Home → ushauri
→ #AFYA: JE! WAJUA SABABU KUU ZA KUHARIBIKA KWA MIMBA?
Vyanzo vikubwa vinavyoweza kusababisha kuharibika kwa mimba
{miscarriage} ni
kama vifuatavyo;
.
1.Chromosome abnormalities,
>mimba nyingi ambazo huharibika hadi
wiki ya ishirini husababishwa na tatizo hili
la chromosomes, na chromosomes huwa
zinabeba genes ambazo huyatambulisha
maumbile ya mwanadamu kwa nje, yaani
jinsia yake, ngozi yake itakuaje, macho yake
na vitu vingine vingi nisingependa tuingie
ndani sana lakini matatizo haya ya
chromosomes huchangia sana kuharibika
kwa mimba.
.
2.Maambukizi katika mji wa uzazi wa
mwanamke {Infections},
>>kuna kitu kinaitwa Pelvic Inflammatory
Diseases {PID} yaani kuvimba kwa kuta za
mji wa mimba au kuvimba kwa mirija ya
uzazi nayo pia huchangia sana kuharibika
kwa
mimba kwa mwanamke, lakini pia Candida
au
fangasi nazo pia huchangia sana kuharibika
kwa mimba.
.
3.Chanzo kingine kikubwa ni utoaji wa
mimba za mara kwa mara, wanawake au
wasichana
wenye tabia ya kutoa mimba moja au mbili
au
tatu basi nao pia hukutwa na tatizo hili la
kuharibika kwa mimba kwani uingizaji wa
vyuma ndani huweza kuharibu shingo ya
kizazi ya mwanamke na pia kukumbwa na
tatizo hili la miscarriage au kuharibika kwa
mimba.
.
4.Chanzo kingine kikubwa ni magonjwa ya
zinaa {sexually transmitted diseases},
magonjwa kama gonorrhea, kaswende
mara nyingi sana huathili mfumo wa uzazi
wa mwanamke na hasa hasa kwenye mji
wa mimba na kuufanya kuwa legevu na
hata ujauzito unapotunga basi huweza
kutoka kwa haraka zaidi na hivyo
kusababisha tatizo hili la kutoka kwa mimba
{Miscarriage}.
.
5.Chanzo kingine cha mimba kuharibika ni
tatizo la kisukari kwa mwanamke, hii nayo
huchangia kwa kiasi kikubwa sana
kuharibika kwa mimba na mtu ambaye
hafanyi uangalizi wa karibu wa tatizo la
sukari basi husababisha glucose isitumike
kama energy na hivyo kuleta madhara katika
kizazi hasa ujauzito.
.
6.Kitu kingine ni hormones {homoni}
kuvurugika, kwa mfano hormone ya
progesterone mara nyingi hufanya ile kazi
ya kutunza mimba iendelee kukuwa, na
kama kunatokea unbalance au kuvurugika
kwa homoni hii basi mara nyingi tatizo hili
la mimba kuharibika hutokea.
.
DALILI ZA KUHARIBIKA KWA MIMBA
(Miscarriage)
1.Dalili kubwa kabisa ya kwanza ni damu
nyepesi kutoka kwa mwanamke mwenye
mimba.
.
2.Dalili kubwa ya pili ni mwanamke kutokwa
na damu yenye mabonge mabonge na
inakuwa nzito.
.
3.Dalili nyingine kubwa ni uchovu na
maumivu makal ya mgongo na kiuno.
.
4.Maumivu makali ya tumbo, wakati
mwanamke anapokuwa ni mjamzito lakini
wakati huo huo
anapatwa na maumivu makali ya tumbo ya
mara kwa mara yakiambatana na maumivu
ya
kiuno pamoja na kutokwa na damu nyepesi
au nzito basi ujue ujauzito wako uko
kwenye hatari
ya kutoka, ni vizuri ukawasiliana na kituo
cha karibu cha afya au ukawasiliana na
mtabibu
.
Kama unakumbwa na moja ya mambo kama
haya na usingependa kupatwa na tatizo hili
la kutokwa kwa mimba basi ni vema kama
ukawasiliana na wataalamu wa afya kwa
msaada zaidi
Ili kuwaokoa wanawake wengi ambao kwa namna moja au nyingine hawajui chochote kuhusiana na chanzo, dalili au namna ya kuepuka tatizo hili la kuharibika kwa mimba tafadhali hakikisha una SHARE post hii kadri uwezavyo elimu iwafikie wengi zaidi katika jamii
Nakutakia siku Njema, Mungu Akubariki na kukulinda
Usisahau ku LIKE
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: