USHAURI WANGU WEEKEND HII. Rafiki zako wanaolewa kila weekend lakini wewe hujui hata uhusiano ulionao unaelekea wapi, kwa sababu umechagua kufumba macho yako juu ya mambo ya msingi na mahusiano yaliyo mwiba kwako. Ni muda mrefu sasa mpo katika mahusiano hajawahi kukukutanisha na mtu yeyote muhimu kwake. Watu anaokukutanisha nao ni rafiki zake anaokula nao bata, Ma DJs, madereva taxi, boda boda na bajaji, wahudumu wa lodge, na waiters/waitresses. Hajawahi hata kujisumbua kukuongelea katika social networks kwa sababu anapenda maisha yake binafsi ya kimya kimya kuficha ufilauni wake. Dada yangu fumbua macho yako yote mawili na funga miguu yako, acha kuitanua. Ficha kabisa na muulize ni nini mustakabali wa mahusiano yenu. Dada zangu ni vema mfanye hivyo, kwa sababu nyie mnacho kitu kinaitwa Saa ya kibailojia. Na pale saa hii inapokukamata, utakua umeshachelewa sana. Utaolewa na mseja, mtalaka, kua mama wa kambo, au kua mchepuko wa babu mstaafu wa bodi ya korosho. Control hali hii ukiwa bado binti mbichi unaevutia, thamini utu wako, thamini your precious body. Wewe ni wa thamani mno. Vinginevyo atakutumia tu, atamuoa mwanamke mwingine na atakutumia wewe kama hadibu za rejea katika mahusiano yake yaliyopita. Fumbua macho na funga miguu yako. Weekend njema na Mungu awabariki!

at 9:44 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top