Walimwengu ndivyo walivyo, Mwenye shibe hamjui mwenye njaa... Alikuja na kiu na sasa ametosheka hana budi tena kujuwa utalipokeaje, Swala la yeye kukuacha wala lisikuumize moyo, Najuwa kinachokuumiza ni marengo uliyoyaweka kwake pamoja na UPENDO uliouwekeza kwake, JE UNAWEZA KUMLAZIMISHA AKUPENDE? Najuwa majibu yako ni HAPANA na hata Mimi najuwa hivyo, Sasa basi nakusihi ondosha hicho kitu akilini mwako, na ujipange kukabiliana na upweke ambao tayari upo mbele yako ili uweze kuruhusu Mawazo mapya, Penzi jipya, Mtu mpya lakini pia FURAHA MPYA! Uwezo wa hayo yote upo ndani yako , Maana kama ni funzo umepata sasa unalialia nini ? Jiamini na uwe na hakika kuwa WEWE NI MZURI ndo maana yeye alikupenda, unajuwa kabisa MUNGU hakukuumba kwa bahati mbaya ila kwa makusudi sasa unajikunyata kwa hudhuni kwa lipi au ameondoka na sababu ya wewe kuitwa mwanamke? Mwache aende maana kilichompata ni ulevi wa MAHABA imempelekea kukuona wewe wa kawaida, Ulevi huo ukimlaza doro ATAKUTAFUTA... Nakushauri USIKUBARI KUENDESHWA NA MLEVI WA MAPENZI! Kutoijuwa thamani yako inatosha sana wewe kujuwa HAKUFAI.

at 1:48 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top