SIRI YA GIZANI NO 9 Ibra akasema "baba usibishe nimemuona dada Nasra kwa macho yangu akiogeshwa na bibi chumbani kwake", baba yake akasema "yaani kumbe wewe na mama yako sio watu wazuri kabisa hivi mnathubutu kumuita mama yangu mchawi" shemeji akasema, "mme wangu sio kwamba tunamuita mchawi jamani, mbona unataka ukuze maneno baba watoto lakini, uwezi jua ya mungu mengi labda mtoto kweli kaona, tufatilie zaidi" baba nasra akasema, "weeeeh, koma uchunguzi wa nini, mama yangu hawezi kuwa mchawi bhana sijawai ata kumuona na mzizi tangu nikiwa mdogo mimi, iweje mseme ni mchawi alafu wewe Ibra nikifanya uchunguzi nikakuta unaleta uongo uongo wako hapa naweza ata kukuua, sipendi masihala na mzazi mimi" baada ya kaka kuongea vile ndipo akamwambia mke wake amuitie bibi nasra ili wamwambie kuhusu tatizo lililo tokea. Kweli bibi nasra alitoka akiwa amevaa kanga zake mwilini. Baba nasra akamwambia, "mama habari za usiku, samahani mama yangu tumepata habari za kusikitisha, eti kwamba Nasra hajafa na wewe ndiyo upo nae ndani unamuogesha na kucheza nae humo chumbani kwako" bibi nasra alipo ambiwa hivyo akaanza kulia akisema, "mwanangu nimekuzaa na kukuweka tumboni miezi 9 leo hii unaniita mchawi kisa familia yako hii, kama ningekuwa mchawi ningekulea mpaka umri huu, sawa najua m'menichoka mi naondoka kijijini usiku huu huu na sitorudi tena hapa kwenu" baba nasra alipo sikia yale maneno alipiga magoti chini akasema, "mama yangu naomba msamaha tafadhali, ni huyu ibra katuamsha usiku usiku anatwambia huu upuuzi, kwamba kamuona Nasra chumbani kwako na amesisitizia kweli kwamba amekuona unamuogesha ndiyo maana nikakuuliza mama yangu, nakuomba sana usiondoke kwangu mama yangu" bibi Nasra akasema, "we ibra kwanini unakua muongo namna hiyo we Nasra umemuona kwangu lini, Nasra si ameisha fariki mjukuu wangu" ibra akasema, "bibi wewe ni mchawi, Nasra unae ndani, kama kweli hayupo ndani turuhusu tukakukague" bibi nasra akasema, "Mama nasra huyu mtoto unamleaje mbona hana heshima kabisa masikini" Ibra alichapwa sana siku hiyo kisha wakaenda kulala bila kugundua chochote.Bibi Nasra aliwaza sana jinsi ya kumzuia Ibra asigundue siri zake za usiku, ndipo akapata wazo la kumpofua macho ibra ili asione tena katika maisha yake.....ITAENDELEA. 10

at 12:32 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top