SIRI ZA GIZANI NO 7 Nasra aliendelea kulishwa unga wa ugali tu mule kwenye diaba, na kila ilipo fika saa nane za usiku mda alio chukuliwa na bibi yake, Nasra alikuwa anatolewa kwenye diaba kisha anaanza kucheka na kuimba na bibi yake, na mala tu baada ya kuimba na kucheka bibi yake anamrudisha kwenye diaba kama kawaida. Ila kaka yake Nasra yaani Ibra kila alipo kuwa akilala alikuwa anaota ndoto za ajabu sana, na mala nyingi alikuwa anaota kuwa mdogo wake yupo hai hajafa, lakini kila alipo kuwa akimwambia baba na mama yake walikuwa hawamuelewi kabisa maana mtoto walimzika na msiba ulifanyika, mda mwingine Ibra alikuwa anachapwa kwa sababu ya usumbufu wake wa kila siku kwamba "dada Nasra hajafa, dada nasra hajafa uwa namsikia akiimba usiku, yaani namsikia kabisaa, akiimba usiku" hayo maneno alikuwa anayataja sana mpaka mama yake akaanza kumgombeza, lakini ibra kila siku alikuwa anaongea hivyo, maana kumbe bibi yake alivyo kuwa anaimba na kucheza usiku na nasra, ibra alikuwa anasikia maana yeye na nasra wote walizaliwa tumbo moja hivyo damu ilikuwa nzito, siku moja Ibra akiwa amelala aliota sauti ya dada yake imemuijia ikisema, "kaka ibra nenda kwenye kabuli langu" Ibra alikuwa muoga sana kutoka nje usiku, lakini ile ndoto ilimsumbua sana Ibra ikabidi afungue mlango aende nyuma ya nyumba yao kuangalia kabuli la mdogo wake maana ndipo walipo kuwa wamemzika kule kwa nyuma. Ibra alipo fika kwenye kabuli alishangaa sana maana alikuta ile sehemu ipo tambalale kabisa na hakuna kabuli lolote mda ule, ndipo Ibra akakimbia haraka kuingia ndani, akiwa analia huku watu wote wamelala, isipo kuwa bibi yake maana walikuwa ndani na Nasra wanacheza na kuimba ila hakuna alie kuwa anasikia zile sauti zaidi yao wawili. Siku moja usiku sana bibi yake nasra alikuwa anamuogesha nasra ili asitoe harufu mbaya chumbani maana tangu amfungie hakuwai kuoga ata siku moja. Sasa wakati anamuogesha ibra akawa amesikia sauti za maji kutoka kwenye chumba cha bibi yake huku bibi akisema kwamba "nasra geuka nikusugue na mgongoni kuchafu" ibra alipo chungulia vizuri kwenye kitasa cha mlango akawa amemuona Nasra anaogeshwa kama mtoto mdogo wakati ni dada tu anaeweza kuoga mwenyewe. USIKOSE YA 8...

at 12:31 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top