Home → ushauri
→ MKE WANGU AMEBADILIKA.
Akapokea sms kwenye simu yake. Sms kutoka kwa mkewe. Sms ilisomeka hivi;
"Hi my love, niko katika mood ya maombi. Kuna jambo lolote unataka niliombee?"
Mume akaisoma sms mara mbili mbili kwa mshangao. Mkewe hajamuita kwa jina la "my love" kwa kipindi kirefu sana. Na zaidi mkewe hajawahi kumuuliza jambo la kuombea. Ughafla huu ukamshangaza!
Mume akaona amjibu tu hivyo hivyo..akamrudishia sms kwa kuandika;
"Fanya maombi ya shukrani, mshukuru Mungu kwa ajili ya promotion niliyopata kazini".
"Umepanda cheo? Lini?" Mkewe akamtumia sms ya kumuuliza.
Mume akakukumbuka kuwa hakumwambia mkewe kwamba amepanda cheo. Kwa sababu mkewe ni jeuri huwa hawezi ku-appreciate jitihada zake na kazi ngumu anazofanya. Yeye hua ni kulalamika tu. Hivyo alivyopanda cheo aliona akimwambia mkewe ataishia kulalamika.
"Ni mwezi, niko na ofisi mpya hivi sasa. Samahani, sikukwambia mapema". Mume akajibu.
Dakika nne zikapita bila mkewe kumjibu sms ya mwisho. Mume akajua mkewe ameshakasirika kama kawaida yake.
Simu yake ikaita. Mkewe alikuwa anapiga.
Mume akaguna. Hiki ni kimbembe, anahofia drama za mkewe.
"Hello" mume akapokea simu.
"Hi my love" mke akaongea upande wa pili.
"Mmh" Mume akaguna baada ya kuitwa 'my love'. Sio kawaida hii.
Mke akaendelea kuongea kwenye simu..
"Samahani mume wangu, nilikua na-drive nimetoka shule kwa binti yetu Monalisa kwenye siku yao ya vipaji shuleni. Oh, tumebarikiwa na Mungu kuwa na huyu binti wa ajabu. Anakipaji kikubwa cha kuimba. Ameshinda tuzo shuleni. Shule imemtunuku nishani". Mke akamwambia mumewe kwenye simu kwa furaha.
Mume akashikwa na mshangao. Hakutarajia mke ataongea na yeye kwa ustarabu na kwa furaha kiasi kile.
"Ameshinda tuzo ya uimbaji? Oh my God. Hongera sana kwa binti yetu Mona." Mume nae akajibu kwa furaha.
"Ndio ameshinda tuzo, amekuwa wa kwanza. Inabidi tuanze kumpeleka kwenye darasa la muziki pia. Natamani na wewe ungekuwepo. Ila usijali nimerekodi video alivyokua akiimba" Mke akaongea.
Mume akawa bado amechangamyikiwa. Kwa kawaida mkewe angeanza kumlaumu kwa namna gani alivyo baba mbaya kwa vile hashiriki kwenye shughuri za shuleni kwa watoto wao wawili.
Mfano siku za wazazi na siku za vipaji vya watoto shuleni. Ingawa mkewe anafahamu kabisa kazi zinambana na kazi ya mkewe kidogo inao unafuu hivyo mke anaweza kwenda. Mume angependa kweli kuhudhuria lakini kazi sio rafiki kwake. Licha ya hayo mkewe alikua akimlalamikia.
"Anyway my love, nilikupigia simu kukupongeza kwa kupanda cheo. Ninajivunia sana kuwa na wewe. Najua uko busy na kazi, je naweza kuomba na wewe kwenye simu?" Mke akaongea.
Mume akakohoa kidogo kwa mshangao.
"Ndio, ndio tuombe tu haina shida" mume akaongea.
Kwa mara ya kwanza kama wanandoa wakasali pamoja kupitia simu. Ilikuwa ni sala fupi lakini yenye faraja.
"Amen" mke akamaliza.
"Amen" mume nae akaitikia.
"Ok my love. Nikuache uendelee na kazi. Tutaonana baadae nyumbani. Nakupenda eeh!".
Akakata simu.
Mume akaangalia kwenye screen ya simu yake. Akaona picha ya kwake, mkewe na watoto wao wawili. Picha ya muda kama mwaka mmoja hivi uliopita na akai-save kama wallpaper na screensaver.
Akajikuta akitabasamu huku akiangalia screen.
"Mambo mazuri" akawaza kichwani mwake.
Akajikuta akiwa na mood nzuri na akafanya kazi vizuri zaidi. Akawa na furaha pamoja kujiamini fulani hivi baada ya kuongea na ile simu ya mkewe. Akawa akicheka na kufurahi zaidi na wafanyakazi wenzake pale ofisini.
Akapokea sms kutoka WhatsApp.
Alikuwa ni mkewe. Amemtumia ile video ya binti yake Mona akiimba shuleni kwenye siku ya vipaji.
"Muangalie binti yetu. Awww..inafurahisha na inatia moyo" ilikuwa ni caption ya hiyo video aliyotuma.
Mume akaidownload video na kuangalia binti yake akiimba kwenye stage.
"Nimemiss vingi mke wangu" mume akamjibu mkewe baada ya kuiangalia video.
"Oh ndio. Ila nimemwambia Mona kwamba baba hajaweza kuja kukuona ukiimba kwa sababu amebanwa na kazi. Na kwamba wewe ni baba bora" Mke akamjibu mumewe.
Mume akajihisi kusisimka mwili. Akaweka simu yake mezani. Akatafakari. Mkewe ambae mara kwa mara amekuwa akimtuhumu kuwa hawajibiki kama baba bora, leo amemsifia na kusema yeye ni baba bora??
"Asante sana mke wangu. Hayo maneno yamenipa faraja na kuniongezea nguvu". Mume akamjibu sms baada ya kuichukua mezani tena.
"Mona ana macho kama yako" mke akamjibu mumewe.
"Hahaa hahaa. Asante mama. Mona analips na nywele kama zako" Mume nae akamjibu.
"Kweli? Natamani niwe na nywele kama za Mona. Hata hivyo leo wakati naoga niliona unywele mweupe. Naanza kuota mvi sasa hivi" Mke akamtumia sms mumewe.
"Karibu kwenye ulimwengu wa mvi. Mimi nimeshaona mvi tatu mpaka saa hizi" mume nae akamjibu.
"Ukirudi kazini utaungana na mimi kuoga leo usiku? Then uniangalie huenda nina mvi nyingi tu huku nyuma ya kichwa..wink wink.." mke akatuma tena sms.
Mume akajawa na furaha. Hakumbuki ni lini yeye na mkewe kwa mara ya mwisho wame-chat kwa furaha hivi kwenye simu.
Wakawa wana-chat huku mume akifanya kazi. Mpaka muda wa kuondoka ulipofika.
Mume Akajipiga selfie akiwa katika ofisi yake mpya na akamtumia mkewe aione ofisi.
Hajawahi kufanya hivi. Kupiga picha sehemu alipo na kumtumia mkewe. Ila muda huu kutokana na sms nzuri za mkewe, amejikuta akifanya yale aloshindwa kufanya hapo kabla.
Akaendesha gari kuelekea nyumbani. Huku akitabasamu na kusikiliza muziki mzuri.
Mume akafika nyumbani. Akafungua mlango na kukuta watoto wake wawili wakifanya homework.
"Hello love" mke akamuita mumewe na kumbusu kwenye shavu.
Nini kinaendelea? Mke wake hajawahi kumsalimia kwa style hiyo ya kimahaba. Mara nyingi hata hua hamjali...hua wanasalimiana utafikiri masela wa Kigogo sambusa.
"Habari za kazi Mume wangu" mke akauliza.
"Nzuri tu love. Unaonekana mzuri" mume automatically akajikuta akisukumwa kueleza ukweli wa jinsi anavyomuona mkewe. Hajawahi kumsifia kwa kipindi kirefu sasa.
Mke na mume wakaangaliana kwa muda kidogo kwa macho ya kutamaniana. Mke akaelekea jikoni, alikuwa anapika.
Mume akaenda mezani kwa watoto wake. Mona akamsimulia baba yake kuhusu tuzo aliyoipata shuleni kwa kipaji cha kuimba na mwanae mdogo wa kiume Piere akamsimulia kuhusu kuwika katika kikosi cha soka cha shule yao na kuwa nyota wa mchezo (man of the match).
Mume akagundua watoto wake wanafuraha kubwa sana tofauti na siki zingine huko nyuma. Ni kama wamechukua mood ya mama yao leo.
"Babe, umekumbuka kununua chumvi niliyokwambia?" Mkewe akamuuliza mumewe huku akipika jikoni.
Mumewe alisahau. Hapa matatizo yataanza sasa. Siku zote mkewe hulalamika na kuropoka mbele ya watoto kama mumewe akisahau jambo aliloombwa na mkewe.
Mume akasimama na kuelekea jikoni.
"Samahani mama. Nilisahau kupitia supermarket" mume akaongea.
"Honey, usijali" mke akaongea kwa upole.
"Nimejisahau Mama Mona. I'm sorry" Mume akaomba samahani.
Mke akampapasa mkono na kumwambia, "Usijali nitajua nini cha kufanya"
"Kuna duka la Mangi kule chini, ngoja niende nikanunue pale" mume akaongea huku akielekea mlangoni.
"Hapana usijali" mke akamjibu mumewe.
Lakini kwa sababu ya jinsi mkewe anavyom-treat leo mume akataka kufanya lolote kwa ajili ya mkewe.
"Baba, tununulie na lollipops" Mona na Piere wakamueleza baba yao.
Baba akaondoka nyumbani. Akipiga mluzi huku akiwa na furaha.
Akarudi nyumbani na kukuta suprise.
Mkewe na wanawe wawili wakampa keki ndogo.
"Hongera baba" yalikuwa maneno ya Mona na Piere yakiwa yameandikwa kwenye kadi mbili walizompa baba yao.
"Hongera kwa kupandishwa cheo baba" yalikuwa maneno ya mkewe huku akimbusu kwenye shavu.
Mume akajihisi kupendwa na watu wa nyumbani mwake. Na akajivunia utendaji kazi wake.
Mke akamaliza kupika, then yeye na watoto wake wawili wakaandaa chakula mezani; kitu kingine ambacho si cha kawaida pale nyumbani kwao.
Chakula kikaandaliwa. Kwa pamoja wakala kwa furaha.
Ni muda wa watoto kulala.
"Ngoja tupige selfie ya familia" mume akatoa ombi.
Wakaja kwa pamoja, wakakumbatiana na kupiga selfie kadhaa huku wakiwa na furaha.
Mke akaomba wanawe waongoze sala. Watoto wakasali na kwenda kulala.
Mke akaanza kufuta meza. Mume akajikuta nae akisaidia. Akaenda hatua zaidi na kusaidia kuosha vyombo huku wakiongea kuhusu watoto wao na mambo mengine.
Mume akambusu mkewe katika lips.
"Nakupenda" mume akamwambia mkewe huku akiwa ameshika kiuno.
Mke akamtiza mumewe kwa macho ya mahaba. Ni muda mrefu toka mumewe amemueleza kwamba anampenda.
Nae akambusu kwenye lips za mumewe.
"Mke wangu, leo umenikimbusha mwanamke niliyemuoa. Umenikumbusha ile sababu ya kukuoa wewe na kuwaacha wengine. Umenionesha kwamba mke ndiye anaebeba furaha ya nyumba na familia kiujumla.
...Unapokuwa mwanga, nami natoa mwanga, nyumba yetu inamulikwa na mwanga. Umenikumbusha zile siku tulipikuwa tuna-date" Mume akamwambia hayo mkewe na kumbusu.
Mke akamtizama mumewe machoni, akaweka mikono yake kwenye mabega ya mumewe. Na akamueleza haya;
"Nimesoma katika kitabu kwamba mwanamke hata atakapoolewa, abaki kuwa yule yule wa kipindi alipokuwa kwenye uchumba au mahusiano. Natakiwa nikitunze na kujipenda na kuwapenda walio wangu.....
..kuna vitu ambavyo vilikuvutia mpaka ukaonelea niwe girlfriend wako na mwishoe kuwa mkeo. Qualities zangu ulizoziona namna navyoongea na wewe na jinsi ninavyokujali. Sikutakiwa nipoteze hizo qualities baada ya kunioa. Nimerudi mume wangu...nipokee tena.
"Na kama hivyo mke wangu, umenifanya nikupende tena...natamani nikutongoze upya" mume akamwambia mkewe.
Mke akamvuta mkono mumewe, wakaelekea chumbani na kumwambia, "Honey, tulikubaliana leo tunaoga wote"
Wakaingia bafuni...kilichofanyika humo mimi na wewe hakituhusu...ni cha wanandoa tu! Ila walitoka wakiwa na furaha tele na ndio mwanzo wa ndoa yao kuanza upya tena!
Busara yangu; "A successful marriage requires falling in love many times, always with the same person".
Share
MKE WANGU AMEBADILIKA. Akapokea sms kwenye simu yake. Sms kutoka kwa mkewe. Sms ilisomeka hivi; "Hi my love, niko katika mood ya maombi. Kuna jambo lolote unataka niliombee?" Mume akaisoma sms mara mbili mbili kwa mshangao. Mkewe hajamuita kwa jina la "my love" kwa kipindi kirefu sana. Na zaidi mkewe hajawahi kumuuliza jambo la kuombea. Ughafla huu ukamshangaza! Mume akaona amjibu tu hivyo hivyo..akamrudishia sms kwa kuandika; "Fanya maombi ya shukrani, mshukuru Mungu kwa ajili ya promotion niliyopata kazini". "Umepanda cheo? Lini?" Mkewe akamtumia sms ya kumuuliza. Mume akakukumbuka kuwa hakumwambia mkewe kwamba amepanda cheo. Kwa sababu mkewe ni jeuri huwa hawezi ku-appreciate jitihada zake na kazi ngumu anazofanya. Yeye hua ni kulalamika tu. Hivyo alivyopanda cheo aliona akimwambia mkewe ataishia kulalamika. "Ni mwezi, niko na ofisi mpya hivi sasa. Samahani, sikukwambia mapema". Mume akajibu. Dakika nne zikapita bila mkewe kumjibu sms ya mwisho. Mume akajua mkewe ameshakasirika kama kawaida yake. Simu yake ikaita. Mkewe alikuwa anapiga. Mume akaguna. Hiki ni kimbembe, anahofia drama za mkewe. "Hello" mume akapokea simu. "Hi my love" mke akaongea upande wa pili. "Mmh" Mume akaguna baada ya kuitwa 'my love'. Sio kawaida hii. Mke akaendelea kuongea kwenye simu.. "Samahani mume wangu, nilikua na-drive nimetoka shule kwa binti yetu Monalisa kwenye siku yao ya vipaji shuleni. Oh, tumebarikiwa na Mungu kuwa na huyu binti wa ajabu. Anakipaji kikubwa cha kuimba. Ameshinda tuzo shuleni. Shule imemtunuku nishani". Mke akamwambia mumewe kwenye simu kwa furaha. Mume akashikwa na mshangao. Hakutarajia mke ataongea na yeye kwa ustarabu na kwa furaha kiasi kile. "Ameshinda tuzo ya uimbaji? Oh my God. Hongera sana kwa binti yetu Mona." Mume nae akajibu kwa furaha. "Ndio ameshinda tuzo, amekuwa wa kwanza. Inabidi tuanze kumpeleka kwenye darasa la muziki pia. Natamani na wewe ungekuwepo. Ila usijali nimerekodi video alivyokua akiimba" Mke akaongea. Mume akawa bado amechangamyikiwa. Kwa kawaida mkewe angeanza kumlaumu kwa namna gani alivyo baba mbaya kwa vile hashiriki kwenye shughuri za shuleni kwa watoto wao wawili. Mfano siku za wazazi na siku za vipaji vya watoto shuleni. Ingawa mkewe anafahamu kabisa kazi zinambana na kazi ya mkewe kidogo inao unafuu hivyo mke anaweza kwenda. Mume angependa kweli kuhudhuria lakini kazi sio rafiki kwake. Licha ya hayo mkewe alikua akimlalamikia. "Anyway my love, nilikupigia simu kukupongeza kwa kupanda cheo. Ninajivunia sana kuwa na wewe. Najua uko busy na kazi, je naweza kuomba na wewe kwenye simu?" Mke akaongea. Mume akakohoa kidogo kwa mshangao. "Ndio, ndio tuombe tu haina shida" mume akaongea. Kwa mara ya kwanza kama wanandoa wakasali pamoja kupitia simu. Ilikuwa ni sala fupi lakini yenye faraja. "Amen" mke akamaliza. "Amen" mume nae akaitikia. "Ok my love. Nikuache uendelee na kazi. Tutaonana baadae nyumbani. Nakupenda eeh!". Akakata simu. Mume akaangalia kwenye screen ya simu yake. Akaona picha ya kwake, mkewe na watoto wao wawili. Picha ya muda kama mwaka mmoja hivi uliopita na akai-save kama wallpaper na screensaver. Akajikuta akitabasamu huku akiangalia screen. "Mambo mazuri" akawaza kichwani mwake. Akajikuta akiwa na mood nzuri na akafanya kazi vizuri zaidi. Akawa na furaha pamoja kujiamini fulani hivi baada ya kuongea na ile simu ya mkewe. Akawa akicheka na kufurahi zaidi na wafanyakazi wenzake pale ofisini. Akapokea sms kutoka WhatsApp. Alikuwa ni mkewe. Amemtumia ile video ya binti yake Mona akiimba shuleni kwenye siku ya vipaji. "Muangalie binti yetu. Awww..inafurahisha na inatia moyo" ilikuwa ni caption ya hiyo video aliyotuma. Mume akaidownload video na kuangalia binti yake akiimba kwenye stage. "Nimemiss vingi mke wangu" mume akamjibu mkewe baada ya kuiangalia video. "Oh ndio. Ila nimemwambia Mona kwamba baba hajaweza kuja kukuona ukiimba kwa sababu amebanwa na kazi. Na kwamba wewe ni baba bora" Mke akamjibu mumewe. Mume akajihisi kusisimka mwili. Akaweka simu yake mezani. Akatafakari. Mkewe ambae mara kwa mara amekuwa akimtuhumu kuwa hawajibiki kama baba bora, leo amemsifia na kusema yeye ni baba bora?? "Asante sana mke wangu. Hayo maneno yamenipa faraja na kuniongezea nguvu". Mume akamjibu sms baada ya kuichukua mezani tena. "Mona ana macho kama yako" mke akamjibu mumewe. "Hahaa hahaa. Asante mama. Mona analips na nywele kama zako" Mume nae akamjibu. "Kweli? Natamani niwe na nywele kama za Mona. Hata hivyo leo wakati naoga niliona unywele mweupe. Naanza kuota mvi sasa hivi" Mke akamtumia sms mumewe. "Karibu kwenye ulimwengu wa mvi. Mimi nimeshaona mvi tatu mpaka saa hizi" mume nae akamjibu. "Ukirudi kazini utaungana na mimi kuoga leo usiku? Then uniangalie huenda nina mvi nyingi tu huku nyuma ya kichwa..wink wink.." mke akatuma tena sms. Mume akajawa na furaha. Hakumbuki ni lini yeye na mkewe kwa mara ya mwisho wame-chat kwa furaha hivi kwenye simu. Wakawa wana-chat huku mume akifanya kazi. Mpaka muda wa kuondoka ulipofika. Mume Akajipiga selfie akiwa katika ofisi yake mpya na akamtumia mkewe aione ofisi. Hajawahi kufanya hivi. Kupiga picha sehemu alipo na kumtumia mkewe. Ila muda huu kutokana na sms nzuri za mkewe, amejikuta akifanya yale aloshindwa kufanya hapo kabla. Akaendesha gari kuelekea nyumbani. Huku akitabasamu na kusikiliza muziki mzuri. Mume akafika nyumbani. Akafungua mlango na kukuta watoto wake wawili wakifanya homework. "Hello love" mke akamuita mumewe na kumbusu kwenye shavu. Nini kinaendelea? Mke wake hajawahi kumsalimia kwa style hiyo ya kimahaba. Mara nyingi hata hua hamjali...hua wanasalimiana utafikiri masela wa Kigogo sambusa. "Habari za kazi Mume wangu" mke akauliza. "Nzuri tu love. Unaonekana mzuri" mume automatically akajikuta akisukumwa kueleza ukweli wa jinsi anavyomuona mkewe. Hajawahi kumsifia kwa kipindi kirefu sasa. Mke na mume wakaangaliana kwa muda kidogo kwa macho ya kutamaniana. Mke akaelekea jikoni, alikuwa anapika. Mume akaenda mezani kwa watoto wake. Mona akamsimulia baba yake kuhusu tuzo aliyoipata shuleni kwa kipaji cha kuimba na mwanae mdogo wa kiume Piere akamsimulia kuhusu kuwika katika kikosi cha soka cha shule yao na kuwa nyota wa mchezo (man of the match). Mume akagundua watoto wake wanafuraha kubwa sana tofauti na siki zingine huko nyuma. Ni kama wamechukua mood ya mama yao leo. "Babe, umekumbuka kununua chumvi niliyokwambia?" Mkewe akamuuliza mumewe huku akipika jikoni. Mumewe alisahau. Hapa matatizo yataanza sasa. Siku zote mkewe hulalamika na kuropoka mbele ya watoto kama mumewe akisahau jambo aliloombwa na mkewe. Mume akasimama na kuelekea jikoni. "Samahani mama. Nilisahau kupitia supermarket" mume akaongea. "Honey, usijali" mke akaongea kwa upole. "Nimejisahau Mama Mona. I'm sorry" Mume akaomba samahani. Mke akampapasa mkono na kumwambia, "Usijali nitajua nini cha kufanya" "Kuna duka la Mangi kule chini, ngoja niende nikanunue pale" mume akaongea huku akielekea mlangoni. "Hapana usijali" mke akamjibu mumewe. Lakini kwa sababu ya jinsi mkewe anavyom-treat leo mume akataka kufanya lolote kwa ajili ya mkewe. "Baba, tununulie na lollipops" Mona na Piere wakamueleza baba yao. Baba akaondoka nyumbani. Akipiga mluzi huku akiwa na furaha. Akarudi nyumbani na kukuta suprise. Mkewe na wanawe wawili wakampa keki ndogo. "Hongera baba" yalikuwa maneno ya Mona na Piere yakiwa yameandikwa kwenye kadi mbili walizompa baba yao. "Hongera kwa kupandishwa cheo baba" yalikuwa maneno ya mkewe huku akimbusu kwenye shavu. Mume akajihisi kupendwa na watu wa nyumbani mwake. Na akajivunia utendaji kazi wake. Mke akamaliza kupika, then yeye na watoto wake wawili wakaandaa chakula mezani; kitu kingine ambacho si cha kawaida pale nyumbani kwao. Chakula kikaandaliwa. Kwa pamoja wakala kwa furaha. Ni muda wa watoto kulala. "Ngoja tupige selfie ya familia" mume akatoa ombi. Wakaja kwa pamoja, wakakumbatiana na kupiga selfie kadhaa huku wakiwa na furaha. Mke akaomba wanawe waongoze sala. Watoto wakasali na kwenda kulala. Mke akaanza kufuta meza. Mume akajikuta nae akisaidia. Akaenda hatua zaidi na kusaidia kuosha vyombo huku wakiongea kuhusu watoto wao na mambo mengine. Mume akambusu mkewe katika lips. "Nakupenda" mume akamwambia mkewe huku akiwa ameshika kiuno. Mke akamtiza mumewe kwa macho ya mahaba. Ni muda mrefu toka mumewe amemueleza kwamba anampenda. Nae akambusu kwenye lips za mumewe. "Mke wangu, leo umenikimbusha mwanamke niliyemuoa. Umenikumbusha ile sababu ya kukuoa wewe na kuwaacha wengine. Umenionesha kwamba mke ndiye anaebeba furaha ya nyumba na familia kiujumla. ...Unapokuwa mwanga, nami natoa mwanga, nyumba yetu inamulikwa na mwanga. Umenikumbusha zile siku tulipikuwa tuna-date" Mume akamwambia hayo mkewe na kumbusu. Mke akamtizama mumewe machoni, akaweka mikono yake kwenye mabega ya mumewe. Na akamueleza haya; "Nimesoma katika kitabu kwamba mwanamke hata atakapoolewa, abaki kuwa yule yule wa kipindi alipokuwa kwenye uchumba au mahusiano. Natakiwa nikitunze na kujipenda na kuwapenda walio wangu..... ..kuna vitu ambavyo vilikuvutia mpaka ukaonelea niwe girlfriend wako na mwishoe kuwa mkeo. Qualities zangu ulizoziona namna navyoongea na wewe na jinsi ninavyokujali. Sikutakiwa nipoteze hizo qualities baada ya kunioa. Nimerudi mume wangu...nipokee tena. "Na kama hivyo mke wangu, umenifanya nikupende tena...natamani nikutongoze upya" mume akamwambia mkewe. Mke akamvuta mkono mumewe, wakaelekea chumbani na kumwambia, "Honey, tulikubaliana leo tunaoga wote" Wakaingia bafuni...kilichofanyika humo mimi na wewe hakituhusu...ni cha wanandoa tu! Ila walitoka wakiwa na furaha tele na ndio mwanzo wa ndoa yao kuanza upya tena! Busara yangu; "A successful marriage requires falling in love many times, always with the same person". Share
Artikel Terkait
HESABU YA KUONGEZA Niwapo hisabatini, Hufikiri akilini, Kuongeza umakini, Jawabu kulibaini. Jawabu hilo halani, Hukaa makinikoni, Linafaa maishani, Hapa hapa duniani. Ingawa jana nyumbani, Siku niliyobaini, Hata leo furahani, Nakuweka pongezini. Kijana huyu nyikani, Akiwa hisabatini, Kanuniye mkononi, Kaifikiri kichwani. Ndipo nilipobaini, Kafika hisabatini, Kasogea nyongezani, Hapa hapa duniani. Kafika hisabatini, Kashikilia kanuni, Kuingia umrini, Kakaa makinikoni. Hesabuye kabaini, Kamjalia Manani, Kaingia furahani, Yamfaa maishani. Nyongezaye umrini, Hapa hapa duniani, Ufurahi maishani, Singie ubazazini. Sivutwe hisabatini, Duara kulibaini, Ukaidai kanuni, Ukokotozi pupani. Sivutwe hisabatini, Maumbo kuyabaini, Kuchora karatasini, Ukafika ushenzini. Hari yako maishani, Tuliza kichwa nyumbani, Makinika ubwabwani, Ukishibishe tumboni. Busara zako kichwani, Ziongeze kwa makini, Ufike makinikoni, Utulie furahani. Nyongezayo umrini, Ikufae maishani, Hapa hapa duniani, Sichenge msikitini. Wasalamu tamkoni, Nalitoa mdomoni, Ukae mshawashani, Vilevile moralini. Sijiweke haramuni, Kulazimisha kanuni, Iliyo hisabatini, Ukae makinikoni. Na kwa kheri tamkoni, Naitoa mdomoni, Naenda zangu nyumbani, Nikae pumzikoni. UJUMBE Shamsa Cyprian ... Read More
NJIA RAHISI 13 ZA KUWA NA FURAHA KILA SIKU  Mabadiliko yalio mepesi kwenye tabia zako za kila siku yatakuweka kwenye mstari wa furaha unayoitaka Umejikuta uko kwenye siku tofauti, story hizo hizo, imekuwa ni kawaida yako? Basi muda huu , sio kesho , sio wiki ijayo, ni wakati wa kubadilisha historia yako. ni za haraka, rahisi na hazina gharama unapofanya hivyo na matokeo yatakupa furaha unayoitaka. 1.Pata masaa 7 mpaka 8 ya kulala usiku. Kulala usingizi wa kutosha unapata furaha, utaweza kuwa na nguvu ya kufanya kazi zako , na utakuwa na mahusiano mazuri. weka simu yako mbali unapoenda kulala, usitumie chakula kingi wakati wa jioni. 2.Amka mapema , dakika 30 kabla . Kama wewe ni mfanya kazi wa kuajiriwa na una tabia ya kuchelewa kazini, jaribu kuamka mapema dakika 15 au 30 kila siku kwa ajili ya kujiandaa vizuri na kukumbuka vitu vyote vya kufanya, kuchukua siku hio. utaona tofauti ya tabia yako. 3.Meditate. Hii ni kubwa. meditate kwa muda wa dakika 10 au 20, utapata faida nyingi zaidi ya furaha, pamoja na kuwa muwazi, kuwa na malengo ya siku nzima. Anza siku yako na meditation. utajiepusha na tress na wasiwasi na hutachanganyikiwa na kazi zako. 4.Jipe nafasi wengi wetu huwa tunajaza vitu nyumbani, ofisini hata vile ambavyo havina kazi, hatuvitumii. inaharibu mfumo mzima wa akili yako, hisia zako, na mwili wako. Ondoa vitu ambavyo huvitumii, tupa nje au gawia watu ambao wanahitaji kuwa navyo, hali yako ya furaha itaboreka. Na hutalemewa na kazi nyingi. 5.Jifunze kitu kipya Jitahidi kujifunza kitu kipya kila siku, kwa sababu hio ndio changamoto itakayokupa furaha, kujifunza kitu kipya inaboresha afya yako ya mwili na akili, kujifunza utajenga ujasiri pia na utakuwa sharp. 6.Tembea mara kwa mara Kutembea kwa dakika 30 kwa siku moyo wako utakuwa unafanya kazi vizuri, utapunguza hasira, hutakuwa na chuki. Kama unaona ni ngumu kwako kutembea , hasa kama una gari , jifunze kupaki gari yako mahali mbali na ofisi , tembea . anza kutumia maji ya kutosha. utapata faida nyingi . 7.Usijihusishe na mambo ya mitandao. Ni rahisi kuingia instagram, facebook na zingine, lakini wachunguzi wanasema kwamba ukizidisha kujihusisha na mitandao unaweza kuharibu afya yako ya akili. badala ya kutumia nusu saa kwenye mitandao, unaweza kufanya kitu kingine unachokipenda, au kusoma kitabu, kujifunza mafunzo mbalimbali kwa ajili ya kujiboresha mwenyewe kuwa mwenye afya. 8.Kuwa mwema. Ukarimu unakuongoza kwenye furaha yako mwenyewe na utakuwa mwenye afya bora. vitu ambavyo vinavyo chochea furaha ni kutoa , na kuwa mkweli , utapata faida , na utajisikia vizuri kuwa sehemu ya baraka kwa mtu fulani. kujitolea kufanya kitu, au kumwachia mtu kiti kwenye daladala. Sehemu ngumu? lakini nzuri. 9.Kaa na watu wenye furaha. Angalia watu unaoshinda nao, unaofanya nao kazi, ni watu wa aina gani. kwa sababu kuna msemo unasema kuwa ukikaa na ua rose utanukia hata kama ulikuwa hunukii. Fanya hivyo na utaweza kufungua mlango mpya kwa ajili yako maishani. utaiona furaha ikitiririka kama mto. 10.Don’t gossip. Kuseng’enya, umbeya, itakusababishia maradhi ya misongo na kukosa furaha. mtu mmbeya hawezi kusaidia kitu. wakati mwingine jitenge na watu kama hawa, au unapoona kuna kutoelewana na wafanya kazi wenzako, jaribu kutulia kwanza , badilisha negative to positive. Sema kitu kizuri kuhusu mtu. ni vizuri. kwa sababu utajiwekea alama nzuri kwako. 11.Tumia muda wako na watu unaowapenda Unapoongea na familia au marafiki kwenye simu , inatia moyo. mawasiliano hayo yanakupa afya na furaha.Fikiri ilivyo vizuri kama utaenda kula na rafiki yako mahali fulani, au kuamua kupika nyumbani , au kucheza na watoto wako kitu kama game, mpira, inafurahisha. 12.Journal Kuandika vitu vya kufanya kwa siku, au kuandika vitu unavyotaka kuvipata, Lengo hili dogo litaongeza IQ yako na kuleta utulivu wa kuboresha ujasiri wako, ukiwa na tabia hii kila siku , furaha haitakosekana kwako na utapata faida ya akili na hisia zako zitakuwa bora. 13.Jizoeze kujijali. Unapojijali ,Utaona faida zake, pamoja na kuondoa stress na wasiwasi, utakuwa mtu wa kuwaza mazuri na utaboresha immunity.pata muda kila siku kufanya kitu kwa ajili ya furaha, kama vile mazoezi, kupika chakula kizuri, kusoma . utaanza kushangaa jinsi ilivyo rahisi kuwa na furaha unapojijali na utaboresha akili yako na mwili wako, na roho yako. Kama unavyojua , kuna njia nyingi zinazotushambulia kwa siku, Ondoka mahali ambapo panaharibu ratiba yako. sasa, kama kitu kingine chochote,mafanikio ni kufanyia kazi. kwa hio pick one, and let the fun begin! ... Read More
NAOMBA MSIJE KWENYE SHEREHE YA MIAKA 10 YA NDOA YANGU, NJOONI KWENYE MSIBA WANGU. Baada ya kukaa kwenye ndoa takriban miaka 10 kasoro miezi miwili wakafanikiwa kupata watoto wawili wa kwanza angel na wa pili baraka. jamaa akakaa na mkewe wakapanga mipango mizito sana kuhusiana na tukio lingine zito baada ya tukio lao la harusi.yaani kusheherekea miaka 10 ya ndoa yao. Lakini akajisemea, ngoja nipime kiwango cha uaminifu alichonacho mke wangu kabla ya hiyo sherehe haiwezekani kwamba kuna usalama kabisa maana ktk miaka yote nimekuwa MTU wa kazini,safarini in short sina muda mwingi wa kukaa na familia yangu....na kama atavuka hili jaribu basi naweka nadhiri mbele za mbingu nitamtafutia zawadi nzuri ambayo hajawahi kuona na hatokuja kuisahau Akawaambia marafiki zake nataka nifanye party ya kusheherekea miaka kumi ya ndoa yangu nahitaji kampani yenu,walifurahi sana marafiki zake hususani wafanyakazi wenzake. Kamati zikaundwa mara moja,lakini baba angel aliendelea na upelelezi wa kumjaribu mkewe pasipo kujua huyo mkewe aitwaye Elizabeth. Mama angel aliendelea kualika marafiki zake,wazazi wake wakawa wanasubiria kwa hamu kubwa hilo tukio wakimbariki mwenyezi Mungu kwa kuendelea kustawisha ndoa ya mtoto wao.huku asijue mmewe ana nini ndani ya moyo wake. Baba angel akafanya usajili wa line mpya ya tigo asiyoijua mkewe. Akasajili kwa kubuni jina la #Asajile_mwasilu ambaye alikuwa anahisi anatembea na mkewe maana mara kadhaa alishazikuta msg za ajabu kwenye simu ya mkewe kama za mtu na mpenzi wake na alipoichunguza kwenye tigo pesa usajili ukaonyesha jina la Asajile mwasilu. akawa akichat na mkewe mara kwa Mara, kupitia hiyo namba mpya...... siku moja mkewe akaangalia hiyo namba kwenye usajili akaona jina la "Asajile mwasilu" waooooo ooh my dear,akafurahi basi mwenyewe! Akaamua kupiga simu,mumewe hakupokea akakata akamwambia nitext niko mahali hatutaweza kuelewana. Kumbuka Wakati huo mumewe yupo kazini........akamwambia tuendelee kuchat My nikupendae uko wapi mpenzi wangu nikufuate sasa hivi,maana nilivyofrahi kuona SMS yako mungu anajua!namba zako zote baba angel alifuta kwenye simu yangu,na wewe ndio hujanitafuta tena..... baba angel akajibu, we taratibu,si unajua umeolewa wewe unifuate wapi? mumeo alinipigiaga simu kwamba angenifanya kitu kibaya Sana iwapo ningeendelea kuwa na mawasiliano na wewe basi nikaogopa mwenyewe ndio maana nikajikaliaga kimya. Ooh pole my sweet, ndio walivyo wanaume wasiojitambua hawa,yaani yeye anadhani anaweza kunichunga eti! Anasahau kwamba uanaume sio kuchunga mke uanaume ni kumhudumia vzur mkeo kitandani huo ndio ulinzi tosha. Yaani kusema ule ukweli,sijawahi kupata mwanaume wa kunihudumia vile nitakavyo zaidi yako,uko wapii? Mama angel akaendelea kufunguka. Mh!baba angel akajikuta anaishiwa pozi vibaya mno huku mapigo ya moyo yanayoambatana na ghadhabu yakikitesa kifua chake ambacho hata pumzi ilikuwa ni shida kutoka hakuamini kwamba huyo anaechat naye ni mkewe.......akamjibu kwa kicheko cha uongo Hahaaaaaa ina maana unataka kusema jamaa hayuko vzur kitandani?? Na vipi angel hajambo??? Ndio maana nakuuliza uko wapi this time nikufate?maana umelandisha mtoto mpaka sio vizuri,wewe mwanaume una damu kali,wakati mwingine mpaka naona aibu kumwita mume wangu baba angel maana ukweli Mimi ndio naujua....ila yeye hajui kitu anajua ni wake. Baba angel akawazaa wee huku mipango ya sherehe akiona ikiyeyuka taratibu kadri alivyokuwa akiendelea kuchati na mkewe... Akakaa katibu dakika 10 bila kusema chochote akiwaza je ni kweli angel sio wangu???mh! Hawa wanawake vipii?? akatazama saa yake akaona ni saa 8 za mchana akajisemea pale ofsini "hivi mke wangu ana roho mbaya kiasi hiki Kumbe nalea mtoto asie wangu?? Akafungua kwenye gallery akatazama picha za mtoto wake huyo mzur akaendelea kujipa moyo......... Akamrudia mkewe akamwambia Wacha buana uko naye angel hapo?? Mama angel akajibu yes, jamaa akajibu tena "Mi mwenyewe nimekumiss sana na nimemmis sana mwanangu natamani nimwone tu lakini naangalia usawa wa mfuko hauko sawa sana...... Mkewe akajibu hebu ngoja nipe dakika sifuri......... Haraka haraka mama angel akampigia simu mumewe kwa namba yake ya siku zote. "Samahani baby unamkumbuka neema msimamizi wa send off yangu?? Jamaa kwa unyonge huku akijikaza kusikiliza uongo wa mkewe akajibu ndio namkumbuka amefanya nini? Nilikuwa nampa taarifa ya party yetu kumbe alipata ajar yuko nyumbani, sasa nimeona wacha nikamwangalie kabisa sasa hivi naomba hela kidogo..........jamaa akamtumia tsh. laki moja na nusu na msg juu akimhimiza kuwahi kurudi. Vipi uko na angel hapo?? Mama akajibu ndio nikupe uongee naye?? basi akampa simu wakaongea na baba yake...... Akachukua simu mama yake akamwambia mumewe " halafu naenda nae angel mara moja! Jamaa akajibu hamna shida. Upesi mama angel akamwandikia sms anaedhani ni Asajile mchepuko wake kumbe ni mumewe huyo huyo akamtext sasa enda mahali tafuta guest nzur nakutumia elfu 80 sasa hivi Jamaa akajibu waooo ndio maana sijawahi kuacha kukupenda Elizabeth wangu.....basi ntakwambia nikipata. Ila uje na angel Baada ya dakika kama 30 Elizabeth akawa amejiandaa na kumuandaa mwanaye huku akimuahidi house girl kana kwamba atarudi saa 2 usiku....... Jamaa mida kama ya saa 10 jioni akamtext wife njoo hapa...........kuna Lodge inaitwa shelisheli unaijua?wife akaitikia yes.....basi njoo ni chumba namba 6 ghorofa ya 6 ila usimwache mtoto pls. Muda wote huo baba angel alikuwa ameshika kitambaa mkononi maana haipiti sekunde asipojifuta machozi machoni alikuwa akilia tu kwa jinsi alivyokuwa akimpenda mkewe.akajifikiria kuwa ,kwanini Mungu alimficha hilo jambo lililo moyoni mwa mkewe??kwanini Mungu ameruhusu alee mtoto asiye wake?? Kufika hapo Ni kama mwendo wa dakika 20 kwa toyo,basi Mama angel akaona achukue hiyo bodaboda awahi na kweli akawa amewahi.......akaingia hiyo hotel akaenda sehemu ya lift akafika chumba gorofa ya 6 akaenda chumba namba 6 Taratibu akafungua mlango mgongoni akiwa na angel akakuta hakuna mtu kumbe jamaa kaingia kidogo uani Dakika mbili hivi jamaa akawa anatokea kutoka uani Ile kufungua mlango Mama angel hakuamini alichokikuta maana tayari kwenye ubongo wake alikuwa amemtengeneza Asajile.....lakini sio Asajile aliyemkuta........ aligongana USO kwa USO na mumewe wanaetarajia kufanya sherehe ya ndoa yao wiki kama mbili zijazo. Mama angel alipiga yowe yesuuuuu huku akitaka kukimbia kutoka nje........mumewe akamkamata mkono wake akamtuliza na kumwambia "usiogope uko kwenye mikono salama ya baba wa watoto wako kaa utulie! Ooh my god sijui nimefanya nini Mimi!?mkewe alijisemea huku akionyesha kuchanganyikiwa. Wakati huo angel yuko kwa baba yake akistaajabu kuhusu kinachoendelea......... Ilimchukua kama dakika 20 mpaka kutulia mama angel Mumewe akaongea maneno mafupi tu..... MKE WANGU, USIJE UKADHANI MIMI NIPO GIZANI KABISA NISIJUE HATA HATA KIDOGO ULICHONACHO MOYONI MWAKO. AKAONGEA KILUGHA KUMKWEPESHA MTOTO ASIELEWE......LAKINI AKIWA NA MAANA KWAMBA TANGU HUYU MTOTO AMEZALIWA,MOYONI MWANGU NILIJUA SIO MTOTO WANGU,HATA WIFI ZAKO, shemeji zako WAZAZI WANGU WALINIAMBIA HILI JAMBO,NA LISEMWALO LIPO.......mama angel akazidi kupigwa butwaa Akaendelea kumsimulia mkewe....... SIKU MOJA NILIOTA NDOTO MTOTO ANAUMWA,NA TULIPOENDA HOSPITALI ETI KATIKA VIPIMO IKAONYESHA WANAPIMA DNA NIKAKASIRIKA,MBONA MNAMPIMA DNA WAKATI HUYU NI MGONJWA ANAHITAJI VIPIMO VINGINE? YULE DR AKANIAMBIA NITULIE KWANI ANAJUA AFANYACHO NIIKAMKA,NILIPOMPIGIA SIMU MTUMISHI WA MUNGU MMOJA AKANIAMBIA MTOTO SI WANGU LAKINI NISICHUKUE UAMUZI WOWOTE MBAYA BADALA YAKE NIENDELEE KULEA MAANA MALIPO NI KWA MUNGU. Elizabeth, umenitonesha tena kidonda mke wangu, Asante umemleta angel kwa baba yake Asajile lakini hayupo,bado nabaki Mimi ndiye baba yake Mungu atanilipa kwa uaminifu wangu......nashkur kwa uongo wako,asante kwa hela uliyonitumia ya chumba, nataka nikwambie nimefanya kama ulivyonipa maelekezo....... Wakati huo mama angel analia tu hakuna mfano,anaona hata aibu kusema nisamehe,alichojibu ktk kulia kwake ni "Naona nafsi yangu inahukumiwa mno kuliko maneno unayoniambia.....najua mwisho wa ndoa yangu ni hapa hakuna jinsi,siwezi kujitetea mume wangu!naiona jehanamu hii hapa,ninauona ubaya wa kufuga dhambi sasa,hapa ndio naamini hakuna siri duniani,haiwezekani ukafanya kitu ukajua haitajulikana. Niko tayari uniambie chochote na sitapinga,nimeaibika mbeke ya mwanangu Mwanangu nimeaibika mbele ya mume wangu anipendaye na nimeaibika mbele za mbingu na dunia..........nitaficha wapi USO wangu mie?? Jamaa akamwambia mkewe najuta kukujaribu mke wangu najuta kuupima uaminifu wako,ila namshukuru Mungu amenipa kifua kikubwa cha kukabiliana na mambo MAZITO. Lakini wakati mwingine namshukuru Mungu tu maana kila jambo lina makusudi....... Wakatoka pale hotelini wakaingia ndani ya gari ambayo baba angel alikuja nayo wakarudi nyumbani. Usiku mzima mwanamke hakulala usingizi akidhani labda mumewe angemuua hata mtoto........asubuhi kulipokucha jamaa alipowahi kazini mwanamke akaanza kupitia message walizokuwa wanachat na mmewe akaona ni kama yupo uchi tu.......akaenda kununua vidonge duka la dawa baridi akameza akafa huku akiacha ujumbe usemao KUHUSU KUFA KWANGU ASILAUMIWE MTU YEYOTE ILA NILAUMIWE MIMI NAPENDA NIWEKE HADHARANI KILA KITU,KUHUSU MTOTO WANGU ANGEL SIO WA MUME WANGU,JAPO KWA KIPINDI CHOTE ALIKUWA ANAJUA NI WAKE.......BABA YAKE ANAITWA ASAJILE MWASILU......ALINIPA MIMBA NIKIWA NDANI YA NDOA YANGU....... NATUBU KWA WAZAZI WANGU NA WAZAZI WA MUME WANGU MNIOMBEE NIENDAKO NIPUNGUZIWE ADHABU YA KABURI,MWISHO NAWAOMBA MSIJE KWENYE SHEREHE YA MIAKA 10 YA NDOA YANGU,NJOONI MSIBANI. Mwisho sitaki kueleza nini kilitokea kwenye mazishi na msiba kwa ujumla wake Lakini jamaa anaendelea kulea mtoto asiye wake na mtoto wake. Kwenye mazishi alisikika akilia akisema najuta kwanini nilipima uaminifu na msimamo wa mke wangu,yamkini mpaka leo angekuwa hai............... BAADA YA MAZISHI MAKABURINI BABA ANGEL ALIMPELEKEA KARATASI KAKA YAKE AMBAYE NDIYO ANGETOA SHUKRANI KWA WATU NA MATANGAZO MACHACHE YA NINI KINGEENDELEA BAADA YA PALE,BASI AKASOMA ILE KARATASI KWAMBA "TUNAPENDA KUWATAARIFU KWAMBA ILE SHEREHE YA MIAKA 10 YA NDOA YA BABA ANGEL PAMOJA NA MKEWE AMBAYE NI MAREHEMU SASA ILE TAREHE IPO PALEPALE ATAFANYA NA WATOTO WAKE ITAAMBATANA NA KUMSHUKURU MUNGU KATIKA YOTE MAANA IMEANDIKWA "SHUKURUNI KWA KILA JAMBO"........... Siku ya sherehe yenyewe watu walifika kwa wingi sana hamna mfano na miongoni mwao ni baba angel original yaani Asajile....... Itaendelea next time Ila jueni kuwa shetani yuko kaz ... Read More
Wanawake: Mumeo akikukera usilale mpaka pakuche hamjasameheana  Usiku kama mumeo kakukera usilale mpaka pakuche hamjasameheana, hata malaika baraka hawawezi shuka kwenu. Huyo ulionae amezaliwa kwao kaja na tabia zake na wewe umezaliwa kwenu una tabia zako. Sasa ukitaka kila kitu kiwe wewe unavyotaka atakuwa mwanao tena huyo sio mumeo samehaneni kwa kila mnalofanyiana. Usiweke vinyongo tena ukajua unamkomoa mana unavyonuna ndo mchepuko unavopata chance ya kuwasiliana na si kila mwanaume anamchepuko wengine washkaji tu sasa ukijitia umenuna kisa umemuona kachat, sijui umekuta meseji sijui nini utakonda uzikwe na presha na unavyotiwa kaburini tu huku wenzio wanamtext pole kazi ya Mungu mpenzi. Gangamala mtoto wa kike sio kidogo kununa kama unga wa ngano ulokosa amira. Tabasamu njia nzuri na sahihi ya kumuua mtu akikosea ukatabasamu ataanza kutafuta mchawi kumbe mchawi mwenyewe, ataanza kutoka kujua kwanini hujakasirika atatulia tu akiamini anakuvizia kumbe anajivizia. ... Read More
UMESOMA HADITHI NYINGI ZA MAPENZI, LAKINI HII ITAKUSISIMUA KULIKO ZOTE, UTATUMIA DAKIKA 2 KUSOMA LAKINI...  1st year nikiwa nimekaa leacture room nikimuangalia msichana aliyekaribu yangu,niliyekuwa nikimuita "Bestfriend"nilikuwa nikimuangalia nywele zake nzuri na sura yake ya upole huku nikitamani awe wangu,lakini yeye hakuwa akitamani hilo na nilikuwa nikilitambua hilo. Baada ya leacture,alikuja kwangu na kuniomba notes za siku ya nyuma kwa sababu hakuweza kuingia darasani hiyo siku iliyopita.baada ya kumpa akasema "asante" na kushikana mikono na mimi.I wanted to tell her,i want her to know that i don't want us to be just friends,i love her but i'm just to shy,and i don't know why 2nd year Simu yangu iliita,kupokea alikuwa yeye alikuwa akilia akinielezea jinsi gani boyfriend wake broke her heart,she asked me to come over because she didn't want to be alone,kwa kuwa ni rafiki yangu kipenzi ilinibidi kwenda kumfariji,as i sat next to her on the sofa,nilikuwa nikimuangalia Machoni nikitamani awe wangu.Baada ya masaa mawili baada ya kuangalia nae movie mbili tatu na kula nae chakula pamoja akarudi katika hali yake ya kawaida,hivyo akaamua kwenda kulala,before akaniangalia na kuniambia "asante" na kunipa tabasamu tamu,i want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why. 3rd year Siku moja kabla ya Tamasha la muziki chuoni alikuja kwenye meza yangu leacture room na kuniambia "Boyfriend wangu amepata udhuru hivyo naomba unipe campan katika tamasha la muziki leo usiku" kwa kuwa tuliwekeana promice kwamba ikitokea kila mmoja wetu amekosa mtu wa ku-date nae basi tutaenda pamoja just as "bestfriends".hivyo tukaenda. katika tamasha baada ya kila kitu kuisha na muziki kufungwa,nilikuwa nimekaa nje ya ukumbi nikimuangalia jinsi alivyokuwa akicheka na rafiki zake,she saw me looking to her she smiled at me,i want her to be mine lakini yeye alikuwa hafikirii hilo kabisa na nilikuwa nikilitambua hilo,then she said to me "nimekuwa na muda mzuri na wewe asante sana" and she gave me a sweet smile.I want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why. Graduation Day siku,wiki kisha mwezi ukapita ilikuwa ni mahafali yetu tukimaliza masomo ya chuo,akiinuka kwenda kutunukiwa shahada yake ya uchumi nilikuwa nikimuangalia akiwa amependeza sana siku ile,i wanted her to be mine,but she didn't notice me like that,and i knew it. kabla watu hawajatawanyika kwenda makwao,alikuja kwangu akiwa na vazi lake la mahafali,na kulia pale nilipomkumbatia akainua kichwa chake na kuniambia "you are my bestfriend asante sana" i want to tell her to know that i don't us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why. Miaka michache baadae Nikiwa kanisani Yule Msichana akiwa anaolewa sasa,nilimuangalia akisema "ndiyo nakubali " and drive off to new life,kaolewa na mwanaume mwingine,i wanted her to be mine,but she didn't see me like that,and i knew it. but before she drove away,alikuja kwangu na kusema "asante sana" and kissed me on the cheek.I want to tell her to know that i dont us to be just friends,i love her but i'm just too shy,and i dont know why. Kwenye Mazishi Miaka ilipita i looked down katika jeneza lilokuwa na msichna ambaye alikuwa ni "bestfriend" wangu,Katika Service ya mazishi wakasoma diary ya Bestfriend ambayo alikuwa akiiandika enzi za maisha ya chuo' Diary yake ilikuwa Ilikuwa ikisomeka hivi I stare at him napenda awe wangu,but he doesn't notice me like that,and i know it,i want to tell him,i want him to know that i dont want us to be just friends,i love him but i'm just to shy,and i dont know why.I wish he would tell me he loved me! Nilipiga magoti huku nikilia nikijisemea moyoni i wish ningemwambia tu ukweli,nimeshachelewa sipo nae tena katangulia mbele za haki i cried!! Vunja ukimya ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: