❤❤❤❤❤❤❤❤❤❤ 🅱 professional love Mwanaume mwenzangu MWANAMKE YEYOTE NI TULIZO LAKO ikiwa tu UTAMBEBA KATIKA HISIA ZAKO! Wanaume wengi wameoa mke kwa mtazamo na sio kwa hitaji la kujenga familia, Udhaifu huo umepelekea wanaume wengi kukosa maana ya MKE pale mwanamke anapobadilika kuendana na maisha halisi hata kupelekea ule muonekano ambao ulimpa mtazamo mwanaume wake kuona kama AMESHUKA KIWANGO... Kiwango cha mwanamke hakishuki ikiwa MWANAUME utajuwa namna ya kuishi na mkeo, Mwanamke yeyote duniani hitaji lake ki bin adam ni KUPENDWA NA MWANAUME WAKE na hilo ni tofauti sana na sisi wanaume maana MWANAUME HITAJI LAKE KWA MKEWE NI AAMINIWE! Tofauti hiyo ni kubwa kwa watu ambao hawajui kusoma mienendo ya wenzi wao Kwani mwisho wake ni kuona mwenza wake hafai, Nisikilize Mwanaume nikwambie; ¤ USITAFUTE SURA NZURI, siku moja itazeeka. ¤ USITAFUTE NGOZI NZURI, siku moja itakunjamana. ¤ USITAFUTE NYWELE NZURI, siku moja zitakuwa nyeupe. ¤ USITAFUTE UMBO NAMBA NANE, siku moja laweza kukosa mvuto. ¤ USITAFUTE UBORA WA RANGI, siku moja maisha yataipausha. Badala yake tafuta MOYO MKARIMU ambao utakupa amani pamoja na kuishi maisha yenye furaha siku zote, Waswahili na misemo yao MCHAGUA JEMBE SIO MKULIMA😅😅😅 Mtaje mwanamke kwa HEKIMA ZAKE wala usimtaje mwanamke kwa UREMBO WAKE... Sikufichi vile alivyoumbwa mwanamke ni HESHIMA hayo Mengine hutajwa kama mapambo tu na siku moja hutoweka. ❤❤❤❤❤❤❤❤❤❤ Dr Luv🤓🤓🤓

at 9:10 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top