SIRI YA GIZANI NO 10 Ibra alikuwa anakosa raha sana pale nyumbani, maana wazazi wake walijua kuwa Nasra kafariki lakini yeye kilicho kuwa kina muuma ni pale alipo kuwa akimuona dada yake anaogeshwa na usiku kaburi la Nasra alionekani bali linaonekana mchana tu. Siku moja mida ya saa nane usiku, Ibra alianza kusikia joto kali sana kwenye mwili wake, yaani ni usiku lakini joto lake ni kama la mchana hivi. Ibra alikosa usingizi kabisa masikini aka amka kisha akakaa kitandani. Joto lilipo zidi Ibra akaamua kuamka ili achukue kitambaa ajifute jasho, wakati amesimama sakafuni akasikia mtu anamshika begani, "wehh wehh" alipo geuka haraka akaona sura ya bibi yake mala ghafla ikaja sura ya mdogo wake, ibra akamwambia " dada Nasra mbona siku hizi utaki kucheza na mimi" Nasra akaachama mdomo wake kisha akamuonyesha ibra kuwa hawezi kuongea bibi yake tayari ameisha mkata ulimi kwa mbele, ibra aliogopa kumtazama dada yake akiwa vile akaamua kumshika kwanguvu Nasra alafu akaanza kupiga kelele "mamaaaa, babaaa, Nasra huyu hapa nimemkamata njooni" wazazi wake waliamka upesi kisha wakaenda chumbani kwa Ibra ili waweze kumuona Nasra mwenyewe, sasa kilicho washangaza ni kwamba, wanamuona Ibra kama kashika mtu kwa nguvu lakini mtu mwenyewe alie shikwa hawamuoni, wakamuuliza, "Ibra mbona kama umeshika hewa mwanetu, nasra yuko wapi" ibra akasema "baba si huyu hapa nimemshikilia" baba akasema, "hatumuoni sisi mtu mwenyewe ebu acha ndoto za kishirikina rudi ulale", Ibra akasema, "mama njoo umshike Nasra bibi atamchukua, mama nisaidie kumshika" mama nasra alikuwa analia tu, "mwanangu simuoni nasra, simuoni kweli baba angu" Nasra alikuwa kawekewa madawa mengi sana na bibi yake hivyo kuonekana kwake kulikuwa kwa shida sana masikini, ila nasra alikuwa anawaona wazazi wake lakini hasingeweza kuwaongelesha maana ata ndimi yake ilikuwa imepunguzwa tayari, Ibra aliendelea kumvuta dada yake bila kumuachia huku akiwa analia na Nasra pia analia maana hawawezi kucheza tena masikini, sasa kumbe nasra alitoroka bibi akiwa amelala, bibi alipo shituka akakuta nasra ameingia kwa Ibra hapo hapo akamvuta kichawi nasra akapotea ghafla tu, ibra akasema "mama, Nasra amepotea tena" wazazi wa Nasra walilia sana mule ndani.. USIKOSE YA 11

at 12:33 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top