UPENDO USIOSHINDWA! - WIFE'S UNFAILING LOVE..! MIAKA MITANO NYUMA. Mimi Anitha Daniel nakubali kukuchukua wewe Thomas Ben kama mume wangu halali wa ndoa, naahidi mbele ya mashahidi waliopo nitakupenda katika uzima na hali ya ugonjwa mpaka kifo kitakapotutenganisha" "Sasa unaweza kumbusu bibi harusi Mr. Thomas Ben" mchungaji akaongea. Mapigo ya moyo ya Thomas yakaenda mbio wakati akimfunua bibi harusi usoni. Anitha alionekana ni mrembo haswa. Akainamisha shingo na kumbusu kwenye lips za bibi harusi. Anitha nae akamkumbatia Thomas kwa nguvu huku machozi ya furaha yakimtiririka usoni mwake. "Kamwe usiniache Anitha" Thom akamnong'oneza Anitha kwenye sikio. "Sitakuacha mpenzi wangu Thom" Anitha nae akamnong'oneza Thom. Na taratibu wakaachiana baada ya kukumbatiana. "Ninyi mmekua mashahidi wa kiapo hiki ambacho vijana wetu wameweka mbele yenu, sasa natambulisha kwenu ndoa mpya ya Bwana na Bibi Thomas Ben". Mchungaji akaongea huku akiwa nyuma ya maharusi. Kanisa zima likalipuka kwa shangwe na vigeregere na Anitha akalia zaidi huku akiwa ameshikwa mkono na mume wake halali Thomas. MIAKA MITANO BAADAE. Anitha kimya kimya akanyata kufuata alipo mume wake Thomas. Thom alikuwa kwenye meza ya maktaba yake ndogo iliyopo pale nyumbani kwao akisoma kitabu kiitwacho "Tutarudi na roho zetu" kilichoandikwa na mwandishi nguli Ben R. Mtobwa. Anitha akatabasamu kimya kimya na akiwa nyuma yake akamfumba macho Thom kwa mikono miwili. "Ni mimi na wewe tu ndio tunaishi kwenye hii nyumba, Anitha nimeisikia harufu yako ulivyoingia tu huku." Anitha akaondoa mikono machoni mwa Thom, akahema kwa nguvu na akakaa juu ya ile meza ya kusomea. "Kwanini unanigundua mapema hivyo Thom lakini? Yaani siwezi hata kuku-suprise, mimi sipendiii". Anitha akaongea huku akiizungusha mikono yake kwenye kichwa cha Thom. "Ila umekua unasoma huku muda mrefu mno, umeniacha peke yangu mimi niko bored" Anitha akamwambia Thom huku akizungusha macho yake" "Ehee Annie kwaio unataka tufanye nini cha kufurahisha pamoja?" Thomas akaanza kumtekenya Anitha.. "No! Hapana Thom sio hivyo bhana" Annie akamwambia Thomas huku akicheka kweli. Thomas akakunja mikono yake kifuani, na akamtazama Anitha machoni huku aktabasamu. "Kwaio unataka tufanye nini?" "Sio tufanye nini, mimi nataka nicheze play station yako umeificha tena! Naomba nipe nicheze na wewe endelea kusoma kitabu chako pleaaaasee" Anitha akamwambia mumewe.. "Hapana Anitha" Akarudi kwenye kiti chake cha kusomea. "Hapana Anitha, siwezi kukupa play station yangu.." "Kwanini! Kila siku hutaki hata niiguse...ni kama mtoto wako" Anitha akaongea kwa kukata tamaa. "Yes, Thom akazungusha macho yake, Ndio kama mtoto wangu..maana wewe hujanipa mtoto mpaka leo hii mwaka wa tano wa ndoa..". Anitha akapigwa na mshangao kwa muda. Ni Thom ndiye aliyezungumza hayo? Maneno hayo yakamuumiza mno Anitha. "Usingeniambia hayo Thomas..." Anitha akaongea kwa masikitiko makubwa..... "Lakini ni kweli...mimi hapa naongea ukweli Anitha" akageuza uso wake huku akiwa bado amekaa kwenye kiti. "Ukweli? Unafikiri na mimi sipendi tuwe na watoto?" "Usinifikirie vibaya Anitha, mimi simaanishi hivyo..." Thomas akasimama na kumtizama Anitha. "Kwa hiyo unamaanisha nini Thom, niambie..unamaanisha nini?" "Basi yaishe Anitha, unaweza ukachukua play station na cheza utakavyo mwenyewe. Funguo zipo kwenye kabati la nguo" "Sitaki Thom.. kila siku unaniumiza na maneno yako ya kejeli" "Tafadhali Anitha usianze hayo please". "Niambie Thom kwanini umezungumza hayo maneno? Nataka kujua!" "Kwasababu nimechoka! Nataka kuwa baba! Nataka kuwa na watoto wangu Anitha..." "Kwaio unafikiria mimi sihitaji watoto Thom? Anitha akauliza huku machozi yakimlenga lenga! "Sasa kwanini haushiki mimba Anitha? Huu ni mwaka wa tano Annie bado tunajaribu tu." Akapiga meza na kuondoka kwenye chumba cha kusomea. Anitha akawa katika shock. Akakaa kwenye kiti kwa sekunde chache, akainuka na kukaa tena...muda huu akaanza kulia, machozi mengi yakimtiririka. WIKI MBILI BAADAE. "Thomas, amka please" Anitha akawa akimuamsha mumewe. Taratibu Thom akafungua macho yake na kutazama saa iliyokua pembeni mwa kitanda. "Saa hizi ni saa nane Anitha" "Ndio, ni muhimu Thom" "Nakusikiliza Annie" Thom akamjibu kivivu. "Mama amesema twende Mwanza kwa ajili ya vipimo. Amesema amezungumza na daktari wake na amemueleza kwamba twende.." "Nini?" Thom sasa akafungua macho yake, mama yako yuko Mwanza na sisi huku kazi tumwachie nani?" "Tufanye twende Thom. Tunaweza kwenda hata weekend." "No Annie. Hizo gharama saa hizi hapana na..." "Ni siku yangu ya kuzaliwa leo Thom na kitu pekee ninachohitaji kutoka kwako ni hii safari tu ya kwenda Mwanza" Thom akakaa kimya. Kwa miaka miwili sasa amekua akiisahau kabisa siku ya kuzaliwa ya mkewe. "Nisamehe Anitha...nilisahau tena birthday yako." "Nimeshakuzoea Thom" Anitha akamjibu huku akigeukia upande mwingine wa kitanda. Thom akazungusha mkono wake kwenye kiuno cha Anitha na akamwambia.."Nimekuomba msamaha Anitha" Anitha hakujibu lolote. Thomas akapumua kwa nguvu, "sawa basi tutaenda Mwanza weekend". "Kweli Thom?" Akageuka haraka. "Ndio, kama itakufanya uwe na furaha leo" "Asante sana baby" Anitha akamkumbatia Thom. WIKI MOJA BAADAE. Simu ya Anitha ikaita...akaichukua na kuangalia, mama yake ndio alikuwa anapiga. "Mama shikamoo" akaweka simu yake sikioni huku akiibana na bega na mikono ikiendelea kuosha vyombo. "Mwanangu...." "Kuna nini mama?" Akaiweka simu vizuri sikioni huku bega likiibana. "Matokeo ya vipimo vyenu mwanangu..." Mama akasikika akilia... Anitha akaangusha sahani aliyokua akiiosha kwa mshtuko. "Mama niambie...kuna tatizo gani juu ya vipimo vyetu tulivyoacha?," USIKU WAKE. "Sina uwezo wa kushika mimba Thom.." Anitha akamwambia Thom huku akilia. Thom akahisi ulimwengu wote ukimuangukia.."Nini??" "Mama amenipigia leo...amepewa majibu ya vipimo vyetu tulivyoenda kupima Mwanza" "Mungu wangu" Thom akasimama, akaweka mikono yake kichwani... "Ila uliniambia uko sawa kabla sijakuoa Anitha, uliniambia kwamba daktari alisema ulivyotoa mimba mfuko wako wa uzazi haukuharibika" "Thom usizungumzie yaliyopita hapa" Anitha akaongea kwa hasira na Thom akacheka kwa dharau na kuwa serious muda huo huo. "Wewe ni kichaa. Nilioa mwanamke kichaa!" Anitha akamtazama Thom kwa mshangao...ni kama amechanganyikiwa. "Vipimo vinasema hauwezi kupata ujauzito na wote hapa tunajua hili limesababishwa na ulivyotoa mimba hata kabla hatujaonana...umefurahi sasa? Unajua tumeumia ee..hakuna watoto? Tutauambia nini ulimwengu Anitha?" "Thomas tunaweza tuka-adopt mtoto"...Anitha akaongea huku akilia. "Kuasili mtoto? Wow," Thom akacheka tena, "Nimeoa mwanamke kituko pia..." Akawa serious tena, "hata tukiasili hatakua mtoto wetu wa damu" "Wewe ni muongo Anitha...umejawa na uongo najuta kukuoa Anitha" Anitha akashindwa kujizuia machozi yasimtoke. "Thomas stop...unaniumiza Thom..." Anitha akakaa chini na kuangua kilio. "Unataka kujua ninawaza nini saa hizi?" Thom akamuangalia Anitha kwa dharau. "Nafikiria itakuaje kwangu kuendelea kutazama sura yako ya uongo maisha yangu yote". Anitha akaangua kilio zaidi, "usikate tamaa Thomas...bado ninalo tumbo la uzazi...bado ninao uwezo wa kubeba mtoto..." "Anitha mimi sijakata tamaa kuwa na mtoto wangu ila nimekata tamaa kuwa na wewe" Thomas akageuka na kuondoka. "Thomas!" Akamshika miguu, naumia pia Thom" Akaondoa mikono ya Anitha miguuni mwake na akaondoka nyumbani bila kusema neno lingine lolote......Anitha akalia mno. MWEZI MMOJA BAADAE. "Mama, Thom hataki kuongea na mimi. Ghafla tumekuwa wageni ndani ya nyumba yetu. Hali chakula changu, anarudi kwa kuchelewa...ananichukia kweli na hii inaniumiza mama...ninazidi kuchanganyikiwa...naumia mama yangu..." "Utamficha mpaka lini Binti yangu? Nadhani imetosha tu...mwambie ukweli...muache ajue..hauwezi kubeba msalaba wake...." Kukawa na muungurumo wa gari na baadae honi ikapigwa... "Mama nitakupigia kesho, naona huyo anarudi...." "Sawa Mwanangu, sasa nakuomba umwambie ukweli. Inaweza ikasaidia kama wote wawili mkiwa na wazo moja..." "Bye mama" mama akakata simu. Thom akaingia ndani ya nyumba, akawa anataka kupitiliza bila hata ya kumsalimia Anitha. "Thomas" Anitha akamshika koti lake. "Nimechoka Anitha niache" Hakutaka kumuangalia mkewe usoni. "Najua....tunaweza ongea kwa dakika chache?" Akawa akimsaidia kuvua koti la suti. "Niache basi Anitha" Thom akagomba. "Unanichukia kiasi hiki Thom!!..kiasi hutaki hata kuniangalia usoni...kwamba hata kuongea mbele yangu hutaki...Thom mimi ni Anitha, rafiki yako na mke wako...". Macho ya Thom yakawa madogo kwa hasira.. "Siko katika mood kwa hayo maongezi saa hizi" Akageuka na kutaka kuondoka..... "Usiondoke wakati naongea na wewe Thom!" Akamvuta zaidi ili asiondoke. Hapo hapo makaratasi aliyokua amebeba Thom yakaanguka. Anitha akainama haraka kuyaokota...mikono yake ikaanza kutetemeka na mwili wake ukafa ganzi. "Ta...Talaka? Thomas?" Akamtazama Thom "Nijibu Thom goddammit!" Akamshika collar za shati lake, huku akilia.... "Ndio ni talaka zako! Unahitajika kusaini. Nataka tuachane" Thom akamwambia Anitha. "Nini..? Kwanini Thom?" Taratibu akaanza kumuachia collar zake... "Haitaweza kusaidia Annie, wewe hauoni?" "Thom siamini kama ungekuja kufikiria suala la talaka na ukaenda mbali kiasi hiki...kwanini u mdhaifu hivyo!" Anitha akaanza kulia kwa hasira. "Hapana! Wewe ndio dhaifu na muongo.." akamjibu. "Fikiria kuhusu mimi hata mara moja. Mimi ni mwanaume. Wanangu ndio cha kujivunia! Na wewe ndio hivyo huwezi kunipa mtoto katika maisha yangu yote kwa sababu ya upumbavu wako ulioufanya ukiwa binti mdogo!" "Vipi kuhusu mimi! Umeshafikiria hata mara moja na kujiuliza napitia kipindi gani navyoona wanawake wenzangu wakiwa na watoto wao?" "Huo ni msalaba wako Anitha, kila mmoja atabeba msalaba wake" Thom akamjibu mkewe huku akimuangalia kwa hasira. "Hapana, sio msalaba wangu ni wetu sote...na hizo talaka mimi sweki saini yangu! Tulishaweka agano kanisani kwamba hatutaachana!" "Si vema ukasaini mwenyewe Anitha ili uepukane na kuumia zaidi kuliko nije nilete mwanamke mwingine ndani ya nyumba hii?" Thom akaongea kwa msisitizo. Moyo wa Anitha ukamuuma mno. "Nini?" "Umenisikia Anitha, mwanamke mwingine atakuja humu ambae ataweza kunizalia na kulea watoto wangu. Hivyo okoa nafsi yako na stress kwa kutia saini hizo talaka. Nazihitaji kesho" akageuka na kutaka kuondoka tena. "Hataweza kukubebea mimba pia" Anitha akamjibu Thom. "Sio wanawake wote wametoa mimba. Na sio kila mwanamke ni kama wewe." Thomas akageuka. "Unamaanisha nini Anitha" "Wewe ndio mwenye tatizo Thomas, huna uwezo wa kunipa mimba Thom.." Anitha akamwambia Thom huku akilia. Thom akasimama, akageuka na kumsogelea Anitha. ."Kila unachopanga saa hizi hakitasaidia" "Thom Nilikwambia siwezi kupata mtoto kwa sababu ni wewe ndio huna uwezo wa kunipa mtoto..." "Shut up! Shut up Anitha! Unaongea nini hapa" akamshika mabega Huku akimtikisa. "Una matatizo Thom...daktari amesema unatatizo la primary infertility....Hivyo sio rahisi kwako kumpa mimba mwanamke..." Anitha akamwambia Thom huku akilia mno.... Thomas akashtuka, na kupoteza balance... "Mama alinipigia simu kunipa taarifa. Nilichanganyikiwa, nilihisi kama dunia ndio imeisha lakini zaidi nilifikiri kuhusu wewe Thom. Nikafikiri ni kwa kiasi gani taarifa zile zitakuumiza. Nikafikiri namna ya kukwambia....hata siku moja sikufikiria kuhusu kukuacha. Nilikubali unitukane, unidhalilishe kuhusiana na makosa yangu ya kutoa mimba ambayo baadae niliyajutia na kutubu kwa Mungu wangu. Ilikua rahisi sana kwako kinijaji mimi na kujifikiria wewe zaidi. Mimi ndiye naeumia. Mimi ndiye nilikuwa wa kukuletea karatasi za talaka...ila nilifikiri zaidi kuhusu wewe...niliamimi katika matumaini, imani na miujiza...niiafikiri kuhusu kiapo nikichoahidi mbele ya Mungu kwamba nitakuwa na wewe katika uzima na ugonjwa unakumbuka?" Anitha akatabasamu huku akilia,..."Ila yote hayo Thom umekua mdhaifu kama mtoto mdogo...nikikuangalia machoni naona kukata tamaa...wewe n dhaifu mno Thom..." "Anitha..." Thom akaanguka miguuni kwa Anitha. "Hapana!" Nae akaanguka chini... "Hapana Thom..." Hakutaka kushuhudia mumewe akilia "Mimi....mi ni infertile...sina uwezo wa kuzalisha ooh...Thom akalia kwa uchungu mwingi..."nimebakiza nini sasa...me sio mwanaume.." akamtazama mke wake kwa macho ya kujutia... "Thom pleaseeeee..." Anitha akanyanyua sura ya Thom ili amwangalie usoni,.... "Thom nafahamu...imekuwa ngumu mno kwangu...nikijaribu kuvaa viatu vyako kwanza tokea nimepata taarifa...sikutaka nikwambie moja kwa moja kuwa wewe ndio mwenye tatizo..." "Anitha mrembo wangu...haustahili haya...unastahili zaidi....sitaki kuamini jinsi gani nilivyokutenda vibaya...aibu kubwa nimeibeba....please naomba nikuache...sifai kuwa mume wako..." "Hapana Thom..." Akamshika kichwa chake tena.... "Wewe ni mume wangu Thom...siwezi nikakuacha. Sitaruhusu wewe uniache mimi. Bado ninaamini katika miujiza...Mungu yuko upande wetu...hatatuacha yatima.." "Me ni mpumbavu Anitha...ni mpumbavu....ooh Thomas mimi.." Akaacha mkewe amkumbatie kwenye kifua chake na akambembeleza kama mtoto mdogo... ASUBUHI YAKE. Anitha taratibu akafumbua macho yake, akatizama pembeni mwa kitanda...palikuwa tupu. Akainuka na kukaa...Thom hakuwepo...akaona kikaratasi juu ya mahali alipokua amelala Thom. Huku mikono ikimtetemeka, akafungua ike karatasi na kuanza kusoma... "Anitha... Siwezi kuibeba huu mzigo wa aibu. Nimeku-treat visivyo na bado umenonesha kunipenda, uko na mimi hata kwa hali ambayo nimekutwa nayo. Kipindi chote umejua kwamba tatzo ni langu lakini bado ukabeba mzigo wangu kama wako...hilo linanifanya nijione sina thamani tena mbele yako. Ninakupenda sana kiasi cha kukuacha ujenge maisha na mwanaume mwingine bila ya mimi. Nimekukosea sana Anitha...nachoomba ni msamaha tu kutoka kwako. Siku zote nimekupenda na wewe kama unanipenda basi anza maisha yako upya bila ya mimi....samahani sana kwa kuku-disappoint. Thomas. Anitha akashindwa kuzuia machozi kumtoka. Akashindwa kufikiri vizuri tena. Akachukua simu yake huku mikono ikimtetemeka. "Hello Mr. Thom's office tafadhali..." "Hi sara...." Anitha huku akilia... "Umemuona mume wangu Thom amefika ofisini?" "Hapana mama, tunamngoja yeye mwenyewe hapa kazini...kuna kazi anatakiwa afanye presentation sio chini ya dakika tano kuanzia sasa lakini bado hajafika...." "Oh Mungu wangu.." Anitha akashusha pumzi kwa nguvu. "Mama kila kitu kipo sawa..?" "Asante sara" Anitha akakata simu. Haraka haraka akatoka kitandani na akiwa amevaa nguo ya kulalia akaenda haraka kwenye gari yake...akapiga namba ya mumewe huku akiwa anaendesha gari lakini hakuna jibu lolote alilopata... SAA NANE MCHANA. Anitha alikua amefika nyumbani kwa rafiki yake Thom aitwae Fred. "Fred!" Anitha akabamiza mlango akionekana kuchanganyikiwa..... "Mungu wangu....Anitha..nini tatzo?" Fred akawa akimshangaa.... "Ni.....ni Thomas..Fred...umemuona leo? Yuko hapa?" "Hapana...sijamuona wiki sasa" "Mungu wangu."..akashika nywele zake..... "Kuna tatizo gani shemeji?" Lakini tayari alikuwa ameshaondoka na kuelekea kwenye gari yake.. "Anitha...." Fred akamwita lakini tayari alikuwa ameshatokomea... SAA KUMI NA NUSU JIONI. "Mama, baba...simpati Thomas. Simpati mtoto wenu...." Anitha alikua amekaa mbele ya wazazi wa Thom huku akilia kwa uchungu "Unatakiwa utulie na utuambie kinaga ubaga nini kimetokea" Mama yake Thom akaongea huku akimshika mikono Anitha. Anitha ndio akazidi kulia zaidi, "tafadhali baba mpigie simu wewe, labda atapokea simu yako!!" "Umeenda ofisini kwake?" Baba akauliza huku akichukua simu yake na kutafuta namba ya mtoto wake..... "Nimeenda kila sehemu baba, sijampata..." "Sawa mwanangu tulia basi, usile tutampata.." mama akawa akimbembeleza Anitha. "Aisee huyu mtoto hapokei simu. Ni nini mmefanya nyie watoto?" Baba yake Thom akauliza huku akimtizama Anitha machoni. SAA MOJA JIONI. Anitha alikua bado amevaa nguo za kulalia na alikuwa barabarani akirudi nyumbani huku akiwa na mawazo mengi juu ya mume wake aliko...siku nzima amemtafuta bika mafanikio. Alikuwa yupo kwenye foleni akisubiri taa za barabarani ziruhusu. Alikuwa ameshaawambia wazazi wa Thom kila kitu kuhusu wao. Anitha akainamia usukani wa gari, akalia sana na hakugundua kuwa taa za kijani zilishawaka kuruhusu magari yaondoke. "Oyaa acha uboya...ondoa gari yako, unatuwekesha huku nyuma..." Dereva wa gari ya nyuma akamkoromea..... "Mungu naomba umuongoze mume wangu asijiumize wala jambo lolote baya lisimtokee....muweke salama na muongoze..." Akakanyaga mafuta na kuondoka.... Ghafla akakumbuka kanisani alikofungia ndoa na walipokula kiapo cha ndoa. Kutoka hapo mpaka hilo kanisa liliko ilikua ni mwendo wa masaa mawili; akafanya maamuzi ya kwenda kanisani akiwa na matumaini ya kupata amani ya nafsi. Akageuza gari na kuelekea kanisani...... Kiuvivu akashuka kwenye gari na kuelekea mlango wa kuingilia kanisani. Akapatwa na mshtuko kwa muda. Akasimama..alikuwa mumewe Thomas akiwa amepiga magoti madhabahuni kanisa zima akiwa peke yake. "Thomas! Akaanza kukimbia kumfuata mumewe alipo, huku akiwa na furaha ya kumuona mumewe. "Anitha?" Haraka haraka akasimama na kumfuata Anitha.."Anitha......" Wote wakakutana na kukumbatiana kwa nguvu. "Nimekutafuta siku nzima mume wangu....Ni mungu mwenyewe ndio amenifunulia kukuta hapa....ninafuraha sana kukuona mume wangu kipenzi...." Anitha akaongea huku akimshika uso mumewe. "Sikujua niende wapi Anitha...ni kama siwezi kuutizama ulimwengu tena Annie...." "Nishike mkono wangu Thomas"...Thom akasita... "Nishike Thom pleaseeee" Akamshika Thom mkono na akaongozana nae mpaka madhabahuni. "Miaka mitano iliyopita Thomas, wote mimi na wewe tulisimama mbele ya madhabahu hii. Unakumbuka? "Kumbuka ulininong'oneza kwenye sikio langu kwamba kamwe nisikuache...unakumbuka? Nilikujibu kwamba sitaweza kukuacha kamwe..... .....Ndio maana niko hapa. Mimi ni mke wako Thom. Nilimaanisha kuwa na wewe daima katika raha, shida na matatizo till the death do us apart...kwanini nikuache? No way Thom. ....Ninachohitaji kutoka kwako ni imani tu kwamba unaweza kunipa mtoto, lisilowezekana mbele ya macho ya binadamu kwa Mungu linawezekana kabisa. "Nataka uamini katika muujiza.." akamshika uso na kuendelea kumwambia...."unakumbuka ulivyoniambia mimi ni muujiza ktk maisha yako?...watoto wetu watakua ni muujiza pia katika maisha yetu.... "Muamini Mungu katika hili, usikate tamaa mapema, hivi karibuni watoto wataizunguka meza yetu kwa upendo na furaha....hivi karibuni mume wangu! "Mungu wangu, Anitha...wewe ni mwanamke wa aina gani mama....." Thom akaongea huku chozi likimtoka... "Ni mimi Anitha mkeo, yule ambae niliapa hapa mbele kwamba nitakuwa na wewe mpaka mwisho. "God....i love you so much Anitha...." Akamkumbatia mkewe kwa nguvu. "Kwaio sasa unarudi nyumbani na mimi au sio?" Anitha akamtizama Thom machoni..... "Ndio mke wangu, ni mwanaume gani atakayekataa kuongozana na mwanamke mwenye moyo wa almasi kama wako?" Anitha akambusu mumewe kwenye paji la uso.... MIAKA MIWILI BAADAE... Thomas na Anitha walikuwa kwenye sofa wakiangalia movie. Anitha alikuwa amelala kwenye kifua cha mumewe wakati alipohisi tumbo likicheza... "Thom, Thom....kanacheza tena...usipitwe sasa ni muda wako wa kugusa umsikie...." Taratibu akashika mkono wa Thom na kuuweka tumboni kwake...wote wakahisi kucheza cheza kwa mtoto wao tumboni. "Ninahisi akizunguka....i can feel him" Thom akaweka sikio lake tumboni kwa mkewe.... "Yes Thom, Ninamuhisi akikua kila siku ndani ya tumbo langu....." "Unafikiri huko kuzunguka kwake kunamaanisha nini?" "Hapo ujue kanasema asante baba kwa kuniamini" Wote wakacheka..... Anitha akaegama tena kwenye kifua cha mumewe.... "Thom miezi mitatu ijayo utaitwa baba, sasa umepata muujiza wako..." Thom akamuinua mkewe na kumshika uso wake huku akimuangalia machoni..... "Anitha wewe ni muujiza niliokua nautaka siku zote....asante kwa kutoniacha nipotee.." Anitha akagusisha pua yake na ya mumewe, "Nakupenda sana mume wangu...na siku zote itakua hivyo..." "Angalia kule sasa Movie imetupita...." "Achana na movie Mama kijacho, movie inaweza kusubiri lakini hili haliwezi kusubiri....." Akambusu mkewe kwa huba zito....na taratibu wakapeana haki yao ya ndoa pale pale kwenye uwanja wa sofa...... M W I S H O. . Share

at 11:47 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top