®HADITHI PICHA® Mussabhai & YuYuShortstory 👙👙👙 DADA VUA👙👙👙 PICHA NO:_4 Basi Shangazi alimfokea bila kujali kuwa kuna ugeni amekuja nao,Helena hakujibu kitu shangazi alitupa tena dongo"Eheee na huyo ni nani!?? maana wewe hukawii kuniletea mijizi".......Lucy alidakia ....."Looooh!! shaangazi huogopi kutoa mineno hadi kwa wageni".Sule kuona vile alimwambia Helena"Aaaaamh!! hellen acha mi niende nisije kukugombanisha na shangazi yako"......"Bright usiogope huyu yukogo hivi anapenda sana kuongea".....Lucy naye alijichangamsha kwa Sule kama vile anamjua wakati ndio mara ya wa kwanza wanaonana "Kakaaa karibu usiogope mwaya karibu sana".Helena alitangulia ndani akiwa amebeba ndoo yake akawaacha Lucy na Sule nyuma.Lucy alikuwa na machachari sana mpaka Sule alishangaa" Mhhhhh!! huyu dada vipi kadata au!??" Mara Lucy akafunua kidogo nguo yake kwa pale kwenye nyonyo huku akimuonyesha Sule Vichuchu..... Endelea......NAOMBA LIKE YAKO USIWE MCHOYO WA LIKE BHAANA Sule alishindwa kumuelewa Lucy ni nini anakitaka maana sio kwa upumbavu ule aliouonyesha.Sule alimtazama kisha akamwambia"Una maana gani kufanya hivo??"......Lucy hakujibu chochote zaidi ya kujichekesha chekesha tuu kama mjinga.Kwa kuwa Helena alikuwa anamfahàmu vyema dada yake alivyo machepere aliongea kwa sauti"Wewe Lucy usimzoee kaka wa watu".Lucy alikuwa kimbelembele kumkaribisha ndani Sule,Sule alimuangalia kwa dharau kisha akajisemesha kimoyo moyo"We jipendekeze tuu kwangu".Sule aliingia ndani kisha akamwambia helena"Aaaaamh!! Hellen mi naona niwakimbie tuu maana nachelewa huko nakoenda".......kabla hata Helena hajajibu Lucy alidakia"Mmmmmmh!!! jamouny we kaka mbona haraka hivo usiende bwaana"Lucy alionge huku akimsogelea kwa karibu kabisa.......Sule aliamua kumtolea uvivu"Heee!! we vipi mbona kimbele mbele hivyo unanijua mimi??". Basi Lucy alijiona mdogo akajidharau kwani alijiremba kwa ajili ya kumtega huyu kijana handsome lakini majibu aliyopewa yalimkata maini.Wakati Lucy anataka kumuachia Sule mara shangazi naye alifika mlangoni"Eheeee!! upumbavu gani mnaufanya hapo,Umbwa nyie!! we kijana naomba uondoke haraka umetoka wapi kwanza"Shangazi aliongea kwa hasira sana lakini Helena alimpokea shangaziye"heeee!! Shangazi kwanini umfukuze kwani kakukosea nini huyu kijana wa watu".......Shangazi alisunya"nsyuuuuu!!!" kisha akatoka nje,Cha ajabu na cha kushangaza Shangazi aliondoka huku akitabasamu sijui ni kwa nini alitabasamu.Wakati huo Lucy aliamua kukaa pembeni akiwa hana tena furaha kama alivyokuwa.Helena alimtazama kisha akamwambia huku akicheka"iiheeeee!!! limekushuka shuuuuuuu!!!". Sule alianza kujisikia vibaya kwani Lucy alighafilika sana,Basi sule aliona njia rahisi ya kumrudisha kwenye furaha ni kumuita na tupige selfie kwa pamoja" Haya Nataka tupige picha nzuri yenye smile za kutosha".Sule alizama mfukoni ili atoe simu yake,Alijisachi kila mfuko lakini hakuona simu yake,Alishusha begi lake ili atazame kama aliiweka mule ila simu haikuwepo.Alijaribu kukumbuka mara ya mwisho aliiweka kwenye kitanda chumbani kwake"Ooooooh! my god!!!"........Helena alihoji"Wewe unatafuta nini"......."Daaah! nimesahau simu mbali sana"......."ooooh pole sana si iko sehemu salama lakini???"....."ofcoz ni sehwm salama ila sikupaswa kuiacha kwani kuna document zangu kibao ndani ya simu".Sule aliona potelea mbali japo inauma lakini ni ngumu kurudi kwenye ile nyumba iliyojaa chuki dhidi yake. Helena alijaribu kumtoa hofu"Usijali ukirudi utaikuta tuu"Sule alimeza mate na kusahau kuhusu simu"Any way tuachane na hilo maana nilitaka tupige picha ya kumbukumbu".Aliongea kisha akamuita Lucy na kumwambia"Lucy nisamehe kama nimekuudhi lakini mimi huwa sio mtu wa kuongea sana hivyo uliniforce nifanye kitu nisichokipenda".Helena alimfuata Sule kisha akamwambia"Bright mi narudi tena kisimani naenda kuteka maji ila we pumzika tuu nakuja saiv".Sule hakutaka kabisa kubaki pale kwani alijua Lucy ataanza kumsumbua"Aaaammh!! kwanini tusiogozane pamoja Hellen"......"Ni wewe tuu maana mimi nilijua unahitaji kupumzika ndio maana".Walikubaliana kuwa waende pamojampaka kule wanakochota hayo maji. Lakini wakati wanatoka Shangazi alionekana akiendelea na shughuli zake za kuhudumia mifugo,Macho ya shangazi yaliashiria kuwa kuna kitu ndani ya nafsi yake eidha hajapenda ujio wa kijana huyu au anamjua kwa namna moja au nyingine.Je kuna uhusiano gani baina ya huyu kijana na Bibi huyu???....Sule alimwambia Helena"Madam Hellen nimeacha kibegi changu pale kwani kuna shida??"........"Bright usiwe na shaka hakuna shida".Huku nyuma shangazi alimfuata Lucy na kumwambia"Hivi nyie watoto mnataka kunipanda kichwani si ndio!!?,Kwa nini mnapokea watu msiowajua mnajuahuyu ni nani?? Siku moja mtapokea mashetani ndio mkome maumbwa nyie!!!".Shangazi aling'aka sana na kumuacha Lucy akijichekea kwani amemzoea shangazi kwa kuongea.Lucy alilitazama lile begi la Sule kisha akaingiwa na tamaa ya kutaka kujua huyu ni nani,Kwanza alitoka na kuchungulia kama kina Helena wameenda ili aanze kupekua.Alihakikisha wamefika mbali kisha akarudi ndani tayari kabisa kupekua........Je atakutana ni vitu gani humo ndani??? Usikose sehemu inayofuata. Inaendelea........ usiache kudondosha like kwani bila like mimi sipati mizuka yakuleta vitu adimu. ALIKA RAFIKI ZAKO KWA KUSHARE ILI NAO WAPATE uhondo huu

at 10:55 PM

Bagikan ke

0 comments:

Copyright © Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top