Home → simulizi
→ ®HADITHI PICHA®
Mussabhai & YuYuShortstory
👙👙👙 DADA VUA👙👙👙
PICHA NO:_3
Huku upande wa pili Bright(Sule) na Hellen(Helena) Waliagana kila mmoja akimgeukia mwenzake,Helena alimtazama kwa umakini sana huyu kijana na kugundua ya kuwa Sule alikuwa na mawazo sana.Helena aliamua kusimama na kumtazama.Helena alishusha ndoo yake kisha akaamua kumfuata huku akaita "BRIGHT!!! WEE BRIGHT!!!!"
Shuka nayo.........MKIWA WAVIVU KULIKE NAMI NTAKUA MZEMBE KUPOST.DONDOSHA LIKE NA MAONI YAKO
Maadam hellen aliamua kumuita Bright,Bright alisimama kwanza kwa sekunde kadhaa lakini hakugeuka kumtazama Hellen.Hellen alimuita tena " Sasa si uje heee!!!",Kiukweli Sule alivyoachana na Helena alifika mbali sana kimawazo mpaka akajikuta chozi likimdondoka.Sasa baada ya helena kumuita hakugeuka kwa sababu angegundulika kuwa alikuwa analia,Alijifuta machozi haraka haraka kisha akageuka akiwa na tabasamu feki ili kumzuga binti yule mrembo.Hellen alipomtazama Sule aligundua kuwa kuna kitu kinamsibu"Wee Bright uko sawa kweli!!!?"........"Yaah mbona niko poa kwani vipi!!!?........"Huenda hauko vizur ila wanificha tuu,nimekuona mwendo wako yaani kama vile kuna kitu kinakuumiza kichwa? We nambie tuu naweza kukusaidia hata kimawazo eti!!".Sule alikaa kimya kwa sekunde kadhaa akitafakari kwani helena kampa swali ambalo kiukweli sule anahitaji ushauri.
Baada ya Helena kuona Sule kawa mzito kumuelezea kinachomsibu alijaribu kumbembeleza ili wafike hata nyumbani kabla hajaendelea na safari yake.Sule hakuwa na kipingamizi kwani hata anakoenda hana uhakika sana kama atafanikiwa kupata shughuli aliyoikusudia.Helena alijaribu kutumia maneno mazur ili kumuweka sawa huyu kijana Sule.Sule alimuuliza Helena"Sasa Hellen unaishi na nani hapo kwenu!!?"...... Helena alicheka"hehee!! mbona unajishuku sana usiogope Bright naishi na dada yangu pamoja na Shangazi"......."Sule alitamani kumjua kiundani zaidi lakini aliona kama atamchosha binti kwa maswali"mmmmmh!! haya lakiiiiini!!!?"....."Bright acha maswali ya uoga we twende?".Yalikuwa ni mazungumzo ambayo yalimshawishi kidume huyo kukubaliana na sweet manka HELLEN.
Wakati huo shangazi yake helena alikuwa kwenye banda la mifugo akiwahudumia wanyama wake kwani anapenda sana ufugaji.Shangazi alitupa macho kwa mbali alimuona Helena akiwa anakuja na mtu asiyemjua.Shangazi alimuita dada yake Helena"Weee Lucy!!!!".....Lucy alikuwa chumbani"Beee!!"....."Njoo uone huyu mwenzako zoa zoa sijui kabeba limtu gani!!?".Kiufupi shangazi huyu huwa hapendi sana wageni nyumbani kwake na hataki kabisa kina Helena wazoeane na mwanaume yoyote.Basi Lucy alivyosikia vile alitoka kisha akasimama nje na kutazama kule wanakotokea kina helena.Lucy alitazama kisha akarudi ndani haraka,Alivyofika akabadili nguo alizokuwa amezivaa alichukua kioo kisha akaanza kujaribu kama ataweza kucheza na lips ili kumtega huyu jamaa anayekuja na mdogo wake.Aliweka kila aina ya pozi kisha akajipuliza marashi na kutoka.
Wakati huo shangazi yake Helena aliacha hadi kuihudumia mifugo akabaki anamshangaa yule kijana,Alimtazama kwa hasira sana.
HUKU NYUMBA KWA KINA SULE
Baada ya Baba kukataa kabisa swala la kumgawia Sule mali wadogo zake waliamua kumpigia Simu sule ili arudi wakati wanaendelea kumbembeleza baba yao.Wedi alichukua simu kisha akawa anampigia kaka yake Sule,Simu ya Sule iliita lakini haikupokelewa.Wakati anaendelea kupiga mara Sudi alikuja huku akiongea "Simu yenyewe kaiacha chumbani kwake hii hapa".Kweli Sule aliiacha simu ndani na sijui kasahau au aliamua tuu.Wedi alizidi kupata hofu kwani anajua hasira za kaka yake"mhhhh! sasa kwanini kaacha simu!? usikute kaamua kufanya jambo lingine tofaouti" Yalikuwa ni mawazo ya Wedi.Wedi alimfuata mama yake na kumwambia"Mama unafikiria nini kuhusu swala la kaka Sule"......."Achana nae kwanza ana kiburi sana akiamua kurudi atarudi tuu".Wedi alitegemea mama atasaidia kumshawishi baba lakini alionekana kama hajali wala halimuumi swala la Sule kuondoka pale nyumbani.
HUKU KWA KINA HELENA
Lucy alitoka akiwa amejipodoa kweli kweli huku akizichezesha lips zake kama alivyokuwa akifanya zoezi kwenye kioo.Mara simu ya Shangazi iliita akawa anaongea huku akimtazama sana Sule,Sule hakujua ni kwanini Bibi huyu anamuangali huku anaongea na simu.Alimaliza kuongea na simu kisha akampokea Helena kwa maneno"We helena muda wote huo hayo maji ulienda kuyateka Usa au".
📝KWA WALE MLIOWAHI KUFIKA ARUSHA NADHANI MNAJUA USA IKO WAPI NA HUU MSITU WA MOMELA UKO WAPI📝
Basi Shangazi alimfokea bila kujali kuwa kuna ugeni amekuja nao,Helena hakujibu kitu shangazi alitupa tena dongo"Eheee na huyo ni nani!?? maana wewe hukawii kuniletea mijizi".......Lucy alidakia ....."Looooh!! shaangazi huogopi kutoa mineno hadi kwa wageni".Sule kuona vile alimwambia Helena"Aaaaamh!! hellen acha mi niende nisije kukugombanisha na shangazi yako"......"Bright usiogope huyu yukogo hivi anapenda sana kuongea".....Lucy naye alijichangamsha kwa Sule kama vile anamjua wakati ndio mara ya wa kwanza wanaonana "Kakaaa karibu usiogope mwaya karibu sana".Helena alitangulia ndani akiwa amebeba ndoo yake akawaacha Lucy na Sule nyuma.Lucy alikuwa na machachari sana mpaka Sule alishangaa" Mhhhhh!! huyu dada vipi kadata au!??" Mara Lucy akafunua kidogo nguo yake kwa pale kwenye nyonyo huku akimuonyesha Sule Vichuchu.......Usikose sehemu inayofuata maana hii ni zaidi ya movie.
usiache kudondosha like kwani bila like mimi sipati mizuka yakuleta vitu adimu.
®HADITHI PICHA® Mussabhai & YuYuShortstory 👙👙👙 DADA VUA👙👙👙 PICHA NO:_3 Huku upande wa pili Bright(Sule) na Hellen(Helena) Waliagana kila mmoja akimgeukia mwenzake,Helena alimtazama kwa umakini sana huyu kijana na kugundua ya kuwa Sule alikuwa na mawazo sana.Helena aliamua kusimama na kumtazama.Helena alishusha ndoo yake kisha akaamua kumfuata huku akaita "BRIGHT!!! WEE BRIGHT!!!!" Shuka nayo.........MKIWA WAVIVU KULIKE NAMI NTAKUA MZEMBE KUPOST.DONDOSHA LIKE NA MAONI YAKO Maadam hellen aliamua kumuita Bright,Bright alisimama kwanza kwa sekunde kadhaa lakini hakugeuka kumtazama Hellen.Hellen alimuita tena " Sasa si uje heee!!!",Kiukweli Sule alivyoachana na Helena alifika mbali sana kimawazo mpaka akajikuta chozi likimdondoka.Sasa baada ya helena kumuita hakugeuka kwa sababu angegundulika kuwa alikuwa analia,Alijifuta machozi haraka haraka kisha akageuka akiwa na tabasamu feki ili kumzuga binti yule mrembo.Hellen alipomtazama Sule aligundua kuwa kuna kitu kinamsibu"Wee Bright uko sawa kweli!!!?"........"Yaah mbona niko poa kwani vipi!!!?........"Huenda hauko vizur ila wanificha tuu,nimekuona mwendo wako yaani kama vile kuna kitu kinakuumiza kichwa? We nambie tuu naweza kukusaidia hata kimawazo eti!!".Sule alikaa kimya kwa sekunde kadhaa akitafakari kwani helena kampa swali ambalo kiukweli sule anahitaji ushauri. Baada ya Helena kuona Sule kawa mzito kumuelezea kinachomsibu alijaribu kumbembeleza ili wafike hata nyumbani kabla hajaendelea na safari yake.Sule hakuwa na kipingamizi kwani hata anakoenda hana uhakika sana kama atafanikiwa kupata shughuli aliyoikusudia.Helena alijaribu kutumia maneno mazur ili kumuweka sawa huyu kijana Sule.Sule alimuuliza Helena"Sasa Hellen unaishi na nani hapo kwenu!!?"...... Helena alicheka"hehee!! mbona unajishuku sana usiogope Bright naishi na dada yangu pamoja na Shangazi"......."Sule alitamani kumjua kiundani zaidi lakini aliona kama atamchosha binti kwa maswali"mmmmmh!! haya lakiiiiini!!!?"....."Bright acha maswali ya uoga we twende?".Yalikuwa ni mazungumzo ambayo yalimshawishi kidume huyo kukubaliana na sweet manka HELLEN. Wakati huo shangazi yake helena alikuwa kwenye banda la mifugo akiwahudumia wanyama wake kwani anapenda sana ufugaji.Shangazi alitupa macho kwa mbali alimuona Helena akiwa anakuja na mtu asiyemjua.Shangazi alimuita dada yake Helena"Weee Lucy!!!!".....Lucy alikuwa chumbani"Beee!!"....."Njoo uone huyu mwenzako zoa zoa sijui kabeba limtu gani!!?".Kiufupi shangazi huyu huwa hapendi sana wageni nyumbani kwake na hataki kabisa kina Helena wazoeane na mwanaume yoyote.Basi Lucy alivyosikia vile alitoka kisha akasimama nje na kutazama kule wanakotokea kina helena.Lucy alitazama kisha akarudi ndani haraka,Alivyofika akabadili nguo alizokuwa amezivaa alichukua kioo kisha akaanza kujaribu kama ataweza kucheza na lips ili kumtega huyu jamaa anayekuja na mdogo wake.Aliweka kila aina ya pozi kisha akajipuliza marashi na kutoka. Wakati huo shangazi yake Helena aliacha hadi kuihudumia mifugo akabaki anamshangaa yule kijana,Alimtazama kwa hasira sana. HUKU NYUMBA KWA KINA SULE Baada ya Baba kukataa kabisa swala la kumgawia Sule mali wadogo zake waliamua kumpigia Simu sule ili arudi wakati wanaendelea kumbembeleza baba yao.Wedi alichukua simu kisha akawa anampigia kaka yake Sule,Simu ya Sule iliita lakini haikupokelewa.Wakati anaendelea kupiga mara Sudi alikuja huku akiongea "Simu yenyewe kaiacha chumbani kwake hii hapa".Kweli Sule aliiacha simu ndani na sijui kasahau au aliamua tuu.Wedi alizidi kupata hofu kwani anajua hasira za kaka yake"mhhhh! sasa kwanini kaacha simu!? usikute kaamua kufanya jambo lingine tofaouti" Yalikuwa ni mawazo ya Wedi.Wedi alimfuata mama yake na kumwambia"Mama unafikiria nini kuhusu swala la kaka Sule"......."Achana nae kwanza ana kiburi sana akiamua kurudi atarudi tuu".Wedi alitegemea mama atasaidia kumshawishi baba lakini alionekana kama hajali wala halimuumi swala la Sule kuondoka pale nyumbani. HUKU KWA KINA HELENA Lucy alitoka akiwa amejipodoa kweli kweli huku akizichezesha lips zake kama alivyokuwa akifanya zoezi kwenye kioo.Mara simu ya Shangazi iliita akawa anaongea huku akimtazama sana Sule,Sule hakujua ni kwanini Bibi huyu anamuangali huku anaongea na simu.Alimaliza kuongea na simu kisha akampokea Helena kwa maneno"We helena muda wote huo hayo maji ulienda kuyateka Usa au". 📝KWA WALE MLIOWAHI KUFIKA ARUSHA NADHANI MNAJUA USA IKO WAPI NA HUU MSITU WA MOMELA UKO WAPI📝 Basi Shangazi alimfokea bila kujali kuwa kuna ugeni amekuja nao,Helena hakujibu kitu shangazi alitupa tena dongo"Eheee na huyo ni nani!?? maana wewe hukawii kuniletea mijizi".......Lucy alidakia ....."Looooh!! shaangazi huogopi kutoa mineno hadi kwa wageni".Sule kuona vile alimwambia Helena"Aaaaamh!! hellen acha mi niende nisije kukugombanisha na shangazi yako"......"Bright usiogope huyu yukogo hivi anapenda sana kuongea".....Lucy naye alijichangamsha kwa Sule kama vile anamjua wakati ndio mara ya wa kwanza wanaonana "Kakaaa karibu usiogope mwaya karibu sana".Helena alitangulia ndani akiwa amebeba ndoo yake akawaacha Lucy na Sule nyuma.Lucy alikuwa na machachari sana mpaka Sule alishangaa" Mhhhhh!! huyu dada vipi kadata au!??" Mara Lucy akafunua kidogo nguo yake kwa pale kwenye nyonyo huku akimuonyesha Sule Vichuchu.......Usikose sehemu inayofuata maana hii ni zaidi ya movie. usiache kudondosha like kwani bila like mimi sipati mizuka yakuleta vitu adimu.
Artikel Terkait
*Love bite* Sehemu Ya Kwanza (1) Ni siku ya jumapili iliyokuwa na kila aina ya mchanganyiko wa watu kutoka sehemu mbali mbali walionekana kwenye kumbi za starehe. Wengi ambao walikua wanapenda taarab basi walijazana travertine hotel kuwaangalia jahazi. Kwa wengine wanaopenda bongo flavour basi walikutana bills,maisha,masai..Dar live na kumbi zingine zilikuwa na wasanii pendwa waliokuwa wanaburudisha week end hiyo. JOTHAN alikua anapendelea sana mixing za ma dj mbali mbali. Hivyo jumapili hiyo aliamua kwenda coco beach usiku huo. Upepo mwanana uliokuwa ukipuliza huko coco beach na ukichanganya na big screen iliyokuwa inaenda sambamba na mixing za maana alizokuwa anazipiga dj huyo aliyezikonga roho za watu wengi waliokuwa pale, iilikuwa burudani tosha kwa waliohudhuria usiku ule. Jotham alipaki gari yake pembeni, alichagua kiti kilichukokuwa karibu na meza ya mwisho na kuagiza kinywaji alichokipendelea na kuendelea kufurahia mziki uliokuwa unaonyeshwa kwenye screen hiyo. Mara kwa mara madada poa walikuwa wanajipitisha pale alipo, lakini aliwachora tu na hakuwa na mpango nao. Baada ya dakika kadhaa, walitokea madada watatu waliokuwa wameingia pale coco beach na kuanza kutafuta mahali pa kukaa. Waliangaza meza nyingi zilikua na nafasi ya mtu mmoja au wawili tu na wao walikuwa na lengo la kukaa wote watatu kwenye meza moja. Baada ya kuangaza kwa muda, waliiona meza aliyokaa Jothan ikiwa na nafasi tatu za kukaa. Waliisogelea ile meza na walipokaribia tu kuifikia ile meza. Walishuhudia jamaa mmoja akiwa ameenda kukaa pale. “wewe kaka sogea sehemu yetu.” Aliongea mmoja kati ya wale wadada watatu baada tu ya kuifikia ile meza. “mbona hakuna alama yoyote kuwa mlikaa hapa. Hakuna vinywaji wala kitu chochote.” Aliongea yule jamaa huku akionyesha wazi kuvutiwa na ile sehemu iliyokuwa chemba lakini ikiwa inaonyesha vizuri ile tv. “ni vyema uwapishe kwa sababu waongeacho sio uongo.” Aliongea Jotham kumwambia yule jamaa. Hakuwa anapenda makelele ambayo alijua yatatokea baada ya mvutano huo wa kugombania ile sehemu. Yule jamaa akaamua kunyanyuka na kuwapisha wale warembo na yeye kwenda kukaa meza nyingine. “ahsante sana kaka, maana yule jamaa alitaka atubanie wakati sisi tumehangaika kutafuta meza tutakayokaa wote watatu”. Aliongea yule dada aliyeonekana kama kiongozi wao. Mavazi waliyovaa yalitosha kumshawishi mvulana yeyote rijali na kufanya iwe lazima macho ya matamanio kumtoka. Uzuri wa mabinti hao likuwa unashinda lakini huyo aliyekuwa kiongozi wao aliwazidi wenzake kwa kila kitu. Macho ya Jotham yaliona kila kitu kutoka kwa binti huyo mbichi. Chuchu zilitokeza kwa kujichora kwenye gauni ile nyepesi ambayo haikuwa na nguo nyingine ndani. “sikiliza oda zao, ziingize kwenye bili yangu” aliongea Jotham baada ya kumuita muhudumu aliyekuwa anamuhudumia toka afike pale. “ahsante.” Waliitikia wale madada baada ya kupewa ofa hiyo. Waliagiza vyakula na vinyaji walivyopendelea. Walipiga story za kawaida huku wakigongeana glass za vinywaji na kucheka. Jotham alikuwa kimya wakati wote huku akiwa bize kuangalia na kusikiliza mixing ambazo ndizo zilizomleta pale. Baada ya masaa kadhaa, alimuita muhudumu na kulipia bili yake. “ahsante kwa ofa yako.” Aliongea yule kiongozi wao baada ya Jotham kuwaaga. Jotham aliingia kwenye gari yake aina ya opah na kuondoka eneo hilo. Njiani alimkumbuka yule dada lakini aliishia kucheka tu kwakua hakuwa na hisia zozote za mapenzi juu yake. Zaidi alimtamani kuwa nae japo kwa usiku mmoja kwa jinsi alivyotoka. Hakika alikuwa na kila aina ya uchochezi wa kufanya ngono. Alifika kwake usiku mnene na kwenda kulala fofofo kutokana na usingizi uliojaa wakati huo. Asubuhi aliamka na uchovu tele na kwenda kuoga ili kujaribu kuupunguza uchovu aliokuwa nao. Alipomaliza kuoga. Alijiandaa tayari kwa kwenda kazini. Alisumbuka sana kuwasha gari lake lakini halikuwaka. Alipoangalia mafuta, aligundua kuwa wese lilikuwa limekata. Kwa kuhofia kuchelewa zaidi kazini, aliamua kwenda kituoni na kupanda daladala. Alifika kazini huku macho yake yakiwa mekundu yaliyoashiria kuwa bado alikuwa na usingizi. “mshikaji bora ukapate supu, maana hiyo harufu ya pombe uliyamka nayo ni noma. Utaongea vipi na bosi?” alishauri mmoja wa wafanyakazi wenzake aliyekuwa karibu naye. “poa, ngoja nielekee canteen basi.” Aliongea Jothan na kwenda canteen kupata supu ya mbuzi na chapati. Baada ya kunywa chai, alirudi na kuendelea na kazi. Saa nane ndio muda waliokuwa wanatoka kazini. Alienda kupata chakula cha mchana canteen na kuondoka zake kuelekea kituo cha daladala ambacho hakikuwa mbali na ofisini kwao. Alisubiri daladala kwa muda na kupanda gari iliyokuwa inaelekea mwenge kwa malengo ya kushuka kinondoni anapoishi. Usingizi ulichukua nafasi yake baada ya kupanda tu lile gari lililokuwa likisubiri abiria kwa dakika kadhaa pale kituoni Baada ya muda mrefu kidogo kupita, aliamka na kuangalia gari lilikuwa limefika wapi. Wakati akiwa anaanga angaza, macho yake yaligongana na yule mrembo aliyekuwa naye kwenye meza moja siku ya jana yake. Wote walikumbukana na kila mmoja akamuachia mwenzake tabasamu. Hapo alifanikiwa kumuona vizuri huyo msichana mwenye kila sifa ya uzuri. Usingizi uliendelea kumzonga Jotham na kujikuta anapitiwa na usingizi bila kuongea chochote na yule msichana. Gari lilifika mpaka mwenge na kupitiliza kituo alichokua anashuka Jothan. Aliamshwa na konda baada gari kushusha abiria wote. “tuko wapi hapa.” Aliuliza Jothan baada ya kuamka na kuangalia nje ambapo kulikua tofauti na mazingira anayoishi. “tumeshafika mwenge kaka.” Alijibu yule konda. Jothan aliangalia huku na kule na hakuona abiria yeyote aliyekuwa kwenye lile gari zaidi yake. Hakusikitika kupitishwa kituo, bali alisikitika sana kutochukua namba wala kujua jina la yule msichana aliyevutika naye zaidi baada ya kuonana nae kwa mara ya pili. Hakua na budi Jotham, zaidi ya kubaki ndani ya daladala na kugeuza nalo. Alipofika kinondoni kwa manyanya alishuka na kufuata njia ilyoelekea shule ya kambangwa secondary school na kupita chuo cha tumaini na kuingia nyumbani kwake ambapo hapakuwa mbali na pale. Hakuwa na hela nyingi sana, ila uwezo wa kula anachokitaka na kubadilisha nguo alikuwa nao. Alifika nyumbani na kujilaza kitandani kwake. Aliamka sa tatu usiku na kutoka kwenda sheli kununua mafuta kwenye kidumu kisha akaenda bar ya jirani na kupata chipsi kuku kisha akarudi nyumbani na kufungua tv na kuangalia yaliyomo. Saa tano usiku alianza kunyemelewa na usingizi,. Alizima tv yake na kwenda kulala. Alijikuta yupo na msichana yule mzuri kwenye fukwe za bahari wakipanga maswala yao ya kuoana. Alitoa pete na kumvisha mwanamke huyo mwenye kila aina ya sifa zilizompeleka Jotham kudata juu yake. Alikurupuka asubuhi na kugundua kuwa hali ile haikuwa halisi, bali alikua anaota.. aliangalia Alarm yake ambayo ilikuwa inalia wakati huo na kuizima. Alijiandaa na kupanda gari yake ambayo alishainunulia mafuta na kwenda nayo kazini kama kawaida. Baada ya mwezi mmoja kupita, Jothan alipata uamisho kikazi kwa miezi sita huko Morogoro. Alilaani ila hakua na jinsi kukubaliana na matakwa ya kazi. Ile ndoto ya kukutana tena na yule msichana iliyeyuka kwakua alijua kabisa kuwa kukaa kwake huko marogoro utakuwa mwisho wa kukutana tena na yule msichana kwa miezi mingi. Siku ya safari ilipofika. Alijiandaa na kupitiwa na gari la ofini kwao na kusafiri pamoja na wenzake waliopata uhamisho huo wa muda huko morogoro. Alifanya kazi huko kwa miezi mitatu na kupelekwa Arusha kwa ajili ya kumalizia miezi hiyo mitatu iliyobakia. Nia na madhumuni ni kuwafundisha kazi wafanyakazi wa mikoa hiyo kwakua ofisi yao ilikua imefungua matawi mapya katika mikoa hiyo. Zikiwa zimebaki siku mbili kabla ya kurudi Dar, Jothan alipita barabara moja na kumkuta msichana mzuri akiwa ameshika tenga anauza maua. Moyo ulimlipuka ghafla na kujikuta anamsogelea yule dada bila kujitambua. “unauzaje maua” aliuliza Jothan huku akimuangalia binti yule mzuri ambaye alikua anatabasamu baada ya kumuona yeye pale. “shilingi elfu moja kwa kila moja.” Aliongea yule dada bila kumuangalia Jothan usoni. “nikitaka yote utaniuzia shilingi ngapi?” aliuliza Jothan huku akizidi kumtathmini binti yule huku akionyesha kufurahi na muonekano mzuri aliokuwa nao msichana huyo. “nisaidie kuhesabu, kisha nitajie idadi ili nikuuzie kwa bei ya jumla.” Aliongea yule dada na kumfanya Jothan kushangaa. Alijiuliza maswli ya haraka . labda hyule msichana hajui kusoma au alikua anamtega. “kwanini usiniambi tu, maana siyo mengi yaliyobaki.” Aliongea Jothan kwa sauti ya upole. “mi sioni kaka yangu.” Aliongea yule dada na kumfanya Jothan kupigwa na butwaa. “kweli???” aliuliza Jothan huku akiwa haamini alichoambiwa na yule dada. Kwa kumuonyeshea kuwa haoni, yule dada alivua miwani na kumuonyesha macho yake ambayo yalikuwa na watoto ndani. Aliingiwa na roho ya imani Jothan na kukiri moyoni kuwa yule dada alikua nahitaji msaada kwakua tatizo lake linatibika ila matibabu yake yalikuwa ghali sana. “unaishi mbali na hapa?” aliuliza Jothan baada ya kutoa noti ya shilingi elfu kumi na kuyachukua maua sita yaliyobakia. “si mbali na hapa, ni mtaa watatu hapo mbele.” Aliongea yule dada mwenye asili ya kichaga lakini asiyekuwa na lafudhi hiyo wala meno yake kuharibika. Ngozi yake ilikubali baridi na kuwa nyeupe yenye mvuto. “unaonaje kama nikikusindikiza?” aliuliza Jothan. “sawa” Alijibu yule dada na safari ya kuelekea kwao ilianza. Mwendo wa kuupapasa kwa fimbo ndio uliomfanya Jothan kuamini kuwa ni kweli huyo dada alikua kipofu. Alikaribishwa mpaka ndani na kukutana na mama yake huyo binti. “karibu baba,”alikaribisha mama yake yule dada na kuwapisha. “huyo ndio mama yangu wa peke, sina msaada mwengine zaidi yake.” Aliongea yule dada huku anatabasamu. Hakua anamuona Jothan ambaye wakati huo alikua anaumia juu ya msichana huyu ambaye alionyesha hali aliyokuwa nayo ameizoea. Aliaga baada ya kuongea na kupiga stori mbili tati ikiwemo maisha yao kwa ujumla. Alirudi kwenye nyumba waliyopangiwa na kumpa story rafiki yake anayekaa naye kwenye nyumba hiyo. “kwa hiyo unataka ufanyaje ndugu yangu,” aliuliza rafiki yake huyo baada ya kumpa mkanda mzima. “nitajitahidi kwa uwezo wangu wote ili BAHATI apone kabisa.” Aliongea Jothan na kumuonyesha rafiki yake ni jinsi gani ameguswa na mdada huyo. “kwa hiyo unampango wa kumchukua na kwenda naye Dar?” aliuliza rafiki yake huyo huku wakiendelea kula bisi zilizokuwa kwenye meza yao. “exactly” alijibu Jothan kiingereza kuonyesha msisitizo. Asubuhi ya siku ya pili, Jothan aliamka na kwenda tena kwa kina Bahati. Kabla hajafika, tayari alishamuana dada huyo mwenye juhudi na kazi yake akiwa barabarani kama kawaida yake akiuza maua. “mambo Bahati.” Alisalimia Jothan Kwakua sauti ya Jotham alikua ameshaijua, alimng`amua na kuachia tabasamu mwanana lililomuacha hoi Jotham. “safi” alijibu Bahati. Waliongea mengi na kubwa zaidi ni juu ya Jothan kumsaidia Bahati swala lake la macho. Bahati alifuraha sana na wote wakaenda kwa mama yake na kumpa taarifa zile njema. “nitashukuru sana mwanangu..mungu akuzidishie.” Aliongea mama yake Bahati na zoezi la kujiandaa kwa ajili ya safari ya Dar-es-salaam lilianza mara moja kwa kufua nguo zake chafu na kupanga zingine kwenye mabegi. “tutakupitia kesho saa kumi na mbili asubuhi.” Aliongea Jothan na kuaga. Bahati alipanga kila kitu chake akisaidiwa na mama yake tayari kwa safari ya kesho yake ambayo ilikuwa na matumaini makubwa kwake. Alisali na kumuomba mungu afike Dar salama na lengo la kufanyiwa upasuaji lifanikiwe kwa nguvu zake mungu wa viumbe vyote. Asubuhi na mapema gari ya kina Jothan ilimpitia Bahati na safari ya kuitafuta Dar-es-salaam ilianza. Njiani walipiga story na kucheka kama vile walikuwa wamezoeana muda mrefu au walikuwa wameshakutana kabla. Uchangamfu wa Bahati uliwapendeza watu wote waliokuwemo kwenye lile basi. Bahati alipendelea kukaa dirishani kwa ajili ya upepo. Lakini Jothan aliamini kuwa Bahati alikua anatamani pia kuona vilivyokuwa nje. Saa nane mchana walifika mombo na kupaki gari lao kwa ajili ya kupata chakula cha mchana. Waliokwenda haja walienda ilimradi safari ikiendelea pasiwe na usumbufu kati yao. “unapendelea chakula gani?” aliongea Jothan baada ya kuingia naye Bahati kwenye mgahawa huo. “kama kuna wali huwa napenda hata ikiwa na mboga yoyote.” Aliongea Bahati. Jothan alimuagizia wali na nyama ya kuku. “ahsante kwa chakula.” Aliongea Bahati baada ya kumaliza kula kile chakula. Baada ya hapo safari iliendelea na kufika ubungo saa kumi na mbili jioni. Safari ya kuwapeleka makwao ilianza na Jothan na Bahati walishuka kinodoni na kuingia ndani. Kutokana na uchovu wa safari, Jothan alimpeleka Bahati chumba atakachokuwa analala na kutoka nje kununua chakula watakachokula usiku huo. Baada ya kiza kutawla, Jothan alimpelekea chakula Bahati na kumuonyesha choo na bafu ambavyo vyote vilikua mule ndani kwenye kile chumba. Baada ya mapumziko ya siku mbili, Jothan alimpeleka Bahati kwenye hospitali kubwa ya macho CCBRT kwa ajili ya upasuaji. Vipimo vilileta majibu mazuri kuwa kulikowa na uwezekano mkubwa wa kutolewa hivyo vitoto vya jicho na Bahati kona tena. Tarehe ya upasuaji ilipangwa kwa ajili ya upasuaji huo na Jothan alimpeleka Bahati ili apate huduma hiyo ambayo kama itafanikiwa itakuwa imempa maisha mengine kabisa mrembo huyo ambaye alikuwa haoni toka alipozaliwa.. Muenendo mbaya wa utendaji kazi huko marogoro ndio uliomfanya Jothan kurudishwa tena mkoani humo. Alisikitika kumuacha mgeni wake katika hospitali kabla hajashuhudia matokeo ya upasuaji huo, lakini hakuwa na jinsi kwakua aliuachia uongozi jukumu la kumuangalia mgonjwa wake huyo. Miezi sita ilikatika akiwa huko Morogoro huku mawasiliano yakikosekana kati yake na Bahati. Hata alipouuliza uongozi wa kampuni yao walimwambia kuwa walikuwa wamempa kiasi cha hela baada ya kupona na tokea wamkabidhi hawakupata mawasiliano naye. Mawazo yalimsonga Jothan na hakujua kwanini Bahati aliamua kufanya vile. Baada ya uchumi wa kampuni hiyo kutengamaa na kupata uongozi uliokuwa ukipiga kazi kama ipasavyo, Jothan alirudi Dar kuendelea na majukumu yake ya kila siku. Alipofika nyumbani kwake palikuwa pamefungwa kama alivyo paacha. Aliingia ndani na kuikagua nyumba yake kwa macho kisha akaenda kulala kutokana na uchovu aliokuwa nao. Usiku wa jumamosi, aliamua kwenda club kwakua ni muda mwingi alikosa kwenda. Hivyo aliamua kwenda kupata mixing za ma dj wakubwa ambao wanajua kubadilisha nyimbo na kumfanya mtu aburudike na mpangilio wa nyimbo wanazoziweka kulingana na wakati. Wakati akiwa anaburudika na kinywaji chake huku akipata burudani nyingine akiwa kwenye kiti, mzuka alkampanda na kujikuta anaingia kati na kuucheza wimbo ulimvutia zaidi. Style alizocheza ziliwavutia wengi hadi baadhi ya wasichana walimfuata na kucheza nae. Aliifurahia sana hiyo siku na kurudi nyumbani akiwa na hamu ya kwenda tena siku ya jumapili. Kwakua alikua na likizo ya mwezi mzima kazini, hakuona tabu kulala mchana ili usiku akeshe tena kutokana na kuwa mziki ni starehe kubwa anayoipenda japokuwa siyo muimbaji. Siku hiyo alifika mapema na kutulia kwenye meza kwanza za nyuma na kuendelea kupata kinywaji na nyama choma kwa wingi. Wasichana wengi walimshobokea na kuomba ofa za bia. Kwakua Jothan alikuwa akiingia sehemu yoyote ya starehe huwa anakua amependeza mfukoni, basi hakuona shida kumwaga ofa mbali mbali kwa wanaomuomba bila kujali jinsia. Wakati disco likizidi kuchanganya. Kwa mbali kwenye mwanga hafifu Jothan alimuona msichana aliyemfananisha. Hakujiuliza mara mbili, alinyanyuka na kumfuata pale pale kwenye meza yao. Kadri alivyozidi kumsogelea, ndipo sura ya yule binti iliyozidi kumjia kichwani. Alimsogelea na kumuangalia kwa ukaribu zaidi. “kaka,tukusaidie nini?” aliuliza yule dada baada ya kumuona Jothan akiwa mbele ya meza yao amesimama na kumuangalia kupita kiasi. “sijui ndio wewe au nakufananisha?” aliongea Jothan huku akiwa haamini baada ya kumuona yule binti aliyekuwa kapendeza kupita kiasi. “kaka hizo swaga za kizamani kweli, za kuaza kufananishana mara sijui nilikuona wapi, achana na sisi bro” aliongea yule dada na kuwafanya wenzake kucheka. Kutokana na hadhi aliyokuwa nayo Jothan, alifedheheka kiasi na kumfanya akubali matokeo. Aliwaacha wale mabinti huku wakiwa wanamjadili na yeye kurudi kwenye siti yake. Ladha ya club ilipotea na kuamua kurudi nyumbani kwake. Alijitupa kitandani na kuwaza sana. Kwa jinsi alivyotekoa kufurahi kumuona tena yule msichana na majibu aliyopewa hata kabla hajajitambulisha yalimtia simanzi. “naweza kusema kuwa hawezi kunifahahamu, lakini hata sauti kashindwa kuitambua?… au kwa sababu sauti yangu ilikuwa ya kilevi?” Alijiuliza Jothan maswali mengi bila ya kuwa na majibu. Asubuhi ya siku ya pili alienda kupata supu maeneo ya karibu na kwao. Aliporudi alijitupa kitandani na usingizi ukamchukua mpaka saa kumi jioni. Njaa ilikuwa ina muuma sana. Aliamua kutoka na gari lake na kwenda kwenye Bar kubwa iliyokuwa msasani kwa ajili ya kupata chakula ambacho siku hiyo kilikuwa kinapikwa kwa ustadi mkubwa. Aliagiza oda yake na kuletewa baada ya muda kama wa dakika tano. Kabla hajaanza kula, kwa mbali aliisikia sauti ya yule mmsichana aliyekutana naye Club usiku wa jana yake. Alinyanyuka na kwenda kwenye ile meza ambayo alimkuta akiwa na rifiki yake mmoja wa kike. “samahani, wewe sio BAHATI!!!?” Aliuliza Jothan huku akiwa na uhakika asilimia zote kwakua alikua anafahamu fika kuwa yule ndiye mwenyewe kutokana na sauti yake na muanekano wake ingawaje kwa sasa alikuwa anavutia zaidi. “ndio mimi, umenijuaje?” aliuliza yule dada na Jothan aliachia tabasamu huku akitikisa kichwa chake. “ina maana Bahati hata sauti yangu huikumbuki?” aliuliza Jothan huku akiwa haamini kumuona Bahati akiwa na macho mazuri tena yaliyoongezewa uzuri na kope za bandia alizo bandika. “ningekuwa nakujua nisingekuuliza umenijuaje?” alijibu yule dada na kuendelea kuifyonza juice yake iliyosindikizwa na chpsi pamoja na nyama choma waliyokuwa wanakula yeye na rafiki yake. “nitakushangaa sana ukisema kuwa sauti ya Jothan hauikumbuki.” Aliongea Jothan na kubaki kumuangalia Bahati aliyepigilia mapigo ya ki sister duu. “WHO A JOTHAN BY THE WAY????” Aliuliza yule dada na kumfanya Jothan aondoke bila kuaga. Alienda counter na kulipia oda yake bila kuigusa na kuondoka zake. Hakuamini kuwa Bahati angewaza kuongea yale maneno mbele yake tena kwa nyodo wakati ni yeye ndie aliyemleta mjini na kumpa msaada wa kuyatibu macho yake baada ya yeye kuikubali hali ya ukipofu kutokana na kuwa kulikuwa na uhaba wa pesa nyumbani kwao. Jothan ilibaki kidogo tu agonge wakate anaendesha kutokana na mawazo yaliyochanganyikana na hasira kwa kile alichofanyiwa na Bahati.. Alijilaumu sana kwenda kula chakula pale na kuambulia maumivu. Alijuta kukutana tena na Bahati ingawaje mwanzoni alikuwa na hamu ya kuonana nae. Alifika nyumbani na kujilaza. ”who a Jonathan by the way??” Aliirudia ile kauli ya Bahati na kujikuta anashindwa kuamini kuwa yule ndie bahati halisi aliyemtamkia maneno yale. ITAENDELEA ... Read More
Story........ NI WEWE TU PENINA Sehemu ya kumi na mbili (12) By GIVAN IVAN Phone & whatsapp.... 0769673145 Ilipoishia.......... Penina na Frank walishangazwa Sana na maamuzi ya Nolan lakini hata hivyo Nolan hakutaka wamuulize swali lolote, alimwamuru dereva wa tax ile awashe gari na kuondoka. Kisha Nolan naye akaingia kwenye gari yake na kugeuza kuwafuata vijana wale wa the killer na wakati huo walikuwa tayari wameshaungana wote kwa maana ya kikosi kile cha kwanza kilichokuwa kikimtafuta Nolan na kile cha pili kilichokuwa kikimtafuta Frank. *********Endelea ********* Vikosi vile viwili ambavyo vilikuwa kwenye magari mawili viliweza kumuona Nolan akiwa anarudi kule alikotoka. Vikosi vile navyo haraka haraka vikageuza magari yao na kuanza kumfuata Nolan. Nolan aliweza kuwaona wakimfuatilia na ndio kitu ambacho Nolan alikitaka, lakini kilichomshangaza Nolan ni kwamba Sasa anafuatiliwa na magari mawili tofauti na mwanzo walipokuwa wakimfuatiliwa na gari moja. Lakini Nolan hakujali hilo, akaacha barabara na kukataa kushoto na kuingia kwenye njia moja ya vumbi ambayo haikuwa ikipita watu Mara kwa Mara. Nolan baada ya kuingia kwenye barabara ile akasimamisha gari na kushuka ndani ya gari lile. Na sekunde hiyo hiyo magari mawili ya vijana wale wa the killer wakawasili pale alipo Nolan na kusimamisha magari yao Kisha wote wakashuka kwenye magari yao ambao kwa pamoja walikuwa Nane. Vijana wale wa the killer walishaangaa baada ya kufika na kumkuta Nolan peke yake badala ya kuwakuta wote Nolan pamoja na Frank. Nolan alikuwa amesimama pembeni ya gari yake huku akiwatazama vijana wale waliokuwa wakimsogelea taratibu. "mwenzako yuko wapi?" kijana mmoja wa the killer akamuuliza Nolan huku akijaribu kumkamata Nolan kwenye shingo. Kijana yule alijikuta akipokea ngumi Nzito ya tumbo kutoka kwa Nolan ambayo ilimfanya adondoke chini kwa magoti. Wale vijana wengine walishtuka kuona mwenzao alivyotandikwa ngumi ya tumbo. Lakini hata hivyo bado vijana wale waliamini Nolan hawawezi kwasababu wako wengi na wote wana silaha. Vijana wale kwa pamoja wakaanza kumfuata Nolan, Nolan naye akapiga hatua kadhaa na kurudi nyuma na kuwasubiri. Vijana wale walipomkaribia Nolan kwa pamoja wakaanza kurusha ngumi na mateke kumvamia Nolan. Lakini Nolan alikuwa akiwakwepa tu bila kumgusa mtu yoyote, ndani ya dakika tano Nolan alikuwa akiwakwepa vijana wale waliokuwa wakimshambulia bila mafanikio. Lakini Nolan alizubaa kidogo na kujikuta akipokea ngumi Nzito ya uso kutoka kwa mmoja wa vijana wale. Lakini hata hivyo kijana yule aliyembahatisha Nolan ngumi ya uso ikawa ndio mwisho wake wa kuishi duniani, kwani Nolan alimkamata na kuanza kumshambulia kwa ngumi za haraka haraka na kummaliza kwa kumvunja shingo. Wale vijana wengine ndio walishtuka vibaya mno na kuona huyu mtu sio wa kawaida, wakaamua wamshambulie kwa silaha zao baada ya kuona hawatamuweza kwa mkono. Vijana wale walichomoa bunduki zao na kuziweka tayari kummaliza Nolan. Lakini Nolan alikuwa tayari ameshaingia kwenye gari na kuondoka kwa spidi kali na kuwaachia vumbi kali Vijana wale. Nolan aliamua kukimbia baada ya kuona vijana wale wakitoa bunduki zao, hivyo asingewaweza kwa sababu yeye hakuwa na silaha yoyote. Vijana wale nao hawakumuacha waliingia kwenye gari na kuanza kumfuatilia Nolan. Lakini mpaka pale Nolan alikuwa tayari ameshawapoteza vijana wale na yeye Sasa alikuwa ameshika njia ya kuelekea nyumbani. * Mzee Joel akiwa ameketi sebuleni kwake akisubiri majibu ya kuuwawa kwa Frank na Nolan simu yake ilianza kuita na alipoangalia mpigaji ni nani alikutana na Jina la Dickson, kijana ambaye mzee Joel ndio anataka amuoe mtoto wake Penina. Mara moja mzee Joel akaipokea simu ile. "mzee Joel habari yako?" akauliza Dick baada ya simu yake kupokelewa na mzee Joel. "salama kijana wangu habari ya huko"? Akajibu mzee Joel na kuuliza. " huku Safi tu, Sasa mimi nilikuwa nataka nije kumchukua Penina moja kwa moja nahitaji kuwa na familia Sasa. " akaongea Dick kumwambia mzee Joel. " kijana wangu usiwe na haraka tunaweka mambo Sawa na Muda wowote tutakuita uje umchukue mke wako. " akaongea mzee Joel kumpa moyo Dick. " unaweka mambo Sawa unaweka mpaka lini kama ni pesa nikekupa za kutosha mbona unanizungusha zungusha tu au nikuongezee pesa zingine? " akaongea Dick huku akionesha kuchoshwa na namna mzee Joel anavyomzungusha. "kijana wangu tafadhali naomba utulie Penina ni wako usiogope." mzee Joel akamwambia Dick. "nitulie nitulie mpaka lini nakuja Tanzania kujua Kwanini unanichelewesha kumuoa Penina na wakati nimeshakupa pesa nyingi Sana." akaongea Dick na kukataa simu. Mzee Joel alihisi kuchanganyikiwa hakujua afanye nini ili aweze kumuunganisha Penina na Dick. Na wakati huo huo mlango ulifunguliwa na akaingia Nolan huku akiwa amechafuka kwa vumbi. "Wewe mbwa mbona unaingia ndani kwangu bila hodi?" mzee Joel akamuuliza Nolan huku akiwa amevimba kwa hasira. "mzee tulia huu mchezo umeutaka mwenyewe lazima Frank amuoe Penina." akaongea Nolan maneno hayo ambayo yalizidi kumpandisha hasira mzee Joel na kujikuta akimrushia Nolan glass ya maji iliyokuwa kwenye Meza. Nolan aliigonga ngumi glass ile na kuipasua pasua. "ukiniletea upuuzi na wewe nitakupasua pasua kama hiyo glass." Nolan akamwambia baba yake mzee Joel na kuelekea chumbani kwake. * Frank na Penina baada ya kufika uwanja wa ndege walifuata taratibu zote na hatimaye wakafanikiwa kuingia ndani ya ndege na dakika chache baadae walikuwa angani wakielekea South Africa. "kama tukifanikiwa kufunga ndoa nitafurahi Sana yaani furaha nitakayokuwa nayo sidhani kama itaelezeka." aliongea Penina huku akiwa amejiegemeza kwenye kifua cha Frank. "usijali mpenzi kila kitu ambacho kinatokea kimepangwa na Mungu na vitakavyotokea mbele ni Mungu pia anajua, hakuna mwanadamu asiyependa furaha." akaongea Frank kwa upole kumuambia Penina. "ni kweli mpenzi wangu." akajibu Penina na safari ikaendelea kwa masaa kadhaa na hatimaye wakawasili South Africa Katika jiji la Johannesburg na kuchukua chumba Katika hoteli moja ya kifahari. Baada ya kupumzika kwa dakika kadhaa Penina na Frank waliwasiliana na Nolan na kumjulisha jinsi safari yao ilivyokuwa. Nolan aliwataka wakae kwa amani na wasiwe na hofu yoyote yeye anaweka mambo Sawa na yakiwa tayari bas atawajulisha. * Vijana wa the killer bado walikuwa wakimtafuta Nolan na Sasa waliwasili nyumbani kwa kina Nolan na kukutana na mzee Joel ambaye aliweza kuwaambia Nolan yupo ndani na akawaelekeza chumba chake wakammalizie huko. Vijana wale taratibu walianza kuelekea Katika chumba cha Nolan, lakini kwa bahati mbaya ama nzuri Nolan aliwaona. "mmeamua kunifuata mpaka nyumbani nyie mmeisha." akajisemea Nolan Kisha akatoka chumbani kwake akiwa kifua wazi na kukutana na vijana wale sebuleni. Kilikuwa kitendo cha kushtukiza vijana wale hawakutarajia kukutana na Nolan sehemu Ile. Kitambo waseme waweke silaha zao tayari Nolan alianza kuwashambulia, na baada ya dakika chache Nolan aliwaweka vijana wale wote chini kwa kuwavunja vunja sehemu za miili yao. Mzee Joel ndio hakuamini baada ya kuingia ndani na kukuta vijana wote wamelazwa chini alafu kidogo hivi akatokeza Nolan akiwa amepigilia suti nyeusi Kisha akamwambia baba yake ambaye ni mzee Joel, "naenda kwenye kikao cha harusi ya Penina na Frank na kama utahitaji kadi unijulishe nikuletee ya kwako." ....... Itaendelea. ... Read More
Story...... NI WEWE TU PENINA Sehemu ya kumi na tatu (13) Ilipoishia....... Mzee Joel ndio hakuamini baada ya kuingia ndani na kukuta vijana wote wamelazwa chini alafu kidogo hivi akatokeza Nolan akiwa amepigilia suti nyeusi Kisha akamwambia baba yake ambaye ni mzee Joel, "naenda kwenye kikao cha harusi ya Penina na Frank na kama utahitaji kadi unijulishe nikuletee ya kwako." ***********Endelea ********* Nolan baada ya kumuambia baba yake maneno hayo aliingia kwenye gari na kuondoka. Nolan alifikia sehemu ambayo ilikuwa maalumu kwa ajili ya kutengeneza kadi za harusi. Nolan alitengeneza kadi za harusi zisizopungua Mia moja hamsini kwa ajili ya harusi ya Penina na Frank. Kadi hizo hazikuwa za kuchangia harusi ya Frank na Penina bali kadi za mualiko. Nolan alijipanga kusimamia kila kitu Katika harusi ya Penina na Frank hivyo yeye alitengeneza kadi ambazo ni kama kiingilio cha kuhudhuria harusi hiyo bila kuchangia chochote. Nolan baada ya kukamilisha zoezi la kutengeneza kadi zile akaanza kutafuta ukumbi Mkubwa wenye hadhi ya kufanyia sherehe ya harusi ya Frank na Penina. Nolan alifanikiwa kuupata ukumbii ambao aliuhitaji na baada ya hapo Nolan akaanza kuzigawa kadi zile kwa watu mbali mbali ikiwemo na marafiki pia. Nolan moja kwa moja aliwasili nyumbani kwa kina Frank na kuwakuta Wazazi wake Frank ambao walimpokea kwa furaha Sana. "kikubwa kilichonileta hapa ni kuhusu harusi ya mtoto wenu Frank pamoja na mdogo wangu Penina, napenda kuwaafahamisha kuwa taratibu za harusi ya ndugu zetu hawa inaendelea vizuri na hapa nimewaletea kadi za mualiko." alianza kuongea Nolan baada ya kukaribishwa ndani na Wazazi wake Frank huku akiwakabidhi kadi zile Wazazi wake Frank. "Asante Sana kijana wetu na hongera Sana kwa hapa ulipofikia Mungu azidi kukusimamia zaidi na zaidi." wakaongea Wazazi wake Frank huku wakimshukuru Sana Nolan. "msijali Sana hii kazi ilikuwa lazima niifanye na lazima nitaitimiza, na kingine ninachotaka kukifanya kwa Sasa nataka niwahamishe hapa nyumbani kwenu niwapelekee sehemu mkakae hapo kwa siku kadhaa mpaka pale harusi ya mtoto wenu itakapokamilika, nafanya hivi kwa sababu ya usalama wenu kwasababu kuna vita kubwa inaendelea. " akaongea Nolan na kutoa maelezo hayo ambayo Wazazi wake Frank walikubaliana nayo bila wasi wasi wowote. Wazazi wake Frank pamoja na Mdogo wake Frank walijiandaa na kuondoka na Nolan ambaye aliwapeleka Katika hotel moja iliyopo nje kidogo ya jiji la dar es salam na kuwataka wakae hapo kwa wiki tatu kabla ya harusi ya Frank na Penina na gharama zote atazisimamia yeye Nolan. Nolan baada ya hapo alishika njia ya kurudi nyumbani kwa ajili ya kwenda kupumzika kidogo. * Dickson aliwasili Tanzania kwa Mara nyingine tena Ila awamu hii alikuwa na vijana wake wanne alioongozana nao. Baada ya kuwasili uwanja wa ndege moja kwa moja Dickson pamoja na vijana wake walichukua gari ndogo na kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwa mzee Joel.* Mzee Joel alizidi kuchanganyikiwa baada ya kumaliza siku ya pili Sasa bila kumuona Penina na wala hajui ni wapi Penina alipo. Jambo hilo lilimvuruga Sana mzee Joel na kumfanya ashindwe hata kula chakula anachopikiwa na mkewe. Mzee Joel pia aliweza kuwasiliana na mkuu wa kikosi cha the killer na kumueleza jinsi vijana wake walivyoshindwa kuifanya kazi waliyoagizwa na kujikuta wakipokea kichapo kikali kutoka kwa Nolan. Mkuu yule wa kikosi cha the killer aliyejulikana kwa Jina la buffalo alipigwa na butwaa baada ya kupewa taarifa zile na mzee Joel. buffalo hajawahi kuamini kama kuna mtu yoyote anayeweza kupambana na vijana wake na akawaweza, hivyo taarifa zile zilimshangaza Sana. Buffalo akaamua ni lazima amjue huyo kijana ni nani aliyeweza kuwatandika vijana wake. "mzee hiyo kazi niachie mimi nitapambana nae mwanzo mwisho." akaongea buffalo kumwambia mzee Joel. Mzee Joel aliweza kumuelewa buffalo na kukataa simu na kumsubiri buffalo aingie kazini mwenyewe kwasababu yeye ndio mtu pekee Sasa aliyebaki wa kumtegemea. Dakika chache baada ya mzee Joel kuongea na buffalo, mzee Joel alipata taarifa kuwa kuna wageni nje wanahitaji kuonana na yeye. Mzee Joel alitoa ruhusa wageni hao wakaribishwe ndani. Kitendo bila kuchelewa wageni wale walifunguliwa geti na kukaribishwa mpaka ndani. Mzee Joel alishtuka baada ya kuona ugeni wenyewe ni wa Dickson pamoja na vijana wake wanne. "karibuni karibuni Sana." akaongea mzee Joel huku akijaribu kujichekesha japo hakuwa na amani hata kidogo. "hatuna haja ya kukaa mzee Joel, tumekuja kumchukua Penina nataka kujua kama inawezekana au haiwezekani?" akauliza Dick huku akionesha dhahiri kupandwa na hasira. "inawezekana kijana wangu tafadhali kaeni kidogo bas." akaongea mzee Joel kwa upole. "nimeshakuambia hatuna haja ya kukaa sisi tumekuja kumchukia Penina tu." akaongea Dick kwa msisitizo. "kijana wangu Dick naomba nipe muda wa siku mbili tu nitakuwa tayari nimeshakamilisha hili swala." akaongea mzee Joel kuwaambia wakina Dick. "Mzee umenipotezea Muda na umekula pesa zangu nyingi Sana, Sasa naondoka na kesho nitarudi unikabidhi Penina la sivyo pesa zangu utarudisha na utalipa Muda wangu nilioupoteza kwa ajili yako." akaongea Dick kwa jazba na kuondoka pamoja na vijana wake na kumuacha mzee Joel akitokwa na jasho jembamba. Baada ya dakika chache wakina Dick kuondoka Nolan naye aliwasili nyumbani na kumkuta baba yake akiwa na mawazo tele huku pembeni akiwa chupa ya pombe kali. "Baba shikamoo" akasilimia Nolan lakini alijua baba yake hataitikia salamu yake. Mzee Joel kweli hakuitikia salamu ya Nolan alibaki akimtizama tu kwa hasira. Nolan naye hakujali alitoa kadi tano za harusi ya Penina na Frank na kumwekea baba yake kwenye Meza iliyokuwa mbele yake. "karibu Sana Katika harusi ya Penina na mpenzi wake wa Muda mrefu Frank, wewe pamoja na rafiki Zako mnakaribishwa. " Nolan ndio alimwambia baba yake mzee Joel baada ya kumuwekea kadi zile kwenye Meza iliyokuwa mbele yake, Kisha akaondoka na kuelekea chumbani kwake. ............ Itaendelea ... Read More
HOUSE GIRL DIARY; NAITWA RAYA NI HOUSE GIRL MSTAAFU—SEHEMU YA TATU (ILIPOISHIA SEHEMU YA PILI; Raya anarekodi Video ikimuonyesha yule Mama akimtesa mtoto wake wa kambo, akimpiga na kumfanyisha kazi. Anamkabidhi Baba Jack ili aone kinachoendelea. Je nini kitatokea ENDELEA.. Kama hujasoma sehemu ya pipi basi bonyeza hapa; Iddi Makengo Dada alimuona namna Baba anavyobadilika, namna ambavyo uso wake alikua anaukunja, ghafla nilimuona Baba machozi yanamtoka, nikitegemea kama atapandwa na hasira kama nillivyokua mimi na kuanza kumtandika Dada makofi niliona anamgeukia taratibu, alimuangalia kwa uchungu kama vile alikua anataka kusema kitu lakini maneno hayatoki. “Ni…ni nini hiki?” Alijitahidi kuuliza, wakati huo Dada alikua kimya akiangalia chini kwa aibu. “Nisamehe mume wangu ni hasira tu, huyu mtoto wakati mwingine ananiudhi nalazimika kumpiga…” Alijitetea. Mimi bado nilikua nashangaa ni kwanini Dada hakua amelala chini akitokwa damu kwa kipigo. “Hasira ndiyo unwe unampiga mtoto namna hii, hizi ni hasira gani?” Hapa Baba aliuliza kwa hasira kidogo, nilipata faraja labda atamtandika makofi lakini haikutokea. Dada alianza kulia, “Hata mimi sijui mume wangu, sijui hata nini kilinitokea siku hiyo nikampiga mtoto, mimi sina mkono wakupiga kabisa, wewe mwenyewe unanijua labda ni hii mimba…nikiwa katika hali hii nakua tofauti sana…” “Muongo, ni kila siku anampiga, hata haya anayoita mapele ni yeye. Hata chakula anamnyima, anamtukana, anamfanyisha makazi kama Mbwa, huyu si mwanamke ni shetani!” Niliongea huku nikinyanyuka kwa hasira, Baba alikua kama zezeta flani hivi, baada ya kutajiwa neno mimba ni kama alisahau kuwa yule mwanamke alikua ni shetani. Nilikua nasikia mambo ya limbwata lakini nilikua sijawahi kuona mtu kalogwa akalogeka. Kwa namna ile video ilivyokua mtu yeyote mwanye akili timamu hata kama asingekua mzazi wa Jack angekasirika na asingemsikiliza yule mwanamke. “Una mimba mke wangu, ina miezi mi ngapi? Mbona hukuniambia?” Alisahau kabisa kuhusu Jack na kuanza kuulizia upuuzi mwingine ambao nilijua kabisa ni uongo. “Hakluna cha mimba wala nini, hivi wewe huoni kama anataka kukuchota akili!” Niliongea kwa hasira, pale nilikua kama mfanyakazi ila kwa wakati ule nilijua kazi sina hivyo ilikua ni lazima kumtetea Jack na kuhakikisha haki inatendeka. Nilipiga kelele na harakaharaka nilitaja karibu kila kitu ambacho mimi nilikishuhudia Dada akimfanyia Jack. “Mume wangu unaona, huyu binti ndiyo sababu ya kila kitu. Hataki kufanya kazi, nyumba ikakua chafu na kamjaza mwanao kiburi, mbona kabla ya kuja tulikua tunaishi salama. Jack namfundisha kazi na ananisaidia kufanya kazi za ndani, kwa hali yangu hii siwezi kufanya chochote, wewe mwenyewe unakumbuka kilichotokea kipindi kile. Unajua namna tulivyohangaikia huyu mtoto, hivi kweli kumfundisha mtoto wa kike kazi za nyumbani ni kosa? Au kumchapa akikosea ni kosa? Au kwakua mimi sina kazi nipo hapa nyumbani, au kwakua mimi ni Mama wa kambo ndiyo mnaniona kama shetani. Huyu binti anajazwa maneno na Mama yake, kila siku wanaongea na ndiyo wanataka kutuvuruga. Mimi siwezi, mimi siwezi kama umenichoka niambie tu niondoke zangu!” Aliongea huku akilia, kila kitu kilikua ni uigizaji, wakati anaongea alianza kunyanyuka, alinyanyuka huku akishika tumbo kama vile ana maumivu tumboni. “Nini? Kuna nini kimetokea, tumbo linauma?” Baba alimuuliza lakini hakujibu zaidi ya kumuambia niache kama umeamua kumsikiliza huyo baki naye mimi naondoka. Alinyanyuka kwa kupepesuka kisha taratibu alidondoka chini. Niliona kabisa kafanya makusudi kwani hakudondokea sakafuni, alipiga jicho pembeni kisha akapepesa macho na kudondokea kwenye sofa, akawa kama kakaa kiupende kisha ndiyo akafika chini. Baba alipaniki, alianza kuhaha, simu alitupa pembeni na kuacha kuangalia, watoto wake nao walikuja kulia na kumlilia Mama yao. Ilikua ni kama maigizo flani, Baba alianza kuongea habari za Hospitali ndipo alijifanya kufungua macho na kulazimisha kupelekwa chumbani. Aliniambia nimsaidie kumnyanyua lakini sikua tayari, nilimshika Jack mkono na kuondoka naye mapaka chumbani, nilimuacha Baba akihangaika kumnyanyua ili kumpeleka chumbani, alisahau kabisa ishu ya mwanae. **** Usiku mzima sikulala, nilijua nafukuzwa lakini suala la kumuacha Jack pale halikuingia akilini. Nilimuambia Jack nimpeleke kwa Bibi yake lakini alikataa katakata. “Watakuja tu kunichukua, hata nikisema nini hakuna mtu wa kunisikiliza. Wewe dada ondoka tu uniache hapa, nimeshazoea kila dada anayekuja anachoka na kuondoka mimi naendelea tu kubaki. Baba hawezi kuruhusu niondoke, alishagombana na Bibi mara nyingi lakini anasema ananipenda na hawezi kukaa mbali na mimi. Kumbe sikua mimi peke yangu niliyeona yale mateso na kukerwa nayo, kulikua na wafanyakazi wengine wawili nyuma ambao walishafukuzwa kwaajili ya Jack ndiyo maana alikata tamaa. Mmoja alisema kwa Bibi yake Jack na mwingine alimpa chakula na alikua anawasiliana na Mama yake Jack. Asubuhi Baba aliamka kama kawaida, ni kama kulikua hakuna kitu kilichotokea, Dada alijifanya kuamka na kumuamsha Jack kwaajili ya shule, alijidai kumuandaa na kujifanya hana kinyongo. Waliwaaandaa na kuwapeleka shule, alipoondoka tu Dada aliniambia nikusanye kila kilicho changu na kuondoka. Alinitukana sana kwa kutaka kuingilia nyumba yake akiniambia kuwa pale hawezi kuondoka. Alitaka kunipiga lakini kwakua sikuwa nikihitaji kazi tena na nilishajua siwezi kubaki tena pale kumlinda Jack niliamua kumtolea hasira. Baba alishaondoka kwenda kazini hivyo tulibaki wawili tu, pamoja na mwili wangu mdogo lakini nilipitia mengi, maisha ya kupigana mtaani nilishayazoea. Nilimsubiri aliponipiga kofi la kwanza na la pili. Nilimuacha anogewe ndiyo nikaanza kumtandika, hakuamini. Nilimtandika kama vile mtoto mdogo, nilimpiga sana akapiga kelele lakini hakukua na mtu wa kumsikia. Baada ya hapo nilichukua kilicho changu na kuondoka. Nilimuambia naondoka lakini nitarudi, nitarudi kwaajili ya Jack. Alinyamaza kimya bila kusema chochote. Kumbe mtu mwenyewe alikua mayai mayai halafu anajifanya kuonea watu. Niliondoka na kwenda kwa kijana mmoja, huyo alikua ni X wangu, tulizinguana kitambo kabla sijaacha kazi nilipokua nikifanya mwanzoni, yeye alikua ni Kondakta wa daladala hivyo mchana alikua kazini. Mlango wake nilikua naujua vizuri hivyo niliufungua hata bila funguo. Sikua na pakwenda kwani sikua na ndugu Dar, ingawa sikuachana naye vizuri lakini nisingelala mtaani. Jioni alirudi na kunikuta, hata hakukasirika, alianza kucheka na kunitania kama siwezi kuishi bila yeye. Nilimuambia ishu yangu, nikamuonyesha ile video katika simu yangu, hata yeye pamoja na Bangi zake hakuamini kama kuna mtu anaweza kufanya vile tena kwa mtoto mdogo kama yule. “Huyo mwanaume kashatengenezwa, cha kufanya hapo ni kwenda Polisi, mbona siku mbili huyo akikaa ndani anakaa sawa…” Aliongea huku akinigusa, najua alitaka mapenzi lakini sikua katika mood kabisa, ila aliongea jambo amaalo sikuliwaza kabisa hapo awali. “Baba yake anaweza asijali lakini sidhani kama Polisi hawatajali.” Niliwaza kufanya hivyo lakini ulikua ni usiku, niliamua kusubiri mpaka asubuhi. Lakini niliwaza kama itakua vizuri nikienda na Jack kwani nilijua kuwa wakiangalia makovu yake basi utakua ni ushahidi tosha na watamuonea huruma. Lakini ningempataje wakati yuko shuleni, niliamua kwenda nyumbani kwao kumsubiri wakati anatoka shule. Wakati wanashushwa na gari kabla ya kuingia ndani nimchukue na kuondoka naye. Mchana muda wa wao kutoka shule nilichukua Bajaji, nilimuambia Dereva kupaki karibu na geti kabisa, Gari la shule lilipokuja na kuwashusha nilishuka na mimi. Wote waliniona, wale wengine walikimbilia ndani lakini Jack ambaye alikua anaogopa alisimama na kuniambia niondoke kwani atapigwa. Sikumsikiliza wala sikusubiri kumuelezea. Nilimshika na kumvuruta mpaka kwenye Bajaji, nikamuingiza kwa lazima kisha nikamuambia Dereva tuondoke. Kwakua nilishamuambia kila kitu aliwahsa Bajaji mpaka kituoni. Kule nilienda mpaka mapokezi, hakukua na watu wengi, nilianza kuelezea kila kitu, nikawaonyesha na Video. Kila askari aliyeiona alikasirika, tulipewa askari wa kike ambaye alienda kumkagua Jack. Alikua ni Mama mtu mzima, wakati anamkagua alianza kutokwa na machozi ingawa alijizuia sana. Mwanzoni Jack alikataa kusema lakini baada ya kuhakikishiwa usalama wake lielezea kila kitu. Niliandikisha maelezo kisha tukapewa PF3 ili akatibiwe, askari mmoja alitupeleka hospitalini na gari yake binafsi. Baada ya hapo ilitolewa RB, Dada na Baba wote walikamatwa na kufikishwa kituoni. Wote walikua na kesi, haikua ni ya mtu mmoja tena. Polisi waliwasiliana na ndugu wengine kwaajili ya kumchukua Jack na kukaa na wale watoto wengine kwani wote hawakupewa dhamana. Mimi niliondoka lakini nilikua naenda Hospitalini kumuangalia Jack mara kwa mara. Alilazwa kupatiwa matibabu kwa muda wa wiki moja hivi, Mama yake alikuja na baadaye kukabidhiwa mtoto wake. Baba na Dada walikaa mahabusu kwa wiki moja na kutoka kwa dhamana lakini cha kushangaza hawakupelekwa mahakamani. Sijui nini kilitokea lakini binafsi naamini walitoa pesa nyingi kwani Baba Jack alikua na pesa na kacheo flani. Kesi iliisha chinichini na mimi sikuweza kufuatilia, baada tu ya Jack kurudi na kukabidhiwa kwa Mama yake kwangu hilo lilitosha hayo mengine yalikua hayanihusu. Hela yenyewe ya kula ilikua ni shida nisingeweza kufuatilia maisha ya wengine. Sasa hivi imepita kama miaka miwili hivi tangu hili tukio litokee, nipo hapahapa Dar lakini nimehama mtaa. Sifanyi tena kazi za ndani, nimefungua Genge langu ambalo nauza mbogamboga na matunda. Bado nawasiliana na Jack kupitia Mama yake na anaendelea vizuri, wanaishi maisha ya kawaida sana lakini yenye furaha. Katika kazi yangu hii ya kuuza Genge wateja wangu wengi ni wadada wakazi ‘House Girl’ mengi wanayokutana nayo katika nyumba za watu ni kubwa. Kwa wa mama ambao ndiyo mabosi wetu kumbukeni hata sisi ni wanadamu kama nyinyi. ***MWISHO MAMA KWANI BABA YETU NDIYO HUYU HUYU AU SISI NI MAYATIMA? Baba yao ndiyo alikua na kila kitu, mali zote zilikua za kwao lakini kila akisafiri walikua wakiishi kama mashetani, Shangazi zao na Baba zao wadogo waliungana kuwachukia, Mama yao alikua akinyanyaswa na kutukanwa. Kila siku walimuambia yeye ni mzigo na hawezi kuchukua mali za Kaka yao. Bibi yao ambaye alitegemewa kuwa upande wao naye walimjaza maneno. Walimuambia huyu mwanamke kama Kaka akimuacha watagawana mali na Kaka akifa basi atachukua mali zote. Kilichopo hapa ni kuhakikisha Kaka hawi na kitu chochote cha yeye kuchukua…. JE UNATAKA KUJUA KISA HIKI KINAHUSU NINI…Kama kisa kilichopita kilikutoa machozi hiki kitakupigisha mayowe… Lakini nacho kimetokea niseme kinaendelea kutokea, unaweza kuwa na mali nyingi na wanao wakaishi kama mashetani hata kabla hujafa. Kama unataka kuwa wa kwanza kukisoma basi hakikisha umelike ukurasa ... Read More
*LOVE BITE EP 05* 🌹🌹🌹🌹🌹💞💞💞🌹🌹🌹 MWISHOOOOOOO “OOOOH MY GOD……..WHY ME?????” Alijikuta nguvu zinamuishia Jothan na kukaa chini. Aliiangalia nyumba yake aliyoijenga kwa gharama kubwa na machozi yalianza kummiminika kama maji. ITAENDELEA………… Alsimama na kuamua kwenda kwa rafiki yake John ambaye alikua anakaa magomeni. Alikaribishwa ndani na mke wa rafiki yake huyo na kukutana na rafiki yake sebuleni kwake. Walikumbatiana kwa kuwa siku nyingi walikuwa hawajaonana. Kwakua muda wa msosi ulikua unakaribia, mke wa John alipakua chakula na baada ya dakika kumi waliitwa kwenye meza ya chakula. Walikula huku kila mmoja akijaribu kumuhadithia mwenzake yaliyotokea nyuma kwa kipindi chote hicho cha takribani miezi nane. Jothan ndiye alikuwa wakwanza kumuhadithia mwenzake yaliyomkuta kuanzia safari yake ya Arusha hadi kufikia pale alipoenda kwenye nyumba yake na kukuta imeuzwa na mwanamke aliyekuwa anampenda na kumuamini kupita maelezo. John alisikitika sana kuisikia story ile iliyomuumiza hata yeye. “usijali rafiki yangu,. Kuhusu pa kukaa tu. Hapa umefika maana kuna vyumba vingi vya kutosha. Sasa vipi kuhusu docomments zako muhimu kama vyeti na vitambulisho vyako?” aliuliza John kwa kugundua umuhimu wa hivyo vitu. “ndio maana nikakwambia kuwa nimechanganyikiwa sana. Yaani sijui nianzie wapi?” aliongea Jothan huku akionyesha wazi kuwa akili yake imeeshia pale kimawazo. “usijali, vitapatikana tu.” Aliongea John na kuonyesha wazi nia yake thabiti ya kumsaidia rafiki yake huyo. “vipi kazini, wameshamuajiri mtu mwengine wa kukaa katika nafasi yangu?” aliuliza Jothan huku akionyesha wazi kuwa na wasi wasi na nafasi yake ya kazi. “mbona company imeuzwa kwa mzungu ambaye kaamua kuibomoa na kujenga hotel. We ukienda utaona tu mabati yamezunguka katika jengo la ofisi yetu. Sasa angalau ungekuwa na docoments zako zingekusaidia kupata malipo na mafao yako kutoka NSSF.” Aliongea John na kumfanya Jothan ashike kichwa kwakua alikua anaamini kuwa maisha yake yanaweza kunyanyuka tena kama akivipata vitu vyake muhimu. Kadi za benk, nyaraka mbali mbali na vyeti vyake alivyovihangaikia kuvipata ndivyo vilimnyima raha Jothan. “mimi hivi sasa nimeajiriwa na kampuni ya Fast jet. Hata wewe ungekuwa na vyeti vyako tungekuwa tunafanya kazi wote . Maana watu wenye sifa kama zako wanahitajika sana pale.” Aliongea John na kumfanya Jothan ajiinamie. Walikaa pamoja na baadae Jothan alielekezwa chumba atakachukuwa analala. Usiku baada ya kula chakula, alienda chumbani kwake Jothan na kulala. Asubuhi ilipofika, John alimgongea Jothan na kumuaga. Alitoka na kwenda zake kazini. Aliandaliwa chai Jothan na shemeji yake baada ya kuamka asubuhi na kutoka sebuleni. Alikunywa chai na kwenda chumbani kwake. Alioga na kubadilisha nguo. “shemeji.. natoka kidogo.” Aliaga Jothan na kuondoka. Alienda kinondoni ili kuangalia kuwa kama watu walionunua ile nyumba yake wameshahamia. Alikuta hali ile ile ya kama alivyoiacha. Alijitahidi kumuulizia Shani kwa majirani wa pale, lakini hakuna hata mmoja aliyempa majibu chanya juu ya kumpata Shani. Roho ilimuuma kila akiitazama nyumba yake. Alilia sana na kuamua kukubali yote kuwa hata kama atalia na kumaliza machozi yake, basi hawezi kuirudisha nyumba yake. Alirudi nyumbani kwa rafiki yake aliye muhifadhi na kwenda chumbani kwake. Alikaa huko na baaae aliitwa na shemeji yake wakati wa chakula cha mchana. Walikula pamoja na rafiki yake aliwasili pale baada ya nusu saa. “leo nimechelewa kurudi kwa sababu nilikuwa nashughulikia swala lako kwa kuvitangaza vyeti vyako kwenye magazeti mbali mbali yatokayo kesho.” Aliongea John na kumfanya Jothan afurahi kusikia hivyo. Alikaa pale kwa wiki mbili zilizokwenda kwa amani. bada ya hapo, alianza kupata mitihani midogo midogo kutoka kwa Shemeji yake huyo aliyekuwa anapenda kumuonyesha tabasamu kila wakati. Kadri siku zilivyozidi kusonga mbele, ndivyo majaribu kutoka kwa shemeji yake yalivyopamba moto hadi kufikia kuingia chumbani kwake akiwa na upande mmoja wa khanga nyepesi iliyoonyesha kila kitu alichokivaa ndani. Alimuonya mara kadhaa lakini bado msichana huyo aliyekumbwa na pepo wa ngono juu yake alizidi kumuandama. Kamwe hakupenda kuwa sehemu ya tatizo . Alipenda kuwa mtatuzi wa tatizo. Baada ya kuona visa vinazidi kutoka kwa mke wa rafiki yake. Aliamua kuihama nyumba bila kumuambia rafiki yake sababu iliyomuhamisha pale nyumbani kwake kwa kuhufia kuharibu ndoa ya watu waliodumu kwa takribani miaka kumi. Japokuwa hakua na pa kwenda, ila aliamini kuwa kufanya vile basi Mungu atamnyooshea njia yake.. Fedha kidogo alizokuwa nazo zilimuwezesha kujihudumia mwenyewe na kulala gesti kwa wiki moja tu. Baada ya hapo alikuwa choka mbaya. Hakuwa na hata senti tano. Siku hiyo aliamua kuuwa winga kwa kushinda na njaa hadi kiza kilipoingia. Hakuwa na mahali pa kulala, aliamua kwenda kukaa stendi ya daladala maeneo ya kinondoni huku akimuomba mungu usiku ule ukuche akiwa salama maeneo yale. Masaa yalisogea na usiku mnene ulianza kutokea baada ya idadi ya magari kupungua huku watu waishio maeneo hayo kutoonekana nje. Hata yeye mwenyewe hakujua alipataje usingizi. Ila alishtuka baada ya kuona mwanga mkali wa taa za gari ukimulika maeneo aliyokuwa yeye. Alishtuka na kuyazuia macho yake kwa mikono kutokana na ukali wa mwanga wa taa zile. Sekunde kadhaa baadae, zile taa zilizimwa , mara akaona mlango unafunguliwa wa ile gari aina ya Range na kiatu aina ya high hills kikionekana kikikanyaga ardhi. Hali hiyo ilimonyesha kuwa mtu ashukaye kwenye ile gari ni msichana. Uteke wa mguu ule pia ulimuwezesha Jothan kupima age ya mtu anayeshuka. Wakati anausumbua ubongo wake kufikiria na kuwaza lengo la yule mtu kupaki gari lenye thamani pale, yule mtu alishuka na kufunga mlango. Kutokana na mawenge ya taa, hakuweza kumuona mtu aliyekuwa akizihisabu hatua kuelekea pale alipo. Yule dada alimsogelea mpaka pale. Hakuamini alichokiona mbele yake, alikuwa msichana wa ndoto zake toka alipokuwa anasoma. Hakujua ni kitu gani kilichomsukuma mpaka kufika maeneo yale. Ila aliamini kuwa ni Mungu pekee ndio amekisikia kilo chake na kuamua kuwakutanisha tena pale. “PRISCA???”” Alinyaanyuka Jothan na kuita kwa mshangao mkuu huku akiwa haamini macho yake kuwa yule ndiye Prisca wake wa zamani. Bila kujibu chochote, yule dada alianguka kifuani mwa Jothan huku machozi yanamtoka. Hakuamini Jothan macho yake. Alimuangalia Prisca ambaye alikua anafuta machozi yake. “tuondoke eneo hili, sio salama Jothan.” Aliongea Prisca na kumchukua Jothan na kwenda naye kwenye gari. Safari ilianza huku kila mtu akiwa amenyamaza bila kuongea chochote. Jothan alishangaa kuona gari linaelekea mtaa aliokuwa anakaa yeye zamani kabla ya nyumba yake kuuzwa. Gari lilipiga honi kwenye geti la nyumba yake Jothan. Mlinzi alifungua mlango na Jothan hakuamini kuwa mmiliki wanyumba yake ni Prisca. “siamini Prisca kama ni wewe ndio umeinunua nyumba hii?” aliongea Jothan baada ya kuingia kwenye nyumba ile ambayo haikubadilishwa kitu chochote zaidi ya rangi tu. “siku zote huwa napenda kukuona ukiwa mwenye furaha. Ndio maana niliposikia nyumba hii inauzwa ndipo niliamua kuinunua kwa sababu sikupenda ipotee kwenye upeo wa macho yako. Sio nyumba tu, na kila kilichukuwa ndani pia nimevinunua. Hata gari lako pia ukilihitaji nitakupatia kwa sababu kwa sasa halipo hapa. Nimevinunua vitu vyote hivi kwa ajili yako Jothan.” Aliongea Prisca huku machozi yanamtoka. Jothan naye hakuweza kuyazuia machozi yake na kumfuata Prisca na kumkumbatia. “moyo wa mtu ni kichaka Prisca, sikuweza kufikiria kama ipo siku Shani angeweza kuyabadili maisha yangu na kunifanya niwe hivi… nashukuru sana kwa yote uliyoyafanya kwa ajili yangu Prisca.” Aliongea Jothan maneno yale na kumfanya Prisca azidi kulia. “kesho nitachukua begi langu na kuondoka. Maana kazi yangu ya kukutafuta wewe nimeshaimaliza Jothan.” Aliongea Prisca na kumuangalia Jothan ambaye wote walikuwa wanalia wakati huo. “hapana, hutakiwi kuondoka Prisca. Na kama utaondoka basi hii numba na kila kitu kilichomo humu ndani bado vitakuwa havitoshi kutimiza furaha yangu bila ya wewe kuwa karibu yangu.” Aliongea Jothan huku analia. “mimi sio chaguo lako Jothan, siwezi kukaa karibu na wewe. Nitakuwa naumia roho tu na sitaweza kuvumilia kukuona ukiwa na msichana mwengine mbele yangu.” Aliongea Prisca huku analia kwa uchungu. “nilikosea kuchagua kwakua sikujua upi ni mchele ni zipi ni pumba. Niliacha mchele kwakua pumba zilinivutia angi yake. Leo najuta kwakua pumba zimenilaza njaa. Wewe ndio mchele wa kunifanya nishibe na kunitoa njaa hii ya kufa inayonikabili. Nakupenda sana Prisca.” Aliongea Jothan na kujikuta ameeanguka kwa magoti mbele ya Prisca ambaye wakati huo na yeye alikuwa haoni vizuri kutokana na ukungu wa machozi ulikuwa kwenye macho yake. “toka siku uliyonikana Jothan kule Peacock hotel kuwa mimi sio chaguo lako. Moyo wangu uliingia ganzi na kuamua kuishi single Jothan. Sihitaji tena kupenda kwakua nina bahati mbaya ya kupenda nisipopendwa. Sipendi kuumizwa tena kwakua maumivu yake siwezi kuyastahimili. Nikuache tu na maisha yako na mimi naiche na maisha yangu” aliongea Prisca kwa uchungu maneno yalimchoma sana Jothan ambaye bado alikuwa analowanisha viatu vya Prisca kwa machozi yake pale chini. “nisamehe mimi, nimeshajifunza Prisca,” aliendelea kuomba Jothan huku sauti iliyojaa uchungu ikiendelea kumtoka mtoto wa kiume. Nguvu ya mapenzi inaweza kuhamisha milima, wahenga walisema hayo na mimi nawaunga mkono kwa kusadiki maneno hayo. Prisca alijikuta anamnyanyua Jothan na kumkumbatia. Wote walilia sana na kila mmoja kwa muda wake alimbembeleza mwenzake kwa mumfariji. Ukurasa mpya wa mapenzi kwa wapendanao hao walioanza mapenzi toka walipokuwa shuleni yalianza kwa kasi kubwa. Hakukua na sababu ya kuchunguzana wala kupeana muda. Walikubaliana kupima ukimwi kabla ya kufanya mapenzi. Zoezi hilo lilifanikiwa kwa asilimia mia moja. Wote walikuwa wazima na mipango ya ndoa ilifanyika haraka. Vitu vyote vilivyokuwa kabatini alivikuta vile vile. Kasoro hati ya nyumba tu ambayo alirudishiwa na mpenzi wake Prisca. Alifurahi sana na kwenda kupeleka cv zake kwenye kampuni ya Fast jet. Alipata kazi haraka na kuungana na rafiki yake kipenzi John. Ndoa ya aina yake ilifungwa kati ya Jothan na Prisca. Wageni wengi kutoka sehemu mbalimbali walihudhuria harusi ile. Kwenye Hight table walikwepo John na mkewe, Bahati na mumewe Saimon pamoja na mama yake. Hakika furaha ambayo ilipotea kwa muda mrefu kwa Jothan ilirudi alifurahia uwepo wa watu hao muhimu katika maisha yake kwa vipindi tofauti.. Miezi saba baadae, Jothan na mkewe Prisca walikuwa wanatoka kwenye matembezi yao usiku wa saa sita. Wailpofika msasani. Walilakuta wasichana wengi walikuwa wamejiremba na kuvaa nusu uchi wakiashiria kuwa walikuwa wanauza miili yao. Jothan hakuamini kumuona Shani akiwa amejiingiza kwenye kundi hilo. Alisikitika sana kumuona Shani akikimbilia magari na kuanza kujinadi kama wafanyavyo mada wengine wanaojiuza hapo. Alisimamisha gari lake na kumuangalia mkewe ambaye alimpa ishara ya kuondoka na kumuacha mwanamke huyo na maisha yake. Walirudi nyumbani na kumshukuru Mungu kwa kuwaunganisha tena na kuyahesabu yote yaliyotokea nyuma ni mitihani tu, na wao ndio couple iliyokubaliwa na Mungu. ***********MWISHO************** Maisha ni sahani iliyojaa mazuri na mabaya. Kuna wakati unaweza kukubali kuwa maisha ni jinsi unavyoishi. Ila wapo wanaoishi nje ya malengo waliojiwekea. Hakuna anayependa kupata hasara, ila kama una muamini Mungu basi utaamini kuwa kupata hasara katika jambo Fulani ni moja ya mitihani na huenda mungu amekuEpushia kitu Fulani katika jambo hilo. Kila hatua unayopitia ni moja ya changamoto katika mafanikio yako. Ukianguka jikaze na jaribu kuruka tena hata kama utasikia maumivu. Tochi ya mungu hummulkika kila mtu isipokuwa kwa atakayekataa mwenyewe. Ridhiki ya mtu ipo kwenye mikono yake mwenyewe ndio maana huwezi kuizuia. Mungu ametoa vitu vitatu vikubwa kuliko Mali. Kwanza Mungu katoa akili za kipekee. Nikisema akili za kipekee namaanisha kuwa kila mtu Mungu kampa akili lakini hawa wenye akili za kipekee huweza kufanya mambo makubwa na ya kushangaza hali ambayo mtu uliyepewa akili ya kawaida huwezi kufanya hata kama una pesa. Pili Mungu katoa vipaji. Mtu mwenye kipaji Fulani basi huweza kufanya mambo makubwa ikiwemo kufikisha ujumbe haraka kwa watu kutokana na kukubalika na watu wengi zaidi ya mtu wa kawaida. Kimfano matangazo, tangazo hilo akipewa mtu Fulani atangaze basi muitikio utakuwa mdogo kuliko akipewa tangazo hilo Diamond, Mrisho Mpoto na wengne wengi. Kipaji ni kitu cha pekee alichotoa mungu kama zawadi kwa mtu Fulani na kama kitathaminika na yeye kukiwekea mkazo basi hiyo ndio inaweza kuwa njia ya mafanikio yake kupitia kipaji hicho. Tatu mungu katoa Moyo wa pekee. Moyo huu amewapa watu wachache. Na cha ajabu kuwa mtu mwenye moyo wa kutoa basi hutoa kitu kikubwa bila kujali kubakiwa na kidogo. Humshinda mwenye mali ambaye akitoa hata kitu kidogo huhisi anapungukiwa. Mtu mwenye moyo wa pekee hupenda kutenda mambo yanayompendeza mwenzake hata kama yanaweza kuharibu furaha yake. Hapendi kumuona mtu akilia au akihuzunika wakati yeye anaweza kumfanya mtu huyo kuwa na furaha hata kwa kumuongopea. Hawezi kula yeye kabla ya kuangalia wenzake wenye njaa. Hayo na mengine mengi kajaaliwa mtu mwenye moyo wa pekee. Na huwashinda wenye vipaji na akili za pekee. Watu hawa mungu huwajaalia kwa kuendelea kuwapa na kutia Baraka mali zao hata kama ni kidogo. Nia na madhumuni ni kujifunza kupitia burudani hii iliyowaacha watu kwenye majonzi au kufurahia mwisha mzuri wa Jothan kuwa na mtu ampendaye. *****************************************MWISHO****************************************** ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: