Home → simulizi
→ ®HADITHI PICHA®
Mussabhai & YuYuShortstory
👙👙👙 DADA VUA👙👙👙
PICHA NO:_14
LIKE PAGE UWE WA KWANZA KUIPATA HII KILA SIKU.
https://www.facebook.com/YuYuTzHotStory
HAYA HAYAAA ZILE SIDIRIA AMBAZO KWA SASA NDO HABARI YA MUJINI TUNAZO
KAZI KWENU MASTISA DUU
UKIVAA MUGONGO WAZI KWA AJILI YA MTOKO NDO ZENYEWE HAZINA MIKANDA
NZURI KWA MABIBI HARUSI PIA
UKINUNUA LEO UTAUZIWA KWA BEI YA OFA
30000
WAHII KABLA OFA HAIJAISHA
TUPO DAR
MIKOANI TUNATUMA ILA BAADHI YA MIKOA TUNA MAWAKALA
mawasiliano
0711462866
0711462866 WhatsApp
TUNAUZA JUMLA PIA
Bonyeza link hapo chini kuangalia jinsi ya kuzivaa
👇👇👇👇
https://youtu.be/oWwe9rFZaxo
..........ilipoishia
Upande wa pili kule Sule aligomea kabisa kunywa kinywaji cha Helena.Sule alimwambia"Mbona unaning'ang'aniza sana kwanza sitaki hicho kinywaji hata wewe pia sikutaki tena"Sule aliongea kwa hasira kisha akawa anaondoka.Shangazi yake Helena alikuwa kwa mbali anatazama,Alivyoona sule amekataa alisema "Ahaaaaa!! unajifanya mjuaji eeeeh!! ngoja nikuonyeshe adabu" Aliongea huku akiingia ndani.........
Endelea.........Hakikisha unailike ili nilete vitu mubashara.
Shangazi alionekana amekasirika sana kitendo cha sule kukataa kunywa kile kinywaji.Aliingia ndani akiwa na jazba sana.Wakati huo Helena alibaki akimtazama sule anavyoondoka kwani kiukweli alimpenda sana ila siku zote kisicho riziki hakiliki.Lucy aliamua kumfuata Helena pale na kumuuliza "Hivi helena huyu kaka hujachukua hata namba yake??"......"Lucy nawe namba ya nini na hata nikiichukua inakuhusu nini sasa!!?"......" Heee!!Weee vipi kukuuliza imekua nongwa!!?".Helena na Lucy walianza kubishana pale mpaka ikawa kama ugomvi,Lakini kwa mbali walimuona shangazi yao anakuja kwa kasi sana.Helena na Lucy walianza kutazamana kwa hasira sana na hakuna anayemsemesha mwenzake kwani wakikutwa wanagombana itakuwa kesi nyingine kwa shangazi yao.Shangazi alifika pale kisha akuliza"Huyu kikaragosi yuko wapi??"Akimaanisha Sule.
Basi Sule aliondoka kabisa na nia yake ilikuwa ni kwenda huko ngare lakini sasa kutokana na tamaa alijikuta amekaa kwa kina Helena mpaka giza limeingia.Sule akiwa anatembea alisikia mlio wa pikipiki,Kwa kuwa alikuwa bado hajafika kwenye barabara kubwa inakopita hiyo pikipiki aliamua kukimbia ili awahi hiyo pikipiki.Ni kweli aliwahi kisha akaisimamisha"Samahani kaka unaelekea wapi unipe lift"......."Mi siendi mbali ni hapo tuu hata nikikubeba ni bure tuu maana mi nshafika"......."oukey basi naomba unisaidie simu yako nimpigie mtu nyumbani anifuate samahani lakini".Sule alipewa simu na kaingiza namba na kupiga alionekana anaongea na mama yake huku akimuelekeza pale alipo.Alimaliza kuongea kisha akamrudishia simu yule jamaa na yeye taratibu akawa anatembea kurudi nyumbani.
Wakati harakati za shangazi au bi kidako akihangaika namna ya kumteka sule ili amrudishe nyumbani kwao huku nyumbani kwa kina Sule watu walikuwa wamelewa sana,Walilewa wote kasoro mzee tuu kwani hakutaka kuuchosha mwili kwani anasafiri asubuh.Pamoja na watoto kumjali mama yao wa kambo wazo la mama lilikuwa pale pale,Alipanga kumpoteza mume wake ili aweze kumiliki mali zote kwani hati miliki zote kaachiwa yeye.Wakati huo mama alishawasiiana na Sule na hakumuambia yeyote kama amewasiliana na sule.Mama alienda pembeni kisha akampigia mtu na kumuelekeza kule aliko Sule na alimwambia asimlete nyumbani bali ampeleke MOUNT MERU HOTEL.
Huku kwa sule Kumbe hata ile pikipiki aliyoiona ilikuwa ni mauzauza tuu ilikuwa ni kazi ya bi kidako kuhakikisha sule anarudi kwao.Shangazi aliwafuata kina Helena kisha akawabadilisha wote kuwa wanyama na lengo lake ni kuwaamrisha kina Helena wamfuate Sule na kumtisha ili aogope huo msitu kabisa.Bi kidako tayari alishawabadili kina Lucy kuwa madubwasha ili yakaifanye kazi hiyo aliyoikusudia,Akili ya Bi kidako iliwazia ile Milioni 20 alizoahidiwa na mama yake sule alijisemesha kimoyo moyo"Ooooh! mizimu yangu asante sana,Hiyo kazi ni ndogo sana kesho namaliza kila kitu" Aliongea Bi kidako huku akiwaachia wanyama wake wamfuate Sule.Lucy na Helena waliachiwa wakaanza kutimua mbio kama vile wanashindana huku ndimi zao zikiwa nje.
Wakati huo huku watoto wa mzee Nassor waliitana ndani na kuanza kuongea kwa furaha"Yaani leo tumewafanyia wazee wetu bonge la suprise,Hebu cheki wanavyofurahia pale njee"Walikuwa wakiwatazama wanavyoshangilia kila mmoja anafurahi.Kumbe mama moyoni anamkejeli tuu mzee wa watu masikini wa mungu.Basi usilolijua ni giza nene,Basi baada ya hapo mama na mzee waliingia ndani kila mmoja akaendelea na shughuli yake.Mama cha kwanza alipiga simu Mount meru hotel na kumfanyia mwanae booking Ili akae pale kwa siku kadhaa wakati yeye anaweka mambo sawa ili amiliki kila kitu kutoka kwa mume wake.Baada ya hapo aliongea na dereva kujua amefika wapi.
Wakati huo Sule alikuwa anatembea huku hofu na mashaka vikiwa vimemtawala kwani giza lilikuwa limetanda na isitoshe ni porini.Wakati anaendelea na safari zake alihisi mchakacho kwa mbali kama vile kuna kitu kinakuja kwa kasi ,Aligeuka nyuma kuangalia ni nini kinakuja,Aliona wanyama kama chui wanakuja kwa kasi tena wawili,Sule alivuta pumzi akatupa begi lake kisha akaanza kutimka mbio........Unafikiri nini kitafuata hapo,Usikose sehem inayofuata hapo kesho
PATA SIMULIZI 4 TOFAUTI KWA SIKU UWAPO KATIKA GROUP LA KIJANJA KULE WHATSAPP.STORY ZOTE NI HOT NA UNAZIPATA MAPEMA YAANI ZIKIWA ZAMOTO KABISA KAZI KWAKO,JIUNGE NA WENZAKO KWA TSH 3000/-TUU ZA KITZ
Kwa wewe unayehitaji kuungwa group nicheki kupitia 0678641147 au 0688911112 whatsapp ni kuhusu simulizi tuu mambo mengine nicheki fb inbobo
KAMA HUJALIKE PAGE FANYA IVO SASA ILI UWEZE KUPATA VITU MUBASHARA.
#MussaBhai & #YuYuTz_ ®Newvission_2017
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: