MCHORO WA AJABU (12) “ile pale kwenye meza.” aliongea huku akihema na kujaribu kujizuia utofauti wake usionekane kwa wasichana hao. Tina aliichukua chupa hiyo na kupuliza kidogo. Kweli harufu waliyokua wakiinusa ilifanana kabisa na harufu inayotoka kwenye chupa hiyo. “umenunua shilingi ngapi” aliuliza Tina baada ya kuishika chupa hiyo na kuiangalia kwa muda. “mimi mwenyewe nimeletewa tu zawadi na sijui hata amenunu shilingi ngapi.” alijibu Mudrick. “ina harufu nzuri sana...sio siri yaani.” alisifia Tina. Baada ya maongezi ya hapa na pale, Vyonne alinyayuka na kutoa hela alizopewa na mama yake amkabidhi. “mama amenituma nikuletee tu hela zako.. Maana alikua na wasi wasi sana utamchkuliaje kwa kukucheleweshea mzigo wako.” alionea Vyone. “usijali...ni wazi kua hakutakiwa kuwa na wasiwasi juu ya hili.. Maana kama kupanga nimeshapanga na hivi sasa sina deni useme kua nilikua naitegemea sana hiyo hela ili nilipe madeni yangu... So mwambie kua sina wasi wasi na wala hakua na haja ya kuhofua kitu chochote.” Vyonne aliaga na kumshtua Tina ambaye alitokea kuvutiwa na filamu aliyokua ameiweka Mudrick kwa ajili ya wageni wake. “hii cd si ipo?.. Au mwambie asimamishe utakuja kuangalia ukirudi wangu.” aliongea Vyonne na kumvuta Tina. Wakiwa kituoni , Tina aliamua kuongea ya moyoni kwa rafiki yake, kwani ukaribu wao ambao unaonekana ungeweza kuleta madhara kwake. “shoga yangu nikuambie tu ukweli kua mimi nampenda sana Wizard... Naomba kama huna mahusiano nae, basi unisitiri rafiki yangu na hata kama akikutongoza usimkubali wangu.” aliongea Vyonne na kumuangalia Tina ambaye alitabasamu. “kwanza mimi nilikua najua kua nyinyi ni wapenzi na wala sikua najua kua huna mahusiano nae. Pia unafahamu kabisa kua mimi nina Jimmy wangu na ninampenda sana kuliko mwanaume yeyote yule. So ondoa shaka kabisa na mawazo yoyote juu yangu mimi.” aliongea Tinna na kumuahakikishia mwenzake usalama wa mtu wake. “yaani shoga yangu nampenda sana ...yaani hivi nipo mbali nae ndio nazidi kabisa kuteseka kwa ajili yake.” aliongea Vyonne. “sasa umeshamuambia ukweli ili ajue kua umempenda kiasi gani?” aliuliza Tinna. “mimi sina ujasiri huo wa kumuambia mwanaume kama nampenda..nitaanzia wapi mie?” aliongea Vyonne. “wanawake tunatakiwa tuamkwe na kujijua kua tuna uhuru wa kuchagua kitu kutoka kwenye mioyo yetu...ukimpenda mtu muambie ukweli tu na najua kua kwa Wizard hawezi kupindua kwa msichana mrembo kama wewe.” aliongea Tina na kucheka. “sawa mama..nitajaribu kuongea nae kama atanielewa.” aliongea Vyonne na kuliona gari la kwao. “sasa mpenzi mimi acha niwahi home..tutawasiliana.” aliongea Vyonne na kupada gari na kuondoka. Tina alirudi nyumbani kwao na kukuta mlango wa Mudrick upo wazi. Aligonga na kukaribishwa ndani. Alikuta filamu aliyokua akiiangalia ikiwa imegandishwa akisubiriwa yeye aje kuangalia. Wakati anaendelea kuangalia movie hiyo, alianza kupatwa na hisia za ajabu. Yaani ilikua ni hali fulani kama mtu aliyekua akiangalia filamu ya X. Alijihisi kusisimkwa kama vile alikua akitekenywa na kuguswa sehemu zake zote zenye muamko. Alianza kulegea mpaka akawa anajishangaa mwenyewe. “mudrick, mimi naondoka. Nitakuja kuendelea kuangalia siku nyingine.” aliongea Tinna “mbona piche yenyewe ipo mishoni hii?” aliongea Mudrick “acha tu niende...nilikua nasinzia tu hata sijaielewa.” aliongea Tinna na kunyanyuka. “basi ichukue ukaiangalie kwenu.” aliongea Mudrick na kwenda kuitoa filamu hiyo kwenye deki na kumkabithi “shukrani.” Aliichukua filamu hiyo na kuondoka nayo. Aliwaza sana na kujishangaa kwa kutokewa na hali hiyo. Alikua anawaza ni kwanini hali kama hiyo ilimtokea wakati hakua na wazo lolote juu ya mwanaume huyo wala filamu hiyo haikua na kipande chochote chenye uchochezi wa kufanya ngono. Baada ya kuona anajirundikia maswali ambayo hayana majibu. Akaamua kupotezea na kuamua kwenda kuoga. Alikula chakula cha usiku na kulala. Aliota anafanya mapenzi na Mudrick na kuamka asubuhi akiwa hali mbaya. Alikusanya shuka lake haraka na kwenda kufua. Kabla hajamaliza kufua shuka lake, Mudrick alitokea akiwa na ndoo yake ya maji ya kuoga huku akiwa anatabasamu kama vile alikua akielewa kilichomtokea Tina usiku kwenye ndoto yake. “nilete na mimi nguo zangu unifulie Tina.” alitania Mudrick. “lete tu.” alijibu Tina huku akimuangalia Mudrick. Mudrick alienda kuoga na alipomaliza alitoka na kwenda kazini kwake kama kawaida. “niambie ndugu yangu.. Kuna usumbufu wowote unaoendelea kuupata kutoka kwa jini huyo?” aliuliza Bob. “hakuna..tena ndio kwanza kanisaidia walipokuja watu kuulizia harufu iliyokua ikinukia ndani kwangu.” aliongea Mudrick. “sema mwanangu unaishi na maajabu kama jina lako... Maana kuwa na kiumbe cha ajabu na kukuambia kinakupenda basi ni kweli una shughuli nzito.” aliongea Bob na kucheka. “mimi kinachonishangaza ni huu mvuto wa ghafla niliokua nao kutoka kwa wasichana mbali mbali ninaokutana nao.. Yaani nikikumbuka zamani kila msichana niliyekua nikimtongoza alivyokua akinikataa ndio nakosa majawabu kabisa.. Sijui jini huyo ndio kaniongezea mvuto ili ninase kwenye mtihani wake?” aliongea Mudrick na kumfanya Bob acheke. “sasa unacheka nini mshkaji?” aliuliza Mudrick. “wewe mambo yako mazito sana...mimi nashindwa hata nikushauri vipi?”aliongea Bob. “nashindwa hata kujua nifanye nini ili niweze kuwa huru katika jambo hili.” aliongea Mudrick. “mimi nimekushauri vizuri tu..ila wewe mwenyewe umegoma kwenda kwa mtaalamu.sasa unataka watu tukushauri vipi?” alionge Bob na kumfanya Mudrick anyayuke. “wewe hujui kwanini nilikataa..ila ni bora kukaa bila demu kuliko kuanza kuhofia kuuliwa.” aliongea Mudrick na kuamua kuondoka baada ya kuona hawezi kupatia msaada wa kutosha kutokana na tatizo lake. Alirudi nyumbani kwake na kulala. Siku hiyo ikapita tena bila kutokewa na jini huyo wala kuisikia sauti yake. Kwa muda wa wiki nzima, Tina alikua akimuota Mudrick kua anafanya nae mapenzi. Na kila akimuota basi ni lazima ajikute katika hali ile ile kama mtu aliyetoka kufanya mapenzi kweli. Aliamua tu kuvumilia hali hiyo kwakua alikua na aibu ya kueleza mambo yake ya kike kwa baba yake ambaye anaishi nae kwenye nyumba hiyo. Alijikuta kua anatamani kulionja penzi linalomsumbua ndotoni kila siku. Kila akimuangalia Mudrick alipata mshawasha mkali wa kujaribu kujihakikishia kua uwezo wa Mudrick ulikua ukifanana na uwezo wake kwenye ndoto. Aliandaa safari na kumualika Mudrick ambaye alikubali kutoka na Tina bila kujua dhamira ya msichana huyo. “tunaenda wapi sasa?” aliuliza Mudrick walipokua wanatoka nje na kukuta kuna coster inawasubiri nje. “maeneo fulani hivi twende tukale bata.” aliongea Tina na kumshika mkono Mudrick na kuongozana nae. Aliingia kwenye coster na kukuta kuna watu wasiopungua kumi huku kila mmoja akiwa na mpenzi wake wamekaa na kushikana hapa na pale. Safari ilianza huku makelele ya hapa na pale yakiinogesha safari hiyo. Gari iliingia kunduchi beach na kupokelewa vizuri wa wahudumu. “nimechukua chumba tayari...ukijisikia uchovu niambie nikupeleke ukapumzike.” aliongea Tina na kumuangalia Mudrick kwa macho malegevu. “kwani tunalala huku?” aliuliza Mudrick. “yeah.. Tena tunalala chumba kimoja coz nimeamua tuifurahie hii siku pamoja Wizard.” aliongea Tina na kumfanya Mudrick atoe macho kidogo. Alimuangalia Tina ambaye kimea kilikua kimesha mkolea. ITAENDELEA

at 12:05 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top