Sunday, October 6, 2019

*MAMBO 10 YA KUMFANYIA MKEO KILA SIKU* ...... _Kuna mambo madogo madogo ambayo unatakiwa kumfanyia mkeo kila siku ili kuufanya uhusiano wenu uendelee kuwa hai._ ...... _Yanaweza kuwa madogo lakini yanaleta tofauti kubwa sana. Ifuatayo ni orodha ya mambo 10 unayoweza kumfanyia kila siku:_ πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’– *1. Wapende watoto wake:* ...... _Kama mna watoto, hakuna kitakachomfurahisha sana kama kukuona kama baba mwenye upendo._ πŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’ž *2. Mbusu:* ...... _Kila unapotoka na kuingia nyumbani, mbusu. Hakika busu linatuma ujumbe maridhawa kwenye moyo wake._ πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’– *3. Mkumbatie:* ...... _Kumbatio huwaweka karibu na humfanya ajihisi amani na kuwa na hisia ya kupendwa. Inapendekezwa kuwa umguse mkeo angalau mara 31 kwa siku._ πŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’ž *4. Mpe sifa ya kipekee:* ...... _Kuna vitu vingi vya kuvutia kuhusu mkeo. Kila siku tafuta kitu kipya na umwambie kuhusu kitu hicho. Mpambe na umsifu._ πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’– *5. Mchokoze:* ...... _Wakati fulani mkeo anahitaji kukumbushwa kuwa anatakiwa kuwa laini na asiyekuwa na ugumu; anahitaji kutaniwa, kuchokozwa na kuchekeshwa._ πŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’ž *6. Mfanye ajisikie kuwa yu salama:* ...... _Fungeni milango na umbebe, hasa kama nje kuna watu au kuna kelele zinazowanyima utulivu._ πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’– *7. Zima simu yako:* ...... _Tenga muda angalau kidogo wakati wa usiku na ukae na mkeo badala ya simu yako._ πŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’ž *8. Muombee dua:* ...... _Kila siku katika sala na maombi yako, usimsahau mkeo… muombee kwa Allaah ._ πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’–πŸ’– *9. Mchekeshe:* ...... _Kama unaweza kumchekesha kila siku, mtaweza kukabiliana na chochote._ πŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’žπŸ’ž *10. Mwambie* *“Ninakupenda”:* ...... _Kila siku litamke neno hilo, hatochoka kulisikia na kulisikiliza._ πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’– πŸ’ž *MAFUNZO YA NDOA* πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’žπŸ’–πŸ’–πŸ’ž

No comments:

Post a Comment