SIMULIZI: JINA LA URITHI SEHEMU YA PILI (02) ⚪⚪⚪ILIPOISHIA⚪⚪⚪ ni sauti ya mwanaume mzee kati ya watu hao wawili waliojitokeza kimiujiza,,kisha akaisogelea maiti hiyo akachomoa kisu na kukata kipande cha nyama katika mwili wa maiti hiyo. Njile akatamani kutimua mbio,,lakini alishindwa kwa sababu mwili wake haukuwa na nguvu hata za kumuwezesha kutembea,,akastaajabu kumuona mzee huyo,,akimfuata,,na kumnyang'anya mtoto kwa nguvu! punde si punde yule bibi akazioiga hatua kumsogelea mzee huyo aliyekuwa kamshikilia mtoto mchanga,,Njile alipowatazama kwa makini wazee hao akashtuka kuona ni baba na mama wa mumewe,,kilichomshangaza zaidi wazee hao walikufa na wakazikwa miaka mingi iliyopita....wakati anatafakari nini cha kufanya mara ghafla!!!! TAHARUKI!!!!!! ⚪⚪⚪ENDELEA⚪⚪⚪ Mzee huyo akachukua kile kipande cha nyama ya maiti ya baba wa mtoto huyo mchanga,,pamoja akamlambisha mtoto huyo,,kisha akamsogelea Njile kwa hatua za taratibu,,lakini hakuonekana kama anatembea,,miguu yake ilikuwa haikanyagi kwenye ardhi! mzee huyo naye akasema,,"mtoto huyu aitwe LAULA. Njile akaingiwa na hofu lakini akajikuta anakuwa jasiri,,na kumpokea mtoto wake mchanga! alipomgusa mtoto huyo,,akahisi anaishiwa nguvu,,mwili wake ukawa regevu maradufu! akaona giza totoro limetanda mbele ya macho yake akapoteza fahamu,,,hakujua kilichoendelea.... Baada ya masaa kadhaa kupita,,akajikuta yumo ndani ya nyumba ya mwanamke ambaye alikuwa anaishi jirani na nyumba ya Njile,,mwanamke huyo alimpa msaada baada ya kumkuta Njile akiwa kalala kando ya barabara ndogo,huku mtoto mchanga akiwa juu ya kifuachake,,alimuonea huruma,,akamshawishi mumewe wampe msaada mwanamke huyo,,ndipo wakashirikiana kumbeba na kumpakiza kwenye kiti cha baiskeli,,wakaondoka nae mpaka nyumbani kwao, Njile akauliza kwa mshangao! ,,"hapa ni wapi,,na nimefikaje hapa? mwanamke aliyempa msaada akasema,,"mimi na mume wangu tulikukuta ukiwa umelala kando ya barabara, na ulikuwa umemkumbatia mtoto wako kifuani..mwanamke huyo aliongea maneno hayo huku akimuonyesha mtoto...Njile akachukua mwanae na kuanza kumtazama kwa macho ya huruma,,akajikuta anatokwa na machozi! akainua uso wake kumtazama mwanamke huyo,,kisha kafuta machozi na kusema,,"asante kwa kuokoa uhai wa mimi na mwanangu,,Mungu akubariki! pumde si punde Njile akahisi maumivu makali sehemu zake za siri...kumbe wakati anamsukuma mtoto atoke tumboni alichanika sehemu zake za siri,,sasahivi kapata ufahamu na maumivu anayasikia! ye msamalia akauliza ,,"ilikuwaje mpaka ukajifungua katika mazingira hayo!? Njile akasita kuongea kwa sekekunde kadhaa kisha akasema,,"ndugu we acha tu, ni stori ndefu,,ambayo hata mimi sielewi imekuaje! kifupi ni kwamba uchungu uliponishika nilihangaika sana,,,nilijitahidi kutoka nje ya nyumba,,angalau nipate msaada lakini,,Mungu si Athumani,wala Mabula,,wakati natoka nje ya nyumba,,ndio wakati ambao mume wangu alikuwa anarudi nyumbani...baada ya kuongea maneno hayo,,Njile akasita kuendea kusimulia...akajikuta anatokwa na machozi... ye msamalia akaingiwa na wasiwasi,,akihisi huenda mume wa Nje alimoiga mkewe n akumtelekeza huko....hivyo msamalia huyo akawa na shauku ya kutaka kujua mume wa Njile yuko wapi? na ni sababu zipi zilizomfanya amtelekeze mkewe katika hali ile! Njile akafuta machozi kisha akasema,,"mume wangu amekufa.. msamalia akashtuka! akauliza kwa mshangao,,kafa?? Njile akaitikia ,,"ndio kauwawa! Msamalia huyo akazidi kustaajabu! akajisemea moyoni ,,"mara kafa mara kauwawa! bila shaka mwanamke huyu atakuwa kaathiriwa na mazingira yale aliyojifungulia,,lakini naimani akili zake zitakaa sawa,, na ufahamu wake utarejea...lakini cha kushangaza Njile alionekana kuendelea kulia mfululizo tena kwa uchungu wa hali ya juu! kitendo hicho kilimfanya msamalia huyo,,ahisi kunajambo ambalo halipo sawa! na linamtatiza Njile. akauliza kwa sauti ya unyenyekevu,,"niambie umeoatwa na nini? naomba usinifiche jambo hata moja,,ili nijue namna ya kukusaidia. aliongea maneno hayo huku akimfuta Njile machozi yaliyokuwa yametapakaa kwenye mashavu. Njile akaendelea kusimulia,,"wakati tupo njiani kuelekea hospitali...uchungu ulinizidia,,na chupa ya uzazi ilikuwa tayari imeshapasuka,nikamwambia mumewangu anilaze chini nijifungue,,kwa sababu niliamini hatutofika mbali,,kutokana na hali yangu ilivyokuwa,,wakati na najifungua,,,nikashangaa mume wangu anahangaika,,kuvuta pumzi,,huku akiwa kashikilia sehemu ya shingo yake,,mwanzo nilihisi ni utani,,lakini kadri sekunde zilivyozidi kusonga akadondoka chini na kutulia tuli.. ghafla wakajitokeza wazee wawili,,ambao ni baba na mama yake..lakini wazee hao walishakufa miaka mingi iliyopita! wakati Njile anaendelea kusimulia,,ghafla yule mzee akajitokeza ndani ya nyumba ya msamalia huyo! Nje aliweza kumuona mzee huyo,,akasita kuendea kusimulia,,macho yakamtoka na hofu ikazidi kuongezeka,, Ye msamalia akastaajabu,,kumuona Njile amebaki kimya huku macho yake yakitazama uoande mwingine kwa muda mrefu...akaamua kugeuza shingo yake naye aone Nje anatazama kitu gani kilichomfanya akodoe macho. alipogeuza shingo yake,ghafla mlango ukafunguliwa kwa pupa!!! KIZAA ZAA!!!!! ↔↔↔↔↔ITAENDEA↔↔↔↔↔ Usikose kufatilia SIMULIZI hii ya kusisimua yenye maajabu ya kutisha,,iliyojaa mafunzo katika jamii zinazotuzunguka. Ungana nami katika sehemu ya 3. wingi wa Like zenu ndizo zitafanya nilete muendelezo kwa wakati. SIMULIZI: JINA LA URITHI SEHEMU YA TATU(03) ⚪⚪⚪ILIPOISHIA⚪⚪⚪ mwanzo nilihisi ni utani,,lakini kadri sekunde zilivyozidi kusonga akadondoka chini na kutulia tuli.. ghafla wakajitokeza wazee wawili,,ambao ni baba na mama yake..lakini wazee hao walishakufa miaka mingi iliyopita! wakati Njile anaendelea kusimulia,,ghafla yule mzee akajitokeza ndani ya nyumba ya msamalia huyo! Nje aliweza kumuona mzee huyo,,akasita kuendea kusimulia,,macho yakamtoka na hofu ikazidi kuongezeka,, Ye msamalia akastaajabu,,kumuona Njile amebaki kimya huku macho yake yakitazama uoande mwingine kwa muda mrefu...akaamua kugeuza shingo yake naye aone Njile anatazama kitu gani kilichomfanya akodoe macho. alipogeuza shingo yake,ghafla mlango ukafunguliwa kwa pupa!!! KIZAA ZAA!!!!! ⚪⚪⚪ENDELEA⚪⚪⚪ akashtuka,,,akashika kifua chake upande wa moyo,,huku akipumua kwa haraka,,,kumbe Njile alikuwa katika dimbwi zito la mawazo,,,akikumbuka matukio yaliyotokea miaka sita iliyopita, na aliyefungua mlango si mwingine,,ni yule mtoto wake,,kwa sasa anamiaka sita...hizo ni kumbukumbu zilizomjia katika mawazo, Njile akauliza kwa mashangao! ,,"kulikoni mbona umefungua mlango kwa pupa? mtoto Laula akajibu,,"nimeona limtu linaniita, linatisha! Njile akashtuka akaanza kudadisi kwa kumuuliza maswali mtoto wake,,"anafananaje? Laula akajibu,,"ni mzee nilishawahi kumuona,, Njile akamtazama mwanae kwa macho ya umakini huku akisikiliza kile anachokiongea Laula. Njile akahisi kuchanganyikiwa,,akasema,,"mwanzo ulimuona wapi? kama ilivyokawaida ya watoto,,huwa wanaeleza jambo kama jinsi alivyoliona,,hapunguzi neno wala haongezi neno,,Laula akasema,,"kunasiku alikuja nyumbani usiku,,nikakuamsha lakini haukuamka,,akqsema eti ni babu yangu..akanichukua na kunipeleka hukooo!!!! Njile akashtuka! akajisemea moyoni,,"bila shaka yale mambo yameanza upya! lakini kwanini mimi tu? alijisemea maneno hayo kwa uchungu...kisha akamkumbatia mwanae,,ghafla Laula akauliza,,"baba atakuja lini? mbona harudi? Njile akajikuta anaangua kilio! kwa sababu alimdanganya mwanae kuwa baba yake amesafiri...alishindwa kumwambia ukweli wa mambo yaliyotokea miaka sita iliyopita hivyo miaka hiyo yote Laula anajua kuwa baba yake kasafiri,,huwa anamuuliza mama yake mara kwa mara kuhusu baba yake! lakini Njile aling'ang'ania msimamo wake kuwa baba yake Laula kasafiri. ****BAADA YA MIAKA MINNE KUPITA***** Laula alitimiza umri wa miaka kumi(10) siku zilisonga na maisha yakaendelea,,lakini katika kijiji hicho kukawa na uvumi kuwa Laula ananguvu za kimiujiza,,watoto wa lika lake walishuhudia maajabu mbalimbali wakati wakiwa wanacheza na Laula....lakini hakuna aliyeamini maneno ya watoto hao! kadri miezi ilivyozidi kusonga Laula akawa tishio kwa watoto wenzake! hata shuleni walimu walimuogopa kwa sababu,,kila mwalimu aliyethubutu kunyanyua mkono wake kumpiga Laula,,basi mwalimu huyo,,anapoteza uhai usiku wa siku hiyo hiyo... pamoja na hayo yote,,Laula huyafanya hayo pasipo kujitambua,,na wakati anafanya matukio hayo,, huwa anapoteza kumbukumbu juu ya alichokifanya! failia ya Laula ikawa ni tishio la kijiji hicho,,, siku moja nyakati za usiku wa manane,, Laula alidamka kutoka usingizini,,lakini macho yake hakuyafumbua! akazioiga hatua kuufuata mlango,,ghafla akatoweka kimiujiza! akajitokeza kwenye eneo la makaburi,,akaendelea kuzipiga hatua na kulifuata kaburi moja lililokuwa katikati ya makaburi mengine! kaburi hilo linasadikika kuwa ni kaburi la Muanzilishi wa ukoo wao,,alizikwa miaka zaidi ya miamoja iliyopita,,na jina lake aliitwa LAULA,,na mrithi wa jina lake ni Laula huyu ambaye ni mtoto pekee wa mwanamke Njile! kumbe kuna siri nzito ambayo alikuwa anaijua Baba yake Laula...mbaya zaidi alikufa pasipokusema maana chimbuko la Jina hilo alilomrithisha mwanae wa pekee. ilikuwa hivi,,enzi za ujana wa baba Laula,,alikuwa anaugua ugonjwa ambao haikujulikana ni ugonjwa gani,,kumbe baba baba mzazi aliwahi kumtukana marehemu baba yake ambaye ni babu yake baba Laula,,na siku ambayo anakufa mzee huyo alisema,,daima kizazi chako hakitafanikiwa kuishi katika dunia hii,,aliongea maneno hayo na kukata roho papohapo... miaka ilizidi kusonga,,hatimae baba Laula akazaliwa,,,lakini aliishi na kufanikiwa kuoa Lakini akaanza kuota magome ya miti katika mwili wake akapelekwa hospitali lakini haikufahamika anaumwa ugonjwa gani,,,ndugu zake wakaamua kumpeleka kwenye tiba mbadala wakampeleka kwa mganga wa kienyeji....mganga akasema,,mkitaka mtu huyu apone,,ni lazima akafukue kaburi la muanzilishi wa ukoo wake,,achukue jino la mbele katika fuvu la muanzilishi wa ukoo wake...ikalazimika afanye hivyo! siku hiyo akadamka usiku wa saa sita akaelekea makaburini! alipolikaribia kaburi hilo mara ghafla!!!!! ↔↔↔↔↔ITAENDEA↔↔↔↔↔ Kila msomaji hakikisha una LIKE hadithi hii kuipa nguvu..niirushe kila siku. Ungana nami katika sehemu ya 4. wingi wa Like zenu ndizo zitafanya nilete muendelezo kwa wakati. 2017®

at 3:47 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top