Home → simulizi
→ KURUDI KWA MOZA: 34
Rose aliongoza hadi ndani kwake na kuingia sebleni, alishangaa kumuona rafiki yake akiwa amekaa sebleni, halafu pembeni yake yupo Doto, Sara, Kulwa na Salome ila kabla hajaita hata jina moja alishangaa kuona rafiki yake akianguka chini na kuanza kujipigiza kama mtu mwenye kifafa huku mapovu yakimtoka.
Alijikuta anainama kumpa rafiki yake huduma ya kwanza huku akimuita,
“Mama Jack, jamani mama Jack”
Kile kitendo cha kumuita tu kilimfanya awe kimya gafla hata kule kujipigiza aache, kwakweli Rose alichanganyikiwa yani kama kuchanganyikiwa sasa hapa alichanganyikiwa tena sio kwa kujifanyisha ila ni kuchanganyikiwa kweli.
Alijikuta akikazana kumita ila kadri alivyomuita ndivyo alivyozidi kukauka, yani watoto wake wote walikuwa wakishangaa lile tukio huku wakitaka kwenda kumsaidia mama yao ila Salome aliwazuia,
“Muacheni”
Sara alimuangalia kwa gadhabu Salome na kumwambia,
“Hivi una nini wewe? Yani mama yetu yupo kwenye matatizo unasema muacheni, unataka tukusikilize au?”
Sara akataka kwenda, ila Salome aliwazuia na kuanza kuwaambia,
“Hivi nyie hata hamjui mtu ameanza kutapatapa sababu ya nini halafu manataka mkamsaidie, mkipata kesi ya kujibu je?”
Walitamani kwenda kumsaidia mama yao ila kuna uzito uliingia ndani kwao na kujikuta wakiishia kuongea tu bila ya kwenda kumsaidia.
Rose alilia sana huku akimuita rafiki yake, yani kwa muda huu hata hakukumbuka kama kakosea masharti au vipi maana alishachanganyikiwa kuwa rafiki yake kaanguka ndani ya nyumba yake, ila kwavile yeye alikuwa na mwili na rafiki yake alikuwa mwembamba, alijikuta akimbeba bila hata msaada wa watoto wake, alimbeba na kumtoa nje kisha akampakiza kwenye gari na yeye kupanda kwenye gari na kuondoka.
Njiani alikuwa akiendesha kwa kasi sana kwani alikuwa anamuwaisha rafiki yake kwa mganga kwani alijua akichelewa tu ataharibu kila kitu na rafiki yake anaweza akapoteza maisha kweli.
Ila leo ilimchukua muda mrefu sana kufika kwa mganga kiasi kwamba aliendesha gari hadi alichoka huku ana machungu kuhusu rafiki yake ila mara kidogo alipofika mbele ya safari yake alijikuta akishindwa kuendesha gari tena halafu akapitiwa na usingizi mzito sana.
Pale ndani walibaki watoto wa Rose wakiwa na Yule Salome huku wakimlaumu Salome kwanini kawakataza kumsaidia mama yao,
“Hivi nyie hamuwezi kujiongeza au? Mama yenu anajua kilichompata rafiki yake ndiomana kambeba hapa bila msaada wa mtu yeyote sababu anajua ni kipi kimempata nan i wapi atampeleka”
“Kwani wewe Salome kuna chochote unatambua?”
“Mngekuwa misukule leo ndio mngeniuliza kuna kuna chochote natambua, mama yenu alitaka kuwatoa kafara”
Wote wakashangaa, kuwa mama yao awatoe kafara kwa misingi ipi na kumbishia Salome kuwa mama yao hawezi kuwatoa kafara,
“Aaah ningemuacha awatoe eeh!”
“Mama anatupenda sana, hawezi kufikia hatua hiyo. Kwanza atutoe kafara kwa lipi!”
“Sasa nitamuacha awatoe kafara halafu hayo maneno yenu mkayazungumzie kuzimu huko”
“Sidhani kama umetuelewa Salome, tunauliza mama atutoe kafara kwasababu ipi!”
“Tulieni tu tena mnishukuru mie, la sivyo mngekuwa marehemu nyie. Mnafikiri Yule mama anaenda kupona? Yule ndio basi tena, mama yenu akirudi hapa muulizeni kuhusu Yule mama atawaambia”
Walikaa kimya, baada ya muda mfupi Ana nae alirudi ila leo ndio hakuongea na mtu yeyote kwani alipitiliza chumbani kwake hata ndugu zake wakamshangaa kwani walijipaga moyo kuwa Ana amebadilika ila kitendo cha kupitiliza bila kuwasalimia kiliwafanya waanze kuhisi kuwa amesharudi kwenye matendo yake.
Ana hakuwaongelesha sababu alikuwa akienda kwenye dawa zake, na aliweza kutazama na kuona mama yake alipewa masharti ya aina gani na alitaka kufanya nini na kitu gani kimetokea, Ana kwa kutumia dawa yake mara nyingine alikuwa na uwezo wa kuona matendo yaliyotokea ila tu hakuweza kuona matendo yatakayotokea, kwahiyo aliweza kuona masharti ambayo mama yake alipewa na alichokifanya hadi ameondoka.
Ana akahisi kuwa mama yake amerudi tena kwa Yule yule mganga, aliweza kuangalia njia vizuri kwa dawa zake na kuiona, kisha akabalisha nguo za shule na kuondoka tena bila ya kuongea chochote maana alitaka akakutane na mama yake na amzuie kutokwenda tena kwa Yule mganga kwamaana kunapoendelea aliona mama yao anaweza kumtoa kafara hata yeye ukizingatia anaogopa kufa.
Kwahiyo aliwaacha wote wakiwa wanamshangaa anatoka hadi anaishia zake, walimuangalia tu na hawakuelewa kuwa alikuwa anaenda wapi.
Usiku ulimkuta Ana akiwa njiani na kuamua kwenda kulala hotelini, ingawa alikuwa anajiamini sana ila hakutaka kutembea usiku ule peke yake. Alijiaminisha kuwa asubuhi ya siku hiyo angeondoka zake, pale hotelini alienda kula kwanza na kusikia watu wakipiga stori huku wakisema kuhusu wachawi,
“Yani wachawi bhana hakuna kinachowashinda, natamani kuwa mchawi”
“Mimi ningekuwa mchawi ningekuwa naingia benki kuchukua hela si mchawi bhana hawanioni”
“Mimi ningekuwa mchawi wangenikoma mtaani kwangu, yani ukiwa mchawi hakuna kitu kinachokushinda”
Ana alitabasamu na kuinuka kisha kuingia kwenye chumba alichokodi huku akijaribu kuzitafakari akili za wale watu kuwa wana akili mbovu na wanaona kuwa mchawi hakuna kinachoweza kukushinda wakati wao Salome tu anawatoa jasho. Ila kadri alivyokaa mule ndani alijisikia kwenda kuwafundisha adabu wale wote waliokuwa wanazungumzia mada za kichawi, na usiku wake alienda kuwatembelea kwa uchawi na kwa bahati mbaya alimuua mmoja wao na kurudi kwenye chumba chake huku akijiambia kuwa hakutaka kuua ila Yule mmoja kiherehere chake kimemponza ila yeye binafsi hakutaka kuua, toka muda huo hakuweza kulala hata alivyorudi kwani muda mwingine roho ya kibinadamu inamjia na anaona huruma ila muda mwingine anaona ni sawa kwa Yule mtu kufa. Kulipokucha alisikia kelele za vilio sehemu ile na kuamua kuondoka zake kwani hakutaka kusikiliza kelele za vilio vya msiba aliosababisha mwenyewe.
Kwahiyo aliendelea na safari yake ya kwenda alipoenda mama yake.
Salome alirudi nyumbani kwao siku ya leo na kumkuta mama yake na baba yake wanataka wajiandae kwenda kuwatafuta wale vijana ili wawaonyeshe ile maiti ya Ashura na waifanyie utaratibu wa maziko, aliwauliza kuwa wanajiandaa kwenda wapi,
“Mwanangu, kumbe mamako mdogo Ashura amekufa”
“Kwani nyie mmejuaje?”
Wakamshangaa vile ambavyo hajaonyesha kushtushwa hata kidogo, kisha Patrick aliamua kumueleza vile ambavyo alikutana na wale vijana na jinsi walivyomueleza na kushutumu kuwa atakuwa ni Salome ndio kahusika na kumuua Ashura, ila cha kushangaza Salome akacheka na kuwafanya waangaliane kwa zamu maana hawakumuelewa anachochekea kisha akamuuliza Patrick,
“Ni ushahidi gani wamekuonyesha kuwa Ashura amekufa?”
“Wamenionyesha picha ya maiti yake ikiwa imeharibika sana”
“Matapeli hao”
“Matapeli! Kivipi?”
“Msiwafatilie hao ni matapeli, watawatapeli na kuwafanya muumie tu. Hakuna cha mwili wa Ashura wala nini, amekufa wakati tunawasiliana nae kila siku! Achana na hao”
Kisha Salome akaenda chumbani kwake na kufanya Patrick na Neema wazidi kupatwa na maswali, ila bado hawakutaka kubadili wazo lao la kuwatafuta hao vijana ili kama ni kweli basi wamzike Ashura sehemu stahiki, kwahiyo wakaondoka hivyo hivyo.
Walifanya ile safari yao, ila wakiwa njiani wakashangaa gari yao ikisimamishwa kisha kijana mmoja wapo kati ya wale vijana ambao Patrick aliwaona jana aliwasimamisha halafu akawasalimia na kuwaambia kuwa ataenda kuwaonyesha ulipo mwili wa Ashura kwahiyo walipanda nae kwenye gari na kuanza safari ila walivyofika mbele ya safari, walishangaa wakishikwa na usingizi na kulala kwenye gari tena fofofo kamavile wapo kitandani.
Nyumbani nako ambapo walikuwepo Kulwa, Doto na Sara walikuwa wakizungumzia kuhusu tukio la jana yake, kuhusu Yule mtu ambaye alienda na Salome nyumbani kisha kurudi mama yao na Yule mtu kuanguka akitapatapa kisha mama yao kumbeba na kuondoka nae, walikuwa wakijiuliza sana kuhusu lile tukio na jinsi mdogo wao alivyorudi kutoka shuleni na kuondoka ambapo mpaka siku hiyo hakuwa amerudi nyumbani,
“Ila jamani mara nyingine kwenye hii nyumba tunafanya vitu kama tumerogwa vile, hivi kweli sisi tunalala kabisa wakati mdogo wetu hatujui alipo! Bora mama ni mtu mzima ila Ana bado mdogo sana”
“Weee Kulwa nawe umeanza kuugua kichaaa nini, si ulimuona mwenyewe akitoka hapa jana mbona hukumuuliza mdogo wangu unatoka unaenda wapi?”
“Yani wewe Sara badala umuhurumie mtoto wa kike mwenzio eti na wewe unamkandamiza na kuona ni sawa kabisa Yule mtoto kutokurudi nyumbani”
“Mimi dada ila nyie ni kaka zake, mmeshindwa kuwa na sauti kweli kwa mdogo wenu wa kike? Kumbukeni nishawahi fanywa kipofu, nishawahi fanywa bubu na huyo mnaemuita ni mtoto, Ana ni mtoto kwa nje ila ndani ni mkubwa”
“Mmmh jamani Sara, sasa unashauri nini?”
“Mimi mwenyewe roho inaniuma sana kuhusu mama na Ana, mama yetu amekuwa mtu wa kutojielewa kabisa siku hizi kwakweli roho inaniuma sana ila nashindwa cha kusema. Kuna kitu nikiwaonyesha kaka zangu na nyie pia mtashangaa sana”
“Kitu gani hicho?”
“Ndani ya nyumba hii, kuna chumba cha siri cha mama ambacho hatukijui ila cha kushangaza Salome alikijua”
Wote walishangaa kusikia habari za chumba cha siri na wakatamani kwenda kukishuhudia hiko chumba cha siri walichoambiwa.
Patrick na Neema walikuwa kwenye usingizi mzito sana, ila aliyekuwa wa kwanza kushtuka alikuwa ni Neema ambaye alimuamsha Patrick walishangaa wakiwa nyumbani tena wakiwa wamechoka sana hata vichwa vilikuwa vinawauma na kuwafanya kutokukumbuka kwa muda huo huo kuwa walikuwa wapi mara ya mwisho, muda kidogo Patrick akakumbuka tena akiwa na macho ya usingizi bado na kumwambia Neema,
“Si tulikuwa kwenye gari sisi?”
Neema nae akakumbuka vilivyo ila nay eye macho yalikuwa mazito hatari, yani yalizingirwa na usingizi,
“Ndio tulikuwa kwenye gari tunaenda kufata mwili wa Ashura. Yuko wapi Yule kijana wa kutupeleka? Halafu mbona tuko nyumbani?”
“Hata mimi sielewi kabisa, tumerudije hapa? Gari yangu imepona kweli”
Patrick akataka kuinuka ili akaangalie kama gari yake ipo lakini usingizi ukamzidia na kumfanya ashindwe hata kuinuka zaidi ya kulala vizuri, Neema nae alipomuangalia Patrick amelala akajikuta nay eye akilala usingizi wa nguvu tena usingizi wa safari hii haukuwa sawa na ule usingizi wa kwanza kwani huu ulikuwa mzito zaidi.
Kwahiyo wenyewe walilala chumbani kisha Salome akawaandalia wadogo zake chakula ambapo walikula bila kuhoji zaidi kuhusu wazazi wao, halafu akawapeleka nao kulala huku yeye akiondoka kabisa hapo nyumbani kwao.
Ana ilikuwa inamchukua mud asana kufika kwa Yule mganga sababu alitumia usafiri wa jumuiya tofauti na mama yake alitumia gari lake, Ana alikuwa anapanda kwenye gari hii na kushuka mbele sababu safari yenyewe kwa kutumia madaladala ilikuwa ni ya kuunganisha unganisha, ila Ana alikuwa akisumbuliwa sana kichwa na Yule mtu aliyemmaliza kichawi usiku uliopita, ilikuwa ni kwenye hasira tu akajikuta akimmalizia ila hakupanga kummalizia. Ila damu ya huyu mtu ilimuumiza sana kichwa Ana, ikabidi atafute mto kwanza kwahiyo alivyofika kwenye maeneo ya karibu na kwa mganga alitafuta mto kwanza na kwenda kuoga mtoni kwani yeye aliamini kuwa unapooga kuna vitu vinaondoka kwenye mawazo yako haswa kumfikiria huyo mtu ambaye alimuua bila ya hatia.
Alichukua muda mrefu sana kuoga huko mtoni kisha alipomaliza akavaa nguo zake vizuri tu, ila kuangalia pembeni akaona kitu kinang’aa sana na kuhisi kuwa huenda ikawa dhahabu na kwavile kule kulikuwa sehemu ya ndani ndani kwahiyo uwezekano wa kitu hicho kuwa dhahabu ulikuwa mkubwa sana, ingawa Ana ni mtu mwenye machale sana ila kitendo cha kuona dhahabu kilimaliza machale yake, akainama na kuiokota kisha kuiweka vizuri kwenye mifuko yake kuwa ataenda nayo kila mahali na atarudi nayo mjini kwaajili ya kuiuza, baada ya kuiweka vizuri ndipo akaendelea na safari yake ya kufika kwa mganga.
Sara aliwachukua wenzie mpaka ile sehemu aliyochukua funguo na Salome kisha kufungua hiko chumba na kuingia ndani, wote wakashangaa,
“Inamaana siku zote hizi tulikuwa hatujui kama hiki chumba kinaingilika au ni nini jamani mbona sielewi yani hatujawahi kukihisi hata mara moja!”
“Sasa nasikia kuna watu mama kawafungia kwenye hiki chumba, unaambiwa ukisukuma lile kabati utaona mlango mwingine na hapo kuna chumba kingine”
Ikabidi Kulwa asukume kabati kwani hawakutaka kuandikia mate wakati wino upo, na kweli alivyosukuma kabati aliona mlango wa chumba kingine kinachoonekana kama choo cha ndani, Kulwa alitaka kuwa shahidi bado na kukisogelea kile chumba kisha akashika ule mlango ila aliganda pale pale, akawa anajaribu kuutoa mkono wake ila haikuwezekana na mara chumba kile kikaanza kutingishika na kuwafanya wengine yaani Sara na Doto waanguke chini huku Kulwa akiwa kaganda pale pale mlangoni na mara akaanza kukauka kama anapigwa na shoti ya umeme.
Itaendelea kesho usiku…….!!!!!!
By, Atuganile Mwakalile.KURUDI KWA MOZA: 34
Rose aliongoza hadi ndani kwake na kuingia sebleni, alishangaa kumuona rafiki yake akiwa amekaa sebleni, halafu pembeni yake yupo Doto, Sara, Kulwa na Salome ila kabla hajaita hata jina moja alishangaa kuona rafiki yake akianguka chini na kuanza kujipigiza kama mtu mwenye kifafa huku mapovu yakimtoka.
Alijikuta anainama kumpa rafiki yake huduma ya kwanza huku akimuita,
“Mama Jack, jamani mama Jack”
Kile kitendo cha kumuita tu kilimfanya awe kimya gafla hata kule kujipigiza aache, kwakweli Rose alichanganyikiwa yani kama kuchanganyikiwa sasa hapa alichanganyikiwa tena sio kwa kujifanyisha ila ni kuchanganyikiwa kweli.
Alijikuta akikazana kumita ila kadri alivyomuita ndivyo alivyozidi kukauka, yani watoto wake wote walikuwa wakishangaa lile tukio huku wakitaka kwenda kumsaidia mama yao ila Salome aliwazuia,
“Muacheni”
Sara alimuangalia kwa gadhabu Salome na kumwambia,
“Hivi una nini wewe? Yani mama yetu yupo kwenye matatizo unasema muacheni, unataka tukusikilize au?”
Sara akataka kwenda, ila Salome aliwazuia na kuanza kuwaambia,
“Hivi nyie hata hamjui mtu ameanza kutapatapa sababu ya nini halafu manataka mkamsaidie, mkipata kesi ya kujibu je?”
Walitamani kwenda kumsaidia mama yao ila kuna uzito uliingia ndani kwao na kujikuta wakiishia kuongea tu bila ya kwenda kumsaidia.
Rose alilia sana huku akimuita rafiki yake, yani kwa muda huu hata hakukumbuka kama kakosea masharti au vipi maana alishachanganyikiwa kuwa rafiki yake kaanguka ndani ya nyumba yake, ila kwavile yeye alikuwa na mwili na rafiki yake alikuwa mwembamba, alijikuta akimbeba bila hata msaada wa watoto wake, alimbeba na kumtoa nje kisha akampakiza kwenye gari na yeye kupanda kwenye gari na kuondoka.
Njiani alikuwa akiendesha kwa kasi sana kwani alikuwa anamuwaisha rafiki yake kwa mganga kwani alijua akichelewa tu ataharibu kila kitu na rafiki yake anaweza akapoteza maisha kweli.
Ila leo ilimchukua muda mrefu sana kufika kwa mganga kiasi kwamba aliendesha gari hadi alichoka huku ana machungu kuhusu rafiki yake ila mara kidogo alipofika mbele ya safari yake alijikuta akishindwa kuendesha gari tena halafu akapitiwa na usingizi mzito sana.
Pale ndani walibaki watoto wa Rose wakiwa na Yule Salome huku wakimlaumu Salome kwanini kawakataza kumsaidia mama yao,
“Hivi nyie hamuwezi kujiongeza au? Mama yenu anajua kilichompata rafiki yake ndiomana kambeba hapa bila msaada wa mtu yeyote sababu anajua ni kipi kimempata nan i wapi atampeleka”
“Kwani wewe Salome kuna chochote unatambua?”
“Mngekuwa misukule leo ndio mngeniuliza kuna kuna chochote natambua, mama yenu alitaka kuwatoa kafara”
Wote wakashangaa, kuwa mama yao awatoe kafara kwa misingi ipi na kumbishia Salome kuwa mama yao hawezi kuwatoa kafara,
“Aaah ningemuacha awatoe eeh!”
“Mama anatupenda sana, hawezi kufikia hatua hiyo. Kwanza atutoe kafara kwa lipi!”
“Sasa nitamuacha awatoe kafara halafu hayo maneno yenu mkayazungumzie kuzimu huko”
“Sidhani kama umetuelewa Salome, tunauliza mama atutoe kafara kwasababu ipi!”
“Tulieni tu tena mnishukuru mie, la sivyo mngekuwa marehemu nyie. Mnafikiri Yule mama anaenda kupona? Yule ndio basi tena, mama yenu akirudi hapa muulizeni kuhusu Yule mama atawaambia”
Walikaa kimya, baada ya muda mfupi Ana nae alirudi ila leo ndio hakuongea na mtu yeyote kwani alipitiliza chumbani kwake hata ndugu zake wakamshangaa kwani walijipaga moyo kuwa Ana amebadilika ila kitendo cha kupitiliza bila kuwasalimia kiliwafanya waanze kuhisi kuwa amesharudi kwenye matendo yake.
Ana hakuwaongelesha sababu alikuwa akienda kwenye dawa zake, na aliweza kutazama na kuona mama yake alipewa masharti ya aina gani na alitaka kufanya nini na kitu gani kimetokea, Ana kwa kutumia dawa yake mara nyingine alikuwa na uwezo wa kuona matendo yaliyotokea ila tu hakuweza kuona matendo yatakayotokea, kwahiyo aliweza kuona masharti ambayo mama yake alipewa na alichokifanya hadi ameondoka.
Ana akahisi kuwa mama yake amerudi tena kwa Yule yule mganga, aliweza kuangalia njia vizuri kwa dawa zake na kuiona, kisha akabalisha nguo za shule na kuondoka tena bila ya kuongea chochote maana alitaka akakutane na mama yake na amzuie kutokwenda tena kwa Yule mganga kwamaana kunapoendelea aliona mama yao anaweza kumtoa kafara hata yeye ukizingatia anaogopa kufa.
Kwahiyo aliwaacha wote wakiwa wanamshangaa anatoka hadi anaishia zake, walimuangalia tu na hawakuelewa kuwa alikuwa anaenda wapi.
Usiku ulimkuta Ana akiwa njiani na kuamua kwenda kulala hotelini, ingawa alikuwa anajiamini sana ila hakutaka kutembea usiku ule peke yake. Alijiaminisha kuwa asubuhi ya siku hiyo angeondoka zake, pale hotelini alienda kula kwanza na kusikia watu wakipiga stori huku wakisema kuhusu wachawi,
“Yani wachawi bhana hakuna kinachowashinda, natamani kuwa mchawi”
“Mimi ningekuwa mchawi ningekuwa naingia benki kuchukua hela si mchawi bhana hawanioni”
“Mimi ningekuwa mchawi wangenikoma mtaani kwangu, yani ukiwa mchawi hakuna kitu kinachokushinda”
Ana alitabasamu na kuinuka kisha kuingia kwenye chumba alichokodi huku akijaribu kuzitafakari akili za wale watu kuwa wana akili mbovu na wanaona kuwa mchawi hakuna kinachoweza kukushinda wakati wao Salome tu anawatoa jasho. Ila kadri alivyokaa mule ndani alijisikia kwenda kuwafundisha adabu wale wote waliokuwa wanazungumzia mada za kichawi, na usiku wake alienda kuwatembelea kwa uchawi na kwa bahati mbaya alimuua mmoja wao na kurudi kwenye chumba chake huku akijiambia kuwa hakutaka kuua ila Yule mmoja kiherehere chake kimemponza ila yeye binafsi hakutaka kuua, toka muda huo hakuweza kulala hata alivyorudi kwani muda mwingine roho ya kibinadamu inamjia na anaona huruma ila muda mwingine anaona ni sawa kwa Yule mtu kufa. Kulipokucha alisikia kelele za vilio sehemu ile na kuamua kuondoka zake kwani hakutaka kusikiliza kelele za vilio vya msiba aliosababisha mwenyewe.
Kwahiyo aliendelea na safari yake ya kwenda alipoenda mama yake.
Salome alirudi nyumbani kwao siku ya leo na kumkuta mama yake na baba yake wanataka wajiandae kwenda kuwatafuta wale vijana ili wawaonyeshe ile maiti ya Ashura na waifanyie utaratibu wa maziko, aliwauliza kuwa wanajiandaa kwenda wapi,
“Mwanangu, kumbe mamako mdogo Ashura amekufa”
“Kwani nyie mmejuaje?”
Wakamshangaa vile ambavyo hajaonyesha kushtushwa hata kidogo, kisha Patrick aliamua kumueleza vile ambavyo alikutana na wale vijana na jinsi walivyomueleza na kushutumu kuwa atakuwa ni Salome ndio kahusika na kumuua Ashura, ila cha kushangaza Salome akacheka na kuwafanya waangaliane kwa zamu maana hawakumuelewa anachochekea kisha akamuuliza Patrick,
“Ni ushahidi gani wamekuonyesha kuwa Ashura amekufa?”
“Wamenionyesha picha ya maiti yake ikiwa imeharibika sana”
“Matapeli hao”
“Matapeli! Kivipi?”
“Msiwafatilie hao ni matapeli, watawatapeli na kuwafanya muumie tu. Hakuna cha mwili wa Ashura wala nini, amekufa wakati tunawasiliana nae kila siku! Achana na hao”
Kisha Salome akaenda chumbani kwake na kufanya Patrick na Neema wazidi kupatwa na maswali, ila bado hawakutaka kubadili wazo lao la kuwatafuta hao vijana ili kama ni kweli basi wamzike Ashura sehemu stahiki, kwahiyo wakaondoka hivyo hivyo.
Walifanya ile safari yao, ila wakiwa njiani wakashangaa gari yao ikisimamishwa kisha kijana mmoja wapo kati ya wale vijana ambao Patrick aliwaona jana aliwasimamisha halafu akawasalimia na kuwaambia kuwa ataenda kuwaonyesha ulipo mwili wa Ashura kwahiyo walipanda nae kwenye gari na kuanza safari ila walivyofika mbele ya safari, walishangaa wakishikwa na usingizi na kulala kwenye gari tena fofofo kamavile wapo kitandani.
Nyumbani nako ambapo walikuwepo Kulwa, Doto na Sara walikuwa wakizungumzia kuhusu tukio la jana yake, kuhusu Yule mtu ambaye alienda na Salome nyumbani kisha kurudi mama yao na Yule mtu kuanguka akitapatapa kisha mama yao kumbeba na kuondoka nae, walikuwa wakijiuliza sana kuhusu lile tukio na jinsi mdogo wao alivyorudi kutoka shuleni na kuondoka ambapo mpaka siku hiyo hakuwa amerudi nyumbani,
“Ila jamani mara nyingine kwenye hii nyumba tunafanya vitu kama tumerogwa vile, hivi kweli sisi tunalala kabisa wakati mdogo wetu hatujui alipo! Bora mama ni mtu mzima ila Ana bado mdogo sana”
“Weee Kulwa nawe umeanza kuugua kichaaa nini, si ulimuona mwenyewe akitoka hapa jana mbona hukumuuliza mdogo wangu unatoka unaenda wapi?”
“Yani wewe Sara badala umuhurumie mtoto wa kike mwenzio eti na wewe unamkandamiza na kuona ni sawa kabisa Yule mtoto kutokurudi nyumbani”
“Mimi dada ila nyie ni kaka zake, mmeshindwa kuwa na sauti kweli kwa mdogo wenu wa kike? Kumbukeni nishawahi fanywa kipofu, nishawahi fanywa bubu na huyo mnaemuita ni mtoto, Ana ni mtoto kwa nje ila ndani ni mkubwa”
“Mmmh jamani Sara, sasa unashauri nini?”
“Mimi mwenyewe roho inaniuma sana kuhusu mama na Ana, mama yetu amekuwa mtu wa kutojielewa kabisa siku hizi kwakweli roho inaniuma sana ila nashindwa cha kusema. Kuna kitu nikiwaonyesha kaka zangu na nyie pia mtashangaa sana”
“Kitu gani hicho?”
“Ndani ya nyumba hii, kuna chumba cha siri cha mama ambacho hatukijui ila cha kushangaza Salome alikijua”
Wote walishangaa kusikia habari za chumba cha siri na wakatamani kwenda kukishuhudia hiko chumba cha siri walichoambiwa.
Patrick na Neema walikuwa kwenye usingizi mzito sana, ila aliyekuwa wa kwanza kushtuka alikuwa ni Neema ambaye alimuamsha Patrick walishangaa wakiwa nyumbani tena wakiwa wamechoka sana hata vichwa vilikuwa vinawauma na kuwafanya kutokukumbuka kwa muda huo huo kuwa walikuwa wapi mara ya mwisho, muda kidogo Patrick akakumbuka tena akiwa na macho ya usingizi bado na kumwambia Neema,
“Si tulikuwa kwenye gari sisi?”
Neema nae akakumbuka vilivyo ila nay eye macho yalikuwa mazito hatari, yani yalizingirwa na usingizi,
“Ndio tulikuwa kwenye gari tunaenda kufata mwili wa Ashura. Yuko wapi Yule kijana wa kutupeleka? Halafu mbona tuko nyumbani?”
“Hata mimi sielewi kabisa, tumerudije hapa? Gari yangu imepona kweli”
Patrick akataka kuinuka ili akaangalie kama gari yake ipo lakini usingizi ukamzidia na kumfanya ashindwe hata kuinuka zaidi ya kulala vizuri, Neema nae alipomuangalia Patrick amelala akajikuta nay eye akilala usingizi wa nguvu tena usingizi wa safari hii haukuwa sawa na ule usingizi wa kwanza kwani huu ulikuwa mzito zaidi.
Kwahiyo wenyewe walilala chumbani kisha Salome akawaandalia wadogo zake chakula ambapo walikula bila kuhoji zaidi kuhusu wazazi wao, halafu akawapeleka nao kulala huku yeye akiondoka kabisa hapo nyumbani kwao.
Ana ilikuwa inamchukua mud asana kufika kwa Yule mganga sababu alitumia usafiri wa jumuiya tofauti na mama yake alitumia gari lake, Ana alikuwa anapanda kwenye gari hii na kushuka mbele sababu safari yenyewe kwa kutumia madaladala ilikuwa ni ya kuunganisha unganisha, ila Ana alikuwa akisumbuliwa sana kichwa na Yule mtu aliyemmaliza kichawi usiku uliopita, ilikuwa ni kwenye hasira tu akajikuta akimmalizia ila hakupanga kummalizia. Ila damu ya huyu mtu ilimuumiza sana kichwa Ana, ikabidi atafute mto kwanza kwahiyo alivyofika kwenye maeneo ya karibu na kwa mganga alitafuta mto kwanza na kwenda kuoga mtoni kwani yeye aliamini kuwa unapooga kuna vitu vinaondoka kwenye mawazo yako haswa kumfikiria huyo mtu ambaye alimuua bila ya hatia.
Alichukua muda mrefu sana kuoga huko mtoni kisha alipomaliza akavaa nguo zake vizuri tu, ila kuangalia pembeni akaona kitu kinang’aa sana na kuhisi kuwa huenda ikawa dhahabu na kwavile kule kulikuwa sehemu ya ndani ndani kwahiyo uwezekano wa kitu hicho kuwa dhahabu ulikuwa mkubwa sana, ingawa Ana ni mtu mwenye machale sana ila kitendo cha kuona dhahabu kilimaliza machale yake, akainama na kuiokota kisha kuiweka vizuri kwenye mifuko yake kuwa ataenda nayo kila mahali na atarudi nayo mjini kwaajili ya kuiuza, baada ya kuiweka vizuri ndipo akaendelea na safari yake ya kufika kwa mganga.
Sara aliwachukua wenzie mpaka ile sehemu aliyochukua funguo na Salome kisha kufungua hiko chumba na kuingia ndani, wote wakashangaa,
“Inamaana siku zote hizi tulikuwa hatujui kama hiki chumba kinaingilika au ni nini jamani mbona sielewi yani hatujawahi kukihisi hata mara moja!”
“Sasa nasikia kuna watu mama kawafungia kwenye hiki chumba, unaambiwa ukisukuma lile kabati utaona mlango mwingine na hapo kuna chumba kingine”
Ikabidi Kulwa asukume kabati kwani hawakutaka kuandikia mate wakati wino upo, na kweli alivyosukuma kabati aliona mlango wa chumba kingine kinachoonekana kama choo cha ndani, Kulwa alitaka kuwa shahidi bado na kukisogelea kile chumba kisha akashika ule mlango ila aliganda pale pale, akawa anajaribu kuutoa mkono wake ila haikuwezekana na mara chumba kile kikaanza kutingishika na kuwafanya wengine yaani Sara na Doto waanguke chini huku Kulwa akiwa kaganda pale pale mlangoni na mara akaanza kukauka kama anapigwa na shoti ya umeme.
Itaendelea kesho usiku…….!!!!!!
By, Atuganile Mwakalile.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: