❤❤❤❤❤❤❤ JE WEWE NI MIONGONI MWA WALE WANAWAKE AMBAO WAMEBEBA DHAMANA YA NDOA KULINDA MAHARI ULIYOLIPIWA? Ni kweli unalinda ndoa iliyojaa machungu na mateso mengi kisa ukitunza heshima ya mzazi wako ambaye alipokea mahari ya Mumeo na ukiitazama mahari hiyo huioni machoni pako nawe unakosa namna ya kujiokoa katika kifungo cha mahari? Mwanamke wewe sio kama mnyama ambaye ananunuliwa kwa manufaa fulani, Mahari ni HESHIMA kulinda tamaduni zetu katika kuileta maana ya NDOA... Ndoa yoyote ikibebwa kwa mahari ama mashuhuda wa ndoa mara nyingi hutawaliwa na UVUMILIVU wala sio UPENDO TENA! Thamani yako mwanamke hailinganishwi na MBEGE wala NG'OMBE ila thamani yako mwanamke ni moja tu WEWE NI PUMZIKO LA MUMEO na katika hilo hakuna mbadala wake na likitokea Basi ujue HAKUNA HAKIKA YA FURAHA ila Kuna uvumilivu kiasi mtu hukosa namna na kujikuta akikosa tumaini ila sio kwa kulitaja PENDO ila tuseme TAMAA... Usikubari woga ukakutawala hata ukashindwa kujitetea mbele za nafsi yako pamoja na hisia zako, Yaani usiruhusu kuolewa na mtu ambaye MOYONI MWAKE ANALINDWA NA MAHARI ALIYOKULIPIA! Kataa kuolewa na mtu ambaye siraha yake ni mahari, Yaani ubora wako pamoja na heshima yako kuumbwa mwanamke eti uolewe na Mwanaume ambaye AKILINI MWAKE ANAJIVUNIA KUKULIPIA MAHARI... Kumbuka MAHARI ni vitu na kwa vyovyote vile juhudi yaweza kuvileta hivyo lakini FURAHA HAITENGENEZWI KWA MAHARI bali mtu huitengeneza FURAHA YAKE ikiwa atampata mtu aijuaye thamani yake. ❤❤❤❤❤❤❤❤❤❤ Dr Luv🤓🤓🤓

at 9:39 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top