Story: Sitaki tena – 07 Ilipoishia.. "Ni..mi..mi.. Ndo nimemu..uaaaaaaa Peeeeeendo... Endelea... Nilijikuta nimeropoka kila kitu huku kwa ghafla yule mzee akamuwahi kumshika mke wake kisha akanigeukia na kuniuliza tena., "Binti ulikuwa unasema?... Samahani sana sijakusikia vizuri nilikuwa namuwekea karibu na mdomo mama yako mfuko aweze kutapika..." Aliongea yule mzee bila ya kuonyesha wasi wasi wowote kama kuna neno baya ambalo Levina mimi nimeropoka, "Nilitaka kukupa mfuko huu hapa mkubwa nimeona huo mdogo hautatosha kwa maana mama anatapika sana.." Nilimjibu kwa kuzuga huku macho nimeyaelekezea chini kwa aibu kubwa niliokuwa nayo pale, nikajifanya kihere here kwa kumpa maji yakunywa yule mama aliyekuwa anatapika ambaye ni mama yake na Pendo, Mzee alinishukuru sana kwa wema wangu japokuwa ukweli nilibaki nao moyoni, "Umesema binti unaelekea wapi?" Aliniuliza yule mzee na kwa mda ule tulikuwa tukiendelea kupiga story za kawaida kuhusiana na maisha njia nzima japo ukweli kuhusu pendo nilikuwa nao moyoni., "Naelekea Dar es salaam kutafuta kazi" "Kazi gani binti yangu?" "Naenda kutafuta kazi za ndani" Nilimdanganya sana kuhusu maisha yangu kwa ujumla na aliweza kuniamini kwa asilimia kubwa kuwa natokea Iringa naelekea Dar kutafuta kazi za ndani, Ile roho ya kikatili,ilikuwa imeshaanza kunikabili kwani sikuwa hata na huruma ya aina yoyote..huku tukiwa tumeshasafiri mwendo wa kama masaa manne hivyo nikamwambia mzee kwakua gari ilikuwa inapitia Morogoro halafu ndo inaenda Dodoma ilinibidi nimwambie mzee kuwa tukifika morogoro anishtue kwa sababu nimeshapasahau sitapakumbuka vizuri.. * * * * Ndani ya masaa kama sita huku kausingizi kakinipitia mzee alinishtua na kuniambia kuwa tulikuwa tayari tupo maeneo ya mzumbe tukikaribia kuingia morogoro,hivyo niwe tayari nisilale tena, nilianza kujawa na furaha isiyotabirika huku furaha yangu zaidi nikiielekeza katika mifuko ya ile traki suti niliyokuwa nimeivaa na kuchomoa zile karatasi za ramani kisha nikazing'ang'ania mikononi mwangu nikisubiri niingie Morogoro.. *** Hatimaye tukaingia ndani ya mkoa wa Morogoro,kisha nikamuaga mzee pale lakini nilishindwa kumuaga mama kwakua tayari alikuwa ameshapitiwa na usingizi., "Usijali binti utafanikiwa nakutakia maisha mema na ubarikiwe upate kazi na uishi kwa amani huko uendako.." Yale maneno hayakuniingia akilini hata kidogo kwani hayakuwa na ukweli wa aina yoyote pale ila nikaamua nimuitikie tu kwa kumridhisha yule mzee., "Ahsante sana mzee na poleni sana kwa msiba uliowakuta" Nilimwambia huku nikionesha tabasamu la huruma la uongo, nikampa mkono kisha nikamuaga kuelekea stendi ya upande wa pili huku yule mzee akiamini kabisa kuwa nlikuwa naelekea dar kumbe naweka kwanza kituo.. *** Mda ulikuwa umeshatimia kama saa nane mchana huku kukiwa na hali ya uvugu vugu iliyojawa na baridi lakini siyo kali sana kama la Iringa kwani manyunyu yalikuwa yakidondoka taaratibu kuashiria mvua inataka kunyesha,huku nikiwa nimejikunyata mikono yangu niking'ang'ania zile ramani ndani ya mifuko ya suruali,niliweza kutoa na kufungua mojawapo ya ramani iliyokuwa inaelekeza kwa 'Baba Ali' huku nikiiongoza inavyoelekeza.. "Sasa, hapa ndo nimeambiwa panaitwa 'Boma Road' na ramani inaelekeza kota hizi hizi... embu ngoja nimuulizie huyu mtu.." "Samahani kaka..Sijui unamfahamu 'Baba Ali'..?" Nilimuuliza mpita njia niliyeamini kuwa atanisaidia kumpata mtu ninayemhtaji., "Baba Ali..Baba Ali.. Yeeah, nimemkumbuka anaishi maeneo ya paleee juu tena mnene hivii alikuwa anaishi na mke wake na watoto lakini sasa hivi anaishi peke yake?.." "Ndo huyo huyo..",nilimuitikia tu huku nikiamini atakuwa ndo huyo huyo kutokana na maelezo aliyonipa Gervas., "Nyosha na hii barabara ukifika pale njia panda anza kuhesabu nyumba ya kwanza mpaka ya tatu ndo hapo hapo" "Ok., asante sana.." Furaha ilinizidia zaidi ya pale nilipokua naelekezwa sikutaka hata kugeuka nyuma akili yangu ikaelekea mpaka kwenye njia panda na nilipofika kwenye lile eneo nikaanza kuhesabu nyumba ya kwanza mpaka ya tatu, nikaingia ilikuwa ni nyumba kubwa iliyojaa wapangaji mbalimbali nilipofika nikapokelewa na majirani na kuwaulizia 'Baba Ali' kisha wakaninyoshea chumba anachoishi na kuanza kugonga hodi., "Karibu karibu.." ilisikika sauti yakiume niliyoamini ndo mwenyewe 'Baba Ali..' "Wewe ndo baba Ali?" "Ndo mimi karibu binti" Niliingia ndani kwake japo alikuwa na chumba na sebule,ni kweli sikuona dalili yoyote ya mke wala watoto ,niliweza kumwelezea matatizo yangu yote kisa cha mimi kupelekwa gerezani na wema wote alionitendea mdogo wake ambaye ni Gervas,misukosuko yote hadi nilivyokwenda kwa Gervas akanipa ramani mpaka nimefika hapa, aliitikia kuwa ilikuwa ni kweli alikuwa akimfahamu Gervas kama ndugu na alikuwa akiishi na mkewe na watoto lakini wameshaachana na kuhusu kuelekea nyumbani kwetu nisijali kesho yake atanipeleka mpaka mlangoni kwetu, hivyo akanizidishia furaha na msisimko ndani ya mwili wangu zile ramani zikawa hazina tena maana kwangu nikampa akazichukuwa na kuzichanachana kisha akaenda kuzitupa nje. Ilikuwa imeshatimia saa tatu za usiku hivyo akaniandalia maji ya kuoga nikaenda kuoga niliporudi nikakuta kashanunua chakula (chipsi mayai) hivyo tukakaa mezani na kula,baada ya hapo akanielekeza chumba nitakacholala kisha taa zikazimwa nikamwacha akijilaza kwenye kochi pale sebuleni.. Ikiwa ni usiku wa manane huku nikiwa nimejifunika shuka sio zito sana huku nikiwa nimejikunja kwa kaubaridi kalichokuwa kakininyemelea nilianza kuhisi kama kuna mtu anahema mgongoni mwangu tena kwa pumzi ya hali ya juu,nilipaamini sana pale na pia nilivyomuheshimu 'Baba Ali' sikufikiria hata kidogo kama anaweza kunifanya chochote, kadri mda ulivyokuwa unaenda ndivyo nilihisi kama mikono inapenya katika makwapa yangu kisha inashika na kutekenya matiti yangu huku ikiteleza kwa kunipapasa pasasa ikihamia taratibu katika sehemu zangu za siri na kuanza kuzitekenya, nilishtuka lakini kwa ujasiri niliokuwa nao sikutaka kupiga kelele kwanza mpaka nimjue ni nani anayenifanyia vile, sasa nikawa napapaswa maeneo ya mapajani kwangu huku yule mtu akigeukia upande wa mbele yangu.. "Kohh..! kohh..! kohh..!" Nikakohoa kwa nguvu japo yule mtu ashtuke lakini hakutaka kuniachia, "Wewe nani? Naomba uniache..!" Niliamua kutoa sauti ya juu kidogo huku nikiwa na hasira kali na mishipa iliyonitanda usoni,lakini haikusaidia kwani kilichofuata nilihisi kama panga au kisu kikiumana na sakafu kisha haraka taa ikawashwa.. "Heee Baba Ali..?" Sikutaka kuamini hata kidogo kwani ni kweli alikuwa 'Baba Ali' juu ya kifua changu, aliyejitambulisha na kunipa hifadhi hapa kwake ndo alikuwa akitaka kunibaka.. "Shhh.. Nani Baba Ali..? Tena ukome siku nyingine kuniita hivyo,Gervas mie simjui na huyo 'Baba Ali' unayedhania ni mimi siyo na huko kwenu sikujui malaya mkubwa we..!" Yale maneno yalinichoma sana sikuwa na jinsi kwakuwa alinishikia panga na kunilazimisha kufanya atakavyo hivyo akaniingilia kinyume na maumbile usiku kuchwa huku akinisababishia maumivu makali na damu nyingi kunitoka mwilini mwangu.. Sikuweza kupata usingizi hata baada ya kunifanya atakavyo na kuniacha pale usiku ule Kitandani nikiwa sijiwezi, nilimshuhudia akichukuwa suruali yake na kutoa noti ya shilingi elfu moja na kunipatia.. "We malaya, chukuwa hii itakusaidia japo ukapate chai" Nilijikuta napandwa na hasira kali,huku nikihema haraka haraka pale bila hata kuongea chochote nikachukua ti sheti yangu na ile traki suti nyeupe aliyoniachia Gervas kisha nikamgeukia na kumwambia.. "Ahsante sana kwa wema wako ulionitendea" Kisha nikatoka nje,kupitia kwenye kakorido ambapo pembeni kulikuwa na beseni la vyombo vichafu vya majirani kwa bahati nzuri nikaona kisu katika vile vyombo hivyo halmashauri ya kichwa changu ikafanya kazi fasta, nikakichukuwa na kurudi ndani kwa kasi ya ajabu na kumkuta 'Baba Ali' akiwa kainama chini uku akifunga kamba za viatu,nikamuwahi kabla hajageuka na kuinuka na kumchoma kisu cha mgongoni kisha nikakichomoa haraka na kumuwahi tena kabla hajapiga kelele na kumchoma tena maeneo ya shingoni kisha nikachukuwa kitambaa na kumjaza mdomoni ,hivyo nikamshuhudia 'Baba Ali' akigala gala pale chini huku akitoa macho na mishipa ya shingoni ikimlegea. Zoezi lililofuata ni kuingia mpaka chumbani kwake na kutafuta hela zilipo, nilitumia kama dakika tano bila ya mafanikio huku nikishuhudia kuona madawa ya kulevya pamoja na vitambulisho mbalimbali vya watu tofauti feki hivyo nikagundua kuwa 'Baba Ali' alikuwa ni jambazi tena sugu lililoshindikana tena lilikuwa likitafutwa, baada ya kutafuta hela bila ya mafanikio hatimaye nikazipata pesa nyingi sana kwenye kisanduku alichokuwa amekificha chini ya kitanda, lakini mimi nilikuwa nahtaji kama shilingi elfu hamsini tu hivyo nikazichomoa, "Liwalo na liwe..!" Nilijihisi kama yule stelingi wa muvi za kichina 'Jet Li', kwakuwa ilikuwa usiku sana kama mida ya saa kumi,niliweza kutoka pale bila hata ya kuonana na majirani wowote haraka haraka nikafuata ile njia niliokuja nayo na kuondoka kuelekea msamvu ambapo ndipo ilipo stendi ya mabasi ya mikoani., **** Nikiwa tayari nimeshakata tiketi katika basi la Abood, safari ya kutoka Morogoro kuelekea Dar ilianza na nilikuwapo ndani ya basi la kwanza kabisa lililotoka sa kumi na moja na nusu, na tangu nilipoingia katika basi sikuwa na wasiwasi wowote kwani moyo wa kishujaa na kijasiri ulikuwa umenitawala, lakini sasa takribani nusu ya watu kwenye lile basi walikuwa wakinishangaa huku wakiangaliana na kutikisa vichwa vyao, nilishindwa kujizuia nikajiangalia juu mpaka chini.. "Mmmh...! mmmh...!" Safari hii niliweza kuwah kujiziba mdomo ili nisiropoke jambo lolote baya kwani traki suti yangu yote ilikuwa imejaa damu huku na mikono yangu ikitapakaa damu mpaka sehemu za usoni kitendo kilichofanya njia nzima abiria wanishangae kwa kuwa vile.. Tukiwa tunakaribia kuingia chalinze, basi letu likasimamishwa na trafiki wawili mmojawapo akiwa ni askari polisi,kwa mara nyingine moyo ukawa kama unawaka,nywele zilinisisimka huku mdomo ukinitetemeka kisha nikalitega sikio langu kwa upande wa nje kusikia maneno ya kondakta wa basi letu akiwa na trafiki., "Umesema mmepakiza abiria wangapi?" "Sitini na mbili tu" "Hakuna waliosimama?" "Hakuna" "Usiniambie hakuna wacha nipande niingie nijionee mwenyewe ndo uniambie hakuna sawa?" Maneno hayo yalinifanya nizidi kulegea kwani aliyekuwa anaongea na kondakta alikuwa hajavalia mavasi meupe bali alivalia mavazi ya kaki yale yenyewe ya polisi huku akiwa kashikilia bunduki akapanda ndani ya basi huku akiangaza siti moja baada ya nyingine na alipofika kwangu.. "We vipi tena Mmepata ajali wapi?" "Hatujapata ajali yoyote huyo kapanda basi hivyo hivyo..!" Aliropoka dereva wa basi huku akisaidiana na kondakta wake kunimaliza.. "Haya shuka., shuka upesi chini.,we dereva endeleeni na safari yenu" Nilijikuta nipo mikononi mwa yule polisi haraka akiniwahi kwa kunifunga pingu baada kushushwa chini na kuacha basi likiendelea na safari.. "Mungu wangu...! Mungu wangu...! mbona umeniacha..? Mbona wanitenda hivi....!" Nilijikuta nikiandamwa na mikosi na kumshushia lawama Mwenyezi Mungu alieniumba na kujiona sifai kuishi katika dunia hii, huku nikiwa chini ya ulinzi pale barabarani,Yule askari polisi akaniangalia juu mpaka chini akawa anatingisha kichwa huku akicheka kuashiria kama mtu anayenifahamu sana.. "Levina..?" Sikuamini amini kama jina hilo atakuwa amelitaja yule askari au ameambiwa na mtu kuwa naitwa Levina,nilihisi kama moyo ukinipasuka ghafla,hivyo nikawa sina tena jinsi kwani nikawa nimeshapatikana, lakini swali lililoniumiza kichwa ni kwamba nipo pale kwa kosa lipi la mauaji? "maskini isikute baba yake 'Pendo ndo kamtuma huyu polisi..? ....Au., nilivyomuua 'Baba Ali taarifa zimemfikia huyu polisi..?" Nikiwa bado najiuma uma pale huku akili ikiwa haifanyi kazi kabisa,ghafla nikamuona yule polisi kabadilika zaidi ya pale kwani sura yake ilikunjamana ghafla huku akinifokea.. "Kwanini umeua Tena..?" Lile swali lilinifanya nilegee na kudondoka mpaka chini kwani nilikuwa sina nguvu tena ya kusimama huku nikishindwa kujua kipi cha kufanya pale chini... "Au unapenda kwenda tena gerezani., naona safari yako nyingine sasa imefika..?" "Hapana nisamehe afande sijakusudia nii...l..ii...piii...ti...wa...,tu..na shetani..?" Kabla sijamalizia kujitetea nilishangaa kuinuliwa kwa kushikwa shati kwa nguvu kisha kilichofuata ni kupigwa vibao na mitama huku nikishindwa hata kujizuia kutokana na zile pingu nilizokuwa nimefungwa mikononi., "Kaka mkubwa, wacha nimpeleke kituoni Dar huyu mpumbavu ana kesi kubwa na nitampigia simu afande Geofrey aje msaidiane hapa.." Nilijihisi kama mtu asiye na bahati hapa duniani,maumivu aliyonisababishia 'Baba Ali wakati akiniingilia kinyume na maumbile ukiongezea maumivu aliyonisababishia huyu polisi vilinifanya niumie sana moyoni,huku mwili wangu ukiwa hautamaniki kwa majeraha.. ******* * * Levina amekamatwa kwa mauaji yapi, ya 'Pendo' au 'Baba Ali..? Inaendelea...

at 8:56 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top