Riwaya :JICHO LA TATU SEHEMU YA KWANZA. Hahahahahaha mimi sidanganyi nakwambia ukweli kabisa...unajua usiku wa jana sijalala kabisa..niliota ndoto..ikawa inajirudia rudi kama mara tatu hivi.. Sauti hiyo ilisikika ikitokea ndani ya chumba katika nyumba ya Kijana aitwae MAKALA..alikuwa akimsimulia mkewe kuhusu ndoto ya kutisha aliyoiota usiku wa jana.....mke wa Makala alifahamika kwa jina la NOREGA... Makala akasema,,"kama umemaliza kufunga nywele zako zima taa tulale,sasahivi ni saa sita kasorobo...Norega akafanya kama alivyoagizwa na mumewe..akazipiga hatua kadhaa kuifuata swichi iliyokuwa ukutani karibu na mlango wa kuingilia chumbani humo...akazima taa akapanda kitandani wakaanza kuutafuta usingizi.... *************** Upande mwingine ilionekana Nyumba moja ikiwa imejitenga peke yake....jirani wa karibu na nyumba hiyo alikuwa umbali mrefu kama kilomita sita hivi kutoka kwenye nyumba hiyo iliyojitenga peke yake alionekana mwanaume mmoja wa makamo akichimba shimo usiku huhuo wa saa sita. nje ya nyumba hiyo....mwanaume huyo alifahamika kwa jina la JOSHI....aliendelea kuchimba shimo takribani kama masaa mawili mfululizo....aliopohakikisha kachimba shimo lenye urefu aliokuwa amekusudia,,akatoka ndani ya shimo hilo na kuzipiga hatua kuingia ndani kwake......na baada ya dakika tatu hivi...akatoka huku amebeba maiti ya binadamu...akazipiga hatua kulifuata lile shimo alilolichimba akadumbukiza maiti hiyo ndani ya shimo,,akaanza kufukia kwa kutumia koleo.... ilipofika saa kumi za usiku,,alimaliza kufukia shimo hilo...kisha akamwaga mbegu za za mchicha..ili paonekane kama ni bustani ya mbogamboga..... kisha akaingia ndani ya nyumba yake..akafunga mlango...ndani ya nyumba hiyo palionekana kutisha kutokana na makorokoro kuwa mengi yamewekwa bila mpangilio...nyumba hiyo ni kubwa sana ilikuwa na vyumba Tisa...akazipiga hatua akaingia kwenye chumba kimojawapo..akawasha taa...kikaonekana kiti cha mbao kikiwa na kamba...pia chumba hicho kilijaa zana kutisha..... alizitumia katika shughuri zake ambazo hazifahamiki mpaka muda huu...Joshi hakuwahi kuwa na rafiki tangu utotowake mpaka uri huo alionao sasa....ni baada ya wazazi wake kuuwawa na mtu asiyejulikana...wazazi wa Joshi waliuwawa akiwa na umri wa miaka saba..alishuhudia mauwaji hayo..akiwa amejificha chini ya meza iliyokuwa sebuleni... yule mtu katiri aliyefanya mauwaji hayo...alipokuwa anatoka nje ya nyumba ya kina Joshi...akatereza kwenye vigae kutokana alikuwa amekanyaga Damu zilizokuwa zimetapakaa chini akadondoka na kuangukia kisogo akupoteza fahamu....Joshi alipo ona muuwaji huyo kadondoka,,akajua amekufa...akaatoka pale alipokuwa amejificha chini ya meza akaanza kulia huku akitazama maiti ua Baba yake pamoja na Mama yake...waliuwawa kwa kuchinjwa shingo na kukatwakatwa mapanga mwili mzima... Joshi akazipiga hatua kwa hofu kubwa..akamsogelea yule muuwaji....akamtazama usoni akaina kovu kubwa la mda mrefu lililokuwa kwenye shavu la kushoto mwa muuwaji huyo...akahisi kuwa amekufa....akazipiga hatua akarudi ndani.....baada ya sekunde kadhaa..muuwaji alizinduka akapata fahamu..Joshi alipomuona ananyanyuka akajificha haraka,,chini ua meza....yule muuwaji akajishika kisogo huku akiugulia maumivu...akazipiga hatua na kuondoka zake,akatokomea kusikojulikana.... **************** Joshi alijificha hapo masaa mengi kiasi...alipo ona kuna hali ya itulivu akatoka chini ya meza,,akakumbuka baba yake alimfundisha kuwa endapo akiona kunahatari..au siku nyumba ikiwaka moto alafu wazazi wake hawapo nyumbani basi apigege simu ya mezani kwenda namba 112..kisha ataje namba ya nyumba yao ambayo ni S/0043......joshi alikariri maneno hayo ya baba yake sikunyingi.... akachukua simu ya mama yake haraka,,akapiga namba hizo za Dharura 112..simu ikapokelewa kwenye kituo cha polisi..Joshi akaelezea tukio zima,,pia akatoa anuani ya nyumba..baada ya dakika kadhaa maaskari walikuja mpaka kwenye nyumba hiyo....wakachukua maiti zile mbili na kuzipeleka mochwari...kutokana zilikuwa zinamajeraha makubwa ya kukatwa na mapanga..ililazimika wazikwe siku hiyo hiyo ili maiti hizo zisiharibike na kutoa harufu.... taratibu za mazishi zikafanyika...wakazika... Shangazi wa Joshi ambaue ni mdogo wa mwisho wa baba yake Joshi..alichukua jukumu la kuishi na kumlea Joshi katika nyumba hiyo....Jishi aliendelea kukua kadri miaka ilivyozidi kwenda.. alipotimiza umri wa miaka ishirini na tatu....shangazi yake ambaye alikuwa mlezi wake alifariki dunia..... kutokana alikuwa tayari kafikisha umri wa kujitegemea Joshi aliamua kuishi mwenyewe ndani ya nyumba hiyo.....akiwa peke yake.. ********BAADA YA MIAKA TISA KUPITA******** Joshi alitimiza umri wa miaka therathini na mbili(32)alikuwa anafanya kazi ya kupasua kuni anazikusanya..zikiwa nyingi anaziuza kwa pamoja....siku moja akiwa mjini kwenye matembezi alimuona mtu..akamfananisha..mtu huyo alionekana kuwa mzee kiasi.. Joshi akamsogelea mzee huyo akamtazama kwa makini..akaona lile kovu shavuni mwa mzee huyo. akakumbuka kuwa huyu ndiye muuwaji aliyewauwa wazazi wake..akaamua kumfatilia mzee huyo mpaka anapokwenda..akagundua nyumba anayoisgi mzee huyo....akamteka na kumpeleka nyumbani kwake..kwenye ile nyumba waliyokuwa wakiishi wazaziwake..yule mzee alistuka kuona anapelekwa kwenye nyumba hiyo..akakumbuka kuwa miaka 25 iliyopita,,alifanya mauwaji kwenye nyumba hiyo...aliamua kumuuwa baba Joshi pamoja na mkewe....kwa sabavu walikuwa wanamdai pesa nyingi baada ya kuuziwa nyumba na baba yake Joshi...aliwauwa ili asilipe deni hilo... Joshi akamtesa mzee huyo kwa mateso makali sana mpaka akafa... kumbe ile maiti aliyoizika Joshi ilikuwa ni maiti ya mzee huyo aliyewauwa wazazi wa Joshi.. ********BAADA YA MEAKA MMOJA KUPITA***** Mzimu wa mzee huyo ukafufuka na kuanza kufanya mauwaji ya kikatiri na yenye kutisha.. Siku moja majira ya usiku wa saa saba..ule mzimu ulionekana ukifufuka kutoka kwenye ile bustani ya mbogamboga alizozipanda Joshi.... ITAENDELEA....... ASANTENI....‎

at 1:20 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top