Home → Love sms
→ *ππΉ UTULIVU MUMEO MPATIEππΉ*
"
*Vipi ulale na juba,*
*ondosha uchakarike ,*
*Tena usiwe mjuba ,*
*Legea utamanike,*
*Onesha zako shuruba,*
*mume kijiwe asikishike.*
*Kwake hukufata kula,*
*Utulivu mumeo mpatie,*
πΉπππππΉ
ππΉππππ
*Niqabu weka pembeni,*
*Sura sifichikane,*
*Chumbani ufiche nini,*
*funua uonekane.*
*Ukweli huu shikeni,*
*majambo msiyabane,*
*Kwake hukufata kula,*
*Utulivu mumeo*
πΉπππππ
πππΉπππΉ
*Soksi nazo ondoa,*
*na hina imdatishe.*
*Mwingine hatoopoa,*
*Moyoni mnururishe,*
*Mapema apate lowa,*
*Makeke yote yaishe,*
*Kwake hukufata kula,*
*Utulivu mumeo mpatie.*
ππππΉπ
πΉππΉππΉπ
*Autambue msuko,*
*hisia zimuandame,*
*Tena ujaze vituko,*
*midomo aiachame,*
*Tembea kwa mbinuko,*
*mwili wake ulalame.*
*Kwake hukufata kula,*
*Utulivu mumeo mpatie.*
πΉππΉππΉπ
ππΉππππΉ
*Shedo na wanja ziishe,*
*nyingine atanunua,*
*Jioni ukinukishe,*
*uzidi kumzuzua.*
*Uwanja unyamazishe,*
*kwa burudani murua,*
*Kwake hukufwata kula,*
*Utulivu mumeo mpatie.*
πΉπππππ
πΉπππΉπΉπ
*Vipedo ndani ruhusa,*
*sheria mekuachia.*
*Furahi akikugusa,*
*sinune au kulia,*
*Onesha we ni kipusa,*
*nyanza zote unajua,*
*Kwake hukufwata kula,*
*Utulivu Mumeo mpatie.*
πΉπππππ
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: