Home → simulizi
→ SIMULIZI YA KUSISIMUA... Ndoa Yangu Inanitesa part 10 mwisho
By brayton starpoz
Tukiwa sebuleni nilianza kumueleza Getruda. Moyo uliniuma kila nilipo kumbuka aliyonifanyia “Mke wangu kama ingenipasa kusema, nini kinacho ikera nafsi yangu ni kuni dhalilisha ndani ya kadamnasi, sio wafanyakazi wangu wa wageni, wote wanafahamu ulilolifanya, na isitoshe ile ni hotel yangu unadiriki kufanya mapenzi ukitoa kashfa ili kuinufaisha jamii, kumbuka aibu si yangu pekee, ni yetu wote.”
Sijui ni mkate sikio au nimpe kilema kwenye via vya uzazi ni mchome na moto wa umeme (hita)asiweze kufanya tendo la ndoa maisha?.Ndio itakuwa fundisho,kiherehere kitamuisha”wakati na waza cha kumfanyia, nilikatishwa na sauti.
“Mume wangu kumbuka wewe ndio uliyenitafutia mwanaume wa kuniridhisha kimapenzi, ilinijisikie nina mume, basi kama ni hivyo nami sitaki penzi la mtu mwingine wa nje. Nataka penzi lako nilikubali kwa kukuheshimu. Mwanamke kawaida hatafutiwi mume, anatafuta mwenyewe, hisia zote nilizoweka kama nipo na wewe, iweje useme na kudhalilisha, kama utashindwa leo kesho nataka talaka yangu,asubuhi na mapema, umenielewa?”Getrudaalinisemesha kwa ukali.
“Sio nimekukataza usiwe naye, kinachonikera ni kunidhalilisha na kutoa siri ya unyumba wetu, sina wivu na mapenzi yako.Ninachotaka unihifadhie siri moyoni mwako”niliinamisha kichwa chini kama kobe.
“Mume wangu nakutunzia heshima kuliko mtu yeyote duniani, nashangaa!unapo sema nainfaisha jamii. Kama angekuwa msichana mwingine asinge vumilia hata wiki moja, na washukuru wazazi kunifundisha uvumilivu ndani ya nyumba”Aliendelea kuongea,asijue nina mawazo nini moyoni.
Tukiwa kwenye mazungumzo,nilisikia simu ikiita,nilijipapasa kama ilikuwa simu yangu.Nilipotizama pembeni nilimuona Getruda akitoa simu yake kwenye pochi ndogo ya rangi nyeusi iliyojaa nakishi nyingi.
“Hallo, uko wapi?”Getruda alipokea tu,baada ya kuona jina juu ya kioo cha simu.Niligutuka nikahisi mtu huyo anamfahamu,ndio maana alimuuliza aliko.
“Aaaa..nipo Makutano bar hapa napata moja baridi moja moto.Vipi mume bwege yupo?”
“Yupo anakusalimia”Getruda alisema na kunitupia jicho ,akacheka kidogo na kuendelea, “Utakuja kutusalimia?”Getruda aliongea akiniongoa wasi wasi.
“Ninani huyo unaongea naye?”Nilijikuta nikisema wakati Getruda anaongea na simu.
“Wivu umekuzidi mume wangu.Kila kitu unataka kujua hebu chukua basi uongee naye”Getruda aliibadilikia kwa ghafla,alinyoosha mkono wake akitakakunikabidhi simu.
“Sihitaji kuongea nae,nimekuuliza kwani vibaya?.Nilifikiri ni mama amekupigia simu”
“Hapana.Nirafiki yangu”Kisha akaendelea kuongea nae.
“Samahani kwa usumbufu uliojitokeza.Mume wangu anwivu ilembaya”
“Sasa wivu wanini wakati hayawezi?”Sauti nzito upande wa pli ilisikika ikisema.
“Hata mimi nashangaa!”Getruda alidakia na kuangua kicheko kikubwa.
“Mpenzi sikia…..naomba ufike sasa hivi hapa Makutano bar”
“Mama anaumwa sana!.Ehhe mmempeleka hospitali?”Getruda aliongea maneno hayo akiwa tayari kesha kata simu.Aliendelea kuongea simu ikiwa imekatika ilimradi anipumbaze “Ana umwa na nini hasa?” alitulia sekunde mbili hivi akaendelea, “Ooo! My god .Kuna uwezekana wa kupona?”
alitulia tena sekunde kadhaa hivi, “Sawa.Ninakuja sasa hivi huko”Akajidai kukata simu.
“Vipi mbona jasho linakutoka?.Mama anaumwa na nini?”
Nilimwuliza sekunde chache alipokata simu. “Mama alidondoka ngazi akiingia kanisani”Getruda aliongea kiupole kabisa, akionekana kujizuia kulia.
“Kanisani?”
“Ndio.Na hivi sasa yupo amepelekwa hospitali ya Kcmc kwa matibabu” Safari hii alifura na alifanya kulalamika chini chini.
“Ooo! Pole sana mke wangu.Unaonaje nikaoga tukaenda wote?”
“Utanichelewesha sana”
“Basi siogi tena. Ngoja nivae twende,tena nina siku nyingi sijaenda kumsalimu”Niliongea nikiamka kitini, tayari kwa safari.
“Hapana.Nitakuletea taarifa ya hali yake.Nyumba tutamuachia nani?”
“Hilo halina shida.Nisubiri”
“Sitaki bwana. Wee kila mahali unataka kuongozana na mimi.Nimeshachoka, ngoja niende kisha kesho nikirudi nitakuja kukuchukua kwani hata kupajua hupajui.Unapafahamu pale tulipokuwa tukiishi zamani” Nilisimama kama mlingoti ,nikavuta pumzi na kuzishusha kwa nguvu.Nikatikisa kichwa na kusema “Sawa.Kama hutaki nikapajua kwenu leo ….hata kesho nitapajua”
Niliona Getruda akitoa tabasamu kubwa ,hakuishia hapo alinifuata nakunibusu shavuni “Mwaaaa”Kisha akaokota kipima joto chake,na kutoka kwa haraka akionekana mwenye wasi wasi mkubwa.Alipofika mlangoni aligeuka na kunitizama kama akinihurumia vile,sikugundua kitu ,nilibaki nimeduwaa.Akanipungia mkono na kusema “Bye bye”Nami nikapunga kono langu zito kigoigoi bila tabasamu.
Getruda alimpigia simu mteja wetu wa kila siku katika usafi,si mwingine bali Jangala. “HalloJangala tafadhali naomba unichukue hapa nyumbani”alisema baada ya simu kupokelewa.
“Sawa.Namshusha abiria hapa mjini nakuja”
“Ok”Alijibu na kukata simu.
Kama kawaida yake Jangala huwa hakaidi na hana tamaa.Aliingia na kusimama mbele ya Getruda binti Kimario.
“Shem vipi.Wapi leo pa kula kuku.Si unaelewa wiki end”Jangala alimtania Getruda.
“Ndio. Wiki end lakini kwangu imenijia vibaya .Nimepata taarifa mama yangu mgonjwa.Naomba unifikishe karibu na Makutano bar nikampe taarifa shangazi yangu.Kisha utaendelea na safari yako.Mimi nitakupigia kama nitakuhitaji tena”Getruda alidanganya.
“Sawa.Riziki ndogo ndogo hizi usininyime shem.Pole sana kwa kuuguliwa na mama yako”
“Nishapoa shem”Alimjibu kiunyonge.Getruda hakuuguliwa wala nini.Alipokuwa akienda ni Makutano bar kukutana na Mzee Jophu Kundy.
Katika mazungumzo yao walijikuta kufika Makutano bar, “Tafadhali nishushe hapa.Kuna uchochoro gari haliwezi kuingia huko.Shilingi ngapi?”
“Elfu nne zinatosha shem”Jangala alisema akimtizama Getruda.
“Punguza shem.Hujui mimi mteja wako?”
“Petroli imepanda bei sana shem. ‘Any way’ nipe tatu unusu”Jangala alisema .
Getruda alimpatia Jangala elfu tatu na mia tano,akashuka garini. “Usihaike shem.Nitafunga mwenyewe mlango.Mteja kwangu ni mtukufu”Jangala alisema baada ya kumuona Getruda anataka kufunga mlango. Getruda alijidai kama anaingia uchochoroni ili Jangala aondoke zake.Alipogeuka aliona gari la Jangala likiishia bali kabisa.Aligeuka na kurudim kuelekea kule Makutano bar.
*****************
Ndani ya makutano bar,alionekana mwanaume wa makamo.Kwa kumtizama ungeweza kukisia anamiaka hamsini ama hamsini na tano.Kichwa chake kilikuwa na mvi za kuhesabika.Uso wake ulisha anza kuwa na makunyanzi ya uzee.Alivaa suti ya kahawia,na viatu vya pembe nne ‘Four angile’.Shingoni alinyonga tai ya bluu iliyozidi kumfanya maridadi.Mkononi alivaa saa ya seiko 5 ya dhahabu.Meza aliyoketi ilijaa vyakula na vinywaji.
Mara kwa mara aliinua mkono wake wa kushoto akitizama muda,alipomaliza aligugubia glasi ya bia mdomoni na kuirudishia glasimezani.Pia muda wa kuiacha pombe ishuke vema tumboni alitupa macho yake lako la kuingilia wateja.Safari hii ilikuwa mara ya kumi kutizama lango hilo,alipohamisha macho aliyapeleka kwenye glasi ya kinywaji,akaona kama bia ilishaisha glasini,alikamata chupa ya bia na kumimina kiasi kwenye glasi ya bia.Hakuchelea aligugubia kama mikupuo miwili bila kuishusha mezani,alipomaliza akacheua kama mara tatu hivi,alihisi kilevi kikipanda vema ndani ya ubongo.Akajikuta akicheka mwenyewe
“Mimi ndiye.Mwingine hakuna”Alisema nakutizama simu yake.Aliiokota nakujaribu kupiga,simu aliyopiga iliita bila kupokelewa.
“Shiit.Kwanini hapokei?”alipayuka kwa ghadhabu.
Hakuchoka akapiga mara ya pli,iliita tena,akasikia ikipokelewa “Hallo Prety girl.Uko wapi mbona hupokei simu yangu?”
“Nakaribia jengo la Makutano hapa”
“Sawa. Nakusubiri kwa hamu wa moyo”Walikata simu.Mzee Jophu akawa habandui macho lango la kuingilia,alitaka kumwona Getruda akiingia kwa madaha.Ghafla aliona mlimbwende akiingia kwa mapana na kumfanya kila aliyeko mle ndani kumtupia jicho.Getruda hakuwa mzuri sana wa sura,lakini umbo lake na makalio ndio kichochezi kwa wanaume rijali.Kila alipovuta hatua ,makalio yake yalitikisika mithili ya mawimbi baharini.Nafiki jambo hilo ndilo lililomfanya Mzee Jophu ammezee mate mke wangu.Si kwamba na msifia kwa vile ni mke wangu,hapana.Njoo kwangu Arusha ushuhudie, ukweli wangu.Lakini kwa sasa ni mzee sana.
“Kaaaa, kakaka!”alionekana kijana mmja aliyeko nyuma ya mzee Jophu akihamaki,mfdomo ukiwa wazi kwa mshangao na mkono ukiwa umeshika mdomo wa chini,Jicho likiwa limemtoka kama ndulele iliyoiva.
“Mkindu wavona ilo ibora ledha aho”Kijana huyu alimwambia mwenzake kwa kilugha.
Akimaanisha “Mkindu umeona lisichana hilo linalo kuja hapo?”
“Nikirumo ilo!”Mkindu alijibu.
“Hilo ni balaa!” Wakacheka.
Mzee Jophu alimsindikiza Getruda kwa macho ya matamanio hadi alipomkaribia kabisa.
“Vipi.Mbona umechelewa ?”
“Mume bwege alikuwa akinichelewesha”Getruda aliongea akivuta kiti kilicho wazi.
“Achana nae.Ukisha mkabidhi fisi bucha unamatarajio gani?”
“Kuokota mifupa”Getruda alidakia.
“Hakuna kinachobaki.Fisi gani anakuachia mfupa!”Wakacheka na kupigana mabusu.Kisha akagonga meza.
“Muhudumuuu”aliita.
“Nakuja”sauti ilisikika kwa mbali kidogo.
“Kuja haraka.Watu wanapesa zao hazina pakwenda”Alisema akijiamini kabisa.Getruda alimtizama akagundua mzee Jophu alishaanza kulewa.
“Mpati wa moyo wangu kinywaji chochote anachotaka upesi”Muhudumu akaitikia sawa.
“Dada nikupatie kinywaji gani?”
“Henken ya kopo.Usisahau mrija tafadhali”
“Ya baridi au moto?”
“Aaaa! Vuguvugu.Nitapata?”
“Usihofu,utapata”Muhudumu aliondoka.
“Mpenzi nimekuita nina jambo muhimu la kukueleza,hivyo basi naomba uwemsikivu”Alitulia kidogo na kuokota glasi ya bia,hakuchelewa alimimina bia yote na kurudisha glasi tupu.Akacheua mara mbili nakuendelea “Kwanza kabla ya yote. Napenda unihakikishie kwamba unanipenda”
“Nakupenda sana mpenzi inamaana hujagundua bado?”
“Ninyi wanawake mnabadilika sana.Lazima kila tunapokutana tuulizane jambo hili”
“Si wote bwana.Unajua ninyi wanaume mkionyeshewa kama mnapendwa sana vichwa huvimba na kujiona mna matilaba ya kufanya lolote juu ya mwanamke”
“Ni baadhi ,si mimi Jophu”Akasema na kusogeza kiti jirani na Getruda.Kabla hajaendelea tayari vinywaji vililetwa,Henken ya Getruda na safari ya Mzee Jophu.
“Karibuni”Muhudumu alisema.
“Ahsante”Getruda akajibu.
“Wee binti mwite mchoma nyama tafadhali”Hakukawia kufika mchoma nyama. “Kata nyama ya kidari,ile laini…umeelewa?”
“Ndio,bosi”
“Haya futikaa”Alisema kiulevi ulevi.Akamgeukia Getruda, “Wife,sasa tuendelee na mazungumzo yetu”
“Kama umenidhihirishia unanipenda utakuwa upande wangu kwa lolote lile,si ndivyo”
“Ndivyo”
“Nikisema kitu kwa manufaa yetu lazima tusaidiane,sivyo?”
“Ndivyo”alijibu kiupole hakujua ni jambo gani anataka kuelezwa wakati huo.Kwa sasa Mzee Jophu akapunguza sauti akamweleza Getruda kwa sauti ya chini kabisa.Nafikiri alihofu watu kung’amua maneno yake.
“Getruda naomba iwe siri kubwa sana.Nataka tumuondoe Sweedy Duniani”Getruda alishituka sana kama aliyeamshwa usingizini. “Heee!”
“Usishituke laazizi wangu.Nimeamua hivyo kwa manufaa yetu pia.Kila siku kujiiba iiba ,tutajiiba mpaka lini?.Heri afe tupate uhuru….”
“Haiwezekani Jophu.Unajua dhambi ya kuua lakini?”Getruda aliuliza.
“Acha ujinga, nani kakuambia kuna dhambi.Nani aliyeenda akarudi akasema kuna adhabu kali?.Niambie”
“Kwenye maandiko takatifu,maneno hayo yapo.”Getruda alijibu akimtizama Jophu.
“Kumbe nimaandiko yaliyotungwa kama hadithi tu.Nitajie nani alikufa akafufuka na kutuonyeshea adhabu alizopata ahera?”
“Bwana acha mizengwe yako.Uhusiano wetu hauwezi kuzuilika kwa sababu ya Sweedy”
“Nitakupa chochote lakini tumuue Sweedy.Uko tayari?”Getruda alikaa kimya,safari hii alishindwa kijibu. “Nijibu basi?”Mzee Jophu alimhimiza.
“Nikujibu nini?”
“Kwani hujui.Sina jibu lolote.”Akamtizama Mzee Jophu ,na kuvutakumbukumbu ya siku ya kwanza tulipokuwa kanisani,alikumbuka maneno mengi ya mchungaji.Akanikumbuka nilipompiga busu la kwanza nikiwa namvisha pete ya ndoa.Pia akakumbuka maneno ya mama yake akimweleza juu ya unyumba wetu.Machozi yakamtiririka mashavuni bila kujijua.Akapandisha mkono wa kuume ulioshika leso na kujifuta. Mzee Jophu alinyoosha mkono na kumpatia funguo Getruda.
“Kuanzia dakika hii.Land cruiser iliyoko nje ni mali yako.”Getruda alishangaa hakuamini kile alichokuwa akikiona wakati huo.
“Mpenzi ni kweli ama ni mipombe inakusumbua akili?”
“Sijalewa wa moyo.Ninachohitaji sasa hivi, ni kutoa uhai wa huyu hanithi”Akatulia kama nukta tano hivi ,kisha akasema,“Sawa sawa?”
“Sawa”Getruda alijibu mapigo ya moyo yakimwenda mbio.Alifikiri na kuona kwanza alishachoka kukodi teksi kila siku.Naye alitaka kutembelea gari la kifahari.Alitamani akawatambishie mabinti wenziye aliosoma nao pale Mkuu Rombo.Watajuaje kwamba naye nitajiri pasipo kutembea na gari la kifahari?.Aliamini mtu akiwa na pesa huheshimika kuliko hata kitu chochote duniani.Akajikuta moyo ukipamba na furaha kali, “Acha afe bwana kwani nini bwana. Mtu kama furushi la nguo, heri afe , wangapi wameuawa na kuwaacha wake zao na mapesa kibao.Mungu nisamehe”aliwaza akilini.
Waliendelea kunywa na kula nyama choma pale.Getruda alimaliza bia yake na kuongezwa zingine mbili,tayari ubongo ukafa ganzi.Alianza kuongea sana,tena bila kujali kwamba alisikiwa na watu. “Mpenzi wangu nasema hivi…nitamuua kwa mikono yangu mwenyewe.Haina haja ya kuishi wakati hana sifa ya kumfanya hai. Eti mume, mume gani bwege kilasiku hapandi kitandani mpaka nishikwe na usingizi ndio nae apande!!!!”
“Hatakama ingelikuwa mimi.Ningetumia akili hiyo hiyo.Unafikiri ni kazi ndogo hiyo…fedheha bwana!”
Mzee Jophu na Getruda alikunjwa na kuondoka zao.Walielekea nyumba moja ya wageni ambako waliingiza gari la Gertuda na kujipumzisha.
**************
Katika maisha yangu nina kijitabia fulani cha kutotoka siku za mwisho wa wiki,isipokuwa jioni tena nikiwa na mke wangu ,Getruda. Huwa natoka katika matembezi mafupi na kurudi nyumbani.Juma pili hii ilikuwa ngumu kwangu.Kwanza mke wangu hakuwepo,usishangae nikimuita mke wangu japo sikufanikiwa kufanya tendo la ndoa.Ni mke wangu kwa sababu nimefunga ndoa kanisani.
Mawazo bado yalinizonga sana akilini,niliwaza safari ya ghafla ya mke wangu.Nilitamani sana nijue maendeleo ya wazazi wake huko mkuu Rombo.Kingine ni tatizo linaloniletea utata ndani ya ndoa yangu.Nilizidi kuwaza ,kwanini ugonjwa huo uwe kwangu tu.Kwanini usiwe kwa fulani?.Nilitamani kunywa bia lakini lakini nikaona si kutatua tatizo zaidi ya kuliongeza.
Nikiwa kwenye dimbi la mawazo,nilisikia simu ikiita,nilishituka sana.Kwa haraka nikaiendea simu ambayo niliiacha Varandani juu ya meza.Nilifikiri mambo mengi ,nikahisi aliyepiga simu alikuwa mke wangu akinipa habari za mama yake,nilitegemea kupata habari mbaya kutokana na maneno aliyoniacha nayo Getruda jana alipokurupuka akionekana wazi kuchanganywa na hali ya mama yake.Nilipofika nikaiokota simu upesi na kuipokea , “Hallo mume wangu.Umzima ?”
“Ndio.Vipi kuhusu hali ya mama.Anaendeleaje?”Nilimwuliza.
“Kidogo amepata ahueni.Kuna uvimbe gotini unamsumbua”
“Utakuja lini?”
“Aaa kesho jioni.Namsaidia kumuuguza hospitalini”
“Sawa.Nimebaki mwenyewe kama mkiwa”
“Usijali mpenzi.Upo nyumbani, na hutoki leo?”
“Ndio,nipo sitoki bila wewe.Kwanza najisikia vibaya kabisa sijui ni kwanini mpenzi”
“Pole sana mume wangu,bye”
Getruda akakata simu.
*********************
Kulikuwa na kundi la patao watu watano,aliyekuwa msemaji mkuu akiwa mzee Jophu.Pembeni aliketi Getruda na kushoto kwake mwanaume mmoja mwanye umbo kubwa,unaweza ukamfananisha na mcheza mweleka.Mikono yake minene iliyojaa na kujengeka misuli.Kushoto kwa mwanaume yule alikuwepo kijana mwingine,mrefu mwembamba lakini anasura ya kukatili.Ukimuona lazima ungemtambua kama ni muuaji.Huyu aliweka bastola kibindoni,bastola aina ya Revolver.Aliyebaki alionekana mdogo sana,ukitadhimini umri wake ni miaka kumi na tano,alionekana alikulia mitaani.Huyu ni kibaka mzoefu ,achilia mbali bangi ,sigara na dawa za kulevya, kuvuta petroli na gundi ya viatu kwake si tatizo.Mtoto huyu walimtumia sana katika matukio ya ujambazi na upelelezi wa wapi kuna pesa ,wapi tukaibe leo.
Walicheka muda mfupi tu baada ya Getruda kukata simu, “Anasemaje huyo maiti”Mzee Jophu aliuliza akiwa anamtizama Getruda kwa udadisi.
“Anasema leo yupo nyumbani hatoki,ni jambo ambalo liko wazi bila mimi habandui mguu wake.Hivyo kazi yake imeisha”
“Patamu sana hapo.Naomba vijana wangu waingie kazini.Kama nilivyo waelekeza na mfanye kwa tahadhari sana msije kubainika kama ninyi ndio mlioua.Mmenisikia?”
“Mzee usitufundishe hii ndio kazi yetu kama kazi nyingine.Tumeua sana na tutaendelea kuua.Pesa ya kazi mbele”Alisema jambazi mmoja nene lenye kifua kama pipa,lilitambulika kwa jina moja tu ‘Man Kaugo’Man Kaugo ana kasumba moja hataki kufundisha kazi ya uuaji,nasema anaielewa vema na ujuzi huo kwake ume komaa.
“Naona mchukue lita arobaini za petroli.Mzungushie nyumba yake yote na muitie kiberiti”
“Eeee!kuna vitu vyangu vya muhimu.Kwanini msimuue bilakuchoma nyumba”
“Vitu vyako nitakulipa.Tatizo ni nini?”
“Nyumba yamgu.Nilitaka mumuue nibaki na nyumba”
“Nyumba nitakununulia njiro”
“Haya, usinidanganye mpenzi”
“Sikudanganyi.Mimi na wewe kwani wa tani?”
“Hapana”
“Sasa kumbe…” akatulia kidogo kisha akasema, “Nafikiri tumemaliza makomando wangu”
“Pesa zetu bado.”
“Kiasi gani ?”
“Milioni tatu kwa kichwa kimoja”
“Ok,subirini kidogo nakuja.”
Mzee jophu alitia gari moto na kuondoka zake.alielekea benki ambako alichukua milioni tano na kuzihifadhi.Hakuchelewa alirudi. “Kamata milioni tatu hizi.Naomba mharakishe tafadhali”
“Sawa mzee.Utasikia mwenyewe mambo yakijibu”Wale vijana waliondoka zao.
Nilisikia kama watu wakiongea nje ya jengo langu,kila nilipojaribu kutega sikio kwa makini,nilishindwa kun’gamua mazungumzo yao.Nilitunguza redio kabisa ,japo nilikuwa macho lakini nilihisi bado kiko usingizini,watu hao walinikaribia dirishani ,kwambali nikasikia mmoja wapo akisema “Hili ndilo dirisha lake”
Mwingine akasema “Basi hapa tumwage petroli nyingi iliafe haraka”kilikuwa kitendo cha haraka nilisikia petroli ikimwagwa dirishani,nilikurupuka na kushituka ,nilipofungua macho kumbe nilikuwa nikiota njozi mabaya kabisa.Kukurupuka kwangu hata mke wangu Suzan ambaye tulibahatika kupata mtoto wa kiume aitwaye Samji ,alinisikia nikipiga kelele, “Nakufaaaaa”
“Nini mume wangu?”Suzan, mke wangu aliniuliza akiwa na masalio ya usingizi.Nilihisi mapigo ya moyo yakinienda mbio utadhani nilikimbia umbali mrefu bila kupumzika.
“Baba samji,ni nini mbona umepiga kelele kiasi hicho?”
“Ndoa yangu inanitesa”Niliropoka nikipikicha macho, sikuamini yale niliyoyaona nikiwa usingizini.
“Ndoa yako inakutesa kivipi?”
“Nafikiri nilikuwa nikiota ndoto ya mateso kabisa”
“Ndoto?.Nilikusikia hata wakati mwingine ukilia ukiwa usingizini.Nilikutingisha lakini huku shituika, ulikuwa ukisema Getruda Getruda .Getruda ninani?”Nilitulia kidogo nikajaribu kumkumbuka, “Getruda ni huyo mwanamke niliyemuoa, akawa ananitesa”
“Usinidanganye mume wangu.Madhambi unayofanya na mahawara wako ,ndio unayaota usiku?”
“Basi nisamehe mke wangu,ni ndoto tu.Sina mtu nimpendaye zaidi yako.Sijui njozi ya ajabu namna hii imetokea wapi.Yote niliyoota hakuna hata kimoja kilichowahi kunitokea”
Ilikuwa usiku ,majira ya saa kumi na moja.Suzan, mke wangu alinisamehe na tukaanza kusali.
MWISHo
By brayton starpoz Master
SIMULIZI YA KUSISIMUA... Ndoa Yangu Inanitesa part 10 mwisho By brayton starpoz Tukiwa sebuleni nilianza kumueleza Getruda. Moyo uliniuma kila nilipo kumbuka aliyonifanyia “Mke wangu kama ingenipasa kusema, nini kinacho ikera nafsi yangu ni kuni dhalilisha ndani ya kadamnasi, sio wafanyakazi wangu wa wageni, wote wanafahamu ulilolifanya, na isitoshe ile ni hotel yangu unadiriki kufanya mapenzi ukitoa kashfa ili kuinufaisha jamii, kumbuka aibu si yangu pekee, ni yetu wote.” Sijui ni mkate sikio au nimpe kilema kwenye via vya uzazi ni mchome na moto wa umeme (hita)asiweze kufanya tendo la ndoa maisha?.Ndio itakuwa fundisho,kiherehere kitamuisha”wakati na waza cha kumfanyia, nilikatishwa na sauti. “Mume wangu kumbuka wewe ndio uliyenitafutia mwanaume wa kuniridhisha kimapenzi, ilinijisikie nina mume, basi kama ni hivyo nami sitaki penzi la mtu mwingine wa nje. Nataka penzi lako nilikubali kwa kukuheshimu. Mwanamke kawaida hatafutiwi mume, anatafuta mwenyewe, hisia zote nilizoweka kama nipo na wewe, iweje useme na kudhalilisha, kama utashindwa leo kesho nataka talaka yangu,asubuhi na mapema, umenielewa?”Getrudaalinisemesha kwa ukali. “Sio nimekukataza usiwe naye, kinachonikera ni kunidhalilisha na kutoa siri ya unyumba wetu, sina wivu na mapenzi yako.Ninachotaka unihifadhie siri moyoni mwako”niliinamisha kichwa chini kama kobe. “Mume wangu nakutunzia heshima kuliko mtu yeyote duniani, nashangaa!unapo sema nainfaisha jamii. Kama angekuwa msichana mwingine asinge vumilia hata wiki moja, na washukuru wazazi kunifundisha uvumilivu ndani ya nyumba”Aliendelea kuongea,asijue nina mawazo nini moyoni. Tukiwa kwenye mazungumzo,nilisikia simu ikiita,nilijipapasa kama ilikuwa simu yangu.Nilipotizama pembeni nilimuona Getruda akitoa simu yake kwenye pochi ndogo ya rangi nyeusi iliyojaa nakishi nyingi. “Hallo, uko wapi?”Getruda alipokea tu,baada ya kuona jina juu ya kioo cha simu.Niligutuka nikahisi mtu huyo anamfahamu,ndio maana alimuuliza aliko. “Aaaa..nipo Makutano bar hapa napata moja baridi moja moto.Vipi mume bwege yupo?” “Yupo anakusalimia”Getruda alisema na kunitupia jicho ,akacheka kidogo na kuendelea, “Utakuja kutusalimia?”Getruda aliongea akiniongoa wasi wasi. “Ninani huyo unaongea naye?”Nilijikuta nikisema wakati Getruda anaongea na simu. “Wivu umekuzidi mume wangu.Kila kitu unataka kujua hebu chukua basi uongee naye”Getruda aliibadilikia kwa ghafla,alinyoosha mkono wake akitakakunikabidhi simu. “Sihitaji kuongea nae,nimekuuliza kwani vibaya?.Nilifikiri ni mama amekupigia simu” “Hapana.Nirafiki yangu”Kisha akaendelea kuongea nae. “Samahani kwa usumbufu uliojitokeza.Mume wangu anwivu ilembaya” “Sasa wivu wanini wakati hayawezi?”Sauti nzito upande wa pli ilisikika ikisema. “Hata mimi nashangaa!”Getruda alidakia na kuangua kicheko kikubwa. “Mpenzi sikia…..naomba ufike sasa hivi hapa Makutano bar” “Mama anaumwa sana!.Ehhe mmempeleka hospitali?”Getruda aliongea maneno hayo akiwa tayari kesha kata simu.Aliendelea kuongea simu ikiwa imekatika ilimradi anipumbaze “Ana umwa na nini hasa?” alitulia sekunde mbili hivi akaendelea, “Ooo! My god .Kuna uwezekana wa kupona?” alitulia tena sekunde kadhaa hivi, “Sawa.Ninakuja sasa hivi huko”Akajidai kukata simu. “Vipi mbona jasho linakutoka?.Mama anaumwa na nini?” Nilimwuliza sekunde chache alipokata simu. “Mama alidondoka ngazi akiingia kanisani”Getruda aliongea kiupole kabisa, akionekana kujizuia kulia. “Kanisani?” “Ndio.Na hivi sasa yupo amepelekwa hospitali ya Kcmc kwa matibabu” Safari hii alifura na alifanya kulalamika chini chini. “Ooo! Pole sana mke wangu.Unaonaje nikaoga tukaenda wote?” “Utanichelewesha sana” “Basi siogi tena. Ngoja nivae twende,tena nina siku nyingi sijaenda kumsalimu”Niliongea nikiamka kitini, tayari kwa safari. “Hapana.Nitakuletea taarifa ya hali yake.Nyumba tutamuachia nani?” “Hilo halina shida.Nisubiri” “Sitaki bwana. Wee kila mahali unataka kuongozana na mimi.Nimeshachoka, ngoja niende kisha kesho nikirudi nitakuja kukuchukua kwani hata kupajua hupajui.Unapafahamu pale tulipokuwa tukiishi zamani” Nilisimama kama mlingoti ,nikavuta pumzi na kuzishusha kwa nguvu.Nikatikisa kichwa na kusema “Sawa.Kama hutaki nikapajua kwenu leo ….hata kesho nitapajua” Niliona Getruda akitoa tabasamu kubwa ,hakuishia hapo alinifuata nakunibusu shavuni “Mwaaaa”Kisha akaokota kipima joto chake,na kutoka kwa haraka akionekana mwenye wasi wasi mkubwa.Alipofika mlangoni aligeuka na kunitizama kama akinihurumia vile,sikugundua kitu ,nilibaki nimeduwaa.Akanipungia mkono na kusema “Bye bye”Nami nikapunga kono langu zito kigoigoi bila tabasamu. Getruda alimpigia simu mteja wetu wa kila siku katika usafi,si mwingine bali Jangala. “HalloJangala tafadhali naomba unichukue hapa nyumbani”alisema baada ya simu kupokelewa. “Sawa.Namshusha abiria hapa mjini nakuja” “Ok”Alijibu na kukata simu. Kama kawaida yake Jangala huwa hakaidi na hana tamaa.Aliingia na kusimama mbele ya Getruda binti Kimario. “Shem vipi.Wapi leo pa kula kuku.Si unaelewa wiki end”Jangala alimtania Getruda. “Ndio. Wiki end lakini kwangu imenijia vibaya .Nimepata taarifa mama yangu mgonjwa.Naomba unifikishe karibu na Makutano bar nikampe taarifa shangazi yangu.Kisha utaendelea na safari yako.Mimi nitakupigia kama nitakuhitaji tena”Getruda alidanganya. “Sawa.Riziki ndogo ndogo hizi usininyime shem.Pole sana kwa kuuguliwa na mama yako” “Nishapoa shem”Alimjibu kiunyonge.Getruda hakuuguliwa wala nini.Alipokuwa akienda ni Makutano bar kukutana na Mzee Jophu Kundy. Katika mazungumzo yao walijikuta kufika Makutano bar, “Tafadhali nishushe hapa.Kuna uchochoro gari haliwezi kuingia huko.Shilingi ngapi?” “Elfu nne zinatosha shem”Jangala alisema akimtizama Getruda. “Punguza shem.Hujui mimi mteja wako?” “Petroli imepanda bei sana shem. ‘Any way’ nipe tatu unusu”Jangala alisema . Getruda alimpatia Jangala elfu tatu na mia tano,akashuka garini. “Usihaike shem.Nitafunga mwenyewe mlango.Mteja kwangu ni mtukufu”Jangala alisema baada ya kumuona Getruda anataka kufunga mlango. Getruda alijidai kama anaingia uchochoroni ili Jangala aondoke zake.Alipogeuka aliona gari la Jangala likiishia bali kabisa.Aligeuka na kurudim kuelekea kule Makutano bar. ***************** Ndani ya makutano bar,alionekana mwanaume wa makamo.Kwa kumtizama ungeweza kukisia anamiaka hamsini ama hamsini na tano.Kichwa chake kilikuwa na mvi za kuhesabika.Uso wake ulisha anza kuwa na makunyanzi ya uzee.Alivaa suti ya kahawia,na viatu vya pembe nne ‘Four angile’.Shingoni alinyonga tai ya bluu iliyozidi kumfanya maridadi.Mkononi alivaa saa ya seiko 5 ya dhahabu.Meza aliyoketi ilijaa vyakula na vinywaji. Mara kwa mara aliinua mkono wake wa kushoto akitizama muda,alipomaliza aligugubia glasi ya bia mdomoni na kuirudishia glasimezani.Pia muda wa kuiacha pombe ishuke vema tumboni alitupa macho yake lako la kuingilia wateja.Safari hii ilikuwa mara ya kumi kutizama lango hilo,alipohamisha macho aliyapeleka kwenye glasi ya kinywaji,akaona kama bia ilishaisha glasini,alikamata chupa ya bia na kumimina kiasi kwenye glasi ya bia.Hakuchelea aligugubia kama mikupuo miwili bila kuishusha mezani,alipomaliza akacheua kama mara tatu hivi,alihisi kilevi kikipanda vema ndani ya ubongo.Akajikuta akicheka mwenyewe “Mimi ndiye.Mwingine hakuna”Alisema nakutizama simu yake.Aliiokota nakujaribu kupiga,simu aliyopiga iliita bila kupokelewa. “Shiit.Kwanini hapokei?”alipayuka kwa ghadhabu. Hakuchoka akapiga mara ya pli,iliita tena,akasikia ikipokelewa “Hallo Prety girl.Uko wapi mbona hupokei simu yangu?” “Nakaribia jengo la Makutano hapa” “Sawa. Nakusubiri kwa hamu wa moyo”Walikata simu.Mzee Jophu akawa habandui macho lango la kuingilia,alitaka kumwona Getruda akiingia kwa madaha.Ghafla aliona mlimbwende akiingia kwa mapana na kumfanya kila aliyeko mle ndani kumtupia jicho.Getruda hakuwa mzuri sana wa sura,lakini umbo lake na makalio ndio kichochezi kwa wanaume rijali.Kila alipovuta hatua ,makalio yake yalitikisika mithili ya mawimbi baharini.Nafiki jambo hilo ndilo lililomfanya Mzee Jophu ammezee mate mke wangu.Si kwamba na msifia kwa vile ni mke wangu,hapana.Njoo kwangu Arusha ushuhudie, ukweli wangu.Lakini kwa sasa ni mzee sana. “Kaaaa, kakaka!”alionekana kijana mmja aliyeko nyuma ya mzee Jophu akihamaki,mfdomo ukiwa wazi kwa mshangao na mkono ukiwa umeshika mdomo wa chini,Jicho likiwa limemtoka kama ndulele iliyoiva. “Mkindu wavona ilo ibora ledha aho”Kijana huyu alimwambia mwenzake kwa kilugha. Akimaanisha “Mkindu umeona lisichana hilo linalo kuja hapo?” “Nikirumo ilo!”Mkindu alijibu. “Hilo ni balaa!” Wakacheka. Mzee Jophu alimsindikiza Getruda kwa macho ya matamanio hadi alipomkaribia kabisa. “Vipi.Mbona umechelewa ?” “Mume bwege alikuwa akinichelewesha”Getruda aliongea akivuta kiti kilicho wazi. “Achana nae.Ukisha mkabidhi fisi bucha unamatarajio gani?” “Kuokota mifupa”Getruda alidakia. “Hakuna kinachobaki.Fisi gani anakuachia mfupa!”Wakacheka na kupigana mabusu.Kisha akagonga meza. “Muhudumuuu”aliita. “Nakuja”sauti ilisikika kwa mbali kidogo. “Kuja haraka.Watu wanapesa zao hazina pakwenda”Alisema akijiamini kabisa.Getruda alimtizama akagundua mzee Jophu alishaanza kulewa. “Mpati wa moyo wangu kinywaji chochote anachotaka upesi”Muhudumu akaitikia sawa. “Dada nikupatie kinywaji gani?” “Henken ya kopo.Usisahau mrija tafadhali” “Ya baridi au moto?” “Aaaa! Vuguvugu.Nitapata?” “Usihofu,utapata”Muhudumu aliondoka. “Mpenzi nimekuita nina jambo muhimu la kukueleza,hivyo basi naomba uwemsikivu”Alitulia kidogo na kuokota glasi ya bia,hakuchelewa alimimina bia yote na kurudisha glasi tupu.Akacheua mara mbili nakuendelea “Kwanza kabla ya yote. Napenda unihakikishie kwamba unanipenda” “Nakupenda sana mpenzi inamaana hujagundua bado?” “Ninyi wanawake mnabadilika sana.Lazima kila tunapokutana tuulizane jambo hili” “Si wote bwana.Unajua ninyi wanaume mkionyeshewa kama mnapendwa sana vichwa huvimba na kujiona mna matilaba ya kufanya lolote juu ya mwanamke” “Ni baadhi ,si mimi Jophu”Akasema na kusogeza kiti jirani na Getruda.Kabla hajaendelea tayari vinywaji vililetwa,Henken ya Getruda na safari ya Mzee Jophu. “Karibuni”Muhudumu alisema. “Ahsante”Getruda akajibu. “Wee binti mwite mchoma nyama tafadhali”Hakukawia kufika mchoma nyama. “Kata nyama ya kidari,ile laini…umeelewa?” “Ndio,bosi” “Haya futikaa”Alisema kiulevi ulevi.Akamgeukia Getruda, “Wife,sasa tuendelee na mazungumzo yetu” “Kama umenidhihirishia unanipenda utakuwa upande wangu kwa lolote lile,si ndivyo” “Ndivyo” “Nikisema kitu kwa manufaa yetu lazima tusaidiane,sivyo?” “Ndivyo”alijibu kiupole hakujua ni jambo gani anataka kuelezwa wakati huo.Kwa sasa Mzee Jophu akapunguza sauti akamweleza Getruda kwa sauti ya chini kabisa.Nafikiri alihofu watu kung’amua maneno yake. “Getruda naomba iwe siri kubwa sana.Nataka tumuondoe Sweedy Duniani”Getruda alishituka sana kama aliyeamshwa usingizini. “Heee!” “Usishituke laazizi wangu.Nimeamua hivyo kwa manufaa yetu pia.Kila siku kujiiba iiba ,tutajiiba mpaka lini?.Heri afe tupate uhuru….” “Haiwezekani Jophu.Unajua dhambi ya kuua lakini?”Getruda aliuliza. “Acha ujinga, nani kakuambia kuna dhambi.Nani aliyeenda akarudi akasema kuna adhabu kali?.Niambie” “Kwenye maandiko takatifu,maneno hayo yapo.”Getruda alijibu akimtizama Jophu. “Kumbe nimaandiko yaliyotungwa kama hadithi tu.Nitajie nani alikufa akafufuka na kutuonyeshea adhabu alizopata ahera?” “Bwana acha mizengwe yako.Uhusiano wetu hauwezi kuzuilika kwa sababu ya Sweedy” “Nitakupa chochote lakini tumuue Sweedy.Uko tayari?”Getruda alikaa kimya,safari hii alishindwa kijibu. “Nijibu basi?”Mzee Jophu alimhimiza. “Nikujibu nini?” “Kwani hujui.Sina jibu lolote.”Akamtizama Mzee Jophu ,na kuvutakumbukumbu ya siku ya kwanza tulipokuwa kanisani,alikumbuka maneno mengi ya mchungaji.Akanikumbuka nilipompiga busu la kwanza nikiwa namvisha pete ya ndoa.Pia akakumbuka maneno ya mama yake akimweleza juu ya unyumba wetu.Machozi yakamtiririka mashavuni bila kujijua.Akapandisha mkono wa kuume ulioshika leso na kujifuta. Mzee Jophu alinyoosha mkono na kumpatia funguo Getruda. “Kuanzia dakika hii.Land cruiser iliyoko nje ni mali yako.”Getruda alishangaa hakuamini kile alichokuwa akikiona wakati huo. “Mpenzi ni kweli ama ni mipombe inakusumbua akili?” “Sijalewa wa moyo.Ninachohitaji sasa hivi, ni kutoa uhai wa huyu hanithi”Akatulia kama nukta tano hivi ,kisha akasema,“Sawa sawa?” “Sawa”Getruda alijibu mapigo ya moyo yakimwenda mbio.Alifikiri na kuona kwanza alishachoka kukodi teksi kila siku.Naye alitaka kutembelea gari la kifahari.Alitamani akawatambishie mabinti wenziye aliosoma nao pale Mkuu Rombo.Watajuaje kwamba naye nitajiri pasipo kutembea na gari la kifahari?.Aliamini mtu akiwa na pesa huheshimika kuliko hata kitu chochote duniani.Akajikuta moyo ukipamba na furaha kali, “Acha afe bwana kwani nini bwana. Mtu kama furushi la nguo, heri afe , wangapi wameuawa na kuwaacha wake zao na mapesa kibao.Mungu nisamehe”aliwaza akilini. Waliendelea kunywa na kula nyama choma pale.Getruda alimaliza bia yake na kuongezwa zingine mbili,tayari ubongo ukafa ganzi.Alianza kuongea sana,tena bila kujali kwamba alisikiwa na watu. “Mpenzi wangu nasema hivi…nitamuua kwa mikono yangu mwenyewe.Haina haja ya kuishi wakati hana sifa ya kumfanya hai. Eti mume, mume gani bwege kilasiku hapandi kitandani mpaka nishikwe na usingizi ndio nae apande!!!!” “Hatakama ingelikuwa mimi.Ningetumia akili hiyo hiyo.Unafikiri ni kazi ndogo hiyo…fedheha bwana!” Mzee Jophu na Getruda alikunjwa na kuondoka zao.Walielekea nyumba moja ya wageni ambako waliingiza gari la Gertuda na kujipumzisha. ************** Katika maisha yangu nina kijitabia fulani cha kutotoka siku za mwisho wa wiki,isipokuwa jioni tena nikiwa na mke wangu ,Getruda. Huwa natoka katika matembezi mafupi na kurudi nyumbani.Juma pili hii ilikuwa ngumu kwangu.Kwanza mke wangu hakuwepo,usishangae nikimuita mke wangu japo sikufanikiwa kufanya tendo la ndoa.Ni mke wangu kwa sababu nimefunga ndoa kanisani. Mawazo bado yalinizonga sana akilini,niliwaza safari ya ghafla ya mke wangu.Nilitamani sana nijue maendeleo ya wazazi wake huko mkuu Rombo.Kingine ni tatizo linaloniletea utata ndani ya ndoa yangu.Nilizidi kuwaza ,kwanini ugonjwa huo uwe kwangu tu.Kwanini usiwe kwa fulani?.Nilitamani kunywa bia lakini lakini nikaona si kutatua tatizo zaidi ya kuliongeza. Nikiwa kwenye dimbi la mawazo,nilisikia simu ikiita,nilishituka sana.Kwa haraka nikaiendea simu ambayo niliiacha Varandani juu ya meza.Nilifikiri mambo mengi ,nikahisi aliyepiga simu alikuwa mke wangu akinipa habari za mama yake,nilitegemea kupata habari mbaya kutokana na maneno aliyoniacha nayo Getruda jana alipokurupuka akionekana wazi kuchanganywa na hali ya mama yake.Nilipofika nikaiokota simu upesi na kuipokea , “Hallo mume wangu.Umzima ?” “Ndio.Vipi kuhusu hali ya mama.Anaendeleaje?”Nilimwuliza. “Kidogo amepata ahueni.Kuna uvimbe gotini unamsumbua” “Utakuja lini?” “Aaa kesho jioni.Namsaidia kumuuguza hospitalini” “Sawa.Nimebaki mwenyewe kama mkiwa” “Usijali mpenzi.Upo nyumbani, na hutoki leo?” “Ndio,nipo sitoki bila wewe.Kwanza najisikia vibaya kabisa sijui ni kwanini mpenzi” “Pole sana mume wangu,bye” Getruda akakata simu. ********************* Kulikuwa na kundi la patao watu watano,aliyekuwa msemaji mkuu akiwa mzee Jophu.Pembeni aliketi Getruda na kushoto kwake mwanaume mmoja mwanye umbo kubwa,unaweza ukamfananisha na mcheza mweleka.Mikono yake minene iliyojaa na kujengeka misuli.Kushoto kwa mwanaume yule alikuwepo kijana mwingine,mrefu mwembamba lakini anasura ya kukatili.Ukimuona lazima ungemtambua kama ni muuaji.Huyu aliweka bastola kibindoni,bastola aina ya Revolver.Aliyebaki alionekana mdogo sana,ukitadhimini umri wake ni miaka kumi na tano,alionekana alikulia mitaani.Huyu ni kibaka mzoefu ,achilia mbali bangi ,sigara na dawa za kulevya, kuvuta petroli na gundi ya viatu kwake si tatizo.Mtoto huyu walimtumia sana katika matukio ya ujambazi na upelelezi wa wapi kuna pesa ,wapi tukaibe leo. Walicheka muda mfupi tu baada ya Getruda kukata simu, “Anasemaje huyo maiti”Mzee Jophu aliuliza akiwa anamtizama Getruda kwa udadisi. “Anasema leo yupo nyumbani hatoki,ni jambo ambalo liko wazi bila mimi habandui mguu wake.Hivyo kazi yake imeisha” “Patamu sana hapo.Naomba vijana wangu waingie kazini.Kama nilivyo waelekeza na mfanye kwa tahadhari sana msije kubainika kama ninyi ndio mlioua.Mmenisikia?” “Mzee usitufundishe hii ndio kazi yetu kama kazi nyingine.Tumeua sana na tutaendelea kuua.Pesa ya kazi mbele”Alisema jambazi mmoja nene lenye kifua kama pipa,lilitambulika kwa jina moja tu ‘Man Kaugo’Man Kaugo ana kasumba moja hataki kufundisha kazi ya uuaji,nasema anaielewa vema na ujuzi huo kwake ume komaa. “Naona mchukue lita arobaini za petroli.Mzungushie nyumba yake yote na muitie kiberiti” “Eeee!kuna vitu vyangu vya muhimu.Kwanini msimuue bilakuchoma nyumba” “Vitu vyako nitakulipa.Tatizo ni nini?” “Nyumba yamgu.Nilitaka mumuue nibaki na nyumba” “Nyumba nitakununulia njiro” “Haya, usinidanganye mpenzi” “Sikudanganyi.Mimi na wewe kwani wa tani?” “Hapana” “Sasa kumbe…” akatulia kidogo kisha akasema, “Nafikiri tumemaliza makomando wangu” “Pesa zetu bado.” “Kiasi gani ?” “Milioni tatu kwa kichwa kimoja” “Ok,subirini kidogo nakuja.” Mzee jophu alitia gari moto na kuondoka zake.alielekea benki ambako alichukua milioni tano na kuzihifadhi.Hakuchelewa alirudi. “Kamata milioni tatu hizi.Naomba mharakishe tafadhali” “Sawa mzee.Utasikia mwenyewe mambo yakijibu”Wale vijana waliondoka zao. Nilisikia kama watu wakiongea nje ya jengo langu,kila nilipojaribu kutega sikio kwa makini,nilishindwa kun’gamua mazungumzo yao.Nilitunguza redio kabisa ,japo nilikuwa macho lakini nilihisi bado kiko usingizini,watu hao walinikaribia dirishani ,kwambali nikasikia mmoja wapo akisema “Hili ndilo dirisha lake” Mwingine akasema “Basi hapa tumwage petroli nyingi iliafe haraka”kilikuwa kitendo cha haraka nilisikia petroli ikimwagwa dirishani,nilikurupuka na kushituka ,nilipofungua macho kumbe nilikuwa nikiota njozi mabaya kabisa.Kukurupuka kwangu hata mke wangu Suzan ambaye tulibahatika kupata mtoto wa kiume aitwaye Samji ,alinisikia nikipiga kelele, “Nakufaaaaa” “Nini mume wangu?”Suzan, mke wangu aliniuliza akiwa na masalio ya usingizi.Nilihisi mapigo ya moyo yakinienda mbio utadhani nilikimbia umbali mrefu bila kupumzika. “Baba samji,ni nini mbona umepiga kelele kiasi hicho?” “Ndoa yangu inanitesa”Niliropoka nikipikicha macho, sikuamini yale niliyoyaona nikiwa usingizini. “Ndoa yako inakutesa kivipi?” “Nafikiri nilikuwa nikiota ndoto ya mateso kabisa” “Ndoto?.Nilikusikia hata wakati mwingine ukilia ukiwa usingizini.Nilikutingisha lakini huku shituika, ulikuwa ukisema Getruda Getruda .Getruda ninani?”Nilitulia kidogo nikajaribu kumkumbuka, “Getruda ni huyo mwanamke niliyemuoa, akawa ananitesa” “Usinidanganye mume wangu.Madhambi unayofanya na mahawara wako ,ndio unayaota usiku?” “Basi nisamehe mke wangu,ni ndoto tu.Sina mtu nimpendaye zaidi yako.Sijui njozi ya ajabu namna hii imetokea wapi.Yote niliyoota hakuna hata kimoja kilichowahi kunitokea” Ilikuwa usiku ,majira ya saa kumi na moja.Suzan, mke wangu alinisamehe na tukaanza kusali. MWISHo By brayton starpoz Master
Artikel Terkait
*LOVE BITE EP 04* ILIPOISHIA…… Aliongea Jothan huku machozi yakimlenga lenga. Hakika ni uamuzi mgumu aliouchukua kwakua aliamini ilikuwa ni mtihani mkubwa katika mapokezi ya mlengwa. Alipoinua macho yake kumtazama Prisca, tayari mashavu ya prisca yalishalowana kwa machozi huku macho yakiwa mekundu. Kilio cha kwiki kilianza kusikika na kumfanya Jothan kuingiwa na imani baada ya kumtaza mpenzi wake huyo anaye amua kumuacha bila kosa lolote. SONGA NAYO…………….. Machozi na kilio cha kwikwi kiliendelea kwa dakika kadhaa, Prisca alimuangalia Jothan ambaye alikua ana muonea aibu wakati huo. Hakuamini kuwa ndiye yeye aliyetamka maneno yale,. “kwanini mimi?…. kwanini Jothan umeamua kuzichezea hisia zangu kwa miaka yote hiyo niliyokuwa na wewe kumbe ulikuwa huna malengo ya kuwa na mimi. Kwanini Jothan umeamua kunifanyia hivyo?” aliongea Prisca huku analia. “sorry Prisca. Unafikiri ningefanyaje kwa hali niliyokuwa nayo hivi sasa. Sina jinsi japokuwa bado nakupenda sana. Ningekuwa mtu mwengine hivi sasa ningeendelea kuwachanganya wote wawili. Ila roho huwa inanisuta kufanya hivyo kwakua hata mimi sihitaji kuchezewa hisia zangu. Naomba kubaliana tu na maamuzi yangu japokuwa unaumia.” Aliongea Jothan huku na yeye akijifuta machozi yaliyomdondoka kutokana na hali aliyokuwa nayo Prisca inavyosikitisha. “thank you for everything.” Aliongea Prisca na kunyanyuka na kuondoka. Alimuacha Jothan ambaye alijiinamia na kujilaumu kwa alichokifanya. Akili nyingine ilimwambia kama mwanaume wa ukweli na mwenye msimamo basi alifanya maamuzi sahihi na ya busara. Alirudi nyumbani na kumkuta Shani amejaa tele nyumbani kwake. Alipofika tu, Shani alimfuata na kumkumbatia. Ingawaje Jothan alijichekesha, lakini Shani aligundua kuwa hakuwa sawa. “una nini mume wangu?. Aliuliza Shani baada ya kumuangalia usoni Jothan. “kawaida tu mke wangu.. kwani naonyesha nina tatizo?” aliuliza Jothan kuhakikisha alichokisikia kutoka kwa Shani. “sura yako inaonyesha kama ullikuwa unalia au ulikuwa unahuzunika muda si mrefu.” Aliongea Shani na kumfanya Jothan kumuangalia usoni Shani. “kichwa kilikua kinanigonga sana, hata hivyo sasa hivi niko sawa.” Aliongopa Jothan “pole mume wangu, kama bado kinaendelea we niambie nikununulie panadol au nikusindikize hospital… usidharau mume wangu.” Aliongea Shani huku akionyesha kwa alikua anajali sana afya ya mwenzi wake. “usijali, niko sawa tu.” Aliongea Jothan na kuingia chumbani kwake. Alijilaza na kuwaza yaliyotokea muda mfupi uliopita. Aliamua kupiga moyo konde na kuona yote yalikuwa ni majaribu tu. Maisha yalikuwa mazuri huku kila mmoja akifurahia uwepo wa mwenzake. Hata Jothan mwenyewe alikiri kuwa uamuzi wake ulikuwa sahihi sana kumchagua Shani katika maisha yake badala ya Prisca ambaye mpaka kipindi hicho alikuwa ameshakatisha mawasiliano naye. Shani naye alijitahidi kuhakikisha anafanya yale yote apendayo Jothan na kumteka Jothan kisawa sawa. Ilkuwa akiongelewa mwanamke bora basi Jothan alilipitisha jina la Shani bila kuangalia kuwa alikuwa na nani au alizungukwa na wasichana wazuri. Alitumia muda mwingi kuwa karibu na Shani. Hata kama alikua anataka kwenda kutanua, basi Shani alikuwa ubavuni kila walipoenda. Siku moja ambayo ilikua ni mwisho wa wiki, Jothan aliamua kulala tu Jumaapili hiyo kutokana na uchovu aliokuwa nao wa jana yake kwakua walienda club yeye na Shani na kurudi asubuhi kabisa. Nyumbani kwake aligonga hodi mgeni mmoja wa kike na kufunguliwa mlango na Shani ambaye alishaamka na alikuwa anfanya usafi nyumbani kwake. “za saa hizi dada.” Alisalimia yule mgeni ambaye alionyesha wazi kuwa alikua amechoka kutokana na mimba kubwa aliyokuwa nayo. “salama tu.” Alijibu Shani na kumsikiliza huyo msichana shida yake. “sijui nimemkuta mwenye nyumba hii?” aliuliza yule dada na kumuangalia Shani aliyekuwa makini akimsikiliza. “mwenyewe kalala, ila naweza kukusaidia kama hutajali kunieleza shida yako.” Aliongea Shani na kumuangalia yule dada. “ni vyema kama nita onana nae mwenyewe.” Aliongea yule dada na kumfanya Shani amkaribishe ndani. Kwakua Shani alikua anaandaa chai, hakuona ubaya kuandaa ya kutosha na kumkaribisha yule mgeni aliyekunywa chai kama anafukuzwa kutokana na njaa aliyokuwa nayo. Shani aligundua njaa aliyokuwa nayo mgeni huyo na kumuongezea vyakula mpaka alipohakikisha ameshiba ndio akaamua kumfuata na kumuuliza maswali machache wakati wanamsubiri bwana mkuwa aamke. “tunsubiri aamke, si unajua alikesha jana kwa hiyo sio vizuri kumuamsha mtu akiwa katika uchovu kama huo.” Aliongea Shani na wazo hilo likapitishwa na yule mgeni. Jothan aliamka na kwenda kuoga. Alivaa nguo zake nyepesi na kwenda sebuleni na kumkuta mgeni aliyekuwa anamsubiri. Yule dada alipogeuza shingo kumuangalia Jothan, macho yalimtoka na kujikuta mshangao mkuu umempata. “wewe, umefuata nini nyumbani kwangu?” aliuliza Jothan kwa hasira. Yule mgeni hakua na la kujibu zaidi ya kujiinamia. “na wewe unawakaribishwa watu humu ndani wengine ni nyoka kama huyu mwanamke.” Aliongea Jothan na kumuweka Shani kwenye bumbuwazi. “mbona sielewi, maana mimi aliniambia ni mgeni wako ndio maana nikaona si vibaya kumkaribisha ndani.” Alijitetea Shani. “mimi simjui huyu, .. kwani wewe msichana unaitwa nani?” aliuliza Jothan na kwenda kukaa kwenye moja ya sofa za pale sebuleni. “BAHATI.” Alijibu yule mgeni kwa aibu na kuangalia chini. “WHO A BAHATI BAY THE WAY??” Aliongea Jothan na kumfanya Bahati kupiga magoti mbele yake na kuanza kulia kwa uchungu. “sihitaji kupigiwa magoti mama, mpigie magoti mungu wako na umuombe msamaha kwa ulichokitenda kwangu mimi.” Aliongea Jothan na kumuinua Shani pale chini. “naomba unisamehe, nimehadaika tu na jiji na hivi sasa limeshanifunza Jothan.” Aliongea Bahati huku analia. “leo hii unamjua Jothan wewe?.. si ulikua hunijui wewe?.. nani kakutajia jina langu?” aliuliza Jothan maswali mfulumizo yaliyomshinda Bahati kujibu na kubaki analia tu. “nyamaza kulia dada, kwani tatizo ni nini?.. niewekeni wazi jamani.” Aliongea Shani baada ya kukaa kimya muda mrefu. “sikiliza mke wangu, huyu dada ni mpumbavu na hana akili hata kidogo. Alikuwa na matatizo ya macho yaliyomsababishia upofu na hakuwa anaona hapo mwanzo. Mimi kwa imani yangu nikamchukua kutoka kwa mama yake Arusha na kuja naye hapa Dar kwa nia njema ya kumtibu. Sikuhitaji chochote kutoka kwake. Ila malipo aliyokuja kunilipa haki ya mungu kanifanya moyo wangu uwe na sugu na kuwa mgumu kuwasaidia wengine. Yaani alipopata macho ndio akaniona mimi takataka baada ya bosi wangu kumtaka. Siku niliyokutana naye akajifanya sauti yangu kaisahau. Yaani hata nilipojitambulisha bado akijifanya hanijui. Nikasamehe na kuachana naye, bado akaona haitoshi akaamua kunifanyia fitina mpaka nikafukuzwa kazi bila kosa. Sasa huyu utamuita mtu au kiatu tena kisichokuwa na kamba?” Aliongeea Jothan maneno yaliyomchoma Bahati na kumfanya aanze kulia kwa sauti kubwa zaidi ya aliyokuwa analia. “msamehe mume wangu, mungu kakujaalia umepata kazi nyingine. Na hujui kakuepusha na nini kukutoa kule. Na huyu adhabu yake ndio hii. Maana amepewa mimba na ametimuliwa. Hana msaada mwingine zaidi yako wewe. Msamehe tu mume wangu.” Aliongea Shani na kumsogelea Jothan aliyekuwa kafura kwa hasira na kuanza kumshika shika. Jothan alivuta pumzi ndefu kisha akamuangalia Bahati. “ni msaada gani unaotaka kutoka kwangu?” aliuliza Jothan na kumfanya Bahati kufuta machozi. “naomba unisaidie kunipeleka tu Arusha kwa mama yangu.” Aliongea Bahati huku analia. Kauli hiyo iliwaigia wote wawili. Ghafla walishangaa kumuona Jothan machozi yanamtoka kwa jinsi alivyokuwa anamuonea imani msichana mzuri walivyomtumia vibaya na kuwa kama kituko. Hakua Bahati yule kipofu mwenye bashasha usoni kila wakati. Sasa hivi mashavu yalimuingia ndani, nywele zake hazitazamiki mara mbili. Ngozi yake ilijaa makovu ya kupigwa kila sehemu. Jothan alijikuta ameguswa na kuanza kulia kwa sauti. Alinyanyuka huku analia na kumfuata Bahati na kumuinua kichwa chake na kuitazama sura yake iliyokuwa imelowa machozi na kuvimba kutokana na kulia kwa muda mrefu. “utakaa hapa mpaka utakapojifungua na kurudisha afya yako… pole sana kwa yaliyo kukuta.” Hatimaye aliongea maneno hayo yaliyomfanya Bahati kumkumbatia Jothan bila kujali uwepo wa mke wake pale. Wali muhurumia Bahati na kumpa chumba mule ndani. Siku tatu baadae, Bahati alipatwa na uchungu na kumuwahisha hospitali ya kulipia iliyopo kinondoni. Uchungu ulidumu kwa siku mbili mfululizo na kwa bahati nzuri Bahati alifanikiwa kujifungua salama mtoto wa kike. Aliwashukuru sana Shani na Jothan kwa utu wao waliouonyesha juu yake, maana walikuwa nae bega kwa bega na kuhakikisha kuwa anajifungua salama. Baada ya miezi mitatu kupita, Jothan aliamua kumsafirisha Bahati na kumrudisha kwao Arusha. Alilazimika kwenda naye kwakua Bahati hakua anapajua kutokana na hali yake ya upofu aliyokuwa nayo mwanzo. Walipofika Arusha mjini, Jothan alikodi taksi iliyowafikisha mpaka nyumbani kwa kina Bahati. Ilikuwa zaidi ya furaha kwa mama yake Bahati baada ya kumuona mwanaye akiwa anaona . alimfuata na kumkumbatia. “karibuni…. Karibuni nyumbani.” Alikaribisha mama huyo kwa Furaha. “ahsante, tumeshakaribia.”aliongea Jothan na kuingia ndani. Kwa furaha ya ajabu, mama huyo alikuwa anatabasamu kila muda kutokana na kumkumbuka mwanaye. Wakati wanaendelea na stori za kawaida. Ghafla mlango ulianza kugongwa kwa nguvu. Mama yake Bahati alitoka na kwenda kumsikiliza mtu anayegonga mlango. Alikaa huko kwa dakika kadhaa. Na baadae alirudi huku akiwa hana furaha kama aliyokuwa nayo mwanzo. “samahani baba, namchukua huyu tukatete kidogo.” Aliongea mama yake Bahati. “hamna shida mama.” Aliongea Jothan na kumfanya Bahati anyanyuke na kumfuata mama yake.. “mwanangu, aliyekuja kugonga ni mwenye nyumba. Amesema kuwa ametuchoka kutokana na kutomlipa kodi yake kwa muda mrefu. Yaani nimechanganyikiwa hata sijui tutafanyaje.” Aliongea mama yake Bahati baada ya kumuita mwanaye chemba. “usijali mama, nililijua hili ndio maana nikamuelezea Jothan mapema. Ametuahidi kutusaidia.” Aliongea Bahati na kumfanya mama yake amuangalie. “kwani, wewe na huyo Jothan mkoje?” Alijikuta mama yake Bahati anauliza swali lile kutokana na kutoelewa mazingira na makubaliano ya kumponyesha mtoto wake macho na kumrudisha akiwa na mtoto. “ni story ndefu mama, ila kifupi ni mkombozi wangu na wewe pia. Naweza sema hivyo.” Aliongea Bahati. “kwa hiyo unataka kusema kuwa hata huyu mtoto si wa kwake.” Aliuliza mama yake Bahati. “ndio mama.” Aliongea Bahati kimkato huku akitaka kumuonyesha mama yake ni jinsi gani asivyotaka kuaonngelea ile mada kwa muda ule. Baada ya muda Bahati alirudi sebuleni alipomuacha Jothan na mama yake akaenda kuandaa chakula cha jioni. “mbona hivyo, kwema?” aliuliza Jothan baada ya Bahati kurejea pale. “sio kwema, kama nillivyokuambia siku ile. Mama kashindwa kulipa kodi hivyo mwenye nyuumba anataka hela yake au tuhame.” Aliongea Bahati na kumuangalia Jothan. Baada ya chakula cha usiku, Jothan alimkabidhi mama yake Bahati fedha tasilimu shilingi laki saba kwa ajili ya kulipa deni la laki nne analodaiwa na hiyo nyengine kwa ajili ya mkataba mpya. Mama yake Bahati alifurahi kidogo machozi yamtoke na kumuombea sana dua za mafanikio Jothan. “naomba niwaache, naenda kulala Hotel na mungu akipenda kesho ndio safari yangu ya kurudi Dar-es-salaam” aliongea Jothan baada ya kuangalia saa yake ya mkononi na kumuonyesha kuwa ilishatimu saa tatu kamili. “sawa mwanangu. Mungu akutangulie katika kila jambo lako.” Aliongea mama yake Bahati na jothan akatoka huku Bahati akimsindikiza. “nakushukuru kwa yote ulioamua kuyafanya katika maisha yangu. Nakuomba usichoke kuwasaidia wasiojiweza kama nilivyokuwa mimi japokuwa nilikuumiza… kwa mungu kuna fungu lako Jothan.” Aliongea Bahati walipokuwa njiani wakisindikizana. “usijali, hata mimi naamini mambo yangu yananinyookea kwakua nakigawa kidogo kwa wenzangu wenye shida. Yale yalikuwa maneno tu tena kwa sababu nilikuwa na hasira. Mimi sina kinyongo na wewe. Moyo wangu mweupe na nakuombea pia maisha mazuri na ya furaha na mtoto wako. Naamini hutofanya makosa tena kwakua umeshajifunza.” Aliongea Jothan huku wakiikaribia bara bara. Baada ya kufika kituoni, waliagana huku Bahati machozi yanamtoka kwakujua kuwa ule ulikuwa mwisho wa kuonana na mwanaume huyo wa ajabu maishani mwake. Aliondoka huku kila baada ya hatua moja akigeuka nyuma kumtazama Jothan. Kwa mbali kulikuwa na gari linakuja spidi upande aliokuwa Bahati. Jothan alipotupa macho yake kuitazama ile gari ilikaribia kabisa kumgonga Bahati ambaye wakati huo Bahati hakuiona ile gari kwakua likua bize kumuangalia Jothan. Aliamua kutupa begi lake na kumkimbilia Bahati, alipofika tu alimsukuma na kwa bahati mbaya ile gari ilikuwa inajaribu kumkwepa Bahati na kumgonga Jothan. “MAAAMAAAAAA!” Alipiga kelele Bahati baada ya kumshuhudia Jothan akianguka chini baada ya kugongwa. Damu nyingi zilikuwa zinamtoka puani na mdomoni. Yule dereva aliyemgonga Jothan, alisimamisha gari na kumuingiza Jothan pamoja na Bahati na safari ya kuelekea hospitali kwa ajili ya kujaribu kuokoa maisha ya Jothan ilianza mara moja.. Walipofika hospitali, walipokelewa haraka na Jothan akakimbizwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi. “jamani kwa hali ya mgonjwa wenu, anatakiwa kufanyiwa operation haraka iwezekanavyo ili kuokoa maisha yake.” Aliongea daktari na wote wakakubaliana kuwa tendo lile lifanyike. Bahati alikuwa mtu wa kulia tu usiku nzima. Alijua yeye ndio sababu iliyomsababishia Jothan kugongwa na lile gari.. Alilia na kumuomba mungu asimchukue Jothan. Alirudi nyumbani asubuhi na kumtaarifu mama yake juu ya kilichotokea. Mama yake alisikitika sana na kwenda hospitali ambapo walikaa kwa masaa manne bila kuruhusiwa kumuona mgonjwa. Walirudi nyumbani na kurudi tena hospitalini jioni ambapo waliruhusiwa kuingia ndani na kumkuta yule mtu aliyemgonga Jothan akwa pale hospitalini. Bahati alimuelekeza mama yake kwa yule mtu aliyeonekana na moyo wa pekee kwa kukubali kuisimamia afya ya Jothan kwa kipindi chote atakacholazwa pale hospitalini. “kwa maelezo ya dokta, amesema kuwa atarejewa na fahamu kiasi katikati ya wiki hii,.. ila itachukua muda mrefu kurudiwa na kumbukumbu.” Aliongea yule jamaa alyemgonga baada ya kujitambulisha kwa jina la Saimon. Baada ya taarifa zile, walikubaliana na kuondoka huku zoezi la kumuangalia Jothan likiwa linaendelea kila siku. Baada ya wiki mbili jothan alifumbua macho. Lakini hakuweza kuongea na hakuwa na kumbukumbu yoyote. “kwa hiyo dokta tunaruhusiwa kuondoka naye” aliuliza Saimon baada ya daktari kuridhika na maendeleo ya Jothan. “mnaruhusiwa, ila kwa masharti. Msimsumbue kwa kumlazimisha akumbuke kitu chochote. Maana kumbukumbu zake zitakuja taratibu kutokana na mazingira katika ubongo wake.” Aliongea dakrari katika moja ya kuwapa maangalizo juu ya mgonjwa wao. “sawa, sasa inaweza kuchukua muda gani hadi kurudiwa na fahamu zake sawa sawa?” aliuliza Bahati. “inaweza kuchukua miezi sita, nane au mwaka mzima kutokana na ukubwa wa tatizo lenyewe.” Aliongea daktari na kuwafanya wote waliokuwa pale waishiwe nguvu. Walikubaliana waondoke naye na kwenda kukaa kwa kina Bahati huku Simon akiwaambia kuwa atakuwa pamoja nao katika kila hali. Kutokana na kuchanganyikiwa siku aliyopata ajali Jothan, Bahati hakuokota kitu chochote alichokuwa amebeba Jothan siku ile. Hivyo hakuwa na mawasiliano angalau amjulishe Shani juu ya ajali iliyompata mpenzi wake. Siku zilikatika kwa kasi bila Jothan kuonyesha dalili zozote za kukumba yaliyokuwa nyuma. Hata jina lake tu alianza kulizoea baada ya Shani na mama yake kulitamka kila mara. Kwa upande wa Bahati alijisikia raha kumuuguza Jothan kwakua alikua analipa fadhila kwa yale aliyomtendea. Alihakikisha kuwa kila alichokihitaji mgonjwa wake basi alikua anakipata kwa wakati. Aliamua kurudia kazi yake ya kuuza maua ili alishe familia inayomkabili. Baada ya miezi sita kupita, Jothan alianza kuonekana kukumbuka kidogo kidogo. Aliweza hata kuuliza kuwa yupo wapi na ni nini kilichomleta pale. Alitamani kwenda kazini tena kama zamani. “PRISCA…… PRISCA” Alisikika Jothan usiku akilitaja jina la mwanamke huyo mara kadhaa. Bahati ambaye alikua amekaa kimya wakati wote, aliamka kutoka kwenye godoro la chini alipolala na mtoto wake na kumsogelea Jothan. Alishangaa kumuona Jothan akitokwa machozi. “mimi ni Bahati “ alijitambulisha Bahati mbele ya Jothan ambaye alikua macho usiku huo huku akitokwa na machozi. “yupo wapi Prisca.” Aliuliza Jothan na kumfanya Bahati ashtuke kidogo kwakua hakulifahamu jina hilo.. “Prisca mimi simjui… au ndio Shani ana majina mawili?” aliuliza Bahati na kumfanya Jothan afikirie kwa muda mrefu. “Shani.. Shani… ndio nani huyo?” aliuliza Jothan huku akionyesha kutokuwa na kumbukumbu nae. “si yule aliyekuwa unaishi nae kabla ya kuja huku ?” aliongea Bahati na kumfanya Jothan avute taswira juu ya mtu huyo aliyekuwa anamzungumzia Bahati. “huyo simkumbuki, yupoje kwani?” aliuliza Jothan na kumuangalia Bahati ambaye wakati huo alikuwa mbele yake akiongea kwa sauti ya taratibu kwa kuwa usiku ulikuwa tayari ni mkubwa. Hivyo sauti zao zilipea na kusikika kila mahali mule ndani. “ni mnene kiasi, mweupe na ana shepu Fulani hivi .. anapenda kuvaa ma wigi ya rihanna.” Alijaribu kumkumbusha Jothan kwa kumtajia muonekana halisi wa mtu huyo. “huyo simukumbuki,….. ninaye mkumbuka mimi ni msichana mzuri niliyeanza naye mapenzi toka tukiwa shuleni. Ni msichana mzuri sana. Na kila siku zilivyozidi kujongea, basi uzuri wake ulikua unaongezeka kila siku iendayo kwa Mungu. Nalikumbuka jina lake huyo dada. Anaitwa Prisca. Ila sijui muonekano wake kwa sasa. Labda ikitokea kuonana nae.” Aliongea Jothan huku akijaribu kuvuta hisia zake juu ya msichana huyo anaye mkumbuka kwa machache tu. “daktari alituambia kuwa tusikusumbue kwa kukumbusha ya nyuma. Ila utakumbuka taratibu. Ni vyema ulale Jothan ili uipumzishe akili yako.” Aliongea Bahati na Jothan akakubaliana nae. Kila siku ambayo Bahati alikua anarudi kutoka katika mihangaiko yake, aliutumia muda huo kupiga stori mbali mbali na Jothan. Wakati mwengine alimtembeza sehemu kadhaa maarufu. Kila akipata fedha nyingi, basi humchukua Jothan na kumpeleka shooping kwa ajili ya kumnunulia nguo. Baada ya miezi miwili kupita, Jothan alirejewa na fahamu zake kamili. Alikumbuka kila kitu. Hata siku aliyokuwa anataka kurudi Dar na kupata ajali ya gari pia aliikumbuka. Alimkumbuka pia Bahati ambaye wakati huo alikuwa naye bega kwa bega wakishirikiana na Simon ambaye alikua anakuja kumtembela mara kwa mara na kumuachia chochote kitu. Siku moja Jothan akiwa barazani anapunga upepo, alifuatwa na Bahati aliyekuwa amebeba Juice glasi mbili na kumkabidhi moja. Aliipokea na Bahati akakaa karibu yake. “lete story” aliongea Jothan baada ya kumuona Bahati kama alikua ana kitu Fulani alichokuwa anataka kumwambia. “nina mpya basi, zaidi kama hutojali. Nilikuwa nahitaji ushauri kutoka kwako.” Aliongea Bahati na kumtazama Jothan. “ulikuwa au unahitaji ushauri kutoka kwangu.” Aliongea Jothan kimzaha. “naomba unishauri,.. Simon ameniambia kuwa ananipenda na yupo tayari kufunga ndoa na mimi. Wewe kama wewe unamuonaje Simon. Anafaa kuwa mume wangu?” alifunguka Bahati na kumuangalia Jothan aliyekuwa anamuangalia pia. “kwa muda mfupi toka nimfahamu huyo mtu, sina shaka naye hata kidogo. Maana alikuwa na uwezo wa kukimbia siku ile aliyonisababishia ajali au hata kunikimbia hospitali. Lakini mpaka sasa ametupa hela nyingi kwa ajili yangu. Huwezi jua Bahati, si ajabu Mungu kamkutanisha na wewe kupitia mgongo wangu. Cha msingi zisikilize hisia zako maana wewe ndio utakuwa naye kipindi hicho mimi nitakapokuwa mbali na wewe. Kama na wewe unampenda na yeye yupo tayari kumlea mtoto wako ni dhahiri shahiri kuwa na yeye anakupenda pia.” Jothan aliongea maneno yaliyomkuna sawasawa Bahati. Alibaki anatabasamu na kumuangalia Jothan ambaye naye alikua anatabasamu pia. “nilikuwa nampenda muda mrefu sana, sema nashukuru sana kuwa hata yeye kumbe alikua ananifikiria.” Alingea Bahati. “hongera. Nilitaka kurudi Dar wiki hii, ila kama ndoa iatapangwa mapema basi nitasubiria mpaka muoane.” Aliongea Jothan na kumfanya Bahati afurahi kupita kiasi. Siku ya harusi kati ya Bahati na Simon iliwadia na maharusi walionekana kupendeza kupita kiasi. Jothan alilifurahia tukio lile baada ya Bahati kuonekana kubadilika na kuwa mwema na mtu mwenye jitihada kama alivyokuwa zamani. Baada ya siku mbili, Jothan aliaga na kurudi Dar. Kwakua hakuwa mgeni wa jiji, alitambua magari ya kinondoni na kuelekea kwake. Alifika nyumbani kwake na kukuta kufuli nje ya geti lake. Hakuwa na jinsi zaidi ya kukaa pembeni kwenye Café iliyokuwa inatazamana na geti lake ili Shani atakaporudi aweze kukutana naye. Alikaa mpaka saa mbili usiku, lakini hakukuwa na dalili za mtu yeyote kufika pale. Aliamua kwenda kulala Gesti kutokana na uchovu wa safari aliokuwa nao. Aliamka asubuhi na kupata chai, baada ya hapo akaelekea nyumbani kwake. Pia alikuta geti likiwa limepigwa kufuli kama ilivyokuwa jana yake. Aliamua kumfuata dalali mmoja aliyekuwa ameweka benchi lake pembeni ya nyumba yake na kumuuliza. “samahani mzee Sadi, hivi huyu mke wangu ana muda gani toka afunge hili geti?” aliuliza Jothan baada ya kusalimiana na mzee huyo aliyemzoe kwa muda mrefu akiwa pale nje na kufanya shughuli zake za udalali wa nyumba,viwanja na vyumba vya kupangisha. “hivi hauna habari?” aliongea mzee Sadi na kumshangaa sana Jothan kwakua alikua anajua kila kitu. “sina habari yoyote mzee wangu. Nimeingia jana tu kutoka Arusha, hivyo sina habari yoyote mie!!.” Aliongea Jothan kwa mshangao mkuu. Alianza kuhisi jambo baya linaweza kuwa lilimkumba Shani kipindi ambacho alikuwa hayupo. “mbona hii nyumba imeshauzwa miezi miwili iliyopita?… tena matangazo yalibandikwa muda mrefu. Sema wenye nyumba bado hawajahamia. Si unajua watu wenye fedha zao bwana?.” Aliongea yule dalali na kumfanya Jothan apigwe na bumbu wazi. “OOOOH MY GOD……..WHY ME?????” Alijikuta nguvu zinamuishia Jothan na kukaa chini. Aliiangalia nyumba yake aliyoijenga kwa gharama kubwa na machozi yalianza kummiminika kama maji. ITAENDELEA ... Read More
Story - - - - - NI WEWE TU PENINA Sehemu ya pili (2) By GIVAN IVAN Phone & whatsapp___0769673145 Ilipoishia........ Katika bar moja iliyopo maeneo ya sinza kikao kimoja kilikuwa kikiendelea, na huku kilichokuwa kikipangwa Katika kikao kile ni namna ya kulivunja na kuliharibu penzi la Penina na Frank. Mzee Joel ambaye ni baba yake Penina, pamoja na Angel ambaye ni mdogo wake Penina pamoja na vijana wengine watatu wa kiume na mmoja wa kike, ndio waliokuwa wahusika wakuu wa kikao kile. *********ENDELEA ******** "sitaki mwanangu aolewe na yule mlala hoi kwa namna yoyote Ile naomba muyakatishe mpenzi yao, nitawapa pesa yoyote mnayotaka." alisikika mzee Joel akiwaambia vijana wake. "hamna shinda mzee wetu kuanzia Sasa tupo Katika mipango ya kuliharibu penzi hilo usijali mzee wetu." kijana mmoja aliyeitwa zaza ndio alisikika akiwaambia mzee Joel maneno hayo. "nitafurahi Sana kama hili likifanikiwa siwezi kukubali mwanangu aolewe na yule mnuka jasho." mzee Joel bado alizidi kuongea kwa jazba. "baba hata mimi nakuunga mkono Dada hawezi kuolewa na yule mnuka shombo." aliongea Angel naye kumuunga mkono baba yake. "hamna shida mzee Joel tutafanya mnayotaka." akaongea Zaza. "bas Sawa ngoja niwape pesa ya maji ili muweze kuianza kazi Mara moja." akaongea mzee Joel na kutoa pesa kias cha shilingi laki mbili na kumkabidhi Zaza agawane na wenzake. "Asante Sana mzee wetu na kuanzia Sasa sisi tunaianza Kaz." akaongea Zaza huku akipokea pesa zile, na Kisha wakaagana na mzee Joel na kuondoka.* Katika ukumbi mmoja wa starehe mziki wa taratibu ulikuwa ukipigwa kwa utaratibu wa hali juu kabisa, huku watu wawili wanaopendana kupita maelezo wakiwa ndani ya ukumbi huo huku wakiburudika na mziki mwororo uliokuwa ukipigwa Katika ukumbi ule, watu hao ni Penina pamoja na Frank. "Frank nakupenda Sana mpenzi wangu sijui nifanye nini ili ujue ni kwa kiasi gani, nafahamu jinsi baba yangu anavyokuchukia Ila yeye hawezi kuwa chanzo cha mimi kutokukupenda wewe, hakika nakupenda Sana." aliongea Penina maneno hayo akimuambia Frank na kujilaza kifuani mwake. "nafahamu Penina ni kwa kiasi gani unanipenda na pia unatambua ni kwa kias gani mimi nakupenda, napenda nikuahidi tu kuwa NI WEWE TU PENINA hakuna mwingine zaidi yako." Frank naye alimwambia Penina maneno hayo ambayo yalimfanya Penina azidi kutoa tabasamu tamu usoni mwake na kuzidi kumvuruga Frank, ambaye alijiona ni mwanaume mwenye bahati Sana kuwa na msichana mrembo kama Penina. Kama Kuna zile sifa wanaume huzitafuta kwa wanawake bas Penina alikuwa nazo na zingine za ziada. "yaani mpenzi wangu kila nikikuangalia nakuwa na maswali mengi ya kijinga ya kukuuliza kwa jinsi tu ulivyo mzuri." aliongea Frank akimwambia Penina. "hahahaaaa maswali gani hayo mpenzi wangu hebu niulize moja." akaongea Penina na kumtaka Frank amuulize moja. "swali moja ambalo huwa najiuliza kila ninapokuona huwa najiuliza hivi wewe ulizaliwa na mwanadamu au Mungu ndio alikutengeneza mwenyewe alafu akakuleta duniani?" akauliza Frank huku akiwa anamtazama Penina. "hahahaaaa Frank mpenzi wangu mi nimezaliwa na mwanadamu kama wewe." akajibu Penina huku akicheka kwa maneno ya Frank. "najua wewe umezaliwa na mwanadamu kama mimi Ila wewe ni mrembo Sana Sana sanaaa." akaongea Frank huku akizidi kumsifia Penina. Penina naye alifurahi Sana na kuzidi kuwa na furaha zaidi kwa sifa alizokuwa akipewa na Frank. "Asante Sana mpenzi wangu kwa sifa zote ulizonipa ila Kuna kitu nataka nikuambie." akaongea Penina na kumtizama Frank. "kitu gani tena mpenzi wangu?" akahoji Frank huku akiwa ametumbua macho. "mbona umeshtuka hivyo Sasa?" Penina akamuuliza Frank baada ya kumuona ametumbua macho. "lazima nishtuke si unajua tena namna navyokupenda isije ikawa ni kitu kibaya." Frank akamjibu Penina. "usijali mpenzi sio kitu kibaya na nina Imani utafurahia." Penina akamwambia Frank kumtoa hofu. "ok niambie bas ni kitu gani?" akahoji Frank huku akionekana kuwa na haraka ya kutaka kujua. "nataka siku chache zijazo tufunge ndoa alafu tufanye harusi kubwa ili tuwakomeshe maadui zetu ambao hawataki kutuona tukiwa pamoja.." Penina ndio alimwambia Frank ambaye alikuwa kimya kumsikiliza. "kweli mpenzi wangu hata mimi nimeshaliwaza hilo tatizo lipo kwangu, bila Shaka unatambua hali iliyopo Katika familia yetu, hatuna uwezo kipesa hivyo nahitaji muda zaidi kulitimiza hilo Penina." Frank akamwambia Penina huku akiwa amepoteza tabasamu usoni mwake. "Frank mpenzi wangu ondoa Shaka kuhusu hilo mimi nina uwezo wa kulisimamia hilo mwanzo mpaka mwisho, na kuthibitisha hilo hapa nimekuja na funguo nne, moja ni ya duka kubwa la kuuza bidhaa za jumla na moja, mwingine ni wa gari kubwa la kubebea mizigo, mwingine ni wa nyumba mpya niliyowanunulia wazazi wako kama zawadi ya kunizalia mwanaume anayenipenda kwa dhati na mwingine ni wa gari ndogo nililokununulia wewe mpenzi wangu. " alimaliza Penina kumwambia Frank maneno hayo na kumuacha akiwa mdomo wazi. " waooow ni ngumu Sana kuamini ila acha niamini tu, Asante Sana mpenzi wangu." alisema Frank huku akimkumbatia Penina na kumshushia mabusu mfululizo. "usijali mpenzi wangu ila nataka utambue nayafanya yote haya kwasababu nakupenda Sana, lakini pia ni moja wapo ya maandalizi ya harusi yetu." Penina akamwambia Frank huku akiwa amejilaza kifuani mwake. "nashukuru Sana Penina mpenzi wangu kusikia hivyo na mimi nikuahidi kuwa na wewe mpaka mwisho wa uhai wangu hakika ni wewe tu Penina." Frank akamwambia Penina huku akiwa amemkumbatia kwa nguvu. Wakati huo tayari Muda ulikuwa umeenda Sana na tayari ilikuwa ni saa moja usiku, hivyo Frank na Penina waliondoka kurudi nyumbani huku Penina akimuahidi Frank kumkambidhi vitu vyote alivyomwambia siku inayofuata. Penina alimfikisha Frank nyumbani kwake, Frank akashuka kwenye gari na kumuuga mpenzi wake Penina. Kisha Penina akageuza gari na kuondoka. Baada ya Penina kuondoka tu, Frank kabla hajapiga hata hatua moja kuondoka pale, ghafla alishtukia amezungukwa na vijana watatu wa kiume waliokuwa wamevalia miwani nyeusi kila mmoja. Na hata Frank alipowaangalia hakuweza kuwafahamu. ....... Itaendelea. ... Read More
SHINDU LA KIHAYA-18 ,,,mmmmh,,,aaaaaaaaaaah,,,aashiiiiiiiiiiiiiii,,,aliendelea kulalamika mtoto wa kike ambapo nyege kweli zilimpanda,kujinasua mikononi mwa Mwalimu ilikuwa ni ngumu hasa kwani alilegea mwili wote ,,,sawa,waweza kwenda darasani,nimeacha tabia mbaya,,,aliongea kwa makusudi Hedimasta akitaka kumvalisha nguo Lisa ,,,hapaaanaaa usiniache hivyo,,,kwa sauti ya kelegea kimahaba tena ile yenye uhitaji aliongea Lisa,sura ilikuwa ya huruma sana,yaani hapo huku chini kwenye ndani ya kitumbua chake alihisi kama anawasha balaa hata angewekwa kidole pengine angemwaga Kwa umbo la Lisa,mtu mwenye nguvu hata za wastani anaweza kumbeba kirahisi,ndivyo alivyofanya Hedimasta huyo,alimbeba Lisa akiwa yuko uchi kabisa,Hedimasta mwenyewe dudu lake lilisimama kweli,Lisa alipokuwa akiliona na jinsi alivyokuwa akijisikia nyege basi ndio zilizidi kuongezeka.Kitu kimoja,sio kwamba wanawake huwa hawatamani dudu za wanaume,huwa wanatamani sana,na wanawake walio wengi hupenda dudu kubwa,tena akipatikana mtu anayejua kulitumia vyema ndio kabisa umemaliza kazi,na kama ukitaka kuthibitisha hilo,siku nenda na mschana wako pengine kwa jamaa yako,kisha jamaa yako awe na bukta kisha lile dudu lijichore jinsi lilivyo refu na nene,wewe kuwa makini kumwangalia msichana wako machoni halafu utathibitisha. Hedimasta alipombeba Lisa alimkalsha juu ya meza yake,hapo ni baada ya kusukuma vitabu na nyaraka za Serikali zilizoangukia sakafuni,hakujali hata kidogo.Alimpanua miguu na kuiweka mabegani mwake,ikawa kama inataka kumkaba shingo,mikono ya Lisa ilishika meza,ila mikono ya Hedimasta ilimshika Lisa kiuno chake,huku chini kilibaki kitumbua kikiwa kimelowa utamu Aisee njia nyingine ya kumpagawisha mwanamke kabla ya kuchanganya makongoro ni hiyo aliyoifanya Hedimasta,alilishika dudu lake kwa mkono mmoja kisha akawa anaanzia juu kidogo ya kitumbua yaani kwenye kitobo cha mkojo,kile kichwa cha dudu akawa anakikandamiza huku akikishusha chini taratibu,kilipofika kwenye kiarage mtoto alishtuka na kupiga yowe la utamu,hakuingiza dudu ndani ya kitumbua,akawa anafanya hivyo kwa kurudia,aiseee mtoto wa watu aliweuka kweli kwa utamu,.,,aaaaaaaaaaaaah,,,sssssssssssshiiiiiiiiiiii,,,uuuuuuuuuuuuuh,,,alilalamka hivyo ambapo Hedimasta alichanganua kwenye akili yake na kujua kuwa kilio kile cha mwanzoni ni tofauti kabisa na hiki kwasababu hiko cha mara ya pili ni chenyewe zaidi na kilivutia hisia. Lisa alipata shida kwani alikuwa anataka aingizwe dudu na Mwalimu haingizi ila anakisugua kiarage kwa nje ,,,unanitesa jamaniiii ingizaaaa yoteeee,,,aliongea kabisa Lisa ambapo Hedimasta alipokichusha kichwa cha dudu chini na kulenga mlango wa kitumbua,taratibu alilisukuma kwa ndani,,,aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah,,,,ssssssssssssssssssssh,,,aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah,,,alilalamika Lisa kwa utamu ambapo Mwalimu alilizamisha dudu lote na kuanza kupampu kwa hisia. Unafikiri Lisa alichelewa basi!,mapigo thelathini ya haraka haraka mtoto alikojoa bao lake na kumganda mwalimu wa watu,baada ya hapo alianza mauno yake ya kichokozi,kwanza hakukubali kuwekwa kwenye meza,alimganga mwalimu mpaka akanyanyuka naye,mwalimu kwa kumkomoa na kumpagawisha zaidi alimpeleka kwenye kona na kumbananisha hapo,e bwana kumbe hakufanya kitu mtoto alimkatikia mauno ya nyege mpaka mwalimu akaanza kuona joto la mwili linapanda,utamu ulipanda mpaka akajikuta anamwaga bila kutarajia maana mtoto alikuwa hafai kwa mauno sumu Mwalimu wa watu alikojoa bao lake ambapo ilibaki kidogo amdondoshe Lisa kwa kunogewa utamu,baada ya hapo sasa kila mmoja akawa hana abu na mwenziye,Lisa ndio kabisa hakumwangalia kama Hedimasta,alimwona ni mpenzi wake ambaye anaweza kumfanya lolote.Basi kwa adabu mbaya ya mahaba,Lisa akamshika tako Hedimasta,kidume unafikiri kulipiga kelele wala kuwaka,kilipotezea na kucheka tu. Siku hiyo aliyeshtukia mchezo alikuwa ni sekretari maana ndiye aliyemtetea sana Hedimasta pale alipohisi hali ya tofauti juu ya walimu waliokuwa wana shida naye.Kweli hakuna hata walimu waliojua ila yeye pekee alielewa kila kilichokuwa kinafanyika.Kuna muda hisia chafu zilimjia kichwani lakini alizipinga kwani hapakuwa mahali pake sahihi pa kuziruhusu. Yule mama jirani aliyesuguliwa na Alex ambaye kwa jina alijulikana kama Agnes,alikuwa akimuinjoi mumewe alipokuwa akimuhoji kuhusu jeraha lilipo kwenye paji la uso wake,alijua tu mumewe ndiye aliyekuwa akipiga chabo siku ile,cha kushangaza hakushtukia kitu chochote.Tabu ya kumsaliti mpenzi wako iko hivi,na ndio itakayokufanya ujulikane mapema,kwa mfano Angesi alikuwa mtu wa kulazimishwa sana Sex kutoka kwa mumewe,na akipewa huwa anashukuru sana kwasababu jamaa huwa anajisahau muda mwingine kazi nyingi,tangu apate kitu cha ukweli hakuwahi kumsumbua tena mumewe,sasa hiyo humpelekea mumewe kuanza kuhisi tofauti. Hassan alikuwa amemfanya Agnesi kama chakula chake,ndani akawa hapiki tena,analetewa chakula kuanzia cha asubuhi,mchana na jioni,na mara nyingi akilete cha mchana huwa lazima asuguliwe ndio aondoke hawezi kuachwa hivihivi,na alivyokuwa mtundu wa kupika,Hassana alikamatika hasa ndio maana wanasemaga mwanamke mapishi bwana. Ilipita kama mwezi mzima hivi,Hassana akiendelea kumsugua Agnesi.Siku hiyo akiwa amelala hana hili wala lile,asubuhi hodi ilibishwa mlangoni kwake.Hassan alijua tu ni yule mama ndio anabisha maana ni kawaida imeshakuwa,,,,INAENDELEA SHINDU LA KIHAYA-19 Ile kufungua mlango,alimkuta mtu tofauti kabisa na hakutegemea,yeye mwenyewe alihamaki kwanza kwani mtoto alikuwa mzuri usipime, ,,,mambo vipi,,,alisalimia Hassan ,,,safi,,,alijibu mtoto huku akitabasamu ,,,karibu ndani,,,alimkaribisha kwa sauti fulani ya kukoroma ,,,ahsante,,, Hassan alihisi kama ngekewa,hapo alikuwa ndani ya pensi fulani ya kijanja na vesti yake zinazotaka kufanana rangi,mtoto alipita mpaka ndani bila uwoga wowote na kwenda kukaa kwenye kochi. Hakuwa mwingine,alikuwa ni Lisa.Hassan hakujua kuwa huyo ni mtoto wa mama ambaye anamsugua na kumweka mjini,tayari alishamtamani kwanza,Lisa mwenyewe alivyovaa likuwa ni utata tupu,alivalia gauni fulani lililomwishia juu ya magoti,lilimbana na kumchora umbo lake vyema la kimahaba,hapo kifuani mwake ni kama hakuvaa kitu ndani maana Chuchu zilichomoza na kuhamasisha hasa. ,,,najua hunijui ila napaswa kukuita baba,,,alisema Lisa ,,,kwanini unasema hivyo,,,aliongea Hassan huku akiweka tabasamu usoni ,,,mi mtoto wa Skola,,,alijitambulisha,hapo ndipo akili zilimjia vizuri na kumwangalia vyema,picha alikuwa ameshaonyeshwa lakini hakutegemea kabisa kukutana naye kwenye mazingira hayo,hivyo alimkumbuka ,,,mmmh,ngoja nimuulize kwanza,,,aliposema hivyo alichomoa simu na kujifanya kama anataka kumpigia ,,,hapana usifanye hivyo,ye hajui mi niko wapi,,,aliposema hivyo Hassan aliaghirisha zoezi hilo,tena aliposikia kuwa mama yake hajui kama yuko hapo,ndio moyo ulifurahi kabisa na kuhisi anaweza kufanya jambo Hassan alianza kujihangaisha huku akichangamka hasa kwani Lisa alikuwa sio mchezo,ushawishi wake ni hatari sana.Kwanza alipokaa tu kwenye kochi yale mahipsi yake yalitanuka zaidi halafu tumboni flati,kifuani ndio usiseme.Haraka kidume kilikwenda kutafuta supu na chapatti.Lisa hakujivunga,alikunywa vyema kisha akashushia na soda ya baridi. Musa,rafiki yake kipenzi na Hassan,ambaye ni mzito sana kwenye suala la kuongea na wasichana yaani kutongoza.Aliingilia kati mchezo na kumkuta Lisa ndio anamalizia chakula,baada ya kusalimia Musa,alikaribishwa chakula ambapo kwa sura ya upole alijibu ameshiba.Moyoni Hassan alikasirika ujio huo wa Musa ila kwa nje alionyesha kufurahi. Hassan hakufanya hata utambulisho kwa jinsi alivyo na roho mbaya,kila wakati macho ya Musa yalikuwa kwenye mapaja mazuri yaliyonona ya Lisa,yaani aliyatolea macho ya matamanio yale ya waziwazi kabisa.Lisa alijua kabisa wakati anayopitia musa hata Hassan,kwa makusudi Lisa alimkonyeza Musa,e bwana mapigo ya moyo yalianza kumwenda mbio Musa mpaka alipoongeleshwa na Hassan alijikuta akishindwa kutamka maneno vyema. Alichokifanya Hassan ili kuendeleza harakati za kumvutia mtoto kwenye box.Alimtoa nje Musa na kuanza kumpanga,Lisa naye kwa umbea alijivuta mpaka usawa wa mlango ili kusikiliza ,,,sikia,we hujui kuongea,potea kabisa eneo hili,chukua hii buku tano,,,Hassana alisema hivyo ,,,kaka lakini mbon amenipenda bwana,,,alijibu Musa na kutaka kurudi ndani,kwa kukonyezwa alishahisi kitu.Hassana alicheka kwa nguvu kabisa kisha akarejea ile sauti yake ndogo ,,,una kichaa wewe,mtoto mzuri huyu utampa nini,,, ,,,sa sikia,kila siku mi unaniona mjinga sijui kutongoza,acha niende ndani nikaongee naye,nikishindwa kutoka naye,mi nitaondoka,,, ,,,poa nenda,,,kwa Dharau Hassana alijibu hivyo ambapo alijua Musa hata angeenda kuongea nini asingekubalika. Kiukweli hata dakika haikupita,Musa alitoka na Lisa nje tayari kwa kuondoka,walimkuta Hassan nje kisha Lisa ndiye aliyeaga ,,,baba natoka kidogo,ili mradi nimeshapajua nitakuwa nakuja,ahsante kwa supu,,,kauli hiyo ilimpa wakati mgumu Hassan kujibu lakini alijikaza sana ,,,sawa,lakini mbona unawahi sana jamani,ngoja niwasindikize,,,alisema hivyo na kumkata jicho la husuda Musa aliyekuwa akikenua meno nje kumcheka ujinga Basi wakaanza safari wote watatu,walivyojipanga tu ilikuwa maumivu kwa Hassan,yaani mtoto sijui alipenda nini kwa Musa ghafla.Akajikuta anamshobokea jamaa ambaye hata hawezi kutongoza.Lisa alkuwa pembeni kabisa akiwa ameshikana mkono na Musa,Hassan alimfuatia musa,basi hapo Musa tayari dudu lilishasimama kushika mkono tu ,,,sio mbali sana,,? ,,,hamna ni bajaji tu tunafika,,, ,,,pasiwe mbali bwana,,, ,,,usijali muda si mrefu tutafika,,,maongezi hayo kati ya Musa na Lisa,yalimchoma moyo moja kwa moja Hassan na kumfanya awe kama mtu anayetaka kulia.Alitamani aichukue elfu tano yake aliyompa Musa ili aondoke,matokeo yake elfu tano hiyo ndio ilitumika kumsafirisha Lisa mpaka kwenye gheto la Musa Roho ilimuuma kumwona Lisa na umbo lake tamu kupanda bajaji na kuelekea gheto kwa Musa ila hakuwa na jinsi,mtoto alijituliza kwenye bajaji,mara amshike bega na kuegemeza kchwa chake,mara washikane mikono ndani ya bajaji ilikuwa raha tu kwa Musa,kiukweli Musa alikuwa ndotoni kabisa. Walipofika gheto ndio kabisa hakuamini,sasa kwa Musa ilikuwa ni tofauti,alikuwa anakaa kwenye nyumba fulani kubwa peke yake,aliachiwa na mjomba wake akae kwani mjomba huyo hakuwa na haraka ya kuhamia kwasababu anafanya kazi mbali kidogo.Nyumba ilkuwa na kila thamani ndani yake,Lisa mwenyewe alipapenda ,,,nyumba yako nzuri,,,alsifu Lisa ,,,kama wewe ulivyo mzuri,,,alijishangaa kufungua kinywa na kusema hivyo Musa ,,,mi mzur kweli,,? Alihamaki Lsa kwa makusudi ,,,kweli,hilo la kuuliza jamani,,, ,,,nihakikishie kamani mzuri,,,aliposema hivyo ndio alizua balaa mtoto wa kike,maana jamaa mwenyewe alikuwa na Ugumu hasa,,,ITAENDELEA KESHO SHINDU LA KIHAYA-20 Lisa alimsogelea mpaka kwa karibu,aliubana mdomo wake wa chini na meno kisha taratibu aliuachia huku akiupeleka mdomoni mwa Musa,masikini Musa wa watu alikuwa hajafanya mapenzi kitambo,alisisimka mwili mzima na kujikuta akilegeza mdomo wake bila kutarajia. Mtoto wa kike alifumba macho kuvutia utamu ambapo mikono yake taratibu aliipitisha shingoni kwa Musa,yaani midomo ilipogusana,Musa alijihisi kama anapaa,kule kusogeleana mpaka kugusana kabisa ndio ilimaliza kila kitu,mikono ya Musa ikawa inatalii kwenye kiuno cha Lisa taratibu bila shaka. Lisa akawa anamshikashika kimahaba kichwani Musa wa watu ambaye denda liliendelea,ndani ya mdomo mtoto aliuzungusha ulimi ipasavyo na kumsisimua kweli Musa.Kidume kilimwaga pale ambapo mikono ya Lisa ilishuka mpaka kiunoni mwake na kuingia ndani ya shati,ikawa kama inamkunakuna kimahaba,aisee kuna wanaume wengine huwa wanapagawa sana ukiwashika migongo,Musa alimwaga ambapo Lisa alishangaa kidume kikijihangaisha na kuzidisha nguvu za kumkumbatia,akajua tu kijana wa watu amemwaga. ,,,pole Musa wangu,,,kwa sauti ya chini sana,kuliko kawaida aliongea Lisa ,,,ahsante,,aliitikia kidume huku akijishtukia Lisa alimvuta Musa taratibu na kumtupa kwenye kochi.Akamfuata na kuanza kumvua shati na vesti yake,alipomaliza hapo alipiga magoti kama mtumwa anayetaka kuomba msamaha kwa bwana wake baada ya kukosa,kumbe Lisa ndani ya gauni yake alivaa chupi pekee tena bikini,basi mtoto kwa taratibu alijivua gauni lake na kubaki na bikini tu,mapaja yake manono sasa!,yalionekana laivu bila chenga,hapo kiunoni,kitovu kizuri kilichoingia ndani,rangi adimu aliyonayo Lisa vyote vilimfanya Musa ajione kama yuko ndotoni,hakujion akuwa anastail mtoto mzuri namna hiyo kumsugua. Alipomaliza kuvua gauni lote na kulitupa pembeni,alitembea kwa magoti na kuingia katikati ya mapaja ya Musa,taratibu bila pupa limfungua mkanda na kuishusha suruali,alipoivuta tu na kufika magotini,alijifanya ameshtuka jambo ,,,aaaah!,jamani umemwaga,,!,alishangaa hivyo akiwa anatabasamu Musa na uwoga wake alishindwa hata ajibu nini,alibaki kimya kama mzimu huku akitabasamu. Ni kweli Musa alikuwa hajui kuongea lakini sio kwamba ukimwonyesha shimo hajui kuchomeka,japo alimwaga,lakini dudu liliendelea kusimama,hapo lilikuwa ndan ya Boksa,Lisa alishusha ile suruali mpaka chini kabisa,alipoivua yote,sasa akawa anahema kuliangalia dudu la Musa lilivyotuna kwenye boksa yake,tena lilikuwa kama lnapumua vile ndani ya boksa. Alilegeza mdomo mtoto wa kike na kujaza mate ya kutosha,aliusogeza mdomo wake mpaka kwenye mtuno huo wa dudu,mtuno wenyewe ulionyesha dudu limeelekea kushoto,basi alitoa ulimi wake na kuanza kulifuatisha mpaka kwenye kichwa cha dudu hilo,,,aaaaaaaaaaaah,,,aliguna Musa ambapo mtoto alikiingiza kile kichwa mdomoni kikiwa vilevile ndani ya boksa akawa anafanya kama anakipumulia ile hewa ja moto mdomoni,Musa alijihis raha mpaka kuinua sura yake juu kwa utamu Taratibu alianza kuivua boksa yake mpaka chini kabisa,dudu la Musa liliachwa huru sasa liknesanesa,halikuwa imara sana,basi Lisa akaanza kazi ya kulifanya lwe imara ili miguso mnato ianze,aliutoa ulimi wake nje kama nyoka vile,alikuwa akucheza juu chini haraka haraka,alipokigusa kichwa cha dudu kwa staili hiyo,Musa alianza kuguna tu kwa utamu,,,aaaaaaaaaaaaaaaaaah,,,aaaaaaaaaaashiiiiiiiiiiiiiii,,,ssssssssssssssssss,,aaaaaaaaaaaaaaaaah,,,,alilalamika Musa wa tu huku dudu lake likishughulikiwa kile kichwa tu,Lisa alipoona kdume knapagawa,aliliingiza lote mdomoni,alilizungusha na kulitekenya na ulimi wake hasa kwenye kichwa kile,Musa mwenyewe alishindwa hata kukaa vizuri kwenye kochi. Mikono yake laini Lisa aliipeleka mpaka kwenye kende na kuanza kuzitomasatomasa,nyege zilimpanda Musa mpaka akachanganyikiwa kabisa,dudu lilidinda vyema kiasi kwamba hata kurudi chin halikurudi,lilinesa lakini juu kwa juu.Hapo tena Musa hakufundishwa kitu.Alimshika uso Lisa kama anataka kumpiga kisha akaanza kumnyonya denda huku akimwinua taratibu. Dudu lake bado lilisimama hasa kama kijiti kilichochomekwa ardhini.Alimshika kiuno Lisa na kumvutia upande wake,mtoto naye alijilegeza hasa,Musa aliivuta ile bikini na kuikata mikanda yake kisha kuitupa kule,aliyavamiwa matako laini ya Lisa na kuanza kuyaminyaminya kama anachagua nyanya sokoni,,,,aaaaaaaaaaaah,,,bebiiiiiiiiii aaaaaaaaaaah,,,alilalamika Lisa ambapo ni kama alikuwa akmpandisha mizuka Musa. Bila ya kuambiwa Lisa mwenyewe,alijipanua mapaja na kujiandaa kukalia dudu la Musa lililosimama hasa,Musa aliliandaa lile dole la kati ambalo wengi huliita la matusi kisha akalipenyeza kwenye kitumbua cha Lisa na kuanza kumtekenya kiarage chake kilichosimama,,,aaaaaaaaaashiiiiiiiiiiiiiiiii,,mamaaaaaaaaaaaaaaaaaaa,,aaaaaaaaaaaaaaah,,,musaaaaaaaaaaaaaaaaa,,aaaaaaaaaashiiiiiii,,,oooooooouuuuuh,,,eeeuuuuuuuuuwii,,,mtoto alilalamika kwa utamu mpaka alitia nyege tena.Basi Musa alipokuwa akimchezea kiarage chake,akawa anakishusha kidole chake chini taratibu huku akijua chini kuna dudu limesimama,naye Lisa alikuwa akikifuata kidole taratibu kwa alihisi utamu alipokuwa akitenywa kiarage chake,ilifika muda Lisa alishtuka na kupiga yowe la utamu,pale dudu la Musa lilipogusa mashavu ya kitumbua,,,aaaaaaaaaaaashiiiiiiiiiiiiii,,,taratibu mpenziiiiiiiii,,,,,INAENDELEA ... Read More
*MWAGIA HUMO HUMO EP 02* Sehemu Ya Pili (2) Lakini pamoja na yote sikuwa na sifa ya kumteka mwanaume kimapenzi zaidi ya kunionja na kuniacha. Wasiwasi wangu huenda mwili wangu hauna asali itakayo mfanya mwanaume yoyote atakaye nionja anirudie mara mbili. Basi baada ya kupokea aligeuka na kuondoka kurudi ofisini kwangu. Nilipofika mlangoni nilikumbuka kitu nilitaka kumuuliza bosi, niligeuka ili nimuulize kitu. Niligeuka ghafla na kukutanisha macho na bosi ambaye kumbe nyuma yangu alikuwa akinifuatia. Maskini kaka wa watu alishtuka mpaka akadondoka chini, nilijikuta namuonea huruma. Nilirudi hadi chini alipokuwa amekaa bila kuonesha kujinyanyua, mwili wake haukuwa mkubwa sana nilimshika mkono ili kumnyanyua. “Hapana Manka nitanyanyuka mwenyewe.” “Hapana bosi naomba unipe mkono,” nilimwambia kwa sauti ya huruma yenye kubembeleza. Alinipa mkono na kumnyanyua, baada ya kunyanyuka nilitoa kitambaa changu na kumfuta sehemu yenye vumbi. “Tosha Manka sehemu zingine nitafuta mimi.” “Hapana bosi ni wajibu wangu kufanya hili.” Aliniacha nimfute kisha nilimtengenezea kiti na kumuomba akae. “Unaweza kukaa.” Bila kuongeza neno alikaa kwenye kiti chake huku uso wake ukionesha aibu imemtawala. “Pole bosi,” nilimwambia kwa sauti ya chini. “Asante.” “Hukuumia?” “Nipo sawa.” “Pole sana.” “Asante Manka, nipo sawa kaendelee na kazi.” Niligeuka na kuondoka hata nilichotaka kumuuliza nilikiacha na kupanga kumuuliza kupitia simu yangu ya mezani. Nilitoka hadi ofisini kwangu kuendelea na kazi, kabla ya kuanza kazi nilijikuta nikijiuliza kilichomdondosha bosi wangu ni nini. Wasiwasi ulikuwa uleule bosi kapagawa na mimi, kitu ambacho sikutaka kinitokee kwa muda ule kwani ilikuwa mapema sana. Niliamini kabisa bosi kwa mtazamo wa nje alikuwa amepata bonge la mwanamke, lakini ndani sikuwa na sifa zile za kukaa na mwanaume kwa muda mrefu. Niliyapuuza na kuendelea na kazi, nilikumbuka kuna kazi nilitaka kupata maelekezo kwa bosi. Nilimnyanyua simu kumpigia baada ya kuita kwa muda ilipokelewa. “Haloo bosi.” “Ooh..Aah…Nani Manka,” maskini bosi wangu alionesha kiwewe bado hakijamtoka. “Bosi mbona hivyo?” “Aah, kawaida tu, unasemaje?” “Ok, bosi nilikuwa nauliza hii kazi ya malipo kuna maandishi ya mkono nayo niyaandike?” “Hakuna tatizo, yaandike kama ilivyoandikwa.” Nilikata simu na kuendelea ka kazi yangu kama kawaida, baada ya muda nikiwa bize simu ya mezani iliita, nilinyanyua na kupokea. “Haloo bosi.” “Ndiyo Manka jiandae tukapate lunch.” “Nashukuru bosi.” Baada ya kukata simu, niliangalia saa kubwa ya ukutani iliyokuwa mbele yangu, ilionesha ni saa saba kasoro kumi mchana. Nilimalizia kazi yangu ili nipate muda wa kwenda kula, nikiwa bado nimeinama nikirekebisha tatizo la kisarufi nilishtuliwa na sauti ya bosi. “Manka tunaweza kwenda.” “Hakuna tatizo bosi, namalizia kurekebisha sarufi.” “Utamalizia tukirudi.” Nilisave kisha nilizima computer na kunyanyuka, nilijitengeneza vizuri nguo niliyovaa. Kwa chati nilimuona bosi wangu koo likimcheza kama mtu mwenye kiu kikali. Baada ya kuhakikisha nipo sawa tulitoka hadi kwenye gari lake kisha tulikwenda kwenye moja ya hoteli ya kifahari ambayo ilinikumbusha mbali enzi nipo kwenye ndoa yangu. Tulipofika Mateja alionesha kutojiamini sana kwangu kitu ambacho sikuamini mwanaume kama yeye kuwa katika hali ile. Sikuwa na sifa kubwa zaidi ya mwanamke aliyepoteza matumaini ya kupata hadhi mbele ya mwanaume. Niliamini kaniona kwa nje hanijui ndani nilivyo ndio maana ananipapatikia. Nilijua akikipata anachokitafuta kwangu pengine ndiyo siku ya kunifukuza kazi, lakini sikuwa na jinsi kila mwanaume mwenye pesa aliamini mwanamke sahihi wa kukaa naye ni mimi. Baada ya kuketi kwenye viti vyetu muhudumu alifika na kutaka oda zetu. “Manka agiza chochote ukitakacho kwa bei yoyote.” “Asante, nataka kula unachokipenda wewe,” utanishangaa kwa nini nimesema vile, nilifanya vile ili kumtoa wasiwasi na kumfanya awe huru kwangu japo si katika suala la mapenzi. “Hapana Manka nataka wewe leo ndio uchague chakula tutakacho kula.” “Sawa,” nilichagua chakula ambacho wote tulikuwa. Baada ya chakula wakati wa kunywa vinywaji Shaka aliniuliza. “Samahani.” “Bila samahani.” “Manka, umeolewa?” “Sijaolewa.” “Una mchumba sina?” “Sina.” “Rafiki wa kiume?” “Sina.” “Manka mbona unanidanganya.” “Kweli bosi.” “Hivi Manka kwa umbile alilokujali muumba usiwe na mwanaume?” “Si kwamba sijawahi mwanaume ila kwa sasa sina.” “Kweli?” “Kweli kwa nini nikufiche ili iwe nini?” “Mara nyingi watu wamekuwa si wakweli.” “Huo ndio ukweli wangu.” “Kwa nini mrembo kama wewe huna rafiki wa kiume?” “Sina bahati nimeamua kuishi peke yangu.” “Ina maana hata ombi langu litagonga ukuta?” “Ombi gani?” “Kwa vile huna mtu nilifikili unafaa kuwa mke wangu.” “Aaah, bosi,” kauli ile ilinishtua sikupenda kuisikia masikioni mwangu. Sikuwa na jibu la moja kwa moja, moyo mapigo ya moyo walinienda mbio na machozi yalinitoka. Mateja alishtuka kuniona nikitoka machozi badala kumpa jibu lake. “Manka vipi?” “Hataa,” nilitikisa kichwa. “Mbona machozi yanakutoka.” “Kauli yako imenishtua.” “Kivipi?” “Sikutegemea kuniambia neno hilo mapema kiasi hiki.” “Manka, penzi limuingiapo mtu huwa kama kichaa aliyekatikiwa na mishipa ya fahamu. Niyasemayo si mimi ni moyo wangu naomba unihurumie.” “Ni kweli, lakini sina bahati kila siku mapenzi limekuwa likinitesa.” “Kivipi?” “Mpaka leo sijajua sababu ya kuachwa na wanaume.” “Ni wazi wote waliopita walikuwa na tamaa ya kukujua ulivyo na si mapenzi ya dhati. Lakini nakuamini mimi ndiye mwanaume sahihi kwako.” “Hiyo kauli kwangu nimeizoea, lakini mwisho wa siku mambo huwa kinyume.” “Niamini Manka, nitakuwa mume mwema.” “Mmh nitashukuru, lakini usinitende utaniumiza.” “Siwezi.” Baada ya chakula tulirudi ofisini, hatukufanya sana kazi Mateja alikuwa na uchu wa fisi. Aliniomba tufunge ofisi twende tukastarehe, sikuwa na pingamizi nilifunga kazi na kuongozana naye kwenye gari lake. Mateja alinipeleka kwenye hoteli ya kifahari ya nyota tano. Kwa vile shida yake niliijua sikushtuka kumsikia akiuliza chumba cha VIP, baada ya kulipia tulikwenda kwenye chumba kilichokuwa ghorofa la pili. Chumba kilichokuwa cha kifahari, ambacho kilikuwa kipo katika hadhi ya juu. Katika maisha yangu sikuwahi kuingia kwenye chumba kizuri kama kile. Chumba nilikiona kilikuwa kinapendeza lakini wasiwasi wangu bosi wangu atakipata alichokifikilia kukipata mwilini mwangu. Sikutaka nami kijiweka nyuma kwani nilikumbuka kauli za Bi Shuu mama mlezi wangu shangingi mstaafu, kuwa niwapo mbele ya mwanaume nijionesha nipo tayari kumpa kile anachokitaka. Siku zote aliniambia nijiamini ili kumfanya mwanaume naye ajiliuze mara mbili mbili ataniingiaje. Sikupoteza wakati baada ya kuingia tu chumbani nilivua nguo zote na kubakia kama kuku aliyenyonyolewa. Sikuchelewa kumsaula na yeye tukawa sale sale maua. Nilitembea kama miss kuelekea kwenye kabati kuchukua taulo kwa makusudi nimuoneshe umbile langu ambalo mwanzo huwa utata kwa wanaume. Lakini wakiisha nipata nakuwa kama Big G iliyotafunwa na kuisha utamu mwisho wake hutemwa. Kwa kweli sikupenda kutongozwa siku moja na siku hiyo hiyo kumvulia mwanaume nguo ya ndani. Niliamini kabisa kujilahisi vile lazima thamani yangu ingepungua lakini kama ningemzungusha, kidogo thamani yangu kwake ingepanda. Nilijua lazima ataniona maharage ya Msanga maji nusu kijiko. Lakini sikuwa na jinsi kutokana na njia aliyotumia kwa kweli nilijikuta siwezi kuuruka mtego wake mwepesi. Sikuwa ndege mjanja lakini nilinaswa kijinga sana, japo sikujua tatizo langu lakini nilipokuwa natembea na kumuachia umbile la nyuma lililokuwa linawatesa wanaume wengi. Niliinama makusudi kama najikuna mguu ili tu nizidi kumpagawisha. Kitu kilichofanya Mateja azidi kuwa katika wakati mgumu, wakati nafungua kabati nitoe taulo Mateja alikuwa tayari yupo nyuma yangu na kunikumbatia kwa nyuma. Nilijua uzalendo ulikuwa umemshinda, mambo yalianzia pale. Tulianza kubadilishana mate palepale kwenye kabati, baada ya muda aliona anachelewa, mwanaume alinibeba juujuu mpaka kitandani. Kwa vile mchicha ulikuwa umeishakolea nazi tuliumwaga juu ya ubwabwa na kuanza kujimegea tataribu. Mateja alionekana ana pupa kama mamba mwenye njaa, hakuchelewa kukifikisha chombo ukingoni mwa bahari. Baada ya mapumziko mafupi tulirudi ndani ya ngarawa kuendelea na safari, katika vitu ambavyo katika maisha yangu nilikuwa sivipendi ni usumbufu ndani safari. Ooh geuka hivi, lala hivi, inama hivi, nyanyuka hivi, kwa upande wangu niliona usumbufu lakini nilivumilia kwa vile ndiyo ilikuwa siku yetu ya kwanza kukutana. Kama ningekuwa nimemzoea ningempasha, kwani hakuna starehe ya mapenzi mpaka kusumbuana kumgeuza mwenzako kituko,ile kwangu sikuona mapenzi zaidi ya adhabu. Siku zote niliamini baada ya safari ndefu mtu humwaga mzigo na kutelemka. Siku ile tulikaa kaa mpaka saa tatu usiku baada ya kuoga na kula alinirudisha nyumbani. Kabla ya kuondoka Mateja aliniahidi vitu vingi ikiwemo kunijengea nyumba kuninunulia gari na kuyabadili maisha yangu kwa ujumla. Siku ile moja tu alinipatia laki tano taslimu, sikuamini niliona miujiza kupata raha na kiasi kikubwa cha pesa kama kile. Nilipofika nyumbani nilimkuta Bi Shuu yupo chumbani kwake, Nilifungua mlango wa chumba changu na kuingia ndani. Nilipowasha taa nilishtuka kumuona Bi Shuu kanisimamia nyuma, akuzungumza chochote ila alinikata jicho kali. “Shikamoo Bi Shuu” “Hainisaidii kitu” “Mbona hivyo mama yangu” “Kazi gani ya kutoka saa moja asubuhi kurudi saa tano za usiku?” Mmh, makubwa nimekuwa mtoto mdogo wa kuwa chini yake kwa kila kitu. Nilijua uchawi wa Bi Shuu ni nini, niliinama na kuchukua mkoba wangu na kufungua. Nilihesa nyekundu tano na kumpa. “Za nini?” “Katumie tu” “Za kodi?” “Walaa, nimekutunuku tu mama yangu.” “Kweli!?” “Kweli unafili uliyonifikiza madogo” Bi Shuu alifurahi na kunikumbatia na kusahau aliyobwatuka muda mfupi, baada ya kunipandisha na kunishusha alisema. “Weee mwana kulikoni” “Kaa chini nikupashe kazi imekuwa kaziiiii” “Usiniambie” “Habari ndiyo hiyo shilingi moja kwa sekunde ndio mpango” “Wacha wee leo Mchaka kawa mzaramu” “Umenifundisha wewe, ngoja nikaoge nikupashe upashike” Nilimuacha Bi Shuu chumbani kwangu akizirudia kuzihesabu pesa nilizompa mimi nikaenda kujimwagia maji. Nilipotoka kuoga nilimkuta akinisubiri kwa hamu kubwa. “mmhu, hebu nipe raha” “Bi shuu nitakueleza yote kesho” “Mwana wee siwezi kulala mpaka unipe siri ya rangi nyekundi kupendeza na kusikitisha” Huku nikijifuta maji nilimueleza yote bila kumficha hata moja, mwisho wa yote nilielezea masikitiko yangu ya bahati ya kupendwa na mkosi wa kuachwa. “Bi Shuu, japo nimepata lakini wasiwasi wangu sichelewi kumwagwa” “Kwani una tatizo gani?” “hata silijui hakuna hata mwanaume mmoja aliyenieleza tatizo langu” “Mmh, kuna umuhimu wa kulifanyia kazi” “Siamini kama tatizo langu litaisha” “Hebu kila ukiwa na huyu bwana msikilie na muulize an apenda nini chochote usimnyime” “mmh, Bi Shuu wanaume wengine waharibifu ukimchekea anakuharibu” “Sio unavyo fikiria’ “Kuna nini wanaume wanacho taka zaidi ya kuwaharibu wanawake, sijazaa babu wee cha kuwekewa matambala” “Sina maana hiyo si wote wana penda mchezo huo.” “mmh, nitamsikiliza” “Sasa mwana wee lala nakuomba muheshimu mpenzio kama Mungu wako huoni muda si mrefu nasi tutatembelea gari” “Ndicho ninachokiomba, sijui yatakuwa yale yale.” “Basi mwali lala usingizi unono.” “Nawe pia Bi shuu” Bi Shuu aliniaga na kuondoka na kuniacha nikimalizia kujifuta maji ili nilale. ****** Siku ya pili wakati namalizia kujipodoa kabla ya kwenda kujifusha udi kwa Bi Shuu simu ya Mateja iliingia, niliipokea na kuzungumza naye. “Haloo ma’ Sweet.” “Ooh, ma honey girl.” “Ni mimi, mhu baba nipe habari naona simu za asubuhi asubuhi?” “Aah, kawaida ila kuna dereva nimemtuma atakupitia muda si mrefu.” “Hakuna tatizo Sweet.” Baada ya Mateja kukata simu, kwa vile nilikuwa tayari nimeisha jipodoa nilikwenda chumbani kwa Bi Shuu. Kabla ya kuingia nilikutana na moto uliokuwa ukinukia vizuri, harufu ya asubuhi ile ilikuwa zaidi na ya jana yake Niliingia na kumkuta akiweka udi kwenye kitezo, aliponiona alitabasamu na kusema. “Haya mwali jifushe uwahi kazini.” Niliinama na kufunikwa shuka ili moshi wote wa harufu nzuri uishie kwenye nguo na mwilini, baada ya muda alifunua shuka na kuninusa kama mbwa anayesaka chakula jaani. Asikuambie mtu Bi Shuu havumi lakini yumo, mtu mzima lakini ovyooo. “Umevaa kufuri gani?” Bi Shuu aliniuliza swali ambalo sikufikiria kuniuliza. “Nyeupe.” “Hebu nione.” Mmh, makubwa nilinyanyua gauni na kuiona nilikuwa nimevaa kufuli la mikanda ‘Bikini’. “Mwali ndio nini?” Bi Shuu alishtuka. “Mbona umeshangaa?” “Unakwenda kwenye starehe au kazini?” “Kazini.” “Sasa mbona umevaa kufuri kama unakwenda kwenye kilimo cha mihogo.” “Babu weee kwenda na wakati.” “Acha ushamba vaa kufuri la kawaida, hilo kufuri unalivaa siku unayokutana na mpenzi ukitoa nguo tu akiona anaingia kimuhemuhe.” Mmh, sikutaka kubishana naye nilirudi hadi chumbani kubadili kufuri, wakati namaliza kuvaa honi ya gari ilipigwa nje nilijua mtu aliyetumwa kunifuata amefika. Nilikimbilia chumbani kwa Bi Shuu kumuaga. “Bi Shuu naondoka.” “Umebadili kufuri?” “Ndiyo.” “Hebu nione.” Nilinyanyua tena gauni na kunitazama, nilikuwa nimevaa ya kawaida tena ya rangi nyekundu, alipoiona alisema. “Ewaaa, sasa hapo ndipo nilipopataka.” “Basi nawahi kuna mtu ananisubiri hapo nje katumwa na mzee,” nilisema huku nikiteremsha gauni ili niwahi nje. “Wee Manka ndio nini?” “Vipi tena Bi Shuu mwenzio nachelewa kazini.” “Hebu jifushe na hiyo kufuri linukie.” Nilirudi haraka na kuchutama kwenye kitezo kwa kulitanua gauni langu moshi wote uingie chini. Baada ya kufanya yote niliyoelekezwa na Bi Shuu nilimuaga kwa kumbusu kisha nilipitia mkoba wangu na kutoka nje. Nilimkuta gari likinisubiri, niliingia kwenye gari na gari liliondoka. “Mambo?” “Poa, sijui yako?” “Hata mimi ipo poa.” Safari iliendelea hadi ofisini, nilipofika nilipita moja kwa moja hadi ofisini kwa Mateja, alivyokuwa ameisha ingia ofisini. Baada ya kufungua mlango wa ofisi niliingia huku nikiachia tabasamu pana na kutanua mikono yangu, Mateja aliponiona alizunguka meza yake kunipokea. Tulikutana katikati na kukumbatiana. Tuliporomosheana mabusu moto moto huku tukigandisha midomo kwa muda na kubadilisha mate. “Mmh, tosha,” nilisema huku nikijitoa mikononi kwa Mateja. “Mhu, za nyumbani?” “Mmh, mzuri sijui kwako?” “Kwangu ilikuwa ngumu kidogo kutokana na kuwa na wakati mgumu baada ya kukuota tupo pamoja niliposhutuka nilijikuta nipo peke yangu.” “Pole sana, basi ndio ufanye haraka kunichukua.” “Kwa mateso ya jana kuna umuhimu wa kufanya hivyo.” “Basi mengine baada ya kazi.” “Haya mama, mimi niseme nini.” Nilimbusu tena na kurudi kuendelea na kazi yangu, baada ya kukaa kwenye kiti nilijikuta nikikumbuka jinsi bosi wangu Mateja alivyochanganyikiwa na mimi. Nilimbusu tena na kurudi kuendelea na kazi yangu, baada ya kukaa kwenye kiti nilijikuta nikikumbuka jinsi bosi wangu Mateja alivyochanganyikiwa na mimi. Pamoja na furaha ile bado wasiwasi wangu ulikuwa nini hatima yangu kwake, nitaendelea naye au ndiyo atanitosa kama waliotangulia. Wazo la awali lilikuwa kuomba msaada kwa Bi Shuu ili niweze kumdhiniti. Niliendelea na kazi zangu kama kawaida, muda wa mchana tulikwenda kula pamoja kama wapenzi wasiojificha. Siku ile baada ya kurudi nyumbani aliniomba tuwe wote usiku wa siku ile, sikumkatalia kwa vile ndiye aliyekuwa mmiliki wa mwili wangu. Usiku alinipitia na kuondoka kwenda kulala naye mpaka asubuhi, kaonja kaona tamu sasa anataka kula kabisa. … Ni kweli nilifurahi kulala na Mateja mpaka asubuhi kuonesha jinsi gani alivyopagawa kwangu, lakini usiku kwangu ulikuwa wa karaha sana yaani mambo nisiyoyapenda ya kusumbuana wakati wa mapenzi yalijirudia tena. Nilishindwa kumkatalia kwa vile alikuwa bosi wangu kwa kuogopa kufukuzwa kazi na maisha ya kutangatanga yalinichosha. Usiku mzima kugeuzwa kama chapati ooh geuka hivi, lala hivi fanya hivyo, basi kero mtindo mmoja. Nilijiuliza bila kunisumbua vile hawezi kukidhi haja zake, mpaka kunakucha nilikuwa nimekasirika mtoto wa kike kila kona ya mwili iliniuma hayakuwa mazoezi bali adhabu ya mapenzi. Asubuhi Mateja alifurahi sana na kuniahidi kabla ya yote kukibadili chumba changu kwa kuninunulia sofa za nguvu, alinipa pesa nyingi za kutumia na kunirudisha nyumbani. Huwezi amini nilipofika nyumbani nilimkuta Bi Shuu akinisubiri, kutokana na uchovu nilimsalimia na kuingia ndani nijilaze. Kabla sijabadili nguo na kuvaa kanga nyepesi Bi Shuu aliingia. “Mankaaaaa,” aliniita kimbea. “Unasemaje Bi Shuu,” nilimuuliza huku nikimuangalia jicho zito la usingizi. “Mmh, sikuwezi.” “Kwa nini Bi Shuu?” “Mambo yako mazito.” “Mmh kawaida tu, vipi ushakunywa chai?” “Nilikuwa nakusubiri wewe.” “Mimi kwa sasa hivi siwezi nimechoka sana.” “Eeeeh Manka weee, mlikuwa mnakomoana.” “Wee Acha tu,” niliona kama ananichelewesha kulala kutokana na umbea wake wa utu mzima. Nilivuta pochi na kutoa noti kadhaa za kumi kumi na kumpatia Bi Shuu bila kuzihesabu. “Za nini?” “Za kwako.” Bi Shuu alichanganyikiwa na kunivamia kwa furaha na kujitahidi kunibeba japo uzito wangu ulikuwa mkubwa. Kweli pesa sabuni ya roho Bi Shuu alipagawa na kuniona kama malaika niliyetumwa kuja kumpa furaha ya asubuhi ile. “Bi Shuu niache nipumzike.” “Mwali weee lala, tena utakutana nimekuandalia chakula kizuuuri.” Bi Shuu alitoka na kuniacha nikimalizia kuondoa nguo mwili kisha kuchukua kanga nyepesi kisha kujitupa kitandani. Nililala kwa muda wa saa zaidi ya nane kutokana na uchovu wa mbilinge za Mateja usiku kucha. Majira ya jioni Mateja alifanya kweli kwa kuleta sofa za nguvu kitu kilichofanya Bi Shuu kunipa chumba kikubwa cha nyumba kubwa. Niliamini ule ulikuwa mwaka wangu wa mimi kurudi katika maisha ya kutanua. Niliamini muda si mfupi lazima niwe na gari langu mwenyewe. Baada ya kukipamba chumba changu na kupendeza Bi Shuu aliniweka chini na kunipa somo. “Manka Mungu akupe nini, ukishikwa shikamana mwali wee.” “Hata mimi najua Bi Shuu.” “Unaonekana mwanzo ulikuwa ukifanya makusudi mbona sasa hivi mwanaume kapagawa muda si mrefu utakuwa dunia ya wenye nazo.” “Ndio maana yake.” “Basi Manka nitakuongezea vikorombwezo akigusa amenata.” “Usiniambie!” “Kwanini wazee wenzangu pamoja na umri wangu wakionja wanapagawa itakuwa wewe ukioga maji yanatelemka.” “Tena kweli ufanye haraka maana ameisha tangaza ndoa.” “Basi hiyo kazi niachie.” Mateja alinipigia simu kuwa siku ile angekuja kulala ili jumatatu twende kazini pamoja nami sikumkatalia. Kweli usiku alikuja kulala kwenye chumba changu kilichokuwa na hadhi kubwa kwa mtu yoyote. Kama kawaida ya usiku wa jana yake yalijirudi ya kusumbuliwa lala hivi geuka hivi fanya hivi, basi taabu mtindo mmoja. Na siku ile nilivumilia lakini moyoni nilijisemea siku nyingine nitampasha kweli wake hawezi kunigeuza kama mwanasesele na kunichezea apendavyo. Nikajikuta siyachukia mapenzi na kuyaona kwangu ni karaha na si starehe, mwanaume alikuwa akipanda juu ya mnazi hashuki mpaka nahisi kichefuchefu. Niliamini kabisa alitaka kunikomoa kwa vitu alivyonipa, kwangu sikuona mapenzi zaidi ya mateso. Uvumilivu uliponishinda nilianza kuwa mkali kwa kumgomea kwa usumbufu wake kwa kumueleza makavu kuwa sitaki kama hawezi kifo cha mende tuache. Mateja alinielewa na kustarehe bila usumbufu, nilishangaa kumbe anaweza kukwea mnazi bila kujifunga kamba za miguu. Kilichonishangaza ndani ya mapenzi yetu yaliyochukua miezi minne, Baadhi ya mambo yalianza kutoonesha dalili zozote za kutimiza ahadi yake. Siku zilivyozidi kwenda mbele ndivyo uhusiano na Mateja ulivyozidi kulega, hata kuwa pamoja baada ya kazi ikafutika kila muda alionekana yupo bize. Kitendo cha kutokuwa karibu na Mateja kilimshtua sana Bi Shuu kwani hata vizawadi navyo vilikatika. Siku moja aliniweka chini na kuniuliza. “Manka kulikoni?’ ”Hata mimi sijui.” “Manka kila siku hujui wakati unaharibu.” “Bi Shuu unanilaumu bure.” “Hivi kama na huyu atakuacha unafikiri utampata nani?” “Bi Shuu nimejitahidi kwa kila ulilonifundisha nililifanya lakini matokeo yake ndio hayo lazima kuna mkono wa mtu.” “Manka kuna kitu gani alichokipenda Mateja hukumpa?” “Mmh, kila kitu nimempa.” “Kweli?” “Kweli kabisa, nikudanganye ili iweje.” “Sasa itakuwa nini?” “Hata mimi sijui, huu utakuwa ni mkosi tu” “Basi naomba kesho ukienda kazini niitie Mateja.” “Mmh, sijui kama atakuja, lakini nitafikisha ujumbe.” Siku ya jumatatu nilikwenda kazini kama kawaida huku nikifikilia jinsi ya kufikisha wito kwa Mateja wa kuitwa Bi shuu. Hakuwa Mateja niliyekuwa namfahamu. Ilionesha mapenzi yalikwisha kabisa. Kila alipoingia ofisini alinisalimia lakini hakuna kilichoendelea. Nilipomuuliza alinijibu kwa kifupi “Nipo bize,” nilijikuta nikiiona kazi ngumu kama si Bi Shuu ningeacha kazi kutokana na kujiona sina thamani tena kwa Mateja. Siku moja roho iliniuma sana baada ya msichana mmoja kuingia ofisini kwa Mateja bila kumuulizia kwangu kama ilivyokuwa kwa wateja wengine. Niliacha kazi zangu na kumfuata ndani, nilipoingia ofisini mbona lilinishuka mtoto wa kike. Niliwakuta wamekumbatiana na Mateja huku midomo yao ikiwa imegandiana. Nilitamani ardhi ipasuke inimeze, nilisimama kama sanamu nisijue cha kufanya, machozi yalinitoka bila kizuizi, pamoja na kuniona hawakushtuka ndio kwanza walizidisha kutomasana kimahaba. Niliona wazi kabisa penzi langu na Mateja limefika ukingoni. Nilirudi ofisini kwangu na kukaa chini kazi ilikuwa chungu nilijikuta nikilia peke yangu, nilitamani kuondoka niiache kazi. Lakini niliyakumbuka maneno ya Bi Shuu kuwa siku zote penzi tamu ni lile lisilo sukumwa ninalosukumwa lina kasoro. Nikiwa nimeinama nafuta machozi nilishtushwa na sauti ya Mateja. “Manka.” Bila kuitika nilinyanyua uso kumuangalia huku kitambaa kikiwa karibu na macho kufuta machozi. Mateja alikuwa amesimama mbele ya meza yangu akiwa ameshikana kimahaba mmoja alimshika mwenzake mkono shingoni na mwanaume kiunoni. “Vipi mbona unalia?” Mateja aliniuliza kwa kunikujeli, sikumjibu niliendelea kufuta machozi. “Manka huyu ndiye mke wangu mtalajiwa.” Sikumjibu niliinama chini na kulia kilio cha kwikwi ambacho Mateja na mpenzi wake hawakukijali. Niliwasikia wakiondoka, niliwasindikiza kwa macho mpaka walipotoweka, baada ya kutoweka machoni mwangu nilijikuta nikijiuliza nalia nini kwani tukio lile halikuwa la kwanza upande wangu kutendewa. Ni kweli lazima moyo uniume kutokana na ahadi nzuri za Mateja ambazo nilijua zitanibadilisha katika maisha yangu. Ndoto yangu ya mchana ya kumiliki gari na nyumba iliyeyuka kama bonge la mafuta katika kikaango cha moto. Baada ya muda Mateja alirudi na kunipita kuingia ofisini kwake bila kunisemesha jambo lolote. Nilikumbuka wito niliopewa na Bi Shuu wa kwenda kuzungumza naye juu ya matatizo yangu, kila nilipotaka kumwambia moyo ulisita na kuamua kuipotezea tu. Muda wa kutoka nilijikuta nikijikaza kike na kumueleza. “Samahani bosi.” “Bila samahani,” Mateja alinijibu kistaarabu. “Bi Shuu alikuwa anakuita.” “Bi shuu naye ana shida gani tena?” “Hata sijui.” “Mmh, yule bibi na umri wake yuko vile wakati wa usichana wake alikuwaje?” “Mmh, sijui.” “Basi mwambie nitamtembelea wikiendi.” Jamani kauli ya Mateja ilinipa matumaini labda atarudisha moyo wake, siku zote nilimuamini Bi Shuu kwa maneno yake matamu yaliyojaa misemo nahau na methani ili kumlainisha mtu. “Jamani bosi kwa nini usiende leo?” “Manka nipo bize sana atanisamehe, lakini mwambie sijamdharau nitaitikia wito wake.” ITAENDELEA ... Read More
Story....... NI WEWE TU PENINA Sehemu ya kumi na moja (11) By GIVAN IVAN Phone & whatsapp....... 0769673145 Ilipoishia......... Upande wa Nolan yeye alipanga lazima amfundishe adhabu baba yake kwa namna yoyote ile. "Wewe ni baba yangu ndio sikatai, umenitunza vizuri, umenipa elimu ya kutosha Sawa, lakini kwa unyama huu unaotaka kuufanya hakika sitakuacha lazima nitaenda sambamba na wewe." alijisemea Nolan akiwa chumbani kwake akipanga mipango yake. Lakini pia Nolan aliapa kama asipofanikisha ndoa ya Frank na Penina bas atajiua. *********Endelea ******** Nolan alivunja kibubu chake cha kuhifadhia pesa na kugundua pesa iliyopo huko ni ndogo Sana na haitatosha kutimiza mipango aliyoipanga. Nolan aliamua kuwa mwizi wa ghafla kwa ajili tu ya kutimiza anachokitaka. Lakini hata hivyo hakuenda kuiba sehemu nyingine yoyote, aliamua kumuibia baba yake ikiwa ni njia moja wapo ya kumkomesha baba yake. Nolan alikuwa anajua baba yake ana tabia ya kuhifadhi pesa chumbani kwake. Na baada ya Nolan kugundua kuwa baba yake hayupo haraka akaamua kwenda chumbani kwake na kumuibia pesa kiasi cha shilingi million hamsini. Baada ya zoezi hilo, Nolan alichukua kiasi cha fedha kati ya zile alizomuibia baba yake na Kisha zingine akazificha sehemu ambayo mtu mwingine hawezi kuziona. Kisha Nolan akatoka nje na kuchukua gari Lake na kuondoka nyumbani Muda ule ule. * Mzee Joel alitia nanga Katika kikosi kimoja kilichojulikana kwa Jina la the killer (wauaji) Baada ya kufika mzee Joel alielezea shida Zake zilizompwleka pale na Sasa akitaka Frank pamoja na Nolan wauwawe Mara moja. Mzee Joel alitoa picha ya Nolan pamoja na ya Frank na kumkambidhi mkuu wa kikosi kile cha the killer. "mzee tunahitaji pesa kiasi cha shilingi million thelathini ili kuitimiza kazi yako." akaongea mkuu wa kikosi kile kumwambia mzee Joel. "hakuna tatizo kuhusu pesa nyie fanyeni kazi niliyowapa." akaongea mzee Joel. "Sawa kuanzia Sasa kazi imeanza na tutakuletea majibu Muda si mrefu." mkuu yule wa kikosi cha the killer akamwambia mzee Joel. Mzee Joel aliweza kuondoka huku akiwa na uhakika wa Kaz yake kufanyika kwa ufasaha Sasa. Mkuu wa kikosi kile cha the killer aliwateua vijana wanne kwenda kuanza kazi ya kummaliza Nolan na Kisha wengine wanne akawatuma kwa Frank. * Katika hoteli ile ya kifahari Penina na Frank wakiwa wameketi kitandani wakitizama tv, ghafla bila kutarajia walishtukia kumuona Nolan akigonga mlango. "Eeh kaka mbona umekuja bila taarifa?" akauliza Penina kwa mshangao baada ya kufungua mlango. "lazima nije ghafla na taarifa zangu ziwe za ghafla kwasababu nataka nifanye kitu cha kuwafurahisha, na hivi nimekuja kuwaambia mjiandae tuondoke tayari nimeshawakatia tiketi za kwenda South Africa (Afrika kusini)" akaongea Nolan kumwambia Frank na Penina. Zilikuwa taarifa za ghafla kwa kina Penina na Frank, lakini hata hivyo hawakuwa na namna ilibidi waanze kujiandaa kwa ajili ya safari yao waliyoandaliwa na Nolan. * Vijana wanne waliopewa kazi ya kumuangamiza Frank walichunguza wakachunguza na hatimaye wakafinikiwa kupajua nyumbani kwa kina Frank. Na bila kupoteza muda wakavamia nyumbani kwa kina Frank na kuwaweka chini ya ulinzi Wazazi wake Frank pamoja na mdogo wake Frank. Vijana wale wakawaamuru Wazazi wake Frank waseme sehemu alipo Frank la sivyo watawaangamiza. Wazazi wake Frank kwa kuogopa kuuwawa wakajikuta wakitaja sehemu aliyopo Frank. Vijana wale bila kuchelewa waliachana na Wazazi wake Frank wakaingia kwenye gari na kuanza safari ya kuelekea sehemu aliyopo Frank ambapo ni Katika hoteli moja ya kifahari. * Frank pamoja na Penina walimaliza kujiandaa na moja kwa moja wakatoka ndani ya chumba kile na kuelekea mpaka nje ya hoteli ile na kuingia kwenye gari la Nolan. Lakini wakati huo huo vijana wale wanne wa the killer walikuwa tayari wameshawasili kwenye gari lile na waliweza kumuona Frank pamoja na Nolan ambao ndio walikuwa wakiwatafuta wawamalize. Mmoja kati ya vijana wale wanne wa the killer alitoa simu yake na kuwapigia wale vijana wengine wanne waliokuwa wakimtafuta Nolan, na kuwaeleza sehemu aliyoonekana Nolan pamoja na Frank. Vijana wale waliokuwa wakimtafuta Nolan nao walianza safari ya kutoka sehemu nyingine waliyokuwa wakimtafuta Nolan na kushika njia ya kuelekea Katika hotel waliyoelekezwa na wenzao. Wakati huo huo Nolan aliliondoa gari pale hotelini na kuanza safari ya kuelekea Katika uwanja wa ndege. Vijana wale wanne wa the killer nao wakawasha gari Lao na kuanza kuwafuatilia ili waweze kujua wanaelekea wapi na kama ikiwezekana wakaulie huko huko. Safari ikiwa inaendelea, ghafla Nolan aliona gari moja nyekundu ikiwa nyuma na kuitilia mashaka kuwa inawafuatilia. Nolan aliamua kufanya kitu ili apate uhakika kama gari lile linawafuatilia au haliwafuatilii. Nolan alipunguza mwendo wa gari Lao ili lile gari jekundu lililokuwa nyuma yao liwapite. Lakini cha kushangaza gari lile halikuwapita nalo pia lilipunguza mwendo na kwenda taratibu pia. Nolan akaamua kuongeza mwendo wa gari Lao ili kuliacha gari lile, lakini pia gari lile liliongeza mwendo na kuwa Sawa Sawa kabisa na gari la kina Nolan. Nolan hapo Sasa ndio akapata jibu kuwa asilimia Mia moja hilo gari jekundu linawafuatilia vibaya mno. "hawa hawanijui ngoja niwaoneshe mimi ni nani." akajisemea Nolan kimoyo moyo na hapo hapo akaongeza mwendo wa gari Lao ili kuliacha gari lile lililokuwa likiwafuatilia. Wakati huo huo kile kikosi cha pili cha the killer kiliwasili pale hotelini na kuwapigia wenzao simu ambao ni wale wanaowafuatilia wakina Nolan, na kuwatarifu kuwa tayari wameshafika. Kikosi kile cha kwanza kikawapa maelekezo ya sehemu walipo wakiwa bado wanawafuatilia wakina Nolan. Kikosi kile cha pili bila kupoteza Muda nacho kikatoka pale hotelini na kuanza kuwafuatilia wakina Nolan pia. Wakati hayo yote yanaendelea Frank na Penina walikuwa wakicheka na kufurahi kwenye gari bila kufahamu chochote kinachoendelea, na hata Nolan hakutaka kuwaambia chochote kwa kutokutaka kuwavuruga Katika safari yao. Nolan bado alizidi kujaribu kulipoteza gari lile lakini bado hakufanikiwa. Nolan alifika kwenye mataa ya kuongozea magari na baada ya Nolan kuvuka tu kwenye mataa yale, zikawaka taa nyekundu kuashiria magari yaliyokuwa yakitoka upande ule wa kina Nolan yasimame kwa dakika kadhaa. Lakini Nolan wao walikuwa tayari wameshavuka lakini vijana wale wa the killer walikuwa bado hawajavuka hivyo ikawabidi wasimame. Nolan aliweza kugundua kuwa gari lililokuwa likiwafuatilia limesimamishwa kwenye mataa. Lakini Nolan akataka kuwafahamu ni wakina walikuwa wanawafuatilia. Nolan alipaki gari pembeni Kisha akawashusha Frank na Penina na kuwapakiza kwenye tax iliyokuwa pembeni yao, na kuwakabidhi kila kitu kilichostahili kwenye safari yao na kuwataka watangulie na kuanza safari yao. Penina na Frank walishangazwa Sana na maamuzi ya Nolan lakini hata hivyo Nolan hakutaka wamuulize swali lolote, alimwamuru dereva wa tax ile awashe gari na kuondoka. Kisha Nolan naye akaingia kwenye gari yake na kugeuza kuwafuata vijana wale wa the killer na wakati huo walikuwa tayari wameshaungana wote kwa maana ya kikosi kile cha kwanza kilichokuwa kikimtafuta Nolan na kile cha pili kilichokuwa kikimtafuta Frank. ............ Itaendelea ... Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments: