NIMEZALISHWA NA KUTELEKEZWA JE NAWEZA KUPATA MWANAUME WA KUNIPENDA MIMI NA MWANANGU? NINI CHA KUFANYA? kumpata mwanaume ambaye atampenda huyo mwanao kuliko hata kawaida na ukawa na furaha. lakini hembu usikae na kusubiri mwanaume wa kukusaidia kulea mwanao, hapana hembu anza kusema hapana namlea mwenyewe. Anzisha familia yako, kama bado unaishi kwenu basi tafuta kazi, tafuta biashara anza kujitegemea na huko wakati ukiendelea na maisha yako basi ndiyo utakutana na huyo mwanaume unayemtaka wewe na atakua mume wako. Lakini ni namna gani utakutana na mwanaume wa namna hiyo? Ni namna gani wewe utapata mwanaume wakati wale ambao hawajazaa tu kupata wanaume ni shida? Kitu cha kwanza unatakiwa kujua kuwa, kupata mume hakuna uhusiano na kua na mtoto au la? Lakini jambo la pili nikua kama utajiamini na kuanza kumuona mtoto wako kama baraka na si laana basi itakua rahisi kwako kumpata mwanaume. Hembu jiamini, unapokutana na mwanaume, wakati wa mazungumzo hembu jivunie kuwa na mtoto. Ndiyo sio upite ukitangaza hapana, lakini wakati wa mazungumzo akikuuliza kuhusu wewe muambie, mimi ni mtu flani nafanya kazi flani au biashara, nina mtoto mmoja wa kiume au wakike au nina watoto wawili. Baba yao tulishindwana kidogo ila now ana maisha yake na mimi nina yangu. Usiongelee alivyo kutenda, alivyokuumiza, alivyokutelekeza hapana, haimhusu na hakuna mtu anayetaka mtu aliyetelekezwa. Muambie tu unamlea mwanao mwenyewe na unafuraha, ndiyo usilielie kama una matatizo, msongo wa mawazo au nini, hakuna mtu anayependa watu wenye matatizo. Unaweza hata kuenda mbali kidogo na kutoa picha ya mwanao kwenye wallet na kumuonyesha, ndiyo jivunie kuwa na mtoto na wengine hawataona shida. Lakini kama ukimficha ficha, ukaficha ficha kama una mtoto basi hata huyo mwanaume hatampenda kama wewe mwenyewe humpendi na unamuona kama ni kikwazo badala ya baraka. Muhimu nikuwa usimuonyeshe kila mwanaume kama una mtoto, hapana muonyeshe yule ambaye kakuvutia na unaangalia unasema hapana huyu naweza kuwa naye kama mume. Achana na wale wa siku moja, kanyaga twende, wale usiwaambie mambo mengi ila kama unaona ni mtu ambaye umemtamani hata kama yeye huoni kama anataka kitu siriasi kama moyo wako umemdondokea basi muamini na muambie. Hii ikimaanisha kuwa hata kama akikukataa sababu ya mtoto akukatae kabla hujampa moyo wako. Lakini hata kama akija kukukataa huko mbeleni, au mkavunjana na kisha akakupotezea wala usiwaze kama ni sababu ya mtoto, kuna wengi sana ambao huachwa na bikira zao wapya kabisa hivyo kuachwa na mwanaume kusiipeleke akili yako kuwa ni sababu una mtoto. Furahia mahusiano yako furahia kuwa na mtoto na utona wengine nao hufurahia. Usmsingizie mtoto kwa kushindwa kuwa na mtu, hapana wapo wengi ambao hawana wati na wala hata hawajaanza mapenzi na wapo wenye watoto mpaka watatu na wanaume wanawahangaikia kila siku. Muhimu acha kuwa mtu wahuzuni, kukatakata tamaa na kulia lia hapana ukiwa mtu wa majonzi basi utawakimbiza wanaume, badilika. #SHARE #ShuleRafiki #ChaguaFuraha

at 9:20 PM

Bagikan ke

Lintaskan

0 comments:

Copyright © 2025 Braytonofficiallove
Designed by Siyamdezign | Edited By braytonofficiallove
braytonofficiallove | braytonofficiallove | braytonofficiallove
Powered By Blogger
Back to Top