Home → simulizi
→ JINA: NYOKA WA KUTUMWA
SEHEMU YA 3
………… ILIPOISHIA SEHEMU YA PILI ………….
Huyo kijana bila kujua akasogea mpaka karibu na sehemu ambayo Yoka alikuwa amekaa akimvizia, ndipo yoka akaruka na kumbana yule kijana mguuni , kijana aligumia sana na kuanza kuangalia chini ili aone ni kitu gani ambacho kilikuwa kimemng'ata ila kwa bahat mbaya akufanikiwa kuona maana yoka baada ya kufanya vile tu akapotea. Ndugu wa yule kijana baada ya kusikia ile sauti ya ndugu yao ikipga kelele walitoka nje haraka na kwenda kuangalia kilichompata. Walipofika walimkuta ndugu yao akiwa amekaa chini huku akiwa amejishika mguuni, wakaanza kumuuliza maswali nini kimempata ndipo akaanza kueleza kilichomtokea.
………… Inaendelea ………………………..
NDUGU 1: Kaka kwani umepatwa na tatizo gani?
KIJANA: Mimi sijui jamani ila nahisi kuna mdudu ameniuma lakini sijajua ni mdudu gani nilipoangalia chini sikumuona.
NDUGU 2: sasa itakuwa nini hiko?
KJNA: hata sijui . { alijibu huku akiwa analia kutokana na maumivu makali ambayo alikuwa anayapata }
NDUGU 1: Basi tumpeleke ndani ili tuone hiyo sehemu aliyobanwa maana hapa atupaoni kutokana na hili giza.
Ndugu yake mwingine alitoa hilo wazo baada ya kushindwa kuona sehemu alipokuwa ameumia kutokana na giza nene lililope sehemu ile. Walimchukua yule kijina na kumpeleka ndani kuangalia hiyo sehemu ambayo alikiwa ameng'atwa, wakamuweka karibu na taa na kuanza kumkagua wakabahatika kupaona sehemu ambayo yule ndugu yao alikuwa ameng'atwa maana ilikuwa inamatobo manne pia ilikuwa nyeusi kama amepaka masizi. Kutokana na ile hali walioina kwenye kile kidonda moja kwa moja wakagundua ndugu yao alikuwa kabanwa na nyoka tena mwenye suma kali, ndipo wakaanza kutafuta dawa za kumsaidia kupunguza maumivu na kufanya ile sumu isiendee kumletea matatizo zaidi mwilini mwake. Waliangahika huku na kule kwa majirani zao wakitafuta dawa ya kumsaidia ndugu yao hatimae wakafanikiwa kuipata kisha wakampatia. Kwa mawazo yao walidhani kama wamefanikiwa kumsaidia ndugu yao kwa kumpatia ile dawa kumbe ilkuwa tofauti kabisa maana siku iliyofuatia asubuhi walimkuta ndugu yao akiwa ana hali mbaya na kile kidonda kikiwa kimechimbika na nyama ya ile sehemu kuoza. Jambo lile liliwashangaza sana wale ndugu zake maana ile dawa ambayo walimpatia usiku ilikuwa mzuri kwa kutibia sumu ya nyoka. Walipoona vile wakamchukua ndugu yao na kwenda nae kwa tabibu wa kijiji kwa ajili ya kupata dawa ambayo ingezeweza kumsaidia ndugu yao, walipofika wakamuelekeza kila kitu kilichompata ndugu yao.
NDUGU 1: Tabibu tumekuja tumemleta huyu ndugu yetu kapatwa na matatzo.
TABIBU: Matatizo gani ? { Aliuliza huku akimtazama mgonjwa }
Baada ya kuuliza vile ndipo wale ndugu wa yule kijina wakaanza kumsimulia.
NDUGU 1: Hayo matatizo amepata usiku wakati ameenda kujisadia na mwenyewe amesema kuna mdudu amemng'ata na sisi baada ya kumuangalia vizuri tukagundua kuwa kabanwa na nyoka. Kwahyo tukamtafutia ile dawa ya kutulizia maumivu pamoja na kupunguz a makali ya sumu tukampatia tukiamini kuwa tumemsaidia ndugu yetu cha ajabu leo asubuhi tumeamka tumemkuta akiwa kwenye hii hali.
Walipomaliza tabibu akaanza kuangalia kile kidonda cha yule kijana na kuwaeleza alichokiona yeye.
TABIBU: Jamani nimekiangalia kile kidonda inaonyesha ni kweli kang'atwa na nyoka tena mwenye sumu kali ila sasa kinacho nishangaza, kama mulimpa dawa kwanini awe kwenye hali kama ile maana mimi ninavyoijua dawa ile hata kama ukabanwa na nyoka wa aina gani endapo utaitumia lazima upate uafadhali sasa imekuaje kwa huyu mwenzenu ? { Aliongea kwa mshangao mkubwa }
NDUGU 1: Na ndio maana hata sisi tumeshangaa.
TABIBU: Alafu mbona kile kidonda chake kimechimbika vile na nyama yake naona imekuwa nyeusi sana imekuwaje ?
NDUGU 2: Hata hatufahamu na ndio maana tumekuja kwako ili utusaidie.
TABIBU: Mh hili ni tatizo kubwa na mimi wala sina dawa ya kumsaidia kutokana na tatizo lake maana dawa niliyonayo mimi ndio kama mliotumia huko kwenu.
Walipojibiwa vile waliumia sana na kuanza kumuangalia ndugu yao kwa huzuni, lakini hawakukata tama waliendelea kumuuliza tabibu maswali zaidi ili wapate msaada kwa ndugu yao.
NDUGU 2 : Kwahiyo tufanye nini maana sisi tunakutegemea wewe.
TABIBU: Mimi ninaona bora tumpeleke kwa mfalme ili atangazie watu kama kuna mtu atakaweza kumsaidia kabla ajapata madhara makubwa.
Aliposema vile wote walikubali na kumchukua yule ndugu yao na kumpeleka nyumbani kwa mfalme kwa ajili ya kuwatangazia watu ili wamsaidie kumpa dawa za kumponyesha.
Walipofka kwa mfalme wakasalimiana nae kisha tabibu akaanza kumwambia mfalme juu ya tatizo lililomkuta yule kijana.
TABIBU: mtukufu mfalme huyu kijina kapatwa na matatizo jana usiku.
Mfalme alishangaa kusia vile maana hata siku moja yule tatbibu hakuwai kumpeleka mgonjwa pale kwake,.
MFALME: Matatizo gani hayo tabibu?
TABIBU: Jana usiku huyu kijana alitoka nje kujisahdia ila kwa bahati mbaya aling'atwa na mdudu na baada ya kumchunguza vizuri tukagundua aling'atwa na nyoka. Ila cha ajabu amepewa ile dawa ya kuzuia sumu ya nyoka ila hali yake bado imekuwa mbaya zaidi.
MFALME: Sasa wewe ndio tabibu wa hiki kijiji cha mbaka unamsaidiaje huyu kijana?
TABIBU: Kusema kweli mtukufu mfalme mimi nimeshindwa kumsaidia kwa sababu dawa niliyonayo mimi ndio ambayo amepewa na haikumsaidia ndio maana nikaona bora nimlete kwako ili uwatangazie wanakijiji wengi waje kumsaidia.
MFALME; Sasa kama wewe umeshindwa nani ataweza kumsaidia na wakati wewe ndio unategemewa hapa kijijini.
TABIBU; Ni kwel mtukufu mfalme ila kwa hili lpo nje ya uwezo wangu na ndio maana nikaona bora uwatangazie watu wengine ili waje wamsaidie kama wao wataweza.
MFALME: Sawa nmekuelrwa.
Mfalme akamuagiza kijina apige ng'oma ya dharula kwa ajili ya kuwaita wanakijiji katika ule uwanja wao wa mkutano, kijana akafanya kama alivyo agizwa. Wakati inapigwa ile ng'oma mzee sube pamoja na mke wake walibahatka kuisikia ile sauti na moja kwa moja wakahisi kuwa labda Yule nyoka wao mwenye jina la YOKA alikuwa kafanya kazi yake ambayo alikuwa ametumwa, mzee sube akamuomba mke wake abaki pale nyumbani na yeye aende huko kwa mfalme.
MZEE SUBE : Mke wangu hiyo ng'oma inayopigwa huko nahisi kunatatizo limetokea kwa mfalme alafu kichwani mwangu naona hilo tatizo kama kalisababsha Yoka.
BIBI SUBE: Yani kama ulikuwa kichwani mwangu hivi maana hata mimi ninmehisi hivyo hivyo
MZEE SUBE: Sasa tufanye kitu kmoja mimi ngoja niende alafu wewe baki hapa nyumbani chochote kitakachotokea kule nitakuja kukuambia.
BIBI SUBE: Sawa safari njema ila kuwa makini.
MZEE SUBE: Wala usijari mke wangu.
Mzee sube akatoka nje na kuanza safari ya kwenda nyumbani kwa mfalme, alijtahi kutembea haraka sana na hatimae akafika na kuwakuta watu wengine wameshafika pale uwanja ndipo mfalme akasimama akawasalimia wanakijiji na kuanza kuongea juu ya jambo ambalo limfanya awaite pale.
MFALME: Jamani wananchi wa hiki kijiji cha mbaka nimewaita hapa kwa ajili ya jambo moja na ninahitaji msaada wenu juu ya jambo hili.
Mfalme baada ya kusema vile ndipo wanakijiji wakaanza kutazamana huku wengine wakiwa wananong'ona wakiulizana Ila kwa upande wa mzee sube moyo wake ulikuwa unaenda mbio na hakutaka kuongea na mtu yoyote bali alikuwa makini kusikiliza anachokisema mfalme, wanakijiji waliponyamaza mfalme akaendelea kuongea.
MFALME: Jambo lenyewe ni hili , hapa kuna kijana ameletwa ameumwa na nyoka na alipewa ile dawa ambayo huwa tunaitumiaga kuuwa sumu ya nyoka ila bado hali yake mbaya .Kwahiyo mimi sipo tayari kumpoteza huyu kijina kama kuna mtu anadawa ya kumsaidia naomba ajitokeze ila iwe tofauti na ile dawa ya kijiji iliyotengenezwa na mababu zetu.
Mzee sube aliposikia vile moyo wake ulilpuka kutokana na furaha ambayo alikuwa nayo, haraka bila uwoga akapita mbele na kumueleza mfalme kuwa yeye anaweza kumsaidia yule kijana, Mfalme alifurahi sana kusikia vile mda huo wananchi walikuwa wakinong’onezana kutoka na mzee sube kujitokeza.
MZEE SUBE: Mtukufu mfalme mimi ninaweza kumsaidia huyo kijana.
MFALME: Kweli mzee ?
MZEE SUBE: kweli mtukufu mfalme.
MFALME: Aya mzee anza kazi na endapo utafanikiwa kumsaidia huyu kijana nitakupatia zawadi.
MZEE SUBE: Sawa mtukufu mfalme ila naomba uniruhusu nikachukue dawa yangu nyumbani ninakuahidi huyu kijna atakuwa mzima kabisa.
MFALME: Sawa fanya haraka kabla hatujampoteza huyu kijana.
Baada kuruhusiwa akakimbia haraka na akafanikiwa kufika nyumbani kwake na kumkuta mke wake akiwa amekaa kwenye mkeka ajui hili wala lile linaloendelea kwenye mkutano kule kwa mfalme. Alipofika alikuwa anahema haraka haraka kutokana na kukimbia kwa speed { haraka } Baada ya kukaa sawa ndipo akamsimulia mke wake kwa ufupi kilchotokea kwa mfalme.
SEHEMU YA 4
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: