Mara kadhaa amejitahidi kukwambia "Nakupenda, usiniache please", ila sasa hawezi kusema tena. Ametaka kusema "Kwanini hauelewi jinsi navyoumia moyoni", ila amejua kwamba hawezi kukulazimisha umpende. Ametaka kujaribu kusema "sijali tena", ila ametambua haitasaidia tena kukurudisha kwake. Ametaka kusema "samahani" ila amejua kwamba hajakutendea kosa lolote kupelekea usimpende tena!k Ametaka kusema, "Mbona umebadilika, haukua hivi", ila ametambua kwamba hawezi kukuomba au kukulazimisha ubadilike. Ametaka kusema "tujaribu kukaa chini, tujadiliane na kurudisha mapenzi yetu", ila ametambua hataweza kwani wewe hauko serious hata kidogo. Amejitahidi kuonesha kila aina ya upendo, ila wewe umeshindwa kumpenda. Amekupigia simu mara kwa mara hupokei. Amefikiria labda utakuwa busy, lakini siku nzima inapita wala hupati call yake kuonyesha aliona missed call zako! Amekupigia simu usiku, amekukuta busy ukiongea na simu, na ulipomaliza kuongea wala hukumpigia tena simu. Amekutumia messages watsapp zinaonesha kabisa tick ya blue lakini hukuhangaika hata kumjibu, busy ukichati na watu wengine! Mapenzi yanauma asikwambie mtu, hufika hatua ukachukia kila mtu na kila kitu. Ukatamani Dunia ikumeze japo kwa dakika chache usahau maumivu unayopitia. Mtu hutamani uwe na uwezo wa kuteka mawazo ya mpenzi wako na kujua nini anachokiwaza kichwani mwake. Watu wengi wanapitia magumu katika mapenzi, sio masikini, tajiri au wa daraja la kati. Mahusiano yameteka akili za binadamu. Badili gia angani, kubaliana na hali halisi, mwaka mzima mtu habadiliki, utakumbatia mti wenye miba mpaka lini? Mtu akikupenda ni vigumu sana kukusababishia maumivu moyoni! Labda hilo halikuwa fungu lako. Moyo ukipenda ni vigumu sana kubishana nao, ila utafanya nini sasa? Najua maumivu ni makali, moyo unauma, akili haifanyi kazi, inauma zaidi ukikumbuka nyakati zile zilizo njema, kipindi mapenzi yakiwa mapenzi kweli! Nyakati alipokuwa mtu wa kweli kwako...ila sasa mambo yamebadilika, ni kama kibatari kilichozimika ghafla katika kiza kinene penye uhitaji wa mwanga. Busara yangu, "one of the happiest moments in life is when you find the courage to let go of what u can not change" Tuache masihara mapenzi yanauma asikwambie mtu, Mungu wangu aliye muaminifu akakuvushe katika gumu unalopitia, akakusaidie kurudisha furaha yako uliyoipoteza. Ukiona ugumu nitafute unishirikishe tuliite jina la Mungu wetu aliye mkuu teso hilo litaondoka na mungu atakurehemu mahali ulipokosea.

at 12:09 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top