Home → simulizi
→ KURUDI KWA MOZA: 22
Rose alijua Salome ataanguka chini ila ilikuwa kinyume maana Salome hakuanguka chini, Rose akamsukuma tena ila Salome alisimama kamavile mlingoti. Muda huu Rose alipotaka kumsukuma tena Salome alishangaa mkono wake ukianza kutetemeka. Kila mmoja ndani ya nyumba yake alimshuhudia Rose akitetemeka mkono, Ana akainuka kwani aliona mama yake asije akaumbuka yeye kisha Ana akamsukuma yeye Salome ila kwake ndio ikawa kinyume kabisa kwani mkono wake uliganda kwenye mwili wa Salome, kila mmoja alikuwa akishangaa na kati ya wale mapacha na Sara hakuna aliyeweza kuongea neno lolote.
Mara Salome alianza kuelekea vyumbani ila Ana ambaye mkono wake uliganda kwa Salome alikuwa akimfata nyuma, halafu Rose naye ambaye mkono wake ulikuwa ukitetemeka alikuwa akimfata nyuma pia, kitendo hiko kiliwafanya wale mapacha na Sara wafate nyuma kwani walitaka kujua ni nini kinaendelea au ni kitu gani huyo Salome anataka kufanya.
Salome aliongoza moja kwa moja mpaka chumbani kwa Rose na kufungua mlango, kila mmoja alikuwa akimfata nyuma huku wengine hawaelewi elewi, alikutwa Patrick akiwa amelala chini sakafuni, Salome akamuangalia Rose na kumuamuru,
“Muamshe”
Rose akiwa anatetemeka, alisogea kwa Patrick na kujaribu kumuamsha. Alimuamsha kwa muda akashindwa, akainua kichwa chake na kumtazama Salome kwa uoga kisha akamwambia,
“Nakuomba basi wanangu watoke humu chumbani nimuamshe”
“Unashindwa nini kumuamsha hivyo hivyo?”
“Tafadhali usinidhalilishe, nakuomba watoke kwanza ndio nimuamshe. Nipeni dakika chache tu nitakuwa nimemuamsha”
Salome akatoka nje na wengine wote walimfata nyuma hadi sebleni kwahiyo walimuacha mama yao akiwa chumbani na Patrick.
Kila mmoja alikuwa akimshangaa tu Salome na wala Ana hakuweza kuutoa mkono wake kwenye mwili wa Salome maana uligandia alipotaka kumsukuma, kwahiyo walikuwa wamesimama tu na hakuna yeyote aliyethubutu kukaa wala kusema neno lolote kwa wakati ule kwani wote walijikuta wakimtazama tu Salome.
Baada ya muda kidogo, mama yao alirudi na Patrick sebleni na muda huu hata Ana akaweza kuutoa mwili wake kwenye mwili wa Salome, basi Salome alienda kumfata Patrick na kumkalisha kwenye kiti kisha akapitisha mkono wake machoni pake na kusema,
“Nataka uone yote na zaidi ya yote amabayo mkeo amekuwa akikutendea kwa miaka yote hii”
Ikawa kama akili ya Patrick imefunguka kiasi hivi kwani alianza kujishangaa na kuhoji kuwa yuko wapi,
“Nikowapi hapa?”
Ni Salome pekee aliyekuwa na ujasiri wa kumjibu,
“Unatakiwa kutulia kwanza maana ndio umetoka kifungoni ni ngumu kujua kwa mara moja ulipo. Tulia kwanza tuliza akili halafu utajua ulipo na kila kitu ingawa kuna baadhi ya vitu utavitambua badae sana”
Patrick alikaa kimya kwani alikuwa kama haelewi elewi vile.
Walitamani kumuhoji Salome lakini hakuna aliyekuwa na ujasiri wa kufanya hivyo, kisha Salome akainuka na kwenda zake ndani kisha akawaacha wote pale sebleni. Yani kama kuna siku ambayo Rose aliwaonea wanae aibu basi ilikuwa ni siku ya leo maana nae hakuweza tena kukaa pale sebleni bali aliondoka na kwenda chumbani kisha Ana nae akafata na kwenda chumbani kwake. Kwahiyo sebleni walibaki wale mapacha, Sara na Patrick. Muda kidogo Patrick alimuangalia Sara na kumuomba jambo,
“Naomba kaniletee simu yangu na funguo za gari chumbani”
Sara hakubisha wala nini, alifanya hivyo na kwenda chumbani kwa mama yake ambapo aligonga na mama yake alimkaribisha kwani alijua ni Ana, akashangaa kumuona ni Sara. Akamuuliza kwa mshangao,
“Vipi tena?”
“Baba kanituma funguo za gari na simu yake”
“Chukua hivyo hapo mezani mpelekee”
Yani siku ya leo hata kuhoji hakuhoji zaidi ya kusema funguo zilipo na simu ya mumewe, simu ambayo mume wake ana kitambo sana hajaishika wala kuwasiliana na watu. Sara alichukua na kwenda kumpelekea baba yake huyo wa kambo. Alipompa tu Patrick alitoka nje na kuondoka zake, tena hakuna aliyemuaga kuwa anaenda wapi.
Wale mapacha waliangaliana na dada yao Sara, halafu Sara akawaambia,
“Yani kwa matukio haya naogopa hata kulala peke yangu”
“Sasa utalala na nani?”
“Sijui yani”
“Basi kalale na Ana au Salome”
“Mmmh hao watu ni bora uniambie nikalale getini na mlinzi, nawaogopa hao watu kama kitu gani”
Mara Salome akatokea, Sara akajikuta tu akimwambia
“Baba kaondoka tena bila kuaga, halafu leo kachukua na simu yake”
“Ungekuwa ni wewe ungeweza kuaga?”
“Kivipi?”
“Unajifanya hujui ambayo baba yangu alikuwa akitendewa kwenye nyumba hii? Sasa anatambua kila kitu, maswala ya kumfanya mwenzenu kama ndondocha mwisho”
Sara aliwaangalia wenzie, halafu Salome alitoka nje kabisa na alionekana akielekea getini ambako alitoka na kuondoka.
Sara aliwauliza wenzie,
“Jamani mnamuelewa huyu mtoto?”
“Simuelewi na sitaki kuongea sana”
“Hata mimi pia simuelewi na naogopa kuongea sana”
Kisha wale mapacha wakaondoka zao na Sara akaondoka zake.
Rose alipoona mwanae Ana hajaenda chumbani kwake ikabidi yeye mwenyewe ndio aende chumbani kwa Ana, aliingia na kumuuliza mwanae,
“Hivi wewe umeweza kumuelewa huyu Salome?”
“Mama naomba tuzungumze usiku kwenye muda wetu sio muda huu”
“Hata tukisema tuzungumze usiku hatatusikia kweli?”
“Mama, mimi ndio nimekwambia na bado natafakari maana sipo sawa kabisa. Amewezaje Yule kugandisha mkono wangu mama? Yule msichana ana majini sio bure”
“Ndiomana nakwambia tujadili sasa hivi, unajua ile majuzi nilienda kwa mganga mwingine halafu ndani kwa mganga nilimkuta Moza”
“Moza!”
“Ndio nilimkuta Moza”
“Si amekufa huyo mama”
“Mwanangu hatuna uhakika na kifo cha Moza, kumbuka maiti yake ilitoweka kaburini”
“Ndio ilitoweka ila nikajua utafanya jambo, na imekuwaje hadi Moza awe hajafa kweli?”
“Sijui mwanangu, ila kama ile dawa iliyomuua Moza ilichomwa moto basi tumeisha”
“Unamaana gani mama?”
“Ile dawa mwanangu nilipewa na ilikuwa hairuhusiwi kuonekana na mtu yeyote halafu sitakiwi kuiweka mbali na nyumba yangu ndiomana nikaifukia kwenye ua ili nijue ni ua gani nimeifukia. Ni ya muda mrefu sana ile dawa na ilikuwa hairuhusiwi kuonekana na mtu yeyote wala kuungua na moto ndiomana hata kuunguza mboga humu kwenye nyumba yangu huwa sitaki. Sasa kama imechomwa moto sijui itakuwaje, ndiomana tulitakiwa kumzika nayo Moza”
“Sasa mama kama imechomwa moto imechomwa na nani wakati Moza alikuwa amekufa nayo mkononi”
“Kwamaana hiyo inawezekana ipo mahali eeh! Lakini mbona tuliitafuta bila kuiona popote”
“Mi nadhani mama tufanyie usafi kile chumba cha Moza tuitafute kabla hayajawa majanga”
“Sasa lile shetani linalolala kwenye chumba kile tutalifanya nini?”
“Yani huyo mtu ananiumiza kichwa balaa, ila mama na wewe kwanini dawa ya maana hivyo ukaenda kuifukia kwenye ua? Mbona mimi dawa yangu ile ipo chini ya godoro”
“Ni masharti ya ile dawa, kwanza haikutakiwa kuwekwa ndani ya nyumba ila inatakiwa iwe karibu na nyumba halafu haitakiwi mtu aione.”
“Basi mama nitatumia dawa yangu kufanya kitu ili tuweze kupekua kile chumba cha Moza”
“Sawa mwanangu, ndiomana nilikuwa nakufata tujadili. Sasa wewe unataka tufanye kwenye muda wetu, unadhani mambo yalivyotinga hivi tutakumbuka kujadiliana kweli! Ni ngumu mwanangu”
“Kweli mama ila chanzo cha mambo yote haya ni mwanao Sara, yani simpendi Yule mdada simpendi kabisa”
“Kweli mwanangu ni chanzo cha yote lakini ni mwanangu, kumbuka hilo. Yule ni dada yako mpende tu”
Rose akajiribu pale kumshawishi mwanae ili ajende upendo kwa ndugu yake maana alikuwa anapenda watoto wake wapendane.
Salome alienda nyumbani kwa mama yake na kumkuta kama kawaida akiwa na wale wadogo zake John na Joseph. Aliwasalimia kisha mama yake akamuomba chumbani kwake ili wakazungumze
“Kwanza imefurahi umerudi nyumbani maana mambo yako siku hizi siyaelewi kabisa. Halafu ngoja nikuulize, hivi una simu”
Salome akacheka,
“Sio unacheka Salome, nijibu una simu?”
“Ndio nina simu”
“Umeitoa wapi?”
“Baba yangu kaninunulia ili niweze kuongea nae”
“Haya, wadogo zako wameniambia Ashura hakuja huku kwenye nyumba mpya, halafu wewe na Ashura kuna mchezo mlikuwa mnacheza kisha Ashura akaanguka. Unajua sijaelewa naomba nieleweshe maana huyo Ashura hata nikimpigia simu zangu hapokei zaidi ya kunitumia ujumbe tu”
“Hivi hat nikikueleza unaweza ukanielewa!”
“Nieleze tu, kwanini nisikuelewe?”
“Acha tu ufahamu unavyofahamu, Yule Ashura si ndugu yako? Uliza kwa ndugu zenu alipo”
“Hivi wewe mtoto unaongelea nini mbona sikuelewi?”
“Huyo mamdogo Ashura yupo kwenye kijiji cha baba yenu amesema anaenda kuangalia kaburi la baba yenu kwahiyo ungeenda na wewe kijijini ili uulize vizuri kuhusu Ashura”
“Tutaenda na wewe?”
“Hapana, mimi nitabaki ila utaenda na wadogo zangu. Mimi nabaki na baba yangu.”
“Haya nitafikiria kwenda”
Salome akainuka, na kumfanya Neema amuulize tena,
“Sasa mbona unaondoka kabla hata sijamaliza maongezi na wewe”
“Subiri nakuja sasa hivi”
Salome aliondoka zake, Neema nae alitoka ila kiukweli hakumuelewa kabisa mwanae na mambo aliyokuwa anayafanya.
Alipokaa muda kidogo mwanae alirudi kisha akampa mama yake tiketi,
“Nimeshakukatia tiketi, wewe na wadogo zangu ya kwenda kutembelea kaburi la babu”
“Kheee kwahiyo ndio unataka tusafiri!”
“Ndio, si mnaenda kukaa wiki tu mnarudi”
“Kwahiyo tiketi umekata ya kuondoka lini?”
“Kuondoka kesho”
“Kheee Salome hebu acha masikhara, tutaondokaje kesho wakati hatujajipanga!”
“Unataka mjipangaje?”
“Sijapanga nguo za watoto, sijawanunulia mama zangu vitenge”
“Ni hayo tu au kuna mengine?”
“Ni hayo ndio”
“Basi nitakusaidia, yani wewe tulia tu nitakusaidia kupanga ila tiketi ni ya kesho”
Neema alimshangaa sana Salome kuwa mtoto wake amebadilika sana na amekuwa na maamuzi ya haraka haraka, akawa anaziangalia tu zile tiketi ambazo alikuwa amekatiwa na Salome.
Usiku kwenye mida ya saa tatu, Neema akiwa amejipumzisha kidogo akamsikia Salome akiingia ndani kwake na kumwambia,
“Mama kila kitu nimekupangia kwahiyo kesho safari”
“Na nguo zangu, na za wadogo zako umepanga?”
“Ndio tayari”
“Ila vitenge bado sijanunua”
“Nilishaenda kununua”
“Kheeee hebu tuvione”
Salome alimtolea Neema vitenge ambavyo aliviangalia na kushangaa tu kuwa Salome amewezaje kwenda mjini kwa muda mfupi vile na kuchagua vitenge bvizuri vile, akainuka na kuangalia mabegi ni kweli yalikuwa yamepangwa vizuri kabisa kwahiyo hakuwa na cha kubisha kuhusu safari ya kesho, swala hilo hata likamsahaulisha kuwa alishauriwa mwanae ampeleke kwenye maombi.
“Nishaongea na dereva tax, kwahiyo atakuja kuwachukua kesho asubuhi”
“Kwahiyo nyumba nani atafunga?”
“Mimi nitafunga, na mkiwa mnarudi mtanikuta maana nitakuwa narudi mara kwa mara”
Neema alimuangalia mwanae Salome hakummaliza maana kwa kawaida Salome wake ni muoga ila leo hii anakubali kuachwa mwenyewe nyumbani na anasema atakuwa anaenda mara kwa mara hata wakirudi watamkuta, alimshangaa kwakweli ila akajisemea labda ndio kukua kumemfanya abadilike.
Usiku wa manane, Rose alichukuana na mwanae kwenda kufanya msako kwenye chumba cha Moza kutafuta ile dawa iliyomuua Moza maana walihisi bado ipo ndani. Basi walipekua na kupekua lakini hawakufanikiwa kuiona, ndipo walipoanza kupekua nguo moja moja ya Moza ila Ana akamwambia mama yake,
“Mama, tutajichosha bure. Ngoja twende chumbani kwangu nikachukue ile dawa yangu ituonyeshe”
Rose aliafikiana na mwanae na kujilaumu kuwa kwanini walikuwa wakijichelewesha wakati kuna njia rahisi ya kufanya, basi wakatoka mule chumbani kwa Moza na kuelekea chumbani kwa Ana walipofika walishangaa kumuona mtu amekaa kitandani kwa Ana halafu mtu huyo akawaangalia na kuwafanya wagundue kuwa ni Moza.
Itaendelea kesho usiku…….!!!!!!!
By, Atuganile Mwakalile.
KURUDI KWA MOZA: 22 Rose alijua Salome ataanguka chini ila ilikuwa kinyume maana Salome hakuanguka chini, Rose akamsukuma tena ila Salome alisimama kamavile mlingoti. Muda huu Rose alipotaka kumsukuma tena Salome alishangaa mkono wake ukianza kutetemeka. Kila mmoja ndani ya nyumba yake alimshuhudia Rose akitetemeka mkono, Ana akainuka kwani aliona mama yake asije akaumbuka yeye kisha Ana akamsukuma yeye Salome ila kwake ndio ikawa kinyume kabisa kwani mkono wake uliganda kwenye mwili wa Salome, kila mmoja alikuwa akishangaa na kati ya wale mapacha na Sara hakuna aliyeweza kuongea neno lolote. Mara Salome alianza kuelekea vyumbani ila Ana ambaye mkono wake uliganda kwa Salome alikuwa akimfata nyuma, halafu Rose naye ambaye mkono wake ulikuwa ukitetemeka alikuwa akimfata nyuma pia, kitendo hiko kiliwafanya wale mapacha na Sara wafate nyuma kwani walitaka kujua ni nini kinaendelea au ni kitu gani huyo Salome anataka kufanya. Salome aliongoza moja kwa moja mpaka chumbani kwa Rose na kufungua mlango, kila mmoja alikuwa akimfata nyuma huku wengine hawaelewi elewi, alikutwa Patrick akiwa amelala chini sakafuni, Salome akamuangalia Rose na kumuamuru, “Muamshe” Rose akiwa anatetemeka, alisogea kwa Patrick na kujaribu kumuamsha. Alimuamsha kwa muda akashindwa, akainua kichwa chake na kumtazama Salome kwa uoga kisha akamwambia, “Nakuomba basi wanangu watoke humu chumbani nimuamshe” “Unashindwa nini kumuamsha hivyo hivyo?” “Tafadhali usinidhalilishe, nakuomba watoke kwanza ndio nimuamshe. Nipeni dakika chache tu nitakuwa nimemuamsha” Salome akatoka nje na wengine wote walimfata nyuma hadi sebleni kwahiyo walimuacha mama yao akiwa chumbani na Patrick. Kila mmoja alikuwa akimshangaa tu Salome na wala Ana hakuweza kuutoa mkono wake kwenye mwili wa Salome maana uligandia alipotaka kumsukuma, kwahiyo walikuwa wamesimama tu na hakuna yeyote aliyethubutu kukaa wala kusema neno lolote kwa wakati ule kwani wote walijikuta wakimtazama tu Salome. Baada ya muda kidogo, mama yao alirudi na Patrick sebleni na muda huu hata Ana akaweza kuutoa mwili wake kwenye mwili wa Salome, basi Salome alienda kumfata Patrick na kumkalisha kwenye kiti kisha akapitisha mkono wake machoni pake na kusema, “Nataka uone yote na zaidi ya yote amabayo mkeo amekuwa akikutendea kwa miaka yote hii” Ikawa kama akili ya Patrick imefunguka kiasi hivi kwani alianza kujishangaa na kuhoji kuwa yuko wapi, “Nikowapi hapa?” Ni Salome pekee aliyekuwa na ujasiri wa kumjibu, “Unatakiwa kutulia kwanza maana ndio umetoka kifungoni ni ngumu kujua kwa mara moja ulipo. Tulia kwanza tuliza akili halafu utajua ulipo na kila kitu ingawa kuna baadhi ya vitu utavitambua badae sana” Patrick alikaa kimya kwani alikuwa kama haelewi elewi vile. Walitamani kumuhoji Salome lakini hakuna aliyekuwa na ujasiri wa kufanya hivyo, kisha Salome akainuka na kwenda zake ndani kisha akawaacha wote pale sebleni. Yani kama kuna siku ambayo Rose aliwaonea wanae aibu basi ilikuwa ni siku ya leo maana nae hakuweza tena kukaa pale sebleni bali aliondoka na kwenda chumbani kisha Ana nae akafata na kwenda chumbani kwake. Kwahiyo sebleni walibaki wale mapacha, Sara na Patrick. Muda kidogo Patrick alimuangalia Sara na kumuomba jambo, “Naomba kaniletee simu yangu na funguo za gari chumbani” Sara hakubisha wala nini, alifanya hivyo na kwenda chumbani kwa mama yake ambapo aligonga na mama yake alimkaribisha kwani alijua ni Ana, akashangaa kumuona ni Sara. Akamuuliza kwa mshangao, “Vipi tena?” “Baba kanituma funguo za gari na simu yake” “Chukua hivyo hapo mezani mpelekee” Yani siku ya leo hata kuhoji hakuhoji zaidi ya kusema funguo zilipo na simu ya mumewe, simu ambayo mume wake ana kitambo sana hajaishika wala kuwasiliana na watu. Sara alichukua na kwenda kumpelekea baba yake huyo wa kambo. Alipompa tu Patrick alitoka nje na kuondoka zake, tena hakuna aliyemuaga kuwa anaenda wapi. Wale mapacha waliangaliana na dada yao Sara, halafu Sara akawaambia, “Yani kwa matukio haya naogopa hata kulala peke yangu” “Sasa utalala na nani?” “Sijui yani” “Basi kalale na Ana au Salome” “Mmmh hao watu ni bora uniambie nikalale getini na mlinzi, nawaogopa hao watu kama kitu gani” Mara Salome akatokea, Sara akajikuta tu akimwambia “Baba kaondoka tena bila kuaga, halafu leo kachukua na simu yake” “Ungekuwa ni wewe ungeweza kuaga?” “Kivipi?” “Unajifanya hujui ambayo baba yangu alikuwa akitendewa kwenye nyumba hii? Sasa anatambua kila kitu, maswala ya kumfanya mwenzenu kama ndondocha mwisho” Sara aliwaangalia wenzie, halafu Salome alitoka nje kabisa na alionekana akielekea getini ambako alitoka na kuondoka. Sara aliwauliza wenzie, “Jamani mnamuelewa huyu mtoto?” “Simuelewi na sitaki kuongea sana” “Hata mimi pia simuelewi na naogopa kuongea sana” Kisha wale mapacha wakaondoka zao na Sara akaondoka zake. Rose alipoona mwanae Ana hajaenda chumbani kwake ikabidi yeye mwenyewe ndio aende chumbani kwa Ana, aliingia na kumuuliza mwanae, “Hivi wewe umeweza kumuelewa huyu Salome?” “Mama naomba tuzungumze usiku kwenye muda wetu sio muda huu” “Hata tukisema tuzungumze usiku hatatusikia kweli?” “Mama, mimi ndio nimekwambia na bado natafakari maana sipo sawa kabisa. Amewezaje Yule kugandisha mkono wangu mama? Yule msichana ana majini sio bure” “Ndiomana nakwambia tujadili sasa hivi, unajua ile majuzi nilienda kwa mganga mwingine halafu ndani kwa mganga nilimkuta Moza” “Moza!” “Ndio nilimkuta Moza” “Si amekufa huyo mama” “Mwanangu hatuna uhakika na kifo cha Moza, kumbuka maiti yake ilitoweka kaburini” “Ndio ilitoweka ila nikajua utafanya jambo, na imekuwaje hadi Moza awe hajafa kweli?” “Sijui mwanangu, ila kama ile dawa iliyomuua Moza ilichomwa moto basi tumeisha” “Unamaana gani mama?” “Ile dawa mwanangu nilipewa na ilikuwa hairuhusiwi kuonekana na mtu yeyote halafu sitakiwi kuiweka mbali na nyumba yangu ndiomana nikaifukia kwenye ua ili nijue ni ua gani nimeifukia. Ni ya muda mrefu sana ile dawa na ilikuwa hairuhusiwi kuonekana na mtu yeyote wala kuungua na moto ndiomana hata kuunguza mboga humu kwenye nyumba yangu huwa sitaki. Sasa kama imechomwa moto sijui itakuwaje, ndiomana tulitakiwa kumzika nayo Moza” “Sasa mama kama imechomwa moto imechomwa na nani wakati Moza alikuwa amekufa nayo mkononi” “Kwamaana hiyo inawezekana ipo mahali eeh! Lakini mbona tuliitafuta bila kuiona popote” “Mi nadhani mama tufanyie usafi kile chumba cha Moza tuitafute kabla hayajawa majanga” “Sasa lile shetani linalolala kwenye chumba kile tutalifanya nini?” “Yani huyo mtu ananiumiza kichwa balaa, ila mama na wewe kwanini dawa ya maana hivyo ukaenda kuifukia kwenye ua? Mbona mimi dawa yangu ile ipo chini ya godoro” “Ni masharti ya ile dawa, kwanza haikutakiwa kuwekwa ndani ya nyumba ila inatakiwa iwe karibu na nyumba halafu haitakiwi mtu aione.” “Basi mama nitatumia dawa yangu kufanya kitu ili tuweze kupekua kile chumba cha Moza” “Sawa mwanangu, ndiomana nilikuwa nakufata tujadili. Sasa wewe unataka tufanye kwenye muda wetu, unadhani mambo yalivyotinga hivi tutakumbuka kujadiliana kweli! Ni ngumu mwanangu” “Kweli mama ila chanzo cha mambo yote haya ni mwanao Sara, yani simpendi Yule mdada simpendi kabisa” “Kweli mwanangu ni chanzo cha yote lakini ni mwanangu, kumbuka hilo. Yule ni dada yako mpende tu” Rose akajiribu pale kumshawishi mwanae ili ajende upendo kwa ndugu yake maana alikuwa anapenda watoto wake wapendane. Salome alienda nyumbani kwa mama yake na kumkuta kama kawaida akiwa na wale wadogo zake John na Joseph. Aliwasalimia kisha mama yake akamuomba chumbani kwake ili wakazungumze “Kwanza imefurahi umerudi nyumbani maana mambo yako siku hizi siyaelewi kabisa. Halafu ngoja nikuulize, hivi una simu” Salome akacheka, “Sio unacheka Salome, nijibu una simu?” “Ndio nina simu” “Umeitoa wapi?” “Baba yangu kaninunulia ili niweze kuongea nae” “Haya, wadogo zako wameniambia Ashura hakuja huku kwenye nyumba mpya, halafu wewe na Ashura kuna mchezo mlikuwa mnacheza kisha Ashura akaanguka. Unajua sijaelewa naomba nieleweshe maana huyo Ashura hata nikimpigia simu zangu hapokei zaidi ya kunitumia ujumbe tu” “Hivi hat nikikueleza unaweza ukanielewa!” “Nieleze tu, kwanini nisikuelewe?” “Acha tu ufahamu unavyofahamu, Yule Ashura si ndugu yako? Uliza kwa ndugu zenu alipo” “Hivi wewe mtoto unaongelea nini mbona sikuelewi?” “Huyo mamdogo Ashura yupo kwenye kijiji cha baba yenu amesema anaenda kuangalia kaburi la baba yenu kwahiyo ungeenda na wewe kijijini ili uulize vizuri kuhusu Ashura” “Tutaenda na wewe?” “Hapana, mimi nitabaki ila utaenda na wadogo zangu. Mimi nabaki na baba yangu.” “Haya nitafikiria kwenda” Salome akainuka, na kumfanya Neema amuulize tena, “Sasa mbona unaondoka kabla hata sijamaliza maongezi na wewe” “Subiri nakuja sasa hivi” Salome aliondoka zake, Neema nae alitoka ila kiukweli hakumuelewa kabisa mwanae na mambo aliyokuwa anayafanya. Alipokaa muda kidogo mwanae alirudi kisha akampa mama yake tiketi, “Nimeshakukatia tiketi, wewe na wadogo zangu ya kwenda kutembelea kaburi la babu” “Kheee kwahiyo ndio unataka tusafiri!” “Ndio, si mnaenda kukaa wiki tu mnarudi” “Kwahiyo tiketi umekata ya kuondoka lini?” “Kuondoka kesho” “Kheee Salome hebu acha masikhara, tutaondokaje kesho wakati hatujajipanga!” “Unataka mjipangaje?” “Sijapanga nguo za watoto, sijawanunulia mama zangu vitenge” “Ni hayo tu au kuna mengine?” “Ni hayo ndio” “Basi nitakusaidia, yani wewe tulia tu nitakusaidia kupanga ila tiketi ni ya kesho” Neema alimshangaa sana Salome kuwa mtoto wake amebadilika sana na amekuwa na maamuzi ya haraka haraka, akawa anaziangalia tu zile tiketi ambazo alikuwa amekatiwa na Salome. Usiku kwenye mida ya saa tatu, Neema akiwa amejipumzisha kidogo akamsikia Salome akiingia ndani kwake na kumwambia, “Mama kila kitu nimekupangia kwahiyo kesho safari” “Na nguo zangu, na za wadogo zako umepanga?” “Ndio tayari” “Ila vitenge bado sijanunua” “Nilishaenda kununua” “Kheeee hebu tuvione” Salome alimtolea Neema vitenge ambavyo aliviangalia na kushangaa tu kuwa Salome amewezaje kwenda mjini kwa muda mfupi vile na kuchagua vitenge bvizuri vile, akainuka na kuangalia mabegi ni kweli yalikuwa yamepangwa vizuri kabisa kwahiyo hakuwa na cha kubisha kuhusu safari ya kesho, swala hilo hata likamsahaulisha kuwa alishauriwa mwanae ampeleke kwenye maombi. “Nishaongea na dereva tax, kwahiyo atakuja kuwachukua kesho asubuhi” “Kwahiyo nyumba nani atafunga?” “Mimi nitafunga, na mkiwa mnarudi mtanikuta maana nitakuwa narudi mara kwa mara” Neema alimuangalia mwanae Salome hakummaliza maana kwa kawaida Salome wake ni muoga ila leo hii anakubali kuachwa mwenyewe nyumbani na anasema atakuwa anaenda mara kwa mara hata wakirudi watamkuta, alimshangaa kwakweli ila akajisemea labda ndio kukua kumemfanya abadilike. Usiku wa manane, Rose alichukuana na mwanae kwenda kufanya msako kwenye chumba cha Moza kutafuta ile dawa iliyomuua Moza maana walihisi bado ipo ndani. Basi walipekua na kupekua lakini hawakufanikiwa kuiona, ndipo walipoanza kupekua nguo moja moja ya Moza ila Ana akamwambia mama yake, “Mama, tutajichosha bure. Ngoja twende chumbani kwangu nikachukue ile dawa yangu ituonyeshe” Rose aliafikiana na mwanae na kujilaumu kuwa kwanini walikuwa wakijichelewesha wakati kuna njia rahisi ya kufanya, basi wakatoka mule chumbani kwa Moza na kuelekea chumbani kwa Ana walipofika walishangaa kumuona mtu amekaa kitandani kwa Ana halafu mtu huyo akawaangalia na kuwafanya wagundue kuwa ni Moza. Itaendelea kesho usiku…….!!!!!!! By, Atuganile Mwakalile.
Artikel Terkait
Story - - - - - NI WEWE TU PENINA. BY GIVAN IVAN PHONE & WHATSAPP____0769673145 Karibuni tuianze story yetu hii mpya yenye kusisimua iliyojaa visa mbali mbali kuhusu mapenzi. Sehemu ya kwanza (1) Mapenzi ya vijana wawili walionza kupendana toka wakiwa wadogo mpaka Sasa wakiwa na umri wa miaka 25 kila mmoja, yalikuwa yakizidi kukolea kila siku na kuwa matamu zaidi na zaidi. Vijana Hawa ni Frank pamoja na Penina. "nahisi kuvurugwa nahisi kufa kufa yaani najiona kama napepea juu juu kwa jinsi navyompenda mpenzi wangu Penina." alikuwa frank akiongea maneno hayo mbele ya wazazi wake pamoja na mdogo wake Wa kike aitwaye Angel. "na siku si nyingi utakuwa chizi wewe sio kwa kupenda huko kaka yangu." akaongea Angel kumuambia Frank. "acha niwe chizi tu mdogo wangu, lakini sio chizi wa kutembea uchi barabarani bali chizi wa kupenda." akaongea Frank maneno hayo na kuwafanya wazazi wake wacheke sana. "lakini mwanangu Sasa inabidi mfanye taratibu mfunge ndoa Sasa." aliongea baba yake Frank. "Hamna shida baba usijali yote hayo yatafanyika muda mfupi ujao. " Akaongea Frank ambaye muda wote furaha ilijaa usoni mwake. *wakati huo huo Penina mpenzi wake Frank naye alikuwa katika moja saloon akitengeneza nywele zake ikiwa ni maandalizi ya kwenda kukutana na mpenzi wake Frank. " Dada nitengeneze vizuri tafadhali maana napenda muda wote niwe navutia mbele ya mpenzi wangu." aliongea Penina kumwambia mwanadada aliyekuwa akimtengeneza nywele. "usijali dada nitakutengeneza vizuri mpaka mwenyewe ufurahi." Dada yule akamjibu Penina na kumfanya atabasamu. Baada ya dakika kadhaa Penina alimaliza kutengenezwa nywele zake na moja kwa moja akazama kwenye pochi yake na kutoa simu yake, kisha akatafuta Jina lililoandikwa my love Frank na moja kwa moja akazipiga namba hizo. * Frank akiwa bado anaongea na wazazi wake ghafla simu yake ilianza kuita, akatoa na kuangalia mpigaji ni Nani. Frank alianza kutabasamu baada ya kukuta mpigaji ni Penina kipenzi cha moyo wake. "haloo mke wangu mtarajiwa mambo vip?" akaongea Frank baada ya kupokea simu. "poa tu mpenzi wangu nimekumiss hadi nahisi kizunguzungu." akajibu Penina. "Asante mpenzi wangu yaani kuachana Jana tu ndio kunimiss hivyo?" " yeah nimekumis sana hebu jiandae nakupitia Sasa hivi tukale bata kidogo. " akaongea Penina kumwambia Frank. " waoow ok najiandaa Sasa hivi utanikuta tayari my love." akajibu Frank na simu ikakatwa. Frank aliwaacha wazazi wake pale sebuleni kisha yeye akaenda kujiandaa kwa ajili ya kutoka na mpenzi wake. Penina naye baada ya kukataa simu aliingia kwenye gari yake nyeupe aina ya rava4 na kuanza kuelekea nyumbani kwa Frank. Tumfahamu Penina vizuri. Penina ni mwanamke mrembo sana aliyebarikiwa na Mungu kuwa na kila kitu kizuri katika mwili wake. Popote pale Penina alipopita aliacha gumzo kwa wanaume ambao walikuwa wakimmezea mate. Penina ametoka katika familia ya kitajiri yenye watoto watatu, wawili wa kike na mmoja wa kiume ambao ni Nolan, Penina na Irene. Penina amefanikiwa kusoma mpaka elimu ya juu kabisa na kufanikiwa kuwa mfanyabiashara mdogo anayechipukia kwa kasi sana. Penina alianza uhusiano wa kimapenzi akiwa kidato cha tatu, na alianza uhusiano na kijana aliyeitwa Frank ambao mpaka Sasa wapo pamoja. Lakini kitu kimoja ambacho kanalitia dosari penzi tamu kabisa la Penina na Frank, ni baba yake Penina kutopenda mwanawe aolewe na Frank. Baba yake Penina hakutaka kabisa mtoto wake aolewe na Frank, yeye alitaka mtoto wake aolewe na mzungu kutokana na uwezo wao wa kipesa. Mama yake Penina pamoja na Nolan kaka yake Penina ndio Watu pekee waliokuwa wanayaunga mkono mapenzi ya Penina na Frank katika familia yao. Lakini Irene mdogo wake Penina pamoja na baba yake Penina ndio watu pekee ambao walikuwa hawataki kabisa kuyaona mapenzi ya Penina na Frank yakiendelea. * Frank yeye anatoka katika familia yeye hali ngumu kimaisha, hawakuwa na uwezo hata wa kuwa na nyumba nzuri kama wenzao. Frank aliishia kidato cha pili kutokana na wazazi wake kutokuwa na uwezo wa kumuendeleza zaidi. Kadhalika pia Angel mdogo wake Frank naye aliishia darasa La saba kutokana na Wazazi wao kutokuwa na uwezo wa kuwaendeleza zaidi. * Baada ya dakika kadhaa Penina aliwasili nyumbani kwa kina Frank, akapaki gari yake pembeni na kushuka Kisha akaingia katika nyumba ya kina Frank ambayo ilikuwa imechoka Sana. "waoow mkwe wetu karibu Sana." mama yake Frank ndio alimpokea Penina kwa furaha Sana. "Asante Sana mama yangu nimekaribia." akajibu Penina huku akiketi pembeni ya mama yake Frank. "eeh mwanetu lete habari." akaongea mama yake Frank. "Sina hata mpya nimekuja kumchukua mtoto wenu." akajibu Penina. Na Muda huo huo Frank akajitokeza akiwa tayari ameshajiandaa. Licha ya umaskini uliopo katika familia Yao, bado Frank alijitahidi Sana katika kuupendezesha mwili wake ili aweze kuendana na mpenzi wake Penina ambae Muda wote alikuwa mtu wa kupendeza tu. "waoow my love mwaaa." Penina ndio alinyanyuka na kumkumbatia Frank na kumuachia busu Zito la shavu. Frank naye hakuwa nyuma alimpokea mpenzi wake kwa furaha pia. Penina pamoja Na Frank waliaga na kutoka nje, wakaingia kwenye gari na kuondoka. "tunaelekea wapi Sasa mpenzi wangu?" akahoji Frank. "surprise my love sikuambii tunaelekea wapi." Penina akamjibu Frank huku akitabasamu. "haya bhana bas nafunga macho mpaka tufike." akaongea Frank na kumfanya Penina azidi kutabasamu.* Katika bar moja iliyopo maeneo ya sinza kikao kimoja kilikuwa kikiendelea, na huku kilichokuwa kikipangwa Katika kikao kile ni namna ya kulivunja na kuliharibu penzi la Penina na Frank. Mzee Joel ambaye ni baba yake Penina, pamoja na Angel ambaye ni mdogo wake Penina pamoja na vijana wengine watatu wa kiume na mmoja wa kike, ndio waliokuwa wahusika wakuu wa kikao kile. .... Itaendelea ... Read More
Story....... NI WEWE TU PENINA Sehemu ya Tatu (3) BY GIVAN IVAN Ilipoishia........ Baada ya Penina kuondoka tu, Frank kabla hajapiga hata hatua moja kuondoka pale, ghafla alishtukia amezungukwa na vijana watatu wa kiume waliokuwa wamevalia miwani nyeusi kila mmoja. Na hata Frank alipowaangalia hakuweza kuwafahamu. .......... .. Endelea............ "tulia hivyo hivyo na sikiliza tunachokuambia." akaongea kijana mmoja huku akiwa ametoa kisu na kumuwekea Frank shingoni. Frank naye alikuwa kimya na kuwasikiliza walichokuwa wanataka kumuambia. "sikiliza wewe kijana wewe bado mdogo Sana, hivyo bas tunakusihi uachane na Penina haraka iwezekanvyo, hili ni onyo tu tunakupa na ukikaidi bas shingo yako tutaikata kama ya kuku." akaongea kijana ambaye alikuwa kiongozi wa wenzake, kijana huyo aliitwa Zaza. Baada ya Zaza kumwambia Frank maneno yale ya kumtisha aliondoka na wenzake na kuingia kwenye gari moja nyeusi iliyokuwa imepaki pembeni Yao, Kisha gari likaondolewa kwa kasi ya ajabu huku dereva wao akiwa ni mwanamke anayejulikana kwa Jina la Melissa, moja Kati ya vijana waliopewa kazi nzito ya kuliharibu penzi la Frank na Penina. Frank alianza kuingiwa na hofu na kujiuliza "ni nini tena kinaendelea juu yake? " Frank alijivuta na kuondoka sehemu Ile na kuingia nyumbani kwao akiwa mnyonge kuliko kawaida yake. " eeh kaka vip mbona mnyonge hivyo kulikoni tena? " akauliza Angel mdogo wake Frank. " aah kuna vijitu vinataka kuniharibia siku hapo nje." akajibu Frank na kuketi kwenye kigoda. "watu gani tena hao mwanangu?" akauliza pia mama yake Frank. "mama kuna watu hapo nje wamenisimamisha na kunitishia niachane na Penina la sivyo wataniua." akaongea Frank kuwaambia wazazi wake wakiwa wamepigwa na butwaa. "haa mwanangu katoe taarifa haraka polisi kwa usalama wa maisha yako." akaongea baba yake Frank kumpa ushauri mtoto wake. "Polisi siendi baba nachojua mimi Penina ni mpenzi wangu nampenda na yeye ananipenda, yoyote atakayeingilia penzi langu na Penina ama zake ama zangu na kukuonesha mfano naanza na hawa walionitisha leo." akaongea Frank kwa jazba Kisha akanyanyuka na kuondoka kuelekea chumbani kwake. "kuwa makini mwanangu tusije tukakupoteza mapema." akaongea baba yake Frank, lakini Muda huo Frank alikuwa ameshatoweka mbele ya macho yao. "Mimi ni mwanaume rijali nitakubalije kutenganishwa na Penina kirahisi hivi?" alikuwa Frank akijiuliza swali hilo huku akizunguka zunguka chumbani kwake. "naamini hakuna mwenye uwezo wa kunitenganisha mimi na Penina isipokuwa Mungu tu." akaongea Frank huku sasa akiwa amejilaza chali kitandani kwake.* Hatimaye Penina naye aliwasili nyumbani na Muda huo ikiwa ni majira ya saa tatu usiku. Geti lilifunguliwa na taratibu Penina akaingiza gari ndani na kulipaki sehemu yake, Kisha yeye akashuka na kuanza kuelekea ndani Katika jumba la kifahari kwa mwendo madaha kama kinyonga. Lakini kabla hajaingia ndani alikutana na baba yake mlangoni ambaye alionesha wazi kuwa alikuwa anamsubiri Penina. "shikamoo baba!" akasalimia Penina, lakini baba yake badalaa aitikie salamu ile akamuuliza Penina, "umetoka wapi usiku huu?" "nilikuwa na mpenzi wangu Frank kuna sehemu tulienda ndio narudi Sasa hivi." Penina akamjibu baba yake bila uoga. "wewe ni Mara ngapi nimekukataza kurudi nyumbani kwangu usiku? Na si nimeshakuambia uachane na huyo chokora wako?" akauliza baba yake Penina huku akiwa amezira. "Kwa kosa la kurudi nyumbani usiku naomba unisamehe baba yangu, Lakini muda si mrefu nitakuondolea hii kero ya kurudi nyumbani usiku kwasababu mimi na huyo mpenzi wangu unayemuita chokora tumeshaanza harakati za kufunga ndoa na tutahamia kwetu muda si mrefu." akaongea Penina kumuambia baba yake bila uoga wowote. "hivi wewe mpumbavu unajua unaongea na nani? Maana naona unaropoka ropoka tu kama umekunywa maji machafu." akaongea baba yake Penina. "ndio najua naongea na nani, najua naongea na wewe hapo baba yangu kipenzi tena nakupenda Sana lakini najua wewe hunipendi." akaongea Penina maneno hayo ambayo yalimfanya baba yake apoe kidogo. "hapana mwanangu sio kwamba sikupendi, nakupenda sana tena Sana Ila huyo unayemuita Frank mi ndio ananikera kupita maelezo yaani nikimuona nahisi hata kutapika." akaongea baba yake Penina kwa upole kidogo. "Baba unataka niachane na Frank?" akauliza Penina. "ndio mwanangu tena nitafurahi Sana na nitakupa zawadi kubwa Sana." akaongea baba yake Penina. "ok bas subiri kidogo." akasema Penina Kisha akaondoka kwa Kas mpaka jikon ambapo alichukua kisu na kurudi nacho mpaka kwa baba yake. Wakati hayo yote yanatendeka Noel ambaye ni kaka yake Penina alikuwa akiyashuhudia yote hayo. "kama unataka niachane na Frank niue kwasababu hiyo ndio njia pekee." akaongea Penina huku akimkabidhi baba yake kisu kile. "haa mwanangu Sasa huu utoto gani unaleta mbele yangu?" akauliza baba yake huku akikitupa kisu kile pembeni. "sio utoto baba bali namaanisha ninachokiongea, na kama umeshindwa kutekeleza nilichokuamuru bas tambua hakuna wa kunitenganisha na Frank na siku si nyingi tutafunga pingu za maisha, na sitojali kama wewe utaudhuria ama hutoudhuria." akaongea Penina kumuambia baba yake Kisha akaondoka na kuelekea chumbani kwake. Nolan naye alitoka sehemu aliyokuwepo akisikiliza malumbano ya Penina na baba yake na kumfuata Penina chumbani kwake. Huku nyuma baada ya Penina kuondoka, baba yake alitoa simu yake na Mara moja akampigia Zaza. "hallow mzee Joel.!" akaongea Zaza baada ya kupokea simu. "Zaza nisikilize kwa makini, Penina na yule chokora wapo Katika mipango ya kufunga ndoa, Sasa nachotaka mfanye ni kuwatenganisha kwa namna yoyote ile, mnachotakiwa kufanya ni kumteka nyara huyo chokora alafu mkamtupe mbali kabisa sehemu ambayo mnajua anaweza chukua hata mwaka mmoja Kuja kuonana na Penina tena. " akaongea mzee Joel kwa kusisitiza (mzee Joel ni baba yake Penina) " Sawa hamna shida mzee wetu tutafanya hivyo." akajibu Zaza. "ok bas fanyeni haraka iwezekanavyo kama mtahitaji pesa zaidi mtanijulisha." mzee Joel akamwambia Zaza na kukataa simu. * Penina baada ya kuingia chumbani kwake ghafla kaka yake naye akaingia pamoja naye. "hee kaka kumbe ulikuwa nyuma yangu?" akahoji Penina kwa mshangao. "ndio na pia nilikuwa nasikiliza malumbano yenu mzee." akaongea Nolan ambaye ni kaka yake Penina. "yaani kaka wewe acha tu, baba angejua navyompenda asingenifanyia hivi anavyonifanyia." akaongea Penina kwa huzuni kumuambia Nolan. "Ila mdogo wangu usijali wewe simamia kile unachokiamini na mimi nitakuwa nyuma yako kukusaidia." akaongea Nolan kumtia moyo Penina. "nashukuru kaka kusikia hivyo angalau wewe ndio uko upande wangu." akaongea Penina kumshukuru kaka yake. "usijali mdogo wangu wewe lala kwa amani tutaonana kesho." akaongea Nolan na kuondoka chumbani kwa Penina.* Kwa upande wa kina zaza usiku ule ule walianza kupanga mikakati ya kumteka Frank na kwenda kumtupa mbali kabisa na jiji la dar es salam. Lakini hii ilikuwa kazi ngumu Sana ambayo walihitaji pesa za kutosha na pia wachore ramani ya sehemu watakayoenda kumtupa Frank. ....... Itaendelea ... Read More
CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA TATU (03) ILIPOISHIA SEHEMU YA PILI : kas0ro Niram peke yake ambae alisema, "wala sina mpango huo, ntampeleka wapii mimi, ila nimemsifiatu! sababu katika wavulana niliowai kuwaona, kwa hapa mtanzania, yule kaka ni handsome sanaa" alisema Niram huku anawaangalia marafiki zake, ambao wakakubaliana nae, kwakiikisa vicwavyao juu chini, na wakati huo kengele ya darasani ikagongwa, wakasimama tayari kwa kuanza safari ya kuingia darasani, ENDELEA....... Waliingia darasani, na vipindi vikaedelea kama kawaida. Niram alitafakari sana maneno ya rafiki zake,,akujua hata kwanini awazia lile jambo, maana hata sababu ya kuliwazia akuiona. "mmh mimi sasa ntakuwa nataka kurukwa na hakili haki ya Mungu" alijisemea kimoyo moyo Niram. Ila akaamua aachane na fikra zile, ambazo mwenyewe alizoziona za kipuuzi, na kuendelea na ratiba zake nyengine. ****** "hallo mmewangu nimekumisi mno utakuja lini?".ilikuwa sauti ya mama niram, aliye kuwa amepozi kwenye moja ya kochi zuri huku ameweka miguu juu ya meza. "ooh mkewangu kipenzi ratiba zinabana kazi zimekuwa nyingi mno hata mi nimekumisi kipenzi ila sina la kufanya mama".ilisikika sauti upande wa pili, ikiongea kwa masikitiko na mapenzi makubwa kwa mkewe. "ooh darling uwezi kuomba ruhusa ukaja hata kwa siku chache tu?".aliongea kwa kudeka mama niram huku akimpachika na swali mumewe huyo,aliyekuwa mbali na nchi ya Tanzania. "ooh sitawahi, unajua natakiwa kwenda india kuna Mahafali ya Razaki".ilisisitiza sauti ya baba niram. "ooh Mungu wangu nilisahau nasikitika sitoenda kwenye mahafali ya mwanangu".aliongea mama niram kwa unyonge ilionyesha hakuwa na furaha kuikosa hiyo sherehe ya mtoto wake wakiume. "usijali mke wangu, najua uwezi kuja sababu niramu hatokuwa na wakubaki nae wacha niende kukuwakilisha mimi sawa mamaa".aliongea kwakubembeleza baba niram huku akimfariji mkewe ili asijione mkosefu. "oky honey kazi njema nitafute baadae utapomaliza kazi".alisisitiza mama niram, "oky honey byeee ilove you"."love u too mume wangu byee". Waliagana mtu na mumewe, mama niramu akanyanyuka kuelekea jikoni,kuangalia kama msichana wake kama ameshamaliza kupika chakula cha mchana. ********* "eeeh ujue vincent ukumalizia story".alisikika suma akimuambia vicent, wakati huo walikuwa katika uwanja wa mpira, wakiangalia watu wanaofanya mazoezi, akiwemo Richard, yeye alikuwa akifanya mazoezi ya mpira wa kikapu, vicent na suma walikuwa wakimuangalia rafiki yao huyo, ambae alijua kuutumia uwanja vizuri aliku Hodari kweli kweli katika mchezo huo, "hahhhhah suma wewe mshkaji wangu mmbeya sana duuuh! yani kumbe ulisubiri tutoke tu!, yani wewe sikuwezi" aliongea vicent, vikafata vicheko vikaliii, suma alikuwa hana mbavuuu, ungewaona ungesema walikuwa wameona jambo la kuchekesha hapo walipo, "sasa mi nimesubiri we unihadithie naona kimya nikaona bora niseme yanini nife kiholo".aliongea suma huku anakalisha tako vizuri akimgeukua mlengwa. Basi vicent alimuadithia mwanzo mwisho, jinsi alivyokutana nae mpaka ilipofikia kusahau kumuomba namba. "hahahhhah hizo ndoto ndugu yangu yani ndo maana ukamzingua vanessa?".aliongea suma kwa mbwembwe, huku akumuona rafiki yake huyo kama anaota ndoto za mchana kweupe. "sikia suma vanessa mimi simpendi bora tu akate tamaa mapema kuliko nikaja kumuumiza zaidi huko mbele na kuhusu huyo dem ata asiponipenda baridi tu! ilimradi mi nimuekeze hisia zangu tu".aliongea vicent kwa msisitizo akimaanisha anachokisemaa. "aaah naona mnakula tu ubuyu". Aliingia Richard, katikati ya mazungumzo, mwili ukiwa umelowa jasho, aka kaa pembeni yao ilionyesha ashamaliza kufanya mazoezi ******* "mama simu inaita".aliita msichana wa kazi wakina Vincent, akimpelekea simu bosi wake ambae alikuwa amekaa nje kwenye bustani. "asante karunde kaendelee na kazi". Alisema mama yake vicent huku anaweka mkonga sikioni. "hallow magreth niambia rafiki yangu".aliongea mama vicent, aikusikika upande wapili,mara mama vicent akaongea na kuaga"aaah! Sawa basi usijali ntakuambia tarehe ikufika nikutakie siku njema".simu ikakatwa.******** "hahahhhh!! Yani na wewe huo ubuyu tule tumekuwa shilawadu?".aliongea vicent huku anacheka, mabega yote yakifanya kazi ya kunesanesa."yani we acha tu katuchukuliaje huyu sijui huyu bwege".alijibu suma huku akimpiga kofi la bega la kiutani utani. "aaah!bac kausheni vipi ile story ya asubuh nimalizie basi mwana".aliongea Richard huku anajiweka sawa kusikiliza. Vilifwata vicheko hatari. "kumbe na wewe shilawadu" aliongea suma baada ya kumaliza kucheka. Basi story zikaanza upyaa, visent akampa fully data. Richard Akuwa na la kuchangia zaidi ya kumtia moyo na kumwambia akaze buti. mara wakasikia ...... Itaendelea......CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA NNE (04) ILIPOISHIA SEHEMU YA TATU: "aaah! basi kausheni vipi ile story ya asubuh nimalizie basi mwana".aliongea Richard huku anajiweka sawa kusikiliza. Vilifwata vicheko hatari. "kumbe na wewe shilawadu" aliongea suma baada ya kumaliza kucheka. Basi story zikaanza upyaa, visent akampa fully data. Richard Akuwa na la kuchangia zaidi ya kumtia moyo na kumwambia akaze buti. mara wakasikia... endelea....... mara wakasikia, kama kuna vishindo vinakuja mahali walipo wao .ilibidi wakatishe story yao.nakuangalia mbele palipotokea,sauti ya viatu."mmmmh!!", alishusha pumnzi vicent baada ya kumuona mtu huyo aliyekuwa anakuja usawa waliokuwepo wao. Hakuwa mwengine bali ni vanessa, vanessa alizidi kuiongea taratibu kuja mahali pale, walipokuwepo wakina vicent.hatimae alifika."mambo zenu". Aliwasabahi huku akisubiri atajibiwa kwa hali gani salamu yake."nzuri vp vanessa"alijibu suma, mara kabla ajamaliza kuitikia suma, alidakia richard pia."tuambie shemela wa ukweli".kauli hii ili mchukiza, sana vicent alijikuta anamkata jicho moja kali rafiki yake huyo.ila vanessa alipotezea japo vicent,hakujibu salamu yake. "mi niko poa sana samahanini shemeji zangu nilikuwa naomba mnipishe kidogo nna mazungumzo na vicent".aliongea vanesa, huku akiwaangalia shemeji zake hao kwa zamu."ooh!!usijali mama suma eeh tuwapishe wapendanao".aliongea tena richard safari hii huku anatabasamu tabasamu la kichokozi,maana alijua ni jinsi gani anamkera rafiki yake." twenzetu mwanangu uwanja wenu jamani".aliongea suma huku ananyakua kibegi, chake kilicho kuwa pembeni yake, amesimama na kuanza kuondoka,wakati huo richard alikuwa ameshatanguli mbele." oyaa wanangu msifike mbali mnisubiri maana sitachukua mda mwingi hapa".aliongea vicent huku akiwa bize anatazama walipo kuwa wana tokomea wenzie. " poa".walijibu wote kwa pamojaa na kuendelea kutokomea mbele. "nakusikiliza unaweza kuongea" aliongea vicent bila kupepesa macho, akiwa mkavu kabisa." vincent kwani una nini mbona sikuelewi baba"aliongea vannesa huku anakaa pembeni ya vincent. Ila akupata jibu toka upande wapili."vincent si naongea na wewe au kuna kitu nimekukosea niambie ili nijue nikuombe radhi baba,nakupenda sitaki tukosane".aliongea vanesa kwa huzuni huku machozi yakiwa yanalengalenga kwenye macho yake. "sikia vanessa naomba usipoteza muda wako kwa ajili yangu focus katika masomo ujui kuwa tuna karibia mitihani ya kuhitimu kidato cha Sita ".alisema visent bila alama ya uoga,usoni kwake."najua baba lakini hiyo siyo sababu ya kufanya uwe serious ni kuelewana tu" alilalama vanessa huku akijisigeza karibu na vicent."oky basi ndo hivyo vanessa tuzingatie masomo now mapenzi yasimame kwanza".alimaliza vicent huku akijifuta vumbi, kwenye makalio tayari kwakuondoka. "vicent ntawezaje kukuchunia siwezi ntajitahidi nisome kwa bidii ila tusisitishe uhusiano wetu nakupenda sana". "vanessa tuelewane basi au nimefanya kosa kukusikiliza hapa?". Aliuliza vicent,pasipo kusubiri jibu akaanza,kuondoka.ila vanessa alimdaka mkono,na kumvuta asiondoke.daaaaah!! Lilikuwa kosa kubwa maana alisukumwa,akadondoka kama mzigo wa kuni pwaaaaaaah!!.aisee!! Vanessa aliumia akaanza kulia, maana alijiona kama mtu asiekuwa na thamani tena, aliumia kupita kiasi. Kitendo kile, kilimfanya vicent aingiwe na huruma, akaghairisha alipokuwa anakwenda, maana alijiona ana hatia sana. "nyanyuka mpenzi sikuzamilia kufanya hivyo nisamehe mama ". Alisema vicent huku akiinama, kumnyanyua vanessa na kwa bahati nzuri, hakuna alieliona tukio lile. "pole mama nisamehe sana". Alisisitiza vicent akionyeshwa kuchukizwa, na tukio alilolifanya." usijali vicent najua aikuwa kusudio lako kuna vitu haviko sawa kwako". Alijibu vanessa huku anajifuta vumbi, akisaidiwa na vicent. Baada ya hapo vicent alimchukua na kumkalisha chini. " vanessa siyo kama sikupendi laah hasha!! Nakupenda ila nielewe unatakiwa tusome kwanza tukimaliza mitihani tutaendelea, nafanya haya kwaajili yetu mama".aliongea vicent,siyo kama alimaanisha ila aliona si busara, kumuhukumu mtu kisa kampenda ni dhambi kubwa sana. " sawa ila niahidi tutakuwa tuna ongea hata mara moja moja, kwani bila kusikia sauti yako au kukuona sitaweza kusoma". Aliongea kwa kudeka, huku akijiegemeza kwa vicent. " sawa mama itakuwa hivyo ila naona muda unatutupa mkono, sitaki kuwachosha wenzangu wananisubiri". Alisema vicent huku akisimama tayari kwa kuondoka. "oky bby tutawasiliana ukifika".alisema Vanessa huku akiachia, busu matata shavuni mwa vicent. Basi waliagana na vicent akawafata washkaji zake, safari ikaanza..****** Nyumbani kwa kina niramu, palipoa alifika moja kwa moja mpk nyumbani kwao, akamsalimia dada wa kazi " da anna mamy yuko wapi?" aliuliza huku ana jibwaga juu ya kochi, begi akilitupia juu ya meza kubwa ya kioo, " ametoka kaniaga anaenda supermarket kununua bidhaa zimepungua".alijibu anna msichana wao wa kazi.niramu akajizoazoa kivivu, akaliokota begi lake, akaelekea chumbani kwake. Anna aliondoka kuendelea na shughuli zake.******* Vanessa alifika kwao, alikuwa amechoka, alifika akamkuta baba yake, ametulia kwenye kochi,akisoma gazeti. Nyumba yao ilikuwa, kubwa kiasi yenye uzuri wa kawaida.baba yake alikuwa daktari hospitali ya muhimbili, mama yake alikuwa mwalimu wa shule ya msingi.walizaliwa watano yeye ni watatu kati ya wanaume wawili, na wasichana watatu, wakwanza ni kaka yao.alipita akamsalimia baba yake, na kupitiliza chumbani. Hakika alijikuta anawaza sana matukio, yaliyomtokea shule. " mmh!! Au vicent amepata msichana mwengine?". Alijiuliza."kama ni kweli sitakubalii kwanza sina imani hiyo, labda atakuwa na jambo lingine, ila shule ile nzima, hakuna anaenikamata kwa uzuri".alijiwazia mwenyewe,akijiuliza na kujipa majibu mwenyewe. Ila gafla aka...... Itaendelea SEHEMU YA TANO (05) ILIPOISHIA SEHEMU YA NNE: wakwanza ni kaka yao.alipita akamsalimia baba yake, na kupitiliza chumbani. Hakika alijikuta anawaza sana matukio, yaliyomtokea shule. " mmh!! Au vicent amepata msichana mwengine?". Alijiuliza."kama ni kweli sitakubalii kwanza sina imani hiyo, labda atakuwa na jambo lingine, ila shule ile nzima, hakuna anaenikamata kwa uzuri".alijiwazia mwenyewe,akijiuliza na kujipa majibu mwenyewe. Ila gafla aka...... ENDELEA. Ila gafla akakumbuka kitu. "mmh si alisema kuwa, tunawasiliana kama kawaida ngoja tuone kama itakuwa hivyo kweli". Alijisemea peke yake, vanessa huku akijiuliza, na kujipa majibu mwenyewe.kiufupi mapenzi yalisha mchanganya, hakujua afanye nini, kumueka vicent kwenye mstari. Aliwaza sana, mpka akapitiwa na usingizi,akasahau hadi kwenda kula chakula.. ****** Niram akiwa bado yupo chumbani, alikuwa ana mfikiria sana vicent, mpka akawa anajiuliza,ni kwa nini amfikirie kama vile. " mmh mbona sasa nawaza upuuzi, kipi ambacho kinanifanya nikumbuke lile tukio la asubuhi".ila gafla kuma kitu akakumbuka, kikamfanya aangue kicheko siyo cha nchi hii. "hahhhhhhahhh!! hhhah!! uwiiii mama weeeeh hhh!!". Alicheka niram kama kichaa. " hivi sasa kilichokuwa kimemgandisha mpka asiondoe gari ni nini?".alijiuliza kisha akaendelea. "maana mtu aliduwaa kama kaona ela alafu yupo pekee yake anavizia jinsi ya kuikwapua hahhhah!!".alijisemesha mwenyewe kisha akacheka tena kwanguvu. Mala mlango ukafunguliwa, Akaingia mama yake ,inaelekea ndo kwanza alikuwa anafika,maana kipochi kilikuwa kwapani. " Eeeeh!! Mwenzetu vipi unaumwa ukichaa, mbona unacheka peke yakoo?".aliuliza mama yake,huku akiwa amesimama mlangoni, kwenye chumba cha binti yake.Niram alishtuka, maana hakutegemea uwepo wa mama yake eneo lile. Ila aliuficha mshtuko wake. "Eeeeeh!! Mama bwana kuna mwalimu wetu alianguka, wakati anaingia darasani, basi nikikumbuka nachekaaa".alivunga niram huku akijifanya kuwa makini na anachokingea. "wewe mtoto shetani si bure mwalimu kaanguka ndo unacheka hivyoo haaahhhhah hatarii, haya vua hizo nguo ukale, maana nakujua wewe hapo ulipo ujala ". Aliongea mama niramu, huku anapiga hatua kwenda nje. "sawa mama naja". Alijibu niram, mara ukasikika mlango paaaaah!, alikuwa mama niramu anafunga mlango . "uhhhhhhhhuh!!"alishusha punzi ndefu niramu, maana akutegemea kama angeweza kudanganya, haraka hivyo. Alibadili nguo nakutoka kwenda kuchukua chakula.. ******* Vicent alikuwa chumbani kwake, akichezea laptop yake.huku ana kula lakini mawazo mengi, yalikuwa kwa niramu. Alijiuliza kwanini ametumbukia juu ya mapenzi ya msichana, wakihindi hakika chakula hakikulika ,alikuwa na mawazo ya hatari yaliyo mfanya, chakula aone kichungu. " ntajitahidi kumtafuta naimani ntampata tu".alijiwazia kimoyomoyo, asijue aanzie wapi, amalizie wapi.ila gafla akiwa kwenye dimbwi la mawazo, alisikia simu yake inaitaaa. Ngrrrrrrrri ngrirrrrrrr!! "nani tena huyoo?". Alijiuliza huku akijiinua kuifata ,kwenye kochi maana yeye alikuwa kitandani. " daaaah!! Anataka nini tena huyuuu aaah!!".alilalamika vicent huku anaipokea simu. "hellow vanessa". Aliongea " yes bby nimekumic nikaona nikupigie". Ilisikika simu upande wa pili alikuwa vaness. " Oooh!! Kumbe niambie". "vicent nilikuwa na kukumbusha lile ombi langu nililokuomba". " lipi hilo?".alihoji vicent huku akimsikiliza kwa makini. "ni lini utanipa penzi lako?, nashindwa kujizuia vicent". Alilalama vanessa huku akisubiria, jibu upande wa pili. "Vanessa hivi kumbe jini wako apendi amani eeh!!?".aliuliza vicent, na kabla ajajibiwa akaongeza neno. " hivi leo nilitoka kukuambia nini hivi upo serious kweli wewe?, naomba usinitibue kama unawaza ngono badala ya kusoma ni wewe mimi naomba unikaushie kabisa".aliongea kwa jazba vicent, huku mikunjo kwenye paji la uso,likionyesha ni jinsi gani amechukia. "ooh nisamehe bby, mi nilikueleza tu hisia zangu wala sitaki tugombane".alijitetea vannesa maana alijua ashaharibu. " oky nikutakie jioni njema kesho mungu akipenda" aliongea vicent, na bila kusubiri jibu simu ikakatwa. Kiukweli vanessa, alijilaumu kwanini aliongea vile, aliilaani ile siku kwani aliiona siku mbaya kuliko zote. Baada ya kukata simu, vicent alikirudia kitanda na kujibwaga bado kidogo angemwaga chakula, kwenye kitanda. " Oooohsh!! Yote sababu ya huyu mwanamkee aaah!!". Alilalama vicent, huku lawama zote akimtupia vanessa. Eti wadau ukipenda sana unaonekana msumbufuu eeeh?.. Tuendeleee.. Basi vicent akachukua kile chakula na kukiweka chini akaendelea na ratiba zake . ******** Ilikuwa muda wa saa mbili kamili usiku(02.00) vanessa alikuwa yupo selbeni na mdogo wake wa mwisho wa kike, aliitwa juliana.kifupi unaweza mwita juli, walikuwa wanaangalia tv.wengine wakiwa na mishemishe zao, huku wazazi wao wakiwa wameshaingia chumbani,maana hata muda wa kuangalia taharifa ya habari aukuwepo, kutwa watoto wanaangalia movie zao. Ndio maana mzee wao anaamua ajununulie gazeti.. Muda wote wapo sebleni ila vanessa alikuwa kimya, kama anawaza jambo. Ila juli aliiona hali tofauti aliyokuwa nayo dada yake .. "vipi dada unaumwa mbona ueleweki leo?". Swali la juli lilimshtua vanessa ,kwenye dimbwi la mawazo akawa hana jibu sahihi la kumpa akabaki, kumbabaisha tu " hamna juli mdogo wangu nawaza mitihani sijui itakuwa migumu?".alivunga vanessa na kujifanya kuuliza ili kupoteza mada. " mmmh!! Dada usiwaze mbona nakuaminia itakuwa ya kawaida muhimu usome ". Alimjibu juli, vanessa akatingisha kichwa kukubali. Ila hakukaa sana akamuaga nduguye akaingia ndani kwake. ********* Siku ya pili, vicent alitoka mapema nyumbani, aliwahi shule kabla hata ya rafiki zake. Hii yote ni kutokana hata usingizi haukupatikana,kutokana na mawazo aliyo nayo. Alikuta baadhi ya wanafunzi wapo darasani, Alifika akakaa kwenye kiti na kufungua begi,kuchukua kitabu na kuanza kusoma. Ila hata sijui nini kilimtuma kutazama mbele maaana alijikuta anatoa macho......itaendelea ... Read More
Story........ NI WEWE TU PENINA Sehemu ya kumi na mbili (12) By GIVAN IVAN Phone & whatsapp.... 0769673145 Ilipoishia.......... Penina na Frank walishangazwa Sana na maamuzi ya Nolan lakini hata hivyo Nolan hakutaka wamuulize swali lolote, alimwamuru dereva wa tax ile awashe gari na kuondoka. Kisha Nolan naye akaingia kwenye gari yake na kugeuza kuwafuata vijana wale wa the killer na wakati huo walikuwa tayari wameshaungana wote kwa maana ya kikosi kile cha kwanza kilichokuwa kikimtafuta Nolan na kile cha pili kilichokuwa kikimtafuta Frank. *********Endelea ********* Vikosi vile viwili ambavyo vilikuwa kwenye magari mawili viliweza kumuona Nolan akiwa anarudi kule alikotoka. Vikosi vile navyo haraka haraka vikageuza magari yao na kuanza kumfuata Nolan. Nolan aliweza kuwaona wakimfuatilia na ndio kitu ambacho Nolan alikitaka, lakini kilichomshangaza Nolan ni kwamba Sasa anafuatiliwa na magari mawili tofauti na mwanzo walipokuwa wakimfuatiliwa na gari moja. Lakini Nolan hakujali hilo, akaacha barabara na kukataa kushoto na kuingia kwenye njia moja ya vumbi ambayo haikuwa ikipita watu Mara kwa Mara. Nolan baada ya kuingia kwenye barabara ile akasimamisha gari na kushuka ndani ya gari lile. Na sekunde hiyo hiyo magari mawili ya vijana wale wa the killer wakawasili pale alipo Nolan na kusimamisha magari yao Kisha wote wakashuka kwenye magari yao ambao kwa pamoja walikuwa Nane. Vijana wale wa the killer walishaangaa baada ya kufika na kumkuta Nolan peke yake badala ya kuwakuta wote Nolan pamoja na Frank. Nolan alikuwa amesimama pembeni ya gari yake huku akiwatazama vijana wale waliokuwa wakimsogelea taratibu. "mwenzako yuko wapi?" kijana mmoja wa the killer akamuuliza Nolan huku akijaribu kumkamata Nolan kwenye shingo. Kijana yule alijikuta akipokea ngumi Nzito ya tumbo kutoka kwa Nolan ambayo ilimfanya adondoke chini kwa magoti. Wale vijana wengine walishtuka kuona mwenzao alivyotandikwa ngumi ya tumbo. Lakini hata hivyo bado vijana wale waliamini Nolan hawawezi kwasababu wako wengi na wote wana silaha. Vijana wale kwa pamoja wakaanza kumfuata Nolan, Nolan naye akapiga hatua kadhaa na kurudi nyuma na kuwasubiri. Vijana wale walipomkaribia Nolan kwa pamoja wakaanza kurusha ngumi na mateke kumvamia Nolan. Lakini Nolan alikuwa akiwakwepa tu bila kumgusa mtu yoyote, ndani ya dakika tano Nolan alikuwa akiwakwepa vijana wale waliokuwa wakimshambulia bila mafanikio. Lakini Nolan alizubaa kidogo na kujikuta akipokea ngumi Nzito ya uso kutoka kwa mmoja wa vijana wale. Lakini hata hivyo kijana yule aliyembahatisha Nolan ngumi ya uso ikawa ndio mwisho wake wa kuishi duniani, kwani Nolan alimkamata na kuanza kumshambulia kwa ngumi za haraka haraka na kummaliza kwa kumvunja shingo. Wale vijana wengine ndio walishtuka vibaya mno na kuona huyu mtu sio wa kawaida, wakaamua wamshambulie kwa silaha zao baada ya kuona hawatamuweza kwa mkono. Vijana wale walichomoa bunduki zao na kuziweka tayari kummaliza Nolan. Lakini Nolan alikuwa tayari ameshaingia kwenye gari na kuondoka kwa spidi kali na kuwaachia vumbi kali Vijana wale. Nolan aliamua kukimbia baada ya kuona vijana wale wakitoa bunduki zao, hivyo asingewaweza kwa sababu yeye hakuwa na silaha yoyote. Vijana wale nao hawakumuacha waliingia kwenye gari na kuanza kumfuatilia Nolan. Lakini mpaka pale Nolan alikuwa tayari ameshawapoteza vijana wale na yeye Sasa alikuwa ameshika njia ya kuelekea nyumbani. * Mzee Joel akiwa ameketi sebuleni kwake akisubiri majibu ya kuuwawa kwa Frank na Nolan simu yake ilianza kuita na alipoangalia mpigaji ni nani alikutana na Jina la Dickson, kijana ambaye mzee Joel ndio anataka amuoe mtoto wake Penina. Mara moja mzee Joel akaipokea simu ile. "mzee Joel habari yako?" akauliza Dick baada ya simu yake kupokelewa na mzee Joel. "salama kijana wangu habari ya huko"? Akajibu mzee Joel na kuuliza. " huku Safi tu, Sasa mimi nilikuwa nataka nije kumchukua Penina moja kwa moja nahitaji kuwa na familia Sasa. " akaongea Dick kumwambia mzee Joel. " kijana wangu usiwe na haraka tunaweka mambo Sawa na Muda wowote tutakuita uje umchukue mke wako. " akaongea mzee Joel kumpa moyo Dick. " unaweka mambo Sawa unaweka mpaka lini kama ni pesa nikekupa za kutosha mbona unanizungusha zungusha tu au nikuongezee pesa zingine? " akaongea Dick huku akionesha kuchoshwa na namna mzee Joel anavyomzungusha. "kijana wangu tafadhali naomba utulie Penina ni wako usiogope." mzee Joel akamwambia Dick. "nitulie nitulie mpaka lini nakuja Tanzania kujua Kwanini unanichelewesha kumuoa Penina na wakati nimeshakupa pesa nyingi Sana." akaongea Dick na kukataa simu. Mzee Joel alihisi kuchanganyikiwa hakujua afanye nini ili aweze kumuunganisha Penina na Dick. Na wakati huo huo mlango ulifunguliwa na akaingia Nolan huku akiwa amechafuka kwa vumbi. "Wewe mbwa mbona unaingia ndani kwangu bila hodi?" mzee Joel akamuuliza Nolan huku akiwa amevimba kwa hasira. "mzee tulia huu mchezo umeutaka mwenyewe lazima Frank amuoe Penina." akaongea Nolan maneno hayo ambayo yalizidi kumpandisha hasira mzee Joel na kujikuta akimrushia Nolan glass ya maji iliyokuwa kwenye Meza. Nolan aliigonga ngumi glass ile na kuipasua pasua. "ukiniletea upuuzi na wewe nitakupasua pasua kama hiyo glass." Nolan akamwambia baba yake mzee Joel na kuelekea chumbani kwake. * Frank na Penina baada ya kufika uwanja wa ndege walifuata taratibu zote na hatimaye wakafanikiwa kuingia ndani ya ndege na dakika chache baadae walikuwa angani wakielekea South Africa. "kama tukifanikiwa kufunga ndoa nitafurahi Sana yaani furaha nitakayokuwa nayo sidhani kama itaelezeka." aliongea Penina huku akiwa amejiegemeza kwenye kifua cha Frank. "usijali mpenzi kila kitu ambacho kinatokea kimepangwa na Mungu na vitakavyotokea mbele ni Mungu pia anajua, hakuna mwanadamu asiyependa furaha." akaongea Frank kwa upole kumuambia Penina. "ni kweli mpenzi wangu." akajibu Penina na safari ikaendelea kwa masaa kadhaa na hatimaye wakawasili South Africa Katika jiji la Johannesburg na kuchukua chumba Katika hoteli moja ya kifahari. Baada ya kupumzika kwa dakika kadhaa Penina na Frank waliwasiliana na Nolan na kumjulisha jinsi safari yao ilivyokuwa. Nolan aliwataka wakae kwa amani na wasiwe na hofu yoyote yeye anaweka mambo Sawa na yakiwa tayari bas atawajulisha. * Vijana wa the killer bado walikuwa wakimtafuta Nolan na Sasa waliwasili nyumbani kwa kina Nolan na kukutana na mzee Joel ambaye aliweza kuwaambia Nolan yupo ndani na akawaelekeza chumba chake wakammalizie huko. Vijana wale taratibu walianza kuelekea Katika chumba cha Nolan, lakini kwa bahati mbaya ama nzuri Nolan aliwaona. "mmeamua kunifuata mpaka nyumbani nyie mmeisha." akajisemea Nolan Kisha akatoka chumbani kwake akiwa kifua wazi na kukutana na vijana wale sebuleni. Kilikuwa kitendo cha kushtukiza vijana wale hawakutarajia kukutana na Nolan sehemu Ile. Kitambo waseme waweke silaha zao tayari Nolan alianza kuwashambulia, na baada ya dakika chache Nolan aliwaweka vijana wale wote chini kwa kuwavunja vunja sehemu za miili yao. Mzee Joel ndio hakuamini baada ya kuingia ndani na kukuta vijana wote wamelazwa chini alafu kidogo hivi akatokeza Nolan akiwa amepigilia suti nyeusi Kisha akamwambia baba yake ambaye ni mzee Joel, "naenda kwenye kikao cha harusi ya Penina na Frank na kama utahitaji kadi unijulishe nikuletee ya kwako." ....... Itaendelea. ... Read More
CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA KWANZA (01) Ilikuwa alfajiri moja nyepesi, katika jiji la dar-es-salaam, katika mtaa mmoja tulivu sana mbezi beach, dio kwanza nikama pilika zilikuwa zinaanza, yalionekana magari machache ya kifahari, yakikatiza kwenye viji barabara vya mtaa, na kupoteea barabara kuu, watu wakikwep foleni kwa kuwai makazini na mashuleni, au sehemu mbali mbali za kijamii, mapema namna hii, huku watu wachache walio tembea kwa miguu wakionekana wakitembea haraka kuelekea barabarani, Ndani jumba moja la kifahari lililo zungukwa na uzio(fensi) wa ukuta mkubwa, ilisikika sauti ya msichana mmoja, mrembo mwenye asili ya Kihindi akiongea na mama yake, ilionekana alikuwa anataka kutoka. "mama mi naondoka naenda shule, maana kuna mitihani muhimu nawahi ingekuwa bila ya hiyo mitihani nisingeenda" alisikika binti mwenye sauti kinanda, akimwambia mama yake, ambae pia, ni mwenye asili ya Kihindi,japo alionekana ni mama wa makamo, lakini akika alifanana na binti yake., maana unge weza kuona uzuri wa mama huyu, japo tayari alisha kuwa mkubwa, "basi haya, chukua gari hiyo nyeusi, uwahi mwanangu" alisema mama huyu huku anawonyeshawanae funguo ya hili gari alilo mtajia, "hapana mamy, ntaomba lifti huko huko, leo sijisikii kuendesha" alijibu binti mrembo, huku akichukuwa begi lake juu ya meza na kuanza kuondoka, akiufwata mlango mkubwa wa kutokea nje. "haya basi baadaye mwanangu, jitazame huko uendako" aliongea mama huku anamsindikiza kwa macho binti yake, ambae toka akiwa mdogo amekuwa nae makini sana, ungesema amezaliwa peke yake, "ok mumy" alijibu binti chotara, huku anainua mkono wake na kuchezesha vidole, akimaanisha ana mpungia mkono mama yake, kisha akatoweka. Naam huyu ni binti mrembo NIRAM, ni binti wakihindi, mwenye sura nzuri ya kuvutia, macho ya duara, pua iliyochongoka vizuri, mwenye midomo mipana ambayo kila anapo tabasamu, basi uacha vijishimo mashavuni mwake, alikuwa na urefu wa futi tano, na pointi kadhaa, kifua cha wastani na tumbo dogo, kiuno chake kilibeba makalio ma nene kihasi na pia, vi hips vya kumwagika vilivyojazia na kuchomoza pembeni, vilizidi kumpendezesha, asa anapokuwa katika mwendo, kiufupi mdau wa story hii, ilikuwa si rahisi upishane nae, ushindwe kumgeukia, iliuone uumbaji. Huyu anaitwa Niram Popat, baba yake ni mfanya biashara mkubwa, na kwa sasa yupo nchini Uingereza, kwa shughuli zake za kibiashara, binti huyu akualiwa peke yake, Niram alikuwa na kaka yake, ambae kwa sasa yupo chuo kikuu cha Indira Gandhi nchini india akijichukulia masters yake, kifupi katika familia yao wamezaliwa wawili tu! yani yeye na kaka yake, Niram alipendwa kuliko kawaida. Hiyo ndo historia fupi ya niram, ebu tuendelee na kisa hiki cha Chaguo langu, Niram alitembea taratibu akiongozana na watu waliokuwa wanaelekea huko kwenye kituo cha dala dala, dakika chache baadae, Niram alifika kituoni, nakuwakuta watu wengi wakisubiri usafiri,binti huyu, alijitenga pembeni kabisa na abiria wengine, usafiri ilionyesha ulikuwa wa shida sana siku hiyo, maana magari yalifika pale yakiwa yamesha jaa, hivyo waliofanikiwa kupanda, walijibana kama nyanya kwenye matenga, Niram alijikuta ana kumbuka gari ambalo amelikataa nyumbani,”haaa, kwanini niliamua hivi?” alijilahumu binti huyu mzuri, ambae asilimia tisini ya wanaume waliokuwepo pale, walikuwa wanamkodolea macho, wakisanifu uumbaji, Lakini wakati anawaza hayo,mara ghafla ilisimama range nyeusi, mbele yake na paka shushwa vioo, ilionekana sura moja matata sana, ya mwanaume mtanashati, hakika alifaa kuitwa handsome wa Kiafrika "hellow" yule kijana ndani yagari alimsabahi Niram, nae akajibu kwa kichwa, yule jamaa akatabasamu kidogo, "naweza kukupa lifti? Aliuliza kijana yule. na Niram akuwa mbishi, aliitikia kwa kichwa kama kawaida yake, hapo ukafunguliwa mlango Niram akaingia. na kufunga mlango, sasa akawa ametulia kwenyeseat yake, huku macho mbele, akitegemea kuona gari linaondoka, na maswali yanaanza, lakini zika pita dakika kadhaa na gari halikuondoka. Muda wote haku endesha gari, alikuwa ameduwaa, kumshangaa msichana alie ingia garini mwake. Alizidi kushangaa "sorry kaka mimi nashuka vituo vinne mbele ndipo ilipo shule yetu"aliongea niram. Maskini kijana yule aligutuka, akababaika huku anaondoa gari, "oooh! aaagh sawa unasoma shule ipi dada?" aliongea huku gari ikienda taratibu "shadhiliya slamic internation school" alijibu Niram, "ooh ile shule ya kiislam "aliuliza kijana. "yap! nasoma kidato cha tano pale" alijibu niram "ok mi mwenyewe nasoma pale st joseph international school kidato cha sita "alisema kijana "aah kumbe" alisema Niram kwa uchangamfu kidogo, akiona kuwa yupo na mwanafunzi mwenzie, "ndiyo ninaitwa Vincent, sijui naweza kulijuwa juna lako kama hutojali?" aliuliza Vincent huku anatabasamu, kidogo wengee lilianza kumtoka, "mimi naitwa Niram..” alisema Niram lakini kama alistuka kidogo, “ooh! kaka nishushe unapitiliza" aliongea niram kwa mshtuko "ooh sorry, kwa kweli" alijibu Vincent,huku ana peleka mguu wake wkulia katikati na kukanyaga bleack, akippunguza mwendo na kuweka gari pembeni ya barabara, kisha akasimama, Niram alishuka, na akashukuru Vincent kwa kupitia kwenye dirisha la upande aliokaa, na kuondoka zake. Vicent alibaki kaduwaa, maana alishangazwa na uzuri wa aina yake, kwa yule msichana. "daah nimesahau kuomba namba" alijilahumu Vicent, lakini hakuwa na lakufanya, akawasha gari akasepaaa. Anaitwa Vicent Ngosha, ni mtoto wa mzee Emanueli Ngosha mfanya biashara mkubwa nchini Tanzania na nje ya nchi.Vincent alikuwa ni mvulana wa kisukuma, mama yake ni muhaya, Vicent ni mtoto pekee kwenye familia yao, ni familia yenye uwezo mkubwa, baba yake alikuwa mkoani kibiashara, hivyo alibaki pale nyumbani na mama yake, pamoja na house girl, Vicent alifika shuleni akiwa na mawazo lukuki, “ok! mdau huu nimwanzo wa mkasa huu wakusisimua, ...... CHOICE OF MY HEART (chaguo la moyo wangu) SEHEMU YA PILI (02) ILIPOISHIA SEHEMU YA KWANZA : Anaitwa Vicent Ngosha, ni mtoto wa mzee Emanueli Ngosha mfanya biashara mkubwa nchini Tanzania na nje ya nchi.Vincent alikuwa ni mvulana wa kisukuma, mama yake ni muhaya, Vicent ni mtoto pekee kwenye familia yao, ni familia yenye uwezo mkubwa, baba yake alikuwa mkoani kibiashara, hivyo alibaki pale nyumbani na mama yake, pamoja na house girl, Vicent alifika shuleni akiwa na mawazo lukuki. ENDELEA......... Vincent alifika shule akiwa na mawazo kibao. Aliwaza kwamba alikutana na jini au mtu wa kawaida, hakika alikuwa hayupo sawa alishachanganywa na mtoto wa Kihindi, akujua afanye nini ili aweze kuwa karibu na binti yule, akika Vicent likuwa katika wakati mgumu, alijikuta anatembea bila kujielewaakinyoosha moja kwamoja mpaka darasani, “dah! nime kuwa mjinga sana, ninge omba namba, mbona demu alikuwa poa kabisa” alijilahimu Vicent, akiwa amekaa kwenye kiti chake, na kuegemea meza, kama vile anataka kulala, "hey! niggar vipi mbona umezubaa mwanangu?, yani tumekutafuta pande zote, mpaka kule bustanini, kumbe umekuja kujichimbia class, tena hata assemble ukuja" Vicent aligutushwa kidogo na kuinua kichwa kumtazama alie msemesha, japo sauti alisha itambua, kuwa alikuwa Richard, ni rafiki kipenzi wa vicent, nikama Vicent aliganda kidogo, akimtaza Richard, ambae alishangazwa na rafiki yake,Richard akageuka nakumtazama kijana mwingine alie kuwepo pembeni yake, "vipi Rich mbona leo amepoa sana, yani kama amemwagiwa maji, unanini wewe?" alidakia suma rafiki yake mwengine. maana awakumuelewa mwenzao, Vincent akujuwa amjibu nani kati yao, na awajibu nini, hivyo aliishia kutabasamu kisha akajikohoza kidogo, na kuanza kuwaambia "yani leo najiona kama nipo ndotoni, kwa nilichokutana nacho" ilikuwa sauti iliyo jaribu kuonyesha msisitizo wakile anacho kiongea, "hahahahaha! kashaanza sound zake huyu" alisema suma, huku wote wanacheka,kabla mmoja wao ajakumbuka jambo, "hoya! alafu nimekumbuka, Vannessa alikuwa anakuulizia" aliongea Richard, kama unge msikia unge juwa kuwa huyo Vannesa, alikuwa anainshu muhimu sana na Vicent, maana aliongea kwa msisitizo, "mmh! yani huyo Vanessa naomba usinitajie, maana leo ana nafasi ya kuzungumziwa hapa" alisema Vincent, ila kabla ya kuongeza neno, mara ikasikika "waoooh! jaman baby nilikutafuta huko nje kotesijakuona" wote watatu wakageuza shingo zaona kutazama upande wa mlangoni sauti iliko tokea, macho yao yaka mshuhudia binti mrembo wa ki afrika, alie kuwa anatembea taratibu kuja pale walipo kuwepo wakina Vicent, huyu ni Vanessa alie zungumziwa, “mpaka nikawa na wasi wasi kuwa leo auto kuja” aliongea tna Vanessa, kwa sauti iliyojaa furaha na mania moyoni, Wakati hiuo tayariwanafunzi walishaanza kuingia darasani, Vanesa alienda moja kwa moja mpaka kwa Vicent na kumkumbatia kwa furaha, lakini cha kushangaza kijana huyu akuonyesha ushirikiano, ushirikiano kwa mrembo Vanessa, "baby una nini leo?" alihoji vannessa.kwa mshngao huku anajitoa kwenye kumbatiao lake kwa Vicent, "sina kitu"lilikuwa jibu la mkato,toka kwa Vicent, "sasa kwanini huko hivyo?" aliuliza tena Vanessa, kwa sauti iliyoanza kubadirika na kunyongea, huku wezao wakiwatazama, yani Richard na Ismail wenyewe wana mwita Suma, “nimekuambia niko sawa, unielewi wewe unataka nikuambieje” safari hii Vicent aliongea kwa sauti ya juu, iliyo jaa ukali wa wazi, kihasi cha kulitikisa darasa zima, sekunde kadhaa, wtu wote kimya, wakigeuza shingo zao na kuwatazama wakina Vicent, kwa mshangao. Kitendo hiki akikuwashangaza walewanafunzi wenzao peke yao, ata Richard na Ismail, nao walishangaa, Vanesa alitanzana chini kwa aiu, maana macho yake haya kuweza kutazama, macho ya wanafunzi wenzake me darasani, tenamacho hayo yalishindwa kuya zuwia machozi, ambayo yalianza kumtoka, akika binti huyu, akashindwa kuendelea kusimama mbele ya mvulana ambe sikuzote ame nae karibu, hivyo akageuka na kuondoka zake, huku anakimbia, akielekea nje ya darasa, "una nini mwanangu, mbona kama umeurugwa?" alihoji Richard, huku suma akidakia "mbona si kawaida yako mshikaji wangu" akika wakina Suma walionekana kusikitishwa na kitendo kile, ambacho awakukitarajia, kutokana na ukaribu wa wawili awa, hapo Vicent alikuwa ametulia nikama anawaza jambo, kisha akainua usowake taratibu, "sikilizeni niwaambie washakaji, mimi toka zamani niliwaambia kuwa, Vanesa simpendi, nyie mkasema ooh! mkubalie sijuwi hooooh! mtoto mzuri yule, et! shule nzima wanamfukuzia, bahati imekuja kwako, mala ooh! sasa nimegundua leo kuwa, mwanamke ninaempenda yupo, tena nimemuona, kwa macho yangu" alijibu vincent.marafiki zake wakatazamana kwa mshngao, huku wakimsikia Vicent anaendelea, "leo nimekutana na mwanamke ambae naweza sema ni wa ndoto zangu, sijawahi kujihisi hivi kabla, ila kwasasa ndo naanza kuhisi nimependa kwa mara ya kwanza" Vicent alizidi kuwashangaza marafiki zake, lakini kabla ajawaeleza zaidi juu ya mtoto wa Niram, mara Mwalimu akaingia darasani, na mazungumzo yakaisha kwa muda huo. ****** Vanessa ni binti mmoja mzuri mwenye sura ya duara macho ya kusinzia ana kimdomo furahi hivi cha rangi ya pink, nyuma amefungashia balaha, kiasi cha kupendezwa na kunguo yoyote atakayo ivaa, kifupi kila mwanaume, iwe mtaani au hapa shuleni, alikuwa anammezea mate, na rangi yake ya chocolate ndo kabisa, ilichangia uzuri wake kwa kwa kihasi kikubwa, ikichangia na urefu wake wa wastani,ila binti huyu Vannesa alivutiwa sana vincent mpaka akawa anashindwa kujizuia, japo alikuwa akisumbuliwa na wanaume wengi hadi walimu ila yeye limfanya Vicent kuwa ndie mwanaume wa ndoto zake, Vannesa alijitahidi kufanya kila njia na ushwishi, mpaka akafanikiwa kumfata na kumwambia, ukweli kijana huyu, Ilikuwa ni vigumu kwa vicent kukubali, maana hakuwahi kumpenda msichana, na hakujua afanye nini, ila vishawishi vilimfanya akubali, kwa maana yeye aliona labda ndo inavyokuwa mapenzi yapo hivyo, japo alisumbuliwa na wanawake wengi, ila vicent akuwahi kujihusisha na msichana yeyote yule. Kwahiyo Vanessa ni mwanamke wake wa kwanza, kimahusiano, lakini leo tangu amekutana na Niram alijihisi tofauti, yani kama kuna kitu kina Uchoma moyo wake, hapo ndipo alipojua kuwa, kumbe sasa huku ndiko kupenda kwenyewe, maana ukiachilia kuwa alisha ona waschana wazuri wengi katika maisha yke, yaliki yule binti alimwingia sana moyoni mwake, na kuivuruga hakiri yake, Vanessa aliingia darasani kwao, huku akifuta machozi, kwakutumia kitambaa chakechepe, akiofia wenziewasije wakaona, na kugundua kuwa alikuwa analia, hilisiyo darasa ambalo Vincent yupo, maana walisoma madarasa tofauti, licha ya kuutamachozi na kujaribu kujizuwia kulia, lakini aikuwezekana, maana donge la uchungu lilikuwa lime laa shingoni mwa Vanessaalijikuta anashindwa na kuendelea kuangua kilio cha kwikwi, Vanesa aliwai kwenyekiti chake na kukaa, huku akijizima uso kwakuegemea kwenye meza, akizuwia na mikono yake miwili, ilimuuma sana binti huyu, akika machungu haya ya ghafla, sizani kama nitaweza kuya eezea, "nimemkosea au anipendi tena" alijiwaziwa kimoyo moyo, binti huyu, huku machozi yakizidi kutililika machonimwake na kulowesha mikono yake,mala akastuka kunamtu akimshika begani,aka jifutamacho ziharaka na kumtazama alie mshika begani, "Vanessa una nini, mbona unaonekana kama umetoka kulia" aliuliza Maria, rakifi yake na Vanessa, huku anakaa chini kwenye kiti chakee, pembeni ya Vanessa alimwangalia rafiki yake kwa macho yenye majonzi, hakika kama ungemuona usingetofautisha na mtu aliefiwa, alinyongea kupita kiasi."Maria sijui nimemkosea nini vicent amenikaripia kama mtoto mdogo" aliongea Vanessa kwasautia mbayo nikama kilio kilitaka kurudi upyaa, ila alijitahidi kukizuwia, akaendelea kuzungumza "nilimtafuta sana nje, sikumuona, baada ya kuzunguka kwa muda mrefu, ndo likanijia wazo la kumfata darasani kwao, hakika niliingia kwa bashasha ila nikapokelewa kwa hasira na dharau" mpaka hapo Vanessa alishindwa kuendelea nakuanza kulia kwa kwikwi, ilibidi Maria aanze kumbembeleza kwa kumpiga piga mgongoni, inaonyesha wanafunzi wengine awakujuwa kunacho endelea kwa Vanessa, maana kila mtu aliendelea na mambo yake,******** Mida ya saa nne, ndani ya viunga vya Shadhiliya slamic internation school, yani shuleni kwa kina Niram, mambo yalikuwa shwari, ulikuwa wakati wa mapumziko, wanafunzi walikuwa wametawanyika kwenye viunga vya shule, mida hii binti mrembo Niram, alikuwa na rafiki zake watatu ndani ya canteen ya shule, wanapata chai, mara Niram akawa kama amekumbuka jambo fulani. "jamani mwenzenu leo nimepewa lift na kijana mmoja wa Kiswahili, lakini mzuri sijapata kuona" kabla ajamaliza kuongea binti Niram, akadakia shira huyu nae ni jamii ya kina Niram yani ni muhindi pure kasoro, hawa wengine hajra na Salma, ni tofauti, wakati Salma alikuwa mpemba mweusi, ila Hajra alikuwa Mwarabu kabisaaaaa, "ahhhhh usitake kusema umempenda mswahili, hivi mzee Popat uta mbebea mbebeo gani?, si ata kuchinjaa" alisema Shira, na hapo vikafata vicheko kwa woteee, kasro Niram peke yake ambae alisema, "wala sina mpango huo, ntampeleka wapii mimi, ila nimemsifiatu! sababu katika wavulana niliowai kuwaona, kwa hapa mtanzania, yule kaka ni handsome sanaa" alisema Niram huku anawaangalia marafiki zake, ambao wakakubaliana nae, kwakiikisa vicwavyao juu chini, na wakati huo kengele ya darasani ikagongwa, wakasimama tayari kwa kuanza safari ya kuingia darasani itaendelea ...... ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: