JAMANI BABA Sehemu 16 ILIPOISHIA Asante ila mimi nataka talaka yangu tu kama amekwambia kuhusu kumfumania na mwanangu. ” “Ameniambia lakini unakumbuka mwaka huu , mwezi wa pili na wewe ulifumaniwa kule kwa mzee Bakari na yule mzee wa genge la Mwembeni, ulimwambia mumeo ?” TEMBEA NAYO MDOGOMDOGO. ... Kitendo cha kusema maneno hayo tu, Masilinde akaona afadhali kwamba naye alipata pa kujitetea kwani hata mke wake aliwahi kufumaniwa. “Kumbe alishawahi kufumaniwa?” “Ndiyo.” “Na nani?” “Kwa mzee Bakari, yule mzee muuza genge mtaa wa pili ” alisema mzee Kimanama . “Mama Mwaija umesikia hayo? Unanishia bango wakati hata wewe umewahi kufumaniwa ?” Masilinde alimwambia mkewe . “Wala sijawahi kufumaniwa, halafu we mzee acha uchuro wako hapa. Nataka talaka yangu ... ” “Talaka sikupi, kama umenifumania, na wewe ushawahi kufumaniwa, kwa hiyo ngoma droo, kama umefunga na mimi nimefunga. ..”“ Nasema hivi nataka talaka yangu. ” “Mimi si ndiye muandikaji wa talaka , siwezi kutoa ...halafu niliweka nadhiri kwamba katika maisha yangu sitakuja kutoa talaka mpaka naingia kaburini... ” Kwa hasira, mama Mwaija akamgeukia Mwaija . “Halafu na wewe ni lazima uondoke hapa nyumbani, nikipewa talaka na wewe safari kwani siwezi kuendelea kuishi na mtoto mwenye tabia chafu kama yako ... ” “Nisamehe mama, sitorudia tena ... ” “Hakuna cha msamaha, ungekuwa umefanya kosa lingine ningekusamehe lakini siyo kufanya mapenzi na baba yako, kwa mwanamke yeyote ni aibu kubwa sana .” Hapohapo akamgeukia mzee Kimanama .“ Na wewe mzee mbeya , umesema kwamba nimefumaniwa, lini nimefumaniwa?” “Unajifanya hukumbuki ?” “Na nani?” “Si yule mzee muuza genge, alijifanya kukuongezea vimbogamboga kumbe alikutaka na ukaingia mkenge, tena mzee nuksi sana kwa wake za watu yule. ..” Mama Mwaija akakasirika, alijua kwamba hakuwahi kufumaniwa ila mzee huyo alikuwa akidanganya, alichokisema ni kwamba waende kwa mzee huyo, kweli wakaenda na kumkuta akiwa amesimama nje . “Karibuni. ..” “Asante , wewe mzee , hujawahi kufumaniwa na huyu mwanamke ?” aliuliza mzee Kimanama . “Mwanamke gani ?”“Usijifanye hujui, kwani hapa wanawake wapo wangapi?” “Namuona mmoja tu. .” “Sasa kama unamuona mmoja kwa nini unauliza jibu? Aya tujibu .” “Sijawahi kufumaniwa naye , kwanza hata mapaja yake tu sijawahi kuyaona .” “Wewe mzee muogope Mungu , leo unaruka na wakati siku ile ulipigwa mpaka picha !’ “Nimekumbuka sasa , kweli nilishawahi kufumaniwa, ila si na huyu mwanamke, yule alikuwa mama Mwajabu , yule wa mtaa wa tatu, mwanamke mweupe wa Kitanga aliyefanana na mkeo ,” alisema mzee huyo , alionekana kukasirika na hivyo kumzingua mzee Kimanama. “Huo sasa utani .. .” “Kama ni utani basi jua wewe ndiye umeanza kunitania, kwanza naomba muondoke nyumbani kwangu kabla sijawaitia polisi . ”Hawakuendelea kusubiri, tayari Masilinde akaonekana kushindwa, alichokifanya mara baada ya kufika nyumbani ni kuanza kuomba msamaha kwa mkewe kwa kilichotokea . “Mke wangu naomba unisamehe ni shetani alinipitia nakuahidi sitarudia tena kosa hilo , nisamehe mama na nipo chini ya miguu yako,” Masilinde alimwangukia mkewe . “Ukitaka tuelewane kuna sharti moja .” “Lipi ?” “Huyu malaya sitaki akae hapa nyumbani. ” “Eeeh ! Amekuwa malaya tena, huyu si mtoto wako wa kumzaa!” “Hata kama , umekubaliana na mimi?” “Sawa . Kwa hiyo nikampangie chumba ili atoke hapa?” “Umpangie chumba! Nani kasema hivyo , unataka uwe unajiachia kila siku, haiwezekani, huyu arudi Tanga.” “Arudi Tanga?” “Ndiyo.” “Mbona unamtupa hivyo ?” “Mimi si ndiye mama yake ! Arudi Tanga .” Kwa sababu mke wake aliamua hivyo na hakutaka kumpoteza kwa kuendelea kudai talaka, akakubaliana naye. Alichokifanya mzee huyo ni kumsisitizia Mwaija kwamba waendelee kuwasiliana hata kama angekuwa wapi kwani bado moyo wake ulimpenda sana na hakutaka kumuacha. “Kwa hiyo ndiyo hivyo baby, tuwe tunawasiliana, usimuogope mama yako, kutembea nje ya ndoa ni faulo za kawaida tu, kama kuchezewa rafu uwanjani, ” alisema mzee huyo .Siku iliyofuata mama Mwaija aliamua kumrudisha Mwaija Tanga. Mawasiliano na msichana huyo yaliendelea kisiri na baada ya wiki moja, mzee huyo akamtumia binti huyo nauli na kumvuta tena Dar , kipindi hiki akampangia chumba kabisa, mtaa wa Tandale karibu na Kwa Mtogole. “Utakuwa ukiishi hapa mpenzi , hapa sasa kwa raha zetu , mama akipiga simu, mwambie upo Tanga, siku nyingine akisumbua sana, kata simu kisha baadaye utamwambie network inazingua, ” alisema mzee huyo . “Sawa kipenzi .” Wakabusiana na mzee kupata kiburudisho chake kwa saa moja na kisha kurudi nyumbani huku akiwa mwepesiii, hakuacha kumtembelea Mwaija nyumbani hapo , kazi ikawa ni kujilia tunda kila siku. Itaendeleaaa.

at 12:41 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top