Home → ushauri
→ TATIZO NI NINI MKE WANGU..............
Aliingia ndani ya nyumba na kukuta mkewe akiwa na huzuni, hasira iliyochanganyikana na jazba.
"Hey babe" alimuita huku akiweka gazeti lake katika meza iliyokuwepo pale sebuleni. " Sema" mke alimjibu kimkato huku akivua viatu vyake.
"Na wewe ndio umeingia mida hii?" Mume alimuuliza mkewe huku mkewe akielekea lilipo jokofu kuchukua maji ya kunywa.
"Ndio" mke alijibu.
"Watoto je?" Mume aliuliza tena.
"Wako chumbani kwao kuoga na kubadili nguo" mke alimjibu huku akichukua vile viatu vyake na kuweka sehemu ya kutunzia viatu karibu na mlango.
"Uko sawa?" Mume alimuuliza.
"Ndio" mke alijibu.
" Hapana hauko sawa. Unaonekana kabisa hauko sawa babe. Tafadhali ongea na mimi tatizo ni nini mpenzi" mume alimwambia huku akimsogelea mkewe karibu zaidi.
"Aah! Wewe nawe na maswali yako mengi mimi nimeshayachoka. Hauwezi kuniacha hivi bwana? Leo nimekua na siku mbaya sana siko sawa wewe niache tu!" Mke alimjibu mumewe.
Mume akamtazama mkewe akielekea jikoni. Akaanza kusikia sauti za vyombo vikioshwa ktk sink na kuwasha moto ili aanze kupika. Unataka kuanza kupika? Mume akauliza huku nae akimfuata mkewe jikoni.
"Wewe unaona ninafanya nini? Maswali yako mengine ni ya kitoto kweli Baba James. inatosha sasa" mkewe alimueleza.
"Usianze kupika saa hizi. Njoo. Twende chumbani" mume alimwambia mkewe huku akimshika mkono waondoke.
"Muda umeenda sana. Natakiwa nipike haraka vinginevyo watoto watachelewa kula na hvyo kuchelewa kulala. Sina muda" mke alimgomea mumewe.
"Please wife, wewe twende. Mimi nitakusaidia" mume aliongea.
" Kama ni tendo la ndoa, siko katika mood kabisa." Mke aliongea huku akichukua mchele uliokuwemo kwenye kabati.
"Mpenzi wangu please" mume aliongea huku akimshika mkono mkewe. Mkewe alimpa mkono na mume akazungusha mkono kiunoni kwa mkewe na kuanza kuelekea chumbani kwao.
Wakaingia chumbani. Mume akafunga mlango.
"Unaweza kuungana na mimi kumuabudu Mungu kidogo? tafadhali naomba tupige magoti tumuombe Mungu kwa dakika chache mpenzi wangu" Mume alimwambia mkewe huku akiwa ameegemea mlango.
Wote wakapiga magoti na wakaanza kumuabudu Mungu. Mume akaanza kuimba na mkewe nae akajiunga nae. Wakaanza kusali kwa pamoja. Mke akaanza kuinua mikono juu huku akiomba na kuongea na Mungu wake.
Mume akamnong'oneza mkewe na kumwambia "ni muda wako huu sasa wa kuongea na Mungu kuhusu ya kuudhi yaliyokutokea leo, yeye ni muaminifu atakurudishia tena furaha yako"
Midomo ikawa ikicheza. Sauti haitoki. Macho yakiwa yamefumbwa. Machozi yakitelemka mashavunu mwake. Tabasamu likiwa kwa mbali. mke akainua mikono juu na kuanza kuomba;
"Asante baba yangu wa mbinguni kwa neema na rehema. Kwa kubeba mizigo yangu yote, kwa kuwa mwamba wangu usiotikisika. Asante kwa kunipa mume bora anaenikumbusha kukuabudi na kukusifu wewe pale ninapokua na furaha hata ninapokuwa nimelemewa na maudhi ya binadamu.
"Mume ambae ananirudisha kwenye mstari pale ninapokuwa busy na haya ya kupita ya duniani hapa kazi na biashara ambayo si kitu bila ya wewe. Ndio maana ninalitukuza jina lako kwani ninavyokuabudu wewe unanirudishia furaha yangu.
"Nisamehe Mungu wangu kwa kumuonyesha hasira mume wangu, kila alichokuwa akikifanya leo ni kuonyesha jinsi gani ananijali mkewe. Sikutakiwa kumjibu kwa hasira kwani sio yeye alionikosea. Juu ya jina lako lipitalo majina yote ninaomba nikiamini AMEN!!
Mume akainuka na kumbusu mkewe kwenye paji la uso na kumwambja haya;
"Saa hizi unaonekana ukiwa poa. Nimekusamehe mke wangu. Maisha yana mabonde na milima. Unaweza ukajikuta hutaki kuongea na mtu kabisa kwa sababu ya kuudhiwa, lakini tafadhali sana ongea na Mungu. Acha mambo mnengine yote yasubiri, ongea na Mungu. Usiwe busy sana mpaka umsahau Mungu, kwani kwa kufanya hivyo unamkaribisha shetani kuja kukuharibu.
Mke akajisogeza kwa mumewe na kumbusu mdomoni kimahaba zaidi. Akamkumbatia na kujilaza kifuani kwa mumewe. Mumewe akaanza kumchezea nywele zake huku mke akimsimulia jinsi gani alivyokua na siku ngumu, hasara aliyoipata baada ya mali aliyonunua kuharibika, kuibwa kwa 'power window' ya gari yake na purukushani zingine za siku nzima.
Mke akajisikia akiwa salama mikonon mwa mumewe. Akacheka..akatabasamu.
"Ok honey, twende tukapike. Nitakusaidia kupika. Wewe utapika wali mimi nitapika mboga" mume akaongea.
Wakainuka na kuelekea jikoni, wakaanza kupika huku wakiimba na kutaniana. Watoto wakawa wakiwatazama wazazi wao wakicheka na kuimba kwa pamoja.
Chakula kikawa tayari haraka na ilikua ni furaha kukitengeneza kwa pamoja, wakaungana na watoto wao kwenye meza. Wakala kwa furaha kama familia.
Wakaenda kuwalaza watoto wao, na wao wakaelekea kulala. Usiku ule Wakapeana chakula cha wanandoa kwa furaha na amani tele.
1 Wakorintho 11:3 “Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.”
Mungu abariki ndoa yako, Mungu abariki mahusiano yako yakawe yenye kuleta tija, ukajenge familia yenye amani, mshikamano na upendo. #AMEN
Share
TATIZO NI NINI MKE WANGU.............. Aliingia ndani ya nyumba na kukuta mkewe akiwa na huzuni, hasira iliyochanganyikana na jazba. "Hey babe" alimuita huku akiweka gazeti lake katika meza iliyokuwepo pale sebuleni. " Sema" mke alimjibu kimkato huku akivua viatu vyake. "Na wewe ndio umeingia mida hii?" Mume alimuuliza mkewe huku mkewe akielekea lilipo jokofu kuchukua maji ya kunywa. "Ndio" mke alijibu. "Watoto je?" Mume aliuliza tena. "Wako chumbani kwao kuoga na kubadili nguo" mke alimjibu huku akichukua vile viatu vyake na kuweka sehemu ya kutunzia viatu karibu na mlango. "Uko sawa?" Mume alimuuliza. "Ndio" mke alijibu. " Hapana hauko sawa. Unaonekana kabisa hauko sawa babe. Tafadhali ongea na mimi tatizo ni nini mpenzi" mume alimwambia huku akimsogelea mkewe karibu zaidi. "Aah! Wewe nawe na maswali yako mengi mimi nimeshayachoka. Hauwezi kuniacha hivi bwana? Leo nimekua na siku mbaya sana siko sawa wewe niache tu!" Mke alimjibu mumewe. Mume akamtazama mkewe akielekea jikoni. Akaanza kusikia sauti za vyombo vikioshwa ktk sink na kuwasha moto ili aanze kupika. Unataka kuanza kupika? Mume akauliza huku nae akimfuata mkewe jikoni. "Wewe unaona ninafanya nini? Maswali yako mengine ni ya kitoto kweli Baba James. inatosha sasa" mkewe alimueleza. "Usianze kupika saa hizi. Njoo. Twende chumbani" mume alimwambia mkewe huku akimshika mkono waondoke. "Muda umeenda sana. Natakiwa nipike haraka vinginevyo watoto watachelewa kula na hvyo kuchelewa kulala. Sina muda" mke alimgomea mumewe. "Please wife, wewe twende. Mimi nitakusaidia" mume aliongea. " Kama ni tendo la ndoa, siko katika mood kabisa." Mke aliongea huku akichukua mchele uliokuwemo kwenye kabati. "Mpenzi wangu please" mume aliongea huku akimshika mkono mkewe. Mkewe alimpa mkono na mume akazungusha mkono kiunoni kwa mkewe na kuanza kuelekea chumbani kwao. Wakaingia chumbani. Mume akafunga mlango. "Unaweza kuungana na mimi kumuabudu Mungu kidogo? tafadhali naomba tupige magoti tumuombe Mungu kwa dakika chache mpenzi wangu" Mume alimwambia mkewe huku akiwa ameegemea mlango. Wote wakapiga magoti na wakaanza kumuabudu Mungu. Mume akaanza kuimba na mkewe nae akajiunga nae. Wakaanza kusali kwa pamoja. Mke akaanza kuinua mikono juu huku akiomba na kuongea na Mungu wake. Mume akamnong'oneza mkewe na kumwambia "ni muda wako huu sasa wa kuongea na Mungu kuhusu ya kuudhi yaliyokutokea leo, yeye ni muaminifu atakurudishia tena furaha yako" Midomo ikawa ikicheza. Sauti haitoki. Macho yakiwa yamefumbwa. Machozi yakitelemka mashavunu mwake. Tabasamu likiwa kwa mbali. mke akainua mikono juu na kuanza kuomba; "Asante baba yangu wa mbinguni kwa neema na rehema. Kwa kubeba mizigo yangu yote, kwa kuwa mwamba wangu usiotikisika. Asante kwa kunipa mume bora anaenikumbusha kukuabudi na kukusifu wewe pale ninapokua na furaha hata ninapokuwa nimelemewa na maudhi ya binadamu. "Mume ambae ananirudisha kwenye mstari pale ninapokuwa busy na haya ya kupita ya duniani hapa kazi na biashara ambayo si kitu bila ya wewe. Ndio maana ninalitukuza jina lako kwani ninavyokuabudu wewe unanirudishia furaha yangu. "Nisamehe Mungu wangu kwa kumuonyesha hasira mume wangu, kila alichokuwa akikifanya leo ni kuonyesha jinsi gani ananijali mkewe. Sikutakiwa kumjibu kwa hasira kwani sio yeye alionikosea. Juu ya jina lako lipitalo majina yote ninaomba nikiamini AMEN!! Mume akainuka na kumbusu mkewe kwenye paji la uso na kumwambja haya; "Saa hizi unaonekana ukiwa poa. Nimekusamehe mke wangu. Maisha yana mabonde na milima. Unaweza ukajikuta hutaki kuongea na mtu kabisa kwa sababu ya kuudhiwa, lakini tafadhali sana ongea na Mungu. Acha mambo mnengine yote yasubiri, ongea na Mungu. Usiwe busy sana mpaka umsahau Mungu, kwani kwa kufanya hivyo unamkaribisha shetani kuja kukuharibu. Mke akajisogeza kwa mumewe na kumbusu mdomoni kimahaba zaidi. Akamkumbatia na kujilaza kifuani kwa mumewe. Mumewe akaanza kumchezea nywele zake huku mke akimsimulia jinsi gani alivyokua na siku ngumu, hasara aliyoipata baada ya mali aliyonunua kuharibika, kuibwa kwa 'power window' ya gari yake na purukushani zingine za siku nzima. Mke akajisikia akiwa salama mikonon mwa mumewe. Akacheka..akatabasamu. "Ok honey, twende tukapike. Nitakusaidia kupika. Wewe utapika wali mimi nitapika mboga" mume akaongea. Wakainuka na kuelekea jikoni, wakaanza kupika huku wakiimba na kutaniana. Watoto wakawa wakiwatazama wazazi wao wakicheka na kuimba kwa pamoja. Chakula kikawa tayari haraka na ilikua ni furaha kukitengeneza kwa pamoja, wakaungana na watoto wao kwenye meza. Wakala kwa furaha kama familia. Wakaenda kuwalaza watoto wao, na wao wakaelekea kulala. Usiku ule Wakapeana chakula cha wanandoa kwa furaha na amani tele. 1 Wakorintho 11:3 “Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.” Mungu abariki ndoa yako, Mungu abariki mahusiano yako yakawe yenye kuleta tija, ukajenge familia yenye amani, mshikamano na upendo. #AMEN Share
Artikel Terkait
NIFANYE NINI ILI MUME WANGU AWE NA HAMU NAMI?  Mume wangu anasema ananipenda sana, nami nampenda sana. Tuna watoto wawili wa kiume. Nimejaribu kila kitu cha kumfurahisha, kama vile kuvaa vizuri, kuandaa chakula kizuri akipendacho na kinywaji lakini Lakini mwenzangu haonekani kuridhishwa na jitihada zangu. Baada ya chakula cha usiku huwa tunakaa na kuangalia Luninga huku tukiwa na vinywaji. Lakini cha ajabu nikimsogelea na kutaka niwe karibu naye ananiepuka. Yaani HATAKI hata nimguse ni kama NINANUKA au ninamsumbua vile. Je, tatizo ni nini hasa, Je nanuka? Najiuliza na jibu sipati….Alimalizia kusema huyu mama huko chozi likimdondoka…...... Naam mara nyingi hivyo ndivyo inavyokuwa kwa sisi wanawake pale tukutanapo, si jambo geni sana kwa sisi wanawake kushirikiana kihisia. Ni jambo la kawaida kabisa kukuta mwanamke akimsimulia shoga yake anayemuamini juu ya madhila yake. Yote hiyo ni katika kutafuta nafuu na kuondokana na msongo wa mawazo. Mara nyingi simulizi nyingi zinazowakutanisha wanawake ni zile zinazohusiana na mambo ya Ndoa, mahusiano, watoto au mambo ya kifamilia kwa ujumla, mara nyingi tunatamani kupata mahali pa kulinganishia, ili kutaka kujua kama tatizo nililo nalo lina ukubwa kiasi gani. Ni hivi majuzi nikiwa kazini na mfanyakazi mwenzangu ndipo aliponieleza kile kinachomsibu kwa muda mrefu sasa, inavyoonekana, ni jambo ambalo alikaa nalo muda mrefu akijaribu kupambana nalo kimya kimya huku likiendelea kumtafuna, dada huyu wa Kiswidish. Ili kujiridhisha na kutaka kujua ukweli halisi nikamuuliza kama amemuuliza mume wake jambo hili akajibu amefanya hivyo na jawabu alilolipata ni kwamba, mume wake huwa anachoka. Yaani kazi zake ni nyingi pia malezi ya watoto yanamchosha. Nikamuuliza kama hawawezi wakati wa wikiendi watoke ili kuwa peke yao? Hapo nikapata jibu ambalo sikutegemea. Alidai kwamba akisema hivyo mume wake anaona kama yeye anaamua nini wafanye. Huyu mama akaendelea kusema, mimi ni binadamu Yasinta.,,,,,,,,,, Na nahitaji tendo la ndoa na sitaki kutoka nje kwani nampenda sana mume wangu. Nami sikuachia hapo kama mnavyonifahamu na u-Kapulya wangu nikamuuliza kama tatizo hilo lina muda gani au limeanza siku za karibuni? Mama yule akashusha pumzi, akaniangalia kwa jicho la huzuni, kisha akajibu kuwa inatokea wanafanya tendo la ndoa mara moja kwa mwezi na hapo ni ile ya haraka haraka na halafu baada ya hapo mume wake anampa mgongo na kulala . Hapo….akasita kidogo …nikamuuliza ulitaka kusema nini? Akaendelea unajua Yasinta mwanamke anahitaji kuandaliwa kwanza, mimi huwa siandaliwi kabisa........ Mweh! Nikaona makubwa haya ......nilikosa Jawabu la kumpa kwa kweli, nikabaki kuguna tu. Hata hivyo nilijaribu kumshauri aende kwa washauri nasaha wa masuala ya Ndoa na mahusiano, lakini akadai kuwa mumewe ni mkaidi na hawezi kukubali. Mwenzenu swala hili limenishinda maana sijui nimsaidieje! Je Wewe kama msomaji unaweza kunisaidia ni ushauri gani nimpe mama huyu, ili awe na furaha katika Maisha ya ndoa yake? Ushauri tafadhali........... ... Read More
Mimba kuharibika na Sababu zake  Tatizo la kuharibika kwa mimba limekuwa tatizo kubwa, na limekuwa likiwatesa wengi, kama we ni mongoni mwa watu hao nakusihi usome makala haya ili kuepukana na matatizo haya. Somo hili ni mahususi kwa sababu waawake wengi wamekuwa wakaiharibikiwa na mimba bila kujua sababu. Na zifuatazo ndizo sababu za kuharibika kwa mimba. 1.Mama anapokuwa na matatizo uvimbe (fibroid), huweza kuwa na madhara na kusababisha mimba kuharibika mara kwa mara. 2. Uzito mkubwa (unene) Nayo huweza kuchangia tatizo hilo kinachohitajika ni kuwa na uzito unastahili kulingana na mhusika mwenyewe. Pia inasadikika kuwa uwepo wa manyama uzembe tumboni ni chanzo pia kwa kuharibika kwa mimba kwani, mtoto hukaa kwa shinda. 3. Historia ya kuharibika mimba mara kwa mara Mama aliepata kukumbwa na hali hii ya kuharibika kwa mimba 'miscarriage' zaidi ya mara 2 anauwezo mkubwa wa kuharibika kwa mimba yake kila anaposhika. 4. Utoaji mimba Mwanamke anapotoa mimba mara kwa mara kizazi huweza kuchangia kizazi chake kushindwa kuhimili kubeba mimba zinazokuja mbeleni kwa miezi tisa, hivyo epuka kutoa mimba. 5. Matumizi ya Pombe,Sigara Wanawake wanaotumia vilevi hivyo nao huwa katika hatari ya k?kumbwa na tatizo hili, hivyo ni vyema kuepuka matumizi ya vitu hivyo. 6. Magonjwa sugu Mama anapokuwa anazongwa na magonjwa sugu kama kisukari , moyo nk huweza kuwa chanzo cha tatizo hili pia. ... Read More
*SIMULIZI DARASA* *STORY FUPI* *USIMDHARAU USIYEMJUA* Msichana mmoja alikuwa amempenda kijana mmoja mtanashati na mcha Mungu.. Malengo yao ilikua waje kuoana baada ya muda. Kijana huyu alijitoa sana kwa binti huyu hadi wenzie wakamuona mjinga, lakini ukweli ni kuwa alimpenda msichana yule kwa dhati. Alimtafutia kazi alipomaliza chuo, alimshauri kuhusu mipango ya maisha na alikua akimuombea kila alipopata nafasiya kuomba. Siku moja binti alikua anasherehekea siku yake ya kuzaliwa…hivyo akaalika marafiki zake, na watu wengine muhimu akiwemo mpenzi wake. Wageni wote walifika kwa wakati isipokua yule kijana alichelewa kidogo… Hivyo msichana akatumia muda ule ambao mpenzi wake hajafika kuwaeleza wageni namna yule kijana alivyokua wa muhimu kwake.. Akamsifia sana, akasema atamvalisha pete ya uchumba soon, na akasema siku hiyo ya birthday yake anategemea zawadi kubwa sana kutoka kwa huyo mpenzi wa nafsi yake. Baadae kijana akaingia na kuketi high table.. Muda wa zawadi ulipofika watu wakamtunza binti zawadi mbalimbali na kijana akawa wa mwisho… Hivyo wageni wote wakawa na hamu ya kutaka kujua zawadi aliyoleta hasa baada ya yule msichana kumsifia sana. Kijana akaamka na kutoa mfuko.. kila mtu akataka kujua kilichokua ndani ya mfuko..mara kijana akafungua mfuko na kutoa mkate..!! Lahaula… watu wote wakastaajabu.. mkate??? Lakini kabla hajasema lolote kuhusu ule mkate, yule msichana akaanza kulia.. akapandwa hasira kwa kuwa mpenzi wake amemuaibisha..!! Akiwa analia kwa kwikwi, akamkwida shati na kumvua tai yake, akamwagia juisi, kisha akauchukua ule mkate na kuutupa.!! Maskini..yule kijana akaukimbilia ule mkate na kuuokota.. Kisha akarudi high table na kusema “baby nakushukuru kwa yote..Huenda umenidharau kwa kuwa nimekuletea zawadi hii ndogo kwenye siku yako muhimu kama hii. Lakini kama ungetambua thamani ya zawadi hii, usingefanya haya..” Kisha akafungua ule mkate na kutoa vitu viwili alivyoficha ndani ya mkate.. Kwanza akatoa ufunguo wa gari, ambalo alikuwa amemnunulia mpenzi wake na alitaka amkabidhi siku hiyo ya birthday. Kisha akatoa pete ya uchumba na kusema “Nilimuomba Mungu anipe mwanamke atakayenipenda katika hali yoyote. Nilipanga leo nikuvalishe pete hii ili kuelekea ndoto yetu ya ndoa.. ..Lakini kwa kuwa uliangalia nje, uliona mkate, badala ya pete hii ya thamani iliyokua ndani.. Naamini mwanamke niliyemuomba kwa Mungu bado sijampata.. Nashukuru kwa yote uliyonifanyia, nimekusamehe, nawe naomba unisamehe kama nimekukwaza..” Kisha akachukua mkate wake, huyoo akaondoka. Msichana akaomba msamaha lakini ilikua too late.. MORAL OF THE STORY..! Usidharau kitu/mtu kwa kumtizama nje.. Mungu huangalia thamani ya kitu ndani lakini Wanadamu huangalia nje.. Thamani ya kitu/mtu ipo ndani na si rahisi kuonekana.. Usiwe mwepesi wa kuhukumu kwa kutizama umbo la nje.. Wale wanaokudharau leo na kukuona mkate, ipo siku watagundua haukua mkate wa kawaida… kuna vingi vya thamani ndani yako. Wote wanaokudharau leo ipo siku watakusalimia kwa heshima..!! 🌹TUELIMISHANE MEMA🌹 Subra ndio inayotakiwa katika maisha. *akida* ... Read More
UMESOMA HADITHI NYINGI ZA MAPENZI, LAKINI HII ITAKUSISIMUA KULIKO ZOTE, UTATUMIA DAKIKA 2 KUSOMA LAKINI...  1st year nikiwa nimekaa leacture room nikimuangalia msichana aliyekaribu yangu,niliyekuwa nikimuita "Bestfriend"nilikuwa nikimuangalia nywele zake nzuri na sura yake ya upole huku nikitamani awe wangu,lakini yeye hakuwa akitamani hilo na nilikuwa nikilitambua hilo. Baada ya leacture,alikuja kwangu na kuniomba notes za siku ya nyuma kwa sababu hakuweza kuingia darasani hiyo siku iliyopita.baada ya kumpa akasema "asante" na kushikana mikono na mimi.I wanted to tell her,i want her to know that i don't want us to be just friends,i love her but i'm just to shy,and i don't know why 2nd year Simu yangu iliita,kupokea alikuwa yeye alikuwa akilia akinielezea jinsi gani boyfriend wake broke her heart,she asked me to come over because she didn't want to be alone,kwa kuwa ni rafiki yangu kipenzi ilinibidi kwenda kumfariji,as i sat next to her on the sofa,nilikuwa nikimuangalia Machoni nikitamani awe wangu.Baada ya masaa mawili baada ya kuangalia nae movie mbili tatu na kula nae chakula pamoja akarudi katika hali yake ya kawaida,hivyo akaamua kwenda kulala,before akaniangalia na kuniambia "asante" na kunipa tabasamu tamu,i want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why. 3rd year Siku moja kabla ya Tamasha la muziki chuoni alikuja kwenye meza yangu leacture room na kuniambia "Boyfriend wangu amepata udhuru hivyo naomba unipe campan katika tamasha la muziki leo usiku" kwa kuwa tuliwekeana promice kwamba ikitokea kila mmoja wetu amekosa mtu wa ku-date nae basi tutaenda pamoja just as "bestfriends".hivyo tukaenda. katika tamasha baada ya kila kitu kuisha na muziki kufungwa,nilikuwa nimekaa nje ya ukumbi nikimuangalia jinsi alivyokuwa akicheka na rafiki zake,she saw me looking to her she smiled at me,i want her to be mine lakini yeye alikuwa hafikirii hilo kabisa na nilikuwa nikilitambua hilo,then she said to me "nimekuwa na muda mzuri na wewe asante sana" and she gave me a sweet smile.I want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why. Graduation Day siku,wiki kisha mwezi ukapita ilikuwa ni mahafali yetu tukimaliza masomo ya chuo,akiinuka kwenda kutunukiwa shahada yake ya uchumi nilikuwa nikimuangalia akiwa amependeza sana siku ile,i wanted her to be mine,but she didn't notice me like that,and i knew it. kabla watu hawajatawanyika kwenda makwao,alikuja kwangu akiwa na vazi lake la mahafali,na kulia pale nilipomkumbatia akainua kichwa chake na kuniambia "you are my bestfriend asante sana" i want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why. Miaka michache baadae Nikiwa kanisani Yule Msichana akiwa anaolewa sasa,nilimuangalia akisema "ndiyo nakubali " and drive off to new life,kaolewa na mwanaume mwingine,i wanted her to be mine,but she didn't see me like that,and i knew it. but before she drove away,alikuja kwangu na kusema "asante sana" and kissed me on the cheek.I want to tell her to know that i dont us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why. Kwenye Mazishi Miaka ilipita i looked down katika jeneza lilokuwa na msichna ambaye alikuwa ni "bestfriend" wangu,Katika Service ya mazishi wakasoma diary ya Bestfriend ambayo alikuwa akiiandika enzi za maisha ya chuo' Diary yake ilikuwa Ilikuwa ikisomeka hivi I stare at him napenda awe wangu,but he doesn't notice me like that,and i know it,i want to tell him,i want him to know that i dont want us to be just friends,i love him but i'm just to shy,and i dont know why.I wish he would tell me he loved me! Nilipiga magoti huku nikilia nikijisemea moyoni i wish ningemwambia tu ukweli,nimeshachelewa sipo nae tena katangulia mbele za haki i cried!! Vunja ukimya ... Read More
NJIA RAHISI 13 ZA KUWA NA FURAHA KILA SIKU  Mabadiliko yalio mepesi kwenye tabia zako za kila siku yatakuweka kwenye mstari wa furaha unayoitaka Umejikuta uko kwenye siku tofauti, story hizo hizo, imekuwa ni kawaida yako? Basi muda huu , sio kesho , sio wiki ijayo, ni wakati wa kubadilisha historia yako. ni za haraka, rahisi na hazina gharama unapofanya hivyo na matokeo yatakupa furaha unayoitaka. 1.Pata masaa 7 mpaka 8 ya kulala usiku. Kulala usingizi wa kutosha unapata furaha, utaweza kuwa na nguvu ya kufanya kazi zako , na utakuwa na mahusiano mazuri. weka simu yako mbali unapoenda kulala, usitumie chakula kingi wakati wa jioni. 2.Amka mapema , dakika 30 kabla . Kama wewe ni mfanya kazi wa kuajiriwa na una tabia ya kuchelewa kazini, jaribu kuamka mapema dakika 15 au 30 kila siku kwa ajili ya kujiandaa vizuri na kukumbuka vitu vyote vya kufanya, kuchukua siku hio. utaona tofauti ya tabia yako. 3.Meditate. Hii ni kubwa. meditate kwa muda wa dakika 10 au 20, utapata faida nyingi zaidi ya furaha, pamoja na kuwa muwazi, kuwa na malengo ya siku nzima. Anza siku yako na meditation. utajiepusha na tress na wasiwasi na hutachanganyikiwa na kazi zako. 4.Jipe nafasi wengi wetu huwa tunajaza vitu nyumbani, ofisini hata vile ambavyo havina kazi, hatuvitumii. inaharibu mfumo mzima wa akili yako, hisia zako, na mwili wako. Ondoa vitu ambavyo huvitumii, tupa nje au gawia watu ambao wanahitaji kuwa navyo, hali yako ya furaha itaboreka. Na hutalemewa na kazi nyingi. 5.Jifunze kitu kipya Jitahidi kujifunza kitu kipya kila siku, kwa sababu hio ndio changamoto itakayokupa furaha, kujifunza kitu kipya inaboresha afya yako ya mwili na akili, kujifunza utajenga ujasiri pia na utakuwa sharp. 6.Tembea mara kwa mara Kutembea kwa dakika 30 kwa siku moyo wako utakuwa unafanya kazi vizuri, utapunguza hasira, hutakuwa na chuki. Kama unaona ni ngumu kwako kutembea , hasa kama una gari , jifunze kupaki gari yako mahali mbali na ofisi , tembea . anza kutumia maji ya kutosha. utapata faida nyingi . 7.Usijihusishe na mambo ya mitandao. Ni rahisi kuingia instagram, facebook na zingine, lakini wachunguzi wanasema kwamba ukizidisha kujihusisha na mitandao unaweza kuharibu afya yako ya akili. badala ya kutumia nusu saa kwenye mitandao, unaweza kufanya kitu kingine unachokipenda, au kusoma kitabu, kujifunza mafunzo mbalimbali kwa ajili ya kujiboresha mwenyewe kuwa mwenye afya. 8.Kuwa mwema. Ukarimu unakuongoza kwenye furaha yako mwenyewe na utakuwa mwenye afya bora. vitu ambavyo vinavyo chochea furaha ni kutoa , na kuwa mkweli , utapata faida , na utajisikia vizuri kuwa sehemu ya baraka kwa mtu fulani. kujitolea kufanya kitu, au kumwachia mtu kiti kwenye daladala. Sehemu ngumu? lakini nzuri. 9.Kaa na watu wenye furaha. Angalia watu unaoshinda nao, unaofanya nao kazi, ni watu wa aina gani. kwa sababu kuna msemo unasema kuwa ukikaa na ua rose utanukia hata kama ulikuwa hunukii. Fanya hivyo na utaweza kufungua mlango mpya kwa ajili yako maishani. utaiona furaha ikitiririka kama mto. 10.Don’t gossip. Kuseng’enya, umbeya, itakusababishia maradhi ya misongo na kukosa furaha. mtu mmbeya hawezi kusaidia kitu. wakati mwingine jitenge na watu kama hawa, au unapoona kuna kutoelewana na wafanya kazi wenzako, jaribu kutulia kwanza , badilisha negative to positive. Sema kitu kizuri kuhusu mtu. ni vizuri. kwa sababu utajiwekea alama nzuri kwako. 11.Tumia muda wako na watu unaowapenda Unapoongea na familia au marafiki kwenye simu , inatia moyo. mawasiliano hayo yanakupa afya na furaha.Fikiri ilivyo vizuri kama utaenda kula na rafiki yako mahali fulani, au kuamua kupika nyumbani , au kucheza na watoto wako kitu kama game, mpira, inafurahisha. 12.Journal Kuandika vitu vya kufanya kwa siku, au kuandika vitu unavyotaka kuvipata, Lengo hili dogo litaongeza IQ yako na kuleta utulivu wa kuboresha ujasiri wako, ukiwa na tabia hii kila siku , furaha haitakosekana kwako na utapata faida ya akili na hisia zako zitakuwa bora. 13.Jizoeze kujijali. Unapojijali ,Utaona faida zake, pamoja na kuondoa stress na wasiwasi, utakuwa mtu wa kuwaza mazuri na utaboresha immunity.pata muda kila siku kufanya kitu kwa ajili ya furaha, kama vile mazoezi, kupika chakula kizuri, kusoma . utaanza kushangaa jinsi ilivyo rahisi kuwa na furaha unapojijali na utaboresha akili yako na mwili wako, na roho yako. Kama unavyojua , kuna njia nyingi zinazotushambulia kwa siku, Ondoka mahali ambapo panaharibu ratiba yako. sasa, kama kitu kingine chochote,mafanikio ni kufanyia kazi. kwa hio pick one, and let the fun begin! ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: