SIRI ZA GIZANI No_6 Kaka yangu hakufanikiwa kabisa kuona ule uvimbe kwenye sehemu nyeti za mke wake, hivyo kaka hakutaka kabisa kumlazimisha mke wake maana alikuwa anampenda sana mkewe na kwakuwa alikuwa anaumwa akaona sio vyema kumlazimisha kitu ambacho hataki. Siku hiyo ikapita bila mafanikio yoyote, sasa kesho yake usiku mida ya saa nane kamili, mkwe wa shemeji aliamka mida hiyo kukiwa na giza sana akaenda kwenye chumba cha mjukuu wake wa kike binti Nasra, alipo fika chumbani akiwa amejifunga kitambaa chekundu kichwani, akafungua mkono wake wa kushoto kisha akapuliza unga alio kuwa ameushikilia kuelekea kwenye uso wa mjukuu wake, palepale nasra akaamka na kupanda kwenye mgongo wa bibi yake akiwa hajitambui na hasikii chochote, mama alimbeba Nasra watu wote wakiwa wamelala ndani, kisha akamuweka kwenye diaba chumbani kwake alafu akaweka na dawa mule kwenye diaba ili Nasra asiweze kabisa kuongea, sasa kulipo kucha kila mtu aliamka lakini cha kushangaza Nasra siku hiyo hakuamka, na wakati Nasra alizoeleka kuamka mapema kila siku pale nyumbani. Ikabidi waende chumbani kwake kumuangalia, walipo fika wakamkuta amelala, akiwa amejinyoosha, alafu akiwa na unga unga usoni, shemeji alijaribu sana kumuamsha binti yake lakini alikuwa haamki, kumbe mwili wa Nasra ulikuwa umewekwa kwenye diaba chumbani kwa bibi yake, na ule ulio onekana umelala hakuwa yeye Nasra mwenyewe bali ilikuwa ni kama egesho tu kuonekana Nasra amefariki, mama Nasra alijaribu kumuamsha Nasra ila ikashindikana ndipo mkwe wake akasema "mkwe usilie hii ni mipango ya mungu tu, huyu mtoto ameisha fariki tayari" shemeji alianguka chini hapohapo mpaka akajitonesha vidonda vya mguu wake, alilia akasema, "hii ni mikosi gani jamani nani anatufanyia hivi, binti yangu bado mdogo hajaona hata ndoto zake wameisha mchukua tayari, ehh mungu wangu nisaidie, bora nife ata leo lakini watoto wangu wasife, nime wazaa kwa uchungu sana" dahh kaka yangu alipo ona mke wake analia na mtoto kafariki alichoka sana, ilimuuma mnoo, kumbe hakujua ubaya wote ule alikuwa anaufanya mama yetu mzazi. Nasra alizikwa lakini kumbe hakufa yeye ni egesho tu, yeye alikuwa kwenye diaba chumbani na amekatwa ulimi alafu analishwa unga tu na bibi yake..#7 USIKOSE YA 7

at 9:44 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top