Home → ushauri
→ Related News SABABU YA WANAWAKE KUTOTAMANI TENDO LA NDOA
Na JOACHIM MABULA,
KUKOSA hamu ya ngono ni tatizo ambalo wengi huona aibu kulizungumzia ingawa ni kitu kinachowanyima raha wanawake wengi. Inakadiliwa kuwa asilimia 40 ya wanawake hupatwa na tatizo hili katika maisha yao, hata hivyo tatizo hili huwapata zaidi wanawake wenye umri kati ya miaka 45 na 65.
Wataalamu wengi wa afya huwaambia wanawake wenye tatizo hili kuwa wana matatizo ya homoni. Kuwa na homoni za kutosha katika mwili ni muhimu kwa tendo la ndoa. Homoni iitwayo istrojeni huhamasisha damu kwenda kwenye uke na kusaidia kulainisha uke wakati homoni iitwayo testosteroni huchochea hamu ya ngono. Hata hivyo, hamu ya ngono kwa wanawake ni kitu chenye utata mwingi kwa maana msongo wa mawazo, mkazo, afya yake na uhusiano aliopo huchangia kuwa na hamu au kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa.
Wanawake wengi mwanzo wanakuwa wanafanya ngono mara tano kwa wiki na baadae hamu hupotea na kuanza kufanya ngono mara moja kwa mwezi tena kwa kujilazimisha. Tatizo hili linaweza kuanza kwa mwanamke kukosa msisimko (raha ya tendo), kutofikia kileleni au kufika kileleni na kushindwa kuendelea na tendo la ndoa baada ya mzunguko mmoja.
Wanawake walio katika hatari ya kupata tatizo hili
Wanawake ambao waliwahi kupatwa na tatizo la kupungua hamu ya kujamiiana hapo mwanzo wanaweza kupatwa na tatizo hili kwa mara ya pili. Wale ambao wamefanyiwa upasuaji wa kuondoa mayai yao ya uzazi kutokana na sababu mbalimbali kama magonjwa au uzazi wa mpango. Wanawake ambao waliofika umri wa kukoma hedhi mara nyingi huanzia kati ya miaka 45 na 55 ingawa kuna wachache huanza kabla ya umri huo.
Matatizo ya homoni si chanzo pekee cha kukosa hamu ya ngono. Sababu zingine ni pamoja na:
Mzunguko mbovu au kukosa kabisa hedhi
Ikiwa mwanamke ana mzunguko wa kati ya siku 24 hadi 34 ni dalili kuwa ovari na homoni zake zinafanya kazi vizuri. Mzunguko mbovu wa hedhi au kutopata kabisa hedhi huwa ni ishara kuwa homoni za mwanake haziko vizuri. Kukosa hedhi kwa zaidi ya miezi sita ni ishara kwamba hakuna uwiano mzuri wa homoni ya istrojeni. Tatizo hili linaweza kuathiri tendo la ndoa hivyo ni vyema kumuona daktari kwa msaada zaidi.
Kukoma hedhi (Menopause)
Baada ya hedhi kukoma, ovari za mwanamke huacha kutengeneza homoni, hivyo kiasi cha homoni ya istrojeni na istrojeni hupungua na wakati mwingine huisha kabisa. Wanawake wengi katika kipindi hiki hupatwa na shida ya uke kukauka (kukosa ute wa kutosha) na kupungua hamu ya tendo la ndoa. Kupungua kwa homoni ya istrojeni husababisha nyama ya uke kuwa nyembamba na kukauka hivyo kusababisha maumivu wakati wa tendo la ndoa.
Ikiwa tendo la ndoa litasababisha maumivu kwa mwanamke hatataka kufanya tendo hilo mara kwa mara na jinsi anavyofanya mara chache ndivyo tatizo linavyozidi kukua. Wakati mwingine tatizo la uke kukauka linaweza kutatuliwa kwa kupaka mafuta ya kulainisha uke au mafuta ya nazi. Matumizi ya virutubishi vya homoni ya testosterone yanaweza kusaidia na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake waliokaribia kukoma hedhi na wale waliokoma, ingawa virutubisho hivi huweza kusababisha chunusi, kuota nywele mwilini na huongeza kiwango cha lehemu (cholesterol) kitu ambacho kinaweza kusababisha matatizo ya moyo.
Matatizo ya kihisia
Kuwa na wasiwasi, msongo wa mawazo na mikazo katika maisha ambayo huchangiwa na matatizo ya uchumi, matatizo katika uhusiano kama ugomvi, kutoelewana, kutoaminiana huathiri mwili na kufanya homoni muhimu kwa ajili ya tendo la ndoa kutotengenezwa kwa kiwango cha kutosha. Pia mzunguko wa damu katika tupu ya mwanamke hupungua na hivyo kusababisha maumivu wakati wa kujamiiana. Historia ya kubakwa au kupata maumivu wakati wa kujamiiana hapo awali kutokana na mwanamke kutokuwa tayari au kutotayarishwa vyema husababisha uke kuwa mdogo kuruhusu uume kupita, tatizo ambalo kitaalamu huitwa vaginismus.
Matumizi ya vilevi
Matumizi ya dawa za kulevya na unywaji pombe kupita kiasi hupunguza hamu ya tendo la ndoa, ingawa kuna baadhi ya watu huamini kuwa unywaji pombe kali huongeza hamu ya kujamiiana au kupunguza uzito. Pombe kali au kilevi cha aina yoyote vikitumiwa kupita kiasi hupunguza hamu ya kujamiiana na pombe huongeza uzito na kusababisha utapiamlo hasa kitambi.
Maradhi
Magonjwa kama kisukari, magonjwa ya mifupa (arthritis), magonjwa ya moyo, saratani ya aina yoyote ile, matatizo ya kupungua kwa homoni ya tezi la koo (hypothyroidism) ambayo hutokea zaidi kwa wanawake kuliko wanaume husababisha kupungua hamu ya tendo la ndoa.
Vilevile madhara ya dawa mbalimbali kama za kushusha shinikizo la damu na za saratani.
Ujauzito, kujifungua na kunyonyesha
Mwanamke anaweza kukosa hamu ya tendo la ndoa kutokana na mabadiliko katika mfumo wa homoni au vichocheo wakati wa ujauzito. Pia kutokana na mabadiliko ya maumbile ya wanawake wakati huo na kufanya mwanamke kutojiamini kufanya tendo la ndoa.
Mwanamke akijifungua na kuanza kunyonyesha homoni ya prolactin huwa katika kiwango cha juu. Homoni hii hufanya kazi ya kumfanya mtu kuridhika baada ya ngono/tendo la ndoa, hushirikiana na homoni/kichocheo nyingine iitwayo dopamine inayofanya mtu kufikia kilele wakati wa tendo la ndoa. Hata hivyo, homoni ya prolactin inaweza kuongezeka wakati mtu akiwa kwenye usingizi mzito hasa wakati wa alfajiri, baada ya kufanya mazoezi, kula, baada ya tendo la kujamiana, baada ya upasuaji mdogo na hata baada ya kupata degedege. Sababu zingine za kuongezeka kiwango cha homoni hii ni kuwa na saratani ya ubongo.
Vidonge vya uzazi wa mpango
Vidonge vingi vya uzazi wa mpango hugandisha homoni ya testosteroni kwenye mwili na huweza kusababisha kupungua kwa hamu ya ngono kwa baadhi ya wanawake. Ikiwa una hofu juu ya njia ya uzazi ya mpango yenye homoni ni vyema kuzungumza na daktari juu ya njia nyingine isiyokuwa na homoni. Usiache tu kutumia vidonge vya uzazi wa mpango kwa kuhisi ndio sababu ya wewe kutopata hamu ya tendo la ndoa bila kuzungumza na mtaalamu wa afya.
Mambo Mengine
Uharibifu wa neva inayohusika na kuongeza msisimko wakati wa kujamiana (pudendal nerve) wakati wa upasuaji wa kuondoa mfuko wa uzazi kwa mwanamke mwenye matatizo ya uzazi au katika mfuko wa kizazi. Uchovu mwingi baada ya majukumu ya kulea mtoto/watoto, kazi na kumhudumia mume wake. Matumizi ya vifaa vya kieletroniki kupita kiasi hasa uraibu wa mitandao ya kijamii kama Facebook & Instagram.
Kupenda kuchat au kutumia intaneti kupita kiasi na hivyo kusababisha msisimko kupotea kati ya wenza wawili mwishowe kupungua uwezo au hamu ya kujamiiana.
Ikiwa unapata hedhi katika mpangilio mzuri, husikii maumivu ukifanya tendo la ndoa na hautumii njia yoyote ya uzazi wa mpango yenye homoni basi tatizo lako la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa linaweza lisiwe tatizo la homoni moja kwa moja. Ni vyema kumuona daktari kwa msaada zaidi
By
🅱 professional love
Related News SABABU YA WANAWAKE KUTOTAMANI TENDO LA NDOA Na JOACHIM MABULA, KUKOSA hamu ya ngono ni tatizo ambalo wengi huona aibu kulizungumzia ingawa ni kitu kinachowanyima raha wanawake wengi. Inakadiliwa kuwa asilimia 40 ya wanawake hupatwa na tatizo hili katika maisha yao, hata hivyo tatizo hili huwapata zaidi wanawake wenye umri kati ya miaka 45 na 65. Wataalamu wengi wa afya huwaambia wanawake wenye tatizo hili kuwa wana matatizo ya homoni. Kuwa na homoni za kutosha katika mwili ni muhimu kwa tendo la ndoa. Homoni iitwayo istrojeni huhamasisha damu kwenda kwenye uke na kusaidia kulainisha uke wakati homoni iitwayo testosteroni huchochea hamu ya ngono. Hata hivyo, hamu ya ngono kwa wanawake ni kitu chenye utata mwingi kwa maana msongo wa mawazo, mkazo, afya yake na uhusiano aliopo huchangia kuwa na hamu au kutokuwa na hamu ya tendo la ndoa. Wanawake wengi mwanzo wanakuwa wanafanya ngono mara tano kwa wiki na baadae hamu hupotea na kuanza kufanya ngono mara moja kwa mwezi tena kwa kujilazimisha. Tatizo hili linaweza kuanza kwa mwanamke kukosa msisimko (raha ya tendo), kutofikia kileleni au kufika kileleni na kushindwa kuendelea na tendo la ndoa baada ya mzunguko mmoja. Wanawake walio katika hatari ya kupata tatizo hili Wanawake ambao waliwahi kupatwa na tatizo la kupungua hamu ya kujamiiana hapo mwanzo wanaweza kupatwa na tatizo hili kwa mara ya pili. Wale ambao wamefanyiwa upasuaji wa kuondoa mayai yao ya uzazi kutokana na sababu mbalimbali kama magonjwa au uzazi wa mpango. Wanawake ambao waliofika umri wa kukoma hedhi mara nyingi huanzia kati ya miaka 45 na 55 ingawa kuna wachache huanza kabla ya umri huo. Matatizo ya homoni si chanzo pekee cha kukosa hamu ya ngono. Sababu zingine ni pamoja na: Mzunguko mbovu au kukosa kabisa hedhi Ikiwa mwanamke ana mzunguko wa kati ya siku 24 hadi 34 ni dalili kuwa ovari na homoni zake zinafanya kazi vizuri. Mzunguko mbovu wa hedhi au kutopata kabisa hedhi huwa ni ishara kuwa homoni za mwanake haziko vizuri. Kukosa hedhi kwa zaidi ya miezi sita ni ishara kwamba hakuna uwiano mzuri wa homoni ya istrojeni. Tatizo hili linaweza kuathiri tendo la ndoa hivyo ni vyema kumuona daktari kwa msaada zaidi. Kukoma hedhi (Menopause) Baada ya hedhi kukoma, ovari za mwanamke huacha kutengeneza homoni, hivyo kiasi cha homoni ya istrojeni na istrojeni hupungua na wakati mwingine huisha kabisa. Wanawake wengi katika kipindi hiki hupatwa na shida ya uke kukauka (kukosa ute wa kutosha) na kupungua hamu ya tendo la ndoa. Kupungua kwa homoni ya istrojeni husababisha nyama ya uke kuwa nyembamba na kukauka hivyo kusababisha maumivu wakati wa tendo la ndoa. Ikiwa tendo la ndoa litasababisha maumivu kwa mwanamke hatataka kufanya tendo hilo mara kwa mara na jinsi anavyofanya mara chache ndivyo tatizo linavyozidi kukua. Wakati mwingine tatizo la uke kukauka linaweza kutatuliwa kwa kupaka mafuta ya kulainisha uke au mafuta ya nazi. Matumizi ya virutubishi vya homoni ya testosterone yanaweza kusaidia na kuongeza hamu ya tendo la ndoa kwa wanawake waliokaribia kukoma hedhi na wale waliokoma, ingawa virutubisho hivi huweza kusababisha chunusi, kuota nywele mwilini na huongeza kiwango cha lehemu (cholesterol) kitu ambacho kinaweza kusababisha matatizo ya moyo. Matatizo ya kihisia Kuwa na wasiwasi, msongo wa mawazo na mikazo katika maisha ambayo huchangiwa na matatizo ya uchumi, matatizo katika uhusiano kama ugomvi, kutoelewana, kutoaminiana huathiri mwili na kufanya homoni muhimu kwa ajili ya tendo la ndoa kutotengenezwa kwa kiwango cha kutosha. Pia mzunguko wa damu katika tupu ya mwanamke hupungua na hivyo kusababisha maumivu wakati wa kujamiiana. Historia ya kubakwa au kupata maumivu wakati wa kujamiiana hapo awali kutokana na mwanamke kutokuwa tayari au kutotayarishwa vyema husababisha uke kuwa mdogo kuruhusu uume kupita, tatizo ambalo kitaalamu huitwa vaginismus. Matumizi ya vilevi Matumizi ya dawa za kulevya na unywaji pombe kupita kiasi hupunguza hamu ya tendo la ndoa, ingawa kuna baadhi ya watu huamini kuwa unywaji pombe kali huongeza hamu ya kujamiiana au kupunguza uzito. Pombe kali au kilevi cha aina yoyote vikitumiwa kupita kiasi hupunguza hamu ya kujamiiana na pombe huongeza uzito na kusababisha utapiamlo hasa kitambi. Maradhi Magonjwa kama kisukari, magonjwa ya mifupa (arthritis), magonjwa ya moyo, saratani ya aina yoyote ile, matatizo ya kupungua kwa homoni ya tezi la koo (hypothyroidism) ambayo hutokea zaidi kwa wanawake kuliko wanaume husababisha kupungua hamu ya tendo la ndoa. Vilevile madhara ya dawa mbalimbali kama za kushusha shinikizo la damu na za saratani. Ujauzito, kujifungua na kunyonyesha Mwanamke anaweza kukosa hamu ya tendo la ndoa kutokana na mabadiliko katika mfumo wa homoni au vichocheo wakati wa ujauzito. Pia kutokana na mabadiliko ya maumbile ya wanawake wakati huo na kufanya mwanamke kutojiamini kufanya tendo la ndoa. Mwanamke akijifungua na kuanza kunyonyesha homoni ya prolactin huwa katika kiwango cha juu. Homoni hii hufanya kazi ya kumfanya mtu kuridhika baada ya ngono/tendo la ndoa, hushirikiana na homoni/kichocheo nyingine iitwayo dopamine inayofanya mtu kufikia kilele wakati wa tendo la ndoa. Hata hivyo, homoni ya prolactin inaweza kuongezeka wakati mtu akiwa kwenye usingizi mzito hasa wakati wa alfajiri, baada ya kufanya mazoezi, kula, baada ya tendo la kujamiana, baada ya upasuaji mdogo na hata baada ya kupata degedege. Sababu zingine za kuongezeka kiwango cha homoni hii ni kuwa na saratani ya ubongo. Vidonge vya uzazi wa mpango Vidonge vingi vya uzazi wa mpango hugandisha homoni ya testosteroni kwenye mwili na huweza kusababisha kupungua kwa hamu ya ngono kwa baadhi ya wanawake. Ikiwa una hofu juu ya njia ya uzazi ya mpango yenye homoni ni vyema kuzungumza na daktari juu ya njia nyingine isiyokuwa na homoni. Usiache tu kutumia vidonge vya uzazi wa mpango kwa kuhisi ndio sababu ya wewe kutopata hamu ya tendo la ndoa bila kuzungumza na mtaalamu wa afya. Mambo Mengine Uharibifu wa neva inayohusika na kuongeza msisimko wakati wa kujamiana (pudendal nerve) wakati wa upasuaji wa kuondoa mfuko wa uzazi kwa mwanamke mwenye matatizo ya uzazi au katika mfuko wa kizazi. Uchovu mwingi baada ya majukumu ya kulea mtoto/watoto, kazi na kumhudumia mume wake. Matumizi ya vifaa vya kieletroniki kupita kiasi hasa uraibu wa mitandao ya kijamii kama Facebook & Instagram. Kupenda kuchat au kutumia intaneti kupita kiasi na hivyo kusababisha msisimko kupotea kati ya wenza wawili mwishowe kupungua uwezo au hamu ya kujamiiana. Ikiwa unapata hedhi katika mpangilio mzuri, husikii maumivu ukifanya tendo la ndoa na hautumii njia yoyote ya uzazi wa mpango yenye homoni basi tatizo lako la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa linaweza lisiwe tatizo la homoni moja kwa moja. Ni vyema kumuona daktari kwa msaada zaidi By 🅱 professional love
Artikel Terkait
UNAJUA KUMPAGAWISHA MPENZI WAKO????  Kama inavyoeleweka, mapenzi ni sehemu muhimu ya afya ya binadamu. So, katika peruzi zangu, nikakutana na hili somo la "Tantric Sex." Kama inavyoelewaka, mapenzi ni sehemu muhimu ya afya ya binadamu. So, katika peruzi zangu, nikakutana na hili somo la “Tantric Sex.” As if hii duinia, especially hii century haiko overloaded na information kuhusu mambo ya mapenzi, jinsi ya kufanya mapenzi and whats hot in the bedroom, whats in and whats not. So, lately nimeona a lot of tzmoms readers wamekuwa wakitembelea sana na kusoma page ya “mapenzi baada ya ujauzito” na “kufanyamapenzi wakati wa ujauzito.” And I thought well, writing about Tantric Sex will be nyongeza kwa kila mmoja, aliye mama na mbaye bado damu inachemka katika mambo ya mapenzi. Anyhu, kama “SEX/MAPENZI” yangekuwa yanaweza kuyu-nite the world/countries/makabila/people I think hii fani ingeshinda. Well, so kama umeshawahi kujifungua ama kama wewe ni mama, you definitely understand ni jinsi gani ni vigumu kuwa upbeat kuhusu mapenzi ama kumfurahisha mumeo/mpenzio everyday. Well, once in a while maybe but not everyday. Ila kama we ni mdada/binti ambaye hujazaa bado well, damu yako bado inachemka so energy bado ipo nyingi ya kukurupushana na mpenzio. Having said that, si maanishi mtu ukishazaa ndo fani ya kuenjoy mapenzi imekwisha but nguvu zinapungua for sure however, kuna vitu vingi tuu ambavyo vinaweza kusaidia kuleta nguvu ya kutaka kukurupushana chumbani lol. Kukosa nguvu/energy to wanna work it all the time its not because mwanamke ni mvivu but hutokana na kuwa na mambo mengi sana ya kutend nyumbani i.e. kuhakikisha watoto wako taken care of, labda kazini pia unahitajika, etc una kuta hupati muda wa kujifurahisha mwenyewe ama na mpenzi wako. Therefore, mara nyingi before you know mupenzi anaanza kulalamika or hata mwanamke mwenyewe unaweza kufeel like you are not doing enough so mambo ndo hivyo yanaanza kwenda south chumbani. Hivyo basi, lets dig in tuone Tantric Sex inatoa msaada wa aina gani ili kurevamp mapenzi. Kwanza kabisa, FYI tantric sex can be weird at the beginning ila nitajitahidi kutoingia so indepth ili kusave miyoyo ya watu wengine. Kwamaana hii ni soft porn “according to me.” Lol. so usishtuke ama kushangaa sana. Well, anythign “sex” can be unconfortable anyways. Okay, so, kwanza kabisa, with Tantric Sex, mtu na mpenziwe wanatakiwa kuwa; SPIRITUALLY CONNECTED (usishtuke sio kidini lol).. Hii inamaainisha kwamba wewe na patner wako kwa pamoja mnajua mnataka nini emotionally and physically. Kwa kufanya hivi inasaidia kuwafanya kwa pamoja kuwa “FREE” na kuondoa wasiwasi wa labda mwenzangu atanijudge kwamba labda mimi ni malaya ama fuska etc. In other words hii process inaitwa “Dropping the Veil, between “Self” and “Other/patner.” THE ENVIRONMENT/mazingira. Wakati mnapractice tantric sex of course, just like when you are in the bedroom unaweza ukavaa lingerie/kuo za ndani zinazovutia or “kuwa kama mlivyotoka tumboni mwa mama zenu” (you know what i mean). Tatu, wapenzi wanaanza kupapasana lol, but in a way kwamba you are feeling the energy of the other person. Na hii energy unaweza kuifeel kwasababu mko free hamna anayemjudge mwingine/there are no worries. You are just in your own created world. Nne, wakati wa kufeel energy ya mwingine lazima wapenzi wawe wana pumua heavely yaani just feeling every move made but the other person mpaka mnapofikia mahali were you are breathing so hard and you are feeling each other. then you start kissing the lips, and then deeper for minutes even hours. Then mengineyo yanaweza kuendelea. So, all this time kumbuka its not about going straight into sex with your partner rather its about getting high by touching and feeling connected with each other. hivyo basi, once in a while take that time and revamp your intimacy, dress good, feel sexy and heey have fun!!. By 🅱 ... Read More
Kwanii Wanaume Waaminifu Kwenye Uhusiano Huachwa.....  Kuachwa na mpenzi kwa sababu umekuwa ni muaminifu sana yaonekane ni jambo lisiloingia akilini lakini linatokea. Moja ya mambo ya ajabu unayoweza kuwa ushawahi kuyasikia ni kwamba mara nyingine uamuzi wako wa kuwa mwanaume mwema sana na unayejitahidi kufanya uhusiano wako wa kimapenzi uwe mzuri muda wote unaweza kukugharimu na kujikuta unaachwa kabisa. Haitakiwi kuwa hivyo lakini mara nyingine inatokea, na inatokea kwa sababu wazo la mwenza wako kuhusu uhusiano wa kimapenzi laweza likawa tofauti na ulionao wewe. Wengine wana mawazo hasi kuhusu jinsi uhusiano/ndoa inavyotakiwa kuwa. Hii ndio sababu hutakiwi kuanzisha uhusiano wa kimapenzi na mtu asiye na vipaumbele sawa na vya kwako au asiye na mtazamo mmoja wa kimaisha kama ulionao wewe. Usipozingatia hilo, utajikuta unaingia kwenye uhusiano na mtu ambaye hatakujali vya kutosha kwakuwa labda humfokei au kumpiga anapokukosea – au utajikuta ameshakupanda kichwani na kuanza kukudai mambo ambayo huwezi kuyatimiza lakini ukajikuta unajitutumua kumtimizia kwa sababu unataka kumfurahisha mpenzi wako na analijua jambo hilo. Kwa sababu baadhi ya wanaume wanapenda kulinda siri na kuwaachia uhuru wapenzi wao, wanajikuta wakiwapa ruhusa wanawake zao kwenda popote wanapojisikia bila kuwafatilia wanachofanya. Nini kinafata baada ya hapo? Mwanamke anatoka, anatafuta mchepuko na kukusaliti. Mwisho inakufanya wewe mwanaume uonekane mjinga mbele ya wengine. Tatizo ni kwamba tabia hii inaibuka kutokana na mazoea ya watu kuingia kwenye uhusiano wakiwa wameficha tabia zao halisi na kuja kufungua makucha yao baada ya kuona ameshaishi na wewe kwa muda mrefu kiasi kwamba huwezi tena kumuacha. Hii inasababisha wanaume walioathirika kutokana na tabia kama hizi kutoka kwa waliokuwa wapenzi wao wasiweze kuwaamini wanawake wengine tena kwa kuona kwamba wote ni sawa na wale waliowaumiza na kusababisha wasiweze kuwaonesha wenza wao wapya mapenzi kwa kiwango cha juu wakihofia kuumizwa tena. Kuwa mpole, mkarimu na mwenye upendo wa hali ya juu kwa mpenzi wako ndio jambo linalotarajiwa kwenye uhusiano. Mtu hatakiwi kufanywa ajisikie vibaya kwa kumuonesha mapenzi ya kweli mwenza wake. Kama wewe unakuwa muaminifu na mwema kwa mpenzi wako lakini umekuwa unadharauliwa au ukaachwa kutokana na tabia hiyo, kaa ukiwa na amani kabisa kwamba lawama za kuvunjika kwa uhusiano huo hazikuhusu wewe – lawama ni za mpenzi wako aliyeshindwa kujua wewe umekuwa mwema kiasi gani kwake. ... Read More
Hatua 5 za kuzungumza na mpenzi wako aliyekasirika Kwenye mapenzi kuna nyakati za kutofautiana, kukasirishana. Katika hali ya kawada kipindi hiki huwa ni za hatari kwa sababu husababisha nyufa kubwa za uhusiano na kulifanya penzi kukosa ladha. Sote tunajua, watu hupigana, huachana, hujeruhiana, hutukanana, hudhalilishana wakiwa na hasira. Hata hivyo si wote wanaojua wafanye nini wanapojikuta wameingia kwenye hatua hiyo mbaya. Msomaji wangu, hebu jaribu kukumbuka ugomvi mmoja uliotokea kati yako na mpenzi wako na ikiwezekana jikumbushe mlivyoanza! Utabaini kuwa mlianza kama utani na mkajikuta mmefura kwa hasira, mkatwangana makonde, mkatamkiana maneno makali ya kuudhi na pengine mkaamua kuachana. Yote hii ni kwa sababu mlikosa elimu ya mazungumzo. Ingekuwa mmoja wenu hasa yule aliyekuwa wa pili kukasirika anafahamu hatua za kuzungumza na mtu aliyekasirika angechukua jukumu la kutuliza machafuko na kuleta amani kwenye mapenzi. Tazama hatua tano za kuzungumza na mpenzi aliyekasirika. MPUNGUZE MHEMKO Hasira hujaza kifua, huathiri mzunguko wa damu na ufahamu. Mtu aliyekasirika huwa vigumu kwake kusikiliza au kutazama mambo kwa jicho la tatu. Mwenye hasira huwa hafikirii matokea yajayo badala yake hutazama zaidi tukio na jinsi ya kupata ushindi iwe kwa maneno au kwa mapambano. Katika hali ya namna hiyo, mtu mwingine akija na busara za kutaka kumgeuza haraka haraka hawezi kumuelewa. Muhimu hapo ni kuacha kumwadama, kujibizana naye, kumshawishi asikilize badala yake mpe nafasi ya kusema atakavyo, abwate ajuavyo huku wewe ukimuitikia na kumkubalia lawama zake. “Basi mpenzi mwenye makosa ni mimi.” Kauli za aina hii zitampunguza hasira kwani atajiona msindi. MSOME SAIKOLOJIA YAKE Kwa kuwa unamfahamu mpenzi wako kwa kina itakuwa rahisi kwako kumtambua kuwa amepunguza hasira na kurudi katika hali yake ya kawaida. Ukisha fahamu hilo chukua jukumu la kumsoma kisaikojia ili kujua kama yuko kwenye hali nzuri ya kusikiliza yale uliyotaka kumwambia wakati alipokuwa na hasira. Zoezi hili linaweza kuchukua saa kadhaa na wakati mwingine hata siku mbili. Lengo ni nini? Ni kupata matokeo sahihi ya kuondoa chuki za mwenza wako na kumfundisha madhara ya kukasirika kwenye uhusiano wenu wa kimapenzi. “J, nakupenda sana, lakini juzi uliniumiza, uliniambia mimi malaya kwa kosa ambalo sikufanya?” Bila shaka muda huo atakusikiliza zaidi kuliko ungebishana naye alipokuwa na hasira. MRUHUSU AKUJIBU Pamoja na kumsoma kisaikojia na kumwambia kinagaubaga makosa yake, usimzuie kujitetea, mpe nafasi ya kuzungumzia kilichomkasirisha. “Unaona bado unanitukana, sasa naamini siku ile ulikuwa umedhamilia.” Usisiseme hivyo, mwache ajibu hoja hata kama atakuwa anakukandamiza na kuzidi kujijengea ushindi. Mvumilie aoshe ubongo wake. EPUKA MARUMBANO Kama nilivyosema kwenye hapo juu, wapenzi wengine huwa wagumu kuelewa, ni watu wa kuficha udhaifu wao na kutopenda kuonekana wamekosea. Watu wa namna hii unapowarejeshea mazungumzo wanaweza kujikuta wanahamaki tena. “Kwa hiyo ulikuwa unasemaje…nilifanya ndiyo,… wewe unaamuaje?” Mkifika kwenye alama hiyo usikubali kurumabana naye mwache aseme halafu wewe ingia kwenye hatua ya tano. MUOMBE MSAMAHA Hata kama atakuwa yeye ndiye mwenye makosa na amekataa kukiri, usijali, chukua jukumu la kumuomba msamaha na kueleza tena nia yako ya kumazungumzo ilikuwa ni kuelewana si kugombana. Kumbuka hata kama amekiri kosa, bado unatakiwa kumuomba radhi kwa kurejea yaliyopita. “Mpenzi inawezekana nikawa nimekuudhi kwa niliyosema, nakuomba sana tusameheane.” Bila shaka kwa haya machache msomaji wangu utakuwa umejifunza na kuchukua hatua za kuzuia migogoro mikubwa inayotokana na hasira za mpenzi wako. Leo niishie hapa, nikushukuu kwa kunisoma. Kaa mkao wa kura, kile kitabu bora cha mapenzi nchini TITANIC, TOLEO LA NNE, kitakuwa mtaani hivi karibuni. Usikose nakala yako. ... Read More
Tatizo la Ugumba kwa wanawake  Ugumba ni hali ya mwanamke kushindwa kushika ujauzito. Linaweza kuwa tatizo pia kwa mwanaume lakini katika makala hii tutaona nini kinasababisha tatizo hili kwa upande wa wanawake. Nini husababisha ugumba kwa wanawake? Mayai kutokomaa ipasavyo: Tatizo la mayai kutokukomaa vema ndilo chanzo na sababu kuu ya wanawake wengi kushindwa kushika ujauzito na hii inachukua karibu asilimia 30 ya wanawake wote wagumba. Habari njema ni kuwa tatizo hili linaweza kurekebishwa kirahisi ikiwa mwili utapewa vile viinilishe mhimu vinavyokosekana hadi kupelekea mayai kutokomaa vizuri. Vinavyosababisha mayai ya mwanamke kutokomaa vema: (1) Matatizo ya kihomoni Matatizo katika homoni ndicho chanzo kikuu cha mayai kutunga bila kukomaa vizuri. Hatua za ukomaaji wa mayai zinategemea uwiano mzuri wa homoni na namna zinavyotegemeana katika kufanya kazi. Jambo lolote linalovuruga homoni kubaki katika uwiano wake sawa na wa kutegemeana na wenye kufanya kazi ipasavyo linaweza kupelekea utungaji wa mayai ambayo hayajakomaa vizuri. Kuna sababu kuu mbili zinazosababisha matatizo katika homoni: Ufanyaji kazi usioridhisha wa hypothalamus Hypothalamus ni sehemu ya mbele ya ubongo ambayo ina jukumu la kutuma ishara (signals) kwenda katika tezi ya pituitari ambayo yenyewe tena hutuma uchochezi wa kihomoni kwenda kwenye ovari katika mfumo wa F.S.H na L.H ili kuanzisha ukomaaji wa mayai. Ikiwa hypothalamus inashindwa kufanya kazi zake vizuri kutungwa kwa mayai ambayo hayajakomaa ndiyo kutakuwa ni matokeo yake. Tatizo hili linachukuwa asilimia 20 katika kesi za mayai kushindwa kukomaa kiasi kinachohitajika. Ufanyaji kazi usioridhisha wa tezi ya pituitari Kazi kubwa ya tezi ya pituitari ni kuzarisha na kutoa homoni mbili maalumu kwa ajili ya mfumo wa uzarishaji kufanya kazi zake vizuri ambazo zinajulikana kitaalamu kama ‘Follicle-stimulating hormone (F.S.H)’ na ‘Luteinizing hormone (L.H)’. Mayai yatashindwa kukomaa vizuri ikiwa ama L.H au F.S.H zinatengenezwa chache sana au nyingi sana kuliko inavyohitajika. Hili linaweza kutokea kama sababu ya ajari, uvimbe au kama usawa usio sawa wa kikemikali katika pituitari. (2) Kovu katika Ovari Uharibifu au ajari katika ovari unaweza kupelekea kuzalishwa kwa mayai ambayo hayajakomaa. Kwa mfano, upasuaji mkubwa, uvamizi au upasuaji wa mara nyingi wa uvimbe katika ovari unaweza kusababisha kapsuli ya ovari kupata majeraha au makovu na hivyo kwa namna moja ama nyingine kuweza kuzuia utungwaji wa mayai ambayo hayajakomaa vema. Pia maambukizi katika njia ya uzazi yanaweza kupelekea tatizo hili. (3) Dalili za mwanzo za kukaribia kufunga kuzaa (Menopause) Hii huchangia kwa asilimia chache na kwa sasa halielezeki kisawasawa. Kwamba wanawake wengi wanapokaribia umri wa kuacha kuzaa kuanzia miaka 40 kwenda juu baadhi yao hutokewa na tatizo la kutunga mayai ambayo hayajakomaa vema. Baadhi ya wanawake wanaacha kupata siku zao mapema kabla ya umri uliozoeleka yaani miaka 40 kwenda juu. Kwa sababu hiyo inadhaniwa kwamba uwezo wao wa asili katika kuzalisha mayai unakuwa umepunguwa na wengi wao huwa ni wale walikuwa wakijihusisha zaidi na michezo ya kukimbia au wale wenye historia ya muda mrefu ya kuwa na uzito pungufu na wafanyaji sana wa mazoezi. Tatizo hili pia linaweza kuwa ni la kurithi. (4) Matatizo kwenye kijishimo yai (follicle) katika ovari: Ingawa kwa sasa bado hili nalo halielezeki, hiki kijishimo yai kwa kitaalamu kinajulikana kama ‘’follicle’’ ndicho hupasuka na yai kutoka. Kuna baadhi ya kina mama wanapata dalili za kijishimo yai kutokupasuka “unruptured follicle syndrome” na matokeo yake kila mwezi mama anazalisha yai kama kawaida lakini hiki kijishimo yai kinashindwa kupasuka. Hivyo yai linabaki ndani ya ovari na utungaji wa mimba unashindwa kufanyika. Kinachosababisha ufanyaji kazi dhaifu wa mirija ya uzazi (Fallopian Tubes): Magonjwa katika mirija ya uzazi yanahusika na ugumba kwa karibu ya asilimia 25 ya wanawake wote wagumba. Hali yenyewe inatofautiana toka kwa mmoja hadi kwa mwingine kutoka kugandana au kunatana kidogo hadi kuzibika kabisa kwa mirija. Matibabu ya mirija iliyozibika huhusisha upasuaji au usafishaji wa mwili kwa kula vyakula na vinywaji maalum kwa muda wa majuma kadhaa. Sababu kubwa zinazopelekea kuzibika au kunatana kwa mirija ya uzazi ni pamoja na zifuatazo: (A) Maaambukizi Maambukizi katika njia ya uzazi ambayo yamesababishwa ama na bakteria au virusi na ambayo kwa kawaida ni magonjwa ya kuambukizana kwa njia ya tendo la ndoa, maambukizi haya kwa kawaida husababisha muwasho au kuungua na kupelekea makovu na uharibifu. Magonjwa ya zinaa kama vile kisonono na mengineyo yanaweza kuwa chanzo cha ugumba kwa wanawake wengi hasa ikiwa hayatatibiwa mapema. (B) Magonjwa yasiyo ya kawaida Magonjwa yasiyo ya kawaida ni pamoja na ugonjwa wa kidole tumbo (appendicitis) na uvimbe katika utumbo mpana (colitis), magonjwa ambayo husababisha muwasho au kuungua chini ya uvungu wa utumbo mkubwa na kuiathiri mirija ya falopiani na kama matokeo yake makovu na kuzibika kwa mirija ya uzazi hutokea. (C) Upasuaji uliopita Upasuaji una chukua nafasi kubwa katika kusababisha ugumba kutokana na matokeo yake ya kusababisha magonjwa ya mirija ya uzazi na uharibifu utokanao na huo upasuaji. Upasuaji katika utumbo mkubwa unaweza kupelekea kunatana au kugandana kwa mirija ya uzazi kutakakopelekea mayai kushindwa kusafiri kirahisi katika mirija hiyo ya uzazi. (D) Mimba kutungwa nje ya mji wa uzazi: Hii ni wakati mimba inapotungwa katikati ya mirija ya uzazi yenyewe. Katika hali kama hii hata kama kutatokea bahati kiasi gani bado kunaweza kusababisha uharibifu katika mirija na hali hii ni moja ya hali mbaya sana kiafya na kimaisha. (E) Hali ya kurithi Kwa nadra au kwa asilimia fulani ndogo baadhi ya wanawake huzaliwa na hali ya kuwa na mirija isiyo ya kawaida kwa uzazi na kwa kawaida hali hii huambatana na mji wa uzazi usio wa kawaida pia. . (5) Sababu za kitabia: Inajulikana wazi kwamba baadhi ya tabia na namna tunavyoishi kunaweza kupelekea wanandoa wakashindwa kupata mtoto. Kwa bahati nzuri nyingi kama si zote ya hizo tabia zinaweza kurekebishika au kuachwa kabisa na kupelekea siyo tu kuwa na uwezo wa kuzaa bali pia kuwa na afya nzuri kwa ujumla. Sababu hizo za kitabia ni pamoja na zifuatazo: Lishe na mazoezi Ili mfumo wa uzazi uwe na uwezo mzuri unahitaji vitu viwili mhimu, lishe kamili na mazoezi. Wanawake wenye uzito uliozidi sana au wenye uzito pungufu sana wanaweza wakapatwa na tatizo la kutopata ujauzito kirahisi. Uvutaji sigara Uvutaji wa sigara una mchango mkubwa na ugumba. Uvutaji sigara husababisha uzarishwaji wa mbegu chache kwa mwanaume (lower sperm count) kwamba mwanaume anatoa mbegu chache sana ama pungufu wakati huo huo uvutaji sigara huchangia katika tatizo la kutoka kwa mimba, kuzaa kabla ya miezi 9 (njiti), na kuzaa mtoto mwenye uzito mdogo kwa wanawake. Unywaji pombe Unywaji pombe kupita kiasi una mchango mkubwa sana katika ugumba na hii hata ikitokea mama akapata ujauzito kama bado anaendelea kunywa pombe inaweza kupelekea matatizo hata kwa mtoto mtarajiwa. Unywaji pombe pia huchangia uzarishwaji wa mbegu chache kwa wanaume. Madawa ya kulevya Utumiaji a madawa ya kulevya kama bangi na mengine ya kujidunga kwa sindano kunaweza kuwa sababu ya kuzalisha mbegu chache kwa wanaume. Utumiaji wa dawa za kulevya kama ‘Cocaine’ kwa mama mjamzito kunaweza kusababisha mtindio wa ubongo na matatizo katika figo kwa mtoto mtarajiwa. Matumizi ya madawa ya kulevya inafaa yaepukwe wakati wa kutafuta ujauzito na wakati wa ujauzito. Utowaji mimba Utowaji mimba wa mara kwa mara pia unahusika sana na tatizo la ugumba kwa karibu ya asilimia 20. Utowaji mimba unaweza kusababisha makovu katika mji wa uzazi na hata kuharibika kabisa kwa mji wa uzazi ikiwa utowaji huo haukufanyika kitaalamu au unafanyika mara kwa mara. (6) Sababu za ugumba za kimazingira: Uwezo wa kushika ujauzito unaweza pia kuathiriwa kutokana na kuwa karibu na baadhi ya kemikali au sumu katika maeneo ya kazi au makazi. Vitu viwezavyo kusababisha mabadiliko, dosari za kuzaliwa, utokaji mimba, au utasa huitwa ‘Sumu kwa mfumo wa uzazi’. Kamikali zifuatazo zinahusishwa na ugumba au utasa: Risasi (Lead) Kuwa karibu na kemikali au sumu zinazounda risasi kunaweza kuwa sababu ya ugumba. Risasi hupelekea kuzalishwa kwa mbegu zisizo za kawaida kwa wanaume zijulikanazo kwa kitaalamu kama ‘teratospermias’ na inafikirika pia kuhusika na utokaji mimba kusiko kwa asili (artificial abortion). Baadhi ya matibabu na madawa ya hospitalini Kuwekwa kwenye matibabu yanayohusisha mionzi (x-rays), mionzi ya kawaida au hata ile ya kutibia kansa (chemotherapy), kunaweza kusababisha matatizo katika uzarishwaji wa mbegu kwa mwanaume na wakati huo huo kuchangia kwa sababu kadhaa zinazopelekea kutungwa kwa mayai ambayo hayajakomaa vizuri. Pia matumizi ya dawa za kuzuia ujauzito kwa muda mrefu yamekuwa yakihusishwa na ugumba kwa miaka ya hivi karibuni ingawa bado kuna mjadala mkubwa katika hili. Ethylene Oxide Hii ni kemikali inayotumika kusafishia vifaa vya upasuaji, pia hutumika katika kutengeneza baadhi ya sumu za kuua wadudu. Ethylene oxide inaweza kupelekea matatizo katika uzazi hasa katika miezi ya mwanzo mwanzo ya ujauzito na inahusishwa sana na tatizo la utokaji mimba katika miezi ya mwanzo ya ujauzito (early miscarriage). Dibromochloropropane (DBCP) Hii pia ni kemikali au dawa inayotumika katika kuua wadudu, ikiwa unafanya nayo kazi kila mara inaweza kusababisha kutungwa kwa mayai yasiyokomaa vizuri, kuelekea mapema kwa ukomo wa kutokuzaa kabla hata ya miaka 40 au 45 (early menopause) na kadharika. (7) Sababu zingine zinazoweza kusababisha ugumba kwa mwanamke: Karibu asilimia 10 ya ugumba kwa wanawake ni matokeo ya mji wa uzazi usio wa kawaida (abnormal uterus). Hali zingine ni pamoja na uvimbe katika kizazi, kugandana au kunatana kwa mji wa uzazi na mirija ya uzazi. Karibu asilimia 3 ya ugumba kwa wanawake ni matokeo ya matatizo ya ute usio wa kawaida katika mlango wa kizazi (femaleís cervical mucus). Ute ute huu unahitaji kuwa na hali fulani maalumu kwa mbegu za kiume kuweza kuogelea kirahisi katikati yake. Chanzo kikubwa cha tatizo hili ni usawa usio sawa wa homoni za kike ambapo homoni ya uzazi ya kike iitwayo ‘estrogen’ yaweza kuwa ni chache sana au homoni nyingine iitwayo ‘progesterone’ yaweza kuwa ni nyingi sana tofauti na inavyohitajika. Vitu vya kuepuka kwa mtu mwenye tatizo la ugumba: ChipsiVinywaji baridiKaffeinaNyama nyekunduVilevi ... Read More
Kufanya Mapenzi Kwa Wiki Mara 3 Kunapunguza Kupata Shambulio La Moyo (Heart Attack) Kwa Asilimia 50%  Utafiti umebainisha kwamba kufanya mapenzi angalau mara tatu kwa wiki kunapunguza uwezekano wa kupatwa Heart Attack (Shambulio la Moyo) kwa 50% ukilinganishwa na yule ambaye anapitisha wiki nzima bila kupiga mambo yetu. Pia utafiti huo unasisitiza ya kwamba mwenye Kufanya Mapenzi killa siku anaondoa uwezekano wa kupata Heart Attack kwa Asilimia 100% ZIJUE FAIDA ZA KUFANYA MAPENZI Kiafya Tendo la ndoa ni moja kati ya mazoezi ya mwili. Wataalamu wanasema kwamba, unapofanya tendo hilo mara tatu kwa wiki husaidia kupunguza kiasi cha mafuta mwilini na pia endapo mtu atafanya tendo mara tatu kwa wiki kwa kipindi cha mwaka mzima ni sawa na kukimbia maili 75. Tendo la ndoa huongeza takriban vizalisha nguvu 150 kwa nusu saa ambayo ni sawa na kukimbia dakika 15 kiwanjani. Kuongeza mwendo wa damu Tendo la ndoa husaidia kuongeza kasi ya mtiririko wa damu kwenye ubongo na sehemu nyingine ya viungo vya mwili, hii huchangia kuongeza kasi ya mapigo ya moyo na kuboresha mfumo wa upumuaji. Msukumo thabiti wa damu mpya yenye oxygen na homoni zenye chembe chembe hai zinapopenya kwenye mishipa ya damu husaidia katika uunguzaji wa chakula, pia huondoa kiasi cha uchafu ambao ungesababisha mishipa na kushindwa kufanya kazi na kumfanya mwanadamu apate maumivu ya mwili. Hupunguza mafuta yenye kileo (Cholesterol) Tendo la ndoa huweka sawa uwiano wa mafuta yenye kileo (Cholesterol) nzuri na cholesterol mbaya na wakati huo hupunguza kwa ujumla kiasi cha mafuta yenye kileo mwilini. Kupunguza maumivu Wakati wa kufanya mapenzi, homoni iitwayo oxytosin huzalishwa mwilini ambayo husababisha kuzalishwa kwa homoni iitwayo endorphin ambazo hupunguza maumivu kama vile kuvimba sehemu za viungo (arthritis) maumivu ya shingo (Whiplash) na maumivu ya kichwa. Ulinzi wa tezi ya kibofu (mwanaume)Majimaji yanayozalishwa katika tezi ya kibofu (prostate) yakizidi husababisha kuleta matatizo mwilini. Tendo la ndoa la mpangilio huondoa uzalishaji wa majimaji hayo yenye madhara. Mabadiliko ya ghafla ya tendo la ndoa huelekea kuleta matatizo yahusianayo na tezi ya prostate. Kupunguza mfadhaiko wa moyo Kujitosheleza na kupumzisha mwili baada ya tendo la ndoa ni muhimu kwa kutuliza akili na kurekebisha mzunguko wa damu mwilini. Watu wenye kushiriki tendo la ndoa wanatajwa kushinda mfadhaiko na kupata usingizi mnono hasa mara baada ya kumaliza kufanya mapenzi. Huongeza uzalishaji wa homoni za kiume(testosterone) na za kike (Oestogen) Faida nyingine inayopatika ni kuongeza uzalishaji wa homoni za kiume na za kike likiwemo suala zima la msukumo wa kufanya tendo hilo ambapo mhusika hutosheka zaidi ya yule ambaye hana mazoea ya kufanya mapenzi. Hata hivyo, baadhi ya madaktari wamegundua kwamba ongezeko la homoni za kiume/ kike huweza kuwakinga wanadamu na magonjwa ya moyo. Kuishi muda mrefu huku ukionekana kijana Wakati wa tendo la ndoa homoni iitwayo DHEA huzalishwa mwili mzima. Hii husaidia msisimko wa mapenzi kuongezeka. Kutokana na elimu hiyo DHEA ni kemikali yenye nguvu duniani ambayo husaidia kuweka sawa kinga ya mwili, huongeza ufahamu, kuimarisha mifupa, kutengeneza na kuimarisha afya na kuimarisha mishipa ya moyo (Cardiovascular). Hupunguza baridi na mafua Elimu inaonesha kuwa wanaofanya tendo la ndoa mara moja au mbili kwa wiki huongeza 30% ya uzalishaji wa chembe chembe hai za mwili ziitwazo Immunogloulin A ambazo huwa na kazi ya kuulinda mwili dhidi ya magonjwa. Hizo ni faida chache tu za kufanya tendo la ndoa. NB: Jambo kubwa la kuzingatia ni kuwa faida hizi hupatikana kwa ufanyaji wa mapenzi usiokuwa na hofu ya kufumaniwa au kuumbuliwa HAYA KWA WANA NDOA FANYENI MAPENZI JAPO KWA WIK MARA 3 MUPATE FAIDA ZA TENDO LA MAPENZI NDANI YA NDOA. KWA WALE WASIOWA HAWAPATI HIZI FAIDA SHAURI YENU MSIE OWA OWENI MUPATE FAIDA ZA TENDO LA NDOA ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: