JAMANI BABA! SEHEMU YA 17 ILIPOISHIA “Sawa kipenzi . ” Wakabusiana na mzee kupata kiburudisho chake kwa saa moja na kisha kurudi nyumbani huku akiwa mwepesiii, hakuacha kumtembelea Mwaija nyumbani hapo , kazi ikawa ni kujilia tunda kila siku. SASA KANYAGA MWENYEWE .. . Mwezi mmoja ulikatika tangu Mwaija aondoke nyumbani hapo . Siku hiyo mama kama mama, uchungu wa mwana ulimwingia , akaamua kumpigia Mwaija japo amjulie hali . .. “Ni mtoto wangu wa kumzaa , siwezi kumtupa hivi. Mwenye makosa ni baba yake, kwani si anajua yule ni mwanangu ? “Sidhani kama Mwaija ndiye aliyemtongoza baba yake wa kambo . Lakini mwanangu yule naye amezidi uzuri . We mtoto mdogo wowowo vile , kiuno kiuno kweli . Mguu wanasema wa bia, halafu yale macho mwanangu yale ndiyo yanayomponza kabisa, ” alisema mama Mwaija simu ikiwa sikioni tayari. .. “Shikamoo mama,” Mwaija alimsalimia baada ya kupokea.. . “Marhaba , hujambo ?” “Mi sijambo.” “Hajambo shangazi yako ?” “Hajambo .” “Maisha yanaendaje?” “Kawaida tu mama. ” Mama Mwaija alishtuka kusikia kelele za wapiga debe wakisema ... “Msasani Posta... Msasani Posta.” “Mwaija ,” aliita. ... “Uko Dar ?” “Hapana mama , niko Tanga.. .” “Unanidanganya mimi wewe?” “Hapana mama , kwa nini ?” “Mbona nasikia watu wa daladala wakisema Msasani Posta?” “Siyo Msasani mama , unasikia vibaya . Wanasema Mkwakwani Posta. Siku hizi Tanga kuna daladala za Mkwakwani Posta, ” alisema Mwaija huku akitetemeka. “Kweli ?” “Kweli mama , kwani we hujui kuna daladala za Mkwakwani Posta?” “Mi nimesikia Msasani Posta.” “Hapana mama bwana. ” “Haya , shangazi yako anaendeleaje ?” “Anaendelea vizuri . Nipe niongee naye .” “Mimi nipo mtaani , nimemwacha nyumbani.” “Ukirudi tu, nipe niongee naye. ” “Sawa mama .” Mwaija alipomaliza kuzungumza na simu na mama yake , akampigia Masilinde.. . “Baby uko wapi ?” “Kazini, vipi ?” “Kimenuka. Njoo haraka sana.” “Nini?” “Ungekuja baby bwana .” “Oke, nakuja sasa hivi . ” Mwaija alizidi kutetemeka, hasa alipoambiwa akifika nyumbani ampe simu shangazi yake ili mama yake aongee naye . Ndani ya nusu saa , Masilinde akawa amefika nyumbani kwa Mwaija huku akiwa na sura yenye mshangao.. . “Vipi Mwaija , kuna nini ?” “Inabidi niende Tanga haraka sana , hata nikiondoka leo hii .” “Kuna nini ?” “Mama. ” “Mama gani?” “Mkeo .” “Kafanyaje?” “Kanipigia simu .” “Enhe , kasema anakwenda Tanga kesho? Maana kama anasafiri kesho tatizo liko wapi, mi si nitamzuia tu?” “Siyo hivyo baby. Mama kasema nimpe simu shangazi aongee naye, nikamwambia nipo mtaani, shangazi nilimwacha nyumbani. ” “Sasa ikawaje?” “Akasema nikirudi atataka aongee naye . Na mimi najua lazima baadaye jioni mama atapiga tena. Halafu akaniuliza Mwaija upo Dar ? Nikamwambia hapana mama, akasema mbona nimesikia sauti za daladala zikisema Msasani Posta? Nikamdanganya siyo Msasani Posta ni Mkwakwani Posta. Ndiyo akatulia.” “Kha! Kwani we leo ulifika Msasani ?” “Si ulinikubalia niende kwa yule rafiki yangu .” “Oo ! Sasa sikia , sidhani kama ni ishu.. .” Kabla Masilinde hajamaliza , mama yake alipiga tena... “Huyo , anapiga ,” alisema Mwaija ... “Usipokee kwanza. ..nataka kujua , kwani shangazi kule Tanga ana simu ?” “Hapana, alikuwa akitumia ya kwangu. ” “Oke. Sasa itabidi tumkodishe mwanamke, tumwambie ajifanye shangazi yako , aiige sauti , wewe utamwambia sauti ya shangazi ilivyo. ” “Shangazi ana sauti ndogo sana , utadhani mtoto.” “Ah! Kumbe ni hivyo , hata mimi naweza kuigiza sauti ya kitoto . Hebu pokea mwambie ongea na shangazi, ” alisema Masilinde. Mwaija aliogopa lakini mama yake aliendelea kupiga, ikabidi apokee . .. “Haloo mama .” “Umesharudi nyumbani?” “Ndiyo.” “Nipe shangazi yako. ” “Huyu hapa , ongea naye. ” Masilinde alijibana sawasawa , akavuta pumzi inavyotakiwa ili atoe sauti ya kitoto .. . “Halo. ” “Ee, wifi za leo?” “Njema, za huko Dar ?” “Huku kwema wifi , unaendeleaje na huyo binti yako?” “Tunaendelea vizuri , ila mi mwenyewe kifua kidogo si kizuri sana .” “Oo ! Pole, ndiyo maana sauti inatoka kama inataka kukatika. ” “Ee. Umeona ee?” “Ee. Pole sana. haya, nilitaka kukusalimia tu wifi maana huyo aliniambia alitoka, nikamwambia akirudi niongee na wewe .” “Asante sana wifi yangu. Msalimie sana Masilinde.” “Haya zimefika wifi .” Baada ya kumaliza kuongea na mke wake akijifanya ni shangazi mtu, Mwaija na Masilinde walicheka kiasi cha kushindwa kuhimili na kujishika matumbo yao lakini kumbe simu ilikuwa haijakatwa upande wa pili.. . itaendeleaaa

at 12:41 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top