Riwaya: SARAI SEHEMU YA KUMI NA MOJA(11) ***ilipoishia*** wakati baba sarai anataamaki alipoinua uso wake ili ampe pole mama yule hakumuona alipojarubu kuangazaangaza macho hakufanikiwa kuona mama yule kapitia njia gani wakati anajiuliza mara ghafla...aliguswa begani alipogeuka kumtazama aliyemgusa!!!baba sarai alistuka sana kumuona mtu huyo..alikuwa ni yule bosi wake aliyemfukuza kazi baada ya sarai kuiba kimiujiza zile nyaraka ofisini kwa baba sarai... ***Endelea*** bosi huyo akauliza"habari za miaka mingi....nimekutafuta sana lakini sikubahatika kukupata....zile nyaraka tulizipata kumbe secretary wangu alizileta ofisini kwangu lakini alisahau kaziweka wapi...chukua hii ni kadi yangu ya bihashara tutawasiliana kupitia namba hizo zilizo andikwa kenye kadi hiyo....baba sarai aliipokea kadi hiyo kisha akasema asante nitakupigia simu. bosi yule akaondoka zake..... ilipofika majira ya jioni baba sarai alionekana akiingia kwenye mgahawa akaagaza chakula...lakini alikuwa anawaza sana kuhusu yule mwanamke muuza mbogamboga..""kutokana na msongo wa mawazo hata hamu ya kula chakula ilitoweka...akanyanyuka na kulipa pesa kwa ajili ya chakula alichoagiza akaondoka zake...akarudi nyumbani kwake....alipofika akachukua simu yake kisha akapiga simu kwenye zile namba alizopewa na bosi wake wa zamani.....simu ilipopokelewa..baba sarai alijitambulisha kisha.... yule bosi akasema kuanzia kesho rudi ofisini uendelee na kazi....baba sarai alifurahi sana.... ************ Asubuhi palipokucha alidamka mapema sana.akajiandaa kuelekea kazini....akiwa njiani alikutana na fukara maarafu kwa jina la ombaomba...fukara yule alikuwa ameketi chini kando ya barabara.. huku ameshikilia kikombe... kikombe hicho alikitumia kwa ajili ya kuomba msaada wa pesa....baba sarai alipopita jirani. ombaomba huyo aliomba msaada...lakini baba sarai alipitiliza na kuendelea kuzipiga hatua huku akitoa maneno ya fedheha kwa kusema"" yani mimi ningekuwa raisi wa nchi hii,basi ombaomba wote ningeamuru wauwawe mnakera sana mnadhani pesa zinatingishwa kwenye mti zidondoke kama maembe pumbavu kabisa... ((((HUJAFA HUJAUMBIKA USIMTUKANE MAMBA WAKATI BADO HUJAVUKA MTO))) baba sarai kabla hajafika mbali alivamiwa na vibaka wakamkaba...alijaribu kupiga kelele lakini hakuna mtu aliyekuja kumsaidia....ghafla ilisikika sauti ikisema nawasihi sana muacheni mtu huyo... wale vibaka waliogopa wakamuachia baba sarai wakatimua mbio....kumbe alikuwa ni yule ombaomba ndio kaamuru wamuachilie baba sarai.. baba sarai alipogeuza shingo yake alistahajabu kumuona yule ombaomba ndiye amekuja kutoa msaada.....kisha omnaomba yule akasema""pole sana ndugu binadamu wote sio wema....kisha akaondoka na kurudi kuketi pale alipokuwa mwanzo....baba sarai alimtazama ombaomba huyo kisha akaindoka zake..... alipofika kazini alianza kazi moja kwa moja.... baada ya wiki moja kupita baba sarai alipandishwa cheo alipewa nyumba pamoja na gari la kutembelea.....akaanza kuwa anawapelekesha wafanyakazi waliokuwa chini yake..wakati mwingine aliwapiga mokofi na kuwatukana...... baba sarai akawa ni mtu anayeogopwa kuliko mmiliki wa kampuni hiyo... siku moja jumamosi baba sarai akiwa nyumbani kwake alipanga kwenda kutembea ufukweni mwa bahari akajiandaa na kutoka nje ya geti huku akiliendesha gari lake.....akamkuta yule mama muuza mbogamboga akiwa kando ya geti huku ameweka beseni lake chini akimnyonyesha mwanae......baba sarai alisimamisha gari lake na kushuka akamfuata mama yule....... alimkumbuka kwa sababu alikuwa anafanana na marehemu mkewe kwa sura na umbo....alipomkaribia alimuuliza mbona umeketi hapa nje ya ukuta wa uzio wangu!!!!bila shaka tulishawahi kukutana sehemu???? je umepajuaje hapa nyumbani kwangu??? baba sarai aliuliza maswali hayo kwa mfululizo..kisha akasema nyinyi mafukara mnapenda sana kumfanya mtu aongee aonekane muongeaji....inaonekana unanifuatilia kila nyendo zangu yani mpaka umepafahamu ninapoishi...haya una shida gani???mama yule hakujibu kitu aliendelea kumnyonyesha mwanae.. baba sarai akasema"" ondoka eneo hili sasa hivi unachafua ukuta wa nyumba yangu... ye mama kasema""samahani nimetembea sana kwenye jua nikitafuta ridhiki kwa kutembeza mbogamboga....naomba dakika moja tu mwanangu amalizie kunyonya kisha nitaondoka... baba sarai akalipiga teke lile beseni la mama yele huku akisema haya matakataka kamlishe mbuzi toka....mama yele alinyanyua uso na kumtazama baba sarai huku machozi yakimlenga machoni...kisha akaondoka zake na kuliacha beseni lililopigwa teke na mboga zote kudondoka kwenye mchanga..wakati huo baba sarai alikuwa akimtazama mama huyo kwa macho ya chuki.. alipogeuza shingo yake ili arudi kwenye gari lake hakuliona gari lake pale alipokuwa amelipaki.. alipogeuza shingo kumtazama mama yule hakumuona hata lile beseni pamoja na zile mboga zilizokuwa zimedondoka chini hakuziona...akiwa anataamaki alistahajabu hata nyumba yake haionekani........ ITAENDELEA....... Usikose kufatilia simulizi hii nzuri ya kusisimua ASANTENI.

at 1:19 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top