Rich mbona leo amepoa sana, yani kama amemwagiwa maji, unanini wewe?" alidakia suma rafiki yake mwengine. maana awakumuelewa mwenzao, Vincent akujuwa amjibu nani kati yao, na awajibu nini, hivyo aliishia kutabasamu kisha akajikohoza kidogo, na kuanza kuwaambia "yani leo najiona kama nipo ndotoni, kwa nilichokutana nacho" ilikuwa sauti iliyo jaribu kuonyesha msisitizo wakile anacho kiongea, "hahahahaha! kashaanza sound zake huyu" alisema suma, huku wote wanacheka,kabla mmoja wao ajakumbuka jambo, "hoya! alafu nimekumbuka, Vannessa alikuwa anakuulizia" aliongea Richard, kama unge msikia unge juwa kuwa huyo Vannesa, alikuwa anainshu muhimu sana na Vicent, maana aliongea kwa msisitizo, "mmh! yani huyo Vanessa naomba usinitajie, maana leo ana nafasi ya kuzungumziwa hapa" alisema Vincent, ila kabla ya kuongeza neno, mara ikasikika "waoooh! jaman baby nilikutafuta huko nje kotesijakuona" wote watatu wakageuza shingo zaona kutazama upande wa mlangoni sauti iliko tokea, macho yao yaka mshuhudia binti mrembo wa ki afrika, alie kuwa anatembea taratibu kuja pale walipo kuwepo wakina Vicent, huyu ni Vanessa alie zungumziwa, “mpaka nikawa na wasi wasi kuwa leo auto kuja” aliongea tna Vanessa, kwa sauti iliyojaa furaha na mania moyoni, Wakati hiuo tayariwanafunzi walishaanza kuingia darasani, Vanesa alienda moja kwa moja mpaka kwa Vicent na kumkumbatia kwa furaha, lakini cha kushangaza kijana huyu akuonyesha ushirikiano, ushirikiano kwa mrembo Vanessa, "baby una nini leo?" alihoji vannessa.kwa mshngao huku anajitoa kwenye kumbatiao lake kwa Vicent, "sina kitu"lilikuwa jibu la mkato,toka kwa Vicent, "sasa kwanini huko hivyo?" aliuliza tena Vanessa, kwa sauti iliyoanza kubadirika na kunyongea, huku wezao wakiwatazama, yani Richard na Ismail wenyewe wana mwita Suma, “nimekuambia niko sawa, unielewi wewe unataka nikuambieje” safari hii Vicent aliongea kwa sauti ya juu, iliyo jaa ukali wa wazi, kihasi cha kulitikisa darasa zima, sekunde kadhaa, wtu wote kimya, wakigeuza shingo zao na kuwatazama wakina Vicent, kwa mshangao. Kitendo hiki akikuwashangaza walewanafunzi wenzao peke yao, ata Richard na Ismail, nao walishangaa, Vanesa alitanzana chini kwa aiu, maana macho yake haya kuweza kutazama, macho ya wanafunzi wenzake me darasani, tenamacho hayo yalishindwa kuya zuwia machozi, ambayo yalianza kumtoka, akika binti huyu, akashindwa kuendelea kusimama mbele ya mvulana ambe sikuzote ame nae karibu, hivyo akageuka na kuondoka zake, huku anakimbia, akielekea nje ya darasa, "una nini mwanangu, mbona kama umeurugwa?" alihoji Richard, huku suma akidakia "mbona si kawaida yako mshikaji wangu" akika wakina Suma walionekana kusikitishwa na kitendo kile, ambacho awakukitarajia, kutokana na ukaribu wa wawili awa, hapo Vicent alikuwa ametulia nikama anawaza jambo, kisha akainua usowake taratibu, "sikilizeni niwaambie washakaji, mimi toka zamani niliwaambia kuwa, Vanesa simpendi, nyie mkasema ooh! mkubalie sijuwi hooooh! mtoto mzuri yule, et! shule nzima wanamfukuzia, bahati imekuja kwako, mala ooh! sasa nimegundua leo kuwa, mwanamke ninaempenda yupo, tena nimemuona, kwa macho yangu" alijibu vincent.marafiki zake wakatazamana kwa mshngao, huku wakimsikia Vicent anaendelea, "leo nimekutana na mwanamke ambae naweza sema ni wa ndoto zangu, sijawahi kujihisi hivi kabla, ila kwasasa ndo naanza kuhisi nimependa kwa mara ya kwanza" Vicent alizidi kuwashangaza marafiki zake, lakini kabla ajawaeleza zaidi juu ya mtoto wa Niram, mara Mwalimu akaingia darasani, na mazungumzo yakaisha kwa muda huo. ****** Vanessa ni binti mmoja mzuri mwenye sura ya duara macho ya kusinzia ana kimdomo furahi hivi cha rangi ya pink, nyuma amefungashia balaha, kiasi cha kupendezwa na kunguo yoyote atakayo ivaa, kifupi kila mwanaume, iwe mtaani au hapa shuleni, alikuwa anammezea mate, na rangi yake ya chocolate ndo kabisa, ilichangia uzuri wake kwa kwa kihasi kikubwa, ikichangia na urefu wake wa wastani,ila binti huyu Vannesa alivutiwa sana vincent mpaka akawa anashindwa kujizuia, japo alikuwa akisumbuliwa na wanaume wengi hadi walimu ila yeye limfanya Vicent kuwa ndie mwanaume wa ndoto zake, Vannesa alijitahidi kufanya kila njia na ushwishi, mpaka akafanikiwa kumfata na kumwambia, ukweli kijana huyu, Ilikuwa ni vigumu kwa vicent kukubali, maana hakuwahi kumpenda msichana, na hakujua afanye nini, ila vishawishi vilimfanya akubali, kwa maana yeye aliona labda ndo inavyokuwa mapenzi yapo hivyo, japo alisumbuliwa na wanawake wengi, ila vicent akuwahi kujihusisha na msichana yeyote yule. Kwahiyo Vanessa ni mwanamke wake wa kwanza, kimahusiano, lakini leo tangu amekutana na Niram alijihisi tofauti, yani kama kuna kitu kina Uchoma moyo wake, hapo ndipo alipojua kuwa, kumbe sasa huku ndiko kupenda kwenyewe, maana ukiachilia kuwa alisha ona waschana wazuri wengi katika maisha yke, yaliki yule binti alimwingia sana moyoni mwake, na kuivuruga hakiri yake, Vanessa aliingia darasani kwao, huku akifuta machozi, kwakutumia kitambaa chakechepe, akiofia wenziewasije wakaona, na kugundua kuwa alikuwa analia, hilisiyo darasa ambalo Vincent yupo, maana walisoma madarasa tofauti, licha ya kuutamachozi na kujaribu kujizuwia kulia, lakini aikuwezekana, maana donge la uchungu lilikuwa lime laa shingoni mwa Vanessaalijikuta anashindwa na kuendelea kuangua kilio cha kwikwi, Vanesa aliwai kwenyekiti chake na kukaa, huku akijizima uso kwakuegemea kwenye meza, akizuwia na mikono yake miwili, ilimuuma sana binti huyu, akika machungu haya ya ghafla, sizani kama nitaweza kuya eezea, "nimemkosea au anipendi tena" alijiwaziwa kimoyo moyo, binti huyu, huku machozi yakizidi kutililika machonimwake na kulowesha mikono yake,mala akastuka kunamtu akimshika begani,aka jifutamacho ziharaka na kumtazama alie mshika begani, "Vanessa una nini, mbona unaonekana kama umetoka kulia" aliuliza Maria, rakifi yake na Vanessa, huku anakaa chini kwenye kiti chakee, pembeni ya Vanessa alimwangalia rafiki yake kwa macho yenye majonzi, hakika kama ungemuona usingetofautisha na mtu aliefiwa, alinyongea kupita kiasi."Maria sijui nimemkosea nini vicent amenikaripia kama mtoto mdogo" aliongea Vanessa kwasautia mbayo nikama kilio kilitaka kurudi upyaa, ila alijitahidi kukizuwia, akaendelea kuzungumza "nilimtafuta sana nje, sikumuona, baada ya kuzunguka kwa muda mrefu, ndo likanijia wazo la kumfata darasani kwao, hakika niliingia kwa bashasha ila nikapokelewa kwa hasira na dharau" mpaka hapo Vanessa alishindwa kuendelea nakuanza kulia kwa kwikwi, ilibidi Maria aanze kumbembeleza kwa kumpiga piga mgongoni, inaonyesha wanafunzi wengine awakujuwa kunacho endelea kwa Vanessa, maana kila mtu aliendelea na mambo yake,******** Mida ya saa nne, ndani ya viunga vya Shadhiliya slamic internation school, yani shuleni kwa kina Niram, mambo yalikuwa shwari, ulikuwa wakati wa mapumziko, wanafunzi walikuwa wametawanyika kwenye viunga vya shule, mida hii binti mrembo Niram, alikuwa na rafiki zake watatu ndani ya canteen ya shule, wanapata chai, mara Niram akawa kama amekumbuka jambo fulani. "jamani mwenzenu leo nimepewa lift na kijana mmoja wa Kiswahili, lakini mzuri sijapata kuona" kabla ajamaliza kuongea binti Niram, akadakia shira huyu nae ni jamii ya kina Niram yani ni muhindi pure kasoro, hawa wengine hajra na Salma, ni tofauti, wakati Salma alikuwa mpemba mweusi, ila Hajra alikuwa Mwarabu kabisaaaaa, "ahhhhh usitake kusema umempenda mswahili, hivi mzee Popat uta mbebea mbebeo gani?, si ata kuchinjaa" alisema Shira, na hapo vikafata vicheko kwa woteee, kasro Niram peke yake ambae alisema, "wala sina mpango huo, ntampeleka wapii mimi, ila nimemsifiatu! sababu katika wavulana niliowai kuwaona, kwa hapa mtanzania, yule kaka ni handsome sanaa" alisema Niram huku anawaangalia marafiki zake, ambao wakakubaliana nae, kwakiikisa vicwavyao juu chini, na wakati huo kengele ya darasani ikagongwa, wakasimama tayari kwa kuanza safari ya kuingia darasani itaendelea ...... ... Read More
Story - - - - - NI WEWE TU PENINA. BY GIVAN IVAN PHONE & WHATSAPP____0769673145 Karibuni tuianze story yetu hii mpya yenye kusisimua iliyojaa visa mbali mbali kuhusu mapenzi. Sehemu ya kwanza (1) Mapenzi ya vijana wawili walionza kupendana toka wakiwa wadogo mpaka Sasa wakiwa na umri wa miaka 25 kila mmoja, yalikuwa yakizidi kukolea kila siku na kuwa matamu zaidi na zaidi. Vijana Hawa ni Frank pamoja na Penina. "nahisi kuvurugwa nahisi kufa kufa yaani najiona kama napepea juu juu kwa jinsi navyompenda mpenzi wangu Penina." alikuwa frank akiongea maneno hayo mbele ya wazazi wake pamoja na mdogo wake Wa kike aitwaye Angel. "na siku si nyingi utakuwa chizi wewe sio kwa kupenda huko kaka yangu." akaongea Angel kumuambia Frank. "acha niwe chizi tu mdogo wangu, lakini sio chizi wa kutembea uchi barabarani bali chizi wa kupenda." akaongea Frank maneno hayo na kuwafanya wazazi wake wacheke sana. "lakini mwanangu Sasa inabidi mfanye taratibu mfunge ndoa Sasa." aliongea baba yake Frank. "Hamna shida baba usijali yote hayo yatafanyika muda mfupi ujao. " Akaongea Frank ambaye muda wote furaha ilijaa usoni mwake. *wakati huo huo Penina mpenzi wake Frank naye alikuwa katika moja saloon akitengeneza nywele zake ikiwa ni maandalizi ya kwenda kukutana na mpenzi wake Frank. " Dada nitengeneze vizuri tafadhali maana napenda muda wote niwe navutia mbele ya mpenzi wangu." aliongea Penina kumwambia mwanadada aliyekuwa akimtengeneza nywele. "usijali dada nitakutengeneza vizuri mpaka mwenyewe ufurahi." Dada yule akamjibu Penina na kumfanya atabasamu. Baada ya dakika kadhaa Penina alimaliza kutengenezwa nywele zake na moja kwa moja akazama kwenye pochi yake na kutoa simu yake, kisha akatafuta Jina lililoandikwa my love Frank na moja kwa moja akazipiga namba hizo. * Frank akiwa bado anaongea na wazazi wake ghafla simu yake ilianza kuita, akatoa na kuangalia mpigaji ni Nani. Frank alianza kutabasamu baada ya kukuta mpigaji ni Penina kipenzi cha moyo wake. "haloo mke wangu mtarajiwa mambo vip?" akaongea Frank baada ya kupokea simu. "poa tu mpenzi wangu nimekumiss hadi nahisi kizunguzungu." akajibu Penina. "Asante mpenzi wangu yaani kuachana Jana tu ndio kunimiss hivyo?" " yeah nimekumis sana hebu jiandae nakupitia Sasa hivi tukale bata kidogo. " akaongea Penina kumwambia Frank. " waoow ok najiandaa Sasa hivi utanikuta tayari my love." akajibu Frank na simu ikakatwa. Frank aliwaacha wazazi wake pale sebuleni kisha yeye akaenda kujiandaa kwa ajili ya kutoka na mpenzi wake. Penina naye baada ya kukataa simu aliingia kwenye gari yake nyeupe aina ya rava4 na kuanza kuelekea nyumbani kwa Frank. Tumfahamu Penina vizuri. Penina ni mwanamke mrembo sana aliyebarikiwa na Mungu kuwa na kila kitu kizuri katika mwili wake. Popote pale Penina alipopita aliacha gumzo kwa wanaume ambao walikuwa wakimmezea mate. Penina ametoka katika familia ya kitajiri yenye watoto watatu, wawili wa kike na mmoja wa kiume ambao ni Nolan, Penina na Irene. Penina amefanikiwa kusoma mpaka elimu ya juu kabisa na kufanikiwa kuwa mfanyabiashara mdogo anayechipukia kwa kasi sana. Penina alianza uhusiano wa kimapenzi akiwa kidato cha tatu, na alianza uhusiano na kijana aliyeitwa Frank ambao mpaka Sasa wapo pamoja. Lakini kitu kimoja ambacho kanalitia dosari penzi tamu kabisa la Penina na Frank, ni baba yake Penina kutopenda mwanawe aolewe na Frank. Baba yake Penina hakutaka kabisa mtoto wake aolewe na Frank, yeye alitaka mtoto wake aolewe na mzungu kutokana na uwezo wao wa kipesa. Mama yake Penina pamoja na Nolan kaka yake Penina ndio Watu pekee waliokuwa wanayaunga mkono mapenzi ya Penina na Frank katika familia yao. Lakini Irene mdogo wake Penina pamoja na baba yake Penina ndio watu pekee ambao walikuwa hawataki kabisa kuyaona mapenzi ya Penina na Frank yakiendelea. * Frank yeye anatoka katika familia yeye hali ngumu kimaisha, hawakuwa na uwezo hata wa kuwa na nyumba nzuri kama wenzao. Frank aliishia kidato cha pili kutokana na wazazi wake kutokuwa na uwezo wa kumuendeleza zaidi. Kadhalika pia Angel mdogo wake Frank naye aliishia darasa La saba kutokana na Wazazi wao kutokuwa na uwezo wa kuwaendeleza zaidi. * Baada ya dakika kadhaa Penina aliwasili nyumbani kwa kina Frank, akapaki gari yake pembeni na kushuka Kisha akaingia katika nyumba ya kina Frank ambayo ilikuwa imechoka Sana. "waoow mkwe wetu karibu Sana." mama yake Frank ndio alimpokea Penina kwa furaha Sana. "Asante Sana mama yangu nimekaribia." akajibu Penina huku akiketi pembeni ya mama yake Frank. "eeh mwanetu lete habari." akaongea mama yake Frank. "Sina hata mpya nimekuja kumchukua mtoto wenu." akajibu Penina. Na Muda huo huo Frank akajitokeza akiwa tayari ameshajiandaa. Licha ya umaskini uliopo katika familia Yao, bado Frank alijitahidi Sana katika kuupendezesha mwili wake ili aweze kuendana na mpenzi wake Penina ambae Muda wote alikuwa mtu wa kupendeza tu. "waoow my love mwaaa." Penina ndio alinyanyuka na kumkumbatia Frank na kumuachia busu Zito la shavu. Frank naye hakuwa nyuma alimpokea mpenzi wake kwa furaha pia. Penina pamoja Na Frank waliaga na kutoka nje, wakaingia kwenye gari na kuondoka. "tunaelekea wapi Sasa mpenzi wangu?" akahoji Frank. "surprise my love sikuambii tunaelekea wapi." Penina akamjibu Frank huku akitabasamu. "haya bhana bas nafunga macho mpaka tufike." akaongea Frank na kumfanya Penina azidi kutabasamu.* Katika bar moja iliyopo maeneo ya sinza kikao kimoja kilikuwa kikiendelea, na huku kilichokuwa kikipangwa Katika kikao kile ni namna ya kulivunja na kuliharibu penzi la Penina na Frank. Mzee Joel ambaye ni baba yake Penina, pamoja na Angel ambaye ni mdogo wake Penina pamoja na vijana wengine watatu wa kiume na mmoja wa kike, ndio waliokuwa wahusika wakuu wa kikao kile. .... Itaendelea ... Read More
CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA SITA (06) ILIPOISHIA SEHEMU YA TANO: Siku ya pili, vicent alitoka mapema nyumbani, aliwahi shule kabla hata ya rafiki zake. Hii yote ni kutokana hata usingizi haukupatikana,kutokana na mawazo aliyo nayo. Alikuta baadhi ya wanafunzi wapo darasani, Alifika akakaa kwenye kiti na kufungua begi,kuchukua kitabu na kuanza kusoma. Ila hata sijui nini kilimtuma kutazama mbele maaana alijikuta anatoa macho. ENDELEA....... Alijikuta Anatoa macho, baada ya kuona,marafiki zake nao wamewahi shule. Aiseeee vicent alichekaaaa sana, mpka akajishika tumbo. "hadi nyinyi mmewahi leo aaah kweli mtihani siyo poa".aliongea vicent huku anawatazama kwa zamu. "mimi mwenyewe sijaamini nilivyo kuona ndo maana nikasimama mlangoni nihakikishe ni wewe au hahhhhhah".aliongea Richard huku anaelekea kule alipo vicent.ila cha kushangaza suma akuchangia neno zaidi ya kuachia tabasamu na kutembea kwenda walipokuwa wenzake. "aiseeee kama tuliambizana yani"aliongea tena vicent. Hapo suma ndo na yeye akanyanyua,mdomo wake na kuongea. " hivi unajua kwanini nimeshindwa kuongea chochote?,nikwasababu naona uchuro hapo nje nimekutana na rich, hapa nakuona wewe, nikawa najiuliza hivi hawa waliambizana nini mimi wamenichunia ila nimewabamba".aliongea suma,huvu anavuta kiti anakaa. "hii ili iweje sasa imetokea tu"alijibu richard. "sisi hatuwezi kukufanyia hivyo kwasababu sote ni wamoja". Alisema vicent, suma hakuwa na neno. " oyaa tusomeni basi kabla muda wa kwenda mstalini aujafika"aliongea tena vicent. "poa mwanangu umeongea point" alijibu suma.basi kikapita kimyaa,kila mtu alifanya yakeee kwa muda huo. ******* Mwezi ulipita,hatimae miezi, na si vicent, wala niram aliye kumbuka kama walishawahi kuonana. Basi ilikuwa weekend, moja walionekana marafiki, watatu wakiwa wamesimama stendi ya mabasi,si wengine bali ni vicent, richard na suma wakiwa wamevalia nguo za nyumbani.ilibaki kama wiki mbili wafanye mtihani. Ilionyesha kuwa walikuwa wamelewa kwenye maongezi sasa sijui vicent, walikuwa wanasubiri usafiri maana vicent hakuwa na gari siku hiyo. Mara gaflaa walishtushwa na sauti, nyororo iliotokea,barabarani. "vicentiiiiiiiiiiiii" ilikuwa sauti ya niramu, aliekuwa ndani ya range nyekundu, huku akiwa amependa,kupindukia wanasemaga kadamshi, ile mbayaaaa. Wote macho yalikuwa mbele,ila hakuna mtu alieshtuka kama vicent, maana akutegemea kuonana na binti yule ana muwaza siku zote. Na ilikuwa muda Awajaonana. Kiukweli vicent, moyo ulikuwa unampenda mbio vibaya.ila alijikaza, huku nyuma suma pamoja na richard, aisee!! Macho yaliwatoka maana walishindwa kuelewa, wanae muona machoni mwao, ni jini au malaika. Vicent alijikongoja mpaka kwenye dirisha la gari, na kumsababishia niram. " mambo niram siamini kama ni wewe, kumbe unani nakumbuka? ".alijikuta anaongea mfululizo vicent huku akiuliza, swali humohumo. "poa vicent, nakukumbuka sana vp leo huna usafiri? Maana naona kama mpo wenyewe mnasubiri usafiri? ".aliuliza niram,huku macho akiwaelekezea wakina rich. "aaah ndiyo tunamsubiri dereva tax mmoja hivi,katuambia hayupo mbali".alijibu vicent huko akiangalia huku na kule kama anaetafuta kitu. "haah kwani mnaelekea wapili niwape lifti?maana mimi naelekea mbezi"aliuliza niram. Vicent akapiga mahesabu ya haraka,alafu akaongea. "aaah! Wale wanarudi nyuma ila mimi naenda kunduchi" alijibu vicent. Ila wadau ngoja niwaambie kitu, vicent ameongopa, kwasababu wenzie wanaenda kawe sawa yeye anaenda kunduchi, ila njia ni ileile wameachwa wakina suma, yeye angeendelea mbele, ila aliamua kusema vile ili aweze, kutupa ndoano Kiulaini. Tuendelee, basi niram akamwambia "basi twende nikupe lifti waage wenzio".vicent akachomoka na kuwafata, wenzie alimkuta suma anashauku si mchezo. " vipi yule ndo yule demu uliesema? Na anaelekea wapi ili atupe lift basi kama vipi" alijikuta anaongea maneno,mfululizo na swali juu. "hamna aendi huko kaniambia nimsindikize kariakoo".aliongea vicent huku anageuka nyuma, akagongana macho na niram,wote wakatabasamu. "duuuh mwana kwahiyo umetuacha? ".aliongea richard huku anakazia macho kwenye gari. "aaah aina jinsi ila chukueni hii mpande tax".alisema vicent huku anazamisha mkono mfukoni na kutoa noti tatu za elfu kumi akamkabidhi suma. Suma alizichukua na kuzitia mfukoni. "oyaaa Usikose kutupigia ukifika home"alisema rich. Na suma akadakia. "ndiyo utupe data zote maana duuuh! Mpaka nakuonea wivu".vicent hakutia neno aliishia kutabasamu huku Anaendelea kutembea, basi aliingia ndani ya gari, huku ukimya mwingi ulitawala.vicent akaona avunje ukimya, "basi nilijua utanisahau kabisa".aliongea Vicent Huku ametoa tabasamu hafifu usoni mwake, Huku macho yanatazama mbele. "Ooooh!!Hapana siwezi kukusahau,mtu muhimu Kama wewe Kwa ule Msaada wako ".aliongea Niram,huku anamwangalia Vicent, macho yakakutana, wote wakatabasamu, Niram akageuka mbele na kuendelea, kuushika usukani akizidi kukanyaga mafuta. "hahhhhah!! Ni kweli niram lakini Siyo wote wanao kumbuka fadhila".aliongea Vicent ,Huku kimoyomoyo akiomba wasifike haraka. "haaahhh sawa bwana Wala ujaongopa, ".aliongea niram,huku akizidi kuuchapa mwendo, na bahati nzuri hakukuwa na foleni. "niram nikuombe kitu Kama hutojali? ".aliuliza Vicent Huku amemgeukia kabisa, aliongea Kwa sauti nzito, tens yakubembeleza. "usijali Kama kipo Ndani ya uwezo wangu ntakupa".alijibu niram. Vicent hakaona asizubae Sana, akasema alilokusudia."nilikuwa naomba unisaidie namba yako ya simu ili niwe nawasiliana nawe hata kukujulia Hali,maana tushakuwa marafiki".aliongea Vicent,kwa umakini wa hali ya juu ili asije kukosea step,akamkwaza Niram. " Ooooh!! Wala usijali Kwa hilo".alisema niram, huku anamtajia namba zake. Vicent aliziandika kwenye simu yake. " asante sana".alishukuru vicent. "asante nawe kwa kushukuru".alijibu niram, mara ikawa kama vituo viwili vicent ashuke. "sasa niram mie nashuka hapo kituo kinachofuata utaniacha hapo" aliongea vicent, lakini kama ungemuona moyoni mwake, alichukia kupita kiasi, alitamani wazunguke mpaka alfajiri. Duuuuh kweli mapenzi siyo poa wadau. "haaah ni hapo oky sawa"alijibu niram, na alipofika, akakanyaga break, na kusimamamisha gari. "oooh!!asante sana umenifaa mungu akufikishe salama".aliongea vicent huku anafungua mlango wa gari na kushuka. "haya asante ufike salama pia".alijibu niram, akawasha gari na kuishia, vicent alibaki anampungia mkono, mpaka alipo ishia. Kiukweli ile siku aliiona ya bahati sana kwake, hakika alikuwa na furaha mno. Alifika kwao. Akagonga geti likafunguliwa, alikuta mlinzi akamsalimu, na kuingia ndani hakumkuta yeyote ndani zaidi ya house girl. Alimsalimia akajitupa kitandaniii , pwaaaaaaah!! Aliangalia sana juu vicent, hakika kuwa na namba ya niram,kwake ilikuwa ni furaha tupu. ********* Vanessa alikuwa mezani wakipata chakula cha usiku, maana leo ilikuwa weekend kwahiyooo alikuwa mwenyewe jikoni, ila leo mawazo yalipungua kwani mawasiliano yalikuwa kama zamani na hadi asubuhi ya siku hiyo, vicent alimuaga kuwa atatoka na wakina richard. Mara ghafla alishtukia, akizibwa macho. "mmmh juliana nini bwana,ebu acha mzaha njoo ule"aliongea vanessa. " mmmh dada kwahiyo wewe mtu wako wa karibu ni Vanessa tu? ".aliuliza kwa manung'uniko Clara. Mdogo wake wa nne akitoka huyo ndo juliana, kumbuka wakiume ni wawili kwenye familia yao na ndio wakwanza na wapili. "hamna mamy wote nawapenda ila nilijua yeye, kaa chini ule mdogo wangu".aliongea Vanessa kwa sauti ya kubembeleza,huku akimvuta akae. Basi mambo yakaisha,walikula kwa furaha, wazazi na kaka zao hawakuwepo, walibaki wenyewe. ********* Niram alikuwa chumbani kwake akijisomea, wakati huo alikuwa ameshakula, alikuwa kitandani miguu kuegemeza ukutani, muda wote alikuwa mtu mwenye tabasamu usoni, kilicho mfurahisha akijulikani Mara ghafla simu ikaanza kuita...... Itaendelea CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA SABA (07) ILIPOISHIA SEHEMU YA SITA: Niram alikuwa chumbani kwake akijisomea, wakati huo alikuwa ameshakula, alikuwa kitandani miguu kuegemeza ukutani, muda wote alikuwa mtu mwenye tabasamu usoni, kilicho mfurahisha akijulikani Mara ghafla simu ikaanza kuita. endelea........ Mara gafla akaona simu inaanza kuita. Niram akaangalia mpigaji, akaona namba ngeni. " mmh! Atakuwa Nani huyu?".alijiuliza niram, alitafakari Sana maana sikawaida kupigiwa na namba ngeni, baada ya kutafakari kwa muda.akaamua kupokea. "hellow".aliitika niram. "hallow Niram huko poa?, Vicent hapa". Ilisikika sauti upande wa pili."oooh! Vicent nashukuru mungu niko poa sijui wewe ulifika salama? ".alijibu niram nakupachika swali. "nilifika salama niram hofu ilikuwa kwako".alisema vicent. "namimi nashukuru mungu nimefika salama".alijibu niram kwa sauti nyororo kabisa. ****** Vanessa alikuwa ndani kwake akaona mbona muda unaenda sana,na ajaona msg wala simu kupigwa kutoka kwa vicent. Alikaa akasubiri na kusubiri weeeeh lakini ikawa kimya. "mmmh!! Ina maana itakuwa ajarudi bado huko alipoenda"alijisemea mwenyewe, akaona muda unaenda lakini simu aipigwi. "mmh ngoja nipige"aliamua apige yeye, akachukua simu yake na kuipiga. Jibu alilokutana nalo ni NAMBA UNAYOPIGA INATUMIKA KWA SASA.. "mmmh saa tano hii au ndo amerudi hivyo anaongea na wenzie kuwa julisha kuwa amerudi?".alijiuliza jibu akakubaliana kuwa anawasiliana na rafiki zake. ****** Huku vicent akiwa anaongea, akaona kama kuna mlio wa simu nyengine kuingia akaiangalia , alipoona mpigaji kuwa ni Vanessa akaendelea kuongea. Simu iliita mpka ikakata. Waliongea mengi na baadae niram akaaga kuwa anahitaji kupumzika. Basi waliagana na simu ikakatwa. Baada ya hapo alipiga simu kwa Vanessa,huku Akiwa ameshaupanga uongo wa kumwambia. "hellow baby mbona kimya, na napiga unatumika?".aliongea vanessa mara baada ya kupokea simu. "aaah amna nilikuwa naongea na mzee maana mchana,hakuwa na nafasi ndo kunitafuta sasahivi".alijibu vicent kwa ujasiri wa hali ya juu,bila kubabaisha maneno. "oooh kumbe haya niambie mizunguko ilikuwaje? ".Aliuliza Vanessa huku alibadili mikao ya kila aina Hapo kitandani. "ilikuwa poa sema nimechoka sana".alijibu vicent huku akijifanya anapiga mihayo. "oooh basi pumnzika baba angu tutaongea kesho".aliongea Vanessa kwasauti fulani hivi ya madeko. "sawa mama ntakuchek kesho ulale salama"alimaliza kuongea vicent akakata simu. Alienda moja kwa moja bafuni akaoga, maana choo kilikuwa ndani kwake humohumo. Alipomaliza alitoka sebleni muda ulikuwa umeenea sana ila alikuwa bado ajala, alikuta msichana ameshaenda kulala,aliwasha taa ya sebuleni akachukua sahani jikoni nakuenda kula chakula. Mara ghafla akasikia mlango unafunguliwa alikuwa mama yake, "yani wewe Bwana mi nilivyorudi nikaambiwa upo ndani nikajua ushakula".aliongea mama yake vicent,huku anavuta kiti pale sehemu ya kulia chakula akakaa. "hapana mama uwezi amini yani nilipitiwa na usingizi nikalala ndo nimeshtuka sasa hivi".aliongopa vicent, aisee huyu jamaa hatari."ooooh pole baba ni uchovu tu huo"aliongea kwa huruma mama yake. "asante mama".alijibu vicent huku anafakamia wali kwa maini. Basi waliongea mengi mama mtu alinyanyuka, na kuenda kulala. "ukimaliza usisahau kuzima taa baba".aliongea mama yake. "sawa mama ntaizima".vicent alikula akashushia juisi, akaelekea kwenye swichi akazima taa na kuenda kulala. ******* Pilikapilika zilikuwa zinaendelea, katika nyumba ya kina niram.ilikuwa Jumapili kulikuwa na ugeni mkubwa kwao, kuna ndugu zao walikuja.basi yalipikwa masontojoo siyo ya kawaida. Zilisagwa juisi za matunda basi ilikuwa tafrani. Niram akutulia alikuwa bize vibaya. "niram ebu kuongezeae chumvi kwenye biriani kule".ilikuwa sauti ya mama yake. "sawa mama".alijibu huku anaacha alichokuwa anafanya na kwenda kuweka chumvi kwenye chakula. Kila kitu kilikuwa sawa sasa niram alikuwa chumbani anajiandaa akaoge. ******** Suma alipoona ajapigiwa jana, akaona isiwe kesi ngoja amchek yeye maana umbea ulikuwa unamuwasha mtoto wa kiume huyu. Akukubali kitu kimpite hivihivi,yani alikuwa tofauti na richard mwenzie hakuwa mpenda kufuatilia yasiyo muhusu. Basi aliweka vocha akampigia "oyaaa mwanangu unayumba"haliongea suma ."hamna nilichoka sana yani uwezi amini ".alijibu vicent. "eeeh ilikuwaje jana na yule mtoto mzuri?".aliongea suma huku akitegesha masikio vizuri kupata udaku "hahhhhah suma eeh nna kazi kama unataka kuhusu hiyo stori ntakupigia baadae " "ok poa basi usisahau ".alijibu suma huku anakata simu. Ila suma akakumbuka kitu ayaaaaaah!! Daaah!!.Nimesahau kumuuliza Kitu, yeye na haraka zake mpaka nimesahau".aliongea suma huku anamlaumu vicent,kwa uamuzi wa kukata simu haraka. "anyway nitamchek baadae".aliongea suma, mara kisimu chake kikaanza kuita."duuuh huyu somoe ana mpya gani nae mi leo nnampango wa kuonana na hadijaa".alijiseme suma kimoyomoyo ,huku anaangalia ile simu bila kuipokea. Labda niwafafanulie vijitabia vya huyu ismail au kwa ufupi ndo unaweza kumuita suma. Yani suma yupo tofauti na wenzake, suma kwanza ni mwingi wa habari,anapenda kujua mambo ya watu ni mwongeaji mno kuliko wenzake.ajatulia hata kidogo isimpitie sketi mbele yake lazima amfate tu, ila richard na vicent wapo tofauti sana na yeye, richard ana mahusiano na binti mmoja anasoma, shule tofauti na yao. Na ni huyohuyo tu ndo yupo nae. Lakini suma weeeeeeh!! Mwiko mkubwa tena uchuro, kutulia na mwanamke mmoja. Basi baada ya simu kukata akaizima na kuendelea na mambo mengine. ******* Ilikuwa ni mida ya jioni. Wageni wameshaondoka, nyumbani kwa kina niram. Na mama yake kama unavyomjua mtu wa pilikapilika usiseme, alikuwa ameshaenda kuzurura muda mrefu. Aaaaah ahhh!!,sijui muhindi gani huyu mwenye tabia za Kiswahili.ok tuachane nae tuendelee. Basi niram alikuwa amekaa sebuleni peke yake, maana mdada wa kazi hupendelea kukaa ndani kwake kama kazi ameshazimaliza. Basi alijikuta mpweke sana na alijikuta anatamani, kuongea na vicent,ili apate kampani na kupoteza muda kidogo. Hata sijui ni kwanini alimuwaza vicent kuwa ndio mtu pekee wa kumtoa upweke. Hata mimi sijui,ila tutajua hivi karibuni. Basi aliingalia simu kwa muda nakujifikiria ampigie au atulie asimpigie. Basi nafsi ya niram ikawa inashindana,moja inamwambia piga nyengine, inamwambia usipige ila akiwa katika mgongano wa kutoa maamuzi nini afanye, gafla akaona kitu moyo ukapiga paaaaah!!! .alishindwa kuamini alichokiita. Itaendelea.... ... Read More
*LOVE BITE EP 03* ILIPOISHIA………. Mawazo yalirudi tena kwenye ile picha na kuamua kuificha bila kuichoma moto kama alivyotaka mwanzo kufanya. Badala yake alienda sehemu ambayo kulikuwa na hati ya nyumba yake na kuiweka ile picha katikati. Ni kweli Prisza alikuwa anampenda na hawakuwahi kuachana. Ni muingiliano tu wa maisha ndi uliowatenganisha. Moyo wake aliona kama si haki kuichoma ile picha kwakua bado alikua na nafasi ndani ya moyo wake japokuwa kuonana na msichana huyo ni ngumu sana. Hata alipomaliza chuo alijitahidi kumtafuta bila mafanikio. Mpaka muda huu anajitegemea ni kipindi kirefu cha miaka sita tuko walipokutana na Prisca kwa mara ya mwisho. Mawazo ya msichana huyo wa kwanza katika maisha yake yalimchanganya kichwa na hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali matokea na kuanzisha ukurasa mwengine wa maisha yake kwenye mapenzi na shani Baada ya usafi huo wa kabati lake, aliamua kujilaza kitandani na usingizi ukamchukua. SONGA NAYO………… Siku ya pili yake Jothan alienda kazini kama kawaida. Alifanya kazi zake na baada ya kurudi kazini alimkuta Shani amejaa tele nyumbani kwake. “karibu mume wangu “ alikaribisha Shani na kumfuata Jothan na kumpokea mizigo yake. “ahsante.” Aliongea Jothan na kumkabidhi mizigo yake Shani. “una oga kwanza au unakula ndio uende kuoga?” aliuliza Shani baada ya kurudi pale alipokuwa Jothan. “vyovyote tu mke wangu. Maana nahisi joto na hata njaa pia ninayo.” Aliongea Jothan na kumfanya Shani atabasamu. “kaoge kwanza, maana ukiwa vizuri hata chakula kitashuka barabara.” Alishauri Shani na mawazo yake yakapitishwa moja kwa moja na Jothan. Alipotoka kuoga Jothan, alirudi mezani na kukuta Shani ameshaandaa mapocho pocho ya kila aina yaliyochafua meza. “unajua mke wangu, hata niwe na njaa vipi, kama wewe upo nyumbani basi hudiriki kuitunza hiyo njaa kwa sababu unajua sana kupika mke wangu. Muda mwengine naomba nipate na njaa ya ajabu ili nikifakamie kisawasawa chakula chako.” Aliongea Jothan na Shani akabaki anatabasamu na kumuangalia Jothan kwa mapozi. Mapenzi moto moto kutoka kwa Shani yalizidi kupamba moto. Muda wote Shani alijitahidi kumuweka Jothan kwenye kundi la wanaoyafurahia mapenzi. Jothan alijisikia raha kutokana na Shani kila wakati kutokana na mauzo anayoyapata kuwa na msichana High classic. Walitamani kila saa wawe karibu na kulishana ndio style iliyowavutia watu wengi waliowashuhudia wawili hao walionyesha kupendana sana. Siku moja Jothan akiwa anatoka kazini, ghafla aliona gari likiwa limepaki pembeni na kuna msichana akihangaika kulishughulikia lile gari. Jothan alipaki gari lake pembeni na kushuka kwa ajili ya kutoa msaada. Alipomfika eneo la tukio, yule dada aligeuka kumuangalia Jothan na wote wakajikuta wanapigwa na butwaa. “JOTHAN!!” aliita yule dada kwa sauti kubwa iliyoambata na mshangao mkuu. “PRISCA!!” hata jothan naye alilitaja jina la yule msichana na kumfanya Prisca kujiachia na kupitisha mikono yake mgongoni mwa Jothan kupitia kweye makwapa yake kama ishara ya kumkumbatia. Jothan naye akampokeaa vizuri kwa kuzungusha mikono yake kwenye kiuno namba 6 cha Prisca. Baada ya kusalimiana, wakaona haitoshi. Waliacha gari zao pale pale na kutafuta sehemu tulivu na kukaa kwa ajili ya kupigiana story mbili tatu kutokana na kukumbukana kupita kiasi. “ ahsante mungu kwa kunikutanisha na kipenzi changu jamani,.. jothan milima haikutani ila binaadamu tunakutana. Leo hii kauli hiyo ndio naikubali kwa asilimia zote.” Aliongea yule dada huku akionyesha furaha ya wazi juu ya Jothan ambaye wakati huo alikua na tabasamu la usoni lakini kichwani alikua kwenye msongo wa mawazo. Anampenda Prisca lakini kwa sasa Shani amechukua nafasi kubwa kwenye moyo wake kutokana na kumpa kila anachokihitaji tena kwa wakati. Alikiri kuwa kwa sasa Prisca alizidi uzuri na kumfunika hata Shani. Maana Shani alikuwa ameridhika na kuzidi kuwa mnene kiasi japokuwa sio kigezo cha kupunguza uzuri wake. Ila Prisca alikuwa mwembaba lakini aliyekuwa na figa iliyojichonga kama glasi ya wine. Kwenye kiuno alikuwa mnene na kufaya hipsi zake kuonekana sana. Pia kijungu cha wastani kilichotupiwa huko nyuma ndio kilizidi kumpa maksi zaidi na kumfanya azidi kuonekana special na wanaume wote wanaojua viwango vya wanawake wazuri na wenye mvuto katika muonekano wa macho ya marijali. Kiuno kilichoingia ndani na muinuko wa kibinda ndio kilitengeneza namba 6. kiuno hicho mungu kawapendelea wasichana wachache sana. Hata wachina wameshindwa kutengeneza dawa ya kutengeneza kiuno hicho. Sura ya mviringo iliyokuwa na macho yenye kilevi bila ya kunywa kileo chochote ndio kilikuwa kivutio kingine. Ukiachana na weupe halisi ambao ulikuwa kiasi na kufanana na maji ya kunde, pia vijisima vidogo mashavuni vilivyojitokeza kila akifanya tendo lolote liliousumbua mdomo wake vilimfanya mtu yeyote kutamani kumuangalia usoni. Uso uliombwa na haya mbele ya mwanaume ndio ulikuwa kivutio hasa kwa mvulana mwenye kutafuta mtu wa kuweka ndani na kuoa kabisa. Mambo yote hayo ndiyo aliyokutana nayo Jothan baada ya kukutana na Prisca kwa mara nyingine baada ya muda mrefu. Hata yeye mwenye alikutana na majaribu hayo aliyoyafananisha na majaribu ayapatayo mwanamke mjane baada ya kusikia sauti ya mwanaume tajiri aliyekuja kumfariji na kwa kumuahidi kumuoa na kuwa tayari kuwalea watoto wake. Alijikaza kiume na kujaribu kuyaficha madhaifu yake yaliyomkumba na kujifanya yupo kawaida. “Hata mimi nimefurahi kukuona, za miaka?” aliongea Jothan na kumuangalia Prisca ambaye alikua na furaha wakati wote huo toka wameonana. “vipi, leo maaskari hawaji??” aliuliza Prisca na kucheka. “leo hakuna mwanafunzi hapa..au wewe mwanafunzi?..maana siku ile nilikataa kuwa mimi ni mwanafunzi halafu wewe ukajitambulisha kuwa mwanafunzi.” Aliongea Jothan na kufanya kicheko kitawale kwa sekunde kadhaa kati yao. “tumetoka mbali sana Jothan, leo naona kabisa kuwa mungu katufanya tusahau kipindi chote ambacho hatukua pamoja.” Aliongea Prisca huku akionyesha wazi kuwa bado alikuwa na mawazo ya mapenzi juu ya Jothan. “hata mimi naona kama vile hatukuonana siku mbili kwa jinsi siku ya leo ilivyofukia mashimo ya miaka mingi niliyoishi bila kuiona sura yako.” Aliongea Jothan na kumuangalia Prisca aliyekuwa na kila kitu cha kutalii umuangalipo usoni. “nikuulize swali Jothan?” Aliongea Prisca na kumfanya Jothan kushangaa kidogo baada ya kuombwa ruhusa ya kuulizwa kitu. Alifikiria kwa nukta kadhaa kisha akaruhusu kusikia kitu alichotaka kuuliza Prisca. “umeshaanzisha uhusiano wa kimapenzi na mwanamke mwengine zaidi yangu?” Aliuliza Prisca swali hilo huku akiwa kawaida na kuonyesha wazi kuwa lile swali linahitaji majibu sahihi na yenye utashi juu yake. Jothan hakuamini kama swali lile lingekuja mapema kabla hajaliandalia maandalizi yoyote ya kujibu. Ubongo wake ulikimbia kwa kasi kutafuta jibu la kumpa kati ya ukweli au kumuongopea kwakua wakati huo swala la kumuepuka au kumpotezea msichana huyo aliyeonja penzi lake toka hajakuwa sister du kama hivi sasa. Elimu ya msichana huyo na maisha mazuri anayoishi pia vilikuja kwenye ubongo wake na kufanya machaguo kuwa mengi. Yaani kama ni mtihani, basi lile swali lilikuwa katika mfumo wa matiple choice tena lililokuwa na mfumo wa A,B,C,D,E na F.. “sina.” Alijibu Jothan huku moyo wake ukimuuma kumkana Shani. “wooh… ni wazi hii couple Mwenyezimungu amekuwa akiismamia kwa kipindi kirefu. Unajua kuwa hata mimi nilikuwa naamini kuwa kuna siku tutakuja kuonana tena. Ndio maana sikuona uzito wowote kuwakataa wanaume wengi huku nikiwa sijui ni lini tutakutana. Roho ingeniuma sana ungeniambia kuwa kuna mwengine umeshampa moyo wako.” Aliongea Prisca bila kujua kuwa huo ndio ulikuwa ukweli wenyewe. Maneno hayo yalimfanya Jothan ajione kuwa hakuwa na makosa kumuongopea kwa sababu angemwambia ukweli chochote kingeweza kutokea na kusababisha maongezi ya amani kati yake na Prisca kutoweka. “unataka kuniambia kuwa mpaka hivi sasa hauna mtu mwengine aliyerithi mikoba yangu?” aliuliza Jothan kimitego. “hakuna… yaani toka uliponiacha sijaguswa na mtu mwengine. Yaani hata kama ungekuwa umenifunga luku basi zingesoma unit zile zile ulizoziacha.” Aliongea Prisca na kumfanya Jothan kutabasamu. Waliongea mengi na kila mmoja alifurahia uwepo wa mwenzake pale. Waliachana baada ya kumrekebishia Prisca gari lake na kila mmoja kupata mawasiiliano yote ya mwenzake. Waliachana na ahadi ya kukutana naye tena walikubaliana kuwa watapeana taarifa kwenye simu. Siku hiyo iliwekwa kwenye Diary ya Jothan ambaye alikuwa anatemba nayo kwenye mkoba wake wa kazini. Usingizi ulikuja ukiambata na ndoto iliyojirudia kuanzia mwanzo hadi pale walipoachana. Aliamka asubuhi na kukuta Shani ameshamuandalia maji ya moto kwa kuwa asubuhi hiyo ilikuwa na kiubaridi kidogo. Alipoamka tu aliletewa nguo za bafuni pamoja na mswaki ambao ulisha wekwa dawa kabisa. Alipokuwa bafuni mawazo yaligeuka upande wa pili na kumfanya amuwaze pia Shani kwa jinsi alivyokuwa akitimiza wajibu wote kama mke bora anavyotakiwa kufanya. Kila aliloliwaza kutendewa na msichana basi Shani alikuwa wa kwanza kufanya hata kabla hajaambiwa fanya. Hayo na mengine mengi ndio yalimfunga Jothan na kuyatuliza macho yake kwa wasichana wengine na kumfanya kuwa mtiifu kwa kurudi nyumbani mapema. Na kama anataka kupata moja moto maja baridi basi hutoka na mpenzi wake huyo ambaye alimfanya kuinjoy kwa kuwa sehemu nyigi walizoingia hakukua na mtu mwenye demu mkali kama wake. Alimaliza kuoga huku kichwani hakujua jibu nini kati ya A au B. kuna wakati alitamani kuyaweka kuwa yote ni majibu. Kuna wakati alitamani arushe shilingi ila alishindwa kumjua nani amuweke mwenge na nani amuweke bichwa. Prisca ndio msichana waliyebikiriana kwakua yeye hakuwahi kufanya mapenzi kabla kutokana na ulinzi thabiti wa wazazi wake alipokuwa anasoma. Na Prisca ndiyo yeye aliyekata utepe. Shani ndio mpenzi wake wa ukubwani ambaye anamuonjesha matamu ya ndoa hata kabla hajafikia maamuzi ya kuoa. Hata sasa anaanza kuonekana na kitambi kidogo kwa sababu ya raha azipatazo kwa mpenzi wake huyo. Japokuwa walikuwa wapenzi kwa kipindi kirefu, lakini hawakuwahi kukaa pamoja hata wiki moja kwa sababu kila mmoja alikuwa anaishi na wazazi wake. Ila Shani na yeye wamekuwa wakilala pamoja mara tatu kwa wiki. “itakavyokuwa ndio hivyo hivyo.” Aliongea Jothan baada ya kuona anaisumbua akili yake bila majibu sahihi. Siku waliyo ahidiana kukutana kati ya Jothan na Prisca iliwadia huku kila mmoja akiwa amewasili bila kukosa huku wakiwa wamejitupia vitu vya thamani kila mmoja. Make up na mpangilio wa nguo alizovaa Prisca zilimfanya kuonekana katika muonekano mwengine wa kuvutia zaidi. Jothan hakuamini kuwa ndiye yeye alikuwa analala kwenye kifua cha yule msichana zamani. Pia hakuamini kuwa huyo msichana ndiye aliyekuwa akilipigania penzi lake miaka yote japokuwa walikuwa hawajaonana miaka mingi. Walikutana huku kila mmoja akiwa ameshuka kwenye gari lake na kwenda kwenye hotel moja yenye hadhi hapa Dar. Walipata chakula cha mchana na baadae wakaenda kwenye swimming pool kuogelea. Hamadi !, Macho yalimtoka Jothan baada ya Prisca kuvua nguo zake na kubaki na nguo ya ndani huku juu kukiwa na sidiria ndogo iliyobana maziwa yake na kuyafanya yapande juu na kuonekana sehemu kubwa ya maziwa iliyoteganishwa na msitari mmoja kati kati kuwa wazi. Jothan hakuona ubaya kuvua nguo na yeye na kubaki na boxer na kujumuika naye kwenye swimming pool huku wakiwa peke yao eneo hilo lililokuwa na mabwawa mengi ya kuogelea. Waliogelea na kujikuta michezo yote wanacheza. Kuanzia bembea, mpira wa pete na mwisho wakamaliza na mchezo usio hitaji kocha wala mashabiki japo kuwa unapendwa na watu wengi hapa duniani. Ukiwa mtoto unaambiwa kuwa mchezo huo ni mmbaya lakini ukikuwa bila kufundishwa unajikuta unacheza huku ukijilaumu kwa nini hukuanza kucheza toka mwanzo. Hawakujua walitumia muda gani kwakua taa za ile hotel ziliwaka muda wote na kufanya mtu asitambue wakati kama hajaangalia saa. Mndinyo wa kitanda murua cha hotel hiyo ndio sababu iliyowafanya kudumu muda mrefu huku kila mmoja akiwa ame miss raha za mwenzake. Mechi hiyo ya marudiano ilikuwa kali na kila mmoja alikiri kuwa walihitaji kuwa karibu na kucheza kila mara. Baada ya muda, Jothan aligutuka kuwa hiyo siku ndio siku Shani alikuwa analala kwake. Aliamka fasta na kutupa macho yake kwenye saa ya ukutani “MUNGU WANGU…. SAA SABA USIKU?” Alishtuka kimoyo moyo na kutaja alichokiona kwenye saa. Aliamka ili aenda kuoga kwa ajila ya kwenda nyumbani kwake. “vipi darling, unaenda wapi tena… mwenzio nahitaji kimoja tu cha mwisho.” Alidakwa mkono kimahaba na Prisca aliyekuwa ameyarembua macho yake na kuonyesha ishara zote za kuhitaji kipindi cha pili baada ya mapumziko. “najisikia uchovu ndio maana nilikua nataka kwenda kuoga.” Aliongea Jothan huku akiwa na wasiwasi mkubwa juu ya Shani kugundua usaliti alioufanya siku ile. “twende wote babie, tukirudi mpango mzima au…” aliongea Prisca na kumfanya Jothan azidi kuchoka. “poa.. twende.” Alikubali kishingo upande na wote wakaenda kuoga na uchokozi alioufaya Prisca huko bafuni ikiwafanya mchezo huo kuanzia huko huko bafuni na kumalizikia kitandani wakiwa hoi na usingizi wa muda wote waliokuwa wakicheza cheza ulikuja na kuwafanya wapate usingizi mnono. Saa nne asubuhi ndio waliachia kitanda na kwenda kuoga. Walipofungua mlango walikutana na wahudumu waliokuwa wakigonga kwa ajili ya kufanya usafi. Walieda kupata supu kutokana na kupotelewa na nguvu nyingi masaa kadhaa yaliyopita. Baada ya hapo. Walijiandaa na kila mmoja akapanda kwenye gari lake huku Prisca akionyesha wazi kuwa aliufurahia uzinduzi wa uhusiano yao uliofanyika kwenye kitanda cha hotel ya SERENA. Jaothan akiwa kwenye gari lake, aliiona simu yake aliyoiacha makusudi kwa ajili usumbufu pindi awapo na Prisca. Alikuta missed call zaidi ya kumi na tano na sms sita zote zikiwa za Shani na zikionyesha kuwa na wasi wasi juu ya usalama wake. Alihuzunika sana kwa kosa alilolifanya japokuwa hakupanga kulala nje. Maisha ya kuendesha mioyo miwili hakuwahi kuishi na tayari kwa siku hiyo aliona adha yake na kutamani kuchuja na kuwa na mmoja tu. Ni nani ambaye angestahili kubaki na ni nani atoke ndio swali lililokosa majibu kwakua wote alikuwa anawakubali kwa wakati wao. Alivyolala na Prisca alikuwa kama alikuwa anamfungua kwa mara ya kwanza hali iliyomfanya aamini kuwa hakutumika muda mrefu. Aliona sio sawa kumuacha msichana huyo mwenye ndoto naye nyigi za maisha yao toka walipokuwa wanasoma. Na Shani hakustahili kutendewa unyama wowote kwakua hata yeye hajawahi kumfanyia unyama wowote zaidi ya kumfariji anapokuwa ana huzuni na daima aliisimamia furaha yake hata ikibidi kuenda kinyume na matakwa ya dini kwa kukubali kuishi nae bila ndoa. Akiangalia kila mmoja alionyesha kumpenda kwa wakati wake na hawakuwa tayari kumuachia. Ila yeye swali la NIMPENDE NANI lilimsumbua kuliko hata DIAMOND. Aliamua kuwasha gari lake na kuelekea nyumbani. “oooh.. ahsante mungu. Umekumbwa na nini kipenzi changu?.” Aliongea Shani baada ya kuupokea mkoba wa Jothan. Hali hiyo ilimshangaza Jothan kwakua hakutegemea mapokezi kama yale. “samahani mke wangu, sikukupa taarifa kuwa ofisini kuliandaliwa warsha na nikaenda kwa kudhani itaisha siku hiyo. Hata hivyo simu yangu niliisahau kwenye gari na kunifanya nisizione missed call zako mapema.” Aljiuma uma Jothan mbele ya Shani ambaye wakati huo ndio kwanza alikuwa anamvua viatu baada ya kukaa kwenye moja ya masofa yaliyokuwa pale sebuleni. “sawa mpenzi wangu. Nimefarijika tu wewe kurudi salama.. maana nilikuwa na wasi wasi juu ya uzima wako tu.” Aliongea Shani na kumuonyesha Jothan jinsi anavyomjali. “samahani sana mpenzi wangu, nitajaribu kukupigia simu kwa kila siku nitakayochelewa kurudi nyumbani.” Aliongea Jothan na kukiri kuwa amefanya makosa makubwa ambayo hata yeye mwenyewe hakuyategemea. Siku hiyo ilipita kwa Jothan kulala muda mrefu kutokana na uchovu wa jana yake. Asubuhi aliamka na kukuta ameandaliwa nguo za kuvaa kwa ajili ya kwenda kazini zikiwa zimepigwa pasi kabisa. Aliwekewa maji ya uvugu vugu kwa ajili ya kuoga kisha kifungua kinywa matata kilikuwa tayari mezani kinamsubiria yeye tu. “ashante mke wangu.” Alishukuru Jothan baada ya kumaliza kunywa chai. “usijali mume wangu, nakutakia safari njema. Take care honey.” Aliongea Shani na kumfungulia mlango wa gari Jothan. Jothan alifika kazini mapema na kufanya kazi zake kama kawaida. Saa nane alitoka kazini na kurudi nyumbani. Alikuta ameandaliwa chakula cha mchana mezani lakini Shani hakuwepo kwakua ilikuwa ni siku ya kwenda kwao. Alijihisi mpweke na alitamani Shani angekuwepo kwake moja kwa moja. Alikata shauri baada ya kula chakula na kuamua kumtafuta mpenzi wake kwenye simu. “hallow” alipokea Shani kwa mapozi. “I miss u babie, unaweza kuja tutoke baadae kidogo tukale mbuzi maeneo ya Facebook pub?” aliongea Jothan. “noo babie, leo nimeenda kwa mama. Sio vizuri kuonyesha tabia mbaya mbele yake ya kurudi usiku. We vumilia babie. Kesho tutakuwa wote.” Aliongea Shani kwa pozi zilizomfanya Jothan kushindwa kukata simu hata kama maneno ya msingi ya kuongea nae yameisha. “basi sawa. Sijui lini utanipeleka kwa mama.” Aliongea Jothan huku anatabasamu. “si wewe mwenyewe tu hujaamua. Ukiamua hata leo nakuleta huku.” Aliongea Shani huku akionyesha wazi kuwa alikua anacheka. “nitakuja tu mine, si unajua mambo mazuri hayahitaji haraka.” Aliongea Jothan na kukata simu. Siku ya pili yake walitoka pamoja na kwenda kula bata maeneo hayo na kurudi mida ya saa tano usiku. Alipokuwa kazini, alisikia simu yake ikiita kwa mlio tofauti. Kabla hata hajasoma jina la mpgaji wa hiyo simu. Tayari alishamtambua kwakua aliihifadhi namba ya mtu huyo kwa mlio tofauti kwa makusudi. “haloo.” Aliipokea ile simu. “haloo babie, I miss u.” sauti nyororo ya kike ilisikika upande wa pili. “I miss u too Prisca, niambie.”aliongea Jothan huku akiangalia wafanya kazi wenzake waliokuwa bize wakifanya shughuli zao. “hata kunitafuta wangu,.. yaani kama uliniroga mwenzako siku ile. Yaani sijielewi mpaka hivi leo.” Aliongea Prisca kwa sauti ya mahaba. Jothan aliangalia na kuona soo kuendelea kuongea maneno yale mbele ya wafanyakazi wenzake. “sema nini babie, nitakupigia nikiwa free. Now nipo kazini halafu nina kazi nyingi.” Aliongea Jothan kwa sauti ya chini. “sawa wangu, baadae.” Aliitkia Prisca na kukata simu. Jothan alifanya kazi zake na kurudi nyumbani kwake. Baada ya kupata chakula cha mchana, alijitupa kitandani na kuchukua simu yake na kumpigia Prisca. “haya lete maneno.” Aliongea Jothan baada ya Prisca kupokea simu. “nina hamu ya kuonana na wewe babie… sihitaji kuwa mbali na wewe hata kwa dakika moja kwa jinsi nillivyozimika mbaya.” Aliongea Prisca kwa sauti iliyomshinda mwana dada wa kipindi cha ala za roho kinachoruka usiku kwenye kituo cha clouds fm. Sauti ilipenya vizuri kwenye masikio ya Jothan na kuhisi labda Prisca alichanganya sauti ya Loveness love (Diva) na wema sepetu. “tupange week end, sababu katikati ya wiki ni majanga.” Aliongea Jothan. “poa, ijumaa si ulisema unatoka mapema. Unaonaje kama tukikutana siku hiyo.” Aliongea Prisca na wazo lake likapitishwa moja kwa moja na Jothan. Siku ya ijumaa ilipofika. Jathan alimpa taarifa Prisca na wakakutana maeneo ya Peacock hotel iliyopo maeneo ya mnazi mmoja. Jothan alifika na kumkuta Prisca alishafika muda mrefu kidogo na tayari alishaagiza kinywaji na alikua anakunywa taratibu. Alipofika, alipokelewa kwa kukumbatiwa na Prisca na kupewa mabusu matatu matakatifu kwenye mashavu yake na moja likiwa sawia mdomoni mwake. Baada ya salamu hiyo adhimu. Walimuita muhudumu aliyekuja haraka na kumpa oda yao. “tuchukue chumba sasa hivi au baadae?” aliuliza Prisca baada ya kumaliza kula. “hapana, leo sijisikii vizuri kabisa na sipo tayari kushiriki tendo lolote Prisca.” Aliongea Jothan na kumfanya Prisca apigwa na butwaa. Maana alijiandaa kabisa kupata mechi nyingine siku hiyo. “kwanini babie….unaumwa???” aliuliza Prisca kwa mshangao. “siumwi, ila mayo wangu unanisuta kila siku nikiongea na wewe kwenye simu au nikikutana na wewe. Najihisi sifanyi fair kwa nikitendacho.” Aliongea Jothan huku sura yake ikionyesha wazi kuwa hakuwa na furaha ingawaje aliingia kwa muonekano wa mtu aliyefurahia uwepo wao pale. “jamani, tatizo ni nini wangu, mbona una nifumba fumbo ambalo sijui nitalifumbua vipi?…naomba uniambie ukweli kuliko kuniweka mwenzako kwenye uzio wa alama ya kuuliza.” Aliongea Prisca huku akionyesha wazi kubadilika kutoka katika hali ya furaha aliyokuwa nayo mwanzo na kuungana na Jothan. “Prisca, hivi bado unanipenda?” aliuliza swali Jothan lililomfanya Prisca apigwe na bumbuwazi kwakua hakulitegemea lile swali. “nakupenda sana tena zaidi ya niwezavyo kuelezea kwa ulimi wangu. Ndio maana nikaweza kukaa kipindi kirefu bila ya kuwa na mtu mwengine japokuwa ni wengi walikuwa wanakuja kunitongoza na bado sikuona umuhimu wa kuanzisha mapenzi mapya kabla mapenzi yako wewe na mimi kufa.” Aliongea Prisca na kumuangalia Jothan aliyekuwa makini kumsikiliza. “hata mimi nakupenda Prisca, ila mimi ni msaliti na sio mwema kwako hata kidogo. Cha kwanza nimekuwa muongo kwa kukuongopea toka siku ya kwanza tulipokutana kwa mara ya pili ukubwani. Cha pili sistahili kuwa wako kwakua tayari nimeshakuharibia mipango na malengo yako kwa kipindi krefu Prisca.” Aliongea Jothan huku akionyesha wazi kuwa alikuwa katia wakati mgumu kufunguka yale yaliyomjaa moyoni. “sikueliwi Jothan.. naomba nidadavulie uyasemayo.” Aliongea Prisca huku akionyesha kuchaganyikiwa. “kwanza naomba unisameha Prisca kwa haya nitakayokuambia. … nilifanya makosa makubwa siku ile kwa kutokuambia ukweli kuwa tayari nina msichana na ninaishi naye. Nampenda sana ingawaje sikuweza kutoka kwenye mitego yako siku ile kwakua wewe ndio wa kwanza kukaa moyoni mwangu na chembe chembe za upendo juu yako ndizo zilizonisukuma mpaka kukuongopea na kukuambia kuwa sina mtu. Siwezi kuweka mafahari wawili kwenya zizi moja. Na kumuacha Shani ni kitu kisichowezekana kwakua ananionyesha mapenzi zaidi ya niliyowahi kufikiria mapenzi kuwa hivyo. Maamuzi yangu ni kwamba. Kuanzia leo sahau kuwa na mimi ni mpenzi wako…. Niwie radhi kwa hili.” Aliongea Jothan huku machozi yakimlenga lenga. Hakika ni uamuzi mgumu aliouchukua kwakua aliamini ilikuwa ni mtihani mkubwa katika mapokezi ya mlengwa. Alipoinua macho yake kumtazama Prisca, tayari mashavu ya prisca yalishalowana kwa machozi huku macho yakiwa mekundu. Kilio cha kwiki kilianza kusikika na kumfanya Jothan kuingiwa na imani baada ya kumtaza mpenzi wake huyo anaye amua kumuacha bila kosa lolote. ITAENDELEA ... Read More
NILIPOTEZA WATOTO WANGU WANNE (Mkasa wa maisha ya ndoa ya Naomi) Sehemu ya kwanza(01) Naitwa Naomi Charles,katika maisha yangu sikuwahi kuamini haswa mambo yanayohusiana na nguvu za giza,kitu pekee nilichojua ni kwamba hivi vitu huwa vipo midomoni mwa watu tu,lakini kadri nilivyozidi kukua na kuingia katika maisha ya ndoa hapo ndipo nilipokuja kushuhudia kwa macho yangu kwamba haya mambo si ya kwenye midomo ya watu,bali yanafanyika na kuishi katika jamii mwa watu. Ndugu yangu amini nakuambia,kama kuna mwanga basi elewa hata giza lipo,na siku zote lengo la kuwepo mwanga ni kwasababu ya kukimbiza giza,kusingekuwa kuna ulinzi wa Mungu endapo kama mambo ya giza yasingekuwepo,nilichokuja kuamini ni kwamba siku zote uwepo wa mwanga wa Mungu wa wanadamu ni kwasababu ya kukimbiza giza linalowanyemelea wanadamu. Niliwahi kusoma vitabu na kama vile "Dollo,Mama yangu anakula nyama za watu" na kitabu cha "Jini lilivyonilelea mwanangu kimiujiza",waliandika na kusema hiyo ni mikasa ya ukweli lakini bado nilisema kwamba huu ni utashi tu wa utunzi wa watu. Ni miaka takribani 15 imepita tangu niamue kuachana na safari ya ndoa na John mume ambae nilipenda kumuita J...Alinioa ndoa ya halali kabisa,nakumbuka kipindi naonana nae alikuwa na miaka 40 wakati huo mimi nilikuwa na miaka 28,alikuwa ameniacha mbali ki umri lakini haikuwa sababu ya penzi letu kufa. Lakini kuna mambo mawili ambayo yalinishangaza kwake,alikuwa na umri mkubwa sana na majukumu ya kumuingizia pesa lakini cha ajabu bado alikuwa anaishi na Mama yake mzazi,cha pili ni kwamba aliniambia kwamba alipokuwa na umri wa miaka 30 alipataga mke ambae walipanga kuoana lakini aliamua tu kuishi nae nyumbani kwao kama mke wake,baada ya miaka mitano kupita John aliniambia mwanamke yule aliamua kukatish safari ya mahusiano na yeye,alibahatika kuzaa nae watoto wawili lakini wote walifariki. John hakuniambia ni sababu ipi iliyomfanya hasa aachane na yule mwanamke. Nakumbuka baada ya ndoa yangu mimi na John nilimshawishi na kumwambia kwamba mimi staki tuendelee kukaa pale na mama yake,tuondoke tukaanzishe maisha yetu na kama Mama tutaendelea kumjali maana si kwamba amezeeka kufikia kipimo cha kuweza kukaa nae na kumlea. John alinikubalia na kusema tutahama lakini tukae kae kwanza pale kwao wakati anajipanga. Miezi miwili ilipita tangu ndoa,hatimae nilishika ujauzito tukiwa bado tunakaa na palepale kwa Mama yake,ambae ni mama mkwe wangu,wote walifurahi baada ya kuona mimi nimekamata ujauzito. Wanasema kulea Mimba sio kazi bali kulea mtoto,miezi tisa si mingi kama ukiwa na subira,hatimae nilishusha mtoto wa kiume,furaha kubwa ilitawala baina ya familia zetu pamoja na mimi na mume wangu,ilikuwa ni furaha isiyo na kifani,wajirani na marafiki wa kutembelea hawakukosekana,taratibu kazi ya kulea mtoto ilianza. Hatimae miezi sita ilipita,mtoto alizidi kuchangamka,kilichobaki kinaniumiza ni kwamba kila nikimuambia mume wangu tuhame kwa mama yake tukaanzishe maisha yetu alikuwa ananijibu bado hajajipanga,likikuwa linaniumiza sana kichwa swala hili na nilijikuta nakata tamaa ya kuwa namuuliza mara kwa mara. Katika safari yangu ya ndoa sintakuja kuusahau usiku,usiku ambao vindumbwe ndumbwe na maajabu vilianza katika maisha yangu,nakumbuka nilikuwa nimelala mimi na mume wangu pamoja na mtoto wangu huyo wa miezi sita,ambae tulimpa jina la Grey,niliota tumezunguukwa na wanawake wanne mimi na mume wangu kwenye kitanda ambacho tulikuwa tumelala,wanawake hao walikuwa wamevalia shuka nyeupe ambazo wamejifunga rubega,nilitaka kupiga kelele lakini moja ya wanawake wale aliniziba mdomo kisha mmoja wao akanyoosha mikono yake na kumchukua mwanangu,nilikodoa macho na kutamani kupiga kelele lakini nilishindwa kwasababu nilishikwa,nilimkazia macho yule mwanamke aliemchukua mwanangu na ndipo niliposhikwa na bumbuwazi baada ya kugundua kwamba ni mama mkwe wangu.Alianza kuondoka na mwanangu huku akifuatiwa na wale wanawake watatu waliobaki,nilianza kupiga kelele za kumlilia mwanangu mpaka nalia huku nikiinuka kitandani kuwafuata,ghafla nilishtushwa na mume wangu huku akiniambia"we Naomi unaenda wapi huko na kupiga kelele na wakati mtoto huyu hapa,umepatwa na nini".Nilianza kuhema huku nikimwangalia mwanangu kama yuko salama,wakati huo nikawa namwaga jasho. Hazikupita sekunde nyingi,mwanangu alianza kulia huku akitoa povu jeupe mdomoni.Nilijikuta naanza kuchanganyikiwa akili.... JE NINI KITAENDELEA Je Grey atapona...? Je ndoto aliyoota Naomi inauhalisia wowote katika maisha yao..? tukutane sehemu ya pili kesho jioni panapo majaaliwa. Ruksa kushare,pia toa maoni yako ili watu wajifunze zaidi. NILIPOTEZA WATOTO WANGU WANNE-(02) (Mkasa wa maisha ya ndoa ya Naomi) Ilipoishia. Hazikupita sekunde nyingi,mwanangu alianza kulia huku akitoa povu jeupe mdomoni.Nilijikuta naanza kuchanganyikiwa akili.... Sasa endelea... Nilijikuta nalia tu huku nikiita"Greeeey....Greeey",wakati huo sasa mume wangu nae ndipo alipomtazama mtoto wetu na kugundua kwamba mdomoni anatoka povu,nilimuona ameshtuka ghafla na kuinuka kutoka kitandani huku akiuliza"Naomi,mtoto amekuwa na nini,inamaana alikuwa anaumwa harafu hukuniambia mpaka amezidiwa hivi..?". Moja kwa moja Mume wangu alijua labda huenda nimemficha sikumwambia kama Grey alikuwa anaumwa kitu ambacho hapana. Grey alizidi kulia zaidi na wakati huo povu jeupe liliendelea kumtoka,wote tulikuwa tumechanganyikiwa hatujui tufanye nini,ndipo Mume wangu alienda sebureni na kuchukua maji haraka haraka kisha kumnywesha Grey,wakati anakunywa maji alitulia kwanza kulia lakini baada ya kumaliza tu kunywa maji kilio kiliendelea tena,nilimchukua na kuanza kumnyonyesha lakini alikataa ziwa,mara muda haukupita Bibi yake ambae ni mama yake na Mume wangu akawa ametugongea mlango"nyie kuna nini tena humu?,mbona mtoto analia hivi".Mume wangu alimfungulia mlango kisha akaingia ndani,alifika na kuanza kumtazama mtoto ambae alikuwa bado analia,mimi nilijikuta naacha kumtazama mwanangu badala yake nilianza kumtazama huyu mkwe wangu huku nikikumbuka nilichoota,nilitamani nijue zaidi hivi nilichoota kina uhalisia au ilikuwa ndoto tu. Ghafla nilimuona Mama mkwe wangu akimuweka mwanangu kitandani na kusema"huyu mtoto mbona ameumwa ghafla hivi kulikoni,au alianza toka mchana lakini hukutuambia,hebu mwangalieni na mwili wake ulivyobadilika na kuwa mwekundu"aliposema hivyo moyo ulinilipuka na kuacha kumtazama yeye kisha kumtazama mwanangu,sikuamini kuona mwili wa mwanangu aliekuwa mweupe umekuwa mwekundu rangi ya damu kabisa,kulia nako kukazidi,nilimchukua na kuanza kumbembeleza lakini haikusaidia kitu,matokeo yake na mimi nilijikuta naanza kulia huku nikisema"Baba Grey mwanangu anakufa,Mwanangu anakufaaa"Nililia sana wakati huo Baba Grey nae anawaza afanye nini. Mama mkwe alitoka ghafla kisha kuelekea sebureni,alikaa huko kwa dakika kadhaa kisha akarudi na maji kwenye kikombe akasema"Hebu mnyweshe haya maji nimeyachanganyia chumvi na sukari huenda yakamsaidia",kweli niliyachukua haraka haraka kisha nikamnywesha,kweli duniani kuna maajabu,kwani baada tu ya kumnywesha yale maji Grey aliacha kulia na kukubali kunyonya lakini mwili wake uliendelea kuwa mwekundu. Ilikuwa mida ya saa kumi usiku na ndipo Baba Grey alisema sasa tumpeleke Grey hospitali,kweli juhudi za kujiandaa kwenda hosipitali zilianza na hatimae safari ilitimia,tulifika kwenye Zahanati moja hivi iliyokuwa jirani na sisi na kumkuta daktari wa zamu,walitupokea kisha wakamuangalia mtoto kitendo kilichofanya daktari ashtuke baada ya kumuona ni jinsi gani Grey alivyokuwa mwekundu,harakati za vipimo na matibabu vilianza,juhudi zilifanyika na wapimaji wakati sisi tukiendelea kusubiri,majibu yalikuja ya kushangaza kwani tuliambiwa kwamba Grey hana ugonjwa wowote,hapo ndipo nilipoanza kuona kwamba huenda kweli kuna mauza uza. Tulipewa kitanda ili mwanangu alale kwa ajiri ya kukicha aendelee na matibabu zaidi,nilikaa na mwanangu pale kitandani wakati huo Baba Grey aliniacha huku akisema kwamba anaenda kutoa taarifa na kufanya mchakato wa chakula asubuhi ili aniletee.Nilibaki na mwanangu mle wodi ya watoto akiwa amelazwa,nilipomnyonyesha alikuwa akinyonya kama kawaida.lakini ghafla alianza kukataa ziwa,hali ya kulia ilizidi,alianza kulia toka saa kumi na moja na nusu ya alfajiri,wauguzi walikuja tena kwa ajiri ya vipimo lakini majibu ni yale yale kwamb hamna ugonjwa,walimpa dawa za kutuliza maumivu lakini hazikuzaa matunda.Hatimae ilipofika mida ya saa moja mwanangu Grey aliaga dunia...... JE NINI KITAENDELEA Je ni nini kipo nyuma ya pazia katika kifo hicho cha Grey. Usikose sehemu inayofuata kesho muda na wakati kama huu. NILIPOTEZA WATOTO WANGU WANNE-(03) (Mkasa wa maisha ya ndoa ya Naomi) Tulipoishia .... Hatimae ilipofika mida ya saa moja mwanangu Grey aliaga dunia...... Sasa endelea... Kilio changu kizito kilitawala ndani ya chumba kile katika wodi ya watoto,uchungu mzito wa uzazi na kuondokewa na mtoto ulitawala ndani ya moyo wangu,mawazo yangu yote nilijua na kufahamu kwamba mwanangu hajafa katika kifo salama,bali ameondolewa Duniani kwa kulazimishwa.Wauguzi na akina mama wengine ambao walikuwa wanauguza watoto zao walijitahidi sana kunituliza lakini ndio kama walikuwa wanazidisha maumivu moyoni mwangu. Mwisho mume wangu alikuja akiwa ameleta chai,alipofika kwenye chumba ambacho ndicho tulikuwa tumelazwa na mwanangu moja kwa moja alijua tayari mtoto wetu hayupo duniani,kwani alinikuta bado nalia lia japo sio kama mwanzo kwasababu Wamama wenzangu walikuwa wakijitahidi sana kunipoza na kunituliza,hapakuwa na kingine zaidi ya mchukua mtoto wetu Grey ambae alikuwa tayari ni marehemu kwa ajiri ya kuanza safari ya kurudi nyumbani kuweka msiba,tulichukua gari huku mimi njia nzima nikienda nalia. Grey alikuwa bado mdogo,alikuwa na miezi sita hivyo hata mazishi yake yalipangwa yafanyike siku hiyo hiyo,kila mara nilikuwa nauchungulia mwili wa mwanangu,sikuamini kama kweli amenitoka,nilikuwa nimemzoea,alikuwa na afya nzuri na mwenye kuchangamka,lakini kilichokuja kunitisha zaidi Grey baada ya kufariki mwili wake uliirudia hali yake kwa maana ya kwamba ile hali ya mwili kuwa mwekundu utafikiri kalowekwa kwenye damu ilitoweka.Nilibaki najiuliza huu ni ushirikina wa namna gani,sikutaka kumtuhumu mama mkwe moja kwa moja kwasababu sikuwa na ushahidi wowote,ndoto pekee huwezi ukaitumia kumuhukumu mtu,japo ilikuwa ni ndoto ya mashaka. Hatimae saa kumi ya jioni ilifika muda ambao ulipangwa kwa ajiri ya mwanangu Grey kuzikwa,watu mbalimbali,majirani ndugu na marafiki walikusanyika kwa ajiri ya kutoa heshima zao za mwisho kwa kichanga changu kile,pale nilijifunza kitu kimoja kwamba siku zote ukiishi na watu vizuri basi utakuwa mtu wa watu,mwanangu alikuwa ni mdogo na asiejulikana sana mbele za watu,lakini watu waliohudhuria walikuwa ni wengi kiasi kwamba ni msiba wa mtu mzima na umaarufu wake. Basi jioni iliisha kwa kumpumzisha mwanangu katika nyumba yake ya milele. Hatimae maisha ya upweke bila kulea bila kunyonyesha yalirudi,tulikaa wiki moja na baada ya hapo ndugu jamaa na marafiki waliokuwa wamekuja kututembelea nao waliondoka na hatimae tulibaki tukiishi watu wanne kama mwanzo yaani mimi,mume wangu,mama mkwe wangu pamoja na mdada wa kazi aliekuwa akiitwa Rhoda. Sikujiskia tena kuendelea kukaa na pale pamoja na mama mkwe wangu,hatimae niliamua kuanza kumsumbua mume wangu kwamba inatupasa tuhame pale tukaanzishe maisha yetu,lakini bado juhudi za mume wangu kujaribu kukataa ziliendelea,na mimi pia neno kuhama nililigeuza wimbo wa taifa mdomoni mwangu kila mara nilipokaa nae.Hatimae siku moja aliniambia kwamba amenielewa na atakaa kuongea na mama yake ili tuweze kuondoka na kwenda kuanzisha maisha yetu. Moja kati ya siku nyingine ambayo sintakuja kuisahau katika maisha yangu ni siku ambayo nilikuwa natokea chumbani naelekea sebureni,nilichungulia kidogo nikaona mtu na mama yake wamekaa wanaongea,yaani mume wangu na mama yake,kwakweli nilinyata taratibu taratibu mpaka karibu na ukuta wa kukatizia kuingia sebureni ili niweze kusikia wanazungumza nini,nilitamani sana kusikia wanazungumzia swala la mimi na mume wangu kuhama,nilikuwakuta wameshaanza mazungumzo ambayo sikujua wanaanzia wapi lakini tumbo lilikuja kushtuka baada ya kumsikia mama mkwe wangu akitoa kauli kwa mume wangu na kumwambia"Sawa kama mnataka kuhama hapa nyinyi hameni lakini ukumbuke kwamba bado una deni kubwa sana kwangu,bado hujakamilisha kile kinachohitajika kwahiyo wewe hama lakini ukae unajua kwamba deni langu ni lazma ulipe"Tumbo lilinikata na kuanza kujiuliza ni aina gani ya deni ambalo mime wangu anadaiwa na mama yake,nilitamani niendelee kusikia mazungumzo zaidi lakini nilimuona mama mkwe wangu akinyanyuka na kushika njia ya mlango kuelekea nje. JE NINI KITAENDELEA Je ni aina gani ya deni ambalo anadaiwa John na mama yake..? Usikose sehemu inayofuata hapa hapa kesho panapo majaaliwa. ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: