BUSARA ZA AJABU ZA BABA KWA KIJANA WAKE Kijana baada ya kuoa na kuingia rasmi katika maisha ya ndoa, alimtembelea baba yake na kumuambia, "BABA NATAMANI KUWA MUME BORA KWA MKE WANGU, NAOMBA UNIPE SIRI, NI TABIA ZIPI HASA MWANAMKE HUZICHUKIA TOKA KWA MMEWE ILI NIJIEPUSHE NAZO" Baba yake alitabasamu akamwambia, "Hakika mwanangu umeuliza swali mubashara wakati muafaka, zifuatazo ni tabia mbaya za wanaume ambazo wanawake huzichukia mno, 1. UBAHILI: tabia ya ubahili waliyonayo wanaume wengi imekua kero kubwa mno kwa wanawake wao hususani kipindi hiki ambapo ela imekua adimu mtaani. Wanawake wengi hawapendi ubahili wa waume zao, wapo wanaofikia kuchepuka ili kupata wanavyovitaka kutokana na waume zao kuwa na mkono wa birika, UBAHILI. 2. UBINAFSI: Wakati fulani mwanaume hupendelea kufanya mambo kwa ubinafsi bila kuzingatia hisia za mkewe au familia yake na mahitaji yao. Wakati mwingine mwanamke anashindwa kuvumilia tabia hii yenye kuudhi na humpendelea mwanaume anajitoa kwa ajili ya furaha ya familia yake. 3. AHADI ZISIZOTIMIZWA: Mwanamke anamchukia mwanaume anayeahidi bila kutekeleza alichokiahidi. 4. UBABE: Mwanamke hapendi kuishi na mwanaume mbabe na anayetumia mabavu katika maisha yake yote. Daima mwanamke humpenda mwanaume anayemheshimu na kumuunga mkono katika maisha, sio mwanaume mbabe, mbinafsi na anayetaka kutumia mabavu yake. 5. WIVU ULIOPITILIZA: Mwanamke hapendi kuishi na mwanaume ambaye muda wote anamuonea wivu na kumshuku kupitia kiwango. Sifa na tabia hii inaweza kuzorotesha uhusiano wa kindoa. 6. UONGO : Mwanamke hampendi mwanaume dhaifu anayeogopa kusema ukweli, na anayemuongopea ili kuficha makosa na kasoro zake. Hivyo, inapendeza zaidi mume akiwa muwazi kwa mke, japo wakati fulani huwa na ugumu, kwa sababu hilo litamfanya apate kuheshimiwa na mkewe. Kama ambavyo ukweli husaidia kuondosha mikingamo baina ya wanandoa, kadhalika uongo huyafanya matatizo yao kuwa magumu zaidi. 7.USALITI Hii ni tabia inayowaudhi mno wanawake hususani pale inapotokea anakupenda kwa dhati toka moyoni na kukuamini mwishowe anakuja kugundua unamsaliti. Hakika moyo wake huumia mno na huweza kupelekea kubadilika na kufanya maamuzi magumu juu yako au ndoa yenu ikiwemo kujiua, kukuua, kurudi kwao au kuwakubalia wote waliokua wakimtaka ili kulipiza kisasi. 8.KUTORIDHIKA inapotokea mwanamke amejitoa kwa moyo wake wote kukupenda na kukutimizia kila hitaji la moyo wako jifunze KURIDHIKA, hata kama hakutimizii kwa asilimia 100 maana hakuna binadamu aliyekamilika, tosheka, mfunde ili kuongeza ufanis wake na kujenga ndoa yenu. Mwisho kabisa jitahidi kufuatilia makala murua na mafunzo mbalimbali ya ndoa na maisha anayotoa 🅱 professional love hakika utajifunza mengi mno katika kufanikisha ndoa imara na familia bora yenye amani, furaha na mafanikio tele". Kama unakubaliana na busara za Baba hapo juu SHARE POST HII IWAFIKIE WENGI ZAIDI Nakutakia siku Njema, Mungu Akubariki na kukulinda Usisahau ku LIKE

at 10:19 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top