STORY YA KWELI YENYE FUNDISHO (Ni story ya mapenzi iliyotokea kweli) ......KATIKA kijiji kimoja hivi wilaya UYUI mkoa wa Tabora,Palikuwa na mtu aliefahamika kwa jina KAPAYA. Kapaya alioa mwaka mmoja uliopita na alibahatika kumuoa mwanamke aliefahamika kwa jina la Elizabeth. Kapaya alimpenda sana mkewe na alikuwa mwaminifu sana na alimjali kwa kila kitu licha ya kuwa na kazi ya ulinzi.Lakini mambo yalikuwa tofauti kwa Eliza licha ya kuhudumiwa kila kitu na kupewa upendo na kapaya lakini bado hakulidhika. SIKU moja Kapaya katika kazi yake ya ulinzi alikuwa zamu ya usiku(Night),Aliondoka mida ya saa kumi na mbili na kumuacha mke wake kwa ajili ya kwenda kukamilisha majukumu yake ya ulinzi katika duka moja kubwa lililokuwepo pale kijijini. Wakati ulinzi unaendelea akiwa na wenzake wawili takribani mida ya saa nne usiku kichwa kilianza kumuuma.Alianza kulalamika maumivu ya kichwa sana mbele ya wenzake,Ndipo wenzake walichukua jukumu la kumruhusu aende nyumbani akapate matibabu na kulala ili hali ikae sawa na kumuambia kuwa wao wapo hapo watamalizia lindo mpaka asubuhi. Kapaya baada ya kupewa ruhusa na wenzake huku maumivu ya kichwa yakiwa yanamsumbua alichukua baiskeli yake halaka sana angalau hata akachimbe mizizi ya mwarobaini anywe kutuliza maumivu maana ilikuwa tayari ni usiku na maduka mengi yamefungwa kama kawaida ya kijijini kufunga maduka mapema. KAPAYA alifika nyumbani kwake mida ya saa sita kutokana na umbali uliopo toka anapolindia na nyumbani kwake,Cha ajabu alipofika nyumbani na kupiga jicho kwenye dirisha la chumbani kwake aligundua kuwa kibatari bado kinawaka,Alijua labda mkewe atakuwa amesahau kukizima alisogea karibu zaidi na dilisha ili amuamshe na hapo ndipo aliposhtuka zaidi na mapigo ya moyo kuanza kwenda mbio kitendo kilichosababisha mpaka hata kutosikia maumivu ya kichwa,Alisikia sauti ya mahaba ya mke wake akiwa anatoa penzi kwa mwanaume mwingine,Moyo wake uliumia sana akajikuta anakosa kwanza la kufanya kwa hasira,Sauti ya kimapenzi ya mke wake eliza ilizidi kumuumiza masikioni aliondoka upande wa ndirisha na kuelekea upande wa mlango kisha kuuvunja. Wale waliomo ndani walishtuka kwa presha na Eliza hakuamini kuona sura ya mme wake imeingia ndani,Pale pale Eliza akazimia na Utamu wake. KAPAYA kwa kama dakika tano alibaki anamwangalia yule jamaa aliekuwa akifanya mapenzi na mke wake na akamjua kuwa ni moja kati ya mwanakijiji mwenzake aliefahamika kwa jina la Omary.Wakati huo Omary alikuwa akilia na kupiga magoti mbele ya kapaya kuomba msamaha kwa kile alichokifanya,Alijua kabisa sasa siku zake za kuishi duniani zimefika kikomo kutokana na kukutwa na mke wa mtu.Kapaya hakutaka kutumia hasira,Alifumba macho yake na kutuliza hasira kisha akafumbua kinywa na kuanza kuongea"Omary mwanakijiji mwenzangu,Wewe ni ndugu yangu halafu tunafanyiana hivi kweli?.Hivi unajisikiaje kumfanyia haya mwanaume mwenzio je ni sahihi?,Kwani kuna wanawake wangapi hapa kijijini kwanini usioe wa kwako?,"Kapaya aliongea maneno mengi huku akilia kwa uchungu na wakati huo pia omary alitoa chozi la uchungu kwa kuomba msamaha.Omary hakuamini kusikia sauti inayotoka kwa Kapaya."Kosa sio lako ni kosa la mke wangu anajua kabisa kuwa ameolewa lakini bado anakubali mwanaume mwingine,najua sisi tabia ya wanaume ya kutongoza tongoza hivyo ni mke wangu ndio alikuwa na jukumu la kukukataa na kwasababu sijakukuta unabaka bali alikubali mwenyewe na kukuingiza chumbani kwangu basi wewe nenda nimekusamehe,Niache na mke wangu tutamalizana".Omary hakuamini kusikia sauti ya "Nimekusamehe"Aliona kama ndoto maishani,alitoka kwenye ile nyumba huku anajikwaa na kuanguka na aliposhika njia alikimbia kama kipanga alieona mzoga wa kuku kifaranga. Kapaya alimwangalia mkewe aliekuwa kazimia pale kitandani,Alimshika na kumlaza vizuri kitandani,Wakati anamtengeneza ghafla mke wake akashtuka alipokumbuka tukio Eliza alianza kulia sana huku akimuomba msamaha Kapaya. Kapaya akiwa anatengeneza shuka ili ajifunike alale alisema"Nimekusamehe mke wangu tulale".Eliza hakuamini kusikia ile kauli bado alizidi kulia kuomba msamaha hakutaka kuamini kama kapaya amemsamehe kirahisi rahisi tu.Kapaya alimshika mke wake na kumlaza kitandani tena kisha kumfunika shuka na kumwambia tulale mimi nimekusamehe.Eliza alinyamaza kuongea na kutulia lakini mawazo yote yakiwa anawaza je Mumewe ataamua nini usiku ule.Eliza hakulala alibaki tu akimwangalia kapaya ambae alikuwa tayari akakoloma kwa usingizi kutokana na homa aliyokuwanayo.Eliza aliendelea kuwaza usiku mzima itakuwaje,Muda mwingine aliwaza huwenda anamtafutia target ili alale amuue kitendo kilichosababisha Eliza asilale kabisa mpaka asubuhi. Asubuhi kulipokucha waliamka na Eliza kuanza tena kuomba msamaha,Ikabidi kapaya amwambie"Mke wangu nimekusamehe na staki kusikia tena unaongelea habari za msamaha wala haya maswala hata mwenzako jana nilimsamehe".Eliza ilibidi sasa anyamaze kimya.Maisha yaliendelea na shughuri za hapa na pale ziliendelea.Mchana yake Eliza alianza kulia tena na kusema"Mume wangu nipige basi yaishe mi siamini kama umenisamehe kiurahisi rahisi hivyo nipige tu mume wangu angalau ntaamini kuwa umenisamehe ila naomba tu usiniue".Kapaya alicheka baada ya kusikia maneno yale na kuendelea na shuguli zake. SIKU mbili zilipita hatimae Kapaya aliendelea na kazi yake ya ulinzi na safari hii pia alienda lindo la usiku.Alimaliza lindo salama na kulejea nyumbani na ndiopo aliposhangaa kukuta mkewe kaondoka.Moja kwa moja alijua mkewe ameenda kwao.Alichukua usafiri na kumfuatilia na kweli alimkuta kwao kijiji kilichopo jirani na kijiji chao.Eliza alifika kwao na kujieleza yote na pia kusema kuwa yeye anaogopa kuishi na mumewe kutokana na kosa hilo na pia mumewe kumsamehe bure bila kufanya kitu chochote. Kapaya alipofika Ukweni yeye alidai mke wake na kusema makosa yaliyotokea ni mambo madogo madogo ya kwenye ndoa na amekwisha kusamehe hivyo anamuomba mkewe eliza wakaendelee kuishi.Baraza lilikaa na maada ikawekwa kisha Eliza akapewa onyo kutokurudia na baada ya hapo kapaya akapewa mke na akarudi nae kwake. Maisha yaliendelea siku zikasonga na hatimae mwaka mmoja ulipita tangu tukio lile litokee.Mapenzi ya kapaya na Eliza yaliludi kama zamani na kusababishabwote wasahau tukio lililotokea SIKU MOJA Kapaya akiwa lindo la mchana simu ilipigwa kwenye simu yake.Ile kupokea anakutana na taarifa kuwa tumeona mkeo kama vile akiingia kwenye getto la Omary.Pale pale kapaya kwa haraka zaidi aliondoka kukimbia kuelekea kwa Omary.Alifika na kuingia moja kwa moja mpaka chumbani kwa Omary na hakuamini tena kuona kumbe mkewe hakusikia wala kukoma na kuona kuwa ile ilikuwa ni kawaida.Alimkuta tena na Omary akiwa na mkewe ndio wanataka waanze. Kapaya aliangalia kwa Pembeni katika chumba cha Omary na kuona panga ile analifuata tu kulichukua Omary aliluka kama paka kuelekea mlangoni na kukimbia,sasa kapaya alibaki na Mkewe wakati huo mkewe alikuwa analia tena kwa kuomba msamaha,Kapaya hakusikiliza sauti ya kilio cha mkewe tena alishika panga na kushika mkono wa kwanza wa mke wake kisha akakata kiganja,Damu nzito ilitoka kama mtu kafungulia bomba,Mke alilia kwa uchungu.Bado Kapaya akaona haitoshi alishika mkono wa pili na kukata kiganja chote kitendo kilichosababisha mkewe kukosa viganja vyote vya mikono.Kisha Kapaya akatupa panga chini na kumuacha mkewe chumbani akilia kwa maumivu makali sana yakiambatana na damu iliyokuwa inamwagika kwa kasi sana. Kapaya alielekea nyumbani kwani na kufika na kulala.Wasamalia walimchukua mke wa kapaya na kumkimbiza zahanati.Kapaya alikuja kushtuka nyumba yake imezunguukwa na polisi,Alikamatwa na kupigwa pigu kisha kupelekwa kituo kidogo cha polisi kijijini hapo huku mkewe akiwa hospitali hajitambuki kutokana na kupoteza damu nyingi.Omary nae alitokomea kusikojulikana na wala hakupatikana. Kapaya Alihukumiwa kifungo jela kwa kosa la kufanya ukatili.Mke nae alisubiliwa apone ili nae apate hukumu yake.Omary hakupatikana licha ya jitihada za jeshi la polisi kumtafuta. MWISHO WA UPENDO NI MACHUNGU * * * * * ** * * * * * ** * * * * * * * * * * * * .....Natumai mkasa huu wa kweli umekuvutia kwa namna moja ama nyingine, pia kwa wewe muda huu unayesoma hii story na unatembea na mke wa mtu unajua uchungu wa mke wewe,Tamaa kutokulidhika na pia kutokujifunza kutokana na makosa vimetujaa sisi binaadamu.Niliona niuandika kama nilivyosimulia ili hata usipojifunza wewe basi uki-share atajifunza yule.Japo natumai kuna kitu flani umeokota kutokana na hii simulizi ya wapenzi hawa kitakachokusaidia mbele ya maisha. Je Unaneno gani kwa hawa watu uliowasoma kutoka katika simulizi hii ya ukweli ya maisha ya KAPAYA? Je Unaujumbe gani wa Kukoment ili tuendelee kujifunza zaidi?.

at 2:00 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top