Home → ushauri
→ NIKIFANYA MAPENZI NACHUBUKA NA KUTOKWA NA DAMU NYINGI KAMA HEDHI

Mimi ni mwanamke wa miaka 32. Ninatatizo ambalo nimeshindwa kupata tiba yake hata bada ya kwenda kumuona Daktari. Mimi na mpenzi wangu tumekuwa pamoja kwa muda wa miaka miwili.
Mwanzo tulikuwa tukitumia Condom tunapofanya mapenzi lakini mimi nilikuwa napatwa na maumivu makali sana na wakati mwingine kutokwa na damu kama vile niko kwenye siku zangu za Hedhi.
Baada ya muda nikaja kugundua kuwa nilikuwa nachanika kidogo kidogo ukeni, basi tukakubaliana kuacha kutumia Condoms. Pamoja na kuacha kutumia Condom bado hali hiyo iliendelea kila ninapofanya mapenzi na Boyfriend wangu.
Nilipokwenda kwa Daktari, nilishauriwa niwe nabana sehemu zangu za siri kama vile navuta pumzi, nikajaribu kufuata ushauri huo lakini wapi! Sasa nimeanza kupatwa na mawazo je kuchanika huku chini kunaweza kunisababishia Cancer, labda sitoweza kushika mimba na kuendelea kuchanika zaidi na zaidi.
Naomba ushauri wenu.
USHAURI
1.Inawezekana mwanamume wako hauju kula, anatumia mwili wako kupiga punyeto(MASTABATORY SEX)!!! Jaribu kuongea naye ajifunze kula kutokana na mahitaji ya mwili wako!
2. Yawezekana hupati maandalizi ya kutosha na kusababisha uke wako kuwa mkavu, kiasi kwamba mume wako au mpenzi wako huyo anapofanya mapenzi na wewe anatumia nguvu nyingi kuingiza uume na kusabisha michubuko, na damu kutoka,
3.Jaribu kuhakikisha kuwa unakuwa katika mudi ya kufanya ngono ili uke uwe na maji maji ya kutosha ikishindakana jaribu kutumumia vilainishi ya uke then jaribu uone kama utatokwa damu
4.Pia yawezekana cervix yako iko jirani kiasi kwamba mumeo anapofanya mapenzi na wewe anaigusa na kusababisha damu kuvuja na machubuko kwenye cervix.
Nenda kwa daktari bingwa wa magojwa ya wanawake na sio alie kushauri uwe unabana uke huyo si dhani kama ana elimu husika katika suala hilo.
NIKIFANYA MAPENZI NACHUBUKA NA KUTOKWA NA DAMU NYINGI KAMA HEDHI  Mimi ni mwanamke wa miaka 32. Ninatatizo ambalo nimeshindwa kupata tiba yake hata bada ya kwenda kumuona Daktari. Mimi na mpenzi wangu tumekuwa pamoja kwa muda wa miaka miwili. Mwanzo tulikuwa tukitumia Condom tunapofanya mapenzi lakini mimi nilikuwa napatwa na maumivu makali sana na wakati mwingine kutokwa na damu kama vile niko kwenye siku zangu za Hedhi. Baada ya muda nikaja kugundua kuwa nilikuwa nachanika kidogo kidogo ukeni, basi tukakubaliana kuacha kutumia Condoms. Pamoja na kuacha kutumia Condom bado hali hiyo iliendelea kila ninapofanya mapenzi na Boyfriend wangu. Nilipokwenda kwa Daktari, nilishauriwa niwe nabana sehemu zangu za siri kama vile navuta pumzi, nikajaribu kufuata ushauri huo lakini wapi! Sasa nimeanza kupatwa na mawazo je kuchanika huku chini kunaweza kunisababishia Cancer, labda sitoweza kushika mimba na kuendelea kuchanika zaidi na zaidi. Naomba ushauri wenu. USHAURI 1.Inawezekana mwanamume wako hauju kula, anatumia mwili wako kupiga punyeto(MASTABATORY SEX)!!! Jaribu kuongea naye ajifunze kula kutokana na mahitaji ya mwili wako! 2. Yawezekana hupati maandalizi ya kutosha na kusababisha uke wako kuwa mkavu, kiasi kwamba mume wako au mpenzi wako huyo anapofanya mapenzi na wewe anatumia nguvu nyingi kuingiza uume na kusabisha michubuko, na damu kutoka, 3.Jaribu kuhakikisha kuwa unakuwa katika mudi ya kufanya ngono ili uke uwe na maji maji ya kutosha ikishindakana jaribu kutumumia vilainishi ya uke then jaribu uone kama utatokwa damu 4.Pia yawezekana cervix yako iko jirani kiasi kwamba mumeo anapofanya mapenzi na wewe anaigusa na kusababisha damu kuvuja na machubuko kwenye cervix. Nenda kwa daktari bingwa wa magojwa ya wanawake na sio alie kushauri uwe unabana uke huyo si dhani kama ana elimu husika katika suala hilo.
Artikel Terkait
HESABU YA KUONGEZA Niwapo hisabatini, Hufikiri akilini, Kuongeza umakini, Jawabu kulibaini. Jawabu hilo halani, Hukaa makinikoni, Linafaa maishani, Hapa hapa duniani. Ingawa jana nyumbani, Siku niliyobaini, Hata leo furahani, Nakuweka pongezini. Kijana huyu nyikani, Akiwa hisabatini, Kanuniye mkononi, Kaifikiri kichwani. Ndipo nilipobaini, Kafika hisabatini, Kasogea nyongezani, Hapa hapa duniani. Kafika hisabatini, Kashikilia kanuni, Kuingia umrini, Kakaa makinikoni. Hesabuye kabaini, Kamjalia Manani, Kaingia furahani, Yamfaa maishani. Nyongezaye umrini, Hapa hapa duniani, Ufurahi maishani, Singie ubazazini. Sivutwe hisabatini, Duara kulibaini, Ukaidai kanuni, Ukokotozi pupani. Sivutwe hisabatini, Maumbo kuyabaini, Kuchora karatasini, Ukafika ushenzini. Hari yako maishani, Tuliza kichwa nyumbani, Makinika ubwabwani, Ukishibishe tumboni. Busara zako kichwani, Ziongeze kwa makini, Ufike makinikoni, Utulie furahani. Nyongezayo umrini, Ikufae maishani, Hapa hapa duniani, Sichenge msikitini. Wasalamu tamkoni, Nalitoa mdomoni, Ukae mshawashani, Vilevile moralini. Sijiweke haramuni, Kulazimisha kanuni, Iliyo hisabatini, Ukae makinikoni. Na kwa kheri tamkoni, Naitoa mdomoni, Naenda zangu nyumbani, Nikae pumzikoni. UJUMBE Shamsa Cyprian ... Read More
Majina Ya Watoto Wa Kiume (26)  Katika tamaduni nyingi, majina ya watoto wa kiume hutokana na majira au matukio ya wakati wanapozaliwa. Kwa mfano, wakati mmoja, mwanamke Mwethiopia alijifungua mtoto wa kiume. Shangwe yake ikageuka kuwa majonzi alipoona mtoto wake akiwa amelala bila kusonga. Nyanya yake alipomchukua mtoto huyo ili amwoshe, kwa ghafla mtoto akaanza kusonga, kupumua na hata kulia. Hali hii ikawa chanzo cha jina la mtoto na hiyo wazazi wake wakaunganisha jina muujiza na neno linguine la Kiamhara na kumwita mvulana huyo Muujiza Umefanyika. Nchini Burundi, majina memgin yalitokana na wakati wa vita vilivyokuwemo mwanzo wa miaka ya tisini. Mtoto aliyezaliwa huku mzazi akijifichakutokana na machambulizi angepatiwa jina kama Manirakiza amabalo maana yake ni’Mungu Ndiye Anayeokoa’. Majina mengine ya wakati ule ni kama Twagirimana na Mwana wa Imana ambayo pia humaanisha mwana wa Mungu au mtu aliyeponea vita kwa muujiza wa Mungu. Desturi hii ya majina ya watoto wa kiume imeenea kote ulimwenguni ambapo kuna majina mengi yaliyo na maana ya nyakati kam wakati wa vita, njaa, shjrehe, makumbusho au tukio amabalo watu hupenda kukumbuka kwa kuwapa watoto majina. Kuna majina kadhaa amabyo ni mashuhuri sana ulimwenguni ;Noah, Liam, Mason, Jacob, William, Ethan, Michael, Alexander, James, Daniel na mengine. MAANA MAJINA TUKIZINGATIA HERUFI YA JINA LA KWANZA (KIUME) HERUFI A Watoto wenye jina linaloanza kwa herufi hii hupenda mambo makubwa,hujiamini sana na huwa na uwezo wa kutimiza malengo yao. Ni watoto wenye tahadhari,wachangamfu na hupenda matukio. Kwa kawaida hupenda kuheshimiwa,hupenda mamlaka,na ana kiburi,watoto wapenda hasira.Kidesturi herufi hii huwakilisha nyota ya punda. HERUFI B Mwenye jina linaloanziana na herufi hii ni watoto wakarimu,waaminifu na hupenda kazi sana. Ni wajasiri, shujaa na wakatili katika vita au popote pale anapotaka kulinda vilivyo katika himaya yake.Herufi hii huwakilisha nyota yangombe. HERUFI C Mwenye jina linaloanzia na herufi hii ni motto wa kubadilikana,ni washindani na hupenda kupigania malengo yao wanayopenda.Ni watu wabunifu na wanapenda mawasiliano,herufi hii huwakilisha nyota ya mapacha. HERUFI D Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni anayependa usawa,biashara ni watu wanaopenda kuamrisha na mwenye kupenda usafi.Ni wajeuri na wenye msimamo. Herufi hii huwakilisha nyota ya kaa. HERUFI E Mwenye jina linaloanza na herufi ni mtu mwenye roho nzuri,mwenye mapenzi na huruma,mwenye kupenda uhuru katika mapenzi na mchangamfu. Ubaya wake ni mtu asiyetegemewa na ni kigeugeu.Herufi hii huwakilishwa na nyota ya samba. HERUFI F Mwenye jina linaloanza na herufi hii n mtu mwenye mapenzi,huruma,roho nzuri na ana uwezo wa kuwafariji watu,ni mtetezi wa watu na mwenye huzuni lakini ni mzito wa kufanya maamuzi.Herufi hii huwakilisha nyota ya mashuke. HERUFI G Mwenye jina linaloanzia na herufi hii ni mtu mwenye imani ya kidini na nguvu za kiroho,ana kipaji cha kubuni na uwezo wa kutatua matatizo ya watu. Ni mtu mwenye hisia kali,msomi,mpweke na mkaidi wa kukubali ushauri kutoka kwa watu.Herufi hii huwakilisha nyota ya mizani. HERUFI H Mwemye jina linaloanzia na herufi hii ni mtoto mwenye ubunifu na nguvu katika biashara,hupata faida kubwa katika anayopenda kutokana na bidii, ni mwenye mawazo mengi,mchoyo na mbinafsi.Herufi hii huwakilisha nge. HERUFI I Mwenye jina inayoanzia na herufi hii ni mtoto mwenye kupenda sharia,ana huruma na utu mzuri.Wakati mwingi ni mtoto mwenye kujiamini sana na mwenye hasira za haraka. Herufi hii huwakilisha nyota yam shale. HERUFI J Mwenye jina inayoanzia na herufi hii ni mtoto mwenye matamanio,mkweli,mkarimu na mwerevu.Huwa asiyekubali kushindwa na hupata mafanikio makubwa,wakati mwingine anakuwa ni mtoto mvivu na anayekosa mwelekeo. Herufi hii huwakilisha nyota ya mbuzi. HERUFI K Mwenye jina linaloanza ha herufi hii ni mtoto mjeuri,mwenye msimamo thabiti,mpenda umashuhuri na mwenye uwezo wa kushawishi na kuamsha hisia za watu, ana uwezo wa utambuzi ambao watu wengi hawana,ni mtoto asiyeridhika. Herufi hii huwakilisha nyota ya ndoo. HERUFI L Mwenye jina linaloanza ha herufi hii ni mtoto wa vitendo,mwenye hisani na aliyejipanga vizuri kimaisha,hupatwa na misiba mara kwa mara.Herufi hii huwakilisha nyota ya samaki. HERUFI M Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mwenye kujiamini sana,mchapakazi na hupata mafanikio,ni mropokaji,mwenye haraka na mwepesi kukasirika. Herufi hii huwakilisha nyota ya punda. HERUFI N Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mbunifu, mwenye hisia kali,hupenda kuwasiliana lakini ana wivu sana.Herufi hii huwakilisha nyota ya ngombe. HERUFI O Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mwenye subira,mvumilivu,na mwenye bidii ya kusoma.Ni mtoto mwenye kupenda kutumikia jamii na mwenye uwezo mkubwa wa kudhibiti hisia.Herufi hii huwakilisha nyota ya mapacha. HERUFI P Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mwenye uwezo wa kuamuru na ana hekima kubwa.Ana nguvu za kiroho lakini anapenda sana kujitumbukiza kwenye mambo ya watu. Herufi hii huwakilisha nyota ya kaa. HERUFI Q Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtotto mwenye kupenda mambo ya asili,ni watu wasioelezeka,wako na uwezo wa kuonyesha vitu visivyojulikana hata hivyo ni mtu aliyepooza sana.Herufi hii huwakilisha nyota ya samba. HERUFI R Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mtulivu,mwenye huruma lakini mwenye hasira za haraka.Muda mwingi yeye ni mpenda amani. Herufi hii huwakilisha nyota ya mashuke. HERUFI S Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mwenye mvuto kali wa kuleta utajiri,ni mtoto mwenye maamuzi ya ghafla na hupenda mageuzi makubwa. Herufi hii huwakilisha nyota ya mizani. HERUFI T Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mwenye kupenda ushauri wa kiroho,anatumia nguvu za ziada kusaidia watu na hupata mafanikio baada ya muda mrefu, ni watoto wenye hisia kali na wepesi sana kushawishika.Herufi hii huwakilisha nyota ya nge. HERUFI U Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mwenye bahati kwa ujumla,anapenda uhuru katika mapenzi,ni mbinafsi,mwenye tama na anayekosa maamuzi. Herufi hii huwakilisha nyota yam shale. HERUFI V Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mchapakazi,mwenye bidii asiye choka lakini ni watu wasiotabirika. Herufi hii huwakilisha nyota ya mbuzi. HERUFI W Mwemye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mwenye mawazo sana,mchangamfu sana,mwenye uwezo wa kutambua watu wabaya na wema, ni wenye tama na hufanya mambo hatari sana.Herufi hii huwakilisha nyota ya ndoo. HERUFI X Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto asiyependa kuwekewa vizuizi hasa katika anasa na ni rahisi kwake kujiingiza kwenye uzinzi na kujitoa uaminifu. Herufi hii huwakilisha nyota ya punda. HERUFI Y Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mpenda uhuru na hapendi kupingwa katika jambo lolote,ni watoto wanaokosa uamuzi na husababisha kupoteza bahati katika maisha. Herufi hii huwakilisha nyota ya punda. HERUFI Z Mwenye jina linaloanza na herufi hii ni mtoto mwenye kupenda matumaini na amani,ni wenye msimamo mkali japo ni wenye kukubali ushauri . Herufi hii huwakiisha nyota ya ngombe. ... Read More
UNAJUA KUMPAGAWISHA MPENZI WAKO????  Kama inavyoeleweka, mapenzi ni sehemu muhimu ya afya ya binadamu. So, katika peruzi zangu, nikakutana na hili somo la "Tantric Sex." Kama inavyoelewaka, mapenzi ni sehemu muhimu ya afya ya binadamu. So, katika peruzi zangu, nikakutana na hili somo la “Tantric Sex.” As if hii duinia, especially hii century haiko overloaded na information kuhusu mambo ya mapenzi, jinsi ya kufanya mapenzi and whats hot in the bedroom, whats in and whats not. So, lately nimeona a lot of tzmoms readers wamekuwa wakitembelea sana na kusoma page ya “mapenzi baada ya ujauzito” na “kufanyamapenzi wakati wa ujauzito.” And I thought well, writing about Tantric Sex will be nyongeza kwa kila mmoja, aliye mama na mbaye bado damu inachemka katika mambo ya mapenzi. Anyhu, kama “SEX/MAPENZI” yangekuwa yanaweza kuyu-nite the world/countries/makabila/people I think hii fani ingeshinda. Well, so kama umeshawahi kujifungua ama kama wewe ni mama, you definitely understand ni jinsi gani ni vigumu kuwa upbeat kuhusu mapenzi ama kumfurahisha mumeo/mpenzio everyday. Well, once in a while maybe but not everyday. Ila kama we ni mdada/binti ambaye hujazaa bado well, damu yako bado inachemka so energy bado ipo nyingi ya kukurupushana na mpenzio. Having said that, si maanishi mtu ukishazaa ndo fani ya kuenjoy mapenzi imekwisha but nguvu zinapungua for sure however, kuna vitu vingi tuu ambavyo vinaweza kusaidia kuleta nguvu ya kutaka kukurupushana chumbani lol. Kukosa nguvu/energy to wanna work it all the time its not because mwanamke ni mvivu but hutokana na kuwa na mambo mengi sana ya kutend nyumbani i.e. kuhakikisha watoto wako taken care of, labda kazini pia unahitajika, etc una kuta hupati muda wa kujifurahisha mwenyewe ama na mpenzi wako. Therefore, mara nyingi before you know mupenzi anaanza kulalamika or hata mwanamke mwenyewe unaweza kufeel like you are not doing enough so mambo ndo hivyo yanaanza kwenda south chumbani. Hivyo basi, lets dig in tuone Tantric Sex inatoa msaada wa aina gani ili kurevamp mapenzi. Kwanza kabisa, FYI tantric sex can be weird at the beginning ila nitajitahidi kutoingia so indepth ili kusave miyoyo ya watu wengine. Kwamaana hii ni soft porn “according to me.” Lol. so usishtuke ama kushangaa sana. Well, anythign “sex” can be unconfortable anyways. Okay, so, kwanza kabisa, with Tantric Sex, mtu na mpenziwe wanatakiwa kuwa; SPIRITUALLY CONNECTED (usishtuke sio kidini lol).. Hii inamaainisha kwamba wewe na patner wako kwa pamoja mnajua mnataka nini emotionally and physically. Kwa kufanya hivi inasaidia kuwafanya kwa pamoja kuwa “FREE” na kuondoa wasiwasi wa labda mwenzangu atanijudge kwamba labda mimi ni malaya ama fuska etc. In other words hii process inaitwa “Dropping the Veil, between “Self” and “Other/patner.” THE ENVIRONMENT/mazingira. Wakati mnapractice tantric sex of course, just like when you are in the bedroom unaweza ukavaa lingerie/kuo za ndani zinazovutia or “kuwa kama mlivyotoka tumboni mwa mama zenu” (you know what i mean). Tatu, wapenzi wanaanza kupapasana lol, but in a way kwamba you are feeling the energy of the other person. Na hii energy unaweza kuifeel kwasababu mko free hamna anayemjudge mwingine/there are no worries. You are just in your own created world. Nne, wakati wa kufeel energy ya mwingine lazima wapenzi wawe wana pumua heavely yaani just feeling every move made but the other person mpaka mnapofikia mahali were you are breathing so hard and you are feeling each other. then you start kissing the lips, and then deeper for minutes even hours. Then mengineyo yanaweza kuendelea. So, all this time kumbuka its not about going straight into sex with your partner rather its about getting high by touching and feeling connected with each other. hivyo basi, once in a while take that time and revamp your intimacy, dress good, feel sexy and heey have fun!!. By 🅱 ... Read More
Jinsi ya kumtongoza mwanamke kwa njia 10 muhimu  Mwanamke ni kiumbe anayependa kuonyeshwa mapenzi kila wakati. Kumtongoza mwanamke kunaweza kuwa kazi ngumu sana usipozingatia mambo kadhaa muhimu. Ukitaka kuweza kumtongoza mwanamke lazima ujue anachotaka yeye. Waweza kushangaa kwamba wanachotaka wanawake ni vitu vidogo ambavyo waweza timiza ili kuweza kumfanya akukubali hata kuzungumza na wewe. Waweza kumtongoza mwanamke ukizingatia mambo yafuatayo Msikilize mwanamke unayemtongoza Wanawake hupenda mtu ambaye anawasikiliza kwa kila jambo wanachosema. Ni muhimu unapopatana na mwanamke sharti uwe makini na anacho simulia. Kuwa mtu ambaye anauliza maswali na anaye taka kujua zaidi juu ya huyu mwanamke. Muulize kazi anayofanya, anakoishi, na mwonyeshe kwamba unamsikiliza kwa kuuliza swali unapotaka ufafanuzi. Mwanamke huskia ako huru kwa mwanamme ambaye anamsikiliza kwa maana hii huonyesha mwanamume anamdhamini huyo mwanamke. Kwa kumwonyesha kwamba wewe una nia ya kujua mahitaji yake, kwa matendo yako, si maneno yako, kutakusaidia kumwonyesha kwamba wewe ni mtu anayeweza kuwa naye maishani mwake. Kuweka kipaumbele mahitaji yake na kumsikiza kutakusaidia kwa kumtongoza mwanamke huyo. Mwanamke hupenda mtu mwenye kujiamini Unapomwongelesha mwanamke lazima uwe mtu mwenye kujiamini. Ujasiri na kujiamini ni kitengo kikubwa kinachofafanua mwanamume. Unapomwongelesha mwanamke lazimi uonyeshe ujasiri mbele yake. Kama Warren Farrell, Ph.D., anavyosema “Jambo linalomvutia mwanamke kwa mwanamume ni mwanamume mwenye ujasisiri”. Ujasiri utamvutia mwanamke kwa kujua mwanamume anazungumza na kujibeba kwa ujasiri. Mwanamke hupenda kuwa karibu na mwanamume anayevutia Kuvutia kwa mwanamume huja kwa njia kadhaa. Mwanamke hupenda mwanamume ambaye hachoshi kwa hadithi zake, ni mcheshi, anachangia kwa mazungumzo kati yao na anaye hakikisha kwamba mwanamke anajiskia huru kwa maongezi. Kama mwanamume, hakikisha unatoa mifano inayoendana na maongezi mliyo nayo. Hakikisha mnayoyaongelea yanachangiwa na nyinyi wawili. Mwanamume aliemcheshi na mwenye kumvutia mwanamke kwa anavyoendeleza mazungumzo ndie aliye na nafasi kubwa ya kumpata mwanamke anayetarajia ama aliye na hamu naye. Kumbuka kwamba usiwe ni wewe pekee unayeongea, mwachie pia mwanamke achangie pia. Ukizingatia haya, mwanamke hujiskia yuko huru nawe na anaweza ongelea chochote. Mwanamke hapendi mtu mwenye haraka Haraka hapa ina maana, kwa kutongoza mwanamke lazima uwe mtu mwenye subra sana. Kinachomfanya mtu awe na hamu ya kuwa na mwingine ni matarajio anayopata rohoni. Unapopatana na mwanamke kwa wakati wa kwanza, usimwonyeshe kwa umbele unachotaka, lakini taka kumsikiliza, mjue jina, anachofanya kazini, na mambo mengine kwanza. Kwa kufanya haya mwanamke ataona kwamba unahamu naye na kwamba atajiskia wa maana kwako. Jambo hili litakusaidia sana kwa kutongoza huyo mwanamke. Kitu cha muhimi ni kwanza upate kuwa marafiki na mwanamke yule ili uweze kupata nafasi nzuri ya kumtongoza. Ubinafsi wa kipekee Mwanamke hupenda vitu vya kipekee sio vitu vinavyoigwa kwingine. Usije ukafanya ama ukanena kama mwanamume mwingine ili kumshinda huyo binti. Kuwa na ubinafsi wako, fanya mambo yako kwa kipekee. Kuiga wengine hakutakusaidia kwani mwanamke atakuona kama mtu asiyejiamini. Mwanamke hupenda manamume ambaye ni tofauti na wanaume wengine ambao amewahi kutana nao hapo mwanzo. Ni vizuri kuwa na vitu ambavyo ni vya kipekee kwako. Kama sauti yako, vile wacheka vile wamtizama mwanamke yule, vile wavaa, vile umejipaka manukato mazuri. Upekee huu hukupa nafasi ya mbele kwa mpango wako wa kumtongoza mwanamke yule. Mavazi na usafi Mwanamke hupenda usafi sana. Ukitaka mwanamke aweze kuvutiwa nawe lazima uvae vizuri na uwe safi. Kuvaa vizuri, nguo zinazokufanya upendeze huwa njia moja ya kuvutia wanawake. Pia kuwa makini na usafi. Kuoga vizuri, kujipaka manukato yanayo vutia, kuweka nywele, nguo safi husaidia sana kwa kukupa ujasiri wa kumwendea mwanamke uliye na hamu naye. Sio lazima uvae mavazi ghali, lakini valia kwa kupendeza. Mwanamke hupenda mtu anayejiamini katika alichovalia. Muziki Kwa miaka mingi muziki umejulikana kuwa chombo cha kuonyesha mapenzi ama kama namna ya kumtongoza mwanamke. Mwanamke hupenda kuonyeshwa kwamba ni mtu wa thamani kwa mwanamume. Muziki waweza kukusaidia kuweka mazingira yenye utulivu na yenye riwaya ya mahaba. Kumbuka kumzingatia wakati unaweka muziki ule, jua mbeleni muziki anaopenda na fanya hima kwamba unamtumbuiza na aina hizo kwa kikamilifu. Ukifanya hivyo, mwanamke ataoona kwamba unathamini. Weka muziki wenye utulivu, wenye mahaba na wenye kumsifu mtu wa kike na uzuri wake kwa kumwonyesha mapenzi. Bidii ya kuwa makini kwa mwanamke na kumpa pongezi wakati wowote Mwanamke ni kiumbe anayependa kusifiwa na kupongezwa sana. Kwa mwanamume ni muhimu kwamba kwa kumtongoza mwanamke, kumbuka kila wakati kumpongeza kwa kuvaa kwake, nywele, viatu, anavyong’aa. Ni muhimu kumwonyesha kwamba umefurahia bidii yake ya kuvaa vyema na kuhakikisha anakaa vyema mnapokutana. Mwanamke hujiskia mwenye thamana sana kwa kujua kwamba kuna mwanamume amemwona anakaa sawa. Mwambie wapenda alivyosongwa, anavyotoa busu, anavyocheka, na kila kidogo anachofanya. Utashangaa kwamba yaweza onekana ni mambo madogo lakini huchangia katika kutongoza mwanamke. Mpikie chajio mwanamke unayemtongoza Kama mwanamume hakuna kitu cha muhimu kama kumpikia mwanamke uliye na macho kwake. Mwanamume ajuaye kupika huwa anawavutia wanawake sana. Unaweza kumwalika mwanamke kwako ka chajio. Fanya hima ukajua chakula anachopenda binti unaye mtarajia, ukahakikisha umepika chakula kitamu na kinachovutia kwa kuangalia na harufu tamu. Mwandalie mezani pamoja na kinyuaji. Kuwa umehakikisha kuna mazingira yenye utulivu na pia weka mziki wenye mahaba. Mwanamke hujihisi mwenye thamani sana. Hapa utakuwa umejiongezea pointi kadhaa kwa mpango wako wa kumtongoza binti yule. Zawadi Kila mwanamke hupenda kupata zawadi wakati wowote. Kama mwanamume itakusaidia pakubwa kwa mpango wako wa kumtogoza binti yeyote. Zawadi zaweza kuwa tofauti. Waweza mtumia maua ya waridi kazini, ukakumbuka kumtumia chokoleti wakati wa wapendanao, ukamtumania kahawa asubuhi akiingia kazini. Kwa kufanya vile, mwanamke hujiskia wa dhamana na anayependwa. Wanawake pia hupenda kupelekwa mahali pa zuri ambapo anaweza kujibinjari. Mpeleke densi, mpeleke mahali mkala chajio, mpeleke mbugani kwa wanyama ama kwa safari. Kufanya vile kutakupatia pointi nyingi kwa mtazamo wako wa kumtongoza mwanamke yule. Kama kawaida wanawake na wanaume huwa na hamu ya kujuana na kuishi maisha pamoja. Katika kumtongoza mwanamke lazima kwanza mwanamume afahamu nini mwanamke yule anachopenda. Pia inabidi mwanamume pia kumpa sikio binti yule wakati wowote wanapozungumza na kuuliza mwaswali asipoelewa kitu. Mpe wanamke pongezi wakati wowote mnapopatana, mpe pongezi kwa kusukwa vizuri, kupaka kucha vizuri, kuvaa nguo vizuri, tabasamu lake na anavyocheka. Mara kwa mara mpe zawadi za hapa na pale. La muhimu sana ni mwanamke huvutiwa na mwanamume anaye jiamini. Ukiwa mwanamume ambaye anajiamini, itamfanya mwanamke yule kujiskia huru kuwa karibu nawe na hio itakusaidia katika hali ya kumtongoza. ... Read More
JIFUNZE KUMTAMBUA MTU MWENYE MAPENZI YA DHATI NA WEWE: Unajua unaweza kuwa na mahusiano na mtu unayempenda sana ila yeye hakupendi kama vile umpendavyo lakini anashindwa kukwambia kuwa "sikupendi". Unawakati mzuri sana wa kumtambua mtu ambaye hakupendi na pia kumtambua anayekupenda. Vilevile kukubaliana na hali halisi. Watu wengi hawapendi kutambua kwamba mtu anayempenda yeye hampendi, kwasababu ni maumivu makubwa sana moyoni. Unapokuwa kwenye mahusiano na mtu huyo nae inamuwia vigumu kukwambia "sikupendi" hufanya hivi katika kuzihurumia hisia zako juu yake. MTU AMBAYE HAKUPENDI KWA DHATI: ==> Anapokuwa nawe inamuwia vigumu sana kukwambia neno NAKUPENDA mara kwa mara, utajikuta wewe ndio unakuwa mtumwa kwake kwa kumwambia nakupenda kila mara. Majibu yake baada ya neno hilo, mara nyingi atakwambia asante kwa kunipenda basi, na akikuhurumia sana atakwambia nakupenda pia ili kukuridhisha wewe na moyo wako. ==> Utajikuta una mawazo sana juu yake na kujiuliza "hivi kweli mtu huyu ananipenda?" Utajaribu kumuuliza, "je unanipenda?" Jibu lake kwanza litafikiriwa sana, sababu ya kufanya hivyo ni kwa vile anatambua kwamba hakupendi sasa kukwambia ukweli wa swali lako anahisi utaumia, kwahiyo baada ya swali hilo anaweza kukuuliza swali na wewe "kwani unaonaje?" kwavile unampenda sana utamjibu, "naona kuwa unanipenda" naye atakwambia "basi ndio hivyo". Mara nyingine baada ya wewe kumuuliza swali kuwa je anakupenda kweli, atakujibu "ukweli unaujua ila kwanini unapenda kuniuliza swali hilo kila mara?" kama umeshaingiza dosari juu ya upendo wake utajikuta unamuuliza "ukweli upi?" naye atakujibu "kuwa nakupenda", hapo utajikuta umepata furaha kugundua kuwa anakupenda kumbe mwenzio amekuhurumia tu. ==> Huwa hajali mambo yako unayomwambia, ukimueleza muda huu badae anajifanya kusahau ili tu akupotezee mueleleo. ==> Unapopanga kukutana nae huwa ni mtu asiyeishiwa na sababu za kushindwa kufika, huwa na aibu ya kukutambulisha kwa watu. Unaweza kufika nae mahali akakwambia kuwa "kuna watu wanafahamiana na mama/baba mahali hapa kwahiyo tusiongozane karibu", hapo anaweza yeye akatangulia mbele au kukuacha wewe utangulie. ==> Hufanya tabasamu la kuigiza au kicheko cha kejeli ili wewe uridhike kwamba anafurahishwa na uwepo wako kwake. ===> Wakati mwingine inampasa mtu kujitambua na kumpa uhuru huyo umpendaye aweze kuamua mwenyewe labda kuendelea na wewe au kumfata anayempenda yeye. Cha muhimu ni kuwa using'ang'anie mahusiano ambayo yanayoumiza moyo kwani yanaweza pasua moyo wako kwa mawazo. MTU ANAYEKUPENDA KWA DHATI: ==> Hachoki kukwambia NAKUPENDA, kwani anajisikia raha sana pale atamkapo neno hilo juu yako kwahiyo unaweza ukawa kama wimbo wake kwako. ==> Anajivunia kuwa na wewe na atapenda kukupa sifa nzuri kila mara, yani Hachoki kukusifia. Atakushauri pale unapokosea ili uwe katika njia nzuri. Unaponuna atajua cha kufanya ili wewe ufurahi na kurudi kwenye hali ya kawaida. ==> Hachoki kukuombea mema na kukutakia mafanikio. ==> Atapenda kukueleza ukweli kila mara ili uweze kujenga uaminifu na imani juu yake. ==> Wewe utakuwa ni mtu muhimu sana katika maisha yake, atakuthamini na kukujali. Tatizo lako litakuwa sawa na tatizo lake, atakupa ushauri bila kuchoka. ==> Kabla ya kumuuliza swali kuwa "je unanipenda?" atakuwa ameshakujibu tena kwa hisia nzito kuwa "nakupenda sana mpenzi wangu". ==> Hatokuonea aibu kukutambulisha kwa watu kuwa wewe ndiye mpenzi wake, kwakuwa wewe ndiye furaha yake. ====> Thamani yako ni kubwa sana kwake, anakuona mpya kila siku na hachoki kuvutiwa na wewe. Anakupenda kwa kumaanisha na si kukupenda kimazoea tu. Neno NAKUPENDA litamtoka moyoni na ataridhihirisha kwa kinywa chake. Mtambue mtu huyu kuwa anakupenda kwa dhati. NB: Hakuna aliyekamilika, kila mtu ana kasoro na mapungufu yake. Si vyema kutumia mapungufu ya mwenzio kama fimbo katika mapenzi, cha muhimu ni kumuelimisha na kumuelekeza ili muweze kwenda sambamba. Nadhani baadhi ya maswali ya wadau yatakuwa yamejibiwa na hiyo mada. Kama kuna nyongeza au swali lolote kuhusiana na hiyo mada tuambiane hapa na kupatiana majibu hapa hapa wadau. ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: