SIRI YA GIZANI NO 11 Sasa Nasra alivyo vutwa kighafla na bibi yake kutoka chumbani, bibi yao alikasilika akasema, "hivi we Nasra kwanini hutulii, unataka nikudhoofishe mwili mzima usiweze kusimama au, sasa toka tena umo uone" Nasra alipo ambiwa vile alikuwa analia tu, maana yale mateso yalikuwa mazito sana, kwasababu alikuwa hatoki ndani na asingeweza kuonekana n'je kama zamani. Bibi Nasra alikuwa amenuna mpaka jicho likawa jekunduuu, akasema, "hivi unajua mwanangu akinigundua mimi ni mchawi nita aibika sana, sasa huyo kaka yako lazima na yeye nimkomeshe atakiona cha moto" Kumbe chumbani mwa ibra wazazi walikuwemo bado wanalia tu, maana kila walipo jitahidi kusahau kifo cha mtoto wao, Ibra alikuwa ana wakumbusha tu kwa matukio ya ajabu ajabu tu, mama Nasra akasema, "mme wangu hii ni mikosi gani jamani, nitazame mguu wangu ulivyo haribika, nusa harufu initokayo sehemu zangu za siri, haya sasa ebu kumbuka mtoto wangu Nasra alivyo fariki kimaajabu tu, hivi tutaishi kwa amani kweli jamani, alafu kila tukio linatokea usiku kuna siri gani za giza humu baba Nasra" Ibra akasema, "wazazi wangu mimi nateseka sana, maana kila ninapo lala tu dada nasra ananitokea ndotoni analia, na bibi ndiye amemficha dada Nasra yaani dada yangu hajafa mama" baba Nasra akasema, "weee husimtaje mama yangu katika hili nakuomba sana, alafu wewe mtoto umeisha kuwa muhuni sana, hivi hutambui kuwa yule bibi yako, ni kama mzazi wako, ata kama hajakuzaa lakini yeye ndiye mzizi bila yeye kunizaa mimi, tungekuzaa vipi sasa" mama Nasra akasema, "mme wangu tatizo lako humsikilizi mtoto unazalau maono yake mme wangu" Ibra akasema "wazazi wangu kama mnataka kuamini kuwa Nasra hajafa, twendeni kabulini kwake, mkiliona kaburi lake usiku mjue amekufa, na msipo liona muamini ninacho wambia hajafa, kipindi wanapanga kutoka nje kumbe bibi nasra alikuwa anawasikia tu, akapuliza dawa haraka sebureni! Sasa wakati wanafungua mlango wa sebreni kutoka nje, hakuna alie weza kufungua, maana baba alijikuta anachoka ghafla tu, Ibra alilala kabisa pale mlangoni na mama Nasra uvimbe wa mguu ulizidi maumivu ata kutembea alishindwa, kwa sababu ya dawa iliyo pulizwa na bibi Nasra . USIKOSE YA 12

at 11:57 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top