Home → simulizi
→ JAMANI MAMA MARO!
Mama Maro alikuwa ni mwanamke mrembo sana, alitingisha mitaani mpaka ofisini, hali hii ilimpa tabu sana mme wake ambaye ndio mzaa Maro mwenyewe sasa. Ilikuwa kila sehemu akienda sehemu na mkewe watu hawaishi kuwaangalia.
Mzee maro wakati akiwa kijana alikuwa akiifurahia sana hali hii huku akijua kuwa anapata sifa na lazima watu watakuwa wanamuonea wivu kwa jinsi alivyo na mwanamke Bomba. Kwakuwa alikuwa ni kijana na kila alipokuwa akimtazama mkewe alikuwa anammezea mate utadhani sio wake mara kwa mara alikuwa akifanya nae ngono.
Wakati mwingine mama maro akiwa jikoni anapika mzee maro alikuwa anaita….
Mama Marooooooooo
Abee mume wangu
Njoo mara moja
Subiri nakuja namaliza kuunga mboga,
Mama maro unanibishia mimi hizo mboga si nanunua mimi, acha ziungue
Duh mume wangu, haya nakuja baba
Mama maro akiingia chumbani anamkuta mmewe kawasha AC kajikunyata kwenye shuka huku mtarimbo wake ukiwa umenyanyuka na kulenga juu.
Hakuna kitu kingine ambacho anafanya zaidi ya kumkamata mkewe kwa nguvu na kumkumbatia huku akimhemea sehem mbalimbali hasa masikioni na shingoni na kumpapasa kisha anamsaula na kumuweka mikao mbalimbali ya kumpa dozi.
Mzee maro alikuwa anampa dozi mkewe mpaka anapitiwa na usingizi na hatimaye kujikuta anasahau kabisa kupika.
Kwakuwa walikuwa wakiishi wawili tu na mtoto mmoja na Housegirl ilikuwa sasa wanalazimika kwenda kula hotelini.
Hii ni kwasababu housegirl kazi yake ilikuwa ni kumhudumia mtoto tu na kufanya usafi huku jukumu la kupika likiwa la mama maro mwenyewe.
Siku zilizidi kwenda huku mzee maro akiwa hataki kabisa kumruhusu mkewe apate ujauzito kwani alihofia kuwa endapo akipata mimba basi atazikosa burudani ambazo huwa anazipata.
Ilikuwa ni lazima kila anapoenda mzee Maro na mkewe yumo, alikuwa hataki kumuacha nyuma hata kidogo.
Ilifika wakati mama Maro alikuwa anaona kero kwani alijhisi anakosa uhuru na kuwa anabanwa sana lakini wakati mwingine ilikuwa ni burudani kwani alikuwa akikatwa kiu kisawasawa na pia alikuwa anapata kila alichokuwa anataka.
Jambo jingine alilokuwa anafurahia ni kwamba walijihakikishia kuwa yuko mwenyewe kwani kila kona mmewe alienda nae, hivyo wazo la kuibiwa na vibinti vya mtaani halikuwepo kabisa akilini mwake, aliamini yeye ni tiba pekee kwa kijana wake ambaye kwasasa anafahamika kama mzee Maro.
…………………………………….
Kwakuwa mzee Maro alikuwa ni bosi ofisini alilazimisha kwa kila namna sekretari awe mke wake na hivyo kufanya kila kona awe na mkewe, iwe nyumbani mpaka ofisini.
Walikuwa asubuhi wanaamka pamoja wanasaidiana baadhi ya kazi za nyumbani na kuoga kisha wanaingia kwenye gari wanaelekea ofisini.
Wakifika ofisini mwanamke anamuandalia mumewe kila anachopaswa kufanya na kisha anamuacha akifanya majukumu mengine huku na yeye akifanya yakwake.
Mda wa chakula walikuwa wanatoka wote na kuelekea kwenye mgahawa maarufu uliokiwa karibu na ofisini ambapo wanakula pamoja na kisha kurejea ofisini.
Walikuwa na kawaida kuwa inapotimia saa 11 jioni wanatoka ofisini wanaingia kwenye gari na kuelekea moja kwa moja bar ambapo wanapata mbili tatu kisha wanarudi nyumbani.
Wakifika nyumbani kabla ya kitu choochote mzee maro ilikuwa lazima ampe dozi mkewe. Kwakuwa wote wanakuwa wameshtua kwa vinywaji basi walikuwa wakibiringishana weeeee mpaka wanakuwa hoi kabisa.
Wakishamaliza wanaoga kisha wanavaa nguo za nyumbani na kutoka sebuleni ambapo wanatazama taarifa ya habari na kukaakaa na familia kisha wanarudi kulala.
Huko kwenye kulala pia mambo yalikuwa ni yale yale, dozi kwa kwenda mbele kisha wanalala usingizi mzito unaokatika alfajiri na kuwafanya wajiandae kwa kwenda ofisini.
Huyu ndio kijana Maro na Mkewe mama Maro ambapo kwasasa Maro tayari anaitwa ni mzee Maro.
……………………………………….
Kwa taarifa yako mama Maro sio mtanzania, yeye ni mzaliwa wa Rwanda huko kwa Rais Kagame, kwa mara ya kwanza anajikuta anaingia Tanzania ni kipindi kile cha machafuko ya huko kwao ambapo anafaniKiwa kutoroka akiwa na baba yake huku ndugu zake wote wakiwa wameuawa.
Alipofika karibuni kabisa na mpaka wa Rwanda na Tanzania waliwaona wanajeshi wa Kihutu wakiwafwata kwa nyuma na mapanga. Japo walikuwa wamechoka lakini iliwabidi wajikaze kwa kukimbia sana huku baba yake akichukua mizigo yote aliyokuwa ameibeba ili kumpunguzia uzito na kuweza kukimbia vizuri.
Kitendo hicho kilimfanya mzee wa watu azidiwe na mizigo huku binti yake Rozina akiwa mwepesi sana na kufanikiwa kukimbia kumzidi baba yake.
Ndani ya mda mfupi tayari baba yake Rozina alikamatwa na vijana hawa na bila kusita walimlaza chini na kumchinja kama kuku kisha kichwa chake walikiweka kwenye begi na kuanza kumkimbiza Rozina.
Bahati nzuri ni kwamba wakati huu tayari Rozina alikuwa ameshavuka mpaka na hapa alikuwa kwenye barabara kuu ya kuelekea kwenye mji wa Ngara.
Huku akiwa anakimbia na Vijana hawa wa kihutu wakiwa wanamfwata kwa kasi alisikia kwa mbali mngurumo wa gari na makelele ya watu wakiimba.
….hata watoto wanajua..
…ccm namba wani…
…na vijana wanajua…
...ccm namba wani….
….nambari wani eeee….
…nambari wani ni cc-emu…
Huu ulikuwa ni msafara wa kampeni za urais uliokuwa unaenda katika mji wa Rusumo uliokuwa mpakani mwa Tanzania na Rwanda ambapo vijana wawili kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam (Ansbert Maro na Oscar Mchome) walikuwa wamepewa kazi ya kukisaidia chama cha mapinduzi kwenye kampeni zake na siku ya leo walikuwa maeneo ya mipakani.
Wakiwa njiani kwa mbele walimuona mtoto wa miaka kama sita hivi akikimbia huku akipiga makelele, walipoangalia vizuri waliwaona watu wenye silaha wakijificha nyuma ya kichaka.
Kumbe nia yao ilikuwa ule msafara upite kisha waendelee kumfukuza Yule mtoto wamkamate na hatimaye wamuue.
Oscar hakukubali, japo msafara ulikuwa na ulinzi wa polisi lakini aliamuru usimame.
Askari walimsihi sana asishuke kwani eneo hilo halikuwa salama.
Oscar alikuwa hataki kuelewa hata kidogo alivyomuona Rozina alihisi huruma na upendo wa ajabu kwa Yule mtoto .
Aliamua kuruka kutokea kwenye kioo cha gari na hatimaye akaenda mbio kule aliko Rozina ambaye nae alianza kumkimbilia akiamini ni mtu salama kwake anayeweza kumnusuru na wale wauaji wa kabila la kitutsi.
Wakati Oscar anashuka na kumuendea Rozina gari za msafara wake zilikuwa zimemuacha zikiendelea na safari.
Oscar alikuwa karibu kabisa na Rozina lakini kabla hajamchukua alishtuka akipigwa na kitu kizito kichwani kiasi cha kumfanya aanguke chini na kumshuhudia Rozina akichukuliwa huku akilia na kupiga makelele.
Alijizoa zoa pale chini na kujitahidi kuamka kisha akawafwata kwa nyuma kule walikoelekea, alipata nguvu na kukimbia kwa kasi ya ajabu na kufanikiwa kuwafikia.
Aliokota jiwe akampima askari mmoja wa kihutu aliyekuwa amembeba Rozina na kuliachia kwa nguvu likapiga kwenye kisogo cha Yule jamaa ambaye alianguka chini puu…..!
TUKUTANE KESHO!
#sory_jaman_Imejipost
JAMANI MAMA MARO! Mama Maro alikuwa ni mwanamke mrembo sana, alitingisha mitaani mpaka ofisini, hali hii ilimpa tabu sana mme wake ambaye ndio mzaa Maro mwenyewe sasa. Ilikuwa kila sehemu akienda sehemu na mkewe watu hawaishi kuwaangalia. Mzee maro wakati akiwa kijana alikuwa akiifurahia sana hali hii huku akijua kuwa anapata sifa na lazima watu watakuwa wanamuonea wivu kwa jinsi alivyo na mwanamke Bomba. Kwakuwa alikuwa ni kijana na kila alipokuwa akimtazama mkewe alikuwa anammezea mate utadhani sio wake mara kwa mara alikuwa akifanya nae ngono. Wakati mwingine mama maro akiwa jikoni anapika mzee maro alikuwa anaita…. Mama Marooooooooo Abee mume wangu Njoo mara moja Subiri nakuja namaliza kuunga mboga, Mama maro unanibishia mimi hizo mboga si nanunua mimi, acha ziungue Duh mume wangu, haya nakuja baba Mama maro akiingia chumbani anamkuta mmewe kawasha AC kajikunyata kwenye shuka huku mtarimbo wake ukiwa umenyanyuka na kulenga juu. Hakuna kitu kingine ambacho anafanya zaidi ya kumkamata mkewe kwa nguvu na kumkumbatia huku akimhemea sehem mbalimbali hasa masikioni na shingoni na kumpapasa kisha anamsaula na kumuweka mikao mbalimbali ya kumpa dozi. Mzee maro alikuwa anampa dozi mkewe mpaka anapitiwa na usingizi na hatimaye kujikuta anasahau kabisa kupika. Kwakuwa walikuwa wakiishi wawili tu na mtoto mmoja na Housegirl ilikuwa sasa wanalazimika kwenda kula hotelini. Hii ni kwasababu housegirl kazi yake ilikuwa ni kumhudumia mtoto tu na kufanya usafi huku jukumu la kupika likiwa la mama maro mwenyewe. Siku zilizidi kwenda huku mzee maro akiwa hataki kabisa kumruhusu mkewe apate ujauzito kwani alihofia kuwa endapo akipata mimba basi atazikosa burudani ambazo huwa anazipata. Ilikuwa ni lazima kila anapoenda mzee Maro na mkewe yumo, alikuwa hataki kumuacha nyuma hata kidogo. Ilifika wakati mama Maro alikuwa anaona kero kwani alijhisi anakosa uhuru na kuwa anabanwa sana lakini wakati mwingine ilikuwa ni burudani kwani alikuwa akikatwa kiu kisawasawa na pia alikuwa anapata kila alichokuwa anataka. Jambo jingine alilokuwa anafurahia ni kwamba walijihakikishia kuwa yuko mwenyewe kwani kila kona mmewe alienda nae, hivyo wazo la kuibiwa na vibinti vya mtaani halikuwepo kabisa akilini mwake, aliamini yeye ni tiba pekee kwa kijana wake ambaye kwasasa anafahamika kama mzee Maro. ……………………………………. Kwakuwa mzee Maro alikuwa ni bosi ofisini alilazimisha kwa kila namna sekretari awe mke wake na hivyo kufanya kila kona awe na mkewe, iwe nyumbani mpaka ofisini. Walikuwa asubuhi wanaamka pamoja wanasaidiana baadhi ya kazi za nyumbani na kuoga kisha wanaingia kwenye gari wanaelekea ofisini. Wakifika ofisini mwanamke anamuandalia mumewe kila anachopaswa kufanya na kisha anamuacha akifanya majukumu mengine huku na yeye akifanya yakwake. Mda wa chakula walikuwa wanatoka wote na kuelekea kwenye mgahawa maarufu uliokiwa karibu na ofisini ambapo wanakula pamoja na kisha kurejea ofisini. Walikuwa na kawaida kuwa inapotimia saa 11 jioni wanatoka ofisini wanaingia kwenye gari na kuelekea moja kwa moja bar ambapo wanapata mbili tatu kisha wanarudi nyumbani. Wakifika nyumbani kabla ya kitu choochote mzee maro ilikuwa lazima ampe dozi mkewe. Kwakuwa wote wanakuwa wameshtua kwa vinywaji basi walikuwa wakibiringishana weeeee mpaka wanakuwa hoi kabisa. Wakishamaliza wanaoga kisha wanavaa nguo za nyumbani na kutoka sebuleni ambapo wanatazama taarifa ya habari na kukaakaa na familia kisha wanarudi kulala. Huko kwenye kulala pia mambo yalikuwa ni yale yale, dozi kwa kwenda mbele kisha wanalala usingizi mzito unaokatika alfajiri na kuwafanya wajiandae kwa kwenda ofisini. Huyu ndio kijana Maro na Mkewe mama Maro ambapo kwasasa Maro tayari anaitwa ni mzee Maro. ………………………………………. Kwa taarifa yako mama Maro sio mtanzania, yeye ni mzaliwa wa Rwanda huko kwa Rais Kagame, kwa mara ya kwanza anajikuta anaingia Tanzania ni kipindi kile cha machafuko ya huko kwao ambapo anafaniKiwa kutoroka akiwa na baba yake huku ndugu zake wote wakiwa wameuawa. Alipofika karibuni kabisa na mpaka wa Rwanda na Tanzania waliwaona wanajeshi wa Kihutu wakiwafwata kwa nyuma na mapanga. Japo walikuwa wamechoka lakini iliwabidi wajikaze kwa kukimbia sana huku baba yake akichukua mizigo yote aliyokuwa ameibeba ili kumpunguzia uzito na kuweza kukimbia vizuri. Kitendo hicho kilimfanya mzee wa watu azidiwe na mizigo huku binti yake Rozina akiwa mwepesi sana na kufanikiwa kukimbia kumzidi baba yake. Ndani ya mda mfupi tayari baba yake Rozina alikamatwa na vijana hawa na bila kusita walimlaza chini na kumchinja kama kuku kisha kichwa chake walikiweka kwenye begi na kuanza kumkimbiza Rozina. Bahati nzuri ni kwamba wakati huu tayari Rozina alikuwa ameshavuka mpaka na hapa alikuwa kwenye barabara kuu ya kuelekea kwenye mji wa Ngara. Huku akiwa anakimbia na Vijana hawa wa kihutu wakiwa wanamfwata kwa kasi alisikia kwa mbali mngurumo wa gari na makelele ya watu wakiimba. ….hata watoto wanajua.. …ccm namba wani… …na vijana wanajua… ...ccm namba wani…. ….nambari wani eeee…. …nambari wani ni cc-emu… Huu ulikuwa ni msafara wa kampeni za urais uliokuwa unaenda katika mji wa Rusumo uliokuwa mpakani mwa Tanzania na Rwanda ambapo vijana wawili kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam (Ansbert Maro na Oscar Mchome) walikuwa wamepewa kazi ya kukisaidia chama cha mapinduzi kwenye kampeni zake na siku ya leo walikuwa maeneo ya mipakani. Wakiwa njiani kwa mbele walimuona mtoto wa miaka kama sita hivi akikimbia huku akipiga makelele, walipoangalia vizuri waliwaona watu wenye silaha wakijificha nyuma ya kichaka. Kumbe nia yao ilikuwa ule msafara upite kisha waendelee kumfukuza Yule mtoto wamkamate na hatimaye wamuue. Oscar hakukubali, japo msafara ulikuwa na ulinzi wa polisi lakini aliamuru usimame. Askari walimsihi sana asishuke kwani eneo hilo halikuwa salama. Oscar alikuwa hataki kuelewa hata kidogo alivyomuona Rozina alihisi huruma na upendo wa ajabu kwa Yule mtoto . Aliamua kuruka kutokea kwenye kioo cha gari na hatimaye akaenda mbio kule aliko Rozina ambaye nae alianza kumkimbilia akiamini ni mtu salama kwake anayeweza kumnusuru na wale wauaji wa kabila la kitutsi. Wakati Oscar anashuka na kumuendea Rozina gari za msafara wake zilikuwa zimemuacha zikiendelea na safari. Oscar alikuwa karibu kabisa na Rozina lakini kabla hajamchukua alishtuka akipigwa na kitu kizito kichwani kiasi cha kumfanya aanguke chini na kumshuhudia Rozina akichukuliwa huku akilia na kupiga makelele. Alijizoa zoa pale chini na kujitahidi kuamka kisha akawafwata kwa nyuma kule walikoelekea, alipata nguvu na kukimbia kwa kasi ya ajabu na kufanikiwa kuwafikia. Aliokota jiwe akampima askari mmoja wa kihutu aliyekuwa amembeba Rozina na kuliachia kwa nguvu likapiga kwenye kisogo cha Yule jamaa ambaye alianguka chini puu…..! TUKUTANE KESHO! #sory_jaman_Imejipost
Artikel Terkait
*LOVE BITE EP 02* ILIPOISHIA……….. Jothan ilibaki kidogo tu agonge wakate anaendesha kutokana na mawazo yaliyochanganyikana na hasira kwa kile alichofanyiwa na Bahati.. Alijilaumu sana kwenda kula chakula pale na kuambulia maumivu. Alijuta kukutana tena na Bahati ingawaje mwanzoni alikuwa na hamu ya kuonana nae. Alifika nyumbani na kujilaza. ”who a Jonathan by the way??” Aliirudia ile kauli ya Bahati na kujikuta anashindwa kuamini kuwa yule ndie bahati halisi aliyemtamkia maneno yale. SONGA NAYO….. Mawazo yalimuandama Jothan kwa kile alichotendewa na Bahati. Lakini alikubali moyoni kuwa msemo wa wahenga kuwa tenda wema nenda zako hawakukosea kusema hivyo. Aliamua kusahau yote ya nyuma ingawaje ubongoni alikosa tafsiri. Alijua kuwa msaada wowote utakaompa mtu basi hujawekeza chochote zaidi ya maumivu pindi utakapo fadhila kutoka kwake. Likizo yake ilipoisha alienda kazini kama kawaida. Alishangaa mabadiliko Fulani aliyoyaona pale ofisini. Meza yake alikuwa amekaa mtu mwingine kabisa. “salama kaka.” Alisalimia Jothan baada ya kumsogelea yule mtu aliyekaa nafasi yake. “safi tu.” Aliitikia yule mtu ambaye alionekana kuendelea na kazi yake kama kawaida. “samahani, nadhani wewe ni mgeni hapa. Hicho kiti ulichokalia ni changu.” Aliongea Jothan na kumuangalia yule mtu ambaye alikua anamshangaa tu na kujifanya hajasikia na kuendelea na mahesabu yake. “sina taarifa zozote hapa juu yako wewe, kwa hiyo hiki kiti nimepangiwa na bosi mkuu na hakuniambia kama nitahitajika kutoka ukija wewe.” Aliongea yule mtu kwa kujiamini. Jothan aliona kuwa alikuwa anapoteza muda kuongea na yule mtu. Maamuzi ya kuingia ofisini kwa bosi wake yalimjia na kuamua kwenda huko. “Mr.Jothan, hukupata barua yako mapokezi pale nje?” aliongea basi wake hata kabla ya salamu. “barua?…barua gani?” aliuliza Jothan kwa mshangao mkuu. “we nenda ukaichukue… utakachokikuta ndio utajua hiyo barua inahusu nini.” Aliongea bosi wake na kumfanya Jothan kuzidi kushangaa mambo yanavyoenda. Muonekana wa bosi wake ulikuwa tofauti kabisa na muonekano wa kila siku aliokuwa nao. Alionekana kama mtu aliyemkasirikia Jothan wakati alitakiwa kuonyesha hali ya kumlaki ikiwezekana kumpandisha cheo Jothan kwa kufanya kazi kubwa ya kuirudisha kampuni katika hali yake ya kawaida. Jothan alitoka mpaka mapokezi na kumuangalia yule dada wa mapokezi. “doh.. nilishasahau. Kuna barua yako Mr. Jothan.” Aliongea yule dada wa mapokezi huku akishika kichwa chake baada ya kumuona Jothan kuonyesha ishara kuwa alipitiwa kumpa ile barua kabla hajaingia ndani. “ndio nimeifuata.” Aliongea Jothan na kumuangalia yule dada aliyeinama na kuanza kupekua barua kadhaa alizokuwa nazo na kutoa moja yenye jina la Jothan na kumkabidhi. Jothan aliichukua ile barua na kuifungua. Hakuamini kitu kilichandikwa kwenye ile barua. Hakuamini kuwa anaweza kufukuzwa kazi kwa kosa ambalo hajawahi kulifanya. Kampuni ilikuwa inamtuhumu kwa kuisababishia hasara kampuni yake huko Morogoro jambo ambalo halikuwa na ukweli ndani yake. Hasara ilitokea kabla hajaenda na yeye ndio aliyesababisha mpaka baadhi ya wahujumu wa kampuni yake kugunduliwa na kuiweka kampuni hiyo katika hali inayoridhisha kwa sasa. Taarifa hizo zilimchanganya na kumfanya arudi tena kwa bosi wake. “kilichoandikwa humo ndio uamuzi wangu,.. bila shuruti naomba utoke ofisini kwangu.” Aliongea bosi wake na kukataa katukatu kumsikiliza hoja zake. Jothan aliona kama mikosi mfululizo inazidi kumuandama. Hakubishana na mtu. Aliamua kusaini alipotakiwa kusaini na kwenda NSSF kwa ajili ya kufuatilia mafao yake. Kwakua vyeti vyake vilikua vimependeza, hakuchukua muda mrefu kupata kazi kwenye kampuni nyingine. Huko alipewa cheo kikubwa zaidi ya alichokuwa nacho kwenye kampuni yake ya zamani. Hapo aliamini kuwa mungu hakuumba ugonjwa bali ulikuwa na dawa yake. Alimshukuru mungu kwa kupata sehemu iliyokuwa inathamini uwezo wake wa utendaji wa kazi tena kwa muda mfupi. Saikolojia na mahusiano ndilo jambo pekee lililompa chati kwa haraka hapo ofisi kwao kutokana na wateja wengi waliokuwa wakiwasiliana na yeye alipokuwa ofisi yake aliyokwa anafanya kazi zamani wote walihamia kwenye ofisi hiyo mpya. Miezi nane baada kampuni ilimuandalia tafrija kutokana na kuipa jina na mafanikio makubwa kampuni hiyo ambayo ilikuwa haijulikani japo kuwa ilikuwa na miaka mitatu toka ianzishwe. Zawadi alizopewa hata yeye hakuzitegemea. Alipewa na gari aina ya prado mpya kabisa kutokana na mchango wake mkubwa ndani ya kampuni hiyo. Baada ya sherehe hiyo kuisha, watu walitawanyika kwenda makwao. Jothan akiwa kwenye gari yake akirudi nyumbani kwake, kwa mbali alimuona msichana mrembo akimpa ishara ya kuomba lifti kwake. Bila hiyana alipunguza mwendo na kupaki pembeni kidogo. Alipigwa na butwaa baada ya kumuona mtu mwenyewe anayeomba lifti. Hata baada ya yule msichana kumuona Jothan alishtuka kidogo na kuonyesha ishara ya kutoamini kwamba angekutana na Jothan maeneo yale. “wewe, za miaka?” aliongea Jothan na kufungua mlango wa prado yake ambayo ndio kwa mara ya kwanza inatembea kwenye lami ya Tanzania toka ilipoagiziwa huko nchi za ng`ambo. Yule dada alipanda na kukaa nae siti ya mbele. “sikutarajia kama ipo siku nitaonana na wewe” aliongea yule dada na kuvua miwani yake na kuiweka kwenye pochi yake. Jothan alimuangalia yule msichana aliyevaa gauni fupi lililomuonyesha mapaja. Juu alivalia kikoti cheusi na kofia aina ya Cow boy. Muonekana wa yule binti ulizidi kuvutia japo kuwa ni muda mrefu Jothan hakumuona yule msichana. Weupe asilia na wa kujiongezea pia ulizidi kumfanya yule dada asijulikane kama ni Mtanzania au kachanganya na watu kutoka nchi za ughaibuni. Nywele za bandia alizobandika zililingana na muonekano wa Marichui. Tabasamu lilipasua midomo minene iliyopendezeshwa na kimsitari chembamba kilichokuwa katikati ya meno yake ndio kilikuwa kivutio kingine kwenye sura ya yule dada. Hakua mwembamba, pia hakua na unene uliomfanya kuchukiza. Alijua kuutumia mwili wake kwa kukataa tumbo kubwa na kuyafanya maziwa yake kujitegemea yenyewe bila kutumia sidiria. Hayo yote yalibainika haraka kutokana na mtoko alionyuka siku hiyo. “hata mimi, yaani nikikumbuka siku ile sijui ilikuaje mpeka nikapitiwa na usingizi.” Aliongea Jothan na kuonyesha kuwa kichwa chake kilikua kimehifadhi kumbumbu kubwa toka mara ya mwisho kuonana na binti yule aliyeushitua moyo wake kabla ya kukutana na Bahati. “una kumbukumbu wewe.. kwani wewe unaishi wapi?” aliuliza yule dada. “naishi kinondoni kwa manyanya.” Aliongea Jonathan na kumfanya yule dada kupigwa na butwaa. “sasa mbona mimi nakaa kinondoni kanisani baada ya kituo cha Biafra?… na mpaka nashuka nilikuacha ndani gari!” aliongea yule dada na kumfanya Jonathan kutabasamu. “unafikiri niliamka tena?.. yaani nilipitiliza kituo na kwenda kuamshwa na konda gari ilipofika mwenge.” Aliongea Jonathan huku akiendesha gari yake hiyo mpya kwa umakini mkubwa. Waliongea mengi ikiwemo kujuana majina na kupeana namba za simu. Jothan alimfikisha yule dada mpaka kanisani kituo anachoshukia na yeye akageuza gari na kurudi kwake. Kwakua saa ilisoma ni saa mbili usiku, aliamua kwenda kuoga na kulala moja kwa moja kutokana na uchovu wa shughuli yao. Macho hayakufumba haraka japokuwa alikuwa kitandani kwa takribani masaa matatu. Alikizunguka kitanda chote na kukumbatia mito huku akijenga taswira ya kuwa na msichana yule waliokuwa wameonana kitambo lakini hawakupata nafasi ya kuongea kama siku hiyo. Alitabasamu peke yake kila wakati huku ubongo wake ukijaribu kumpa data muhimu za uzuri wa msichana huyo kila nukta aliyokuwa akifanya jambo lolote lililoukosha moyo wake. Hakujua alilala saa ngapi, ila alishtushwa na alarm yake iliyokua inamuamsha kila siku saa moja kamili asubuhi. Aliichukua simu yake na kukuta sms tatu zilizomtakia asubuhi njema kutoka kwenye namba aliyoi save kwenye simu yake jina la SHANI. Alitabasamu na kuzijibu zile sms na kuondoka kwenda kazini baada ya kumaliza kunywa chai aliyoiandaa mwenyewe. Walipiga story kwenye simu alipokuwa njiani na msichana huyo na kukubaliana kukutana kwenye chakula cha mchana Bondeni hotel iliyokuwa magomeni. Kwakua alikua hana kazi nyingi ofisini kulingana na siku yenyewe ilikua nusu siku kwao. Siku ya ijumaa waliitumia kumalizia viporo tu na kazi za siku hiyo walizihesabu kuanza nazo wiki ijayo. Japokuwa alikua si mfuatiliaji, Jonathan aliingia facebook na kutafuta jina analo litumia Shani kwenye mtandao huo wa jamii. Baada ya kulitafuta alilipata na kuanza kuperuzi picha za binti huyo. Hakika muonekano wake ulizidi kumfanya Jothan azidi kuwa na hamu ya kuwa naye. Alikua ni binti ambaye hayuko nyuma wala kupitwa na wakati. Alijua jinsi ya kupangilia nguo na pozi zilizowaacha hoi watu wengi waliomuona. Kila picha aliyopiga ilikuwa na comments zisizopungua mia mbili kutoka kwa marafiki zake waliokuwa wanazikubali pigo zake. Akiwa amezama mtandaoni huku akizifurahia picha za Shani, muda wa kwenda kupata chakula cha mchana uliwadia na Jothan akazima computer yake aina ya apple iliyokuwa mezani kwake na kwenda kwenye gari yake kuitafuta Bondeni hotel ilipo. Baada ya dakika chache alishawasili maeneo hayo na kuchukua simu yake ili ampigie Shani na kumpa taarifa kuwa ameshafika walipo ahidiana kukutana. Kabla hajabonyeza kitufe cha kupigia, moyo wake ulipatwa na mshituko wa ajabu baada ya kuangalia mbele ya meza kadhaa za kwenye hotel hiyo na kumuona Bahati akiwa na bosi wake wa zamani wakilishana huku wakiwa hawana habari. LAliamua kuheshimu hisia za ke na kupiga simu kwa Shani. “umefika wapi babie” aliongea Jothan baada ya salamu. “nimeshafika wangu, wewe upo upande gani?” aliuliza Shani kwenye simu. “nipo upande wa mlango wa kuingilia hotelini kabisa…. Upande wa chakula huku.” Aliongea Jothan na Shani akakata simu baada ya kumuona. Mavazi aliyovaa Shani yalizi kumpagawisha Jothan, kila mtu aliyemuona hakusita kuyagandisha macho yake kwa mdada huyo mwenye uzuri wa ajabu. Hatua za Shani zilimfikisha kwa Jothan na kusalimiana kisha wakaingia ndani pamoja. Macho ya Bahati yaligongana na Jothan ambaye alikuwa na msichana mzuri Shani pembeni yake. Bahati aliangalia pembeni na kujifanya hajamuona Jothan na kuendelea kulishana na mpenzi wake. Jothan naye hakujishughulisha nao, aliwaangalia tu na kuwapita. Akaenda kutafuta sehemu nzuri yenye upepo na kukaa. “uliniambia unaisha peke yako, kwa nini sasa?” aliuliza Shani baada ya kukaa na kuletewa vitu walivyoagizwa. “si unajua kuwa bado sijampata mwanamke wa kuishi nae, ndio maana nimekuwa mpweke pale nyumbani.” Aliongea Jothan na kutabasamu. “jamani, wanawake wote waliojaa hapa mjini, ukizingatia your so handsome. Unanitania wewe?” aliomgea Shani na kucheka. “sikutanii, huo ndio ukweli wenyewe. Nipo single mwenzio.” Aliongea Jothan na kucheka. “ila kaka una moyo wa ajabu sana.” Aliomgea Shani na kumuacha Jothan njia panda. “kwanini unasema hivyo?” aliuliza Jothan. “unajua toka siku ya kwanza tuliyoonana mimi na wewe kule coco beach, sijui kwanini ila niseme ukweli nilitokea kuvutiwa na tabia yako. Maana angekuwa mtu mwengine baada ya kutoa ofa tu basi angeanza kutusumbua mara unaitwa nani mara nipeni namba zenu za simu. Lakini wewe ulikuwa bize na mambo yako na ulipochoka ulituaga na kuondoka zako…. Kusema ukweli nilivutiwa sana na tabia yako.” Alionge Shani na kumfanya Jothan atabasamu. “mi naamini kama unampenda mtu si lazima mpaka umpe ofa ndio uanze kumuelezea… hata mimi nilivutiwa na wewe sema nilishindwa kukueleza kwakua ulikua na marafiki zako na nilihofia pia kuniona msumbufu kwakua niliwapa ofa.” Aliongea Jothan na kumfanya Shani atabasamu. Walimaliza kula na na kutoka mule hotelini, Jothan hakuwaona tena wakina Bahati na hapo ndipo aipogundua sababu ya kuachishwa kazi. Alitikisa kicwa kama ishara ya kusikitika na kuelekea kwenye gari yake na kumpakiza Shani ambaye kwa muonekana hawakuwa na tofauti na wapenzi wawapo out. Kama kawaida yake,. Alimfikisha Shani kituo cha kanisani na yeye akarudi kwake. Usiku wa siku ya jumamosi ilikuwa ni siku Spacial ya mtoko kati ya Shani na Jothan kwenda club. Walifika club na kucheza mziki vya kutosha na kila mmoja aliifurahia ile siku. Walirudi nyumbani pamoja, na Shani kwa mara ya kwanza akaingia nyumbani kwa Jothan. Kwakua walikuwa wamelewa, walilala wote mpaka asubuhi bila kufanya lolote na kuamka asumbuhi. Waliangaliana na kucheka huku kila mmoja akiwa hana kumbukumbu sawa sawa kuwa ilikuwaje mpaka wakalala wote chumba kimoja tena kila mtu akiwa amelala kivyake. Mazoea yalizidi mpaka ikafikia wakati Shani akawa anapewa ufunguo wa nyumba na Jothan ambaye akirudi kazini alikuta nyumba safi na amepikiwa chakula kizuri. Upishi wa Shani haukufanana na muonekano wa ke. Wasichana wengi wazuri jikoni huwa hamna kitu. Lakini yeye alikua anatoa vitu ambavyo akati mwengine Jothan alishindwa kuvumilia na kumwambia kuwa alikua anataka kumuoa kabisa ili awe anampkia daima. Uakaribu ukajenga penzi moto moto lililowashinda mpaka wenyewe na kujikuta Shani amehamia kabisa nyumbani kwa Jothan. Maisha ya furaha na yenye raha tele yalizidi kujijenga kwa Jothan. Hakuwa na mawazo tena zaidi ya kumshukuru mungu kwa kumpamsichana ambaye hata yeye alikuwa na mapenzi a kweli kwake. Kuna siku ambazo Shani alikua analala na Jothan na siku nyingine alikuwa analala kwao kutokana na kuwa bado hajawa mke wake halali. Jothan alivizia siku ambayo Shani hayupo mule ndani na kuamua kufungua kabati yake ambayo ilijaa siri zake nyingi za maisha yake na kumbukumbu mbali mbali zinazomuhusu yeye. Vitu vilivyofaa alivirudisha kwenye kabati na vingine ambavyo vilikuwa havifai kwa usalama wa penzi lake alivichukua kwa lengo la kuvitia moto. Baada ya kupekua muda mrefu, aliibamba alburm moja iliyokuwa na picha kadhaa za zamani toka yupo shule. Baada ya kufungua kurasa kadhaa, alishtuka baada ya kuona picha ya msichana mzuri aliyekuwa amemkumbatia huku wanatabasamu. Mawazo yalimpeleka mbali sana. *************************** Ilikua siku ya aina yake baada ya Jothan kupelekwa katika mashinadano na Shule aliyokuwa anasoma. Mashindano hayo yalikuwa yanatafuta mshindi wa mdahalo kwa lugha ya kiingereza. Kila shule ilitakiwa itoe wanafunzi wawili. Wakiume na wakike. Mwanafunzi wa kiume alichaguliwa yeye kutokana na kuwa na lafudhi nzuri na ya kuvutia kwenye lugha hiyo. Ingawaje alikua kidato cha pili, lakini shule ilimuamini na kuona kuwa ni yeye pekee ndio anafaa kutokana na uwezo wake kwenye somo hilo na vile anavyojiamini. Mashindano hayo yalifanyika kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Jitegemee. Kwanza ufunguzi ulifanyika na Bendi ya shule hiyo kwa kupiga ala za muziki zilizokuwa zikifuatishwa na watu wate waliohudhuria pale. Kulikua na shule zisizopungua Arobaini. Kila shule iliwakilishwa kwenye sekta mbali mbali, wapo walioigiza kiingereza na wengine waruka sarakasi. Shule za international zenyewe zilishindana kwenye mdahalo uliokuwa wakibishana kati ya watoto wa mitaani na walio shueni, wapi wanaoharibiwa zaidi na utandawazi?. Mada hiyo ilibeba ubishani mkubwa lakini Jothan aliweza kuifanya shule yake kuibuka kidedea kutokakana na hoja kali na zenye uzito alizokuwa akizitoa kwenye utetezi na kuwashindwa wapinzani wake. Walipowa wakipata chakula baada ya shindano, dada mmoja aliyekuwa shule pinzani alimfuata na kumuomba akae nae kwenye meza moja. “hamna shida, karibu” aliongea Jothan na yule dada akaweka chakula chake na kuanza kumuuliza Jothan maswali. “nifaye nini ili niweze kuongea kingereza kizuri kama wewe?” aliuliza yule dada na kumuangalia Jothan “ni kazi rahisi, kwanza kipende na kuwa na juhudi nacho, ni lazima utakuwa na uwezo wa kukitumia utakavyo.” Aliongea Jothan na kumfanya yule dada atabasamu. “hivi unaitwa nani?” aliuliza yule dada baada ya kimya kifupi kupita. “Jothan” alijibu Jothan kifupi. “wooh.. nice name,… mimi naitwa Prisca.” Alijitambulisha yule msichana, “Prisca, jina la mama yangu hilo.” Aliongea Jothan na kumfanya yule dada atabasamu. “una simu?” aliuliza Prissca. “ndio.” Alijibu Jothan huku akijua ni kitu gani kilifuata baada ya Prisca kumuuliza swali lile. “unaonaje tukipeana contact sababu nahitaji sana ushauri wako na ukaribu pia kati yangu mimi na wewe kama hautajali.” Aliongea yule dada na Jothan alianza kumtajia namba zake na yule dada alitoa simu yake na kuandika zile namba alizokuwa anatajiwa. Baada ya kuihifadhi kwenye kitabu cha simu yake, alimbipu Jothan nay eye akai hifadi pia. Waliagana na kila mmoja akarudi kwao baada ya kuruhusiwa. Kesho yake Jothan alienda shuleni kwao na kupongezwa na mwalimu mkuu baada ya kupigwa kengele ya dharula na wanafunzi wote kukusanyika msitarini. Alimpongeza. pia mwalimu wa Jothan kwa kumpa muongozo mzuri. Aliporudi nyumbani, aliiwasha simu yake na baada ya sekunde kadhaa message tatu ziliingia mfululizo. Alipofungua zote zilikua za Prisca. Na zote zilimtaka akutane naye kama atakuwa na muda. Kwakua kwenye simu yake kulikuwa na vocha za kutosha. Aliamua kumuendea hewani. “niambie” aliongea Jothan baada ya simu yake kupokelewa upande wa pili. “safi tu, nilikuwa nahitaji kuonana na wewe leo kama utakuwa na muda.” Aliongea Prisca na kumfanya Jothan kutabasamu. “tutaonana wapi sasa?” aliuliza jothan huku akionyesha wazi kuafiki swala la kuonana na binti huyo. “popote tu utakapoamua wewe.” Aliongea Prisca na kumpa mwanya Jothan wa kuchagua. “sio mbaya kama tukikutana namanga, au wewe una semaje?” aliongea Jothan. “poa, saa ngapi?.” Aliuliza Prisca.” “mida hii mi najiandaa, nafikiri tukutane baada ya saa limoja kutoka sasa.” Aliongea Jothan. “poa” alijibu yule msichana na Jothan akakata simu. Jothan alienda kuoga haraka na kuvaa nguo zake nzuri mpaka mama yake akamshangaa. “wapi tena hiyo mwanangu?” aliuliza mama yake Jothan baada ya kumuona mwanaye amependeza kupita kiasi. “naenda maktaba kujisomea.” Aliongopa Jothan ili kukwepa maswali mengi kutoka kwa mama yake ambaye alikuwa anampiga vita juu ya kujihusisha na mahusiano na watoto wa kike Jothan alishuka namanga walipopanga kukutana na yule msichana. Dakika tano baade, Prisca naye alishuka na kukutana na Jothan. Mavazi aliyovaa Prisca yalimpendeza sana na kumfnaya Jothan kidogo moyo umshtuke kumuona msichana huyo ambaye ndio mara ya kwanza kukatana nae akiwa nje ya sare za shule. Aliduwaa kwa muda akiutathmini uzuri wa msichana huyo mgeni kwake mwenye kasi ya ajabu. “wooo.. umependeza sana.” Alisifia Jothan baada ya kukutana na yule msichana. “sikushindi wewe.” Alijibu yule msichana na kutabasamu. “kwakua muda bado unaruhusu, unaonaje tukichukua bajaji twende coco beach tukapate kipupwe na kufurahisha nafsi zetu.” Alishauri jothan na kumuangalia msichana huyo aliyemvutia kila akimtazama. “ok, nadhani itakuwa poa zaidi.” Aliongea Prisca na safari ya kuelekea coco beach ilianza mara moja baada ya kupata bajaji ya kukodi iliyowafikisha salama maeneo hayo. Walitembea huku ha huko huko wakila cone na crips. Watu walikuwa wengi na kuchangamsha eneo hilo. Tamasha pia lilikuwepo na baadhi ya wasanii wa bongo flavour walifika na kutumbuiza kwenye ufukwe huo uliomiminika watu kila dakika. Kutokana na kutopenda makelele, Jothan na Prisca walienda kwenye mapango ambapo kulikuwa na watu wachache wakiwa wametulia na wapenzi wao. Na wao waliafuta sehemu tulivu na kukaa na kuongea yao. Wakiwa wamejisahau baada ya kuzama kwenye stori na vicheko vya hapa na pale, ghafla wakajikuta wamezungukwa na watu watatu na mmoja wao akiwa amevalia mavazi ya kiaskari. “aroo, mna fanya nini hapa?” aliuliza yule askari aliyevalia sare kwa ukali. “sisi…sisi tumekaa tu.” Alijibu Jothan huku akitetemeka. “mmekaa tu, mbona mmejitenga?” aliuliza askari huyo na kudakiwa na mwenzake aliyekuwa amevaa nguo za kiraia lakini akiwa na pingu kama nne kiunoni mwake. “walikuwa wanafanya ufuska hawa.” Aliongea yule askari na kumfanya Jothan kukataa kwa kutikisa kichwa. Uoga uliwa jaa kupita kiasi. Huyo Prisca ndio kabisaa, hakuweza kufanya lolote zaidi ya kuanza kulia. “wewe si mwanafunzi?” aliuliza yule askari huku akiendelea kumkazia macha Jothan “hapana.” Alikanusha Jothan “na wewe msichana si bado mwanafunzi wewe?” Yule askari alimgeukia Prisca na kumuuliza kiukali na kumfanya azidi kuogopa na kijasho cha uoga kiliamza kumtiririka. “ndio..bado mwanafunzi afande.” Alijibu kiuoga Prisca. “sasa wewe unaenda kufungwa miaka thelethini jela, unamrubuni mwanafunzi?,,,mfunge pingu mara moja.” Aliongea yule askari na kumfanya Jothan kushangaa. Hakuamini kuwa wale maaskari walikuwa na nia ya kuwakamata. Alizunguka askari yule mwenye pingu na kumfunga Jothan mikononi. Walichukuliwa wote wawili na kwenda nao pembeni ambapo waliwakuta wavulana wengi rika mbali mbali waliokuwa wamekamatwa na wapenzi wao waliokuwa kule mapangoni. Wavulana waliitwa mmoja mmoja na kuhojiwa na baadae waliruhusiwa baada ya kutoa faini kutokana na kosa hilo la kukaa faragha mapangoni kitu ambacho maaskari wanaolinda eneo hilo wamekataza. Waliwaacha Jothan na Prisca wa mwisho kama walivyo wakamata. “unajua kuwa kutembea na mwanafunzi ni kosa kisheria na adhabu yake ni kubwa sana. Sasa usipoteze muda. Una shilingi ngapi tuwaachie?” aliongea askari aliyekuwa anawahoji wale watu waliowakamata. “hapa nimebakiwa na shilingi elfu nane tu.” Aliongea Jothan kiunyonge. “sasa hiyo elfu nane tutagawanaje?.. acha utani dogo utaenda kuozea segerea.” Aliongea yule askari na kuanza kumsachi Jothan. Aligundua kuwa ni kweli salio lake lilikuwa elfu nane. Alimuita Prisca na kumuuliza. “una shilingi ngapi ili tuwaachie?” aliuliza yule askari na kumuangalia Prisca ambaye bado alikuwa analia. “elfu ishirini.” Alijibu Prisca. “zilete hapa, haya na wewe zilete hizo elfu nane zako.” Aliongea yule afande na wote wakatii haraka na kutoa hela walizokuwa nazo. “mna nauli?” aliuliza yule afande na baada ya kupokea zile hela zote. “hatuna, hela zote ndio hizo.” Alijibu Jothan. Yule afande alichomoa elfu tatu na kuwapa kama nauli. “haya poteeni haraka, msirudie tena kujiingiza kwenye vitendo vinavyoshawishi ngono sawa..haya potea kabla sijabadili maamuzi.” Alipiga mkwara yule askari na wao wakaondoka haraka. Hawakuwa na hamu ya kuendelea kukaa pale coco beach, waliamua kuondoka. Walipofika kituoni waliagana na kila mmoja akapanda magari yaendayo kwao. Walipigiana simu na kila mmoja alimtaarifu mwenzake juu ya kufika salama nyumbani kwao. Kisanga kilichowakuta ilibaki kuwa siri yao. Hakuna aliyediriki kumuhadithia mtu yeyote. Mapenzi ya kishule shule yalianza taratibu na mwosho wakajikuta wanapendana kiukweli na hakuna aliyeridhika kupita siku bila tukio la kuonana. Walimaliza elimu yao ya kidato cha nne huku mapenzi yakiendelea kati yao. Waliridhika kuonana na kuchat kupitia simu na mitandao ya kijamii. Jothan alipomaliza kidato cha nne alichaguliwa kwenda kibaha kumalizia elimu yake ya kidato cha tano na sita. Alifaulu vizuri na kwenda chuo kikuu morogoro. Huo ndio ulikuwa mwanzo wa kupotezana na Prisca. Kwani alipoteza simu na akaamua kubadisha line wakati namba ya Prisca haikuwa kichwani mwake kutokana na tabia ya Prisca kutodumu na namba mmoja muda mrefu. Alimuwaza sana mpenzi wake huyo waliyekutana enzi za shule na kukua pamoja. Hakua na jinsi zaidi ya kupiga kitabu baada ya kuona anapoteza muda kumuwaza mtu ambaye hata kwao walipo hivi sasa hapafahamu. Hii ni baada ya kupewa taarifa za kuhama Prisca pale walipokuwa wana kaa mwanzo baada ya kuuza nyumba yao. ***************** Mawazo yalirudi tena kwenye ile picha na kuamua kuificha bila kuichoma moto kama alivyotaka mwanzo kufanya. Badala yake alienda sehemu ambayo kulikuwa na hati ya nyumba yake na kuiweka ile picha katikati. Ni kweli Prisza alikuwa anampenda na hawakuwahi kuachana. Ni muingiliano tu wa maisha ndi uliowatenganisha. Moyo wake aliona kama si haki kuichoma ile picha kwakua bado alikua na nafasi ndani ya moyo wake japokuwa kuonana na msichana huyo ni ngumu sana. Hata alipomaliza chuo alijitahidi kumtafuta bila mafanikio. Mpaka muda huu anajitegemea ni kipindi kirefu cha miaka sita tuko walipokutana na Prisca kwa mara ya mwisho. Mawazo ya msichana huyo wa kwanza katika maisha yake yalimchanganya kichwa na hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali matokea na kuanzisha ukurasa mwengine wa maisha yake kwenye mapenzi na shani Baada ya usafi huo wa kabati lake, aliamua kujilaza kitandani na usingizi ukamchukua. ITAENDELEA ... Read More
*LOVE BITE EP 04* ILIPOISHIA…… Aliongea Jothan huku machozi yakimlenga lenga. Hakika ni uamuzi mgumu aliouchukua kwakua aliamini ilikuwa ni mtihani mkubwa katika mapokezi ya mlengwa. Alipoinua macho yake kumtazama Prisca, tayari mashavu ya prisca yalishalowana kwa machozi huku macho yakiwa mekundu. Kilio cha kwiki kilianza kusikika na kumfanya Jothan kuingiwa na imani baada ya kumtaza mpenzi wake huyo anaye amua kumuacha bila kosa lolote. SONGA NAYO…………….. Machozi na kilio cha kwikwi kiliendelea kwa dakika kadhaa, Prisca alimuangalia Jothan ambaye alikua ana muonea aibu wakati huo. Hakuamini kuwa ndiye yeye aliyetamka maneno yale,. “kwanini mimi?…. kwanini Jothan umeamua kuzichezea hisia zangu kwa miaka yote hiyo niliyokuwa na wewe kumbe ulikuwa huna malengo ya kuwa na mimi. Kwanini Jothan umeamua kunifanyia hivyo?” aliongea Prisca huku analia. “sorry Prisca. Unafikiri ningefanyaje kwa hali niliyokuwa nayo hivi sasa. Sina jinsi japokuwa bado nakupenda sana. Ningekuwa mtu mwengine hivi sasa ningeendelea kuwachanganya wote wawili. Ila roho huwa inanisuta kufanya hivyo kwakua hata mimi sihitaji kuchezewa hisia zangu. Naomba kubaliana tu na maamuzi yangu japokuwa unaumia.” Aliongea Jothan huku na yeye akijifuta machozi yaliyomdondoka kutokana na hali aliyokuwa nayo Prisca inavyosikitisha. “thank you for everything.” Aliongea Prisca na kunyanyuka na kuondoka. Alimuacha Jothan ambaye alijiinamia na kujilaumu kwa alichokifanya. Akili nyingine ilimwambia kama mwanaume wa ukweli na mwenye msimamo basi alifanya maamuzi sahihi na ya busara. Alirudi nyumbani na kumkuta Shani amejaa tele nyumbani kwake. Alipofika tu, Shani alimfuata na kumkumbatia. Ingawaje Jothan alijichekesha, lakini Shani aligundua kuwa hakuwa sawa. “una nini mume wangu?. Aliuliza Shani baada ya kumuangalia usoni Jothan. “kawaida tu mke wangu.. kwani naonyesha nina tatizo?” aliuliza Jothan kuhakikisha alichokisikia kutoka kwa Shani. “sura yako inaonyesha kama ullikuwa unalia au ulikuwa unahuzunika muda si mrefu.” Aliongea Shani na kumfanya Jothan kumuangalia usoni Shani. “kichwa kilikua kinanigonga sana, hata hivyo sasa hivi niko sawa.” Aliongopa Jothan “pole mume wangu, kama bado kinaendelea we niambie nikununulie panadol au nikusindikize hospital… usidharau mume wangu.” Aliongea Shani huku akionyesha kwa alikua anajali sana afya ya mwenzi wake. “usijali, niko sawa tu.” Aliongea Jothan na kuingia chumbani kwake. Alijilaza na kuwaza yaliyotokea muda mfupi uliopita. Aliamua kupiga moyo konde na kuona yote yalikuwa ni majaribu tu. Maisha yalikuwa mazuri huku kila mmoja akifurahia uwepo wa mwenzake. Hata Jothan mwenyewe alikiri kuwa uamuzi wake ulikuwa sahihi sana kumchagua Shani katika maisha yake badala ya Prisca ambaye mpaka kipindi hicho alikuwa ameshakatisha mawasiliano naye. Shani naye alijitahidi kuhakikisha anafanya yale yote apendayo Jothan na kumteka Jothan kisawa sawa. Ilkuwa akiongelewa mwanamke bora basi Jothan alilipitisha jina la Shani bila kuangalia kuwa alikuwa na nani au alizungukwa na wasichana wazuri. Alitumia muda mwingi kuwa karibu na Shani. Hata kama alikua anataka kwenda kutanua, basi Shani alikuwa ubavuni kila walipoenda. Siku moja ambayo ilikua ni mwisho wa wiki, Jothan aliamua kulala tu Jumaapili hiyo kutokana na uchovu aliokuwa nao wa jana yake kwakua walienda club yeye na Shani na kurudi asubuhi kabisa. Nyumbani kwake aligonga hodi mgeni mmoja wa kike na kufunguliwa mlango na Shani ambaye alishaamka na alikuwa anfanya usafi nyumbani kwake. “za saa hizi dada.” Alisalimia yule mgeni ambaye alionyesha wazi kuwa alikua amechoka kutokana na mimba kubwa aliyokuwa nayo. “salama tu.” Alijibu Shani na kumsikiliza huyo msichana shida yake. “sijui nimemkuta mwenye nyumba hii?” aliuliza yule dada na kumuangalia Shani aliyekuwa makini akimsikiliza. “mwenyewe kalala, ila naweza kukusaidia kama hutajali kunieleza shida yako.” Aliongea Shani na kumuangalia yule dada. “ni vyema kama nita onana nae mwenyewe.” Aliongea yule dada na kumfanya Shani amkaribishe ndani. Kwakua Shani alikua anaandaa chai, hakuona ubaya kuandaa ya kutosha na kumkaribisha yule mgeni aliyekunywa chai kama anafukuzwa kutokana na njaa aliyokuwa nayo. Shani aligundua njaa aliyokuwa nayo mgeni huyo na kumuongezea vyakula mpaka alipohakikisha ameshiba ndio akaamua kumfuata na kumuuliza maswali machache wakati wanamsubiri bwana mkuwa aamke. “tunsubiri aamke, si unajua alikesha jana kwa hiyo sio vizuri kumuamsha mtu akiwa katika uchovu kama huo.” Aliongea Shani na wazo hilo likapitishwa na yule mgeni. Jothan aliamka na kwenda kuoga. Alivaa nguo zake nyepesi na kwenda sebuleni na kumkuta mgeni aliyekuwa anamsubiri. Yule dada alipogeuza shingo kumuangalia Jothan, macho yalimtoka na kujikuta mshangao mkuu umempata. “wewe, umefuata nini nyumbani kwangu?” aliuliza Jothan kwa hasira. Yule mgeni hakua na la kujibu zaidi ya kujiinamia. “na wewe unawakaribishwa watu humu ndani wengine ni nyoka kama huyu mwanamke.” Aliongea Jothan na kumuweka Shani kwenye bumbuwazi. “mbona sielewi, maana mimi aliniambia ni mgeni wako ndio maana nikaona si vibaya kumkaribisha ndani.” Alijitetea Shani. “mimi simjui huyu, .. kwani wewe msichana unaitwa nani?” aliuliza Jothan na kwenda kukaa kwenye moja ya sofa za pale sebuleni. “BAHATI.” Alijibu yule mgeni kwa aibu na kuangalia chini. “WHO A BAHATI BAY THE WAY??” Aliongea Jothan na kumfanya Bahati kupiga magoti mbele yake na kuanza kulia kwa uchungu. “sihitaji kupigiwa magoti mama, mpigie magoti mungu wako na umuombe msamaha kwa ulichokitenda kwangu mimi.” Aliongea Jothan na kumuinua Shani pale chini. “naomba unisamehe, nimehadaika tu na jiji na hivi sasa limeshanifunza Jothan.” Aliongea Bahati huku analia. “leo hii unamjua Jothan wewe?.. si ulikua hunijui wewe?.. nani kakutajia jina langu?” aliuliza Jothan maswali mfulumizo yaliyomshinda Bahati kujibu na kubaki analia tu. “nyamaza kulia dada, kwani tatizo ni nini?.. niewekeni wazi jamani.” Aliongea Shani baada ya kukaa kimya muda mrefu. “sikiliza mke wangu, huyu dada ni mpumbavu na hana akili hata kidogo. Alikuwa na matatizo ya macho yaliyomsababishia upofu na hakuwa anaona hapo mwanzo. Mimi kwa imani yangu nikamchukua kutoka kwa mama yake Arusha na kuja naye hapa Dar kwa nia njema ya kumtibu. Sikuhitaji chochote kutoka kwake. Ila malipo aliyokuja kunilipa haki ya mungu kanifanya moyo wangu uwe na sugu na kuwa mgumu kuwasaidia wengine. Yaani alipopata macho ndio akaniona mimi takataka baada ya bosi wangu kumtaka. Siku niliyokutana naye akajifanya sauti yangu kaisahau. Yaani hata nilipojitambulisha bado akijifanya hanijui. Nikasamehe na kuachana naye, bado akaona haitoshi akaamua kunifanyia fitina mpaka nikafukuzwa kazi bila kosa. Sasa huyu utamuita mtu au kiatu tena kisichokuwa na kamba?” Aliongeea Jothan maneno yaliyomchoma Bahati na kumfanya aanze kulia kwa sauti kubwa zaidi ya aliyokuwa analia. “msamehe mume wangu, mungu kakujaalia umepata kazi nyingine. Na hujui kakuepusha na nini kukutoa kule. Na huyu adhabu yake ndio hii. Maana amepewa mimba na ametimuliwa. Hana msaada mwingine zaidi yako wewe. Msamehe tu mume wangu.” Aliongea Shani na kumsogelea Jothan aliyekuwa kafura kwa hasira na kuanza kumshika shika. Jothan alivuta pumzi ndefu kisha akamuangalia Bahati. “ni msaada gani unaotaka kutoka kwangu?” aliuliza Jothan na kumfanya Bahati kufuta machozi. “naomba unisaidie kunipeleka tu Arusha kwa mama yangu.” Aliongea Bahati huku analia. Kauli hiyo iliwaigia wote wawili. Ghafla walishangaa kumuona Jothan machozi yanamtoka kwa jinsi alivyokuwa anamuonea imani msichana mzuri walivyomtumia vibaya na kuwa kama kituko. Hakua Bahati yule kipofu mwenye bashasha usoni kila wakati. Sasa hivi mashavu yalimuingia ndani, nywele zake hazitazamiki mara mbili. Ngozi yake ilijaa makovu ya kupigwa kila sehemu. Jothan alijikuta ameguswa na kuanza kulia kwa sauti. Alinyanyuka huku analia na kumfuata Bahati na kumuinua kichwa chake na kuitazama sura yake iliyokuwa imelowa machozi na kuvimba kutokana na kulia kwa muda mrefu. “utakaa hapa mpaka utakapojifungua na kurudisha afya yako… pole sana kwa yaliyo kukuta.” Hatimaye aliongea maneno hayo yaliyomfanya Bahati kumkumbatia Jothan bila kujali uwepo wa mke wake pale. Wali muhurumia Bahati na kumpa chumba mule ndani. Siku tatu baadae, Bahati alipatwa na uchungu na kumuwahisha hospitali ya kulipia iliyopo kinondoni. Uchungu ulidumu kwa siku mbili mfululizo na kwa bahati nzuri Bahati alifanikiwa kujifungua salama mtoto wa kike. Aliwashukuru sana Shani na Jothan kwa utu wao waliouonyesha juu yake, maana walikuwa nae bega kwa bega na kuhakikisha kuwa anajifungua salama. Baada ya miezi mitatu kupita, Jothan aliamua kumsafirisha Bahati na kumrudisha kwao Arusha. Alilazimika kwenda naye kwakua Bahati hakua anapajua kutokana na hali yake ya upofu aliyokuwa nayo mwanzo. Walipofika Arusha mjini, Jothan alikodi taksi iliyowafikisha mpaka nyumbani kwa kina Bahati. Ilikuwa zaidi ya furaha kwa mama yake Bahati baada ya kumuona mwanaye akiwa anaona . alimfuata na kumkumbatia. “karibuni…. Karibuni nyumbani.” Alikaribisha mama huyo kwa Furaha. “ahsante, tumeshakaribia.”aliongea Jothan na kuingia ndani. Kwa furaha ya ajabu, mama huyo alikuwa anatabasamu kila muda kutokana na kumkumbuka mwanaye. Wakati wanaendelea na stori za kawaida. Ghafla mlango ulianza kugongwa kwa nguvu. Mama yake Bahati alitoka na kwenda kumsikiliza mtu anayegonga mlango. Alikaa huko kwa dakika kadhaa. Na baadae alirudi huku akiwa hana furaha kama aliyokuwa nayo mwanzo. “samahani baba, namchukua huyu tukatete kidogo.” Aliongea mama yake Bahati. “hamna shida mama.” Aliongea Jothan na kumfanya Bahati anyanyuke na kumfuata mama yake.. “mwanangu, aliyekuja kugonga ni mwenye nyumba. Amesema kuwa ametuchoka kutokana na kutomlipa kodi yake kwa muda mrefu. Yaani nimechanganyikiwa hata sijui tutafanyaje.” Aliongea mama yake Bahati baada ya kumuita mwanaye chemba. “usijali mama, nililijua hili ndio maana nikamuelezea Jothan mapema. Ametuahidi kutusaidia.” Aliongea Bahati na kumfanya mama yake amuangalie. “kwani, wewe na huyo Jothan mkoje?” Alijikuta mama yake Bahati anauliza swali lile kutokana na kutoelewa mazingira na makubaliano ya kumponyesha mtoto wake macho na kumrudisha akiwa na mtoto. “ni story ndefu mama, ila kifupi ni mkombozi wangu na wewe pia. Naweza sema hivyo.” Aliongea Bahati. “kwa hiyo unataka kusema kuwa hata huyu mtoto si wa kwake.” Aliuliza mama yake Bahati. “ndio mama.” Aliongea Bahati kimkato huku akitaka kumuonyesha mama yake ni jinsi gani asivyotaka kuaonngelea ile mada kwa muda ule. Baada ya muda Bahati alirudi sebuleni alipomuacha Jothan na mama yake akaenda kuandaa chakula cha jioni. “mbona hivyo, kwema?” aliuliza Jothan baada ya Bahati kurejea pale. “sio kwema, kama nillivyokuambia siku ile. Mama kashindwa kulipa kodi hivyo mwenye nyuumba anataka hela yake au tuhame.” Aliongea Bahati na kumuangalia Jothan. Baada ya chakula cha usiku, Jothan alimkabidhi mama yake Bahati fedha tasilimu shilingi laki saba kwa ajili ya kulipa deni la laki nne analodaiwa na hiyo nyengine kwa ajili ya mkataba mpya. Mama yake Bahati alifurahi kidogo machozi yamtoke na kumuombea sana dua za mafanikio Jothan. “naomba niwaache, naenda kulala Hotel na mungu akipenda kesho ndio safari yangu ya kurudi Dar-es-salaam” aliongea Jothan baada ya kuangalia saa yake ya mkononi na kumuonyesha kuwa ilishatimu saa tatu kamili. “sawa mwanangu. Mungu akutangulie katika kila jambo lako.” Aliongea mama yake Bahati na jothan akatoka huku Bahati akimsindikiza. “nakushukuru kwa yote ulioamua kuyafanya katika maisha yangu. Nakuomba usichoke kuwasaidia wasiojiweza kama nilivyokuwa mimi japokuwa nilikuumiza… kwa mungu kuna fungu lako Jothan.” Aliongea Bahati walipokuwa njiani wakisindikizana. “usijali, hata mimi naamini mambo yangu yananinyookea kwakua nakigawa kidogo kwa wenzangu wenye shida. Yale yalikuwa maneno tu tena kwa sababu nilikuwa na hasira. Mimi sina kinyongo na wewe. Moyo wangu mweupe na nakuombea pia maisha mazuri na ya furaha na mtoto wako. Naamini hutofanya makosa tena kwakua umeshajifunza.” Aliongea Jothan huku wakiikaribia bara bara. Baada ya kufika kituoni, waliagana huku Bahati machozi yanamtoka kwakujua kuwa ule ulikuwa mwisho wa kuonana na mwanaume huyo wa ajabu maishani mwake. Aliondoka huku kila baada ya hatua moja akigeuka nyuma kumtazama Jothan. Kwa mbali kulikuwa na gari linakuja spidi upande aliokuwa Bahati. Jothan alipotupa macho yake kuitazama ile gari ilikaribia kabisa kumgonga Bahati ambaye wakati huo Bahati hakuiona ile gari kwakua likua bize kumuangalia Jothan. Aliamua kutupa begi lake na kumkimbilia Bahati, alipofika tu alimsukuma na kwa bahati mbaya ile gari ilikuwa inajaribu kumkwepa Bahati na kumgonga Jothan. “MAAAMAAAAAA!” Alipiga kelele Bahati baada ya kumshuhudia Jothan akianguka chini baada ya kugongwa. Damu nyingi zilikuwa zinamtoka puani na mdomoni. Yule dereva aliyemgonga Jothan, alisimamisha gari na kumuingiza Jothan pamoja na Bahati na safari ya kuelekea hospitali kwa ajili ya kujaribu kuokoa maisha ya Jothan ilianza mara moja.. Walipofika hospitali, walipokelewa haraka na Jothan akakimbizwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi. “jamani kwa hali ya mgonjwa wenu, anatakiwa kufanyiwa operation haraka iwezekanavyo ili kuokoa maisha yake.” Aliongea daktari na wote wakakubaliana kuwa tendo lile lifanyike. Bahati alikuwa mtu wa kulia tu usiku nzima. Alijua yeye ndio sababu iliyomsababishia Jothan kugongwa na lile gari.. Alilia na kumuomba mungu asimchukue Jothan. Alirudi nyumbani asubuhi na kumtaarifu mama yake juu ya kilichotokea. Mama yake alisikitika sana na kwenda hospitali ambapo walikaa kwa masaa manne bila kuruhusiwa kumuona mgonjwa. Walirudi nyumbani na kurudi tena hospitalini jioni ambapo waliruhusiwa kuingia ndani na kumkuta yule mtu aliyemgonga Jothan akwa pale hospitalini. Bahati alimuelekeza mama yake kwa yule mtu aliyeonekana na moyo wa pekee kwa kukubali kuisimamia afya ya Jothan kwa kipindi chote atakacholazwa pale hospitalini. “kwa maelezo ya dokta, amesema kuwa atarejewa na fahamu kiasi katikati ya wiki hii,.. ila itachukua muda mrefu kurudiwa na kumbukumbu.” Aliongea yule jamaa alyemgonga baada ya kujitambulisha kwa jina la Saimon. Baada ya taarifa zile, walikubaliana na kuondoka huku zoezi la kumuangalia Jothan likiwa linaendelea kila siku. Baada ya wiki mbili jothan alifumbua macho. Lakini hakuweza kuongea na hakuwa na kumbukumbu yoyote. “kwa hiyo dokta tunaruhusiwa kuondoka naye” aliuliza Saimon baada ya daktari kuridhika na maendeleo ya Jothan. “mnaruhusiwa, ila kwa masharti. Msimsumbue kwa kumlazimisha akumbuke kitu chochote. Maana kumbukumbu zake zitakuja taratibu kutokana na mazingira katika ubongo wake.” Aliongea dakrari katika moja ya kuwapa maangalizo juu ya mgonjwa wao. “sawa, sasa inaweza kuchukua muda gani hadi kurudiwa na fahamu zake sawa sawa?” aliuliza Bahati. “inaweza kuchukua miezi sita, nane au mwaka mzima kutokana na ukubwa wa tatizo lenyewe.” Aliongea daktari na kuwafanya wote waliokuwa pale waishiwe nguvu. Walikubaliana waondoke naye na kwenda kukaa kwa kina Bahati huku Simon akiwaambia kuwa atakuwa pamoja nao katika kila hali. Kutokana na kuchanganyikiwa siku aliyopata ajali Jothan, Bahati hakuokota kitu chochote alichokuwa amebeba Jothan siku ile. Hivyo hakuwa na mawasiliano angalau amjulishe Shani juu ya ajali iliyompata mpenzi wake. Siku zilikatika kwa kasi bila Jothan kuonyesha dalili zozote za kukumba yaliyokuwa nyuma. Hata jina lake tu alianza kulizoea baada ya Shani na mama yake kulitamka kila mara. Kwa upande wa Bahati alijisikia raha kumuuguza Jothan kwakua alikua analipa fadhila kwa yale aliyomtendea. Alihakikisha kuwa kila alichokihitaji mgonjwa wake basi alikua anakipata kwa wakati. Aliamua kurudia kazi yake ya kuuza maua ili alishe familia inayomkabili. Baada ya miezi sita kupita, Jothan alianza kuonekana kukumbuka kidogo kidogo. Aliweza hata kuuliza kuwa yupo wapi na ni nini kilichomleta pale. Alitamani kwenda kazini tena kama zamani. “PRISCA…… PRISCA” Alisikika Jothan usiku akilitaja jina la mwanamke huyo mara kadhaa. Bahati ambaye alikua amekaa kimya wakati wote, aliamka kutoka kwenye godoro la chini alipolala na mtoto wake na kumsogelea Jothan. Alishangaa kumuona Jothan akitokwa machozi. “mimi ni Bahati “ alijitambulisha Bahati mbele ya Jothan ambaye alikua macho usiku huo huku akitokwa na machozi. “yupo wapi Prisca.” Aliuliza Jothan na kumfanya Bahati ashtuke kidogo kwakua hakulifahamu jina hilo.. “Prisca mimi simjui… au ndio Shani ana majina mawili?” aliuliza Bahati na kumfanya Jothan afikirie kwa muda mrefu. “Shani.. Shani… ndio nani huyo?” aliuliza Jothan huku akionyesha kutokuwa na kumbukumbu nae. “si yule aliyekuwa unaishi nae kabla ya kuja huku ?” aliongea Bahati na kumfanya Jothan avute taswira juu ya mtu huyo aliyekuwa anamzungumzia Bahati. “huyo simkumbuki, yupoje kwani?” aliuliza Jothan na kumuangalia Bahati ambaye wakati huo alikuwa mbele yake akiongea kwa sauti ya taratibu kwa kuwa usiku ulikuwa tayari ni mkubwa. Hivyo sauti zao zilipea na kusikika kila mahali mule ndani. “ni mnene kiasi, mweupe na ana shepu Fulani hivi .. anapenda kuvaa ma wigi ya rihanna.” Alijaribu kumkumbusha Jothan kwa kumtajia muonekana halisi wa mtu huyo. “huyo simukumbuki,….. ninaye mkumbuka mimi ni msichana mzuri niliyeanza naye mapenzi toka tukiwa shuleni. Ni msichana mzuri sana. Na kila siku zilivyozidi kujongea, basi uzuri wake ulikua unaongezeka kila siku iendayo kwa Mungu. Nalikumbuka jina lake huyo dada. Anaitwa Prisca. Ila sijui muonekano wake kwa sasa. Labda ikitokea kuonana nae.” Aliongea Jothan huku akijaribu kuvuta hisia zake juu ya msichana huyo anaye mkumbuka kwa machache tu. “daktari alituambia kuwa tusikusumbue kwa kukumbusha ya nyuma. Ila utakumbuka taratibu. Ni vyema ulale Jothan ili uipumzishe akili yako.” Aliongea Bahati na Jothan akakubaliana nae. Kila siku ambayo Bahati alikua anarudi kutoka katika mihangaiko yake, aliutumia muda huo kupiga stori mbali mbali na Jothan. Wakati mwengine alimtembeza sehemu kadhaa maarufu. Kila akipata fedha nyingi, basi humchukua Jothan na kumpeleka shooping kwa ajili ya kumnunulia nguo. Baada ya miezi miwili kupita, Jothan alirejewa na fahamu zake kamili. Alikumbuka kila kitu. Hata siku aliyokuwa anataka kurudi Dar na kupata ajali ya gari pia aliikumbuka. Alimkumbuka pia Bahati ambaye wakati huo alikuwa naye bega kwa bega wakishirikiana na Simon ambaye alikua anakuja kumtembela mara kwa mara na kumuachia chochote kitu. Siku moja Jothan akiwa barazani anapunga upepo, alifuatwa na Bahati aliyekuwa amebeba Juice glasi mbili na kumkabidhi moja. Aliipokea na Bahati akakaa karibu yake. “lete story” aliongea Jothan baada ya kumuona Bahati kama alikua ana kitu Fulani alichokuwa anataka kumwambia. “nina mpya basi, zaidi kama hutojali. Nilikuwa nahitaji ushauri kutoka kwako.” Aliongea Bahati na kumtazama Jothan. “ulikuwa au unahitaji ushauri kutoka kwangu.” Aliongea Jothan kimzaha. “naomba unishauri,.. Simon ameniambia kuwa ananipenda na yupo tayari kufunga ndoa na mimi. Wewe kama wewe unamuonaje Simon. Anafaa kuwa mume wangu?” alifunguka Bahati na kumuangalia Jothan aliyekuwa anamuangalia pia. “kwa muda mfupi toka nimfahamu huyo mtu, sina shaka naye hata kidogo. Maana alikuwa na uwezo wa kukimbia siku ile aliyonisababishia ajali au hata kunikimbia hospitali. Lakini mpaka sasa ametupa hela nyingi kwa ajili yangu. Huwezi jua Bahati, si ajabu Mungu kamkutanisha na wewe kupitia mgongo wangu. Cha msingi zisikilize hisia zako maana wewe ndio utakuwa naye kipindi hicho mimi nitakapokuwa mbali na wewe. Kama na wewe unampenda na yeye yupo tayari kumlea mtoto wako ni dhahiri shahiri kuwa na yeye anakupenda pia.” Jothan aliongea maneno yaliyomkuna sawasawa Bahati. Alibaki anatabasamu na kumuangalia Jothan ambaye naye alikua anatabasamu pia. “nilikuwa nampenda muda mrefu sana, sema nashukuru sana kuwa hata yeye kumbe alikua ananifikiria.” Alingea Bahati. “hongera. Nilitaka kurudi Dar wiki hii, ila kama ndoa iatapangwa mapema basi nitasubiria mpaka muoane.” Aliongea Jothan na kumfanya Bahati afurahi kupita kiasi. Siku ya harusi kati ya Bahati na Simon iliwadia na maharusi walionekana kupendeza kupita kiasi. Jothan alilifurahia tukio lile baada ya Bahati kuonekana kubadilika na kuwa mwema na mtu mwenye jitihada kama alivyokuwa zamani. Baada ya siku mbili, Jothan aliaga na kurudi Dar. Kwakua hakuwa mgeni wa jiji, alitambua magari ya kinondoni na kuelekea kwake. Alifika nyumbani kwake na kukuta kufuli nje ya geti lake. Hakuwa na jinsi zaidi ya kukaa pembeni kwenye Café iliyokuwa inatazamana na geti lake ili Shani atakaporudi aweze kukutana naye. Alikaa mpaka saa mbili usiku, lakini hakukuwa na dalili za mtu yeyote kufika pale. Aliamua kwenda kulala Gesti kutokana na uchovu wa safari aliokuwa nao. Aliamka asubuhi na kupata chai, baada ya hapo akaelekea nyumbani kwake. Pia alikuta geti likiwa limepigwa kufuli kama ilivyokuwa jana yake. Aliamua kumfuata dalali mmoja aliyekuwa ameweka benchi lake pembeni ya nyumba yake na kumuuliza. “samahani mzee Sadi, hivi huyu mke wangu ana muda gani toka afunge hili geti?” aliuliza Jothan baada ya kusalimiana na mzee huyo aliyemzoe kwa muda mrefu akiwa pale nje na kufanya shughuli zake za udalali wa nyumba,viwanja na vyumba vya kupangisha. “hivi hauna habari?” aliongea mzee Sadi na kumshangaa sana Jothan kwakua alikua anajua kila kitu. “sina habari yoyote mzee wangu. Nimeingia jana tu kutoka Arusha, hivyo sina habari yoyote mie!!.” Aliongea Jothan kwa mshangao mkuu. Alianza kuhisi jambo baya linaweza kuwa lilimkumba Shani kipindi ambacho alikuwa hayupo. “mbona hii nyumba imeshauzwa miezi miwili iliyopita?… tena matangazo yalibandikwa muda mrefu. Sema wenye nyumba bado hawajahamia. Si unajua watu wenye fedha zao bwana?.” Aliongea yule dalali na kumfanya Jothan apigwe na bumbu wazi. “OOOOH MY GOD……..WHY ME?????” Alijikuta nguvu zinamuishia Jothan na kukaa chini. Aliiangalia nyumba yake aliyoijenga kwa gharama kubwa na machozi yalianza kummiminika kama maji. ITAENDELEA ... Read More
MUUZA MAZIW EP 07 “aaaaahh!! Jamani wifi wao!!” Aliongea kwa furaha baada ya kumuona mgeni aliyekuwa akigonga ni penina. “asante wifi , shikamoo!” Penina aliongea na kisha kumkumbatia wifi yake kwa furaha. “ marhaba wifi ,vipi masomo?” Aliongea huku akiipokea mizigo aliyo ibeba “naendelea vizuri tu wifi” “haya mungu akusaidie” Aliongea lisa na kuelakea sebuleni , aliiiweka mizigo pembeni ya kochi na kasha kuelekea sehemuk ilipo friji. Penina, penina akaamua kuichukua mizigo ili aipeleke chumbani. “hapana wifi, hapana , hiyo iache hapo hapo nitaiingiza mwenyewe,, wewe kwanza kunywa juisi upumzike.“ Aliongea lisa huku akiwa ameshikilia jagi lenye juisi pamoja na glasi, alifanya hivyo kwa sababu chumba anachotakiwa kulala penina ndicho chumba ambacho amemficha muuza maziwa. “usipate tabu wifi wangu kunywa juisi upumzike, nipo kwa ajili yako “ Aliongea lisa huku akiibeba mizigo na kuelekea chumbani na kumuacha penina akinywa juisi taratibu. Alipoingia chumbani alimshutua muuza maziwa na kumweleza hali halisi. “kwahiyo nitatoka saa ngapi humu?” “ itabidi uvumilie mpaka usiku wifi akilala , mlango wa nje nitauacha wazi leo” Aliongea lisa “Sawa lakini vipi kuhusu chakula manaake niana njaa” “ usijali nitakuletea utakula humu humu , jitahidi usitoke nitajaribu kufanya mpango hata kamakabla ya usiku ikiwezekana” “poa” Muuza maziwa aliitikia “alafu nitaa……” Lisa alikatiza kauli yakebaada ya kusikia mlio wa kitasa kikifunguliwa. Haraka haraka muuuza maziwa aliingia kabatini na kisha lisa aliufunga mlango wa kabati hiyo kabla hata hajauachia mlango huo alisikia sauti nyuma yake. “wifi mbona unagombana na hilo kabati!?” Swali hilotoka kwa penina lilimfanya lisa ashikwe na kigugumizi cha ghafla huku akitoa maelezo ya kujikanyagakanyaga. “ah, mh, a-, u-n-a-j-u-a hi-li ka-ba-ti ni bo-vu” “limeharibika , ooh, mungu wangu!” Penina aliongea huku akilisogelea kabati hiloili kuiangalia sehemu ilipoaribika. “ah, hapana wifi usiiguse hapa nimeitegesha , iache hivyo hivyo mpaka atakapokuja fundi kulirekebisha” Aliongea Lisa haraka haraka. “okey”[sawa] Aliongea Penina huku akitikisa kichwa kuonyesha kwamba ameelewa. “nataka kuoga wifi” “na kweli manaake umechoka kweli kweli wifi yangu” Aliitikia Lisa haraka haraka kwani alijua huo ndio upenyo wa kumtoa muuza maziwa. Na kweli penina alipoingia bafuni lisa aliufungua mlango wa kabati haraka na kumtoa muuza maziwa , akala chakula haraka na kuanza safari ya kutoka nje ya nyumba hiyo , walipofika kwenye mlango wa kutokea muuza maziwa alimbusu lisa kwa mara ya mwisho , alipomaliza kufanya hivyo alitoka ndani ya chumba hicho na kutokeza koridoni ili atoke nje kabisa ya nyumba hiyo lakini kabla ya kufanya hivyo alisikia muungurumo wa gari, halikuwa gari lingine bali gari la Jerry mume wa Lisa. Hofu iliwaingia kwa ghafla na haraka haraaka walirudi tena chumbani kwa penina , ambapo kama kawaida alimfungia muuza maziwa kabatini, hawakuwa na njia nyingine tena bali hile waliyoipanga awali, muuza maziwa asubiri mpaka usiku wa manane Penina atakapo lala ndipo atoke kwani Lisa atauacha mlango wa kutokea wazi. Lisa alipomaliza kumfungia muuza maziwa katika kabati alitoka nje ya chumba hicho,akiwa koridoni aligongana ana kwa ana macho na mumewe. Wote wawili waliinamisha vichwa vyao chini. Kwani kila mmoja aliona aibu kwa kumsaliti mwenzake. Lisa kwa muuza maziwa na Jerry kwa sekritari wake. “Ah, mmh, wifi amekuja , kakaribu!” Aliongea Lisa kwa kujiumauma huku akiwa na wasi wasi. “ asante amekuja saa ngapi?” “sio muda mrefu” “aah yuko wapi sasa nimsalimie?” “yuko bafuni anaoga” “Okey” [sawa] Aliitikia na kisha kuelekea chumbani kwake. Lisa nae alimfuata mumewe nyuma hukubado akiwa na hofu juu ya kugundulika kwa uwepo wa muuza maziwa ndani ya nyumba hiyo. “Pole na kazi dear” Aliongea Lisa huku akijibaraguza kwa kumvua tai mume wake, macho yake bado yalikuwa na aibu sababu bado alikuwa na wasi wasi kwamba labda mumewe amegundua chochote. “ah, asante mpenzi” Aliitikia Jerry huku akitabasamu, lakina nae pia tabasamu lake liliishia mdomoni tu moyoni nafsi ilimsuta . Maovu aliyoyafanya na sikritari wake ofisini kwake yalikuwa bado yakionekana katika kichwa chake. Akavua nguo na kuingia bafuni kuoga lisa nae alimfuata na kujumuika nae kuoga . Alifanya hivyo ili Jerry hasihisi chochote. Walioga huku kila mmoja akiwa hana habari na mwenzake. Kwani wote wawili walikuwa wamechoka, walipomaliza kuoga wakavaa na kasha kwenda sebuleni. Huko wakamkuta Penina akianga lia tv. “mdogo wangu huyo!” Jerry aliongea kwa furaha huku wakicheka. “kaka!” Penina aliitikia na kisha kumkimbilia kaka yake. “waoo!!!” Waliongea kwa pamoja na kisha kukumbatiana kwa furaha. “habari za masomo!?” ITAENDELEA.. ... Read More
Story......... NI WEWE TU PENINA Sehemu ya Nne (4) By GIVAN IVAN Phone & whatsapp... 0769673145 ilipoishia....... Kwa upande wa kina zaza usiku ule ule walianza kupanga mikakati ya kumteka Frank na kwenda kumtupa mbali kabisa na jiji la dar es salam. Lakini hii ilikuwa kazi ngumu Sana ambayo walihitaji pesa za kutosha na pia wachore ramani ya sehemu watakayoenda kumtupa Frank. .......... Endelea........... Zaza pamoja na wenzake waliumiza kichwa, na hatimaye mmoja wao akapata wazo ambalo moja kwa moja aliliweka hadharani kwa wenzake ili waweze kulifikiria kama ni wazo zuri. " mimi nina watu wangu nawafahamu, ni watu wazuri sana Katika kazi hizi hata kuua kwao ni kitu kidogo tu, hivyo naona tuwape hili dili warusaidie. " aliongea kijana huyo akiwasilisha Wazo Lake. " Wazo zuri Sana mi naungana na wewe moja kwa moja Sasa inabidi utueleze tunawapataje hao watu. " akaongea zaza kumuuga mkono kijana yule. " ninafahamu makao yao kama vip tuongozane mpaka kwao." akaongea kijana yule, na moja kwa moja zaza pamoja na wenzake wakanyanyuka na kuingia kwenye gari Lao na kuanza safari ya kuelekea kwa watu hao. Hapakuwa mbali Sana na sehemu waliyokuwepo, hivyo baada ya dakika chache waliwasili sehemu hiyo. Wakashuka kwenye gari na kubisha hodi kwenye nyumba kubwa iliyokuwa mbele yao. Hakuna mtu aliyewaitikia ndani ya dakika tano wakiwa bado wapo pale mlangoni, lakini ghafla walishtukia wamezungukwa kila sehemu na watu wasiopungua kumi huku wakiwa na bunduki kila mmoja. "mko chini ya ulinzi mikono juu na mjitambulishe nyie ni nani." ikasikika sauti ikiwaamuru wakina zaza. "zaza pamoja na wenzake walitiii na kuweka mikono juu, Kisha zaza akajitambulisha kwa niaba ya wenzake. Zaza pamoja na wenzake walieleweka vizuri Kisha wale watu wakashusha silaha zao chini na kuwakaribisha wakina zaza Katika jumba Lao. " Elezeni shida yenu hatuna muda wa kuangaliana hapa." ikasikika sauti ikiwaambia wakina zaza. Zaza bila kusita alianza kuelezea mipango ya kumteka Frank na kuwataka wao wakawasaidie tu kumtupa mbali na jiji la dar es salam. "hiyo ni kazi ndogo Sana lakini inahitaji pesa kiasi cha shilingi million kumi." ikasikika tena Ile sauti ikiwaambia wakina zaza. "pesa si tatizo pesa Zipo za kutosha." akajibu zaza. "bas vizuri Sana tutawaelekeza namna ya kutupatia hizo pesa alafu mtatuletea huyo kijana mtuachie tumfanyie kazi." ikasema sauti ile. "hamna shida." akajibu zaza. Na muda huo wakapewa maelekezo namna ya kuwaingizia pesa zao, na bila kupoteza muda. Zaza pamoja na wenzake waliondoka usiku ule ule na kuwasiliana mzee Joel na kuwajulisha kias cha pesa wanachohitaji kulitimiza zoezi la kumteka Frank. Mzee Joel wala hakujali kama pesa ile ni nyingi kias gani, yeye alichotaka ni kuwatenganisha Frank na mtoto wake Penina . Usiku ule ule mzee Joel aliweza kuwakabidhi wakina zaza pesa zile na kuwataka wakina zaza wampoteze kabisa Frank lakini wasijaribu kumuua. Zaza pamoja na wenzake nao walizifikisha pesa zile kwa kikosi kile ambacho waliwapa kazi ile ya kumpoteza Frank. Baada ya kuwakabidhi pesa zile, walikubaliana kuwa siku inayofuata wataifanya kazi hiyo kama ipasavyo.* Asubuhi na mapema siku iliyofuata Frank akiwa bado yupo kitandani alishtushwa na mlio wa simu yake ikiita. Frank aliichukua simu yake na alipoangalia mpigaji akakuta ni kipenzi chake Penina. Bila kusita Frank akaipokea simu ile. "my love umeamkaje?" ilisikika sauti nyororo ya Penina ikimuuliza Frank. "nimeamka salama mpenzi wangu sijui wewe?" akajibu Frank na kumuuliza Penina pia. "mimi pia nimeamka salama kabisa mpenzi, na nimekupigia simu asubuhi na mapema kwasababu nataka leo tukanywe Chai wawili." akajibu Penina na kumuambia Frank. "ooh usijali my dear nipo kwa ajili yako kwa lolote lile." akajibu Frank. "ok nakupitia sasa hivi." Penina akamwambia Frank na kukataa simu. Frank muda huo huo alitoka kitandani na kuanza kujiandaa haraka haraka. * Lakini wakati huo huo zaza akiwa na kikos chake walikuwa tayari wameshawasili nyumbani kwa kina Frank kwa ajili ya kutekeleza kazi waliyoagizwa. Frank akiwa tayari ameshajiandaa aliwaaga wazazi wake na kutoka nje ya kwa ajili ya kumsubiri mpenzi wake Penina. Baada ya Frank kutoka nje Bila kutarajia alijikuta anapigwa chuma ya kichwa na kudondoka chini na kuzimia. Na waliofanya kitendo kile hawakuwa wengine bali ni zaza pamoja na wenzake. Haraka haraka Frank alibebwa na kuwekwa kwenye gari yao Kisha gari likaondolewa sehemu ile kwa kasi ya ajabu. Na wakati huo huo Penina ndio alikuwa anawasili na akapishana na gari la kina zaza likiwa Katika mwendo mkali, lakini yeye Penina hakufahamu chochote kinachoendelea. Penina alipaki gari mbele ya nyumba ya kina Frank Kisha akashuka kwa mwendo wa madaha huku tabasumu tamu likiupamba uso wake na kuanza kuelekea ndani kwa kina Frank. "hodi hodi jamani mpaka ndani." ilisikika sauti ya Penina ikibisha hodi lakini muda huo akiwa tayari ameshaingia ndani. "baba na mama shikamooni." akasalimia Penina. "marahaba karibu uketi ." wakaitikia kwa pamoja wazazi wake Frank. "hata sikai jamani nimekuja kumchukua mtoto wenu." akajibu Penina. "yupo nje mbona anakusubiri hujamuona?" akauliza mama yake Frank kwa mshangao huku akitoka nje. "yupo nje mbona sijamuona?" Penina naye akauliza huku akiongozana na mama yake Frank mpaka nje. "mhhh yuko wapi Sasa hebu ngoja nimpigie simu." akasema Penina huku akitoa simu yake na kumpigia Frank. Simu ya Frank iliita bila kupokelewa na alipopiga Mara ya pili akakutana na sauti hii, "simu unayopiga haipatikana kwa sasa tafadhali jaribu tena baadae." Taratibu Penina alianza kunyongonyea na kupoteza tabasumu Lake zuri usoni mwake. "simu haipatikani mama hebu sikiliza." Penina akamwambia mama yake Frank huku akimuwekea simu sikion. "hee mbona makubwa jamani kaenda wapi Sasa huyu Mara hii tu katoka ndani? ." akauliza mama yake Frank huku akiwa ameshika kiuno. Penina naye alizidi kupiga simu bila mafanikio yoyote ya kumpata Frank. Ilibidi mama yake Frank amwite baba yake Frank pamoja na Angel mdogo wake Frank ili wamtafute Frank kwa pamoja. * Gari ya kina zaza ikiwaa Katika mwendo mkali, zaza pamoja na wenzake walimfunga Frank miguu pamoja na mikono Kisha wakachukua kitambaa cheusi na kumfunga Frank usoni ili hata atakapozinduka asiweze kufanya chochote na pia asiweze kugundua sehemu anayopelekwa. Na Kisha simu yake ilipasuliwa kule ndani ya gari pale tu waliposikia ikipigwa na Penina. Moja kwa moja gari ile iliyombeba Frank iliwasili Katika jumba la kikosi kile ambacho wakina zaza walikubaliana nao kwenda kumtupa Frank mbali kabisa na jiji la dar es salam na kamwe asiweze kurudi tena. Baada ya kufikishwa hapo Frank alitolewa kwenye gari la kina zaza na kuwekwa kwenye gari lingine la kikosi kile kingine huku ndani ya gari lile kukiwa na vijana wengine wanne. Na wakati huo huo taratibu Frank alianza kurudiwa na fahamu Zake. Milango ya gari Ile aliyowekwa Frank ilifungwa, na Kisha gari likaanza kuondoka kwenda kumtupa Frank sehemu ambayo kamwe hatoweza kuonana tena na Penina. ........ Itaendelea ... Read More
HOUSE GIRL DIARY; NAITWA RAYA NI HOUSE GIRL MSTAAFU—SEHEMU YA TATU (ILIPOISHIA SEHEMU YA PILI; Raya anarekodi Video ikimuonyesha yule Mama akimtesa mtoto wake wa kambo, akimpiga na kumfanyisha kazi. Anamkabidhi Baba Jack ili aone kinachoendelea. Je nini kitatokea ENDELEA.. Kama hujasoma sehemu ya pipi basi bonyeza hapa; Iddi Makengo Dada alimuona namna Baba anavyobadilika, namna ambavyo uso wake alikua anaukunja, ghafla nilimuona Baba machozi yanamtoka, nikitegemea kama atapandwa na hasira kama nillivyokua mimi na kuanza kumtandika Dada makofi niliona anamgeukia taratibu, alimuangalia kwa uchungu kama vile alikua anataka kusema kitu lakini maneno hayatoki. “Ni…ni nini hiki?” Alijitahidi kuuliza, wakati huo Dada alikua kimya akiangalia chini kwa aibu. “Nisamehe mume wangu ni hasira tu, huyu mtoto wakati mwingine ananiudhi nalazimika kumpiga…” Alijitetea. Mimi bado nilikua nashangaa ni kwanini Dada hakua amelala chini akitokwa damu kwa kipigo. “Hasira ndiyo unwe unampiga mtoto namna hii, hizi ni hasira gani?” Hapa Baba aliuliza kwa hasira kidogo, nilipata faraja labda atamtandika makofi lakini haikutokea. Dada alianza kulia, “Hata mimi sijui mume wangu, sijui hata nini kilinitokea siku hiyo nikampiga mtoto, mimi sina mkono wakupiga kabisa, wewe mwenyewe unanijua labda ni hii mimba…nikiwa katika hali hii nakua tofauti sana…” “Muongo, ni kila siku anampiga, hata haya anayoita mapele ni yeye. Hata chakula anamnyima, anamtukana, anamfanyisha makazi kama Mbwa, huyu si mwanamke ni shetani!” Niliongea huku nikinyanyuka kwa hasira, Baba alikua kama zezeta flani hivi, baada ya kutajiwa neno mimba ni kama alisahau kuwa yule mwanamke alikua ni shetani. Nilikua nasikia mambo ya limbwata lakini nilikua sijawahi kuona mtu kalogwa akalogeka. Kwa namna ile video ilivyokua mtu yeyote mwanye akili timamu hata kama asingekua mzazi wa Jack angekasirika na asingemsikiliza yule mwanamke. “Una mimba mke wangu, ina miezi mi ngapi? Mbona hukuniambia?” Alisahau kabisa kuhusu Jack na kuanza kuulizia upuuzi mwingine ambao nilijua kabisa ni uongo. “Hakluna cha mimba wala nini, hivi wewe huoni kama anataka kukuchota akili!” Niliongea kwa hasira, pale nilikua kama mfanyakazi ila kwa wakati ule nilijua kazi sina hivyo ilikua ni lazima kumtetea Jack na kuhakikisha haki inatendeka. Nilipiga kelele na harakaharaka nilitaja karibu kila kitu ambacho mimi nilikishuhudia Dada akimfanyia Jack. “Mume wangu unaona, huyu binti ndiyo sababu ya kila kitu. Hataki kufanya kazi, nyumba ikakua chafu na kamjaza mwanao kiburi, mbona kabla ya kuja tulikua tunaishi salama. Jack namfundisha kazi na ananisaidia kufanya kazi za ndani, kwa hali yangu hii siwezi kufanya chochote, wewe mwenyewe unakumbuka kilichotokea kipindi kile. Unajua namna tulivyohangaikia huyu mtoto, hivi kweli kumfundisha mtoto wa kike kazi za nyumbani ni kosa? Au kumchapa akikosea ni kosa? Au kwakua mimi sina kazi nipo hapa nyumbani, au kwakua mimi ni Mama wa kambo ndiyo mnaniona kama shetani. Huyu binti anajazwa maneno na Mama yake, kila siku wanaongea na ndiyo wanataka kutuvuruga. Mimi siwezi, mimi siwezi kama umenichoka niambie tu niondoke zangu!” Aliongea huku akilia, kila kitu kilikua ni uigizaji, wakati anaongea alianza kunyanyuka, alinyanyuka huku akishika tumbo kama vile ana maumivu tumboni. “Nini? Kuna nini kimetokea, tumbo linauma?” Baba alimuuliza lakini hakujibu zaidi ya kumuambia niache kama umeamua kumsikiliza huyo baki naye mimi naondoka. Alinyanyuka kwa kupepesuka kisha taratibu alidondoka chini. Niliona kabisa kafanya makusudi kwani hakudondokea sakafuni, alipiga jicho pembeni kisha akapepesa macho na kudondokea kwenye sofa, akawa kama kakaa kiupende kisha ndiyo akafika chini. Baba alipaniki, alianza kuhaha, simu alitupa pembeni na kuacha kuangalia, watoto wake nao walikuja kulia na kumlilia Mama yao. Ilikua ni kama maigizo flani, Baba alianza kuongea habari za Hospitali ndipo alijifanya kufungua macho na kulazimisha kupelekwa chumbani. Aliniambia nimsaidie kumnyanyua lakini sikua tayari, nilimshika Jack mkono na kuondoka naye mapaka chumbani, nilimuacha Baba akihangaika kumnyanyua ili kumpeleka chumbani, alisahau kabisa ishu ya mwanae. **** Usiku mzima sikulala, nilijua nafukuzwa lakini suala la kumuacha Jack pale halikuingia akilini. Nilimuambia Jack nimpeleke kwa Bibi yake lakini alikataa katakata. “Watakuja tu kunichukua, hata nikisema nini hakuna mtu wa kunisikiliza. Wewe dada ondoka tu uniache hapa, nimeshazoea kila dada anayekuja anachoka na kuondoka mimi naendelea tu kubaki. Baba hawezi kuruhusu niondoke, alishagombana na Bibi mara nyingi lakini anasema ananipenda na hawezi kukaa mbali na mimi. Kumbe sikua mimi peke yangu niliyeona yale mateso na kukerwa nayo, kulikua na wafanyakazi wengine wawili nyuma ambao walishafukuzwa kwaajili ya Jack ndiyo maana alikata tamaa. Mmoja alisema kwa Bibi yake Jack na mwingine alimpa chakula na alikua anawasiliana na Mama yake Jack. Asubuhi Baba aliamka kama kawaida, ni kama kulikua hakuna kitu kilichotokea, Dada alijifanya kuamka na kumuamsha Jack kwaajili ya shule, alijidai kumuandaa na kujifanya hana kinyongo. Waliwaaandaa na kuwapeleka shule, alipoondoka tu Dada aliniambia nikusanye kila kilicho changu na kuondoka. Alinitukana sana kwa kutaka kuingilia nyumba yake akiniambia kuwa pale hawezi kuondoka. Alitaka kunipiga lakini kwakua sikuwa nikihitaji kazi tena na nilishajua siwezi kubaki tena pale kumlinda Jack niliamua kumtolea hasira. Baba alishaondoka kwenda kazini hivyo tulibaki wawili tu, pamoja na mwili wangu mdogo lakini nilipitia mengi, maisha ya kupigana mtaani nilishayazoea. Nilimsubiri aliponipiga kofi la kwanza na la pili. Nilimuacha anogewe ndiyo nikaanza kumtandika, hakuamini. Nilimtandika kama vile mtoto mdogo, nilimpiga sana akapiga kelele lakini hakukua na mtu wa kumsikia. Baada ya hapo nilichukua kilicho changu na kuondoka. Nilimuambia naondoka lakini nitarudi, nitarudi kwaajili ya Jack. Alinyamaza kimya bila kusema chochote. Kumbe mtu mwenyewe alikua mayai mayai halafu anajifanya kuonea watu. Niliondoka na kwenda kwa kijana mmoja, huyo alikua ni X wangu, tulizinguana kitambo kabla sijaacha kazi nilipokua nikifanya mwanzoni, yeye alikua ni Kondakta wa daladala hivyo mchana alikua kazini. Mlango wake nilikua naujua vizuri hivyo niliufungua hata bila funguo. Sikua na pakwenda kwani sikua na ndugu Dar, ingawa sikuachana naye vizuri lakini nisingelala mtaani. Jioni alirudi na kunikuta, hata hakukasirika, alianza kucheka na kunitania kama siwezi kuishi bila yeye. Nilimuambia ishu yangu, nikamuonyesha ile video katika simu yangu, hata yeye pamoja na Bangi zake hakuamini kama kuna mtu anaweza kufanya vile tena kwa mtoto mdogo kama yule. “Huyo mwanaume kashatengenezwa, cha kufanya hapo ni kwenda Polisi, mbona siku mbili huyo akikaa ndani anakaa sawa…” Aliongea huku akinigusa, najua alitaka mapenzi lakini sikua katika mood kabisa, ila aliongea jambo amaalo sikuliwaza kabisa hapo awali. “Baba yake anaweza asijali lakini sidhani kama Polisi hawatajali.” Niliwaza kufanya hivyo lakini ulikua ni usiku, niliamua kusubiri mpaka asubuhi. Lakini niliwaza kama itakua vizuri nikienda na Jack kwani nilijua kuwa wakiangalia makovu yake basi utakua ni ushahidi tosha na watamuonea huruma. Lakini ningempataje wakati yuko shuleni, niliamua kwenda nyumbani kwao kumsubiri wakati anatoka shule. Wakati wanashushwa na gari kabla ya kuingia ndani nimchukue na kuondoka naye. Mchana muda wa wao kutoka shule nilichukua Bajaji, nilimuambia Dereva kupaki karibu na geti kabisa, Gari la shule lilipokuja na kuwashusha nilishuka na mimi. Wote waliniona, wale wengine walikimbilia ndani lakini Jack ambaye alikua anaogopa alisimama na kuniambia niondoke kwani atapigwa. Sikumsikiliza wala sikusubiri kumuelezea. Nilimshika na kumvuruta mpaka kwenye Bajaji, nikamuingiza kwa lazima kisha nikamuambia Dereva tuondoke. Kwakua nilishamuambia kila kitu aliwahsa Bajaji mpaka kituoni. Kule nilienda mpaka mapokezi, hakukua na watu wengi, nilianza kuelezea kila kitu, nikawaonyesha na Video. Kila askari aliyeiona alikasirika, tulipewa askari wa kike ambaye alienda kumkagua Jack. Alikua ni Mama mtu mzima, wakati anamkagua alianza kutokwa na machozi ingawa alijizuia sana. Mwanzoni Jack alikataa kusema lakini baada ya kuhakikishiwa usalama wake lielezea kila kitu. Niliandikisha maelezo kisha tukapewa PF3 ili akatibiwe, askari mmoja alitupeleka hospitalini na gari yake binafsi. Baada ya hapo ilitolewa RB, Dada na Baba wote walikamatwa na kufikishwa kituoni. Wote walikua na kesi, haikua ni ya mtu mmoja tena. Polisi waliwasiliana na ndugu wengine kwaajili ya kumchukua Jack na kukaa na wale watoto wengine kwani wote hawakupewa dhamana. Mimi niliondoka lakini nilikua naenda Hospitalini kumuangalia Jack mara kwa mara. Alilazwa kupatiwa matibabu kwa muda wa wiki moja hivi, Mama yake alikuja na baadaye kukabidhiwa mtoto wake. Baba na Dada walikaa mahabusu kwa wiki moja na kutoka kwa dhamana lakini cha kushangaza hawakupelekwa mahakamani. Sijui nini kilitokea lakini binafsi naamini walitoa pesa nyingi kwani Baba Jack alikua na pesa na kacheo flani. Kesi iliisha chinichini na mimi sikuweza kufuatilia, baada tu ya Jack kurudi na kukabidhiwa kwa Mama yake kwangu hilo lilitosha hayo mengine yalikua hayanihusu. Hela yenyewe ya kula ilikua ni shida nisingeweza kufuatilia maisha ya wengine. Sasa hivi imepita kama miaka miwili hivi tangu hili tukio litokee, nipo hapahapa Dar lakini nimehama mtaa. Sifanyi tena kazi za ndani, nimefungua Genge langu ambalo nauza mbogamboga na matunda. Bado nawasiliana na Jack kupitia Mama yake na anaendelea vizuri, wanaishi maisha ya kawaida sana lakini yenye furaha. Katika kazi yangu hii ya kuuza Genge wateja wangu wengi ni wadada wakazi ‘House Girl’ mengi wanayokutana nayo katika nyumba za watu ni kubwa. Kwa wa mama ambao ndiyo mabosi wetu kumbukeni hata sisi ni wanadamu kama nyinyi. ***MWISHO MAMA KWANI BABA YETU NDIYO HUYU HUYU AU SISI NI MAYATIMA? Baba yao ndiyo alikua na kila kitu, mali zote zilikua za kwao lakini kila akisafiri walikua wakiishi kama mashetani, Shangazi zao na Baba zao wadogo waliungana kuwachukia, Mama yao alikua akinyanyaswa na kutukanwa. Kila siku walimuambia yeye ni mzigo na hawezi kuchukua mali za Kaka yao. Bibi yao ambaye alitegemewa kuwa upande wao naye walimjaza maneno. Walimuambia huyu mwanamke kama Kaka akimuacha watagawana mali na Kaka akifa basi atachukua mali zote. Kilichopo hapa ni kuhakikisha Kaka hawi na kitu chochote cha yeye kuchukua…. JE UNATAKA KUJUA KISA HIKI KINAHUSU NINI…Kama kisa kilichopita kilikutoa machozi hiki kitakupigisha mayowe… Lakini nacho kimetokea niseme kinaendelea kutokea, unaweza kuwa na mali nyingi na wanao wakaishi kama mashetani hata kabla hujafa. Kama unataka kuwa wa kwanza kukisoma basi hakikisha umelike ukurasa ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: