Home → simulizi
→ SIMULIZI YA KUSISIMUA... Ndoa Yangu Inanitesa part 4
Kwa ujumla maisha ya ndoa niliyaona machungu kama shubiri na pengine machungu kama mitishamba. Nilishindwa kuelewa ugonjwa huo ulitokea wapi na umesababishwa na nini? Nyumbani kwangu nilipaona kama jehanamu, sikuona raha kuwa nyumbani kwani mke wangu alikuwa ananilalamikia kila siku , kila dakika kuhusu ndoa yetu. Tofauti na ndoa nyingine zikiwa changa, watu huwa wanatamani wapate hata likizo ya miezi kadhaa ili wawe pamoja na wandani wao, hapo nasemea kwa wale wafanyakazi kama mimi.Mimi Sweedy kama mtu mwenye uwezo wa kutunga uongo basi nilijitahidi kumridhisha kwa maneno matamu niliyoamini yangemfariji. Uwongo una mwisho wake kumbuka hapo. Lakini hata hivyo ni mtu gani atasikiliza uwongo kila siku. “Kuumwa kuumwa ni kuumwa gani hukokusikoisha?”.
Nilikuwa natoka kazini saa kumi jioni, lakini cha ajabu nilikuwa nikitafuta sehemu ya kupoteza muda ili mradi nirudi nyumbani usiku. Nikiamini mke wangu atakuwa amelala. Siku zote nilitumia njia hiyo, hata kunywa pombe nikajifunza ilimradi nikwepe kugungulika udhaifu wangu.Si mitishamba wala hospitali za kawaida kote nilienda bado ikawa si kitu.
Siku moja mke wangu aliamua kuelekea kazini kuuliza kuhusu ratiba ya kazi zangu. Alimkuta Mzee Jophu mwenyewe.
“Shikamoo baba” Mke wangu akamsalimu pale alipofungua mlango wa Mzee Jophu.
“Marahabaa mchumba mzuri”Mzee Jophu akaitikia salamu kamavile anamuona mke wangu mtoto mdogo.
Hata hivo Getruda ,mke wangu hakujali aliona ni utani tu kwani anajua dhahiri ni shemeji yake.
“Shemeji nimekuja ninashida”Getruda akasema na kusubiri kitu ambacho angeelezwa. Mzee Jophu alionekana kutingwa na shughuli nyingi pale ofisini.
Aliinua kichwa chake na kumtizama Getruda kwa macho ya huba.
“Shida gani shemeji?”
“Wala usishituke ni shida ndogo tu”Getruda akasema akiweka pete yake ya ndoa vema.
“Shemu sema kama ni pesa. Nikupatia au nimambo ya familia unataka kunieleza?”
“Ndio, ulijua je?”
“Najua maana nyie wanawake mmeumbwa na aibu sana. Jambo dogo unaweza ukaogopa kumueleza mwanaume”
“Nijambo dogo kwa kulitizama lakini kwa undani nijambo kubwa”
“Sawa ulitaka tukalizungumzie faragha kidogo?”
“Hapana shem. Naomba nikueleze hapa hapa”
“Sawa nimekuruhusu. Lakini nilipendelea tutoke tukazungumze nje ya ofisi kwani mambo ambayo haya husiani na ofisi tunayazungumzia nje ya ofisi”
“Naomba nizungumzie hapa , ni kwamba sitatumia hata dakika tatu”
“Ok, sema”
“Naomba unieleze, mume wangu anatoka kazini saa ngapi?”
“Wewe kwani kakuambia anatoka saa ngapi?”Mzee Jophu hakujibu swali kama alivyoulizwa bali nae aliligeuza swali upande wa Mke wangu.
“Anasema saa tano usiku”
“Basi inawezekana, kwani mama unaweza kuniambia, maana ya kazi?”
Mzee Jophu alimuuliza swali kwa mtego wa kasa
“Kazi kama ninavyoifahamu ni kitu au ni shuhuli inayoniletea kipato,”
“Ahaa kumbe unajua, mama nenda nitakuambia, maana yake siku nyingine ukiwa na muda.”
“Lakini bado hujanijibu mume wangu hutoka saa ngapi kazi kwako?”
“Saa kumi jioni?”
“Kaaa!. Saa kumi jioni halafu hufika nyumbani saa sita usiku?”
“Inamaana Sweedy hurudi nyumbani usiku?”Mzee Jophu alimtolea Getruda macho ya mshangao, huku akishika kiuno kana kwamba haamini maneno ya Getruda.
“Ndio shemeji”
“Siamini kabisa. Siku zingine huwa na mruhusu saa tisa na siku za jumamosi anatoka saa sita mchana”Mzee Jophu alizidi kuongezea chumvi.Nia yake ni kuvunja ndoa yangu ili afaidi yeye.Alipania kuvuruga ndoa yangu.Siku jua hata nguvu zangu ya kiume zilipoisha ni kwasababu yake.Yeye ndiye alituma watu ambao walivaa kama Daktari kuja kunipiga sindano ya kuua nguvu ya kiume.
“Shemeji inamaana maneno yako niyakweli kabisa”
“Shem nikudanganye iliiweje?.Sitaki kukuvunjia ndoa yako lakini ukweli mumeo hakupendi. Anasema sana kila siku hapa kazini kwamba mpaka sasa hajawahi kufanya tendo la ndoa na wewe.Eti mke gani wa kutafutiwa na wazazi.Anampango wa kukufanya kijakazi pale nyumbani kwake….”
“Eti nini?.Shemeji naweza kuyaamini maneno yako kwani ni miezi miwili sasa hajanigusa kabisa. Kila siku anasingizia kuchoka na kuumwa.Raha ya ndoa iko wapi shem?.Naomba unipe ushauri nimechoka kuvumilia na mateso haya”
“Usichoke shemeji vumilia tabia itabadilika. Yule bwana anapenda watoto wa shule sana na mshahara wake mwingi huishia huko.Juzi tu kashikwa ugoni na mtoto wa shulwe ambapo alitolea faini laki saba, huwezi kuamini lakini ndivyo ilivyotokea. Mumeo ni mkware kweli…Naomab ausije ukamueleza maneno haya naomba ufanye siri, nitakueleza mengi siwezi kuvumilia ukateseka bure binti wa watu”
“Ahsante sana. Leo atanikoma nyumbani”Getruda aliondoka akiwa na mawazo chungu zima.Machozi yalimlenga lenga machoni.Moyo uliuuma sana. Waliagana na Getruda, lakini moyoni Mzee Jophu alibaki na sononeko la upendo kwa mke wangu, Na aliamini kumpata, kwa jinsi alivyo nitumia Daktari wanipige sindano ya kuuwa nguvu za kiume, aliamini njia hiyo aliyotumia ya kuuwa nguvu za uume,wangu ungeshindika kumpata Mke wangu basi angeniuwa kabisa
“Yaani Sweedy ndivyo alivyo?.Nimemtunzia boma langu iliawe wa kwanza kulibomoa lakini hataki, anapambana na watoto wa shule?.Haipiti hata siku moja haachi kusema naumwa sijui kichomi mara nimechoka kumbe anachoshwa na hao makahaba wa shule?”Getruda alizidi kuwaza njia nzima .Hakuwa anaelewa sehemu alipokuwa alisha pita nyumba yetu.
Ilikuwa siku ya juma mosi siku hii aliyotokea kazini,hakuweza kuzungumza chochote na mimi.Alionekana mwenye ghadhabu kali . Hakutaka hata kunikaribia, alikwenda kujipumzisha kitandani.Macho yake fika yalinijulisha kwamba alikasirika sana. Nami niliogopa kumuuliza kwani nilijua lazima alichukia kutokana na matatizo yangu.Sikuwa nalingine kichwani.Wakati wa kulala ulipofika ,nilitoka sebleni ambako nilikuwa nikitizama mkanda wa dini, na kuelekea chumbani.Nilijawa na wasiwasi kwamba usiku huo kungekuwa na kitimtim kikali, dalili niliiona toka mapema kabisa.Sikuwa na amani na maisha yangu, hofu kubwa ilikuwa kwa mke wangu ambaye hakuwa na raha kila aliponiona.Sasa hasira yake ikawa kubwa pale alipopewa maneno ya uchochezi na tajiri yangu.Nilitembea kwa kunyata ilitu asisikie kwamba naelekea kitandani.Kwa sasa nikajongea na kukifikia kitanda.Nilipandisha mguu wa kushoto kwa hadhari sana asishituke. Pia nilihakikisha kitanda hakichezi, jambo hilo nililifanya kwa makini zaidi.Wakati huu napandisha mguu macho yangu yalitizama usoni kwamba mke wangu angeshituka ama vipi. Nilifanikiwa kupandisha mguu wa kwanza, sasa nikajaribu wa pili kuupandisha kitandani. Laiti ningekuwa na uwezo ningejitafutia kitanda changu.Ukweli ndoa yangu niliiona chungu na iliyojaa mateso makubwa sana. Nilikuwa mtu wa wasiwasi tupu.Kitu kingine, nilijiona nisiye na dhamani duniani, nilitamani nife kuliko kuishi kwa shida lakini wasiwasi wangu ukawa huko ahera nikukimbiliako je? Ni kwema aba ndio nitakimbilia mateso mengine?.Nilizidi kuzama kwenye dimbi la mawazo.
Nikafanikiwa kupanda kitandani bila mkewangu kushituka,nilihisi angeshituka angetaka tendo la ndoa wakati huo huo.Sikutaka kulala zaidi ya kulala macho wazi, nilijua nikishikwa na usingizi ningeweza kukoroma ambapo mke wangu angeamka, kwani nilijijua toka niliwa shuleni kwamba nimkoromaji mkubwa hata mtu nyumba ya jirani angesikia.
Sikulala kabisa, nilihakikisha simgusi hata kwa shuka ambapo angeamka na kunisumbua.Saa kumi na robo nilisikia jooo za jirani zikiwika nikajua kwamba kunakaribia kupambazuka. Nikiwa kitandani nilishuhudia miale ya mwanga ikiingia kupitia dirishani.Nikajua tayari palisha kucha.Mpaka wakati huo mke wangu hajazugumza kitu chochote na mimi.
Ilikuwa siku ya Jumapili,siku ya mapumziko,nilikuwa nyumbani na Mke wangu lakini maongezi yetu yalikuwa juu ya unyumba wetu,si kuhusu maendeleo.
“Hivi mume wangu umenioa ili niwe pambo lako au kama TV unitizame tu au laa!.Naomba unieleze nimevumilia vya kutosha”Getruda alisema kwa hasira baada ya kunitengea chai mezani.
Nilishindwa hata kuokota kikombe nikabaki nimeduwaa. Nikanyamaza kimya, nilishindwa niongee uwongo gani,kwani kila siku nilikuwa muongo wa kupindukia,mara naumwa, mara nimechoka kazini, mara sijisikii,zote hizo zilikuwa njia za kukwepa aibu.
“Sema”Mke wangu alifoka kwa kunihimiza.
“Kwani baada ya ndoa ni haki kunitendea hivi?Kila siku hupandi kitandani mpaka mimi nishikwe na usingizi………”
Nilinyamaza kwa muda dakika tatu, kichwa nikiwa nimekiinamisha kama kondoo, kisha nikameza mate na kulamba mdomo, kila nilipotaka kuongea nilijikuta machozi yakitiririka kwa kasi,nilihisi labda nililogwa na walimwengu,kweli imani ya kishirikina ilitawala ndani ya ubongo.Niliamua kujikaza na kuanza kuongoa uwongo.
“Mke wangu shughuli zangu nzito sana, halafu ni za usiku mno!huwa nachoka nashindwa kufanya tendo la ndoa na wewe”.
“Eti nini? kwa hiyo kuna wengine unaofanya nao?. Si ndio, hao machangu wa shule ndio wanakusababishia unione kama mboga zilizochacha eee!.Eti nashindwa kufanya tendo la ndoa na wewe”.Mke wangu aliongea kwa kufoka huku akibana sauti na pua akiniigiza nilivyo sema.
“Hapana mke wangu” nilimjibu kwa sauti ya kidhaifu iliojaa uwoga na simanzi. Nilikuwa niiingia baa na kunywa, niliporejea nyumbani uliku usiku wa manane nikiwa chakari. Mke wangu hakuweza kugundua mapema, hata mimi mwenyewe sikujua ugonjwa huu niliupata wapi.
“Mume wangu”
“Naam mke wangu”Nilimwitikia nikiwa nimeangalia chini,kwa mbali mapigo ya moyo yalinidunda.
“Eti unasubutu kuniitikia.Wewe mwanaume kweli?”
Sikutegemea maneno hayo.Nikahisi mwili kufa ganzi.Nilijiona ninaye dhalilisha hapa ulimwenguni.
“Unafurahia nikuite mume wangu,sivyo?”
“Ndio”Nikaitikia kwa sauti ambayo hata mimi mwenyewe sikuisikia vizuri.
Nikanyamaza,nilijikuta machozi yakinitoka.Kwa kweli moyo uliniuma lakini sikuwa na lakufanya.
“Sasa unataka nikuite mume wangu wakati huwezi?”
“Getruda siwezi nini?”
“Kwani umenioa ilinikupikie tu?”
“Hapana”Nilijibu kwa hofu.
“Sasa unategemea mimi nitaishi vipi?”Safari hii Getruda alishika kiuno.
“Mke wangu vuta subira,nitapona”
“Kwani unaumwa?”
“Ndio, sin’shakuambia naumwa?”Nilikuwa na kila sababu ya kumnyenyekea.
“Hivi Sweedy unataka kunifanya mtoto.Kwa taarifa yako nimeshajua siri zako.Juzi umeshikwa ugoni na mwanafunzi ukatozwa laki saba.Na nimepata tetesi kwamba unapenda hawa wa kusoma”Getruda alinishikia kibwebwe.
“Huu ni uzushi wa watu wasipenda niwe nawe.Naomba usisikilize maneno ya wafitini”
“Sio wafitini.Niwatu wanaokujua kwa ukaribu tabia yako”
Zogo lilikuwa kubwa ambalo lilichukua masaa sita.Baada ya hapo mke wangu akaondoka kwenda mjini.
Hakuwa na safari bali aliamua kwenda mjini kununua gazeti la Mwanasport, lililoandikwa mwongozo wa kumridhisha mwenzi kiunyumba, na kuliweka kwenye meza makusudi ilinilione.
“Haya nakuuliza umesoma gazeti nililokuwekea kwenye meza?”
“Gazeti lipi mke wangu?” nilimuuliza kwa sauti ya chini.
“Hili hapa” mke wangu alinionyesha huku akinipatia nisome.
“Mwongozo wa njia za kumridhisha mwenzi kiunyumba”
“Aaaaa! Gazeti hili, kipengele hiki nisha soma….” Nilijaribu kuchangamka kijanja, lakini huzuni ilibaki pale pale.
“Uongo” Getruda alinishupalia
“Haki ya Mungu, nimesoma kipengele hicho tena kinasisitiza swala la unyumba, mume amtendee haki mkewe na mkewe amtendee mume haki yake, tena hii hapa….” Nilijaribu kujitetea kwa unafiki.
Nilichukuwa gazeti lile na kupitisha macho juu juu kwa haraka na kumwambia nimesoma ndani vizuri. Nilifahamu sana nia yake haswa ilikuwa ni nini? Nilimtizama mke wangu kwa masikitiko na kumuonea huruma, lakini ningefanya nini ili kumridhisha, nae aridhike japo mara moja.
“Samahani mke wangu siku hizi na choka kwa shughuli nzito si mchana wala usiku, hata nimesahau kufanya mapenzi nawe”
“Hivi wewe unavyosema siku hivi, ina maana toka tufunge ndoa, tumeshafanya chochote na sasa karibu miezi miwili na nusu?”
“Basi ni samehe mke wangu”
“Nikusamehe kwa lipi?. Usinipotezee muda ninachoomba ni haki yangu bwana”
“Naomba unipe muda wa wiki nzima”
“Sitaki, ninacholilia ni haki yangu.Kwani kanisani uliapa kwamba utanitendea hivi. Ulinioa wanini kama hukunipenda, naomba talaka yangu haraka…”
“Umeenda mbali sana mke wangu…”
“Mimi sio mkeo kuanzia sasa. Naomba uelewe. We mwanaume gani?”Getruda alionekana mwenye hasira ,nikaamua kutulia kama niliyenyeshewa na mvua.
Akrabu za saa zilionyesha saa tisa na robo usiku, mke wangu alijawa na fukutiko la moyo lililokuwa zito, japo alikuwa na hasira lakini alijitahidi kuiondoa ili kunitamanisha. Muda mfupi aliingia chumbani na kufuata kabati lake lenye makorokoro yote ambayo yanampendezesha mwanamke kuwa kivutio mumewe au mchumba au mwanaume rijali. Alichukua muda kidogo akijipodoa na kujipara, mafuta sijui lotion, cream, manukato, wanjaa lipshine nk. Hakuishia hapo alivaa sketi fupo, ambayo wanaita kimini kilichoonyesha mapaja yaliyonona, na kibilauzi kifupi, wengi huita “kitopu” chenye kuonyesha kitovu kilichoumbika sawia, usoni alipaka poda kwa mbali na kujipulizia manukato yenye harufu ya mahaba. Mke mwenye sura mufti, nyororo kwa macho ya kuita japo mke wangu alijitahidi kwa vitu vyote hivyo lakini ilikuwa sawa na kupiga kinyago ukwenzi, nilibaki kama zoba na mbege.
Juhudi zote za kujipara manukato, tabasamum nono! Nilibaki kuwa sikuuwona uzuri ule, kumbe ni kwasababu nilikuwa siyawezi. Uzalendo nae ulimshinda, ndipo alipaanza kuuliza.
“Mume wangu urembo wote nilonao bado hunitamani? niambie unanipenda au hunipendi” “Nakupenda”
“Sasa kama unanipenda mbona hunifa…” alizidi kulalama kila siku, kila dakika, kila sekunde.
“Nisamehe mke wangu ongea taratibu jirani watasikia”. Niliongea kwa sauti ya chini nikiwa nimempigia magoti mke wangu, sikupenda jirani watambue udhaifu nilionao.
“Nirahisi kupata msamaha wangu, lakini nataka ufanye ninachokuambia, umenielewa mume wangu” mke wangu alipunguza ukali kidogo na kuanza kupitisha mkono wake wa kushoto akipapasa kifuani mwangu.
“Haya twende tukatizame mkanda wa X kwenye video ya chumbani” mke wangu aliongea kwa kunibembeleza, aliamini yeye kama mwanamke lazima ambembeleze mumewe,amfanyie vile vitu anavyopenda ili penzi likomaa na kufika kileleni.
Tulifika chumbani nilijitupa kitandani kigoigoi, roho ikiniuma “Ugonjwa huo wa kuuwa nguvu za kiume niliupata wapi? Au huyu mke ni jini nini? Mbona nimemuoa na uume wangu kukosa nguvu, kwanini? Mbona jenifer nilimridhisha vya kutosha. Mama mkwe kaniloga nini?. Hataki niwe na mwanae” Alitoa mkanda kwenye droo za kanda kisha akasema “Mkanda huu nimeaununua kwa ajili yako. Najitahidi kila namana kukuvuta jirani nami mpenzi” Getruda aliongea huku akitoa tabasamu nono.
“Halafu baada ya kuangalia nini kiendeleee?” niliongea kwa wasi wasi mkubwa tena kwa kuropoka, nilihisi kuchanganyikiwa.
“Kwani wewe umenioa niwe nani kwako, au nifanye nini. Niambie sio kuropoka maneno yasiona maana” Getruda alizidi kufoka.
“Vitu vingine vinaleta kero, sijui huyu ni mzigo, au nini?” Getruda alijisemea kimoyo moyo.
“Basi yaishe mpenzi, punguza hasira”
“Ooo! Kumbe ulikuwa unataka tujifunze kitu”
“Ndio, ili tujifunze wazungu wanavyoridhishana”. Getruda alipunguza hasira kidogo yote hayo ni kunifanya nisisimke.
“Kaaa! Pamoja nami?” Kwa kweli nilichanganyikiwa kabisa, nilikkuwa nikiropoka maneno yasiona msingi, hata nilivyomjibu aliniona limbukeni.
“Kwani ajabu, ndio nikae nawe!” Getruda alizidi kushikwa na hasira usiku mzima hatuku lala ni kukoromeana, maneno ya lawama na mengine ya kuomba msamaha.
“Nikae na wewe tu?” nilizidi kumyumbisha kwa maneno ya ajabu ilimradi papambazuke niondoke mikononi mwake. Nilitamani pakuche niondoke niende kazini.
“Hukubali eee!, niambie hutaki?”
“Aaaaa! Na kubali kabisa bila hofu” jibu hilo lilimfurahisha Getruda mke wangu aliamini ningefanya mapenzi muda mfupi.
“Basi vizuri, nitashukuru mume wangu, na nitakupa unachotaka, japo sijawahi kufanya ngono lakini nitakuachia ufanye utakavyo taka.” Mara moja alianza kuimba
“Basi mume wangu Sweedy, wewe ni wewe sina mwingine, kama ni kundi la ndege msituni basi wewe ndio chaguo langu, wengine sioni, nakupenda peke yako naomba uangaze pendo letu ling’are giza,…” Alitunga wimbo wa muda mfupi.
Getruda, mke wangu alinifuata kitandani baada ya kuweka mkanda wa mapenzi, alinikumbatiam tukaanza kuviringishana huku na kule. Lakini wasi wasi ulinijaa pale nilipo kumbuka mapenzi na mke wangu, niliamini hakuna chochote kingeendelea zaidi ya kumtesa Getruda. Wala sikuwa tayari ajue udhaifu wangu, nilihofu pindi angejua basi angeomba talaka, hata hivyo siri ingekuwa hadharani, kila kona ya dunia.
Baada ya kuchoka mabusu, alilala kwa chali akiwa ananitizama, kwa hofu nilitizama pembeni, sikuweza kumuangalia usoni.
“Niangalie basi nijue unanipenda” nilipomtizama kwa kujikaza, nilisikia akisema (Ooooohhh! Honey you look at me, without uttering any word”) “Ooooohhh! Mpenzi unanitizama bila kunena neno!” Nilituliza macho uso mwa Getruda, uso ulijaa ubembe. Ingawa nilifahamu shauku ya mke wangu lakini nilishindwa nimfanyie nini ili nionekane kidume na mume hodari, sio sifa ya kuoa tu ndoa Kanisani. Lakini lazima nimburudishe mke wangu hata kwa kumshika shika maungo yake, ili kumtuliza asionekane mwenye sikitiko moyoni.
Hata hivyo mke wangu hakuchoka na vitimbi vyangu, aliendelea kunishika shika, ili kuniondoa uchovu. Aliona muhimu na dawa ni kwenda na mimi bafuni kuoga, tulienda bafuni na kuanza kuoga pamoja, lakini hakuona uume wangu ukisisimka hata kidogo. Hofu ilianza kumuingia hakuamini alivyonihisi aliona ni uchovu tu wa kawaida. Hakuwa na roho ya kukata tamaa, kule bafuni alijitahidi kuushika na kupapasa maungo yangu, sikuonyesha dalili yeyote ile.
Getruda akaniogesha nami nikamuogesha.Tulipomaliza akachukua sabuni na bush la kuogea tukaelekea chumbani tukiwa tumefunga taulo. Getruda alionekana kuwa na hasira kali moyoni.
“Mume wangu naona hunipendi kutoka rohoni, Bali ulilazimishwa na wazazi wako sio hivi hivi ni miezi miwili sasa inatimia toka unioe hutaki kufanya tendo la ndoa. Heshima ya ndoa iko wapi? Naomba unieleze kama hinitaki niondoke au nini kimekusibu?”
Wakati ananielezea machozi yalikuwa yanambubujika, aliamini kulia sio suluhisho, taratibu alifuta machozi kwa lesso, alinisogelea karibu na kunizungushia mikono kiunoni, huku akininong’oneza “Sweedy kuna kitu chochote nisichokuridhisha mume wangu. Naomba unieleze niweze kujirekebisha. “Tafadhali niambie sasa hivi. Nahitaji kujua, nitaishi vipi bila mapenzi yako?”
“Kila kitu unaniridhisha ila ni…ni…nina…ni….” nilikokoteza maneno yaliyochanganyikanana kigugumizi, nilishindwa kutamka vizuri nilihisi homa kali, nilijua ndoa ingeingia dosari.
“Ila una nini?. Sema mbona humaliziii?” alinikaripia kwa sauti.
“Unaumwa?” aliniuliza.
“Aaaa!, hata kidogo,” nilimjibu kwa sauti ya chini,
“Au…..penginenimekuudhi bila mimi kufahamu…., maana mama husema mimi ni mkaidi na sijui namna ya kumtunza mtu, ni kweli?” Getruda alizidi kunidadisi.
“Hapana” niliitikia kwa sauti ya majonzi.
“Oke, hivi ni kusema kwa sababu ya kazi ndio umenisogeza pembeni?”
“Hivyo ni vibaya mke wangu, nakuahidi nitajitahidi kukupa penzi nono!, ambalo litafuta kumbukumbu zote nilizo kukera”
“Kama sivyo, basi naomba unibusu, nijisikie furaha moyoni” mke wangu aliongea huku akinisogelea karibu zaidi.
Nilisita kidogo kisha nikainamisha kichwa na uso kutokeza upande wa midomo yake na kumbus kwa uvivu uvivu (Kigoigoi). Nilipomgusa tu midomo yake, mara alinikumbatia vilivyo, kwa mikono yake na kuning’ang’ania na mabusu ya mfululizo na muda mrefu na hata aliponiachia hilihisi joto lenye uvuguvugu nikilikosa. Mwanzoni nilimbusu kwa wasi wasi na shingo upande, lakini baadae nikaadhiriwa na mabusu motomoto ya Getruda nikajikuta ashiki zikiwa zimesisimua mwili mzima, nilijibu mashambulizi kwa mabusu ya nguvu huku nikihema roho juu juu.
Baada ya mabusu yaliotuweka hali ya mapenzi, kwani ashiki zilimpanda na kutaka penzi wakati huo huo bila kucheleweshwa. Akrabu ya saa ya ukutani ilionyesha saa kumi na moja na nusu, karibu na kupambazuka. Majogoo yalikuwa yakiwika kila kona ya wafugaji wa kuku.
“Mume wangu sikiliza” Getruda aliniambia, usoni macho yalikuwa yamelegea na kurembua rembua.
“Eee! Sema mama watoto” nilikohoa kinafiki na kusema.
“Karibu kunapambazuka. Nataka uondoe mawazo ya biashara, madeni, sijue kazi mawazo yako yote weka kuhusu penzi langu na wewe, naomba uniridhishe kwa penzi motomoto.Kwani siku sitini sasa toka unioe hujafanya tendo la ndoa na mimi. Hivyo leo ni mwisho, usipofanya tendo la ndoa, talaka yangu naomba, siwezi kukaa kama pambo, katuni ndani ya nyumba yako. Sijaja kukupikia hapa tumbo liende mbele, mimi sio kijakazi wako, uelewe leo, mimi ni mkeo tena wa ndoa” Getruda alibadilika ghafla na hakutaka kucheka na mimi, alikua anahitaji haki yake.
“Hayo yote uliyosema nimeyatia akilini ila naomba unipe mu….” Kabla sijamalizia maneno, nilikatishwana sauti ya ukali ya Getruda.
“Nikupe nini?, mbona sikuelewi?”
“Fahamu kwamba ninahitaji kuwa na mtoto . Nataka nami niitwe mama Fulani, si jina langu Getruda” Getruda alizidi kunifokea, nilishindwa kuelewa ninani aliyekuwa ananitesa kiasi hicho.Niliwafikiria wabaya wangu wote akilini sikupata aliyenitendea ushenzi huo.
“Ndio…” niliitikia kwa sauti ndogo na ya huruma hata mimi mwenyewe sikuamini ilitoka kwenye kinywa changu, wasi wasi ulinijaa moyoni, nilihisi kuumbuka niliwalaumu wazazi walionitafutia mke. Laiti ningelijua kuwa nina matatizo hayo nisinge Kubali kuoa.
“Haya nenda ukazime taa basi basi mpenzi” Getruda alizidi kunifanya miguu ilegee na kukosa nguvu ya kutembea, nafsi ilinyauka kama jani la tumbaku lililosubiri kusagwa, jasho la woga lilinichuruzika. Sehemu ya kuzima taa ilikuwa karibu kama hatua tatu lakini niliona umbali wa kilometer ishirini.
Nilijikamua kikakamavu na kuinuka kwenye kitanda, kwa uvivu nikajongea kwenye swichi ya taa. Kilikuwa kitendo cha sekunde tano lakini nilifanya dakika saba.nilipofika kwenye swichi nilizima taa, mwili ulikuwa ukitetemeka sio kwa baridi bali ni hofu juu ya kufanya tendo la mapenzi na Mke wangu.
Nilitamani kumfukuza mke wangu kwa kero nilizopata si usiku wala mchana, lakini nilishindwa nianzie wapi na niishie wapi?. Licha ya kushindwa kumfukuza,niliogopa siri ingefichuka na kila mwanadamu angenitupia jicho la lawama.
Nilibuni haraka haraka mbinu za kuinusuru ndoa yangu,ili Mke wangu asigundue matatizo niliyo nayo,nilirudi kitandani na kijisogeza ukutani mwa kitanda,taratibu niliingiza vidole vya mkono wa kulia kwenye mkono wangu,mwisho wa kinywa karibu na koromeo,na hazikupita sekunde nane,nilitapika mfululizo. Sehemu ile ya ubavu wangu kwenye kitanda.Niliamini kwa kufanya hivyo mke wangu angeanini kuwa mimi ni mgonjwa. Lakini cha ajabu alianza kunivua nguo zangu badala ya kufikiri njia ya kuondoa matapishi kitandani, alianza kunivua suruali. Alichoka na maneno yangu ya kila siku nikilalamika, kuumwa,mara tumbo, kichomi, kutapika, kichwa nk.
Baada ya kunivua nguo, alivua na za kwake pia. “Maji ukiyavulia nguo huna budi kuyaoga”alisema kwa sauti iliojaa hasira na mahaba. Mapigo ya moyo wa Getruda yalianza kwenda kasi na mwili mzima ulisisimka baada ya kunivua nguo zote.
By brayton starpoz
SIMULIZI YA KUSISIMUA... Ndoa Yangu Inanitesa part 4 Kwa ujumla maisha ya ndoa niliyaona machungu kama shubiri na pengine machungu kama mitishamba. Nilishindwa kuelewa ugonjwa huo ulitokea wapi na umesababishwa na nini? Nyumbani kwangu nilipaona kama jehanamu, sikuona raha kuwa nyumbani kwani mke wangu alikuwa ananilalamikia kila siku , kila dakika kuhusu ndoa yetu. Tofauti na ndoa nyingine zikiwa changa, watu huwa wanatamani wapate hata likizo ya miezi kadhaa ili wawe pamoja na wandani wao, hapo nasemea kwa wale wafanyakazi kama mimi.Mimi Sweedy kama mtu mwenye uwezo wa kutunga uongo basi nilijitahidi kumridhisha kwa maneno matamu niliyoamini yangemfariji. Uwongo una mwisho wake kumbuka hapo. Lakini hata hivyo ni mtu gani atasikiliza uwongo kila siku. “Kuumwa kuumwa ni kuumwa gani hukokusikoisha?”. Nilikuwa natoka kazini saa kumi jioni, lakini cha ajabu nilikuwa nikitafuta sehemu ya kupoteza muda ili mradi nirudi nyumbani usiku. Nikiamini mke wangu atakuwa amelala. Siku zote nilitumia njia hiyo, hata kunywa pombe nikajifunza ilimradi nikwepe kugungulika udhaifu wangu.Si mitishamba wala hospitali za kawaida kote nilienda bado ikawa si kitu. Siku moja mke wangu aliamua kuelekea kazini kuuliza kuhusu ratiba ya kazi zangu. Alimkuta Mzee Jophu mwenyewe. “Shikamoo baba” Mke wangu akamsalimu pale alipofungua mlango wa Mzee Jophu. “Marahabaa mchumba mzuri”Mzee Jophu akaitikia salamu kamavile anamuona mke wangu mtoto mdogo. Hata hivo Getruda ,mke wangu hakujali aliona ni utani tu kwani anajua dhahiri ni shemeji yake. “Shemeji nimekuja ninashida”Getruda akasema na kusubiri kitu ambacho angeelezwa. Mzee Jophu alionekana kutingwa na shughuli nyingi pale ofisini. Aliinua kichwa chake na kumtizama Getruda kwa macho ya huba. “Shida gani shemeji?” “Wala usishituke ni shida ndogo tu”Getruda akasema akiweka pete yake ya ndoa vema. “Shemu sema kama ni pesa. Nikupatia au nimambo ya familia unataka kunieleza?” “Ndio, ulijua je?” “Najua maana nyie wanawake mmeumbwa na aibu sana. Jambo dogo unaweza ukaogopa kumueleza mwanaume” “Nijambo dogo kwa kulitizama lakini kwa undani nijambo kubwa” “Sawa ulitaka tukalizungumzie faragha kidogo?” “Hapana shem. Naomba nikueleze hapa hapa” “Sawa nimekuruhusu. Lakini nilipendelea tutoke tukazungumze nje ya ofisi kwani mambo ambayo haya husiani na ofisi tunayazungumzia nje ya ofisi” “Naomba nizungumzie hapa , ni kwamba sitatumia hata dakika tatu” “Ok, sema” “Naomba unieleze, mume wangu anatoka kazini saa ngapi?” “Wewe kwani kakuambia anatoka saa ngapi?”Mzee Jophu hakujibu swali kama alivyoulizwa bali nae aliligeuza swali upande wa Mke wangu. “Anasema saa tano usiku” “Basi inawezekana, kwani mama unaweza kuniambia, maana ya kazi?” Mzee Jophu alimuuliza swali kwa mtego wa kasa “Kazi kama ninavyoifahamu ni kitu au ni shuhuli inayoniletea kipato,” “Ahaa kumbe unajua, mama nenda nitakuambia, maana yake siku nyingine ukiwa na muda.” “Lakini bado hujanijibu mume wangu hutoka saa ngapi kazi kwako?” “Saa kumi jioni?” “Kaaa!. Saa kumi jioni halafu hufika nyumbani saa sita usiku?” “Inamaana Sweedy hurudi nyumbani usiku?”Mzee Jophu alimtolea Getruda macho ya mshangao, huku akishika kiuno kana kwamba haamini maneno ya Getruda. “Ndio shemeji” “Siamini kabisa. Siku zingine huwa na mruhusu saa tisa na siku za jumamosi anatoka saa sita mchana”Mzee Jophu alizidi kuongezea chumvi.Nia yake ni kuvunja ndoa yangu ili afaidi yeye.Alipania kuvuruga ndoa yangu.Siku jua hata nguvu zangu ya kiume zilipoisha ni kwasababu yake.Yeye ndiye alituma watu ambao walivaa kama Daktari kuja kunipiga sindano ya kuua nguvu ya kiume. “Shemeji inamaana maneno yako niyakweli kabisa” “Shem nikudanganye iliiweje?.Sitaki kukuvunjia ndoa yako lakini ukweli mumeo hakupendi. Anasema sana kila siku hapa kazini kwamba mpaka sasa hajawahi kufanya tendo la ndoa na wewe.Eti mke gani wa kutafutiwa na wazazi.Anampango wa kukufanya kijakazi pale nyumbani kwake….” “Eti nini?.Shemeji naweza kuyaamini maneno yako kwani ni miezi miwili sasa hajanigusa kabisa. Kila siku anasingizia kuchoka na kuumwa.Raha ya ndoa iko wapi shem?.Naomba unipe ushauri nimechoka kuvumilia na mateso haya” “Usichoke shemeji vumilia tabia itabadilika. Yule bwana anapenda watoto wa shule sana na mshahara wake mwingi huishia huko.Juzi tu kashikwa ugoni na mtoto wa shulwe ambapo alitolea faini laki saba, huwezi kuamini lakini ndivyo ilivyotokea. Mumeo ni mkware kweli…Naomab ausije ukamueleza maneno haya naomba ufanye siri, nitakueleza mengi siwezi kuvumilia ukateseka bure binti wa watu” “Ahsante sana. Leo atanikoma nyumbani”Getruda aliondoka akiwa na mawazo chungu zima.Machozi yalimlenga lenga machoni.Moyo uliuuma sana. Waliagana na Getruda, lakini moyoni Mzee Jophu alibaki na sononeko la upendo kwa mke wangu, Na aliamini kumpata, kwa jinsi alivyo nitumia Daktari wanipige sindano ya kuuwa nguvu za kiume, aliamini njia hiyo aliyotumia ya kuuwa nguvu za uume,wangu ungeshindika kumpata Mke wangu basi angeniuwa kabisa “Yaani Sweedy ndivyo alivyo?.Nimemtunzia boma langu iliawe wa kwanza kulibomoa lakini hataki, anapambana na watoto wa shule?.Haipiti hata siku moja haachi kusema naumwa sijui kichomi mara nimechoka kumbe anachoshwa na hao makahaba wa shule?”Getruda alizidi kuwaza njia nzima .Hakuwa anaelewa sehemu alipokuwa alisha pita nyumba yetu. Ilikuwa siku ya juma mosi siku hii aliyotokea kazini,hakuweza kuzungumza chochote na mimi.Alionekana mwenye ghadhabu kali . Hakutaka hata kunikaribia, alikwenda kujipumzisha kitandani.Macho yake fika yalinijulisha kwamba alikasirika sana. Nami niliogopa kumuuliza kwani nilijua lazima alichukia kutokana na matatizo yangu.Sikuwa nalingine kichwani.Wakati wa kulala ulipofika ,nilitoka sebleni ambako nilikuwa nikitizama mkanda wa dini, na kuelekea chumbani.Nilijawa na wasiwasi kwamba usiku huo kungekuwa na kitimtim kikali, dalili niliiona toka mapema kabisa.Sikuwa na amani na maisha yangu, hofu kubwa ilikuwa kwa mke wangu ambaye hakuwa na raha kila aliponiona.Sasa hasira yake ikawa kubwa pale alipopewa maneno ya uchochezi na tajiri yangu.Nilitembea kwa kunyata ilitu asisikie kwamba naelekea kitandani.Kwa sasa nikajongea na kukifikia kitanda.Nilipandisha mguu wa kushoto kwa hadhari sana asishituke. Pia nilihakikisha kitanda hakichezi, jambo hilo nililifanya kwa makini zaidi.Wakati huu napandisha mguu macho yangu yalitizama usoni kwamba mke wangu angeshituka ama vipi. Nilifanikiwa kupandisha mguu wa kwanza, sasa nikajaribu wa pili kuupandisha kitandani. Laiti ningekuwa na uwezo ningejitafutia kitanda changu.Ukweli ndoa yangu niliiona chungu na iliyojaa mateso makubwa sana. Nilikuwa mtu wa wasiwasi tupu.Kitu kingine, nilijiona nisiye na dhamani duniani, nilitamani nife kuliko kuishi kwa shida lakini wasiwasi wangu ukawa huko ahera nikukimbiliako je? Ni kwema aba ndio nitakimbilia mateso mengine?.Nilizidi kuzama kwenye dimbi la mawazo. Nikafanikiwa kupanda kitandani bila mkewangu kushituka,nilihisi angeshituka angetaka tendo la ndoa wakati huo huo.Sikutaka kulala zaidi ya kulala macho wazi, nilijua nikishikwa na usingizi ningeweza kukoroma ambapo mke wangu angeamka, kwani nilijijua toka niliwa shuleni kwamba nimkoromaji mkubwa hata mtu nyumba ya jirani angesikia. Sikulala kabisa, nilihakikisha simgusi hata kwa shuka ambapo angeamka na kunisumbua.Saa kumi na robo nilisikia jooo za jirani zikiwika nikajua kwamba kunakaribia kupambazuka. Nikiwa kitandani nilishuhudia miale ya mwanga ikiingia kupitia dirishani.Nikajua tayari palisha kucha.Mpaka wakati huo mke wangu hajazugumza kitu chochote na mimi. Ilikuwa siku ya Jumapili,siku ya mapumziko,nilikuwa nyumbani na Mke wangu lakini maongezi yetu yalikuwa juu ya unyumba wetu,si kuhusu maendeleo. “Hivi mume wangu umenioa ili niwe pambo lako au kama TV unitizame tu au laa!.Naomba unieleze nimevumilia vya kutosha”Getruda alisema kwa hasira baada ya kunitengea chai mezani. Nilishindwa hata kuokota kikombe nikabaki nimeduwaa. Nikanyamaza kimya, nilishindwa niongee uwongo gani,kwani kila siku nilikuwa muongo wa kupindukia,mara naumwa, mara nimechoka kazini, mara sijisikii,zote hizo zilikuwa njia za kukwepa aibu. “Sema”Mke wangu alifoka kwa kunihimiza. “Kwani baada ya ndoa ni haki kunitendea hivi?Kila siku hupandi kitandani mpaka mimi nishikwe na usingizi………” Nilinyamaza kwa muda dakika tatu, kichwa nikiwa nimekiinamisha kama kondoo, kisha nikameza mate na kulamba mdomo, kila nilipotaka kuongea nilijikuta machozi yakitiririka kwa kasi,nilihisi labda nililogwa na walimwengu,kweli imani ya kishirikina ilitawala ndani ya ubongo.Niliamua kujikaza na kuanza kuongoa uwongo. “Mke wangu shughuli zangu nzito sana, halafu ni za usiku mno!huwa nachoka nashindwa kufanya tendo la ndoa na wewe”. “Eti nini? kwa hiyo kuna wengine unaofanya nao?. Si ndio, hao machangu wa shule ndio wanakusababishia unione kama mboga zilizochacha eee!.Eti nashindwa kufanya tendo la ndoa na wewe”.Mke wangu aliongea kwa kufoka huku akibana sauti na pua akiniigiza nilivyo sema. “Hapana mke wangu” nilimjibu kwa sauti ya kidhaifu iliojaa uwoga na simanzi. Nilikuwa niiingia baa na kunywa, niliporejea nyumbani uliku usiku wa manane nikiwa chakari. Mke wangu hakuweza kugundua mapema, hata mimi mwenyewe sikujua ugonjwa huu niliupata wapi. “Mume wangu” “Naam mke wangu”Nilimwitikia nikiwa nimeangalia chini,kwa mbali mapigo ya moyo yalinidunda. “Eti unasubutu kuniitikia.Wewe mwanaume kweli?” Sikutegemea maneno hayo.Nikahisi mwili kufa ganzi.Nilijiona ninaye dhalilisha hapa ulimwenguni. “Unafurahia nikuite mume wangu,sivyo?” “Ndio”Nikaitikia kwa sauti ambayo hata mimi mwenyewe sikuisikia vizuri. Nikanyamaza,nilijikuta machozi yakinitoka.Kwa kweli moyo uliniuma lakini sikuwa na lakufanya. “Sasa unataka nikuite mume wangu wakati huwezi?” “Getruda siwezi nini?” “Kwani umenioa ilinikupikie tu?” “Hapana”Nilijibu kwa hofu. “Sasa unategemea mimi nitaishi vipi?”Safari hii Getruda alishika kiuno. “Mke wangu vuta subira,nitapona” “Kwani unaumwa?” “Ndio, sin’shakuambia naumwa?”Nilikuwa na kila sababu ya kumnyenyekea. “Hivi Sweedy unataka kunifanya mtoto.Kwa taarifa yako nimeshajua siri zako.Juzi umeshikwa ugoni na mwanafunzi ukatozwa laki saba.Na nimepata tetesi kwamba unapenda hawa wa kusoma”Getruda alinishikia kibwebwe. “Huu ni uzushi wa watu wasipenda niwe nawe.Naomba usisikilize maneno ya wafitini” “Sio wafitini.Niwatu wanaokujua kwa ukaribu tabia yako” Zogo lilikuwa kubwa ambalo lilichukua masaa sita.Baada ya hapo mke wangu akaondoka kwenda mjini. Hakuwa na safari bali aliamua kwenda mjini kununua gazeti la Mwanasport, lililoandikwa mwongozo wa kumridhisha mwenzi kiunyumba, na kuliweka kwenye meza makusudi ilinilione. “Haya nakuuliza umesoma gazeti nililokuwekea kwenye meza?” “Gazeti lipi mke wangu?” nilimuuliza kwa sauti ya chini. “Hili hapa” mke wangu alinionyesha huku akinipatia nisome. “Mwongozo wa njia za kumridhisha mwenzi kiunyumba” “Aaaaa! Gazeti hili, kipengele hiki nisha soma….” Nilijaribu kuchangamka kijanja, lakini huzuni ilibaki pale pale. “Uongo” Getruda alinishupalia “Haki ya Mungu, nimesoma kipengele hicho tena kinasisitiza swala la unyumba, mume amtendee haki mkewe na mkewe amtendee mume haki yake, tena hii hapa….” Nilijaribu kujitetea kwa unafiki. Nilichukuwa gazeti lile na kupitisha macho juu juu kwa haraka na kumwambia nimesoma ndani vizuri. Nilifahamu sana nia yake haswa ilikuwa ni nini? Nilimtizama mke wangu kwa masikitiko na kumuonea huruma, lakini ningefanya nini ili kumridhisha, nae aridhike japo mara moja. “Samahani mke wangu siku hizi na choka kwa shughuli nzito si mchana wala usiku, hata nimesahau kufanya mapenzi nawe” “Hivi wewe unavyosema siku hivi, ina maana toka tufunge ndoa, tumeshafanya chochote na sasa karibu miezi miwili na nusu?” “Basi ni samehe mke wangu” “Nikusamehe kwa lipi?. Usinipotezee muda ninachoomba ni haki yangu bwana” “Naomba unipe muda wa wiki nzima” “Sitaki, ninacholilia ni haki yangu.Kwani kanisani uliapa kwamba utanitendea hivi. Ulinioa wanini kama hukunipenda, naomba talaka yangu haraka…” “Umeenda mbali sana mke wangu…” “Mimi sio mkeo kuanzia sasa. Naomba uelewe. We mwanaume gani?”Getruda alionekana mwenye hasira ,nikaamua kutulia kama niliyenyeshewa na mvua. Akrabu za saa zilionyesha saa tisa na robo usiku, mke wangu alijawa na fukutiko la moyo lililokuwa zito, japo alikuwa na hasira lakini alijitahidi kuiondoa ili kunitamanisha. Muda mfupi aliingia chumbani na kufuata kabati lake lenye makorokoro yote ambayo yanampendezesha mwanamke kuwa kivutio mumewe au mchumba au mwanaume rijali. Alichukua muda kidogo akijipodoa na kujipara, mafuta sijui lotion, cream, manukato, wanjaa lipshine nk. Hakuishia hapo alivaa sketi fupo, ambayo wanaita kimini kilichoonyesha mapaja yaliyonona, na kibilauzi kifupi, wengi huita “kitopu” chenye kuonyesha kitovu kilichoumbika sawia, usoni alipaka poda kwa mbali na kujipulizia manukato yenye harufu ya mahaba. Mke mwenye sura mufti, nyororo kwa macho ya kuita japo mke wangu alijitahidi kwa vitu vyote hivyo lakini ilikuwa sawa na kupiga kinyago ukwenzi, nilibaki kama zoba na mbege. Juhudi zote za kujipara manukato, tabasamum nono! Nilibaki kuwa sikuuwona uzuri ule, kumbe ni kwasababu nilikuwa siyawezi. Uzalendo nae ulimshinda, ndipo alipaanza kuuliza. “Mume wangu urembo wote nilonao bado hunitamani? niambie unanipenda au hunipendi” “Nakupenda” “Sasa kama unanipenda mbona hunifa…” alizidi kulalama kila siku, kila dakika, kila sekunde. “Nisamehe mke wangu ongea taratibu jirani watasikia”. Niliongea kwa sauti ya chini nikiwa nimempigia magoti mke wangu, sikupenda jirani watambue udhaifu nilionao. “Nirahisi kupata msamaha wangu, lakini nataka ufanye ninachokuambia, umenielewa mume wangu” mke wangu alipunguza ukali kidogo na kuanza kupitisha mkono wake wa kushoto akipapasa kifuani mwangu. “Haya twende tukatizame mkanda wa X kwenye video ya chumbani” mke wangu aliongea kwa kunibembeleza, aliamini yeye kama mwanamke lazima ambembeleze mumewe,amfanyie vile vitu anavyopenda ili penzi likomaa na kufika kileleni. Tulifika chumbani nilijitupa kitandani kigoigoi, roho ikiniuma “Ugonjwa huo wa kuuwa nguvu za kiume niliupata wapi? Au huyu mke ni jini nini? Mbona nimemuoa na uume wangu kukosa nguvu, kwanini? Mbona jenifer nilimridhisha vya kutosha. Mama mkwe kaniloga nini?. Hataki niwe na mwanae” Alitoa mkanda kwenye droo za kanda kisha akasema “Mkanda huu nimeaununua kwa ajili yako. Najitahidi kila namana kukuvuta jirani nami mpenzi” Getruda aliongea huku akitoa tabasamu nono. “Halafu baada ya kuangalia nini kiendeleee?” niliongea kwa wasi wasi mkubwa tena kwa kuropoka, nilihisi kuchanganyikiwa. “Kwani wewe umenioa niwe nani kwako, au nifanye nini. Niambie sio kuropoka maneno yasiona maana” Getruda alizidi kufoka. “Vitu vingine vinaleta kero, sijui huyu ni mzigo, au nini?” Getruda alijisemea kimoyo moyo. “Basi yaishe mpenzi, punguza hasira” “Ooo! Kumbe ulikuwa unataka tujifunze kitu” “Ndio, ili tujifunze wazungu wanavyoridhishana”. Getruda alipunguza hasira kidogo yote hayo ni kunifanya nisisimke. “Kaaa! Pamoja nami?” Kwa kweli nilichanganyikiwa kabisa, nilikkuwa nikiropoka maneno yasiona msingi, hata nilivyomjibu aliniona limbukeni. “Kwani ajabu, ndio nikae nawe!” Getruda alizidi kushikwa na hasira usiku mzima hatuku lala ni kukoromeana, maneno ya lawama na mengine ya kuomba msamaha. “Nikae na wewe tu?” nilizidi kumyumbisha kwa maneno ya ajabu ilimradi papambazuke niondoke mikononi mwake. Nilitamani pakuche niondoke niende kazini. “Hukubali eee!, niambie hutaki?” “Aaaaa! Na kubali kabisa bila hofu” jibu hilo lilimfurahisha Getruda mke wangu aliamini ningefanya mapenzi muda mfupi. “Basi vizuri, nitashukuru mume wangu, na nitakupa unachotaka, japo sijawahi kufanya ngono lakini nitakuachia ufanye utakavyo taka.” Mara moja alianza kuimba “Basi mume wangu Sweedy, wewe ni wewe sina mwingine, kama ni kundi la ndege msituni basi wewe ndio chaguo langu, wengine sioni, nakupenda peke yako naomba uangaze pendo letu ling’are giza,…” Alitunga wimbo wa muda mfupi. Getruda, mke wangu alinifuata kitandani baada ya kuweka mkanda wa mapenzi, alinikumbatiam tukaanza kuviringishana huku na kule. Lakini wasi wasi ulinijaa pale nilipo kumbuka mapenzi na mke wangu, niliamini hakuna chochote kingeendelea zaidi ya kumtesa Getruda. Wala sikuwa tayari ajue udhaifu wangu, nilihofu pindi angejua basi angeomba talaka, hata hivyo siri ingekuwa hadharani, kila kona ya dunia. Baada ya kuchoka mabusu, alilala kwa chali akiwa ananitizama, kwa hofu nilitizama pembeni, sikuweza kumuangalia usoni. “Niangalie basi nijue unanipenda” nilipomtizama kwa kujikaza, nilisikia akisema (Ooooohhh! Honey you look at me, without uttering any word”) “Ooooohhh! Mpenzi unanitizama bila kunena neno!” Nilituliza macho uso mwa Getruda, uso ulijaa ubembe. Ingawa nilifahamu shauku ya mke wangu lakini nilishindwa nimfanyie nini ili nionekane kidume na mume hodari, sio sifa ya kuoa tu ndoa Kanisani. Lakini lazima nimburudishe mke wangu hata kwa kumshika shika maungo yake, ili kumtuliza asionekane mwenye sikitiko moyoni. Hata hivyo mke wangu hakuchoka na vitimbi vyangu, aliendelea kunishika shika, ili kuniondoa uchovu. Aliona muhimu na dawa ni kwenda na mimi bafuni kuoga, tulienda bafuni na kuanza kuoga pamoja, lakini hakuona uume wangu ukisisimka hata kidogo. Hofu ilianza kumuingia hakuamini alivyonihisi aliona ni uchovu tu wa kawaida. Hakuwa na roho ya kukata tamaa, kule bafuni alijitahidi kuushika na kupapasa maungo yangu, sikuonyesha dalili yeyote ile. Getruda akaniogesha nami nikamuogesha.Tulipomaliza akachukua sabuni na bush la kuogea tukaelekea chumbani tukiwa tumefunga taulo. Getruda alionekana kuwa na hasira kali moyoni. “Mume wangu naona hunipendi kutoka rohoni, Bali ulilazimishwa na wazazi wako sio hivi hivi ni miezi miwili sasa inatimia toka unioe hutaki kufanya tendo la ndoa. Heshima ya ndoa iko wapi? Naomba unieleze kama hinitaki niondoke au nini kimekusibu?” Wakati ananielezea machozi yalikuwa yanambubujika, aliamini kulia sio suluhisho, taratibu alifuta machozi kwa lesso, alinisogelea karibu na kunizungushia mikono kiunoni, huku akininong’oneza “Sweedy kuna kitu chochote nisichokuridhisha mume wangu. Naomba unieleze niweze kujirekebisha. “Tafadhali niambie sasa hivi. Nahitaji kujua, nitaishi vipi bila mapenzi yako?” “Kila kitu unaniridhisha ila ni…ni…nina…ni….” nilikokoteza maneno yaliyochanganyikanana kigugumizi, nilishindwa kutamka vizuri nilihisi homa kali, nilijua ndoa ingeingia dosari. “Ila una nini?. Sema mbona humaliziii?” alinikaripia kwa sauti. “Unaumwa?” aliniuliza. “Aaaa!, hata kidogo,” nilimjibu kwa sauti ya chini, “Au…..penginenimekuudhi bila mimi kufahamu…., maana mama husema mimi ni mkaidi na sijui namna ya kumtunza mtu, ni kweli?” Getruda alizidi kunidadisi. “Hapana” niliitikia kwa sauti ya majonzi. “Oke, hivi ni kusema kwa sababu ya kazi ndio umenisogeza pembeni?” “Hivyo ni vibaya mke wangu, nakuahidi nitajitahidi kukupa penzi nono!, ambalo litafuta kumbukumbu zote nilizo kukera” “Kama sivyo, basi naomba unibusu, nijisikie furaha moyoni” mke wangu aliongea huku akinisogelea karibu zaidi. Nilisita kidogo kisha nikainamisha kichwa na uso kutokeza upande wa midomo yake na kumbus kwa uvivu uvivu (Kigoigoi). Nilipomgusa tu midomo yake, mara alinikumbatia vilivyo, kwa mikono yake na kuning’ang’ania na mabusu ya mfululizo na muda mrefu na hata aliponiachia hilihisi joto lenye uvuguvugu nikilikosa. Mwanzoni nilimbusu kwa wasi wasi na shingo upande, lakini baadae nikaadhiriwa na mabusu motomoto ya Getruda nikajikuta ashiki zikiwa zimesisimua mwili mzima, nilijibu mashambulizi kwa mabusu ya nguvu huku nikihema roho juu juu. Baada ya mabusu yaliotuweka hali ya mapenzi, kwani ashiki zilimpanda na kutaka penzi wakati huo huo bila kucheleweshwa. Akrabu ya saa ya ukutani ilionyesha saa kumi na moja na nusu, karibu na kupambazuka. Majogoo yalikuwa yakiwika kila kona ya wafugaji wa kuku. “Mume wangu sikiliza” Getruda aliniambia, usoni macho yalikuwa yamelegea na kurembua rembua. “Eee! Sema mama watoto” nilikohoa kinafiki na kusema. “Karibu kunapambazuka. Nataka uondoe mawazo ya biashara, madeni, sijue kazi mawazo yako yote weka kuhusu penzi langu na wewe, naomba uniridhishe kwa penzi motomoto.Kwani siku sitini sasa toka unioe hujafanya tendo la ndoa na mimi. Hivyo leo ni mwisho, usipofanya tendo la ndoa, talaka yangu naomba, siwezi kukaa kama pambo, katuni ndani ya nyumba yako. Sijaja kukupikia hapa tumbo liende mbele, mimi sio kijakazi wako, uelewe leo, mimi ni mkeo tena wa ndoa” Getruda alibadilika ghafla na hakutaka kucheka na mimi, alikua anahitaji haki yake. “Hayo yote uliyosema nimeyatia akilini ila naomba unipe mu….” Kabla sijamalizia maneno, nilikatishwana sauti ya ukali ya Getruda. “Nikupe nini?, mbona sikuelewi?” “Fahamu kwamba ninahitaji kuwa na mtoto . Nataka nami niitwe mama Fulani, si jina langu Getruda” Getruda alizidi kunifokea, nilishindwa kuelewa ninani aliyekuwa ananitesa kiasi hicho.Niliwafikiria wabaya wangu wote akilini sikupata aliyenitendea ushenzi huo. “Ndio…” niliitikia kwa sauti ndogo na ya huruma hata mimi mwenyewe sikuamini ilitoka kwenye kinywa changu, wasi wasi ulinijaa moyoni, nilihisi kuumbuka niliwalaumu wazazi walionitafutia mke. Laiti ningelijua kuwa nina matatizo hayo nisinge Kubali kuoa. “Haya nenda ukazime taa basi basi mpenzi” Getruda alizidi kunifanya miguu ilegee na kukosa nguvu ya kutembea, nafsi ilinyauka kama jani la tumbaku lililosubiri kusagwa, jasho la woga lilinichuruzika. Sehemu ya kuzima taa ilikuwa karibu kama hatua tatu lakini niliona umbali wa kilometer ishirini. Nilijikamua kikakamavu na kuinuka kwenye kitanda, kwa uvivu nikajongea kwenye swichi ya taa. Kilikuwa kitendo cha sekunde tano lakini nilifanya dakika saba.nilipofika kwenye swichi nilizima taa, mwili ulikuwa ukitetemeka sio kwa baridi bali ni hofu juu ya kufanya tendo la mapenzi na Mke wangu. Nilitamani kumfukuza mke wangu kwa kero nilizopata si usiku wala mchana, lakini nilishindwa nianzie wapi na niishie wapi?. Licha ya kushindwa kumfukuza,niliogopa siri ingefichuka na kila mwanadamu angenitupia jicho la lawama. Nilibuni haraka haraka mbinu za kuinusuru ndoa yangu,ili Mke wangu asigundue matatizo niliyo nayo,nilirudi kitandani na kijisogeza ukutani mwa kitanda,taratibu niliingiza vidole vya mkono wa kulia kwenye mkono wangu,mwisho wa kinywa karibu na koromeo,na hazikupita sekunde nane,nilitapika mfululizo. Sehemu ile ya ubavu wangu kwenye kitanda.Niliamini kwa kufanya hivyo mke wangu angeanini kuwa mimi ni mgonjwa. Lakini cha ajabu alianza kunivua nguo zangu badala ya kufikiri njia ya kuondoa matapishi kitandani, alianza kunivua suruali. Alichoka na maneno yangu ya kila siku nikilalamika, kuumwa,mara tumbo, kichomi, kutapika, kichwa nk. Baada ya kunivua nguo, alivua na za kwake pia. “Maji ukiyavulia nguo huna budi kuyaoga”alisema kwa sauti iliojaa hasira na mahaba. Mapigo ya moyo wa Getruda yalianza kwenda kasi na mwili mzima ulisisimka baada ya kunivua nguo zote. By brayton starpoz
Artikel Terkait
Story....... NI WEWE TU PENINA Sehemu ya nane (8) By GIVAN IVAN Phone & whatsapp....... 0769673145 Ilipoishia........ Lakini Sasa watu wale ambao walikuwa ni wakina Zaza hawakujua wanamfuata nani. Wazimu wa wazimu Nolan naye alifungua mlango na kutoka kwenye gari Lake na kuanza kuwafuata wakina Zaza bila kuwa na uoga wowote.* *************Endelea ********* Zaza pamoja na wenzake walishtuka kuona Nolan anashuka kwenye gari na kuona anawafuata bila wasi wasi wowote. Na baada ya sekunde chache Nolan alikuwa mbele yao. "mnataka nini mbona tunapotezeana Muda?" Nolan akawauliza wakina Zaza huku akiwa amesimama mbele yao. "hahahaaaa Nolan kwa siku ya leo huna bahati leo umeingia pabaya." akaongea zaza huku akimsogelea Nolan. "leo hakika tutakufunza adhabu." akaongea zaza na kumshushia Nolan fimbo ya mgongo, lakini kabla fimbo Ile haijamfikia Nolan aliidaka na kuivunja. Kitendo kile kilimshtua Zaza na kumfanya akasirike kwa fimbo yake kuvunjwa. Zaza alimrushia Nolan ngumi ya uso lakini nayo pia ilikingwa vizuri na Nolan. "acha kupoteza Muda wako kupigana na mimi hata mkiwa ishirini bado hamtaniweza." akaongea Nolan kumwambia Zaza. Lakini zaza hakusikia, akachomoa kisu na kutaka kumchoma Nolan cha tumbo, lakini Nolan alimkamata mkono ule wenye kisu Kisha akamtandika ngumi tatu tumboni za haraka haraka na Kisha akauosokota ule mkono wenye kisu na kuuvunja. Zaza alijikuta akipiga kelele kwa maumivu aliyoyapata. Wale vijana wengine kuona mkubwa amevunjwa mkono nao wakachomoa visu vyao na kuanza kumfuata Nolan kwa kasi. Nolan akawaangalia na kuwapigia hesabu za haraka haraka. "wewe nitakupiga teke la tumbo, wewe wa pili nitakupiga ngumi mbili za kichwa alafu wewe wa tatu na wa mwisho nitatukutoboa kwenye paja la mguu na kisu chako mwenyewe." hizo ni hesabu za haraka haraka ambazo Nolan aliwapigia vijana wale. Na wakati huo huo vijana wale walimkaribia Nolan, na kama Nolan alivyowapigia hesabu aliwafanya vile vile na kila mmoja akadondokea upande wake. "nyie ni kina nani na mnataka nini?" Nolan akamuuliza kijana mmoja kati ya wale wanne aliowapiga. "sijui hata sisi ni wakina nani" akajibu kijana yule. "nitakuvunja shingo jibu swali nililokuuliza." Nolan akamuamrisha kijana yule. "si nimesema sijui sisi ni wakina nani." akajibu kijana yule jibu hilo ambalo lilimpelekea apokee ngumi nzito ya uso kutoka kwa Nolan. Lakini kumbe wakati Nolan anamuhoji kijana yule, kulikuwa na mwanamke mmoja ambaye ni dereva wa kina Zaza yeye alibaki kwenye gari na Nolan hakumuona. Mwanamke yule alishuka kwenye gari taratibu akachomoa kisu chake na kuanza kumsogelea Nolan taratibu bila yeye kujua. Mwanamke yule alipofika sehemu ile aliyokuwa Nolan akimuhoji kijana yule alikinyanyua kisu chake juu kwa mikono miwili na kukusanya nguvu Zake zote na kuanza kuhesabu moja mpaka tatu kwa ajili ya kumshushia Nolan kisu kile cha kichwa. Nolan akiwa bado pale chini akimhoji kijana yule ghafla alishangaa kumuona kijana yule akianza kucheka, kumbe kijana yule alimuona yule Mwanamke ambaye ni mwenzao akijiandaa kummaliza Nolan. Lakini kucheka kwa yule kijana kulimfanya Nolan ahisi kitu. Lakini kidogo hivi Nolan aliona kivuli cha mtu pembeni yake, akageuka haraka kuangalia ni nini kipo nyuma, lakini Ile kugeuka Nolan alikutana na kisu kikija kwa kasi kichwani kwake. Nolan alipojaribu kukikwepa kisu alikuwa tayari ameshachelewa, lakini kwa bahati nzuri kisu kile hakikumpata Nolan kichwani, kwani Ile kugeuka nyuma kulimfanya alindishe kichwa kidogo hivyo kisu kile kikampata Nolan bega karibu na shingo. Nolan alisikia uchungu ambao hajawahi kusikia Katika maisha yake. Lakini mwanamke yule alidhamiria kummaliza Nolan, kwani alikichomoa kisu kile kwenye bega la Nolan na kukirudishia tena pale pale na kumfanya Nolan azidi kupiga kelele kwa maumivu aliyoyapata. Mwanamke yule alikichomoa tena kisu kile na kutaka kummaliza Sasa Nolan kwa kumkata shingo. Mwanamke yule alipotaka kumkata Nolan shingo, Nolan alijijaza licha maumivu aliyokuwa nayo alikikamata kisu. Lakini kwa kukimata kisu kile alijikuta akipokea teke Zito kutoka kwa yule yule Mwanamke na kutupwa mbali. Lakini kwa kupigwa teke lile ilikuwa kama vile Nolan ameamshwa kutoka usingizini. Nolan alinyanyuka na kusimama na kumtizama mwanamke yule huku akiapa lazima amuue. "umenipiga Sana hata wewe Sasa umeisha." akaongea Nolan na kuanza kutoka mbio kumfuata yule Mwanamke. Yule Mwanamke naye akatoka mbio na kuanza kumfuata Nolan huku akiwa na kisu chake mkononi. Walipokaribiana yule Mwanamke akaruka juu huku akiwa amekielekeza kisu kichwani kwa Nolan, Nolan kuona vile naye akaruka juu zaidi ya yule Mwanamke na kupita juu kidogo ya kichwa cha Mwanamke yule na kutua nyuma ya Mwanamke yule. Bila kupoteza hata sekunde moja Nolan aligeuka na kuruka juu na kurusha teke Zito ambalo lilimpata sawia kabisa Mwanamke yule la kichwa na kumuweka chini. Nolan hakusubiri yule Mwanamke anyanyuke, akaruka tena juu na kukunja miguu na kutua kwa magoti mgongoni mwa yule Mwanamke yule na kumvunja mgongoni huku wenzake wakishuhudia lakini wasiweze kufanya lolote kwa kuwa nao walikuwa hoi kwa kichapo walichokipata kutoka kwa Nolan. "wewe lazima nikuue umenijeruhi Sana ngombe wewe." Nolan ndio alimwambia Mwanamke yule Kisha akammaliza kwa kumtandika ngumi nzito ya shingo ambayo ilimpandisha ndege ya kuzimu. Baada ya Nolan kummaliza Mwanamke yule naye alijikuta akidondoka chini na kuzimia kutokana damu nyingi iliyomwangika kutoka kwenye mwili wake. Taarifa zilienea kila mahali kwa mauaji yale yaliyotokea sehemu ile huku wengine wakiwa hoi bin taabani. Polisi pamoja na kikosi cha kutoa huduma ya kwanza kilifika pale na bila kupoteza muda, Nolan pamoja na wakina Zaza wakabebwa na kupelekwa hospital.* Mzee Joel akiwa ametulia nyumbani kwake akipata moja baridi moja ya moto, aliweza kupata taarifa Ile ambayo ilimshangaza Sana. "inakuaje wakina Zaza wako hoi na pia Nolan yupo hoi, kuna nini kilitokea?" akajiuliza mzee Joel bila kupata jibu. Huzuni ilianza upya tena kwa Penina baada ya kupata taarifa ya Nolan mtu pekee ambaye alikuwa akimtegemea kwa chochote, kuwa na yeye yuko hoi bin taabani hospitalini. Bila kupoteza Muda Penina aliingia kwenye gari Lake na kuanza safari ya kuelekea Katika hospital aliyolazwa Nolan, Penina alihisi kuchanganyikiwa hasa akifikiria mambo anayotendewa na baba yake, na pia kupotea kwa mpenzi wake Frank. Hali hiyo ilimfanya Penina akose umakini barabarani na akiwa amebakiza mita chache kufika Katika hospital aliyopo Nolan, Penina alijikuta akikosa balance na kupoteza mwelekeo na kutoka nje ya barabara na kwenda kugonga mti uliokuwa pembeni ya barabara Ile. Pale pale Penina alipoteza fahamu baada ya kugonga mti ule, na alipokuja kushtuka alijikuta yupo hospitalini. Taarifa ilimfikia mzee Joel kwamba Penina amepata ajali Muda mchache uliopita. "shit ni bora afe mtu yoyote lakini sio Penina, utajiri wangu upo kwa Penina." akaongea mzee Joel huku akitoka ndani haraka haraka na kuingia kwenye gari na kuanza kuwahi hospitalini kwenda kumuangalia binti yake Penina.* Baada ya kubangaiza huku na kule kwa siku kadhaa hatimaye Frank alifanikiwa kupata pesa ambayo aliihitaji, na bila kupoteza sekunde, dakika wala masaa, moja kwa moja Frank aliianza safari ya kurudi dar es salam huku mawazo yake yote yakiwa kwa Penina tu Mwanamke aliyempenda kwa moyo wake wote. .......... Itaendelea ... Read More
Story - - - - - NI WEWE TU PENINA Sehemu ya pili (2) By GIVAN IVAN Phone & whatsapp___0769673145 Ilipoishia........ Katika bar moja iliyopo maeneo ya sinza kikao kimoja kilikuwa kikiendelea, na huku kilichokuwa kikipangwa Katika kikao kile ni namna ya kulivunja na kuliharibu penzi la Penina na Frank. Mzee Joel ambaye ni baba yake Penina, pamoja na Angel ambaye ni mdogo wake Penina pamoja na vijana wengine watatu wa kiume na mmoja wa kike, ndio waliokuwa wahusika wakuu wa kikao kile. *********ENDELEA ******** "sitaki mwanangu aolewe na yule mlala hoi kwa namna yoyote Ile naomba muyakatishe mpenzi yao, nitawapa pesa yoyote mnayotaka." alisikika mzee Joel akiwaambia vijana wake. "hamna shinda mzee wetu kuanzia Sasa tupo Katika mipango ya kuliharibu penzi hilo usijali mzee wetu." kijana mmoja aliyeitwa zaza ndio alisikika akiwaambia mzee Joel maneno hayo. "nitafurahi Sana kama hili likifanikiwa siwezi kukubali mwanangu aolewe na yule mnuka jasho." mzee Joel bado alizidi kuongea kwa jazba. "baba hata mimi nakuunga mkono Dada hawezi kuolewa na yule mnuka shombo." aliongea Angel naye kumuunga mkono baba yake. "hamna shida mzee Joel tutafanya mnayotaka." akaongea Zaza. "bas Sawa ngoja niwape pesa ya maji ili muweze kuianza kazi Mara moja." akaongea mzee Joel na kutoa pesa kias cha shilingi laki mbili na kumkabidhi Zaza agawane na wenzake. "Asante Sana mzee wetu na kuanzia Sasa sisi tunaianza Kaz." akaongea Zaza huku akipokea pesa zile, na Kisha wakaagana na mzee Joel na kuondoka.* Katika ukumbi mmoja wa starehe mziki wa taratibu ulikuwa ukipigwa kwa utaratibu wa hali juu kabisa, huku watu wawili wanaopendana kupita maelezo wakiwa ndani ya ukumbi huo huku wakiburudika na mziki mwororo uliokuwa ukipigwa Katika ukumbi ule, watu hao ni Penina pamoja na Frank. "Frank nakupenda Sana mpenzi wangu sijui nifanye nini ili ujue ni kwa kiasi gani, nafahamu jinsi baba yangu anavyokuchukia Ila yeye hawezi kuwa chanzo cha mimi kutokukupenda wewe, hakika nakupenda Sana." aliongea Penina maneno hayo akimuambia Frank na kujilaza kifuani mwake. "nafahamu Penina ni kwa kiasi gani unanipenda na pia unatambua ni kwa kias gani mimi nakupenda, napenda nikuahidi tu kuwa NI WEWE TU PENINA hakuna mwingine zaidi yako." Frank naye alimwambia Penina maneno hayo ambayo yalimfanya Penina azidi kutoa tabasamu tamu usoni mwake na kuzidi kumvuruga Frank, ambaye alijiona ni mwanaume mwenye bahati Sana kuwa na msichana mrembo kama Penina. Kama Kuna zile sifa wanaume huzitafuta kwa wanawake bas Penina alikuwa nazo na zingine za ziada. "yaani mpenzi wangu kila nikikuangalia nakuwa na maswali mengi ya kijinga ya kukuuliza kwa jinsi tu ulivyo mzuri." aliongea Frank akimwambia Penina. "hahahaaaa maswali gani hayo mpenzi wangu hebu niulize moja." akaongea Penina na kumtaka Frank amuulize moja. "swali moja ambalo huwa najiuliza kila ninapokuona huwa najiuliza hivi wewe ulizaliwa na mwanadamu au Mungu ndio alikutengeneza mwenyewe alafu akakuleta duniani?" akauliza Frank huku akiwa anamtazama Penina. "hahahaaaa Frank mpenzi wangu mi nimezaliwa na mwanadamu kama wewe." akajibu Penina huku akicheka kwa maneno ya Frank. "najua wewe umezaliwa na mwanadamu kama mimi Ila wewe ni mrembo Sana Sana sanaaa." akaongea Frank huku akizidi kumsifia Penina. Penina naye alifurahi Sana na kuzidi kuwa na furaha zaidi kwa sifa alizokuwa akipewa na Frank. "Asante Sana mpenzi wangu kwa sifa zote ulizonipa ila Kuna kitu nataka nikuambie." akaongea Penina na kumtizama Frank. "kitu gani tena mpenzi wangu?" akahoji Frank huku akiwa ametumbua macho. "mbona umeshtuka hivyo Sasa?" Penina akamuuliza Frank baada ya kumuona ametumbua macho. "lazima nishtuke si unajua tena namna navyokupenda isije ikawa ni kitu kibaya." Frank akamjibu Penina. "usijali mpenzi sio kitu kibaya na nina Imani utafurahia." Penina akamwambia Frank kumtoa hofu. "ok niambie bas ni kitu gani?" akahoji Frank huku akionekana kuwa na haraka ya kutaka kujua. "nataka siku chache zijazo tufunge ndoa alafu tufanye harusi kubwa ili tuwakomeshe maadui zetu ambao hawataki kutuona tukiwa pamoja.." Penina ndio alimwambia Frank ambaye alikuwa kimya kumsikiliza. "kweli mpenzi wangu hata mimi nimeshaliwaza hilo tatizo lipo kwangu, bila Shaka unatambua hali iliyopo Katika familia yetu, hatuna uwezo kipesa hivyo nahitaji muda zaidi kulitimiza hilo Penina." Frank akamwambia Penina huku akiwa amepoteza tabasamu usoni mwake. "Frank mpenzi wangu ondoa Shaka kuhusu hilo mimi nina uwezo wa kulisimamia hilo mwanzo mpaka mwisho, na kuthibitisha hilo hapa nimekuja na funguo nne, moja ni ya duka kubwa la kuuza bidhaa za jumla na moja, mwingine ni wa gari kubwa la kubebea mizigo, mwingine ni wa nyumba mpya niliyowanunulia wazazi wako kama zawadi ya kunizalia mwanaume anayenipenda kwa dhati na mwingine ni wa gari ndogo nililokununulia wewe mpenzi wangu. " alimaliza Penina kumwambia Frank maneno hayo na kumuacha akiwa mdomo wazi. " waooow ni ngumu Sana kuamini ila acha niamini tu, Asante Sana mpenzi wangu." alisema Frank huku akimkumbatia Penina na kumshushia mabusu mfululizo. "usijali mpenzi wangu ila nataka utambue nayafanya yote haya kwasababu nakupenda Sana, lakini pia ni moja wapo ya maandalizi ya harusi yetu." Penina akamwambia Frank huku akiwa amejilaza kifuani mwake. "nashukuru Sana Penina mpenzi wangu kusikia hivyo na mimi nikuahidi kuwa na wewe mpaka mwisho wa uhai wangu hakika ni wewe tu Penina." Frank akamwambia Penina huku akiwa amemkumbatia kwa nguvu. Wakati huo tayari Muda ulikuwa umeenda Sana na tayari ilikuwa ni saa moja usiku, hivyo Frank na Penina waliondoka kurudi nyumbani huku Penina akimuahidi Frank kumkambidhi vitu vyote alivyomwambia siku inayofuata. Penina alimfikisha Frank nyumbani kwake, Frank akashuka kwenye gari na kumuuga mpenzi wake Penina. Kisha Penina akageuza gari na kuondoka. Baada ya Penina kuondoka tu, Frank kabla hajapiga hata hatua moja kuondoka pale, ghafla alishtukia amezungukwa na vijana watatu wa kiume waliokuwa wamevalia miwani nyeusi kila mmoja. Na hata Frank alipowaangalia hakuweza kuwafahamu. ....... Itaendelea. ... Read More
SHINDU LA KIHAYA-18 ,,,mmmmh,,,aaaaaaaaaaah,,,aashiiiiiiiiiiiiiii,,,aliendelea kulalamika mtoto wa kike ambapo nyege kweli zilimpanda,kujinasua mikononi mwa Mwalimu ilikuwa ni ngumu hasa kwani alilegea mwili wote ,,,sawa,waweza kwenda darasani,nimeacha tabia mbaya,,,aliongea kwa makusudi Hedimasta akitaka kumvalisha nguo Lisa ,,,hapaaanaaa usiniache hivyo,,,kwa sauti ya kelegea kimahaba tena ile yenye uhitaji aliongea Lisa,sura ilikuwa ya huruma sana,yaani hapo huku chini kwenye ndani ya kitumbua chake alihisi kama anawasha balaa hata angewekwa kidole pengine angemwaga Kwa umbo la Lisa,mtu mwenye nguvu hata za wastani anaweza kumbeba kirahisi,ndivyo alivyofanya Hedimasta huyo,alimbeba Lisa akiwa yuko uchi kabisa,Hedimasta mwenyewe dudu lake lilisimama kweli,Lisa alipokuwa akiliona na jinsi alivyokuwa akijisikia nyege basi ndio zilizidi kuongezeka.Kitu kimoja,sio kwamba wanawake huwa hawatamani dudu za wanaume,huwa wanatamani sana,na wanawake walio wengi hupenda dudu kubwa,tena akipatikana mtu anayejua kulitumia vyema ndio kabisa umemaliza kazi,na kama ukitaka kuthibitisha hilo,siku nenda na mschana wako pengine kwa jamaa yako,kisha jamaa yako awe na bukta kisha lile dudu lijichore jinsi lilivyo refu na nene,wewe kuwa makini kumwangalia msichana wako machoni halafu utathibitisha. Hedimasta alipombeba Lisa alimkalsha juu ya meza yake,hapo ni baada ya kusukuma vitabu na nyaraka za Serikali zilizoangukia sakafuni,hakujali hata kidogo.Alimpanua miguu na kuiweka mabegani mwake,ikawa kama inataka kumkaba shingo,mikono ya Lisa ilishika meza,ila mikono ya Hedimasta ilimshika Lisa kiuno chake,huku chini kilibaki kitumbua kikiwa kimelowa utamu Aisee njia nyingine ya kumpagawisha mwanamke kabla ya kuchanganya makongoro ni hiyo aliyoifanya Hedimasta,alilishika dudu lake kwa mkono mmoja kisha akawa anaanzia juu kidogo ya kitumbua yaani kwenye kitobo cha mkojo,kile kichwa cha dudu akawa anakikandamiza huku akikishusha chini taratibu,kilipofika kwenye kiarage mtoto alishtuka na kupiga yowe la utamu,hakuingiza dudu ndani ya kitumbua,akawa anafanya hivyo kwa kurudia,aiseee mtoto wa watu aliweuka kweli kwa utamu,.,,aaaaaaaaaaaaah,,,sssssssssssshiiiiiiiiiiii,,,uuuuuuuuuuuuuh,,,alilalamka hivyo ambapo Hedimasta alichanganua kwenye akili yake na kujua kuwa kilio kile cha mwanzoni ni tofauti kabisa na hiki kwasababu hiko cha mara ya pili ni chenyewe zaidi na kilivutia hisia. Lisa alipata shida kwani alikuwa anataka aingizwe dudu na Mwalimu haingizi ila anakisugua kiarage kwa nje ,,,unanitesa jamaniiii ingizaaaa yoteeee,,,aliongea kabisa Lisa ambapo Hedimasta alipokichusha kichwa cha dudu chini na kulenga mlango wa kitumbua,taratibu alilisukuma kwa ndani,,,aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah,,,,ssssssssssssssssssssh,,,aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah,,,alilalamika Lisa kwa utamu ambapo Mwalimu alilizamisha dudu lote na kuanza kupampu kwa hisia. Unafikiri Lisa alichelewa basi!,mapigo thelathini ya haraka haraka mtoto alikojoa bao lake na kumganda mwalimu wa watu,baada ya hapo alianza mauno yake ya kichokozi,kwanza hakukubali kuwekwa kwenye meza,alimganga mwalimu mpaka akanyanyuka naye,mwalimu kwa kumkomoa na kumpagawisha zaidi alimpeleka kwenye kona na kumbananisha hapo,e bwana kumbe hakufanya kitu mtoto alimkatikia mauno ya nyege mpaka mwalimu akaanza kuona joto la mwili linapanda,utamu ulipanda mpaka akajikuta anamwaga bila kutarajia maana mtoto alikuwa hafai kwa mauno sumu Mwalimu wa watu alikojoa bao lake ambapo ilibaki kidogo amdondoshe Lisa kwa kunogewa utamu,baada ya hapo sasa kila mmoja akawa hana abu na mwenziye,Lisa ndio kabisa hakumwangalia kama Hedimasta,alimwona ni mpenzi wake ambaye anaweza kumfanya lolote.Basi kwa adabu mbaya ya mahaba,Lisa akamshika tako Hedimasta,kidume unafikiri kulipiga kelele wala kuwaka,kilipotezea na kucheka tu. Siku hiyo aliyeshtukia mchezo alikuwa ni sekretari maana ndiye aliyemtetea sana Hedimasta pale alipohisi hali ya tofauti juu ya walimu waliokuwa wana shida naye.Kweli hakuna hata walimu waliojua ila yeye pekee alielewa kila kilichokuwa kinafanyika.Kuna muda hisia chafu zilimjia kichwani lakini alizipinga kwani hapakuwa mahali pake sahihi pa kuziruhusu. Yule mama jirani aliyesuguliwa na Alex ambaye kwa jina alijulikana kama Agnes,alikuwa akimuinjoi mumewe alipokuwa akimuhoji kuhusu jeraha lilipo kwenye paji la uso wake,alijua tu mumewe ndiye aliyekuwa akipiga chabo siku ile,cha kushangaza hakushtukia kitu chochote.Tabu ya kumsaliti mpenzi wako iko hivi,na ndio itakayokufanya ujulikane mapema,kwa mfano Angesi alikuwa mtu wa kulazimishwa sana Sex kutoka kwa mumewe,na akipewa huwa anashukuru sana kwasababu jamaa huwa anajisahau muda mwingine kazi nyingi,tangu apate kitu cha ukweli hakuwahi kumsumbua tena mumewe,sasa hiyo humpelekea mumewe kuanza kuhisi tofauti. Hassan alikuwa amemfanya Agnesi kama chakula chake,ndani akawa hapiki tena,analetewa chakula kuanzia cha asubuhi,mchana na jioni,na mara nyingi akilete cha mchana huwa lazima asuguliwe ndio aondoke hawezi kuachwa hivihivi,na alivyokuwa mtundu wa kupika,Hassana alikamatika hasa ndio maana wanasemaga mwanamke mapishi bwana. Ilipita kama mwezi mzima hivi,Hassana akiendelea kumsugua Agnesi.Siku hiyo akiwa amelala hana hili wala lile,asubuhi hodi ilibishwa mlangoni kwake.Hassan alijua tu ni yule mama ndio anabisha maana ni kawaida imeshakuwa,,,,INAENDELEA SHINDU LA KIHAYA-19 Ile kufungua mlango,alimkuta mtu tofauti kabisa na hakutegemea,yeye mwenyewe alihamaki kwanza kwani mtoto alikuwa mzuri usipime, ,,,mambo vipi,,,alisalimia Hassan ,,,safi,,,alijibu mtoto huku akitabasamu ,,,karibu ndani,,,alimkaribisha kwa sauti fulani ya kukoroma ,,,ahsante,,, Hassan alihisi kama ngekewa,hapo alikuwa ndani ya pensi fulani ya kijanja na vesti yake zinazotaka kufanana rangi,mtoto alipita mpaka ndani bila uwoga wowote na kwenda kukaa kwenye kochi. Hakuwa mwingine,alikuwa ni Lisa.Hassan hakujua kuwa huyo ni mtoto wa mama ambaye anamsugua na kumweka mjini,tayari alishamtamani kwanza,Lisa mwenyewe alivyovaa likuwa ni utata tupu,alivalia gauni fulani lililomwishia juu ya magoti,lilimbana na kumchora umbo lake vyema la kimahaba,hapo kifuani mwake ni kama hakuvaa kitu ndani maana Chuchu zilichomoza na kuhamasisha hasa. ,,,najua hunijui ila napaswa kukuita baba,,,alisema Lisa ,,,kwanini unasema hivyo,,,aliongea Hassan huku akiweka tabasamu usoni ,,,mi mtoto wa Skola,,,alijitambulisha,hapo ndipo akili zilimjia vizuri na kumwangalia vyema,picha alikuwa ameshaonyeshwa lakini hakutegemea kabisa kukutana naye kwenye mazingira hayo,hivyo alimkumbuka ,,,mmmh,ngoja nimuulize kwanza,,,aliposema hivyo alichomoa simu na kujifanya kama anataka kumpigia ,,,hapana usifanye hivyo,ye hajui mi niko wapi,,,aliposema hivyo Hassan aliaghirisha zoezi hilo,tena aliposikia kuwa mama yake hajui kama yuko hapo,ndio moyo ulifurahi kabisa na kuhisi anaweza kufanya jambo Hassan alianza kujihangaisha huku akichangamka hasa kwani Lisa alikuwa sio mchezo,ushawishi wake ni hatari sana.Kwanza alipokaa tu kwenye kochi yale mahipsi yake yalitanuka zaidi halafu tumboni flati,kifuani ndio usiseme.Haraka kidume kilikwenda kutafuta supu na chapatti.Lisa hakujivunga,alikunywa vyema kisha akashushia na soda ya baridi. Musa,rafiki yake kipenzi na Hassan,ambaye ni mzito sana kwenye suala la kuongea na wasichana yaani kutongoza.Aliingilia kati mchezo na kumkuta Lisa ndio anamalizia chakula,baada ya kusalimia Musa,alikaribishwa chakula ambapo kwa sura ya upole alijibu ameshiba.Moyoni Hassan alikasirika ujio huo wa Musa ila kwa nje alionyesha kufurahi. Hassan hakufanya hata utambulisho kwa jinsi alivyo na roho mbaya,kila wakati macho ya Musa yalikuwa kwenye mapaja mazuri yaliyonona ya Lisa,yaani aliyatolea macho ya matamanio yale ya waziwazi kabisa.Lisa alijua kabisa wakati anayopitia musa hata Hassan,kwa makusudi Lisa alimkonyeza Musa,e bwana mapigo ya moyo yalianza kumwenda mbio Musa mpaka alipoongeleshwa na Hassan alijikuta akishindwa kutamka maneno vyema. Alichokifanya Hassan ili kuendeleza harakati za kumvutia mtoto kwenye box.Alimtoa nje Musa na kuanza kumpanga,Lisa naye kwa umbea alijivuta mpaka usawa wa mlango ili kusikiliza ,,,sikia,we hujui kuongea,potea kabisa eneo hili,chukua hii buku tano,,,Hassana alisema hivyo ,,,kaka lakini mbon amenipenda bwana,,,alijibu Musa na kutaka kurudi ndani,kwa kukonyezwa alishahisi kitu.Hassana alicheka kwa nguvu kabisa kisha akarejea ile sauti yake ndogo ,,,una kichaa wewe,mtoto mzuri huyu utampa nini,,, ,,,sa sikia,kila siku mi unaniona mjinga sijui kutongoza,acha niende ndani nikaongee naye,nikishindwa kutoka naye,mi nitaondoka,,, ,,,poa nenda,,,kwa Dharau Hassana alijibu hivyo ambapo alijua Musa hata angeenda kuongea nini asingekubalika. Kiukweli hata dakika haikupita,Musa alitoka na Lisa nje tayari kwa kuondoka,walimkuta Hassan nje kisha Lisa ndiye aliyeaga ,,,baba natoka kidogo,ili mradi nimeshapajua nitakuwa nakuja,ahsante kwa supu,,,kauli hiyo ilimpa wakati mgumu Hassan kujibu lakini alijikaza sana ,,,sawa,lakini mbona unawahi sana jamani,ngoja niwasindikize,,,alisema hivyo na kumkata jicho la husuda Musa aliyekuwa akikenua meno nje kumcheka ujinga Basi wakaanza safari wote watatu,walivyojipanga tu ilikuwa maumivu kwa Hassan,yaani mtoto sijui alipenda nini kwa Musa ghafla.Akajikuta anamshobokea jamaa ambaye hata hawezi kutongoza.Lisa alkuwa pembeni kabisa akiwa ameshikana mkono na Musa,Hassan alimfuatia musa,basi hapo Musa tayari dudu lilishasimama kushika mkono tu ,,,sio mbali sana,,? ,,,hamna ni bajaji tu tunafika,,, ,,,pasiwe mbali bwana,,, ,,,usijali muda si mrefu tutafika,,,maongezi hayo kati ya Musa na Lisa,yalimchoma moyo moja kwa moja Hassan na kumfanya awe kama mtu anayetaka kulia.Alitamani aichukue elfu tano yake aliyompa Musa ili aondoke,matokeo yake elfu tano hiyo ndio ilitumika kumsafirisha Lisa mpaka kwenye gheto la Musa Roho ilimuuma kumwona Lisa na umbo lake tamu kupanda bajaji na kuelekea gheto kwa Musa ila hakuwa na jinsi,mtoto alijituliza kwenye bajaji,mara amshike bega na kuegemeza kchwa chake,mara washikane mikono ndani ya bajaji ilikuwa raha tu kwa Musa,kiukweli Musa alikuwa ndotoni kabisa. Walipofika gheto ndio kabisa hakuamini,sasa kwa Musa ilikuwa ni tofauti,alikuwa anakaa kwenye nyumba fulani kubwa peke yake,aliachiwa na mjomba wake akae kwani mjomba huyo hakuwa na haraka ya kuhamia kwasababu anafanya kazi mbali kidogo.Nyumba ilkuwa na kila thamani ndani yake,Lisa mwenyewe alipapenda ,,,nyumba yako nzuri,,,alsifu Lisa ,,,kama wewe ulivyo mzuri,,,alijishangaa kufungua kinywa na kusema hivyo Musa ,,,mi mzur kweli,,? Alihamaki Lsa kwa makusudi ,,,kweli,hilo la kuuliza jamani,,, ,,,nihakikishie kamani mzuri,,,aliposema hivyo ndio alizua balaa mtoto wa kike,maana jamaa mwenyewe alikuwa na Ugumu hasa,,,ITAENDELEA KESHO SHINDU LA KIHAYA-20 Lisa alimsogelea mpaka kwa karibu,aliubana mdomo wake wa chini na meno kisha taratibu aliuachia huku akiupeleka mdomoni mwa Musa,masikini Musa wa watu alikuwa hajafanya mapenzi kitambo,alisisimka mwili mzima na kujikuta akilegeza mdomo wake bila kutarajia. Mtoto wa kike alifumba macho kuvutia utamu ambapo mikono yake taratibu aliipitisha shingoni kwa Musa,yaani midomo ilipogusana,Musa alijihisi kama anapaa,kule kusogeleana mpaka kugusana kabisa ndio ilimaliza kila kitu,mikono ya Musa ikawa inatalii kwenye kiuno cha Lisa taratibu bila shaka. Lisa akawa anamshikashika kimahaba kichwani Musa wa watu ambaye denda liliendelea,ndani ya mdomo mtoto aliuzungusha ulimi ipasavyo na kumsisimua kweli Musa.Kidume kilimwaga pale ambapo mikono ya Lisa ilishuka mpaka kiunoni mwake na kuingia ndani ya shati,ikawa kama inamkunakuna kimahaba,aisee kuna wanaume wengine huwa wanapagawa sana ukiwashika migongo,Musa alimwaga ambapo Lisa alishangaa kidume kikijihangaisha na kuzidisha nguvu za kumkumbatia,akajua tu kijana wa watu amemwaga. ,,,pole Musa wangu,,,kwa sauti ya chini sana,kuliko kawaida aliongea Lisa ,,,ahsante,,aliitikia kidume huku akijishtukia Lisa alimvuta Musa taratibu na kumtupa kwenye kochi.Akamfuata na kuanza kumvua shati na vesti yake,alipomaliza hapo alipiga magoti kama mtumwa anayetaka kuomba msamaha kwa bwana wake baada ya kukosa,kumbe Lisa ndani ya gauni yake alivaa chupi pekee tena bikini,basi mtoto kwa taratibu alijivua gauni lake na kubaki na bikini tu,mapaja yake manono sasa!,yalionekana laivu bila chenga,hapo kiunoni,kitovu kizuri kilichoingia ndani,rangi adimu aliyonayo Lisa vyote vilimfanya Musa ajione kama yuko ndotoni,hakujion akuwa anastail mtoto mzuri namna hiyo kumsugua. Alipomaliza kuvua gauni lote na kulitupa pembeni,alitembea kwa magoti na kuingia katikati ya mapaja ya Musa,taratibu bila pupa limfungua mkanda na kuishusha suruali,alipoivuta tu na kufika magotini,alijifanya ameshtuka jambo ,,,aaaah!,jamani umemwaga,,!,alishangaa hivyo akiwa anatabasamu Musa na uwoga wake alishindwa hata ajibu nini,alibaki kimya kama mzimu huku akitabasamu. Ni kweli Musa alikuwa hajui kuongea lakini sio kwamba ukimwonyesha shimo hajui kuchomeka,japo alimwaga,lakini dudu liliendelea kusimama,hapo lilikuwa ndan ya Boksa,Lisa alishusha ile suruali mpaka chini kabisa,alipoivua yote,sasa akawa anahema kuliangalia dudu la Musa lilivyotuna kwenye boksa yake,tena lilikuwa kama lnapumua vile ndani ya boksa. Alilegeza mdomo mtoto wa kike na kujaza mate ya kutosha,aliusogeza mdomo wake mpaka kwenye mtuno huo wa dudu,mtuno wenyewe ulionyesha dudu limeelekea kushoto,basi alitoa ulimi wake na kuanza kulifuatisha mpaka kwenye kichwa cha dudu hilo,,,aaaaaaaaaaaah,,,aliguna Musa ambapo mtoto alikiingiza kile kichwa mdomoni kikiwa vilevile ndani ya boksa akawa anafanya kama anakipumulia ile hewa ja moto mdomoni,Musa alijihis raha mpaka kuinua sura yake juu kwa utamu Taratibu alianza kuivua boksa yake mpaka chini kabisa,dudu la Musa liliachwa huru sasa liknesanesa,halikuwa imara sana,basi Lisa akaanza kazi ya kulifanya lwe imara ili miguso mnato ianze,aliutoa ulimi wake nje kama nyoka vile,alikuwa akucheza juu chini haraka haraka,alipokigusa kichwa cha dudu kwa staili hiyo,Musa alianza kuguna tu kwa utamu,,,aaaaaaaaaaaaaaaaaah,,,aaaaaaaaaaashiiiiiiiiiiiiiii,,,ssssssssssssssssss,,aaaaaaaaaaaaaaaaah,,,,alilalamika Musa wa tu huku dudu lake likishughulikiwa kile kichwa tu,Lisa alipoona kdume knapagawa,aliliingiza lote mdomoni,alilizungusha na kulitekenya na ulimi wake hasa kwenye kichwa kile,Musa mwenyewe alishindwa hata kukaa vizuri kwenye kochi. Mikono yake laini Lisa aliipeleka mpaka kwenye kende na kuanza kuzitomasatomasa,nyege zilimpanda Musa mpaka akachanganyikiwa kabisa,dudu lilidinda vyema kiasi kwamba hata kurudi chin halikurudi,lilinesa lakini juu kwa juu.Hapo tena Musa hakufundishwa kitu.Alimshika uso Lisa kama anataka kumpiga kisha akaanza kumnyonya denda huku akimwinua taratibu. Dudu lake bado lilisimama hasa kama kijiti kilichochomekwa ardhini.Alimshika kiuno Lisa na kumvutia upande wake,mtoto naye alijilegeza hasa,Musa aliivuta ile bikini na kuikata mikanda yake kisha kuitupa kule,aliyavamiwa matako laini ya Lisa na kuanza kuyaminyaminya kama anachagua nyanya sokoni,,,,aaaaaaaaaaaah,,,bebiiiiiiiiii aaaaaaaaaaah,,,alilalamika Lisa ambapo ni kama alikuwa akmpandisha mizuka Musa. Bila ya kuambiwa Lisa mwenyewe,alijipanua mapaja na kujiandaa kukalia dudu la Musa lililosimama hasa,Musa aliliandaa lile dole la kati ambalo wengi huliita la matusi kisha akalipenyeza kwenye kitumbua cha Lisa na kuanza kumtekenya kiarage chake kilichosimama,,,aaaaaaaaaashiiiiiiiiiiiiiiiii,,mamaaaaaaaaaaaaaaaaaaa,,aaaaaaaaaaaaaaah,,,musaaaaaaaaaaaaaaaaa,,aaaaaaaaaashiiiiiii,,,oooooooouuuuuh,,,eeeuuuuuuuuuwii,,,mtoto alilalamika kwa utamu mpaka alitia nyege tena.Basi Musa alipokuwa akimchezea kiarage chake,akawa anakishusha kidole chake chini taratibu huku akijua chini kuna dudu limesimama,naye Lisa alikuwa akikifuata kidole taratibu kwa alihisi utamu alipokuwa akitenywa kiarage chake,ilifika muda Lisa alishtuka na kupiga yowe la utamu,pale dudu la Musa lilipogusa mashavu ya kitumbua,,,aaaaaaaaaaaashiiiiiiiiiiiiii,,,taratibu mpenziiiiiiiii,,,,,INAENDELEA ... Read More
*LOVE BITE EP 03* ILIPOISHIA………. Mawazo yalirudi tena kwenye ile picha na kuamua kuificha bila kuichoma moto kama alivyotaka mwanzo kufanya. Badala yake alienda sehemu ambayo kulikuwa na hati ya nyumba yake na kuiweka ile picha katikati. Ni kweli Prisza alikuwa anampenda na hawakuwahi kuachana. Ni muingiliano tu wa maisha ndi uliowatenganisha. Moyo wake aliona kama si haki kuichoma ile picha kwakua bado alikua na nafasi ndani ya moyo wake japokuwa kuonana na msichana huyo ni ngumu sana. Hata alipomaliza chuo alijitahidi kumtafuta bila mafanikio. Mpaka muda huu anajitegemea ni kipindi kirefu cha miaka sita tuko walipokutana na Prisca kwa mara ya mwisho. Mawazo ya msichana huyo wa kwanza katika maisha yake yalimchanganya kichwa na hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali matokea na kuanzisha ukurasa mwengine wa maisha yake kwenye mapenzi na shani Baada ya usafi huo wa kabati lake, aliamua kujilaza kitandani na usingizi ukamchukua. SONGA NAYO………… Siku ya pili yake Jothan alienda kazini kama kawaida. Alifanya kazi zake na baada ya kurudi kazini alimkuta Shani amejaa tele nyumbani kwake. “karibu mume wangu “ alikaribisha Shani na kumfuata Jothan na kumpokea mizigo yake. “ahsante.” Aliongea Jothan na kumkabidhi mizigo yake Shani. “una oga kwanza au unakula ndio uende kuoga?” aliuliza Shani baada ya kurudi pale alipokuwa Jothan. “vyovyote tu mke wangu. Maana nahisi joto na hata njaa pia ninayo.” Aliongea Jothan na kumfanya Shani atabasamu. “kaoge kwanza, maana ukiwa vizuri hata chakula kitashuka barabara.” Alishauri Shani na mawazo yake yakapitishwa moja kwa moja na Jothan. Alipotoka kuoga Jothan, alirudi mezani na kukuta Shani ameshaandaa mapocho pocho ya kila aina yaliyochafua meza. “unajua mke wangu, hata niwe na njaa vipi, kama wewe upo nyumbani basi hudiriki kuitunza hiyo njaa kwa sababu unajua sana kupika mke wangu. Muda mwengine naomba nipate na njaa ya ajabu ili nikifakamie kisawasawa chakula chako.” Aliongea Jothan na Shani akabaki anatabasamu na kumuangalia Jothan kwa mapozi. Mapenzi moto moto kutoka kwa Shani yalizidi kupamba moto. Muda wote Shani alijitahidi kumuweka Jothan kwenye kundi la wanaoyafurahia mapenzi. Jothan alijisikia raha kutokana na Shani kila wakati kutokana na mauzo anayoyapata kuwa na msichana High classic. Walitamani kila saa wawe karibu na kulishana ndio style iliyowavutia watu wengi waliowashuhudia wawili hao walionyesha kupendana sana. Siku moja Jothan akiwa anatoka kazini, ghafla aliona gari likiwa limepaki pembeni na kuna msichana akihangaika kulishughulikia lile gari. Jothan alipaki gari lake pembeni na kushuka kwa ajili ya kutoa msaada. Alipomfika eneo la tukio, yule dada aligeuka kumuangalia Jothan na wote wakajikuta wanapigwa na butwaa. “JOTHAN!!” aliita yule dada kwa sauti kubwa iliyoambata na mshangao mkuu. “PRISCA!!” hata jothan naye alilitaja jina la yule msichana na kumfanya Prisca kujiachia na kupitisha mikono yake mgongoni mwa Jothan kupitia kweye makwapa yake kama ishara ya kumkumbatia. Jothan naye akampokeaa vizuri kwa kuzungusha mikono yake kwenye kiuno namba 6 cha Prisca. Baada ya kusalimiana, wakaona haitoshi. Waliacha gari zao pale pale na kutafuta sehemu tulivu na kukaa kwa ajili ya kupigiana story mbili tatu kutokana na kukumbukana kupita kiasi. “ ahsante mungu kwa kunikutanisha na kipenzi changu jamani,.. jothan milima haikutani ila binaadamu tunakutana. Leo hii kauli hiyo ndio naikubali kwa asilimia zote.” Aliongea yule dada huku akionyesha furaha ya wazi juu ya Jothan ambaye wakati huo alikua na tabasamu la usoni lakini kichwani alikua kwenye msongo wa mawazo. Anampenda Prisca lakini kwa sasa Shani amechukua nafasi kubwa kwenye moyo wake kutokana na kumpa kila anachokihitaji tena kwa wakati. Alikiri kuwa kwa sasa Prisca alizidi uzuri na kumfunika hata Shani. Maana Shani alikuwa ameridhika na kuzidi kuwa mnene kiasi japokuwa sio kigezo cha kupunguza uzuri wake. Ila Prisca alikuwa mwembaba lakini aliyekuwa na figa iliyojichonga kama glasi ya wine. Kwenye kiuno alikuwa mnene na kufaya hipsi zake kuonekana sana. Pia kijungu cha wastani kilichotupiwa huko nyuma ndio kilizidi kumpa maksi zaidi na kumfanya azidi kuonekana special na wanaume wote wanaojua viwango vya wanawake wazuri na wenye mvuto katika muonekano wa macho ya marijali. Kiuno kilichoingia ndani na muinuko wa kibinda ndio kilitengeneza namba 6. kiuno hicho mungu kawapendelea wasichana wachache sana. Hata wachina wameshindwa kutengeneza dawa ya kutengeneza kiuno hicho. Sura ya mviringo iliyokuwa na macho yenye kilevi bila ya kunywa kileo chochote ndio kilikuwa kivutio kingine. Ukiachana na weupe halisi ambao ulikuwa kiasi na kufanana na maji ya kunde, pia vijisima vidogo mashavuni vilivyojitokeza kila akifanya tendo lolote liliousumbua mdomo wake vilimfanya mtu yeyote kutamani kumuangalia usoni. Uso uliombwa na haya mbele ya mwanaume ndio ulikuwa kivutio hasa kwa mvulana mwenye kutafuta mtu wa kuweka ndani na kuoa kabisa. Mambo yote hayo ndiyo aliyokutana nayo Jothan baada ya kukutana na Prisca kwa mara nyingine baada ya muda mrefu. Hata yeye mwenye alikutana na majaribu hayo aliyoyafananisha na majaribu ayapatayo mwanamke mjane baada ya kusikia sauti ya mwanaume tajiri aliyekuja kumfariji na kwa kumuahidi kumuoa na kuwa tayari kuwalea watoto wake. Alijikaza kiume na kujaribu kuyaficha madhaifu yake yaliyomkumba na kujifanya yupo kawaida. “Hata mimi nimefurahi kukuona, za miaka?” aliongea Jothan na kumuangalia Prisca ambaye alikua na furaha wakati wote huo toka wameonana. “vipi, leo maaskari hawaji??” aliuliza Prisca na kucheka. “leo hakuna mwanafunzi hapa..au wewe mwanafunzi?..maana siku ile nilikataa kuwa mimi ni mwanafunzi halafu wewe ukajitambulisha kuwa mwanafunzi.” Aliongea Jothan na kufanya kicheko kitawale kwa sekunde kadhaa kati yao. “tumetoka mbali sana Jothan, leo naona kabisa kuwa mungu katufanya tusahau kipindi chote ambacho hatukua pamoja.” Aliongea Prisca huku akionyesha wazi kuwa bado alikuwa na mawazo ya mapenzi juu ya Jothan. “hata mimi naona kama vile hatukuonana siku mbili kwa jinsi siku ya leo ilivyofukia mashimo ya miaka mingi niliyoishi bila kuiona sura yako.” Aliongea Jothan na kumuangalia Prisca aliyekuwa na kila kitu cha kutalii umuangalipo usoni. “nikuulize swali Jothan?” Aliongea Prisca na kumfanya Jothan kushangaa kidogo baada ya kuombwa ruhusa ya kuulizwa kitu. Alifikiria kwa nukta kadhaa kisha akaruhusu kusikia kitu alichotaka kuuliza Prisca. “umeshaanzisha uhusiano wa kimapenzi na mwanamke mwengine zaidi yangu?” Aliuliza Prisca swali hilo huku akiwa kawaida na kuonyesha wazi kuwa lile swali linahitaji majibu sahihi na yenye utashi juu yake. Jothan hakuamini kama swali lile lingekuja mapema kabla hajaliandalia maandalizi yoyote ya kujibu. Ubongo wake ulikimbia kwa kasi kutafuta jibu la kumpa kati ya ukweli au kumuongopea kwakua wakati huo swala la kumuepuka au kumpotezea msichana huyo aliyeonja penzi lake toka hajakuwa sister du kama hivi sasa. Elimu ya msichana huyo na maisha mazuri anayoishi pia vilikuja kwenye ubongo wake na kufanya machaguo kuwa mengi. Yaani kama ni mtihani, basi lile swali lilikuwa katika mfumo wa matiple choice tena lililokuwa na mfumo wa A,B,C,D,E na F.. “sina.” Alijibu Jothan huku moyo wake ukimuuma kumkana Shani. “wooh… ni wazi hii couple Mwenyezimungu amekuwa akiismamia kwa kipindi kirefu. Unajua kuwa hata mimi nilikuwa naamini kuwa kuna siku tutakuja kuonana tena. Ndio maana sikuona uzito wowote kuwakataa wanaume wengi huku nikiwa sijui ni lini tutakutana. Roho ingeniuma sana ungeniambia kuwa kuna mwengine umeshampa moyo wako.” Aliongea Prisca bila kujua kuwa huo ndio ulikuwa ukweli wenyewe. Maneno hayo yalimfanya Jothan ajione kuwa hakuwa na makosa kumuongopea kwa sababu angemwambia ukweli chochote kingeweza kutokea na kusababisha maongezi ya amani kati yake na Prisca kutoweka. “unataka kuniambia kuwa mpaka hivi sasa hauna mtu mwengine aliyerithi mikoba yangu?” aliuliza Jothan kimitego. “hakuna… yaani toka uliponiacha sijaguswa na mtu mwengine. Yaani hata kama ungekuwa umenifunga luku basi zingesoma unit zile zile ulizoziacha.” Aliongea Prisca na kumfanya Jothan kutabasamu. Waliongea mengi na kila mmoja alifurahia uwepo wa mwenzake pale. Waliachana baada ya kumrekebishia Prisca gari lake na kila mmoja kupata mawasiiliano yote ya mwenzake. Waliachana na ahadi ya kukutana naye tena walikubaliana kuwa watapeana taarifa kwenye simu. Siku hiyo iliwekwa kwenye Diary ya Jothan ambaye alikuwa anatemba nayo kwenye mkoba wake wa kazini. Usingizi ulikuja ukiambata na ndoto iliyojirudia kuanzia mwanzo hadi pale walipoachana. Aliamka asubuhi na kukuta Shani ameshamuandalia maji ya moto kwa kuwa asubuhi hiyo ilikuwa na kiubaridi kidogo. Alipoamka tu aliletewa nguo za bafuni pamoja na mswaki ambao ulisha wekwa dawa kabisa. Alipokuwa bafuni mawazo yaligeuka upande wa pili na kumfanya amuwaze pia Shani kwa jinsi alivyokuwa akitimiza wajibu wote kama mke bora anavyotakiwa kufanya. Kila aliloliwaza kutendewa na msichana basi Shani alikuwa wa kwanza kufanya hata kabla hajaambiwa fanya. Hayo na mengine mengi ndio yalimfunga Jothan na kuyatuliza macho yake kwa wasichana wengine na kumfanya kuwa mtiifu kwa kurudi nyumbani mapema. Na kama anataka kupata moja moto maja baridi basi hutoka na mpenzi wake huyo ambaye alimfanya kuinjoy kwa kuwa sehemu nyigi walizoingia hakukua na mtu mwenye demu mkali kama wake. Alimaliza kuoga huku kichwani hakujua jibu nini kati ya A au B. kuna wakati alitamani kuyaweka kuwa yote ni majibu. Kuna wakati alitamani arushe shilingi ila alishindwa kumjua nani amuweke mwenge na nani amuweke bichwa. Prisca ndio msichana waliyebikiriana kwakua yeye hakuwahi kufanya mapenzi kabla kutokana na ulinzi thabiti wa wazazi wake alipokuwa anasoma. Na Prisca ndiyo yeye aliyekata utepe. Shani ndio mpenzi wake wa ukubwani ambaye anamuonjesha matamu ya ndoa hata kabla hajafikia maamuzi ya kuoa. Hata sasa anaanza kuonekana na kitambi kidogo kwa sababu ya raha azipatazo kwa mpenzi wake huyo. Japokuwa walikuwa wapenzi kwa kipindi kirefu, lakini hawakuwahi kukaa pamoja hata wiki moja kwa sababu kila mmoja alikuwa anaishi na wazazi wake. Ila Shani na yeye wamekuwa wakilala pamoja mara tatu kwa wiki. “itakavyokuwa ndio hivyo hivyo.” Aliongea Jothan baada ya kuona anaisumbua akili yake bila majibu sahihi. Siku waliyo ahidiana kukutana kati ya Jothan na Prisca iliwadia huku kila mmoja akiwa amewasili bila kukosa huku wakiwa wamejitupia vitu vya thamani kila mmoja. Make up na mpangilio wa nguo alizovaa Prisca zilimfanya kuonekana katika muonekano mwengine wa kuvutia zaidi. Jothan hakuamini kuwa ndiye yeye alikuwa analala kwenye kifua cha yule msichana zamani. Pia hakuamini kuwa huyo msichana ndiye aliyekuwa akilipigania penzi lake miaka yote japokuwa walikuwa hawajaonana miaka mingi. Walikutana huku kila mmoja akiwa ameshuka kwenye gari lake na kwenda kwenye hotel moja yenye hadhi hapa Dar. Walipata chakula cha mchana na baadae wakaenda kwenye swimming pool kuogelea. Hamadi !, Macho yalimtoka Jothan baada ya Prisca kuvua nguo zake na kubaki na nguo ya ndani huku juu kukiwa na sidiria ndogo iliyobana maziwa yake na kuyafanya yapande juu na kuonekana sehemu kubwa ya maziwa iliyoteganishwa na msitari mmoja kati kati kuwa wazi. Jothan hakuona ubaya kuvua nguo na yeye na kubaki na boxer na kujumuika naye kwenye swimming pool huku wakiwa peke yao eneo hilo lililokuwa na mabwawa mengi ya kuogelea. Waliogelea na kujikuta michezo yote wanacheza. Kuanzia bembea, mpira wa pete na mwisho wakamaliza na mchezo usio hitaji kocha wala mashabiki japo kuwa unapendwa na watu wengi hapa duniani. Ukiwa mtoto unaambiwa kuwa mchezo huo ni mmbaya lakini ukikuwa bila kufundishwa unajikuta unacheza huku ukijilaumu kwa nini hukuanza kucheza toka mwanzo. Hawakujua walitumia muda gani kwakua taa za ile hotel ziliwaka muda wote na kufanya mtu asitambue wakati kama hajaangalia saa. Mndinyo wa kitanda murua cha hotel hiyo ndio sababu iliyowafanya kudumu muda mrefu huku kila mmoja akiwa ame miss raha za mwenzake. Mechi hiyo ya marudiano ilikuwa kali na kila mmoja alikiri kuwa walihitaji kuwa karibu na kucheza kila mara. Baada ya muda, Jothan aligutuka kuwa hiyo siku ndio siku Shani alikuwa analala kwake. Aliamka fasta na kutupa macho yake kwenye saa ya ukutani “MUNGU WANGU…. SAA SABA USIKU?” Alishtuka kimoyo moyo na kutaja alichokiona kwenye saa. Aliamka ili aenda kuoga kwa ajila ya kwenda nyumbani kwake. “vipi darling, unaenda wapi tena… mwenzio nahitaji kimoja tu cha mwisho.” Alidakwa mkono kimahaba na Prisca aliyekuwa ameyarembua macho yake na kuonyesha ishara zote za kuhitaji kipindi cha pili baada ya mapumziko. “najisikia uchovu ndio maana nilikua nataka kwenda kuoga.” Aliongea Jothan huku akiwa na wasiwasi mkubwa juu ya Shani kugundua usaliti alioufanya siku ile. “twende wote babie, tukirudi mpango mzima au…” aliongea Prisca na kumfanya Jothan azidi kuchoka. “poa.. twende.” Alikubali kishingo upande na wote wakaenda kuoga na uchokozi alioufaya Prisca huko bafuni ikiwafanya mchezo huo kuanzia huko huko bafuni na kumalizikia kitandani wakiwa hoi na usingizi wa muda wote waliokuwa wakicheza cheza ulikuja na kuwafanya wapate usingizi mnono. Saa nne asubuhi ndio waliachia kitanda na kwenda kuoga. Walipofungua mlango walikutana na wahudumu waliokuwa wakigonga kwa ajili ya kufanya usafi. Walieda kupata supu kutokana na kupotelewa na nguvu nyingi masaa kadhaa yaliyopita. Baada ya hapo. Walijiandaa na kila mmoja akapanda kwenye gari lake huku Prisca akionyesha wazi kuwa aliufurahia uzinduzi wa uhusiano yao uliofanyika kwenye kitanda cha hotel ya SERENA. Jaothan akiwa kwenye gari lake, aliiona simu yake aliyoiacha makusudi kwa ajili usumbufu pindi awapo na Prisca. Alikuta missed call zaidi ya kumi na tano na sms sita zote zikiwa za Shani na zikionyesha kuwa na wasi wasi juu ya usalama wake. Alihuzunika sana kwa kosa alilolifanya japokuwa hakupanga kulala nje. Maisha ya kuendesha mioyo miwili hakuwahi kuishi na tayari kwa siku hiyo aliona adha yake na kutamani kuchuja na kuwa na mmoja tu. Ni nani ambaye angestahili kubaki na ni nani atoke ndio swali lililokosa majibu kwakua wote alikuwa anawakubali kwa wakati wao. Alivyolala na Prisca alikuwa kama alikuwa anamfungua kwa mara ya kwanza hali iliyomfanya aamini kuwa hakutumika muda mrefu. Aliona sio sawa kumuacha msichana huyo mwenye ndoto naye nyigi za maisha yao toka walipokuwa wanasoma. Na Shani hakustahili kutendewa unyama wowote kwakua hata yeye hajawahi kumfanyia unyama wowote zaidi ya kumfariji anapokuwa ana huzuni na daima aliisimamia furaha yake hata ikibidi kuenda kinyume na matakwa ya dini kwa kukubali kuishi nae bila ndoa. Akiangalia kila mmoja alionyesha kumpenda kwa wakati wake na hawakuwa tayari kumuachia. Ila yeye swali la NIMPENDE NANI lilimsumbua kuliko hata DIAMOND. Aliamua kuwasha gari lake na kuelekea nyumbani. “oooh.. ahsante mungu. Umekumbwa na nini kipenzi changu?.” Aliongea Shani baada ya kuupokea mkoba wa Jothan. Hali hiyo ilimshangaza Jothan kwakua hakutegemea mapokezi kama yale. “samahani mke wangu, sikukupa taarifa kuwa ofisini kuliandaliwa warsha na nikaenda kwa kudhani itaisha siku hiyo. Hata hivyo simu yangu niliisahau kwenye gari na kunifanya nisizione missed call zako mapema.” Aljiuma uma Jothan mbele ya Shani ambaye wakati huo ndio kwanza alikuwa anamvua viatu baada ya kukaa kwenye moja ya masofa yaliyokuwa pale sebuleni. “sawa mpenzi wangu. Nimefarijika tu wewe kurudi salama.. maana nilikuwa na wasi wasi juu ya uzima wako tu.” Aliongea Shani na kumuonyesha Jothan jinsi anavyomjali. “samahani sana mpenzi wangu, nitajaribu kukupigia simu kwa kila siku nitakayochelewa kurudi nyumbani.” Aliongea Jothan na kukiri kuwa amefanya makosa makubwa ambayo hata yeye mwenyewe hakuyategemea. Siku hiyo ilipita kwa Jothan kulala muda mrefu kutokana na uchovu wa jana yake. Asubuhi aliamka na kukuta ameandaliwa nguo za kuvaa kwa ajili ya kwenda kazini zikiwa zimepigwa pasi kabisa. Aliwekewa maji ya uvugu vugu kwa ajili ya kuoga kisha kifungua kinywa matata kilikuwa tayari mezani kinamsubiria yeye tu. “ashante mke wangu.” Alishukuru Jothan baada ya kumaliza kunywa chai. “usijali mume wangu, nakutakia safari njema. Take care honey.” Aliongea Shani na kumfungulia mlango wa gari Jothan. Jothan alifika kazini mapema na kufanya kazi zake kama kawaida. Saa nane alitoka kazini na kurudi nyumbani. Alikuta ameandaliwa chakula cha mchana mezani lakini Shani hakuwepo kwakua ilikuwa ni siku ya kwenda kwao. Alijihisi mpweke na alitamani Shani angekuwepo kwake moja kwa moja. Alikata shauri baada ya kula chakula na kuamua kumtafuta mpenzi wake kwenye simu. “hallow” alipokea Shani kwa mapozi. “I miss u babie, unaweza kuja tutoke baadae kidogo tukale mbuzi maeneo ya Facebook pub?” aliongea Jothan. “noo babie, leo nimeenda kwa mama. Sio vizuri kuonyesha tabia mbaya mbele yake ya kurudi usiku. We vumilia babie. Kesho tutakuwa wote.” Aliongea Shani kwa pozi zilizomfanya Jothan kushindwa kukata simu hata kama maneno ya msingi ya kuongea nae yameisha. “basi sawa. Sijui lini utanipeleka kwa mama.” Aliongea Jothan huku anatabasamu. “si wewe mwenyewe tu hujaamua. Ukiamua hata leo nakuleta huku.” Aliongea Shani huku akionyesha wazi kuwa alikua anacheka. “nitakuja tu mine, si unajua mambo mazuri hayahitaji haraka.” Aliongea Jothan na kukata simu. Siku ya pili yake walitoka pamoja na kwenda kula bata maeneo hayo na kurudi mida ya saa tano usiku. Alipokuwa kazini, alisikia simu yake ikiita kwa mlio tofauti. Kabla hata hajasoma jina la mpgaji wa hiyo simu. Tayari alishamtambua kwakua aliihifadhi namba ya mtu huyo kwa mlio tofauti kwa makusudi. “haloo.” Aliipokea ile simu. “haloo babie, I miss u.” sauti nyororo ya kike ilisikika upande wa pili. “I miss u too Prisca, niambie.”aliongea Jothan huku akiangalia wafanya kazi wenzake waliokuwa bize wakifanya shughuli zao. “hata kunitafuta wangu,.. yaani kama uliniroga mwenzako siku ile. Yaani sijielewi mpaka hivi leo.” Aliongea Prisca kwa sauti ya mahaba. Jothan aliangalia na kuona soo kuendelea kuongea maneno yale mbele ya wafanyakazi wenzake. “sema nini babie, nitakupigia nikiwa free. Now nipo kazini halafu nina kazi nyingi.” Aliongea Jothan kwa sauti ya chini. “sawa wangu, baadae.” Aliitkia Prisca na kukata simu. Jothan alifanya kazi zake na kurudi nyumbani kwake. Baada ya kupata chakula cha mchana, alijitupa kitandani na kuchukua simu yake na kumpigia Prisca. “haya lete maneno.” Aliongea Jothan baada ya Prisca kupokea simu. “nina hamu ya kuonana na wewe babie… sihitaji kuwa mbali na wewe hata kwa dakika moja kwa jinsi nillivyozimika mbaya.” Aliongea Prisca kwa sauti iliyomshinda mwana dada wa kipindi cha ala za roho kinachoruka usiku kwenye kituo cha clouds fm. Sauti ilipenya vizuri kwenye masikio ya Jothan na kuhisi labda Prisca alichanganya sauti ya Loveness love (Diva) na wema sepetu. “tupange week end, sababu katikati ya wiki ni majanga.” Aliongea Jothan. “poa, ijumaa si ulisema unatoka mapema. Unaonaje kama tukikutana siku hiyo.” Aliongea Prisca na wazo lake likapitishwa moja kwa moja na Jothan. Siku ya ijumaa ilipofika. Jathan alimpa taarifa Prisca na wakakutana maeneo ya Peacock hotel iliyopo maeneo ya mnazi mmoja. Jothan alifika na kumkuta Prisca alishafika muda mrefu kidogo na tayari alishaagiza kinywaji na alikua anakunywa taratibu. Alipofika, alipokelewa kwa kukumbatiwa na Prisca na kupewa mabusu matatu matakatifu kwenye mashavu yake na moja likiwa sawia mdomoni mwake. Baada ya salamu hiyo adhimu. Walimuita muhudumu aliyekuja haraka na kumpa oda yao. “tuchukue chumba sasa hivi au baadae?” aliuliza Prisca baada ya kumaliza kula. “hapana, leo sijisikii vizuri kabisa na sipo tayari kushiriki tendo lolote Prisca.” Aliongea Jothan na kumfanya Prisca apigwa na butwaa. Maana alijiandaa kabisa kupata mechi nyingine siku hiyo. “kwanini babie….unaumwa???” aliuliza Prisca kwa mshangao. “siumwi, ila mayo wangu unanisuta kila siku nikiongea na wewe kwenye simu au nikikutana na wewe. Najihisi sifanyi fair kwa nikitendacho.” Aliongea Jothan huku sura yake ikionyesha wazi kuwa hakuwa na furaha ingawaje aliingia kwa muonekano wa mtu aliyefurahia uwepo wao pale. “jamani, tatizo ni nini wangu, mbona una nifumba fumbo ambalo sijui nitalifumbua vipi?…naomba uniambie ukweli kuliko kuniweka mwenzako kwenye uzio wa alama ya kuuliza.” Aliongea Prisca huku akionyesha wazi kubadilika kutoka katika hali ya furaha aliyokuwa nayo mwanzo na kuungana na Jothan. “Prisca, hivi bado unanipenda?” aliuliza swali Jothan lililomfanya Prisca apigwe na bumbuwazi kwakua hakulitegemea lile swali. “nakupenda sana tena zaidi ya niwezavyo kuelezea kwa ulimi wangu. Ndio maana nikaweza kukaa kipindi kirefu bila ya kuwa na mtu mwengine japokuwa ni wengi walikuwa wanakuja kunitongoza na bado sikuona umuhimu wa kuanzisha mapenzi mapya kabla mapenzi yako wewe na mimi kufa.” Aliongea Prisca na kumuangalia Jothan aliyekuwa makini kumsikiliza. “hata mimi nakupenda Prisca, ila mimi ni msaliti na sio mwema kwako hata kidogo. Cha kwanza nimekuwa muongo kwa kukuongopea toka siku ya kwanza tulipokutana kwa mara ya pili ukubwani. Cha pili sistahili kuwa wako kwakua tayari nimeshakuharibia mipango na malengo yako kwa kipindi krefu Prisca.” Aliongea Jothan huku akionyesha wazi kuwa alikuwa katia wakati mgumu kufunguka yale yaliyomjaa moyoni. “sikueliwi Jothan.. naomba nidadavulie uyasemayo.” Aliongea Prisca huku akionyesha kuchaganyikiwa. “kwanza naomba unisameha Prisca kwa haya nitakayokuambia. … nilifanya makosa makubwa siku ile kwa kutokuambia ukweli kuwa tayari nina msichana na ninaishi naye. Nampenda sana ingawaje sikuweza kutoka kwenye mitego yako siku ile kwakua wewe ndio wa kwanza kukaa moyoni mwangu na chembe chembe za upendo juu yako ndizo zilizonisukuma mpaka kukuongopea na kukuambia kuwa sina mtu. Siwezi kuweka mafahari wawili kwenya zizi moja. Na kumuacha Shani ni kitu kisichowezekana kwakua ananionyesha mapenzi zaidi ya niliyowahi kufikiria mapenzi kuwa hivyo. Maamuzi yangu ni kwamba. Kuanzia leo sahau kuwa na mimi ni mpenzi wako…. Niwie radhi kwa hili.” Aliongea Jothan huku machozi yakimlenga lenga. Hakika ni uamuzi mgumu aliouchukua kwakua aliamini ilikuwa ni mtihani mkubwa katika mapokezi ya mlengwa. Alipoinua macho yake kumtazama Prisca, tayari mashavu ya prisca yalishalowana kwa machozi huku macho yakiwa mekundu. Kilio cha kwiki kilianza kusikika na kumfanya Jothan kuingiwa na imani baada ya kumtaza mpenzi wake huyo anaye amua kumuacha bila kosa lolote. ITAENDELEA ... Read More
Story...... NI WEWE TU PENINA Sehemu ya kumi na tatu (13) Ilipoishia....... Mzee Joel ndio hakuamini baada ya kuingia ndani na kukuta vijana wote wamelazwa chini alafu kidogo hivi akatokeza Nolan akiwa amepigilia suti nyeusi Kisha akamwambia baba yake ambaye ni mzee Joel, "naenda kwenye kikao cha harusi ya Penina na Frank na kama utahitaji kadi unijulishe nikuletee ya kwako." ***********Endelea ********* Nolan baada ya kumuambia baba yake maneno hayo aliingia kwenye gari na kuondoka. Nolan alifikia sehemu ambayo ilikuwa maalumu kwa ajili ya kutengeneza kadi za harusi. Nolan alitengeneza kadi za harusi zisizopungua Mia moja hamsini kwa ajili ya harusi ya Penina na Frank. Kadi hizo hazikuwa za kuchangia harusi ya Frank na Penina bali kadi za mualiko. Nolan alijipanga kusimamia kila kitu Katika harusi ya Penina na Frank hivyo yeye alitengeneza kadi ambazo ni kama kiingilio cha kuhudhuria harusi hiyo bila kuchangia chochote. Nolan baada ya kukamilisha zoezi la kutengeneza kadi zile akaanza kutafuta ukumbi Mkubwa wenye hadhi ya kufanyia sherehe ya harusi ya Frank na Penina. Nolan alifanikiwa kuupata ukumbii ambao aliuhitaji na baada ya hapo Nolan akaanza kuzigawa kadi zile kwa watu mbali mbali ikiwemo na marafiki pia. Nolan moja kwa moja aliwasili nyumbani kwa kina Frank na kuwakuta Wazazi wake Frank ambao walimpokea kwa furaha Sana. "kikubwa kilichonileta hapa ni kuhusu harusi ya mtoto wenu Frank pamoja na mdogo wangu Penina, napenda kuwaafahamisha kuwa taratibu za harusi ya ndugu zetu hawa inaendelea vizuri na hapa nimewaletea kadi za mualiko." alianza kuongea Nolan baada ya kukaribishwa ndani na Wazazi wake Frank huku akiwakabidhi kadi zile Wazazi wake Frank. "Asante Sana kijana wetu na hongera Sana kwa hapa ulipofikia Mungu azidi kukusimamia zaidi na zaidi." wakaongea Wazazi wake Frank huku wakimshukuru Sana Nolan. "msijali Sana hii kazi ilikuwa lazima niifanye na lazima nitaitimiza, na kingine ninachotaka kukifanya kwa Sasa nataka niwahamishe hapa nyumbani kwenu niwapelekee sehemu mkakae hapo kwa siku kadhaa mpaka pale harusi ya mtoto wenu itakapokamilika, nafanya hivi kwa sababu ya usalama wenu kwasababu kuna vita kubwa inaendelea. " akaongea Nolan na kutoa maelezo hayo ambayo Wazazi wake Frank walikubaliana nayo bila wasi wasi wowote. Wazazi wake Frank pamoja na Mdogo wake Frank walijiandaa na kuondoka na Nolan ambaye aliwapeleka Katika hotel moja iliyopo nje kidogo ya jiji la dar es salam na kuwataka wakae hapo kwa wiki tatu kabla ya harusi ya Frank na Penina na gharama zote atazisimamia yeye Nolan. Nolan baada ya hapo alishika njia ya kurudi nyumbani kwa ajili ya kwenda kupumzika kidogo. * Dickson aliwasili Tanzania kwa Mara nyingine tena Ila awamu hii alikuwa na vijana wake wanne alioongozana nao. Baada ya kuwasili uwanja wa ndege moja kwa moja Dickson pamoja na vijana wake walichukua gari ndogo na kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwa mzee Joel.* Mzee Joel alizidi kuchanganyikiwa baada ya kumaliza siku ya pili Sasa bila kumuona Penina na wala hajui ni wapi Penina alipo. Jambo hilo lilimvuruga Sana mzee Joel na kumfanya ashindwe hata kula chakula anachopikiwa na mkewe. Mzee Joel pia aliweza kuwasiliana na mkuu wa kikosi cha the killer na kumueleza jinsi vijana wake walivyoshindwa kuifanya kazi waliyoagizwa na kujikuta wakipokea kichapo kikali kutoka kwa Nolan. Mkuu yule wa kikosi cha the killer aliyejulikana kwa Jina la buffalo alipigwa na butwaa baada ya kupewa taarifa zile na mzee Joel. buffalo hajawahi kuamini kama kuna mtu yoyote anayeweza kupambana na vijana wake na akawaweza, hivyo taarifa zile zilimshangaza Sana. Buffalo akaamua ni lazima amjue huyo kijana ni nani aliyeweza kuwatandika vijana wake. "mzee hiyo kazi niachie mimi nitapambana nae mwanzo mwisho." akaongea buffalo kumwambia mzee Joel. Mzee Joel aliweza kumuelewa buffalo na kukataa simu na kumsubiri buffalo aingie kazini mwenyewe kwasababu yeye ndio mtu pekee Sasa aliyebaki wa kumtegemea. Dakika chache baada ya mzee Joel kuongea na buffalo, mzee Joel alipata taarifa kuwa kuna wageni nje wanahitaji kuonana na yeye. Mzee Joel alitoa ruhusa wageni hao wakaribishwe ndani. Kitendo bila kuchelewa wageni wale walifunguliwa geti na kukaribishwa mpaka ndani. Mzee Joel alishtuka baada ya kuona ugeni wenyewe ni wa Dickson pamoja na vijana wake wanne. "karibuni karibuni Sana." akaongea mzee Joel huku akijaribu kujichekesha japo hakuwa na amani hata kidogo. "hatuna haja ya kukaa mzee Joel, tumekuja kumchukua Penina nataka kujua kama inawezekana au haiwezekani?" akauliza Dick huku akionesha dhahiri kupandwa na hasira. "inawezekana kijana wangu tafadhali kaeni kidogo bas." akaongea mzee Joel kwa upole. "nimeshakuambia hatuna haja ya kukaa sisi tumekuja kumchukia Penina tu." akaongea Dick kwa msisitizo. "kijana wangu Dick naomba nipe muda wa siku mbili tu nitakuwa tayari nimeshakamilisha hili swala." akaongea mzee Joel kuwaambia wakina Dick. "Mzee umenipotezea Muda na umekula pesa zangu nyingi Sana, Sasa naondoka na kesho nitarudi unikabidhi Penina la sivyo pesa zangu utarudisha na utalipa Muda wangu nilioupoteza kwa ajili yako." akaongea Dick kwa jazba na kuondoka pamoja na vijana wake na kumuacha mzee Joel akitokwa na jasho jembamba. Baada ya dakika chache wakina Dick kuondoka Nolan naye aliwasili nyumbani na kumkuta baba yake akiwa na mawazo tele huku pembeni akiwa chupa ya pombe kali. "Baba shikamoo" akasilimia Nolan lakini alijua baba yake hataitikia salamu yake. Mzee Joel kweli hakuitikia salamu ya Nolan alibaki akimtizama tu kwa hasira. Nolan naye hakujali alitoa kadi tano za harusi ya Penina na Frank na kumwekea baba yake kwenye Meza iliyokuwa mbele yake. "karibu Sana Katika harusi ya Penina na mpenzi wake wa Muda mrefu Frank, wewe pamoja na rafiki Zako mnakaribishwa. " Nolan ndio alimwambia baba yake mzee Joel baada ya kumuwekea kadi zile kwenye Meza iliyokuwa mbele yake, Kisha akaondoka na kuelekea chumbani kwake. ............ Itaendelea ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
5 comments:
Hello kila mtu jina langu ni Magbon Oshimin nilikuwa nikitambua na misaada ya hiv mwaka 2004 na nimeishi nayo kwa miaka lakini namshukuru Mungu juu ya yote kwa sababu nilikutana na Dr Sagbo Diba yeye ni daktari wa mimea ambaye aliandaa dawa za mimea kwa ajili yangu na baada ya kuchukua dawa wakati anipouliza, baada ya kuchukua dawa nilikwenda kwa mtihani mwingine na ikatoka hasi usijui jinsi ninavyofurahi. Hivyo marafiki zangu wanakuambia kwamba sasa Dr Sagbo Diba ni mmoja wa daktari mkubwa wa Herbalist nchini Afrika na ana tiba ya ugonjwa huu VVU. Yeye ni vizuri kutambua kama moja ya bora caster spell nchini Afrika, nina kutumia hii kati ya kueneza habari njema kuna dawa ya dawa. Pia aliniambia kwamba ana tiba ya VVU, CANCER, DENGE, HERPES, EBOLA, ZIKA, CHICKEN POX, LEUKEMIA, TUMOR YA KIMA NA KAZI ZA MAZINGO. Tafadhali kila mtu aliye na ugonjwa huu wa mauti au anaye na mshirika wa familia au rafiki awe na uhusiano naye, ndiye Dr alimtuma kutoka kwa Mungu kutupa tumaini kumpa jaribu na utafurahi ulivyofanya. Ni ushahidi wa hai. ikiwa unahitaji msaada tafadhali usipoteze wakati wowote.Unaweza kumsiliana naye.
barua pepe (drsagbo6088@gmail.com)
WHATSAPP +2347019642881
Hello, mimi ni Rayna Ham Baada ya kuwa na uhusiano na mume wangu kwa miaka, alivunja na mimi, nilitenda kila kitu kumrudisha lakini yote ilikuwa bure, nilitaka kurudi sana kwa sababu ya upendo ninao kwa yeye, nikamsihi kwa kila kitu, nimefanya ahadi lakini alikataa. Nilielezea tatizo langu kwa rafiki yangu na alipendekeza kwamba nipaswa kuwasiliana na kipaji cha spell ambacho kinaweza kunisaidia kupiga spell kumrudisha lakini mimi ni aina ambayo haijawahi kuamini kwa spell, nilikuwa na chaguo kuliko kujaribu, mimi alipeleka barua ya barua ya barua, na akaniambia hakukuwa na shida kwamba kila kitu kitakuwa sawa kabla ya siku tatu, kwamba mzee wangu atarudi kwangu kabla ya siku tatu, alitoa spell na kushangaza siku ya pili, ilikuwa karibu 4:00 jioni. Wangu wa zamani aliniita, nilishangaa sana, nikamjibu wito na yote aliyosema ni kwamba alikuwa na huruma sana kwa kila kitu kilichotokea kwamba alitaka nirudi kwake, kwamba ananipenda sana. Nilifurahi sana na nikamwendea yeye ni jinsi tulivyoanza kuishi pamoja kwa furaha tena. Tangu wakati huo, nimefanya ahadi kwamba mtu yeyote ninayejua kuwa na tatizo la uhusiano, napenda kumsaidia mtu huyo kwa kumtaja kipaji cha pekee halisi na cha nguvu ambacho alinisaidia kwa tatizo langu. email: dr.zulugreattemple@gmail.com
unaweza kumtuma barua pepe ikiwa unahitaji msaada wake katika uhusiano wako au Uchunguzi mwingine wowote.
1) Upendo Unaelezea
2) Upendo uliopotea unaelezea
3) Talaka inaelezea
4) Inaelezea ndoa
5) Kuzuia Spell.
6) Maelekezo ya kupasuka
7) Piga Mpenzi wa zamani
8.) Unataka kupandishwa kwenye ofisi yako
9) wanataka kukidhi mpenzi wako
10) Tiba ya ugonjwa wowote unaoambukizwa
11) unataka pesa
12) unataka biashara yako kukua kwa kasi
13) unataka mtoto wako mwenyewe
Usichukue moyo wako wasiwasi hadi mwaka mpya wakati kuna suluhisho kwa hilo.Kuunganisha mtu huyu mzuri ikiwa una shida yoyote na suluhisho la kudumu
kupitia dr.zulugreattemple@gmail.com au whatsapp yake kwenye +2349075609697
Asante mimi marehemu
Haya, nimefurahi sana kuwa ndoa yangu iliyovunjika imerejeshwa na mume wangu amerudi baada ya kuniacha mimi na watoto wetu 2 kwa mwanamke mwingine. Baada ya miaka 8 ya ndoa, mimi na mume wangu tulibishana hadi mwishowe aliniacha na kuhamia California kuwa na mwanamke mwingine. Nilihisi kwamba maisha yangu yamekwisha na watoto wangu walifikiria hawatamuona baba yao tena. Nilijaribu kuwa na nguvu kwa watoto tu, lakini sikuweza kudhibiti maumivu ambayo yalitesa moyo wangu. Moyo wangu ulijaa wasiwasi na maumivu kwa sababu nilikuwa nikimpenda sana mume wangu. Ninamfikiria kila siku na usiku na siku zote natamani anirudi kwangu. Nilikasirika sana na nilihitaji msaada. Kwa hivyo nilitafuta msaada mkondoni na nikapata wavuti inayosema whitemagicmaster. , Kwa hivyo nilihisi kama ninafaa kujaribu. Niliwasiliana naye na akaniambia nifanye na nikafanya, kisha akanitengenezea moja (upendo spell) kwa ajili yangu. Masaa 28 baadaye mume wangu alinipigia kweli na kusema ananikosa sana na watoto. Ajabu sana !! Kwa hivyo alirudi kwa upendo na shangwe siku ile ile na akaomba msamaha kwa kosa lake na kwa maumivu aliyonipata mimi na watoto. Basi, tangu siku hiyo kuendelea, ndoa yetu ilikuwa na nguvu kuliko hapo awali, shukrani zote kwa mzungu. Yeye ni mwenye nguvu sana na niliamua kushiriki hadithi yangu mkondoni kwamba whitemagicmaster ni mchawi wa kweli na mwenye nguvu. Nitawaombea kila wakati kuwa anaishi muda mrefu kuwasaidia watoto wake katika wakati mgumu wakati mko hapa na unahitaji baba yako wa zamani au mumeo amehamia kwa mwanamke mwingine, au unataka Herb apate ujauzito.stop kulia, wasiliana na huyu mchawi mwenye nguvu sasa. Hapa ni mawasiliano yake: Barua pepe kwa: wightmagicmaster@gmail.com
Habari zenu. Ilikuwa ngumu sana kwangu wakati mpenzi wangu aliniacha kwa mwanamke mwingine. Niliharibiwa kihisia, nilivunjika moyo na sikujua la kufanya ili kumrudisha. Nilihangaika kwa miezi mingi na niliendelea kutafuta msaada kutoka kila mahali hadi nilipopata kujua kuhusu DR DAWN. Niliwasiliana naye na kumweleza shida zangu. Alikuwa tayari kunisaidia na kunisisitiza nifuate taratibu ili aweze kurejesha penzi kati yangu na mtu wangu na pia kuhakikisha tunarudiana wote wawili. Nilipata mahitaji yote na ilifanya kazi hiyo. Baada ya saa 48, nilipata ujumbe kutoka kwa mpenzi wangu akiniuliza tarehe. Sasa tuko pamoja tena na shukrani zote kwa DR DAWN. Anaweza kukusaidia kumrudisha mpenzi wako,
Anaweza kukusaidia na uchawi wa ujauzito,
Anaweza kukusaidia kuponya aina yoyote ya ugonjwa.
ikiwa uko tayari kuamini na kubaki na matumaini. Watumie barua pepe tu kupitia: dawnacuna314@gmail.com
WhatsApp: +2349046229159
Nilikuwa na uzoefu mgumu na wa kutisha katika mahusiano yangu ya awali na nilisubiri sana hadi nilipokutana na mume wangu na baada ya kukutana, tulipendana na kuoana. Baada ya miaka miwili ya muungano, alibadilika na kuanza tabia za ajabu na hatimaye kuniacha mimi na mtoto wetu. Nilifanya kila niwezalo kumrudisha lakini yote yalikuwa bure. Nilipata maoni mengi na kila mtu alikuwa akisema juu ya Dk Dawn. Niliwasiliana naye na alinijibu na kunipa juhudi zake zote na msaada ili kuifanya ndoa yangu ifanye kazi tena. Yeye ndiye aliyenijulisha kuwa mume wangu alichukuliwa kutoka kwangu na mwanamke mwingine na akafanya uchawi wa kuungana tena ambao uliturudisha pamoja na kurudi nyumbani kwangu na kijana wangu. Hakika, hakuna mtu huko alidanganya kuhusu Dk Dawn na matendo yake mema. Mume wangu alirudi nyumbani saa 73 baada ya kufanya kazi kama alivyoahidi. Wasiliana naye sasa na uwe na uhakika kwamba atakusaidia kuunganisha tena ndoa/uhusiano wako.
Atakusaidia kushinda kesi mahakamani au kulipiza kisasi dhidi ya adui zako.
Atakusaidia kuponya ugumba na kila aina ya magonjwa/magonjwa.
Ana suluhisho la shida yako.
Wasiliana na Whatsapp yake: +2349046229159
Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com