SIRI ZA GIZANI NO 5 Harufu ya shemeji ilipo zidi kwenye kikao, ndugu na jamaa wakashindwa kuvumilia ikabidi waongee tu, "shemeji hiyo harufu mbaya inatokea wapi, yaani kama mizoga ya wafu kunanuka sana hapa" mkwe wake shangazi alie mfanya shemeji awe vile akaanza kucheka "hahahah, ata mimi nahisi harufu mbaya",mme wake shemeji yaani kaka, akasema, "hii harufu kila siku nikiwa nimelala na mke wangu uwa nahisi kwa mbali, sijui ni kitu gani kimeoza maeneo ya hapa nyumbani" shemeji akauliza "mke wangu kitakuwa nini hicho maana balaa zimezidi kwenye familia yetu" shemeji akaanza kulia maana ukweli alikuwa anaujua yeye kwamba harufu inatokea sehemu zake za siri, kaka akasema, "mke wangu unalia nini mbona hatukuelewi" shemeji akasema, "mimi najua wote mnajua kuwa mimi ndiye nanuka, maana n'zi wamenijaa na kunizunguka mimi" kila mtu akaguna, "mhhh" shemeji akasema tena, "mme wangu kwa sasa hivi hatua niliyo fikia ni bora tu nife, maana nimepata kidonda cha ghafla sehemu zangu za siri, na hii harufu mbaya mnayo hisi nyie inatoka kwenye hichi kidonda changu kwa ndani, nakosa raha ya maisha nakosa amani, maana kila mda mimi naenda bafuni, na kinacho nikwaza, ni pale ninapo waona wadudu wadogo aina ya funza wanatembea kwenye kidonda, sijui ni nani ananifanyia hivi, maana natembelewa na funza kabla sijafa, nikifa je?" wakati wanaongea mda ule na hewa pia ilikuwa inaendelea kuchafuka, hivyo shemeji akaomba aende bafuni kujimwagia maji kwanza. Wale walio kuwa wamebaki kwenye kikao wakamwambia kaka kwamba, "itabidi ukamuangalie mke wako hicho kidonda kina fananaje ili utwambie tujue jinsi ya kumsaidia, maana sio kwa harufu hiyo, hiyo harufu sio ya kawaida kwenye mwili wa binadamu alie hai"ikabidi kaka aende chumbani kumuangalia mke wake amekuwaje, wakati huo mkwe wa shemeji amekaa kimya tu na anaonyesha sura ya huzuni uwezi ata kumgundua kama ni yeye anafanya mabaya hayo usiku gizani tena kisiri. Kaka alipo ingia chumbani akamkuta mke wake anajipulizia marashi kwa ndani ili harufu isije kwa ulahisi, kaka akamwambia, "mke wangu naomba nione hicho kidonda kilivyo" shemeji akaogopa na akakataa katakata, maana alihisi mme wake akiona tu jinsi alivyo oza, anaweza kumuacha na akaoa mke mwingine....usikose ya 6

at 10:55 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top