Unapo mzungumzia MAMA unataja jinsia ya MWANAMKE... Mwanamke ni nguzo katika maisha ya kila kiumbe kiitwacho BIN ADAM! Sikatai wapo wanawake wachache wamejaribu kuimega heshima ya Mwanamke, lakini pamoja na hilo Mimi huwaita wanawake wa mwendo kasi, Maana nimjuavyo Mwanamke ni mtu ambaye ana Maono, Mipango, Uthubutu, kujiamini na mengine mengi tu na mwanamke wa aina hiyo huyo ndo MKE... Mizani ya Mwanamke huwezi kuilinganisha na mizani ya Mwanaume, Nafasi ya Mwanamke katika jamii ni kubwa sana japo imemezwa na mfumo dume, Nikijiuliza HIVI HUO MFUMO DUME KWANINI UENDELEE NA HUKU TUNAJUWA VILE MAMA ZETU WALIVYOISHI KWA TAABU KATIKA NDOA ZAO? Mwanaume yeyote ambaye anampenda mama yake na kukumbuka vile Mama huyo alipitia changamoto katika ndoa yake ili kumlinda yeye ikiwa anazo akili timamu YAMBIDI AMPENDE MKEWE NA KUMPA HESHIMA ili pendo hilo liwe kama ushuhuda wa malezi ya mama kwake, Mama aliyepitia magumu katika ndoa yake ombi lake la kwanza ni kuuona uzao wake ukiwa wenye furaha sasa wewe ukijiona kidume na ukafuata vijitabia vya baba yako na ukamtesa mkeo ujue HUPATI RADHI YA MAMA.

at 4:10 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top