AISHA SEHEMU YA - SITA STORY - @⁨Glory😘🥀💫⁩ ILIPO TOKA SEHEMU YA TANO : “mh! huyu atakuwa shangazi, mbona sijawai kumwona?” Aisha alijiuliza na kukosa jibu, akapanga kumwuliza baba yake akirudi kutoka ofisini kwake, ilikuwa saa nane mchana baba Aisha alikuwa ameshaingia nyumbani na kupokelewa na mwanae ambae kwa sasa alisha mfanya mke, akakaribishwa mezani kwa chakula, wakati wana kula ndipo haisha akaona bola aulize swali lake “Baby eti mimi nime fanana na nani?” swali hilo lilimstua baba Aisha lakini akazuga kiume. endelea..... kisha Baba Aisha akamwuliza mwanae “wewe unazani umefanana nanani?” hapo Aisha akainuka bila kusema kitu zaidi yakutabasamu, akaingia chumbani kwao baadaya dakika chache alirudi na picha mkononi akamwonyesha baba yake “ nimefanana na huyu hapa, sijuwi nishangazi au mama mdogo, mimi sijawai kumwona” Aisha alimpatia ile picha baba yake, ambae aliitazama kidogo kisha akaiweka pembeni huku akionekana uso wake umebadilika kidogo, nakuwa wautulivu sana ukutawaliwa na mawazo “ilikuwa lazima umjuwe, subiri tumalize kula nita kuelekeza vizuri” Aisha aliiona hali ya baba yake usoni, ikamtia wasi wasi akizani labda nimmoja wa dada zake labda amefariki au alipatwa nakitu ambacho kinamuumiza baba yake “baba kwani kuna tatizo juu ya hii picha, mbona umekuwa hivyo” Aisha alimchezea nywele za kisogoni baba yake ambae alitabasamu kidogo, kisha akamgeukia mwanaae nakumbusu shavuni “hapana Aisha husijari nitakuelezea vizuri” hapo Aisha akatulia na kuchukuwa kipande cha kuku wa kukaanga aka mlisha baba yake naye aka fanya hivyo, ***** Ilikuwa zamani kidogo, wakati Emili na Jackline wakiwa na miaka minne toka waanze kuishi pamoja kama mume na mke, maisha yao yalikuwa ni mazuri sana, maana walikuwa nivijana wenye uwezo mkubwa kifedha, walimiliki kapuni kubwa ya uuzaji na usambazaji wa vifaanya ujenzi, na furniture za majumbani, kwa fedha walizo ingiza kutokana na kampuni yao, walifanikiwa kujenga nyumba moja kubwa ya golofa moja maeneo ya mbezi ya kimara, ambayo mpaka sasa anaishi humo, pia walimiliki gari tatu nzuri za kifahari, kabla yakuongeza nyumba nyingine mbili kubwa maeneo ya kibamba mloganzila, lakini Tatizo likawa moja kwao, lililoanza baada ya Jackline kuumwatumbo lililo sababishwa na kuaribika kwa ujauzito, ambapo alifanyiwa upasuaji uliosababisha kuondolewa kwa mfuko wa uzazi, na kumfanya Jackline apoteze uwezo wakushika mimba tena, lakini jambo hilo alikusababisha mapenzi yao kupungua, kiukweli Emili alimpenda sana mkewake Jackline, japo walijaribu kuangaika kutembea kwa madaktari bingwa ilikujuwa namna yauwezekano wa Jackline kupata ujauzito, lakini haikuwezekana kilicho fanya waendelee kuangaika nikwamba Jackline aliamni hiposiku mumewake ange tamani mtoto, hivyo ange chepuka nakutafuta mtoto, naingekuwa mwanzo wa kuaribika kwa ndoa yao, lakini mume wake alimpa moyo kuwa hasingeweza kufanya jambo hilo, hapo walipo kuwa wanaishi, Jirani karibu na nyumba yao kulikuwa na binti mmoja alikuwa amepanga kwenye myumba ndogo pamoja na wenzake wawili, binti huyu aalikuwa mrembo sana, aliitwa Jasmini mwenyeji wa nchini Kenya mji a mombasa, alikuja tanzania kutafuta maisha pamoja nawenzake, kazi yao kubwa ilikuwa kuuza bar kubwa hapa mjini Dar es salaam maeneo ya kinondoni, katika kufanya kazi hiyo ya kuuza bar akiwa counter akama muuzaji mkuu, nahii ilitokana na uzuri wake na urembo wake, nandio uliomsababishia akakutana na mzee France Nampo nakuanza urafiki wakimapenzi, France Nampo alikuwa ni mtu mzima tofauti na wakina Emili ambao walikuwa vijana wadogo, ungeweza kukadiria binti yake wakwanza alikuwa na umri sawa na Jasmin, France napo licha ya kuwa na uwezo kifedha pia alibahatika kupata mabinti wa tano bila mtoo wa kiume, na alisha kata tamaa ya kuzaa na mkewake maana mkewak umri ulishaenda, mapenzi ya mzee Nampo na Jasmin yali pambamoto huku mala kwamala akija na kulala pale alipo panga binti huyu jirani na wakina Emili, kadri siku zilivyo zidi ndipo tamaa nyingine ika jitokeza mzee Nampo akaitaji kuzaa na Jasmini akidai anaitaji mtoto wa kiume, wakumlithi jina lake, akitoa ahadi nyingisana za kumlea mtoto huyo, aikupita mda mrefu Jasimin akapata ujauzito, ilikuwa furaha kwa wote, japo wenzake na Jasmin, walimshauli kuitoa mimbahiyo kwamba wanaume hawaaminiki, lakini ilikuwa sawa na kumpigia mbuzi gitaa, miezi ilikatika, mzee Nampo akiendelea kumhudumia Jasin kwa kila kitu, maana atakazi alisha msimamisha kule bar, mpaka miezi tisa ikatimia, hapo ndipo patamu,maana mambo yalibadirika baada ya mtoto kuzaliwa, amini usiamin Jasmin alijifungua mtoto wakike, NAAM UTAMU UNAENDELEA, I

at 10:43 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top