Home → simulizi
→ KURUDI KWA MOZA: 26
Basi wakashuka kwenye gari na kwenda kufungua mlango wa sebleni ili waingie nani, ila walipofungua tu walishangaa kujikuta wapo kibandani kule kule kwa mganga walipotoka.
Yani kila mmoja alimuangalia mwenzie kwa mshangao, tena Rose akawa wa kwanza kumuuliza mganga,
“Mbona tumerudi tena huku huku wakati tulishafika mpaka nyumbani?”
“Hata mimi mwenyewe sielewi imekuwaje, ila ngoja nifanye dawa zangu kwanza. Naomba nisubiri nje”
Rose alitoka nje ya kibanda cha mganga huku akiangalia huku na kule, kwani mazingira ni hay ohayo na waliondoka kabisa hadi akakumbuka kuwa alimuonyesha mganga mlinzi na wakaongea halafu wameruishwa tena kule kule, kwakweli ilikuwa ngumu sana kwa Rose kuelewa.
“Kama ni uchawi basi huu ni wa viwango vingine, inamaana ni Moza au Salome! Yule mtoto atapata wapi nguvu za hivi? Anapata wapi uwezo wa kufanya makubwa haya? Ila sidhani kama ni yeye, ila na huyo Moza kwa staili hii ya kurudishwa na mganga tutaweza kupambana nae kweli? Kuna uwezekano wa kupambana na huyu kiumbe kweli?”
Alijiuliza sana huku akingoja mganga wake afanye dawa, na baada ya muda mganga alimuita tena Rose na kuanza kuongea nae,
“Unajua nguvu aliyokuwa nayo Yule binti nyumbani kwako ni kubwa mno, yani kiasi kwamba tunaweza siku nzima ya leo hadi usiku wa manane tukawa tunaenda kwako na kurudishwa hapa hapa”
“Sasa tutafanyaje?”
“Inabidi tutoe kafara”
“Kafara ipi?”
“Kafara ya damu, damu ya mtu unayempenda”
“Mmmh labda Patrick”
“Huyo ndio umpendae?”
“Ndio”
“Si kweli, mtu umpendae huwezi kukubali kwa haraka haraka hivyo atolewe kafara, huyo humpendi”
“Ya watoto wangu hapana, nimefikia hatua hii sababu yao. Nawapenda sana wanangu, tafadhari kafara isiwe ya wanangu, bora Patrick nipo tayari kumtoa”
“Upo tayari, ila kumtoa huyo mtu ni ngumu sana”
“Kwanini ni ngumu?”
“Huyo mtu analindwa sana, naona amezingirwa na ulinzi wa hali ya juu. Kumtoa kafara haiwezekani”
“Basi nimtoe mlinzi wangu”
“Hausiani na wewe huyo, bora siku ile ungekuwa umefanikisha zoezi la kulala nae ningekuruhusu kumtoa ila kwasasa haiwezekani. Inatakiwa ni mwanao tu”
“Tafadhari mganga bora tutafute mbinu nyingine, wanangu ndio maisha yangu. Tafadhari nisiwatoe kafara wanangu, nawapenda sana. Sijaweza kujiunga makundi ya wachawi wazoefu sababu ya kuogopa kutolewa wanangu, nawapenda sana”
“Unawapenda wanao ila unaishi na hatari ndani ya nyumba yako”
“Tujaribu tena kwenda mganga”
“Hata tukijaribu ni kazi bure, tutarudishwa tena hapa hapa, labda uende kwanza wewe halafu mie nije leo leo au hata kesho”
“Leo leo mganga, pale kwangu hapalaliki mganga, njoo leo leo”
“Ila ngoja nikupe onyo kabla hujaondoka”
“Onyo gani?”
“Msifanye sherehe yoyote pale kwako mpaka nije kufanya dawa, yani msifanye tukio lolote la sherehe sijui ya kuzaliwa, sijui kipaimara msifanye”
“Sinaga tabia ya kufanya sherehe nyumbani kwangu, hata birthday za wanangu huwa nikiamua basi naenda nao hotelini ila huwa hatufanyi sherehe nyumbani”
“Sawa sawa, nimekutahadhalisha kabisa kwani pale kwako hapatakiwi kusikika vigelegele vya shangwe kwa kipindi hiki mpaka nitakapofika na kufanya dawa, kuna nguvu kubwa sana pale kwenye nyumba yako”
“Nimekuelewa ila naomba ufike mapema iwezekanavyo”
“Usijali kwa hilo, ngoja tu nifanye dawa kwanza”
Bas Rose akamuachia mganga nauli ya kutosha kisha yeye akaanza safari ya kurudi nyumbani kwake kwa mara nyingine.
Rose alifika kwake wakati usiku ulikuwa umeshaingia hadi akajishangaa kuwa ametumiaje muda hadi usiku umeingia vile, aliangalia saa yake aliona ni saa tatu ya usiku. Aliingia ndani na kukuta familia yake yote ikiwepo sebleni, halafu wakionekana kama walikuwa wanamngoja kwa shauku kwani alipoingia tu, wote wakapiga kelele,
“Surprise”
Rose akawashangaa sana kuwa ni surprise ya kitu gani, ila wote walianza kumuimba mama yao,
“Happy birthday to you, happy birthday to you, happy birthday dear mommy, happy birthday to you”
Na vigelegele vikasikika, yani Rose alichoka kabisa na kukaa chini kwani aliona wanae wakiharibu kila kitu. Alipokaa chini walidhani mama yao amevutiwa na walichokuwa wanafanya basi wakamuagiza Ana alete keki ambapo Ana alileta keki na kuanza kuimba,
“Kata keki tule……”
Ila mama yao alitahamaki sana na kusema,
“Hadi wewe Ana!”
Akaanguka chini na kuzimia kidogo, wote wakashtuka
“Jamani surprise gani hii kwa mama yetu mpaka amezimia!”
Wakaanza kumpepea, ila Salome akaenda kuchukua maji kidogo na kuja kumwagia kwahiyo Rose akazinduka na alivyozinduka tu watoto wake wakapiga kelele za shangwe kisha Sara akaanza kumwambia mama yao,
“Mama jamani usistaajabu kiasi hiko, watoto wako tunakupenda na hatujawahi kukufanyia kitu cha namna hii hata mara moja. Nashukurun leo Salome katukumbusha kitu hiki, kumbe alikuwa ananikataza kutoka sababu leo ni siku yako ya kuzaliwa. Natumai mama yetu umefurahi! Tumeandaa keki na vyakula tofauti tofauti vya kujipongeza kama familia”
“Naomba niacheni kidogo niende chumbani”
Kisha Rose akainukana kwenda chumbani kwake,watoto wake wakashangaa sana kwani mama yao hakuonyesha kufurahia lile jambo hata kidogo, na keki yao hakukata wala nini.
“Jamani, mama tumemfanyia kitu kikubwa hivi ila haonyeshi kufurahishwa nacho kabisa. Hebu Ana kaongee na mama”
Ana akaondoka na kuwaacha pale sebleni wakijadiliana kwanini mama yao hajapendezwa na kile kitu walichomfanyia, ila Salome akawapooza,
“Mnajua mambo ya kumshtukiza mtu huwa yanachanganya sana, itakuwa leo hakujipanga kabisa kuhusu sherehe labda ndiomana amestaajabu sana ila natumai kafurahia”
“Natumai pia kafurahia”
Kuhusu swala la kuandaa sherehe fupi ya kuzaliwa kwa Rose ni Salome aliipanga na wote walimsifia kwani hawakuwahi kumfanyia mama yao sherehe.
Ana alimfata mama yake chumbani na kuanza kuzungumza nae, alimuuliza mama yake kwanini hajafurahishwa na ile surprise yao,
“Ana nilikuwa nakuamini sana, sikutegemea kama na wewe ungeweza kuingia kwenye mtego kiasi hiko jamani! Toka lini birthday yangu ikawa mwezi huu? Hivi kwanini kupena kuharibiana dawa? Nani ametoa wazo hilo?”
“Mama, mimi sijui. Kama kawaida nimerui kutoka shule na kuwakuta hapa nyumbani wamejipanga vilivyo kuwa kuna sherehe ya kuzaliwa wewe, mwanzoni nilibisha ila Sara alileta vitambulisho vyako na vilionyesha tarehe ya leo na mwezi wa leo, kwakweli hata mimi niliona ni wazo jema kukufanyia wewe sherehe ukizingatia hatujawahi kukufanyia hivyo. Siku zote huwa sishirikiani nao ila leo niliona ni jambo jema”
“Ana mwanangu, ni mtego huo unajua umeharibu dawa zangu na hivyo vigeregere vyenu! Yani mganga amenisisitiza sana kutofanya sherehe ya aina yoyote ile na kutokupiga vigeregere ila nimerudi nyumbani ndio kilichotokea”
Rose alianza kumueleza Ana kuhusu siku hiyo na jinsi walivyofika hadi hapo nyumbani na kurudishwa tena kwenye kibanda cha mganga, hadi mua huo kuamua kuja mwenyewe.
“Mama, kwamaana hiyo huyu Salome ni mchawi eeh!”
“Angekuwa mchawi tungemtambua, ni zaiddi ya mchawi halafu mganga amesema kuwa Salome ana nguvu nyingi sana, ambapo amejaribu kuziangalia ila hajaweza kuzichanganua”
“Mmmh sasa mama tutafanyaje?”
“Hata sijui maana masharti nishayaharibu tena, hapa hata sielewi nianzie wapi na niishie wapi”
“Ngoja nikatafakari mama”
Ana alitoka mule chumbani kwa mama yake na kwenda chumbani kwake kutafakari ambapo alijaribu kufanya dawa zake halafu kitu kikamuonyesha kuwa kama hawatokata ile keki waliyomuandalia mama yao basi wanaweza kidogo wakapona kwenye mtego, kwahiyo akainuka ili aende akaitupe ile keki, kufika sebleni alishangaa kuona dada yake Sara na wale mapacha walishaikata ile keki kitambo na walikuwa wanakula huku wakimuita walipomuona,
“Ana, keki tamu hiyo yani tamu sana”
“Sasa kwanini mmekata kabla mama mwenyewe hajakata? Nani katoa wazo la kuikata kabla ya muhusika kuja?”
“Salome katushauri tukate labda mama amechoka sana, ndiomana tumeamua kuikata na jinsi ilivyokuwa inatamanisha ndio kabisa yani”
Ana alisikitika sana kwani ndugu zake ndio wamekuwa rahisi kabisa kutekwa akili zao tofauti na mtu mwingine.
Akaamua kuichukua ile iliyobaki na kuibwaga chini, ila kabla haijafika chini alishangaa kuiona bado ikiwa kwenye sahani yake, kitendo hiko kilimchanganya sana ingawa ndugu zake walihisi kama Ana amewafanyia mazingaombwe hapo maana walishamjua kwa uchawi, ila hawakujua kama kitendo hiki kilimshangaza sana Ana na akajikuta akikimbilia chumbani kwa mama yake na kumueleza kuhusu dawa aliyokuwa akifanya na jinsi alivyopata ushauri wa kuhusu keki, na alichokiona sebleni.
“Mama, sasa nimeanza kuelewa kuwa ilikuwaje mkajikuta mnarudishwa kwa mganga wakati mlifika hapa nyumbani. Yani ile keki niliona kabisa nimeibwaga chini ila mara gafla naiona tena kwenye sahani, hapa naelewa kabisa kuwa inawezekana leo sio siku yako ya kuzaliwa ila hizi tarehe zimechanganywa changanywa ndani kwetu. Hivi mama hakuna kingine cha kufanya kweli kudhibiti hili maana naona mbona kama hao waganga wako wanashindwa”
“Hapana mwanangu, basi leo tulale wote tufanye vitu wenyewe tuone inakuwaje kuwaje”
“Mmmh mama sijawahi kufikiria kama kuna kiumbe kitakuja kunisumbua sumbua mimi”
“Usijali mwanangu, cha kuhakikisha ni kuwa kila mmoja akalale chumbani kwake halafu mimi na wewe tulale pamoja tushughulike na majanga ya humu ndani”
“Usijali juu ya hilo, yani wale wakimaliza tu kula najua kila mmoja ataena kulala chumbani kwake”
Basi Ana na mama yake wakakubaliana siku hiyo walale pamoja, kisha Ana akaenda chumbani kwake kujipanga kwaajili ya mashambulizi ya usiku huo.
Pale sebleni wale mapacha na Sara, walikula ile keki, walikula chakula na kunywa kwa furaha sana yani siku hiyo walikuwa kama watu waliolewa vile. Kisha walienda kukaa kwenye kochi na kuendelea na maongezi, ilikuwa ni mara ya kwanza kwa wao kufanya maongezi usiku huo sebleni maana muda kama huo kila mmoja kati yao huwa chumbani kwake anajiandaa na kulala ila siku hiyo walikuwa sebleni wakipiga stori, Salome nae alikuwepo sebleni ila alikuwa kimya kabisa kamavile hayupo.
Muda kidogo, wote pale sebleni walipitiwa na usingizi na wakalala pale pale kwenye makochi. Ana alikuja kuwaangalia kama washaondoka, alishangaa sana kuwaona bado wapo sebleni na ubaya wamelala kabisa, Ana aliwashangaa na kumsogelea Sara kisha kuanza kumtikisa,
“Sara, Sara”
“Niache bhana nina usingizi”
“Inuka ukalale ndani”
“Niache bhana”
Alienda kuwatingizha nao kaka zake walimjibu vile vile ila aliposogea ili amtingishe Salome alijikuta mkono wake ukishindwa kumshika Salome, kisha akainuka na kwenda kumwambia mama yake,
“Mwanangu hakuna namna hapo, ila Yule mganga nitaongea nae aje tu hivyo hivyo maana kila tunachokifanya hatuwezi”
“Sawa basi mama tusubiri usiku wa saa nane kasoro ndio mzuri ili na sisi tujaribu ya kwetu”
“Sawa mwanangu”
Walikazana kufanya mambo mengine huku wakisubiria usiku wa saa nane kasoro ufike, ila kila walipoangalia saa iliwaonyesha kuwa ni saa sita yani kila walipoangalia iliwaonyesha ni saa sita. Kuja kutahamaki walisikia jogoo akiwika na walipoangalia saa muda huo ilionyesha ni saa kumi na moja alfajiri,
“Mama tumepitiliza wapi?”
“Kivipi? Muda si bado haujafika”
Ana akamuonyesha saa mama yake, ambaye alishangaa pia kwahiyo siku hiyo wamefanya mkesha usiokuwa na faida yoyote ile. Ila mama yake akamuahidi Ana kuwa siku hiyo watahakikisha kila kitu kitafanikiwa,
“Asubuhi ya leo naenda kuongea na dereva tax amlete Yule mganga hapa kwa gharama zangu, najua akiletwa na mtu mwingine haitotokea zengwe kabisa. Atafika na mambo haya yatafika mwisho”
“Itakuwa vizuri mama, kwahiyo leo nisiende shule eeh!”
“Ndio usiende shule”
Rose alikubaliana pale na mwanae Ana jinsi atakavyofanya siku hiyo.
Kulipokucha kabisa, pale sebleni kila mmoja aliamka na kujinyoosha huku wakiwa na uchovu wa hali ya juu na kila mmoja kusema kuwa hatotoka kwa siku hiyo, watabaki tu nyumbani. Pacha mmoja alimwambia dada yake,
“Leo nitamwita na wifi yako aje umfahamu”
“Sawa ila mama asijue kama ni wifi”
“Mama atajulia wapi? Hakuna kumwambia, atajua siku ya ndoa”
Wakawa wanacheka pale, mama yao nae alitoka sebleni wakamsalimia akaitikia na kutaka kwenda nje. Ila Salome alimuuliza,
“Mama, unataka kwenda wapi?”
“Safari zangu hazikuhusu”
Rose akataka kufungua mlango, ila kabla hajafungua Salome alimwambia,
“Usihangaike, mgeni wako nimekuletea”
Kisha Salome ndio akaenda kufungua mlango na mara akaingia Yule mganga.
Itaendelea Jumatatu usiku…..!!!!!
By, Atuganile Mwakalile.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: