SIRI YA GIZANI NO 12 Kipindi Ibra na wazazi wake wameishiwa nguvu pale sebreni, hakuna ata mmoja alie weza kugundua kama kuzidiwa nguvu kule ni bibi Nasra alisababisha, na alifanya vile kusudi wasiweze kugundua kuwa kaburi la Nasra alionekani usiku. Mama nasra alilia sana siku hiyo kwasababu ule mguu ulimuuma sana, baba nasra alikuwa anasema, "vumilia mke wangu utapona mama Nasra" ibra akasema "baba hamka tukaangalie kaburi sasa" baba Nasra akasema nimechoka sana mwanangu tuta angalia kesho" kweli walilala pale mpaka saa 2 asubui, bibi Nasra alipo toka chumbani kwake akajifanya kama haelewi akasema, "vipi wanangu mbona kama mmelala hapa sebreni tatizo nini" wote wakajishangaa wakaamka na kuendelea na shughuri zingine. Ibra hakulizika kabisa na maisha ya pale nyumbani kwao akakaa na kuwaza kwamba "mhh hivi kwanini bibi anatufanyia hivi lakini, ata kama yeye ndiyo mzizi baba anavyo sema, lakini kwanini anatuloga, hatuishi kwa raha kama zamani tunateseka tu ngoja nimfate nimueleze, kama atanipiga sawa" ibra akaenda mpaka chumbani kwa bibi yake bila kugonga hodi, alivyo ingia tu masikini, akamkuta Nasra amepakwa dawa nyingi sana usoni na anasukwa nywere na bibi yake, bibi alikuwa bado hajamuona Ibra, ila kutokana na ibra kuona mambo kama yale alishindwa kuvumilia kabisaa, akapiga kelele, "bibiii unamsuka dada Nasra kwanini unafanya hivi lakini" bibi aligeuka kwa hasila jicho lekunduu, akasema "We ibra kwanini unaingia bila kugonga" Ibra akasema, "namtaka dada Nasra huyo hapo unamsuka" bibi nasra akasema naona umezidi kunifanyia ushenzi lazima nikukomeshe" Nasra hakuweza kuongea chochote yeye alikuwa kimya tu, ila ibra alishangaa tena kuona Nasra haonekani maana bibi yake alimficha kishirikina, Ibra hakukaa kimya akawafata wazazi wake kisha akawambia "baba na mama nataka kuwambia jambo" mama yake akasema, "twambie" kipindi Ibra ana achama mdomo anataka kusema alivyo muona Nasra, wazazi wake walishangaa, kuona ibra anashindwa kutoa sauti kabisa mdomoni mwake, ibra alijitahidi kuongea ila ikashindikana, kumbe tayari bibi yake alikuwa ameisha mfanya Ibra bubu, na asinge weza kuongea katika maisha yake yote, na bibi Nasra akapanga kumpofua macho Ibra ili asione na kusema chochote tena.... USIKOSE YA#13

at 11:57 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top