MCHORO WA AJABU (11) “nina usingizi mzito sana wangu...Usiku mwema.” aliongea Mudrick na kuingia ndani kwake. Sio kwamba alikua na usingizi kama alivyosema. Sema alijua kua yupo kwenye mtihani mzito sana wa kuwa karibu na wasichana Kwani haruhusiwi kupenda. Tena kwa sasa anajiona ni mwenye mvuto sana na wasichana kuliko kawaida. Sasa mawazo ya kua anaishi na jini yakarudi tena. Akajikuta amekosa raha ghafla na kuuwazia usiku huo kama atakuja tena au mauza uza hayo yamesha isha. Akiwa na mawazo mazito Mudrick juu ya ujio wa jini huyo. Usingizi ulimteka na kumalaza fofofo mpaka asubuhi paka kucha tena. Alidamka na kwena kazini kama kawaida. Walifanya kazi na jioni wakaamua kujidili nini wafanye ili Mudrick asiwe na wasi wasi tena juu ya maisha yake. “kuna mtaalamu wa nyota naitwa Balish..yeye ni mtaalamu sana kutokea na amewasaidia wengi sana kujua tafsiri za ndoto zao...unaonaje kama kesho tukienda kuonana ane?” aliuliza Bob. “sawa..ila haitokua gharama kubwa sana.” aliuliza Mudrick. “hata si hela nyingi sana..ila hata kama gharama itakua kubwa, hela zinatafutwa lakini kuijenga amani ni kazi sana.” aliongea Bob na kumfanya Mudrick aitikie kwa kichwa. Waliagana na kila mmoja akenda kwake huku wote wakiwa na mawazo ya kwenda kwa mtaalamu huyo siku inayofuata asubuhi na mapema. Mudrick alifika kwake na kujifungia mlango. Baada ya muda akatoka na kwenda kutafuta chakula Baada ya kurudi na chakula ndani kwake. Alianza kula huku akiangalia movie aliyokua akiingalia toka awali. Baada ya movie hiyo kuisha. Alichukua maji na kwenda kuoga.sasa aliona ni muda muafaka wa kulala baada ya kuuweka mwili wake sawa na maji hayo. Kelele za vitu kugongwa gongwa zilianza kusikika tena. Tena safari hii vilikua vikigonga kwa nguvu kuliko kawaida. Upepo mkali ukaanza kuvuma na kupeperusha mapazia yake japokua alikua amefunga milango . Upepo huo ulitulia na mwanga mkali ukatokea na kufanya chumba kizima kiwe na nuru hiyo kutoakana na kuwa na giza awali lililotokana na Mudrick kuzima taa wakati ana lala. Harufu nzuri ya manukato ikatawala kwenye chumba hicho na mwanga ukaanza kufifia taratibu na sura ya dada huyo ikaanza kuonekana. Taa iliwaka yenyewe bila kuguswa na kuzidi kumpa uoga Mudrick ambaye muda ho alikua amelowa jasho japokua feni lilikua likimpepea. “samahani kwa kuja bila taarifa...ila nina machache tu nataka nikuambie kuhusu mimi. Nadhani hujanijua vizuri na hufahamu mimi ni vitu gani napenda na vitu gani sivipendi.” aliongea dada huyo mwenye sura nzuri na sauti ya kuvutia pia. “nimekukataza maswala ya kuhusiana na wanawake kimapenzi lakini sijakukataza kuwa karibu nao. Ila ukitaka nitumie nguvu ni pale ninaposikia kua unataka kwenda kwa mganga au kiumbe chochote kitakachokua na uwezo wa kunizuia. Hapo hukasirika sana na kuweza kufanya madhara makubwa sana. Jifikirie mara mbili kabla kesho hujaamka na kuongozana na mwenzako na kwenda huko mlipotaka kwenda.” alingea dada huyo na kuzima taa. Upepo ulikatia ghafla na sauti zikakoma hapo hapo. Mudrick alijikongoja huku akiwa anahema na kuwasha taa. Hakumuona tena yule dada. Alihema kwa nguvu na kukaa kiandani. Usingizi ulikata moja kwa moja na kumfanya Mudrick awe macho mpaka asubuhi. Alishtuka baada ya simu yake kuita. Aliiangalia na kukuta anayempigia ni Bob. “nikuambie ukweli tu Bob kua safari ime kufa ndugu yangu” aliongea Mudrick na kunmfanya Bob ashangae. “kivipi tena unaiua safari hivi hivi.” aliulia Bob kwa mshangao mkubwa. “nimetokewa tena na malikia wa majini.. Ameniambia kua nisiende safari yangu.” aliongea Mudrick na kumfanya Bob ashangae. “wewe unatakiwa umuepuke huyo jini... So kama usipoenda ataendelea kukutesa mpaka lini?” aliuliza Bob na kumfanya Mudrick ashindwe kujibu. “sawa lakini..ila mimi kama ndugu yako wa karibu nilikua nataka nikusaidie tu kwa sababu wewe ndio mwenye matatizo na sio mimi. Maadamu umekataa wenyewe basi sawa. Nadhani tutakutana kazini muda sio mrefu.” aliongea Bob na kukata simu. Mudrick alibaki akijifikiria pale bila kupata jibu. Alikata shauri na kuamua kwenda kazini kama kawaida yake. Wakati akiendelea na kupiga kazi, alipigiwa simu na Vyonne. Aliamua kuipokea na kumsikiliza ni kitu gani anataka kuongea na yeye. “uk pouwa?” aliuliza Vyonne baada ya salamu. “niko pouwa..niambie.” aliongea Mudrick. “nasikia tu umehamia nyumbani kwa rafii yangu Tina...i wish nije nikuone wagu.” aliongea Vyonne huku akicheka. “karibu.” alijibu Mudrick kimkato. “la muhimu lilionifanya nikupigie simu ni kuhusu hela yako ya kodi ...mbona umemsusia mama yangu?” aliongea Vyonne huku akionyesha hali ya kuhuzunika. “mimi najua hali ya mama yako. Alikua anatamani mimi nihame wakati hana hea ya kunirudishia. So nikaamua mpaka atakapopata ndio anitafute, kama sasa anayo nyie nitumieni haki yangu kwenye tigo pesa.. Nadhani nipo sahihi kwa maamuzi yangu.” aliongea Mudrick na kumsikiliza Vyonne ataamua nini. “kwa sasa mama amejua ukweli kua hutembei na mimi.. Anajuta na anatamani uje akuombe msamaha.” aliongea Vyonne. “swala la kuja huko haliwezekani...ila muambie tu kua sina kinyongo nae. Tukikutana barabarani tusalimiane kwani hizi ni changamoto tu za maisha na yupo sahihi kwa ulinzi juu ya mtoto wake. So ukweli kutoka moyoni ni kwamba nimemsamehe kabisa. Muambie hivyo.” aliongrea Mudrick na kumfanya Vyonne ashuahe pumzi ndefu. “sawa...upo wapi muda huu?” aliuliza Vyonne. “nipo kazini.” alijibu Mudrick. “nije saa ngapi ili nikukute?” aliuliza Vyonne. “saa moja nitakua nimesharudi tayari.” alijibu Mudrick na kukata simu. Alitoka kazini jioni kama kawaida yake na kurudi nyumbani. Alimkuta Tina akiwa kibarazani kama kawaida na kumsalimia. Aliingia chumbani kwake na kutulia. Simu yake ikaita na jina la Vyonne likatokea kwenye kioo cha simu yake. “umesharudi?” aliuliza Vyonne. “yeah.” alijibu Mudrick na vyonne akakta simu. Dakika kumi na tano baadae aliisikia sauti ya Vynne kwa mbali akiongea na rafiki yake. Baada ya robo saa, alisikia mlango wake ukigongwa. Alienda kufungua na kuwa karibisha ndani wawili hao. Usafi wa mudrick ulikua kitu kingine cha kuvutia machoni mwa wasichana hao ambao ndio mara ya kwanza kupata nafasi ya kukaribishwa ndani. “mimi nachokaga hapa tu kaka yangu... Yaani mbali na kua hushindi nyumbani na unabanwa sana na kazi zako, lakini kwenye maswala ya usafi una zingatia sana.” aliongea Vyonne na kumfanya Mudrick atabasamu. “mazoea tu..hata mimi napenda kuwa sehemu safi... Hua najihisi amani ninapokua msafi muda wote.” aliongea Mudrick na kuwaangalia kwa zamu wasichana hao waliokua wakitabasamu. “unatumia air fresh ya aina gani..maana pananukia humu balaa.” hilo swali lilimfanya Mudrick ashtuke, kwani ile harufu ya yule jini ni kweli ilikua ikiendelea kunukia mule ndani. Alidhani kua pengine yeye peke yake ndio alikua akiinusa kwakua ndio mlengwa, ila kuulizwa swali hilo alijua wazi kua hata akiamua kutokea tena jini huyo basi atakua anaonekana na wote. Wakati akitaka kujibu swali hilo. Alitupa macho yake kweye meza anayoweka mafuta yake ya kupakaa na perfume na kuiona chupa ya air fresh ambayo ilijiongeza kimiujiza na kumfanya apate la kujibu. “ile pale kwenye meza.” aliongea huku akihema na kujaribu kujizuia utofauti wake usionekane kwa wasichana hao. Tina aliichukua chupa hiyo na kupuliza kidogo. Kweli harufu waliyokua wakiinusa ilifanana kabisa na harufu inayotoka kwenye chupa hiyo. ITAENDELEA

at 12:04 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top