*JE,WAZIJUA SIRI KUMI ZA NDOA* 1. *KILA UNAEMUOA AU KUOLEWA NAE ANA UDHAIFU WAKE* *Mungu* pekee ndio haana udhaifu, Kila ua waridi lina chimbuko lake. 2. *KILA UNAEMUOA AU KUOLEWA NAE ANA HISTORIA YAKE MBAYA* Hakuna mtu ambae ni malaika,epuka kuchunguza mambo ya mtu ya nyuma samehe na usahau. 3. *KILA NDOA INA CHANGAMOTO ZAKE* Ndoa sio kitanda cha maua waridi yanayomeremeta kila muda,kila ndoa yenye mafanikio imepitia misukosuko mingi. 4. *KILA NDOA INA HATUA ZAKE KATIKA MAFANIKIO* Hatuwezi kuwa sawa, kuna watakaokuwa mbele kidogo na watakaokuwa nyuma kidogo. Kupunguza stress, kuwa mtulivu, fanya kazi kwa bidii na kwa muda muafaka ndoto za ndoa yako zitatimia. 5. *KUOA AU KUOLEWA NI KUTANGAZA VITA* Ukishaoa au kuolewa ni kuingia katika uwanja wa mapambano,Kuwa tayari kupambana kuulinda ukanda wa ndoa yako. 6. *HAKUNA NDOA ILIYOKAMILIKA* Hakuna ndoa ambayo imetimilika,Ndoa ni kazi ngumu,jitolee mwenyewe na ufanye kazi ya kuijenga ndoa yako iwe kamilifu. 7. *MUNGU HAWEZI KUKUPA MTU KAMILI UNAYEMTAKA* Mungu atakupa mtu ili wewe umtengeneze jinsi wewe unavyohitaji yeye awe. 8. *KUOA NI KUJIINGIZA KATIKA HATARI* Huwezi jua nini kitatokea baada ya ndoa, hali inaweza badilika,hivyo achia nafasi ya marekebisho. 9. *NDOA SIO MKATABA WA MUDA BALI NI MKATABA WA KUDUMU* Ndoa inahitaji ahadi ya kudumu,mapenzi ni gundi ambayo huwafanya wanandoa kuwa pamoja daima..Talaka huanza katika mawazo. 10. *KILA NDOA HUHITAJI KUJITOA* Hakuna mapenzi rahisi katika ndoa,huwezi kupenda au kupendwa bila kujitoa nafsi yako kwa dhati. *Vijana karibuni sana katika familia za wanandoa ila unatakiwa utoe uoga*

at 9:33 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top