UTAFITI: HAKUNA MWANAUME MPOLE NA MNYENYEKEVU KAMA ANAECHUMBIA #inasikitisha , poleni sana wanawake Huenda binti akahisi anachumbiwa na malaika au shemasi kwa namna kijana anaechumbia anavyoonesha nizamu na unyenyekevu wakati anamchumbia kumbe ndani ni fisi asiye na hata chembe ya huruma. Ikishafungwa ndoa tu ndio inakua kama kipyenga cha ubabe, vipigo, usaliti na kila aina ya ubaya kimepulizwa, ni wanaume wachache mno wanaoenzi ndoa na viapo walivyoapa kwa wake zao, wengi huwakumbuka wake zao warudipo nyumbani, wamewafanya kuwa ni vyombo vya starehe na kuzalishia watoto, inasikitisha sana kuona wanawake thamani yao imekua ikilinganishwa na soda barid au viburudisho. Wanaume wengine wanawageuza wake zao kua punda wa kazi zao za nyumbani na kuwalelea watoto wakati wao wapo vijiweni wanakunywa kahawa na kupiga soga. Laiti kama wanaume wote wangedumisha tabia zao walizoonesha kwa wake zao kipindi cha uchumba leo hii kusingekua na haja ya kua na Taasisi za kutetea haki za wanawake. Wanawake wangezifurahia ndoa zao, visa kama kupigwa, kuachwa, kutelekezwa na watoto, kuuawa, kukatwa mapanga, kusalitiwa n. k visingekuepo katika jamii. Hivyo ndivyo ambavyo ingekua kama WANAUME wangedumisha tabia walizoonesha wakati wa uchumba, Ila kitendawili ni kwamba wanaume wa namna hiyo utawapata wapi miaka hii ya digitali? Wanawake wengi wamekua wakiumizwa sana na kulia kutokana na visa vya waume zao, ila cha ajabu ni kwamba hakuna hata mwanamke mmoja anaekiri kuwa mmewe alikua hivyo toka wanakutana kwa mara ya kwanza. Tabia mbaya za mwanaume ikiwemo ubabe, ukatili, wivu, ugomvi n. k huwa zinajificha anapokua anamfuatilia binti. Utafiti nilioufanya mwenyewe (mimi B professional love) nimegundua wanaume wengi ni kama vinyonga, hubadilika kulingana na mazingira, hivyo ni vigumu sana mwanaume yeyote kuonesha madhaifu yake kipindi cha uchumba ndio maana mwanaume anaweza hata kuazima gari la rafiki yake ili aendee kumchumbia binti ilimradi tu asionekane mtu wa dhiki. Naamini nitakua nimewachoma wanaume wengi ila huo ndio UKWELI, yabidi wanaume kutafakari kiwango cha upendo na mapenzi kwa wake zao je! Ndio kile walichoonesha tangu uchumba au kimeshuka!? Kisha kubadilika itasaidia kuwatua mzigo wake zenu wa kulia na kujutia ndoa kila siku, itasaidia pia kupunguza majanga yasiyo ya lazima katika jamii ikiwemo watoto wa mitaani, mauaji ya wanawake n. k TAFADHALI SHARE IWAFIKIE WENGI ZAIDI Nakutakia siku Njema, Mungu Akubariki na kukulinda Usisahau ku LIKE

at 10:26 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top