FANGASI SEHEM ZA SIRI. (Vaginal candidiasis) Maambukizi ya Fangasi katika Sehemu za SIRI. Share na like page hii. Nimekuwa nipoa sim nyingi na kuwasaidia watu wengi haswa wanawake katika tatizo hili nimeona kunahaja kubwa ya kuongelea swala hili kiundan ili watu wote mpate elimu hii iwasaidie na kwa ambao hawafaham nini chakufanya wapate mwanga sasa endelea. Kati ya maambukizi yanayowasumbua wanawake na wanaume wengi duniani ni maambukizi ya fangasi. Inakisiwa asilimia 75 ya wanawake wote duniani hupata maambukizi haya katika kipindi cha uhai wao. Maambukizi ya fangasi katika sehemu za siri za mwanamke husababishwa na uwepo wa fangasi wanaojulikana kitaalamu kama Candida albicans. Maambukizi haya pia hujulikana kama yeast infection au thrush. Fangasi hupatikana kama vimelea vya kawaida katika mdomo, mpira wa kupitisha chakula sehemu inayojulikana kama pharynx, katika kibofu cha mkojo, uume na hata kwenye uke. Mfumo mzuri wa kinga wa mwili pamoja aina fulani za bakteria wanaoishi pamoja na fangasi hawa husaidia sana katika kuthibiti maambukizi yanayoyosababishwa na aina hi ya fangasi. Nini hutokea? Kwa kawaida, Candida albicans huishi kwenye uke na sehemu nyingine (kama zilivyoelezewa hapo juu) bila kusababisha madhara yoyote yale isipokuwa pale mazingira ya eneo husika yanapobadilika kama vile mabadiliko katika hali ya pH ya eneo husika (ifahamike ya kwamba pH ya kawaida ndani ya uke ni 4.0 - 4.5) au uwiano wake na vimelea (microorganisms) wengine unapoharibiwa kutokana na sababu mbalimbali kama vile matumizi ya madawa aina ya antibiotics, kupungua kwa kinga mwilini kutokana na magonjwa mbalimbali. Maambukizi haya ya fangasi yanaweza kugawanywa katika sehemu kuu mbili Maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi mara moja hadi nne kwa mwaka na dalili zake huwa si mbaya sana na maambukizi haya husababishwa na fangasi wa jamii hii ya Candida albicans. Maambukizi makali yaani complicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi zaidi ya mara nne kwa mwaka, dalili zake kuwa mbaya zaidi au kama maambukizi yatakuwa yametokea kipindi cha ujauzito, ugonjwa wa kisukari, upungufu wa kinga mwilini. Aina hii kusababishwa na vimelea vya aina nyingine tofauti na Candida albicans. Vihatarishi Watu walio katika hatari ya kupata maambukizi ya fangasi hawa ni wale wenye • Kutumia sana dawa aina ya detergents kwenye sehemu za siri au douches (vifaa vinavyotumiwa kusafishia uke kwa kutumia maji yaliyochanganywa na siki au antiseptic yoyote ile) kwa sababu hali husababisha kuharibika kwa uwiano wa fangasi na aina nyingine ya vinyemelezi kama bakteria aina ya lactobacilli • Kutumia sana madawa aina ya antibiotics, steroids ambayo yana tabia ya kushusha kinga ya mwili • Mabadiliko ya mfumo wa homoni mwilini ambayo husababisha mabadiliko katika sehemu za siri na hivyo kufanya kuwepo kwa ukuaji wa kasi wa fangasi hawa • Ujauzito (kutokana na kubadilika kwa mfumo wa homoni mwilini na kupungua kwa kinga ya mwili). Hata hivyo ieleweke hapa kuwa si kila mjamzito hupatwa na maambukizi haya. • Matumizi ya dawa za kupanga uzazi (vidonge vya majira) • Upungufu wa kinga mwilini kutokana na magonjwa sugu kama kisukari, saratani aina yoyote ile, ugonjwa aina ya mononucleosis na nk. • Ugonjwa wa ukimwi (HIV/AIDS) • Matibabu ya homoni (hormonal replacement therapy) kutokana na sababu mbalimbali • Matibabu ya kusaidia kushika mimba kwa wale wenye matatizo ya uzazi (infertility treatment) • Msongo wa mawazo (stress) • Utapia mlo (malnutrition) • Kuvaa nguo au mavazi yanayoleta joto sana sehemu za siri kwa muda mrefu kama nguo za kuogelea (swimwear), nguo za ndani (chupi) zilizotengenezwa kwa kitambaa aina ya nylon, nguo za ndani zinazobana sana nk. • Kujamiana kwa njia ya kawaida mara tu baada ya kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) au matumizi ya vilainishi venye glycerin wakati wa kujamiana pia yamehusishwa na maambukizi haya. • Kuvimba kwa tezi la koo (goiter) • Saratani ya tezi la koo (thyroid cancer) • Wanawake wenye umri wa miaka kati ya ishirini na thelathini wapo kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi haya wakati wale ambao wameshaacha kupata hedhi au wale ambao hawajaanza kupata hedhi kabisa hawako kwenye hatari kubwa. Kwa wanaume vihatarishi vya maambukizi haya ni • Kujamiana na mwanamke mwenye tatizo hili au maambukizi haya • Upungufu wa kinga mwilini • Matumizi ya madawa aina ya antibiotics kwa muda mrefu bila ushauri wa daktari • Magonjwa sugu kama kisukari, saratani ya aina yoyote ile na nk. Dalili na viashiria kwa wanawake • Kuwashwa sehemu za siri (kwenye tupu ya mwanamke) • Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri (burning sensation) • Kufanya kama vidonda katika sehemu za siri (soreness) • Maumivu wakati wa kujamiana (superficial dyspareunia) • Maumivu au usumbufu wakati wa kujisaidia haja ndogo (wakati mtu anakojoa) • Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwa mdomo wa nje wa tupu ya mwanamke (labia minora) • Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au nyeupe kijivu, unaoweza kuwa mwepesi, majimaji au mzito na ambao umefanana na jibini (cottage cheese like discharge) wenye muonekano unaojulikana pia kama curd- like appearance. Kwa kawaida, uchafu huu haumbatani na harufu yoyote isipokuwa panapokuwa na tatizo la ziada kama ugonjwa wa zinaa aina ya Bacteria vaginosis. Uchafu huu unaotoka hapa unaweza kuenea kwenye maeneo mengine yaliyokaribu na tupu ya mwanamke kama kwenye mitoki (groin area) au perineum na kusababisha kuharibika kwa ngozi katika sehemu hizo. Dalili na viashiria hivi huwa mbaya zaidi wakati mwanamke anapokaribia kupata hedhi. Dalili na viashiria kwa wanaume ni • Kuwashwa sehemu za siri • Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwenye ncha ya uume • Kuwepo kwa uchafu wa rangi nyeupe (kama nilivyoeleza hapo juu) kwenye sehemu ya juu ya uume. • Kuwa na vidonda vidogo kwenye uume (sore on the glans) Hata hivyo, mara nyingi wanaume hawaoneshi dalili zozote zile, ni vizuri kwa mwanamke kumueleza mwenza wake pale anapopata maambukizi haya ili naye pia apate kutibiwa. Vipimo vya uchunguzi Kabla ya vipimo vya uchunguzi, ni muhimu kwa daktari kuchukua historia ya mgonjwa kwa usahihi kabisa. Vipimo vitahusisha: Uchunguzi wa uke (per Vaginal Examination (PV exam) Daktari huvaa gloves, na kuzilainisha gloves hizi kwa jelly maalum, mgonjwa hulala kwenye kitanda na kutanua miguu yake ili njia itanuke na kumrahisishia daktari kumfanyia uchunguzi, wakati akiwa tayari, daktari ataingiza vidole vyake viwili (cha shahada na cha kati) ukeni kwa dhumuni la Kuhisi kama kuna uvimbe wowote ndani ya tupu ya mwanamke Kuangalia kama anapata maumivu wakati wa kujamiana Kuangalia kama kuna uchafu wowote unaotoka, wingi wake, rangi yake, harufu yake, uzito wake (mwepesi, majimaji au mzito), na aina ya uchafu unaotoka kama ni sahihi kutokana na maelezo ya mgonjwa au ni tofauti Kuangalia kama sehemu ya siri ipo kawaida Kuangalia kama kuna uvimbe wowote wa tezi za sehemu ya siri (mitoki) Kuangalia nywele za sehemu za siri zilivyo na jinsi zilivyokaa Kuangalia shingo ya kizazi, bartholin glands nk. Kuangalia sehemu ya haja kubwa kama kuna skin tags, bawasiri (haemorrhoids) nk. Kuangalia kwenye kinembe (clitoris) kama kuna tatizo lolote lile. Hayo ni baadhi tu ya malengo na faida za kipimo hiki kwa vile humuwezesha daktari kugundua tatizo au maradhi mengine ya ziada ambayo hayajaanza bado kuonesha dalili zake kwa mgonjwa au mgonjwa mwenyewe hafahamu kama hali aliyo nayo ni tatizo. Hata hivyo inashauriwa sana kabla ya kufanya kipimo hiki, daktari amjulishe mgonjwa aina ya kipimo, lengo lake na jinsi kitakavyofanyika ili kumuandaa mgonjwa kisaikolojia. Aidha ni muhimu pia kumtaarifu wakati anapoanza kuingiza vidole. Kuchunguza uchafu unaotoka kwa kutumia hadubini (microscope). Mara tu baada ya kuchukua sehemu ya uchafu kwa kutumia swab, kipimo hicho humwagiwa tone la 10% potassium hydroxide ambayo huyeyusha chembechembe za ngozi na kubakisha seli za Candida albicans. Kuwepo kwa pseudohyphae (mfano wa aina fulani ya mizizi au miguu ya fangasi hawa) pamoja na budding yeast cells (yaani seli za fangasi zinazojigawa kwa ajili ya kuzaliana) ni uthibitisho wa maambukizi ya fangasi aina ya Candida albicans. Kuchukua kipimo na kuotesha kwenye maabara ili kuangalia aina ya uoto huo kama ni wa fangasi aina ya Candida albicans, ama la. Kipimo cha mkojo (Urinalysis) Vipimo vingine hufanyika kulingana na dalili zinazoashiria uwepo wa magonjwa mengine kama vile ugonjwa wa kisukari, HIV/AIDS, ugonjwa wa kuvimba tezi la koo (goiter), saratani ya tezi koo (thyroid cancer) nk. MATIBABU Kama umeshapitia vipimo hivyo au hata vipimo mbali mbalI na bado tatizo linaendelea au linajiludia mara kwa mara wakati mwingine linaweza kuwa sugu unashauliwa kutumia njia za asili. kwa maelezo zaidi na msaada wa kimatibabu piga 0767421678 au 0655148030 unaweza kutuma sms za aina zote utajibiwa kupitia 0767421678. ASANTE. Share na like page yetu AFYA KWA WANAUME na AFYA YA WANAWAKE Facebook. https://www.facebook.com/hamad1199/

at 8:51 AM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top