CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA TATU (03) ILIPOISHIA SEHEMU YA PILI : kas0ro Niram peke yake ambae alisema, "wala sina mpango huo, ntampeleka wapii mimi, ila nimemsifiatu! sababu katika wavulana niliowai kuwaona, kwa hapa mtanzania, yule kaka ni handsome sanaa" alisema Niram huku anawaangalia marafiki zake, ambao wakakubaliana nae, kwakiikisa vicwavyao juu chini, na wakati huo kengele ya darasani ikagongwa, wakasimama tayari kwa kuanza safari ya kuingia darasani, ENDELEA....... Waliingia darasani, na vipindi vikaedelea kama kawaida. Niram alitafakari sana maneno ya rafiki zake,,akujua hata kwanini awazia lile jambo, maana hata sababu ya kuliwazia akuiona. "mmh mimi sasa ntakuwa nataka kurukwa na hakili haki ya Mungu" alijisemea kimoyo moyo Niram. Ila akaamua aachane na fikra zile, ambazo mwenyewe alizoziona za kipuuzi, na kuendelea na ratiba zake nyengine. ****** "hallo mmewangu nimekumisi mno utakuja lini?".ilikuwa sauti ya mama niram, aliye kuwa amepozi kwenye moja ya kochi zuri huku ameweka miguu juu ya meza. "ooh mkewangu kipenzi ratiba zinabana kazi zimekuwa nyingi mno hata mi nimekumisi kipenzi ila sina la kufanya mama".ilisikika sauti upande wa pili, ikiongea kwa masikitiko na mapenzi makubwa kwa mkewe. "ooh darling uwezi kuomba ruhusa ukaja hata kwa siku chache tu?".aliongea kwa kudeka mama niram huku akimpachika na swali mumewe huyo,aliyekuwa mbali na nchi ya Tanzania. "ooh sitawahi, unajua natakiwa kwenda india kuna Mahafali ya Razaki".ilisisitiza sauti ya baba niram. "ooh Mungu wangu nilisahau nasikitika sitoenda kwenye mahafali ya mwanangu".aliongea mama niram kwa unyonge ilionyesha hakuwa na furaha kuikosa hiyo sherehe ya mtoto wake wakiume. "usijali mke wangu, najua uwezi kuja sababu niramu hatokuwa na wakubaki nae wacha niende kukuwakilisha mimi sawa mamaa".aliongea kwakubembeleza baba niram huku akimfariji mkewe ili asijione mkosefu. "oky honey kazi njema nitafute baadae utapomaliza kazi".alisisitiza mama niram, "oky honey byeee ilove you"."love u too mume wangu byee". Waliagana mtu na mumewe, mama niramu akanyanyuka kuelekea jikoni,kuangalia kama msichana wake kama ameshamaliza kupika chakula cha mchana. ********* "eeeh ujue vincent ukumalizia story".alisikika suma akimuambia vicent, wakati huo walikuwa katika uwanja wa mpira, wakiangalia watu wanaofanya mazoezi, akiwemo Richard, yeye alikuwa akifanya mazoezi ya mpira wa kikapu, vicent na suma walikuwa wakimuangalia rafiki yao huyo, ambae alijua kuutumia uwanja vizuri aliku Hodari kweli kweli katika mchezo huo, "hahhhhah suma wewe mshkaji wangu mmbeya sana duuuh! yani kumbe ulisubiri tutoke tu!, yani wewe sikuwezi" aliongea vicent, vikafata vicheko vikaliii, suma alikuwa hana mbavuuu, ungewaona ungesema walikuwa wameona jambo la kuchekesha hapo walipo, "sasa mi nimesubiri we unihadithie naona kimya nikaona bora niseme yanini nife kiholo".aliongea suma huku anakalisha tako vizuri akimgeukua mlengwa. Basi vicent alimuadithia mwanzo mwisho, jinsi alivyokutana nae mpaka ilipofikia kusahau kumuomba namba. "hahahhhah hizo ndoto ndugu yangu yani ndo maana ukamzingua vanessa?".aliongea suma kwa mbwembwe, huku akumuona rafiki yake huyo kama anaota ndoto za mchana kweupe. "sikia suma vanessa mimi simpendi bora tu akate tamaa mapema kuliko nikaja kumuumiza zaidi huko mbele na kuhusu huyo dem ata asiponipenda baridi tu! ilimradi mi nimuekeze hisia zangu tu".aliongea vicent kwa msisitizo akimaanisha anachokisemaa. "aaah naona mnakula tu ubuyu". Aliingia Richard, katikati ya mazungumzo, mwili ukiwa umelowa jasho, aka kaa pembeni yao ilionyesha ashamaliza kufanya mazoezi ******* "mama simu inaita".aliita msichana wa kazi wakina Vincent, akimpelekea simu bosi wake ambae alikuwa amekaa nje kwenye bustani. "asante karunde kaendelee na kazi". Alisema mama yake vicent huku anaweka mkonga sikioni. "hallow magreth niambia rafiki yangu".aliongea mama vicent, aikusikika upande wapili,mara mama vicent akaongea na kuaga"aaah! Sawa basi usijali ntakuambia tarehe ikufika nikutakie siku njema".simu ikakatwa.******** "hahahhhh!! Yani na wewe huo ubuyu tule tumekuwa shilawadu?".aliongea vicent huku anacheka, mabega yote yakifanya kazi ya kunesanesa."yani we acha tu katuchukuliaje huyu sijui huyu bwege".alijibu suma huku akimpiga kofi la bega la kiutani utani. "aaah!bac kausheni vipi ile story ya asubuh nimalizie basi mwana".aliongea Richard huku anajiweka sawa kusikiliza. Vilifwata vicheko hatari. "kumbe na wewe shilawadu" aliongea suma baada ya kumaliza kucheka. Basi story zikaanza upyaa, visent akampa fully data. Richard Akuwa na la kuchangia zaidi ya kumtia moyo na kumwambia akaze buti. mara wakasikia ...... Itaendelea......CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA NNE (04) ILIPOISHIA SEHEMU YA TATU: "aaah! basi kausheni vipi ile story ya asubuh nimalizie basi mwana".aliongea Richard huku anajiweka sawa kusikiliza. Vilifwata vicheko hatari. "kumbe na wewe shilawadu" aliongea suma baada ya kumaliza kucheka. Basi story zikaanza upyaa, visent akampa fully data. Richard Akuwa na la kuchangia zaidi ya kumtia moyo na kumwambia akaze buti. mara wakasikia... endelea....... mara wakasikia, kama kuna vishindo vinakuja mahali walipo wao .ilibidi wakatishe story yao.nakuangalia mbele palipotokea,sauti ya viatu."mmmmh!!", alishusha pumnzi vicent baada ya kumuona mtu huyo aliyekuwa anakuja usawa waliokuwepo wao. Hakuwa mwengine bali ni vanessa, vanessa alizidi kuiongea taratibu kuja mahali pale, walipokuwepo wakina vicent.hatimae alifika."mambo zenu". Aliwasabahi huku akisubiri atajibiwa kwa hali gani salamu yake."nzuri vp vanessa"alijibu suma, mara kabla ajamaliza kuitikia suma, alidakia richard pia."tuambie shemela wa ukweli".kauli hii ili mchukiza, sana vicent alijikuta anamkata jicho moja kali rafiki yake huyo.ila vanessa alipotezea japo vicent,hakujibu salamu yake. "mi niko poa sana samahanini shemeji zangu nilikuwa naomba mnipishe kidogo nna mazungumzo na vicent".aliongea vanesa, huku akiwaangalia shemeji zake hao kwa zamu."ooh!!usijali mama suma eeh tuwapishe wapendanao".aliongea tena richard safari hii huku anatabasamu tabasamu la kichokozi,maana alijua ni jinsi gani anamkera rafiki yake." twenzetu mwanangu uwanja wenu jamani".aliongea suma huku ananyakua kibegi, chake kilicho kuwa pembeni yake, amesimama na kuanza kuondoka,wakati huo richard alikuwa ameshatanguli mbele." oyaa wanangu msifike mbali mnisubiri maana sitachukua mda mwingi hapa".aliongea vicent huku akiwa bize anatazama walipo kuwa wana tokomea wenzie. " poa".walijibu wote kwa pamojaa na kuendelea kutokomea mbele. "nakusikiliza unaweza kuongea" aliongea vicent bila kupepesa macho, akiwa mkavu kabisa." vincent kwani una nini mbona sikuelewi baba"aliongea vannesa huku anakaa pembeni ya vincent. Ila akupata jibu toka upande wapili."vincent si naongea na wewe au kuna kitu nimekukosea niambie ili nijue nikuombe radhi baba,nakupenda sitaki tukosane".aliongea vanesa kwa huzuni huku machozi yakiwa yanalengalenga kwenye macho yake. "sikia vanessa naomba usipoteza muda wako kwa ajili yangu focus katika masomo ujui kuwa tuna karibia mitihani ya kuhitimu kidato cha Sita ".alisema visent bila alama ya uoga,usoni kwake."najua baba lakini hiyo siyo sababu ya kufanya uwe serious ni kuelewana tu" alilalama vanessa huku akijisigeza karibu na vicent."oky basi ndo hivyo vanessa tuzingatie masomo now mapenzi yasimame kwanza".alimaliza vicent huku akijifuta vumbi, kwenye makalio tayari kwakuondoka. "vicent ntawezaje kukuchunia siwezi ntajitahidi nisome kwa bidii ila tusisitishe uhusiano wetu nakupenda sana". "vanessa tuelewane basi au nimefanya kosa kukusikiliza hapa?". Aliuliza vicent,pasipo kusubiri jibu akaanza,kuondoka.ila vanessa alimdaka mkono,na kumvuta asiondoke.daaaaah!! Lilikuwa kosa kubwa maana alisukumwa,akadondoka kama mzigo wa kuni pwaaaaaaah!!.aisee!! Vanessa aliumia akaanza kulia, maana alijiona kama mtu asiekuwa na thamani tena, aliumia kupita kiasi. Kitendo kile, kilimfanya vicent aingiwe na huruma, akaghairisha alipokuwa anakwenda, maana alijiona ana hatia sana. "nyanyuka mpenzi sikuzamilia kufanya hivyo nisamehe mama ". Alisema vicent huku akiinama, kumnyanyua vanessa na kwa bahati nzuri, hakuna alieliona tukio lile. "pole mama nisamehe sana". Alisisitiza vicent akionyeshwa kuchukizwa, na tukio alilolifanya." usijali vicent najua aikuwa kusudio lako kuna vitu haviko sawa kwako". Alijibu vanessa huku anajifuta vumbi, akisaidiwa na vicent. Baada ya hapo vicent alimchukua na kumkalisha chini. " vanessa siyo kama sikupendi laah hasha!! Nakupenda ila nielewe unatakiwa tusome kwanza tukimaliza mitihani tutaendelea, nafanya haya kwaajili yetu mama".aliongea vicent,siyo kama alimaanisha ila aliona si busara, kumuhukumu mtu kisa kampenda ni dhambi kubwa sana. " sawa ila niahidi tutakuwa tuna ongea hata mara moja moja, kwani bila kusikia sauti yako au kukuona sitaweza kusoma". Aliongea kwa kudeka, huku akijiegemeza kwa vicent. " sawa mama itakuwa hivyo ila naona muda unatutupa mkono, sitaki kuwachosha wenzangu wananisubiri". Alisema vicent huku akisimama tayari kwa kuondoka. "oky bby tutawasiliana ukifika".alisema Vanessa huku akiachia, busu matata shavuni mwa vicent. Basi waliagana na vicent akawafata washkaji zake, safari ikaanza..****** Nyumbani kwa kina niramu, palipoa alifika moja kwa moja mpk nyumbani kwao, akamsalimia dada wa kazi " da anna mamy yuko wapi?" aliuliza huku ana jibwaga juu ya kochi, begi akilitupia juu ya meza kubwa ya kioo, " ametoka kaniaga anaenda supermarket kununua bidhaa zimepungua".alijibu anna msichana wao wa kazi.niramu akajizoazoa kivivu, akaliokota begi lake, akaelekea chumbani kwake. Anna aliondoka kuendelea na shughuli zake.******* Vanessa alifika kwao, alikuwa amechoka, alifika akamkuta baba yake, ametulia kwenye kochi,akisoma gazeti. Nyumba yao ilikuwa, kubwa kiasi yenye uzuri wa kawaida.baba yake alikuwa daktari hospitali ya muhimbili, mama yake alikuwa mwalimu wa shule ya msingi.walizaliwa watano yeye ni watatu kati ya wanaume wawili, na wasichana watatu, wakwanza ni kaka yao.alipita akamsalimia baba yake, na kupitiliza chumbani. Hakika alijikuta anawaza sana matukio, yaliyomtokea shule. " mmh!! Au vicent amepata msichana mwengine?". Alijiuliza."kama ni kweli sitakubalii kwanza sina imani hiyo, labda atakuwa na jambo lingine, ila shule ile nzima, hakuna anaenikamata kwa uzuri".alijiwazia mwenyewe,akijiuliza na kujipa majibu mwenyewe. Ila gafla aka...... Itaendelea SEHEMU YA TANO (05) ILIPOISHIA SEHEMU YA NNE: wakwanza ni kaka yao.alipita akamsalimia baba yake, na kupitiliza chumbani. Hakika alijikuta anawaza sana matukio, yaliyomtokea shule. " mmh!! Au vicent amepata msichana mwengine?". Alijiuliza."kama ni kweli sitakubalii kwanza sina imani hiyo, labda atakuwa na jambo lingine, ila shule ile nzima, hakuna anaenikamata kwa uzuri".alijiwazia mwenyewe,akijiuliza na kujipa majibu mwenyewe. Ila gafla aka...... ENDELEA. Ila gafla akakumbuka kitu. "mmh si alisema kuwa, tunawasiliana kama kawaida ngoja tuone kama itakuwa hivyo kweli". Alijisemea peke yake, vanessa huku akijiuliza, na kujipa majibu mwenyewe.kiufupi mapenzi yalisha mchanganya, hakujua afanye nini, kumueka vicent kwenye mstari. Aliwaza sana, mpka akapitiwa na usingizi,akasahau hadi kwenda kula chakula.. ****** Niram akiwa bado yupo chumbani, alikuwa ana mfikiria sana vicent, mpka akawa anajiuliza,ni kwa nini amfikirie kama vile. " mmh mbona sasa nawaza upuuzi, kipi ambacho kinanifanya nikumbuke lile tukio la asubuhi".ila gafla kuma kitu akakumbuka, kikamfanya aangue kicheko siyo cha nchi hii. "hahhhhhhahhh!! hhhah!! uwiiii mama weeeeh hhh!!". Alicheka niram kama kichaa. " hivi sasa kilichokuwa kimemgandisha mpka asiondoe gari ni nini?".alijiuliza kisha akaendelea. "maana mtu aliduwaa kama kaona ela alafu yupo pekee yake anavizia jinsi ya kuikwapua hahhhah!!".alijisemesha mwenyewe kisha akacheka tena kwanguvu. Mala mlango ukafunguliwa, Akaingia mama yake ,inaelekea ndo kwanza alikuwa anafika,maana kipochi kilikuwa kwapani. " Eeeeh!! Mwenzetu vipi unaumwa ukichaa, mbona unacheka peke yakoo?".aliuliza mama yake,huku akiwa amesimama mlangoni, kwenye chumba cha binti yake.Niram alishtuka, maana hakutegemea uwepo wa mama yake eneo lile. Ila aliuficha mshtuko wake. "Eeeeeh!! Mama bwana kuna mwalimu wetu alianguka, wakati anaingia darasani, basi nikikumbuka nachekaaa".alivunga niram huku akijifanya kuwa makini na anachokingea. "wewe mtoto shetani si bure mwalimu kaanguka ndo unacheka hivyoo haaahhhhah hatarii, haya vua hizo nguo ukale, maana nakujua wewe hapo ulipo ujala ". Aliongea mama niramu, huku anapiga hatua kwenda nje. "sawa mama naja". Alijibu niram, mara ukasikika mlango paaaaah!, alikuwa mama niramu anafunga mlango . "uhhhhhhhhuh!!"alishusha punzi ndefu niramu, maana akutegemea kama angeweza kudanganya, haraka hivyo. Alibadili nguo nakutoka kwenda kuchukua chakula.. ******* Vicent alikuwa chumbani kwake, akichezea laptop yake.huku ana kula lakini mawazo mengi, yalikuwa kwa niramu. Alijiuliza kwanini ametumbukia juu ya mapenzi ya msichana, wakihindi hakika chakula hakikulika ,alikuwa na mawazo ya hatari yaliyo mfanya, chakula aone kichungu. " ntajitahidi kumtafuta naimani ntampata tu".alijiwazia kimoyomoyo, asijue aanzie wapi, amalizie wapi.ila gafla akiwa kwenye dimbwi la mawazo, alisikia simu yake inaitaaa. Ngrrrrrrrri ngrirrrrrrr!! "nani tena huyoo?". Alijiuliza huku akijiinua kuifata ,kwenye kochi maana yeye alikuwa kitandani. " daaaah!! Anataka nini tena huyuuu aaah!!".alilalamika vicent huku anaipokea simu. "hellow vanessa". Aliongea " yes bby nimekumic nikaona nikupigie". Ilisikika simu upande wa pili alikuwa vaness. " Oooh!! Kumbe niambie". "vicent nilikuwa na kukumbusha lile ombi langu nililokuomba". " lipi hilo?".alihoji vicent huku akimsikiliza kwa makini. "ni lini utanipa penzi lako?, nashindwa kujizuia vicent". Alilalama vanessa huku akisubiria, jibu upande wa pili. "Vanessa hivi kumbe jini wako apendi amani eeh!!?".aliuliza vicent, na kabla ajajibiwa akaongeza neno. " hivi leo nilitoka kukuambia nini hivi upo serious kweli wewe?, naomba usinitibue kama unawaza ngono badala ya kusoma ni wewe mimi naomba unikaushie kabisa".aliongea kwa jazba vicent, huku mikunjo kwenye paji la uso,likionyesha ni jinsi gani amechukia. "ooh nisamehe bby, mi nilikueleza tu hisia zangu wala sitaki tugombane".alijitetea vannesa maana alijua ashaharibu. " oky nikutakie jioni njema kesho mungu akipenda" aliongea vicent, na bila kusubiri jibu simu ikakatwa. Kiukweli vanessa, alijilaumu kwanini aliongea vile, aliilaani ile siku kwani aliiona siku mbaya kuliko zote. Baada ya kukata simu, vicent alikirudia kitanda na kujibwaga bado kidogo angemwaga chakula, kwenye kitanda. " Oooohsh!! Yote sababu ya huyu mwanamkee aaah!!". Alilalama vicent, huku lawama zote akimtupia vanessa. Eti wadau ukipenda sana unaonekana msumbufuu eeeh?.. Tuendeleee.. Basi vicent akachukua kile chakula na kukiweka chini akaendelea na ratiba zake . ******** Ilikuwa muda wa saa mbili kamili usiku(02.00) vanessa alikuwa yupo selbeni na mdogo wake wa mwisho wa kike, aliitwa juliana.kifupi unaweza mwita juli, walikuwa wanaangalia tv.wengine wakiwa na mishemishe zao, huku wazazi wao wakiwa wameshaingia chumbani,maana hata muda wa kuangalia taharifa ya habari aukuwepo, kutwa watoto wanaangalia movie zao. Ndio maana mzee wao anaamua ajununulie gazeti.. Muda wote wapo sebleni ila vanessa alikuwa kimya, kama anawaza jambo. Ila juli aliiona hali tofauti aliyokuwa nayo dada yake .. "vipi dada unaumwa mbona ueleweki leo?". Swali la juli lilimshtua vanessa ,kwenye dimbwi la mawazo akawa hana jibu sahihi la kumpa akabaki, kumbabaisha tu " hamna juli mdogo wangu nawaza mitihani sijui itakuwa migumu?".alivunga vanessa na kujifanya kuuliza ili kupoteza mada. " mmmh!! Dada usiwaze mbona nakuaminia itakuwa ya kawaida muhimu usome ". Alimjibu juli, vanessa akatingisha kichwa kukubali. Ila hakukaa sana akamuaga nduguye akaingia ndani kwake. ********* Siku ya pili, vicent alitoka mapema nyumbani, aliwahi shule kabla hata ya rafiki zake. Hii yote ni kutokana hata usingizi haukupatikana,kutokana na mawazo aliyo nayo. Alikuta baadhi ya wanafunzi wapo darasani, Alifika akakaa kwenye kiti na kufungua begi,kuchukua kitabu na kuanza kusoma. Ila hata sijui nini kilimtuma kutazama mbele maaana alijikuta anatoa macho......itaendelea

at 5:13 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top