SIRI ZA GIZANI 2 Wageni walipo mtembelea mke wa kaka yangu, baada ya mda wakaitaji kuondoka, kwasababu ilikuwa tayari ni usiku mida ya kama saa mbili hivi. Shemeji akaamua kuwa sindikiza ili awatoe nje kidogo kisha waendelee na safari yao. Sasa wakati shemeji yangu anarudi nyumbani bahati mbaya kiatu chake cha kushoto kikakatika, maana kilikuwa ni kiatu cha wazi, shemeji hakuwa na jinsi hivyo akaamua kukibeba ili arudi nacho nyumbani kisha kipelekwe kwa fundi kushonwa. Sasa wakati shangazi anatembea mguu ukiwa peku, bahati mbaya akakanyaga mdudu bila kujua ila alihisi kama amekanyaga kitu kisha kikabonyea, ila kutokana na lile giza hakuweza kuangaika kutazama amekanyaga nini wakati ule. Sasa kumbe ulikuwa ni uchawi tu, majirani zake wamemtumia kusudi tu ateseke na familia nzima iwe katika majonzi, kipindi kaka amerudi kutoka kazini akakuta familia yake ipo na furaha na walikuwa na upendo sana. Kibaya zaidi ni pale ilipo fika saa nane usiku sasa, yule mdudu ambae shemeji alimkanyaga ndiyo akaanza kufanya kazi, huwezi kuamini shemeji yangu alianza kuchemka sana mwili, yaani jasho lina mtiririka sana, kaka akajaribu kumkanda na maji ya baridi ila hari iliendelea kuwa mbaya, kipindi shemeji analia maana alikuwa anaogopa sana ugonjwa, kakidonda kadogo tu, kakaanza kujitokeza mguuni, shemeji hakuhisi chochote akaendelea kukaa tu anajua labda kidonda ni kidogo kitapona, lakini kila kulipo kuwa kunakucha mguu unauma, unawasha, anapata maumivu makali mpaka akaacha kwenda kazini, kaka akaamua kumpeleka mke wake hospitali, alipo fika wakampa dawa na kumchoma sindano, kumbe hapo pia ndipo wakawa wamearibu kila kitu, maana uchawi ukichanganya na madawa ya kawaida unakuwa unaua kabisa, mguu wa shemeji ulianza kuvimba, ulivimba sana ukawa mkubwa kuzidi ata mwili wake, ata watoto wakaanza kuogopa! kaka yangu akashangaa kumuoa mke wake vile, ikabidi arudi hospitali, alipo fika huko, daktari akasema "hii itakuwa kansa hivyo itabidi tumkate mguu wake ili asiendee kuvimba hivi maana anaweza akafariki tukiendelea kusubilia". Shemeji alipo ambiwa kukatwa mguu alianza kulia sana akasema, "mme wangu ni bora tu nife, siwezi kutazama nakatwa mguu, nimemkosea mungu mimi nimekosa nini jamani ehh" USIKOSE 3

at 10:54 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top